Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,411
Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini Mhe. Prof Patrick Ndakidemi ambaye kwa ujumla hajui siasa, hajui utendaji, huwa hana mchango Bungeni na si muongeaji , baada ya kuona mwenzake wa Moshi mjini akitoa takrima ya kawaha na mitungi ya gesi kwa wamama wa UWT sasa na yeyeye leo tarehe 06.03.2024 aliwaalikaa Viongozi wa Matawi wa Chama cha Mapinduzi CCM(Wenyeviti wa Matawi, Makatibu wa Matawi na Wenezi wa Matawi) wote katika Jimbo la Moshi Vijijini katika ukumbi wa CCM Mkoa ambapo aliwakabidhi Mitungi ya Gesi kwaajili matumizi ya nyumbani ikiwa ni pamoja na kuwapa Elimu juu matumizi yake na umuhimu wa kutumia gesi.
TAKRIMA ni "rushwa " inayotolewa ili mtu atende jambo fulani mbeeni , na kabla ya 2005 ilikuwa ni kosa la jinai lakini ikaja kutungiwa sheria ikawa si kosa tena maana wabunge wetu wa CCM kila mmoja huwa anatoa. Ni Kosa, dhambi na haipaswi kufanywa hivyo hata kama sheria imeruhusu. Ni sawa na Kufanya mapenzi nje ya ndoa kwa kuvaa kondomu si kosa lakini dhambi mbele za Mungu basi vivyo hivyo TAKRIMA ni halali kisheria lakini ni hongo kama hongo zingine.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya akiwemo Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Vijijini Ndg. Andrew Mwandu,Katibu wa UVCCM Wilaya ya Moshi Vijijini Ndg. Pantaleo Melkiory pamoja na Mjumbe wa H/Kuu ya CCM Wilaya &, Mjumbe wa Baraza la Jumuiya ya Wazazi Mkoa Ndg. Emanuel Mlaki.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi Mhe Mbunge huyu wa Moshi vijijini aliwaeleza mambo mbali mbali yaliyofanywa na Serikali yao Rais wetu Mpendwa Mhe Dkt Samia Suluh Hassan katika kila Kata ndani ya Jimbo la Moshi Vijijini na hivyo kuwataka viongozi hao kuendelea kusemea mazuri yaliyofanywa na Serikali pamoja na Viongozi wengine.
Aidha, Viongozi hao kwa nyakati tofauti wamemshukuru sana Mhe Mbunge kwa kuwakumbuka kwani hawajawahi kukumbukwa kwa kipindi kirefu na kumuhaidi wataendelea kumpa ushirikiano na kumuunga mkono ili maendeleo katika Jimbo la Moshi Vijijini yaendelee kuja kasi na Viwango.
Tunajiuliza, hawa wananchi waliogawiwa, imeumika kriteria gani kuwapata? Wameokotwa kutoka wapi?
Ndakidemi badala ya kumshukuru ROSTAM AZIZ anayegawa hizo takrima kwa wabunge wote wa JMT ili wagawe majimboni anamshukuru SSH , sasa taifa gesi si ya Rostam, na ni mpango maalum wa kuiua kampuni zingine?
Mitungi ya Gesi inagawiwa kwenye ofisi za CCM, je Msabato ambaye dini yake inakatza kujiunga na siasa, atapataje?
CHADEMA ambaye hataki kukanyaga ofisi za CCM atapataje?
In short , Majiko ya Gesi huo ni MRADI WA ROSTAM AZIZ kugawa TAKRIMA kwa wana UWT!
TAKRIMA ni "rushwa " inayotolewa ili mtu atende jambo fulani mbeeni , na kabla ya 2005 ilikuwa ni kosa la jinai lakini ikaja kutungiwa sheria ikawa si kosa tena maana wabunge wetu wa CCM kila mmoja huwa anatoa. Ni Kosa, dhambi na haipaswi kufanywa hivyo hata kama sheria imeruhusu. Ni sawa na Kufanya mapenzi nje ya ndoa kwa kuvaa kondomu si kosa lakini dhambi mbele za Mungu basi vivyo hivyo TAKRIMA ni halali kisheria lakini ni hongo kama hongo zingine.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya akiwemo Kaimu Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Vijijini Ndg. Andrew Mwandu,Katibu wa UVCCM Wilaya ya Moshi Vijijini Ndg. Pantaleo Melkiory pamoja na Mjumbe wa H/Kuu ya CCM Wilaya &, Mjumbe wa Baraza la Jumuiya ya Wazazi Mkoa Ndg. Emanuel Mlaki.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi Mhe Mbunge huyu wa Moshi vijijini aliwaeleza mambo mbali mbali yaliyofanywa na Serikali yao Rais wetu Mpendwa Mhe Dkt Samia Suluh Hassan katika kila Kata ndani ya Jimbo la Moshi Vijijini na hivyo kuwataka viongozi hao kuendelea kusemea mazuri yaliyofanywa na Serikali pamoja na Viongozi wengine.
Aidha, Viongozi hao kwa nyakati tofauti wamemshukuru sana Mhe Mbunge kwa kuwakumbuka kwani hawajawahi kukumbukwa kwa kipindi kirefu na kumuhaidi wataendelea kumpa ushirikiano na kumuunga mkono ili maendeleo katika Jimbo la Moshi Vijijini yaendelee kuja kasi na Viwango.
Tunajiuliza, hawa wananchi waliogawiwa, imeumika kriteria gani kuwapata? Wameokotwa kutoka wapi?
Ndakidemi badala ya kumshukuru ROSTAM AZIZ anayegawa hizo takrima kwa wabunge wote wa JMT ili wagawe majimboni anamshukuru SSH , sasa taifa gesi si ya Rostam, na ni mpango maalum wa kuiua kampuni zingine?
Mitungi ya Gesi inagawiwa kwenye ofisi za CCM, je Msabato ambaye dini yake inakatza kujiunga na siasa, atapataje?
CHADEMA ambaye hataki kukanyaga ofisi za CCM atapataje?
In short , Majiko ya Gesi huo ni MRADI WA ROSTAM AZIZ kugawa TAKRIMA kwa wana UWT!