Twaweza: Maoni na Matakwa ya Wananchi juu ya Uongozi wa Kisiasa Tanzania kuelekea 2015

huu ni utafiti uchwara hakuna la maana hapo! sitashangaa 2015 tume ya uchaguzi ikacheza kwenye huu utafiti kutuletea matokeo ya uraisi!:loco:
 
Utafiti mpya ambao matokeo yake yamepangwa kutangazwa rasmi leo jumatano hii, umeonyesha kwamba endapo uchaguzi mkuu wa Rais wa JMT ungefanyika hivi sasa, Mbunge wa Mondlu, Edward Lowassa angeibuka mshindi. Twaweza imemaliza utafiti wake, matokeo yatatangazwa Dar es Salaam leo. Ndani ya CCM Lowassa alishindanishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe, Waziri wa Africa Mashariki Samwel Sita, Waziri wa Katiba na Sheria Dk.Asha Migiro, Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli na waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Source:Gazeti la Raia Mwema ya leo November 12, 2014.


Katika hatua nyingine utafiti uliofanywa na wahitimu wa chuo kikuu cha Dar Es Salaa kwa wajumbe wa Baraza la Umoja wa Vijana (UVCCM) katika kikao kilichoketi juzi Dodoma, Lowassa aongoza tena....

Baada ya mkutano wa Baraza la umoja wa vijana CCM kumalizika, sasa ni wazi hakuna wa kumzuia Lowassa kuingia Ikulu. Baada ya kikao cha NEC mwezi uliopita nilisema kuwa katika hii safari ya kuingia ikulu Lowassa kafika katika mitaa ya IFM ila baada ya huu mkutano wa vijana wa UVCCM walai kwa sasa Lowassa ni Rais na kashafika katika jengo la wizara ya elimu, adjacent na ikulu zikiwa zimebaki mita chache tu aweze kuingia ndani.


Leo Ocampo four nawaletea utafiti uliofaywa na wahitimu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam kwa wajumbe wa baraza kuu la vijana uvccm. Utafiti huo ulihusu hasa kujua ni nani vijana hao wa chama tawala wanaona anafaa kwa kuongoza nchi 2015; na pili ililenga kuwahoji kuhusu katiba pendekezwa kama wanaona inafaa ipigiwe kura kabla ya uchaguzi mkuu au baada ya uchaguzi mkuu wa 2015. Kwa kuanza na objectice ya kwanza ya kujua nani anafaa kuwa rais wa 2015 kwa kura za wajumbe hao ni kama ifuatavyo…….(Note jumla ya wajumbe wa baraza kuu la vijana ni 150, na huu utafiti uliweza kuwahoji wajumbe 60 kwa maana ya sample; njia kubwa iliyotumika ni dodoso au maarufu kama questionnaires)…..matokeo…..

1. Edward Lowassa alipendekezwa na wajumbe 42 kati ya hao 60 (68.8%).

2. Mizengo Pinda alipendekezwa na wajumbe 6 kati ya hao 60 (10%).

3. John Magufuli alipendekezwa na wajumbe 3 kati ya hao 60 (5%).

4. Dr Asha Migiro alipendekezwa na wajumbe 3 kati ya 60 (5%).

5. Frederick Sumaye alipendekezwa na wajumbe 2 kati ya 60 (3%).

6. Bernard Membe alipendekezwa na wajumbe 2 kati ya hao 60 (3%)

7. Mwigulu Nchemba na January Makamba wakapata kura 1 kati ya hao 60 (1.6%).

Katika huo mkutano kila kona uliyokiuwa unapita wajumbe wa baraza walisikika wakisema Lowassa atoshaa, Lowassa atosha, ukienda sehemu za migahawa ni Lowassa, ukienda maeneo ya jengo kuu la CCM ni Lowassa, ukienda kwenye bar mbali mbali Dodoma carnival, Nyerere Square, kisanju, Maisha club kwa kifupi kila kona ilikuwa jina la Lowassa. Huu ni utafitit uliotoa hamasa, umoja na matumaini mapya katika safari ya matumaini kwa watanzania, naomba niwaambie mlango wa rehema bado uko wazi kwa ajili ya kujiunga na kundi hili la ushindi, mtu asikudanganye na ukadanganyika hakuna kundi la ushindi zaidi ya kundi hili, ni wajibu wako kuwahi haraka ili upate kuhesabiwa na wewe.

Katika kubadilishana mawazo na wajumbe wa baraza la vijana nilipata wasaha wa kusikiliza ujumbe alioutoa mzee wango John Shibuda, kwa kweli huyu mzee amejaa busara ya hali ya juu.

Shibuda aliwaeleza vijana ya kwamba “unaweza kuwa na fedha za sarafu nyingi sana zenye kelele lakini hazina maana, na mwingine akawa na noti moja tu ambayo haina kelele ila ina maana kweli kweli”, tafsiri yake ni kwamba kuna wagombea wengi kweli kweli wakipiga kelele kama fedha za sarafu ila hawana maana na hili ni lile kundi waliokwisha jitangaza huku wengine wakienda Uingereza kupiga kelele zao za kutangaza nia kugombea urais (Kuna clip iliyopata umaarufu ya professor PLO Lumumba wa Kenya anashangaa viongozi kupeleka watoto wao kusoma nje, anashangaa wananchi na viongozi wa leo wakikimbilia kwenye mabalozi ya nchi za magharibi kupigania green card pasipo kujua kuwa wanaenda kuwa watumwa kwa mara ya pili, sasa hili swala la viongozi wetu kwenda kutangaza nia ya kugombea urais wakiwa ulaya kwenye vyombo vya habari vya wakoloni ni wazi huu ni utumwa uliopitiliza na kamwe tuwaogope kama ukoma viongozi wa namna hii).

Kuna wagombea wengine walipiga kelele za sarafu kwa kubebwa na WAMA organization lakini kadri siku zilivyozidi kwenda bila shaka iligundulika kuwa mgombea mwenyewe bwana Membe Bernard ana uwezo mdogo sana kupita kiasi, ndiyo mana kila kukicha kambi yake inazidi kubomoka na kwa taarifa za uhakika saizi kabaki na watu 3 tu ambao ni Nyalandu mume wa Aunt Ezekile, Prince na Richard Kasesela wengine wote wamekimbia.


Kundi lingine lenye kelele ni hili kundi linalojiita vijana, hili kundi kelele zao zinakera sana sana katika jamii na kwa wenye busara kama sisi ocampo four ni mara mia kuangalia katuni za Ben ten au Dora kuliko kusikia kelele za hawa wanaojiita vijana, eti January Makamba naye anataka urais, eti Mwigulu naye anataka urais, hahahahahaha eti na Kwigwangala naye anataka urais, kwenye biblia hawa ni sawa sawa na wale wanaopanda mbegu katika mawe. Kwa maneno hayo hapo juu Lowassa ndiyo fedha yenye thamani (noti), tena noti wekundu wekundu, Lowassa katulia, emekuwa akipuuza uongo na matusi za wahuni na wakora wa nchi hii, kwa kipindi kirefu Lowassa amekuwa jasiri, mpole, kiongozi mkakamavu, mwenye upendo na aliye jaaa tabasamu la furaha.


Tafsiri pana za hizo data zinaweza kuainishwa na kukataliwa kwa waziri mkuu Mizengo Pinda kuwa naibu kamanda wa Umoja wa Vijana, kitendo kilichopelekea Masaburi kufukuzwa kwenye nafasi ya kampeni meneja baada ya kutumia million 400 huku matokeo yakiwa zero (hata ingekuwa mimi lazima ningekasirika sana sana). Na pili haya matokeo kwa upana wake yanaweza kueleza hata kwa nini mchumia tumbo namba moja wa UVCCM na aliyekuwa rafiki mkubwa wa Rizone (kwa sasa ni paka na panya) kukataliwa kuwa naibu katibu mkuu bara na huyu siyo mwingine bali ni bwana Salum Hapi. Kwa sasa huyu bwana kahamia kwa Pinda baada ya kuona kumuuza Membe ni sawa sawa na kuhamisha mbuga ya Serengeti na kuileta Samora Avenue.


NB: Watanzania huu siyo wakati wa kucheza, 2015 siyo wakati wa kucheza, wenzetu wamekuwa wakipiga hatua kumi mbele kwa muda wa miaka hiyo yote, hivyo ili kuwakamata na kwenda nao pamoja sisi kuanzia 2015 tuwatafute viongozi wakutupaisha kimaendeleo, kiongozi mwenye maamuzi magumu siyo tu ndani ya nchi ila hata nje ya nchi ili tusiruhusu ukoloni kwa mara nyingine tena, na huyo sii mwingine zaidi ya Lowassa, tafadhalini sana sana tujitahidi na tuhakikishe hatufanyi makosa na tusije tukajutia katika huo uchaguzi ujao……………

Kuhusu objective ya pili, wajumbe wote 60 waliohojiwa waliona inafaa katiba inayopendekezwa ipigiwe kura kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015 kama ilivyopangwa.

Asante sana
Ocampo four.

Ocampo four umejifunza lini siasa mbona umeanza kutumika kinyume na maumbile mapema namna hiyo.
Napenda kujua weledi wako kwenye masuala ya siasa nchini. Huo utafiti hauna reflection ya uhalisia wa matokeo ya uchaguzi ndani ya chama mwakani na nina uhakika kwa utafiti huo wasomi wala wanahabari na hata wananchi hawawezi kuutumia kama base ya kufanyia maamuzi au ulinganishi kwenye matokeo ya Uchaguzi wa Mkutano Mkuu mwakani 2015.

Nataka nikusaidie, sample ya wajumbe 60 kwa watu 150 haiwezi kuakisi matokeo ya Mkutano Mkuu wa Kura za maoni mwakani ambapo wajumbe wake ni zaidi ya 1800, na hivyo hiyo sample size yako ni Irrelevant kwani sio kweli kuwa wajumbe wote wa Baraza UVCCM ni wajumbe wa Mkutano Mkuu. Hivyo huwezi kutumia sample ya watu ambao sio wapiga kura kufanya utafiti huu wa kipuuzi.

Bado napata shida kuona kijana kama wewe na elimu yako unashindwa kufanya hesabu ndogo za kujumlisha na za asilimia? Ukitafuta 42% ya wajumbe 60 ni 70% na sio 68.8%. Lakini pia ukijumlisha hayo matokeo yako ya kupika bado haifiki jumla ya 100%.

Hivyo ni dhahiri sasa kuwa kijana Ocampo four ni kweli unatumiwa kinyume na maumbile yako na hao mabwana wanaokuweka mjini.

Kajipange upya usitupotezee muda watu wazima
 
Huu ni ushahidi wa lowasa kukubalika na Watanzania .. Hata Ukawa wanamkubali Lowasa
 
Nakubaliana na 'Mpakakieleweke' watu wanahonga pesa kia sehemu ili watajwe auwatangazwe kuwa wanapendwa wakati sisi wananchi tunanyanyasika kwa umaskini. Anayetaka uraisi atoe mali na fedha zake zote kwa wananchi zilizo ndani na nje ya nchi. Hapo tutajua kuwa huyu mtu ana hamu ya kuwatumikia watanzania. Wanaoshabikia CCM wanavuta chochote huko wengi tuko kitaa tunabangaiza na siku nyingine zinapita kwa kushindia maji tena ya bomba au kisima.

utafiti wa kweli ukafanyike vijijini na maswali yawe mepesi kuhusu maisha ya watu sio urais. Wananchi shida yetu kubwa ni hali ya maisha yetu kuboreka. Wengine vijijini watakuuliza uraisi ndio kitu gani kilimo ufugaji ndio mpango mzima.
 
Mnapo ongea hayo wanaccm wenzangu kumbukeni nchi sasa ipo kwenye mfumo wa vyama vingi, je akipita Membe hamtakuwa tayari kumuunga mkono na mtaunga mkono uinzani ?

Hata mimi nawashangaa je akiwa Mizengo Pinda,watakuwa tayari kumuunga mkono au wataamia upinzani?
 
Purposive sampling.... is non probability sample where by no one has equal chance to be selected....therefore such kind of sample can't be inferred to the population concerned....for me this is jus a story with no scientific justification
 
we mjinga kweli kweli yani kuhoji watu 60 kati ya 150 unashangaa........kwa taarifa yako katika huo utafiti wamepitiliza hata sample size..........mburula kweli au ujasoma maelezo hapo juu
[h=1]Topic: Twaweza: Lowassa Aongoza kura ya Maoni
kuhusu Urais
.Inaonekana matusi ni jadi yako.Can you draw conclusion based on 60 people ambao ni vijana wa CCM.Unless iyo heading ibadilishwe muweke aongoza kati ya vijana wa CCM otherwise its totally misleading the entire nation unless kama ndo kampeni imeanza kwa uyu mgombea[/h]
 
NIMESOMA PAGE YA KWANZA YOTE ila kilichonishangaza nikuona wale pro-chadema wakimsapoti lowassa. sijaelewa hasa ni nini kilichonyuma ya hili sakata la kutaka kumpeleka mwizi pale magogoni.
au nina wasiwasi mods wanatumika kwa ku-delete any against content.

inamaana chadema aka wachaga wamehamia kumuunga mkono lowasa kwa sababu ni mkaskazini mwenzao? wonders will never end.
 
NIMESOMA PAGE YA KWANZA YOTE ila kilichonishangaza nikuona wale pro-chadema wakimsapoti lowassa. sijaelewa hasa ni nini kilichonyuma ya hili sakata la kutaka kumpeleka mwizi pale magogoni.
au nina wasiwasi mods wanatumika kwa ku-delete any against content.

inamaana chadema aka wachaga wamehamia kumuunga mkono lowasa kwa sababu ni mkaskazini mwenzao? wonders will never end.

Mkuu chadema wanataka sana CCM impitishe Edward Fisadi Lowassa ili washinde kirahisi uchaguzi 2015 na CCM chini ya uongozi shupavu wa Jakaya Kikwete wanajua hilo na hawawezi kufanya kitu kama hicho watachuja na kumpitisha mtu makini atakayepeperusha bendera ya CCM wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
 
nawaomba sana ukawa hizi tafiti zisiwatoe kwenye mstari ...historia ya tafiti za kisiasa kwenye nchii hii ni za kupikwa na kuwaanda watu kisaikolojia na uchakachuaji...hawa twaweza wanatumika na kambi ya mgombea fulani wa uraisi....wanachokifanya ni kuwavunja nguvu wagombea uarais wa CCM wanaopambana na lowasa vile vile wakicheza karata nyingine kwa ukawa....huu utafiti hata cjui umefanyika lini mpaka kuwahusisha ukawa ...ukisoma raia mwema wansema utafiti huu umefanyika kabla ya ukawa ukicheki data zao leo wanaihusisha ukawa ...na raia mwema pamoja na ulimwengu wanaonekana wasaka tonge pamoja na twaweza yao..............
 
Katika hali ya kushangaza, matokeo ya utafiti wa TWAWEZA uliokusanya maoni ya wananchi yameonesha kuwa waziri mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda maarufu mtoto wa mkulima amewapiku makada wengi wa CCM walioanza mapema mbio za urais.
Kwa mujibu wa TWAWEZA, kama uchaguzi ungefanyika leo Pinda anashika nafasi ya pili kutajwa kufaa kuwa Rais akiwa na asilimia 14 nyuma ya Lowassa mwenye 17%.
Pinda ambaye ameanza kutajwa miezi mitatu iliyopita kuwa yumo Katika wanaotajwa kuwania urais amewapiku wanasiasa wazito ndani ya CCM ambao majina na harakati zao za kujipanga zimekuwa za miaka kadhaa sasa ndani ya CCM. Makada hawa ni waziri wa mambo ya nje Bernard Membe, waziri wa Mahusiano na uratibu Steven Wassira, naibu waziri January Makamba, waziri mkuu mstaafu Frederick Sumaye na wengine.
Kasi ya Pinda akiwa nyuma ya Lowassa kwa mpishano wa 3% pekee ni dalili tosha kuwa mtoto wa mkulima anaendelea kukubalika kwa Kasi kuwa. Lowassa ambae anatajwa kuanza harakati za urais tangu alipojiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu mwaka 2008 (miaka zaidi ya 6) ameshika nafasi ya kwanza akiwa na 17% huku Pinda akimpumulia mgongoni kwa 14% huku mtoto wa mkulima akiwa hana miezi sita tangu aanze kutajwa.
Kuja kwa Pinda kwenye mchakato huu kunatajwa kuzipasua kambi mbili kubwa, ile ya Edward Lowassa na Bernard Membe kwa kuvuna wafuasi miongoni mwa wajumbe wa NEC na mkutano mkuu wa CCM.Hii ni kutokana na Pinda kujitokeza kama mtu wa katikati ya makundi hasimu ya Membe na Lowasa ambayo yameapa kushughulikiana kwa gharama yoyote. Lowassa yuko tayari mtu yoyote awe rais lakini sio Sitta au Membe. Kadhalika Bernard Membe na Sitta hawako tayari kuona Lowassa anakua Rais.
Pinda ametumia mwanya wa kupasua katikati ya wanamtandao wa mwaka 2005 ambao wanahasimiana. Hata hivyo, Pinda anapata bahati nyingine ya kuwa hayuko miongoni mwa makada 6 wa CCM waliopewa adhabu ya kifungo na chama kwa kukiuka kanuni za maadili za CCM kwa kuanza kampeni mapema. Hii inamuweka katika nafasi nzuri kisiasa ndani ya CCM.
Aidha hulka yake ya kuwa mtu wa kawaida ambaye hana majivuno na cheo chake hakijamvaa na kumtenganisha na watu inaelezwa kuwa ni miongoni mwa mambo yanayowavutia wengi kuona kuwa ni kiongozi anayefaa kuvaa viatu vya Rais Kikwete.
Mizengo Pinda ni mwanasheria kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam na amefanya kazi akiwa msaidizi wa karibu wa Mwalimu Julius Nyerere ikulu ya Magogoni na baadae mzee Ali Hassan Mwinyi na Mkapa kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge na baadae naibu waziri,waziri wa TAMISEMI na waziri mkuu mwaka 2008.
Aidha Pinda ni kachero aliyebobea na wa muda mrefu katika utumishi wa nchi jambo linalomfanya kuwa na uelewa mkubwa wa nchi na utendaji wa serikali. Inasemekana mwaka 2005 jina la Pinda lilikuwa katika orodha ya mapendekezo ya nani awe waziri mkuu wa Dr Jakaya Kikwete baada ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT, lakini wanamtandao walilipenyeza jina la Edward Lowasa kuwa ndiye anayefaa kwa nafasi hiyo.
 
Mkuu chadema wanataka sana CCM impitishe Edward Fisadi Lowassa ili washinde kirahisi uchaguzi 2015 na CCM chini ya uongozi shupavu wa Jakaya Kikwete wanajua hilo na hawawezi kufanya kitu kama hicho watachuja na kumpitisha mtu makini atakayepeperusha bendera ya CCM wakati wa uchaguzi mkuu ujao.
Shikamoo mzee Masaburi.......nasikia umenyanganywa ukampeni meneja na mzee wa kulialia
 
Nivizuri sana Kama wote wanaoshabikia LOWASSA wanaongozwa na Uzalendo, lakini kama ni pesa zake taifa limekwisha , naomba hao walio fanya utafiti wamtoe Lowassa ashindanshwe na walioko upinzani,,nakumbuka ni humu humu kwenye jukwaa amebwagwa mara nyingi
 
Nivizuri sana Kama wote wanaoshabikia LOWASSA wanaongozwa na Uzalendo, lakini kama ni pesa zake taifa limekwisha , naomba hao walio fanya utafiti wamtoe Lowassa ashindanshwe na walioko upinzani,,nakumbuka ni humu humu kwenye jukwaa amebwagwa mara nyingi
Hata akishindanishwa nje Lowassa atashinda, labda kidogo Dr.Slaa atamkaribia kwa kura ila at the end lazima Lowassa ataibuka kidedea
 
Back
Top Bottom