TV zetu acheni ujinga na ujuaji

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Huwa napenda sana kutazama TV zetu hizi za hapa nchini .ITV,EATV mTBC lakini sasa naona zinazidisha matatizo kichwani.

SHida na matatizo yaliyo nchini unahisi ukiangalia Tv labda yatatulia kutokana na vipindi mbalimbali vya kufurahisha ,kinachosikitisha na kunihuzunisha ni vipindi hivi kuwa vimekalia fujofujo ,kwa maana hakuna unachokisikia kwa makini ,utaona unatazama mchezo au kipindi halafu kuna mziki nyuma yake, mziki na maneno ya kipindi hujenga fujo na kukuchanganya na kujiona hujui unasikiliza kitu gani.

Kama humu mna watu ambao ni watazamaji wazuri wa Tv bila ya shaka yeyote ile mtaweza kuliona jambo hili ,yaani unakuta kipindi ni kizuri tu ,na unatamani kusikia wanayozungumza washiriki ,lakini mziki ulionyuma au tuseme mziki unaochomekewa huwa unavuluga kila kitu ,hakuna kinachosikilikana ni fujo tupu ,hujui uzidishe sauti au upunguze.

Ningependelea wahusika kama mnasoma hapa JF basi muangalie vipindi vya wengine au TV za wengine muone ,kama mna habari za mitaani basi ziwe habari tu na sio na muziki juu yake ,kama ni igizo basi zisikike sauti za waigizaji pekee zisizo ingiliana na muziki unaovuka sauti za waigizaji au usiwepo mziki kabisa.

Hivi sasa kuna kipindi EATV ,aloo kuna mziki unaharibu kipindi kizima na ni ovyo kabisa ,yaani huwezi kuzidisha, sauti inakuwa ni balaa. sijui wanafikiaria watu wako baa.
 
Hao EATV ndio zaidi, unakuta kipindi cha majadiliano kama 5 Connect wao wanaweka sauti za miziki sijui ndio sound tracks zao ambazo zinaondoa umakini katika kufuatilia mjadala....
 
Huwa nawapigia simu lakini haipokewi na nipo Ngorongoro ,sifahamiani na mtu kule ,na ikiwa saound track au hawana online editor basi ni hatari ,kwani hawajui kama wanachokitangaza kinawafikia watu kwa high grade au ndio anao anao chenga twawala.
 
Acha porojo wewe UK imekuwa Ngoro ngoro ambako hujawahi Tia sura yako!
 
Bora ushinde jf, uwe unaangalia zako ma u tube yanayorushwa na kina VOR.
 
Acha porojo wewe UK imekuwa Ngoro ngoro ambako hujawahi Tia sura yako!
Aloo wewe mtu una dharau sana, au wenye mtandao ni nyie tu wa huko majuu ? Halafu kwa taarifa yako tulipotoka kupigana Uganda ,nilikuwa naishi Murutunguru kule Nansio Ukerewe ,ni kijijini uko ndani kabisa,tuliondoka na rova(Landrover) ya kazini jeshini ,tukapita nayo kuanzia Mara tukakatisha katika mbuga za wanyama hadi tukatokezea Korogwe ,sasa mbuga zote unazozijua wewe tulipita na kulala pale kijijini kwa WaIraqi watz weupe,kabla atujaingia Arusha na Moshi.Njia tuliopita hairuhusiwi kupita gari zingine au private car ,ukitokea Bunda kabla hujaingia Mara kuna kabanda kadogo wanakaa watu wanaolinda pori ,walipoona ni sisi wazee wa kazi wakasema haya piteni wakuu,haoo tukakata mbuga.Sasa leo nipo Ngorongoro unasema wewe pekeyako ndio kwenu ,huachi uzushi.
 
Aloo wewe mtu una dharau sana, au wenye mtandao ni nyie tu wa huko majuu ? Halafu kwa taarifa yako tulipotoka kupigana Uganda ,nilikuwa naishi Murutunguru kule Nansio Ukerewe ,ni kijijini uko ndani kabisa,tuliondoka na rova(Landrover) ya kazini jeshini ,tukapita nayo kuanzia Mara tukakatisha katika mbuga za wanyama hadi tukatokezea Korogwe ,sasa mbuga zote unazozijua wewe tulipita na kulala pale kijijini kwa WaIraqi watz weupe,kabla atujaingia Arusha na Moshi.Njia tuliopita hairuhusiwi kupita gari zingine au private car ,ukitokea Bunda kabla hujaingia Mara kuna kabanda kadogo wanakaa watu wanaolinda pori ,walipoona ni sisi wazee wa kazi wakasema haya piteni wakuu,haoo tukakata mbuga.Sasa leo nipo Ngorongoro unasema wewe pekeyako ndio kwenu ,huachi uzushi.
dah!
 
Haya hivi sasa kuna mchezo hapa EATV ,aloo mchezo mzuri sana ,lakini kuna sijui ni piano au chiriku ,yaani maneno hayasikikani zaidi ya piano ,utafikiri ni Tom & Jerry,akipita mtu dirishani anaweza kusema mnatazama makatuni,au kuna mtoto anachezea redio kwa kupandisha na kushusha sauti ,yaani sauti ya muzeka ni outof control ,hakuna uwiano kabisa ni vurugumechi.
 
Hilo tatizo lipo sana hata kwenye movie zetu za kibongo, vitu vingine sio lazima ukae darasani ni common sense tu, anyway polepole tutafika, wahenga walisema FOOLS LEARN FROM THEIR OWN MISTAKES BUT WISE MAN LEARN FROM OTHER PEOPLES MISTAKES.

Halfu jambo lingine, naona kama jamii firum interface imebadilishwa nina (maana muonekano) lakini mbona haya majina ya wachangiaji yamefifia sana hiyo text nyusei kwenye blue background haisomeki au wenzangu mnaonaje (tutoe kwanza boriti kwenye macho yetu ndipo tutaona vibanzi kwenye TV za wenzetu)
asanteni
 
Back
Top Bottom