Tuzitambue tofauti za vyama vya upinzani (ACT, CHADEMA, CUF, nk) na Wanaharakati

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,879
35,881
Vyama vya upinzani na wanaharakati ni makundi mawili tofauti yenye mwonekano wa kufanana lakini kiuhalisia ni yenye kutofautiana sana. Yote mawili hujinasibu kumtumikia mwananchi kwenye agenda za ukombozi, ila yakiwa na malengo tofauti.

Kwenye muktadha wa siasa za hapa kwetu, agenda kuu ni ukombozi, yaani mabadiliko. Kwa muktadha huo vyama vyote vya upinzani ni wanaharakati. Uanaharakati wa chama hukoma kikiingia madarakani japo baadhi ya wanachama wake wanaweza kuendelea kuwa Wanaharakati..

Vyama vinaundwa na wanasiasa wenye malengo yao likiwamo la kushika dola. Wanaharakati (usu) malengo yao ni mabadiliko. Mabadiliko hayana mwisho.

Kwenye vyama kuna wanasiasa. Si kila mwanaharati ni mwanasiasa. Pia si kila mwanasiasa ni mwanaharakati. Uanaharakati wa mtu haukomi, bali uanaharakati wa vyama hukoma.

Wanasiasa wa upinzani na Wanaharakati hujinasibu kwa wananchi kuwa wanawakilisha matakwa yao, yaani agenda zao. Wawili hawa wanapata uhalali wa uwepo wao (relevance) kutokea kwa wananchi.

Kwa sababu wanasiasa na wanaharakati huwa na malengo tofauti, si nadra makundi haya kusigana.

"Tuzitambue tofauti zao:"

1. Mwanaharakati wa kudumu:

a) Kwenye katiba mpya na bandari: Atataka katiba mpya sasa. Biashara ya bandari haipo, sasa na hata milele.
b). Atasimama na wananchi siku zote.
c). Huyu si kigeugeu. Agenda za wananchi kwake ni za kudumu.
d). Akiitisha maandamano atakuwapo mstari wa mbele. Yuko tayari kufa au hata kufungwa badala au kwa niaba ya wananchi wake.
e) Siyo mnafki, ni muwazi na anachosema au ukimwangalia, (usoni) ana maanisha.
f) Ni kipenzi cha watu.
g) Hushawishi kwa nguvu za hoja si kwa hoja za nguvu.
h) Huyu huwa na wafuasi wa dhati, siyo wafuasi wa kulipwa (chawa). Hoja zake zajiuza. Hahitaji kukingiwa kifua.
I) Amedhamiria. Lugha yake, adui huielewa Kwa ukamilifu wake.

2. Mwanasiasa (asiyekuwa mwanaharakati wa kudumu)

a) Atasimama na suala la katiba au bandari au lolote la wananchi kama ana maslahi nalo binafsi tu. Humo yakiwemo maslahi kiuchumi na ki madaraka.
b) Husimama na wananchi anapoona kuna maslahi yake binafsi yaliyo wazi kwa wakati huo au yaliyo fiche.
c) Huyu gia kubadlika angani ni kawaida.
d) Agenda kipaumbele huwa ni maslahi binafsi. Za wananchi huwa ni kisingizio tu ambazo nazo hutumika kama daraja.
e) Huyu anachosema si lazima kuwa ana maanisha.
f) Hayuko tayari kuwa sehemu ya gharama za ukombozi ikiwamo kufa au kufungwa, yeye au jamaa zake. Huhamasisha wengine kuwa tayari kulipa gharama hizo.
g) Demokrasia kwake mtihani. Yaani alichoona yeye ndiyo masimamo. Haambiliki.
h) Huyu si nadra kuwa na wafuasi wa kulipwa, kumkingia kifua hata bila ya kuwa na hoja.
I) Anampenda mwanaharakati asiyejitambua Ili kumtumia Ili kuyafikia malengo yake.

Zingatia:

"Ni kwa usahihi kabisa anaposema Samia kuwa hata huko vyamani hali si shwari. Kwamba ukiwapa nafasi ya kuunda serikali, wengine humo watageuka na kuanza kuwapinga wenzao."

Bila shaka akimaanisha, pia kina Mpina, Polepole, Bashiru, nk huko kwao, CCM.

Mwanaharakati kamili ni wa kudumu kama Almasi.

Diamonds are forever!

Nyuzi mbili hIzi zinahusika:

1. "Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu"

2. "Upinzani - walio waoga (cowards) si Wafuasi"
 
Vyama vya upinzani na wanaharakati ni makundi mawili tofauti yenye mwonekano wa kufanana lakini kiuhalisia ni yenye kutofautiana sana. Yote mawili hujinasibu kumtumikia mwananchi (yule yule) kwenye agenda za ukombozi, ila yakiwa na malengo tofauti.

Kwenye muktadha wa siasa za hapa kwetu, agenda kuu ni ukombozi, yaani mabadiliko. Kwa muktadha huo vyama vyote vya upinzani ni wanaharakati. Uanaharakati wa chama hukoma kikiingia madarakani japo baadhi ya wanachama wake wanaweza kuendelea kuwa Wanaharakati..

Vyama vinaundwa na wanasiasa wenye malengo yao likiwamo la kushika dola. Wanaharakati (usu) malengo yao ni mabadiliko. Mabadiliko hayana mwisho.

Kwenye vyama kuna wanasiasa. Si kila mwanaharati ni mwanasiasa. Pia si kila mwanasiasa ni mwanaharakati. Uanaharakati wa mtu haukomi, bali uanaharakati wa vyama hukoma.

Wanasiasa wa upinzani na Wanaharakati hujinasibu kwa wananchi kuwa wanawakilisha matakwa yao. Yaani agenda. Wawili hawa wanapata uhalali wa uwepo wao (relevance) kutokea kwa wananchi.

Kwa sababu wanasiasa na wanaharakati huwa na malengo tofauti, si nadra makundi haya kusigana.

"Tuzitambue tofauti zao tokea kwenye agenda zetu pendwa zilizopo mezani kwa sasa za kutaka katiba mpya na bandari zetu:"

1. Mwanaharakati wa kudumu:

a) Atataka katiba mpya sasa. Kwenye suala la biashara ya bandari halipo sasa nahata milele.
b). Mwanaharakati atasimama na wananchi siku zote.
c). Mwanaharakati si kigeugeu. Agenda za wananchi kwake ni za kudumu.
d). Akiitisha maandamano atakuwapo mstari wa mbele. Yuko tayari kufa au hata kufungwa badala au kwa niaba ya wananchi.
e) Siyo mnafki, ni muwazi na anachosema au ukimwangalia ana maanisha.
f) Ni kipenzi cha watu.
g) Hushawishi kwa nguvu za hoja si kwa hoja za nguvu.
h) Huyu huwa na wafuasi wa dhati, siyo wafuasi wa kulipwa (chawa). Hoja zake zajiuza. Hahitaji kukingiwa kifua.
I) Amedhamiria. Lugha yake, adui huielewa.

2. Mwanasiasa (asiyekuwa mwanaharakati wa kudumu)

a) Atasimama na suala la katiba au bandari au lolote la wananchi kama ana maslahi nalo binafsi tu. Humo yakiwemo maslahi kiuchumi na ki madaraka.
b) Husimama na wananchi anapoona kuna maslahi yake binafsi yaliyo wazi kwa wakati huobau yaliyo fiche.
c) Huyu gia kubadlika angani ni kawaida.
d) Agenda huwa ni maslahi binafsi. Za wananchi huwa ni kisingizio tu ambazo hutumika kama daraja.
e) Huyu anachosema si lazima kuwa ana maanisha.
f) Hayuko tayari kuwa sehemu ya gharama za ukombozi ikiwamo kufa au kufungwa, yeye au jamaa zake. Huhamasisha wengine kuwa tayari kulipa gharama hizo.
g) Demokrasia kwake mtihani. Yaani alichoona yeye ndiyo masimamo. Haambiliki.
h) Huyu si nadra kuwa na wafuasi wa kulipwa, kumkingia kifua hata bila kuwa na hoja.
I) Anampenda mwanaharakati asiyejitambua Ili kumtumia Ili kuyafikia malengo yake.

Zingatia:

"Ni kwa usahihi kabisa anaposema Samia kuwa hata huko vyamani hali si shwari. Kwamba ukiwapa nafasi ya kuunda serikali, wengine humo watageuka na kuanza kuwapinga wenzao."

Bila shaka akimaanisha, pia kina Mpina, Polepole, Bashiru, nk huko kwao, CCM.

Mwanaharakati kamili ni wa kudumu kama Almasi.

Diamonds are forever!

Nyuzi mbili hIzi zinahusika:

1. "Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu"

2. "Upinzani - walio waoga (cowards) si Wafuasi"
Kama vile umemtaja kiongozi fulani wa chama cha upinzani
 
Kama vile umemtaja kiongozi fulani wa chama cha upinzani

Mada inawataja watu wote kwenye siasa. Kumbuka CCM ilikuwa chama cha harakati iliyokoma baada ya kuingia madarakani.

Humo wote wamo hadi kina Msukuma.

Hawamo waganga wa kienyeji, wana michezo, na wowote wasiokuwa na cha kufanya na siasa.

Hivyo usijifagilie ndugu. Kwani una u maalumu gani hadi upate fursa hIyo adhimu ya kupigiwa promo kukutambulisha popote?
 
😂 😂 Amemtaja Mtaalamu wa kubadili gia angani....Kwakweli ana kipaji.

Uchambuzi ni standard, world wide and across the board. Uchambuzi haumlengi mtu. Ila kwenye uchambuzi kila mtu ana fit kwenye nafasi yake. Hapo ni Kila mtu Kwa maana yake halisi.

Hawezi kujificha mtu. Hapo ni mwendo wa kuangalia tu niko wapi. Si Samia, Majaliwa, Cheyo, Tulia, Lissu, Mwabukusi, Slaa, Zitto, Kitilla, nk.

Wanaharakati wa kudumu ni kama Nyerere, Mtikila, Maalim Seif, Mandela, Tutu, Raila, nk. Hawa wakiita Maandamano watu wanamwagika mtaani. Si vinginevyo:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Nyerere aliendelea kuwa mwanaharakati hata baada ya kushika dola. Ndiyo maana aliendeleza juhudi za ukombozi Afrika, hata baada ya kushika dola.

Nyerere au mwanaharakati wa kudumu yeyote (baina ya hao) angekuwapo:

1. Angepinga Urusi kuivamia Ukraine.
2. Angeiunga mkono Marekani mgogoro wa Ukraine.
3. Angeiunga mkono HAMAS kwenye mapambano yake na Israel siku zote.
4. Angepinga mauaji ya wa Israel kwa wapalestina siku zote.
5. Angepinga uvamizi wa muda mrefu wa Israel wa maeneo ya Palestina ambacho ndicho chanza cha mgogoro huu.
6. Nk, nk.

Ni kama ilivyo hapa:

Kama tunataka Katiba Mpya, Tusiionee "Haya" Haki ya awaye yote

Si nadra kwa wale wengine kuwa unprincipled. Huwezi kuwatabiri kuwa watasema je, labda uwaulize. Haki kwao si kitu. Bali kwenye migogoro wao ni ushabiki mwingine kama wa Simba na Yanga tu.
 
Back
Top Bottom