Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,162
Baada ya Mwenyekiti wa Chadema kuutangazia Umma kuwa chama chake kinategemea kufanya maandamano ya amani jijini Dar tarehe 24 mwezi huu, kama kawaida viliibuka baadhi ya vyama, wakiongozwa na CCM kuyapinga maandamano hayo.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti Freeman Mbowe, maandamano hayo ya amani, yalikuwa na madhumuni yafuatayo:-
1. Kuitaka serikali kuiondosha miswada 3 ya uchaguzi, ambayo hivi sasa imefikishwa bungeni, kutokana na wananchi walio wengi, kutosikikilizwa hoja zao.
2. Kuwataka serikali kuangalia gharama za maisha, zinazopanda kila kukicha, zikiwemo bei za sukari, bei ya nauli na gharama nyingine, wakati kipato cha mtanzania, kimebaki palepale.
3. Serikali hii ya CCM iweze kuondoa matumizi ya anasa katika serikali yake, wakati wananchi walio wengi, wakiishi katika maisha ya ufukara wa kutisha!
Kwanza aliibuka Mkuu wa Mkoa wa Dar, Albert Chalamila, aliyedai kuwa askari wa JWTZ zaidi ya 8,000 na askari 5,000 wa Jeshi la Polisi, siku hiyo iliyotangazwa maandano, tarehe 24, watashiriki kufanya usafi jijini Dar
Sikushangazwa na kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar kuyapinga maandamano hayo, kwa kuwa ni kawaida ya viongozi wa CCM, kutumia mbinu hiyo ya kuwatisha wananchi wake, kila pale yanapotangazwa maandamano ya amani.
Hata hivyo ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 18(1)(2) maandamano hayo ya amani yanaruhusiwa kwa mujibu wa Katiba hiyo.
Lakini kilichonishangaza zaidi, ni pale vyama 13 vinavyojiita ni vya upinzani, kujitokeza hadharani na kuyapinga maandamano hayo ya amani!
Niviulize hivyo vyama vinavyojiita ni vyama vya upinzani (wakati katika hali halisi, hivyo vyama tunapaswa kuviita ni CCM -B) je nyinyi hamuoni hoja za msingi zikizotolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ya kuitaka serikali hii ya CCM, kutafakari kwa makini jinsi wanavyotutawala, kwa kuwa hivi sasa, maisha ni magumu mno kwa mwananchi wa kawaida, kutokana na kupandisha kila wakati gharama za maisha, mathalani kupanda kwa bei ya sukari na kupanda kwa nauli za mabasi na kukatika kwa umeme bila mpangilio?
Najua kuwa chama tawala kina mbinu nyingi, zikiwemo za kugawa (maokoto) kwa baadhi ya vyama vya upinzani, ili ionekane, hizo hoja zilizotolewa na Chadema, zionekane kuwa siyo za watanzania walio wengi.
Hata hivyo baada ya maandamano hayo ya amani ya Chadema, kufanikiwa sana hapo jana, vyama hivyo vinavyojiita vya upinzani, vijaandalie makaburi yao, kwa kuwa wananchi tumebaini kuwa, wao si watetezi wetu, badala yake, vimeungana na CCM, katika kuyaangamiza maisha ya umma wa watanzania wanyonge!
Mungu ibariki Tanzania
Kwa mujibu wa Mwenyekiti Freeman Mbowe, maandamano hayo ya amani, yalikuwa na madhumuni yafuatayo:-
1. Kuitaka serikali kuiondosha miswada 3 ya uchaguzi, ambayo hivi sasa imefikishwa bungeni, kutokana na wananchi walio wengi, kutosikikilizwa hoja zao.
2. Kuwataka serikali kuangalia gharama za maisha, zinazopanda kila kukicha, zikiwemo bei za sukari, bei ya nauli na gharama nyingine, wakati kipato cha mtanzania, kimebaki palepale.
3. Serikali hii ya CCM iweze kuondoa matumizi ya anasa katika serikali yake, wakati wananchi walio wengi, wakiishi katika maisha ya ufukara wa kutisha!
Kwanza aliibuka Mkuu wa Mkoa wa Dar, Albert Chalamila, aliyedai kuwa askari wa JWTZ zaidi ya 8,000 na askari 5,000 wa Jeshi la Polisi, siku hiyo iliyotangazwa maandano, tarehe 24, watashiriki kufanya usafi jijini Dar
Sikushangazwa na kauli hiyo ya Mkuu wa Mkoa wa Dar kuyapinga maandamano hayo, kwa kuwa ni kawaida ya viongozi wa CCM, kutumia mbinu hiyo ya kuwatisha wananchi wake, kila pale yanapotangazwa maandamano ya amani.
Hata hivyo ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya mwaka 1977, ibara ya 18(1)(2) maandamano hayo ya amani yanaruhusiwa kwa mujibu wa Katiba hiyo.
Lakini kilichonishangaza zaidi, ni pale vyama 13 vinavyojiita ni vya upinzani, kujitokeza hadharani na kuyapinga maandamano hayo ya amani!
Niviulize hivyo vyama vinavyojiita ni vyama vya upinzani (wakati katika hali halisi, hivyo vyama tunapaswa kuviita ni CCM -B) je nyinyi hamuoni hoja za msingi zikizotolewa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ya kuitaka serikali hii ya CCM, kutafakari kwa makini jinsi wanavyotutawala, kwa kuwa hivi sasa, maisha ni magumu mno kwa mwananchi wa kawaida, kutokana na kupandisha kila wakati gharama za maisha, mathalani kupanda kwa bei ya sukari na kupanda kwa nauli za mabasi na kukatika kwa umeme bila mpangilio?
Najua kuwa chama tawala kina mbinu nyingi, zikiwemo za kugawa (maokoto) kwa baadhi ya vyama vya upinzani, ili ionekane, hizo hoja zilizotolewa na Chadema, zionekane kuwa siyo za watanzania walio wengi.
Hata hivyo baada ya maandamano hayo ya amani ya Chadema, kufanikiwa sana hapo jana, vyama hivyo vinavyojiita vya upinzani, vijaandalie makaburi yao, kwa kuwa wananchi tumebaini kuwa, wao si watetezi wetu, badala yake, vimeungana na CCM, katika kuyaangamiza maisha ya umma wa watanzania wanyonge!
Mungu ibariki Tanzania