Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 21,498
- 37,792
Muda mfupi uliopita kabla ya mechi ya CHAN 2021 kati ya Zambia na Tanzania, kama ilivyo ada zimepigwa nyimbo za Taifa za mataifa hayo mawili.
Umetangulia wimbo wa Taifa la Zambia na umepigwa wote kama ulivyo, lakini ilipofika zamu ya wimbo wa Tanzania wenye beti 2 umepigwa ubeti mmoja tu na kwa vile umepigwa kwa ala hatujui ni ubeti gani kati ya ubeti wa kwanza na wa pili. Wakati wachezaji na viongozi wakianza ubeti wa pili ghafla vyombo vikazimwa na ukawa mwisho wa wimbo.
Ninachotaka kusema hapa ni kwa nini wimbo wetu wa Taifa upigwe ubeti mmoja pekee? Je, hili ni la makusudi au menejimenti ya CAF inajua wimbo wetu wa Taifa una ubeti mmoja?
Umetangulia wimbo wa Taifa la Zambia na umepigwa wote kama ulivyo, lakini ilipofika zamu ya wimbo wa Tanzania wenye beti 2 umepigwa ubeti mmoja tu na kwa vile umepigwa kwa ala hatujui ni ubeti gani kati ya ubeti wa kwanza na wa pili. Wakati wachezaji na viongozi wakianza ubeti wa pili ghafla vyombo vikazimwa na ukawa mwisho wa wimbo.
Ninachotaka kusema hapa ni kwa nini wimbo wetu wa Taifa upigwe ubeti mmoja pekee? Je, hili ni la makusudi au menejimenti ya CAF inajua wimbo wetu wa Taifa una ubeti mmoja?