Eee Mungu baba wa rehema, asante kwa kuwa wewe ni mwema. Mungu/Allah/Yehova/Jah tumekuja kwako kukuomba yafuatayo.
Mola tunakuomba UWALAANI wale wote wanaojifanya kumuenzi Baba wa Taifa, huku wakijua fika ni longolongo tu, ndio hao hao walilivunja Azimio la Arusha, ndio hao hao wamechanganya siasa na biashara, ndio hao hao wamejimilikisha ranchi zilizoanzishwa na baba wa taifa, ndio hao hao wameleta ubaguzi katika elimu, leo tuna shule za Kanumba aka Msondo na FM Academia, Ee Mungu walaani!
Allah tunakuomba UWALAANI wale wote wanaoapa kwa kutumia kitabu chako kitakatifu (Biblia/Quran) kudai kwamba watailinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wakati huo huo baada ya kiapo wanafanya kinyume na kiapo! Ndio hao wanawalinda wavunja sheria kwa madai eti suala la Deepgreen, Meremeta ni masuala nyeti ya kiusalama ambayo hayafai kujadiliwa na Bunge, eti wanapata tabu na nyaraka mbali mbali za kutoa miongozo kuelekea uchanguzi, eti kwa kisingizio nchi yetu ni Secular State, wanasahau kwamba demokrasia sio Secular!
Yehova tunaomba washindwe na walegee, eti wanaogopa hata tangazo la Sidanganyiki wamefikia mahali wanalipiga marufuku, eti hawataki wananchi wapewe elimu ya uraia, taasisi nyingi zimenyimwa vibali vya kuendesha civic education mikoani bila sababu za msingi, eee Yehova tunaomba washindwe na walegee na watoe hivyo vibali!
Mungu tunakuomba upumbaze akili zao hasa wale ambao wana nia chafu ya kutaka kununua/kuhonga vyombo vya habari au waandishi ambao ni critical, watie uzuzu ili washindwe kufanya hivyo, tazama Mungu kwa takribani muongo mmoja tumepoteza waandishi ambao walikuwa very critical pamoja na vyombo vya habari. Ee Mungu watie uzuzu!
Mola tunakuomba uwatie UBUBU wale wanaojifanya nao wanapinga ufisadi huku moyoni wanabariki na kuwalinda mafisadi. Ni hao hao walikuja juu na kuikandia LIST OF SHAME iliyotajwa na Dr. Slaa pale Mwembeyanga, ndio hao hao walitishia eti kufungua mashtaka kwamba wamekashfiwa, ndio hao hao waliwaandalia wanaotuhumiwa kwa ufisadi mapokezi ya kishujaa katika majimbo yao, twakuomba MUNGU uwatie UBUBU pindi watakapojaribu kuzungumzia ufisadi kinafiki.
Endeleza sala hii .
Mola tunakuomba UWALAANI wale wote wanaojifanya kumuenzi Baba wa Taifa, huku wakijua fika ni longolongo tu, ndio hao hao walilivunja Azimio la Arusha, ndio hao hao wamechanganya siasa na biashara, ndio hao hao wamejimilikisha ranchi zilizoanzishwa na baba wa taifa, ndio hao hao wameleta ubaguzi katika elimu, leo tuna shule za Kanumba aka Msondo na FM Academia, Ee Mungu walaani!
Allah tunakuomba UWALAANI wale wote wanaoapa kwa kutumia kitabu chako kitakatifu (Biblia/Quran) kudai kwamba watailinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wakati huo huo baada ya kiapo wanafanya kinyume na kiapo! Ndio hao wanawalinda wavunja sheria kwa madai eti suala la Deepgreen, Meremeta ni masuala nyeti ya kiusalama ambayo hayafai kujadiliwa na Bunge, eti wanapata tabu na nyaraka mbali mbali za kutoa miongozo kuelekea uchanguzi, eti kwa kisingizio nchi yetu ni Secular State, wanasahau kwamba demokrasia sio Secular!
Yehova tunaomba washindwe na walegee, eti wanaogopa hata tangazo la Sidanganyiki wamefikia mahali wanalipiga marufuku, eti hawataki wananchi wapewe elimu ya uraia, taasisi nyingi zimenyimwa vibali vya kuendesha civic education mikoani bila sababu za msingi, eee Yehova tunaomba washindwe na walegee na watoe hivyo vibali!
Mungu tunakuomba upumbaze akili zao hasa wale ambao wana nia chafu ya kutaka kununua/kuhonga vyombo vya habari au waandishi ambao ni critical, watie uzuzu ili washindwe kufanya hivyo, tazama Mungu kwa takribani muongo mmoja tumepoteza waandishi ambao walikuwa very critical pamoja na vyombo vya habari. Ee Mungu watie uzuzu!
Mola tunakuomba uwatie UBUBU wale wanaojifanya nao wanapinga ufisadi huku moyoni wanabariki na kuwalinda mafisadi. Ni hao hao walikuja juu na kuikandia LIST OF SHAME iliyotajwa na Dr. Slaa pale Mwembeyanga, ndio hao hao walitishia eti kufungua mashtaka kwamba wamekashfiwa, ndio hao hao waliwaandalia wanaotuhumiwa kwa ufisadi mapokezi ya kishujaa katika majimbo yao, twakuomba MUNGU uwatie UBUBU pindi watakapojaribu kuzungumzia ufisadi kinafiki.
Endeleza sala hii .