Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 6,376
- 6,720
umekuwa na hisia hata minyukano baina ya wapenzi na wapinzani wa Kikwete na CCM yake. Wapinzani wanajitahidi kumshauri huku wapenzi wake wakijitahidi kuonyesha kuwa kufanya hivyo ni kumchukia huku wapinzani wakisema ni kumpenda. Je wewe kama mwana JF unalionaje hili?
Mfano, Kikwete ameshauriwa na wapinzani aache kukwepa matatizo na kukimbilia nje huku mashabiki zake wakisema safari zake za kuombaomba ni neema kwa taifa. Kikwete ameshauriwa kuachana na style yake ya kutawala kwa kutumia autopilot huku watu wake wakisema anachofanya ni uungwana. Kikwete ameshauriwa abadili kauli mbinu yake ya maisha bora kwa watu ambayo yametafsiriwa na wapinzani kama maisha bora kwa wote walio wake na chama chake.
Kikwete ameshauriwa aachane na mitandao ya kifisadi na kuwahudumia wananchi. Wapinzani wake wanasema muda unamwacha mkono.
Je wewe unasemaje? Ni mapenzi au chuki hata umbea au uzalendo?