Tundu Lissu Umepotoka!

Muundo wa muungano uko "flawed" na hilo linaeleweka. Muundo si mbaya kwa sababu muundo wa serikali mbili hauwezekani, la hasha; muundo ni mbaya kwa sababu walio madarakani wamekataa kuufanyia kazi muundo huo kuurekebisha. Mambo mawili muhimu sana ambayo hayajawekewa mipaka vya kutosha na ambayo yatakuja kuusambaratisha huu muungano ni yafuatayo;
  • Mambo yasiyokuwa ya muungano kwa upande wa bara kushughulikiwa na serikali ya muungano bila muongozo wa aina yoyote (yaani inategemea busara ya viongozi waliopo) - Yaani hapa assumption ni kuwa siku zote rais wa muungano atatokea bara. Siku akitokea rais Zanzibar, G55 mpya itazaliwa na Mwalimu wa kuisambaratisha hatakuwepo - Muungano utatumbukia kaburini
  • Nafasi ya Serikali ya mapinduzi zanzibar na rais wa Zanzibar ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano ni ipi? Hapa kumekuwa na kufunga bandeji kidonda mara kwa mara bila kukitafutia tiba ya kudumu. Kila ikijitokeza migogoro hapa na pale wakubwa wanakubaliana makubaliano ya behind scenes ambayo mengi yanaishia watu kupewa vyeo vikubwa vikubwa bila kuweka wazi hasa makubaliano yalikuwa ni nini! Katika mambo ya muungano na ndani ya serikali ya muungano rais wa Zanzibar hatakiwi kupewa hadhi ya urais wa zanzibar - wakati wa karume alisimama kama makamu wa Rais. Sasa hivi ni waziri asiye na wizara ......... haha; hapa pana mushkeli sana tu!
Sasa mambo haya hatutaki kuyafanyia kazi na ukiangalia kwa undani sana haya ndo mara nyingi yamekuwa yakiibuka hapa na pale. Enzi za mwalimu, alikuwa akitumia nguvu za hoja na wakati mwingine hoja za nguvu; ila kwa sababu alikuwa ni mwalimu haya mambo aliyaweza. Lakini kwa hali ilivyo sasa hivi na upepo wa kisiasa unavyovuma kote visiwani na bara, huu muungano uko ICU. Unatakiwa mjadala utakaoyafumua hayo mambo na kuyaweka wazi ili mipaka iwe wazi.

Lakini mpango wa wanasiasa wetu wengi dhaifu dhaif imekuwa ni kuahirisha matatizo. Wengi wanasema "haya hata mwalimu yalimshinda". Hakuna kingozi yeyote ambaye ameonesha nia na mwenye uwezo wa kuyashughulikia mambo hayo makubwa mawili. Approach imekuwa ni kuahirisha matatizo na kutarajia yatajimaliza yenyewe, tujue kwa uhakika kabisa haya mambo hayatajimaliza yenyewe! Au yakijimaliza yenyewe yatajimaliza kwa njia ambayo wengi wetu hatutarajii.
 
muungno kama haujabadilishwa hauna maana kwa tanganyika.wazanzibar wanafaida wanayoipata ambayo si halali,gusa hayo maslahi uone wanavyolalamika.
muungano ndio umetufanya wabara tuishi zanzibar na tuna haki zetu katiba zote zinataka uishi mahali popote bila kuvunja sheria.bara wameishi zanzibar kwa hofu wamevunjiwa vibanda,wamechomewa bar ambazo ziko kisheria na zinalipa kodi.bara tumenyamaza.
wabunge wa zanzibar wanakuja bungeni wanalipwa hela ambayo si haki,wanalala baduel guest house chumba kimoja watu wawili kinyume na sheriabado tupo kimya tu leo barubaru na mwezio mnakuja na utumbo kwa sababu mmepewa midomo ya kuongea?
wabara tuna akili na mkituudhi tubadilike,nyie sio watu nimetembelea znz ni wabinafsi,mnaoangalia mambo madogo yasiyo na tija.
kifupi muungano ufe tu.
 
muungno kama haujabadilishwa hauna maana kwa tanganyika.wazanzibar wanafaida wanayoipata ambayo si halali,gusa hayo maslahi uone wanavyolalamika.
muungano ndio umetufanya wabara tuishi zanzibar na tuna haki zetu katiba zote zinataka uishi mahali popote bila kuvunja sheria.bara wameishi zanzibar kwa hofu wamevunjiwa vibanda,wamechomewa bar ambazo ziko kisheria na zinalipa kodi.bara tumenyamaza.
wabunge wa zanzibar wanakuja bungeni wanalipwa hela ambayo si haki,wanalala baduel guest house chumba kimoja watu wawili kinyume na sheriabado tupo kimya tu leo barubaru na mwezio mnakuja na utumbo kwa sababu mmepewa midomo ya kuongea?
wabara tuna akili na mkituudhi tubadilike,nyie sio watu nimetembelea znz ni wabinafsi,mnaoangalia mambo madogo yasiyo na tija.
kifupi muungano ufe tu.

Nilipo RED.

Kama maneno yako ni sahihi. Kwanini WA TNG mnaulinda tena kwa nguvu zote huo muungano?
Je kuna siri gani hapo?
 
Back
Top Bottom