Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati huna muda mrefu tangu uteuliwe na Mhe. Rais kuwa Waziri wa Nishati. Tunaona mambo mazuri yanakuja mbeleni. Niko hapa Mwanza tulikuwa tunakatiwa umeme tangu saa moja asubuhi mpaka saa moja jioni au tangu saa moja jioni mpaka saa nane usiku lakini leo ni siku ya tatu umeme haujazimwa katika eneo langu. Ahsante sana Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Lisemwalo lipo na yaliyokuwa yanasemwa kuhusu mtangulizi wako yawezekana ni ya kweli. Jitahidi ili suala la ukosefu wa umeme uwe wa historia.