Peter Stephano 809
Senior Member
- Feb 29, 2020
- 120
- 162
Nguvu kubwa iliyotumika kuusaka ubunge kwa mbunge wa Mbeya mjini DK. Tulia Ackson iliwaaminisha wengi kuwa ndiyo itakua dhamira ya utendaji ofisini pindi atakapopata idhini hiyo.
Ndoto ya kuusaka ubunge ikatimia katika uchaguzi mkuu wa Mwezi Oktoba 2020 kwa kushinda ubunge wa Mbeya mjini pamoja na baraza la madiwani zaidi ya viti 30 vikienda chama cha mapinduzi.
Baada ya ushindi matarajio yakaanza kujaa miongoni mwa watu wa Mbeya kutokana na cheo alichonacho kitaifa kama Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Imani hiyo ilikuwa zaidi na kuchochea mtazamo mpya kwa wakazi wa Mbeya kwa kuamini kuwa Tulia atafungua milango mipya ya maendeleo ndani ya mji wa Mbeya na mkoa kwa ujumla kwakuwa anashikilia cheo chenye ushawishi kitaifa.
Kwa muda mrefu yaelekea muongo mmoja sasa, mkoa wa Mbeya umetengwa kwenye ajenda za maendeleo kitaifa ingawaje sababu hazijulikani.
Aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati John Magufuli aliwahi kunukuliwa akisema Uwepo wa mbunge wa upinzani jijini Mbeya kwa wakati ule ulikwamisha maendeleo.
Kauli hii ya hayati Magufuli iliwapa watu imani ya mabadiliko wakiamini kuwa baada ya kumchagua Tulia ambae ni wa chama Tawala basi mambo yangebadilika waanze kushuhudia ajenda za maendeleo zikimiminika mkoani Mbeya.
Kwanini Tumzungumzie Tulia kwenye hili?
Kama ilivyoelezwa kwenye utangulizi ni kwamba Tulia alipewa Imani akiwa mbunge wa kuteuliwa na Sasa ni mbunge wa kuchaguliwa hivyo anategemewa kufanya makubwa zaidi.
Jiji la Mbeya ndilo funguo ya mkoa na Ukanda wa nyanda za juu kusini, hivyo maendeleo yake yanainua sehemu nyingine za mkoa Kama Tukuyu, Chunya, Kyela, Mbarali Na nyingine nyingi.
Uwepo wa Tulia uliaminiwa kuwa nuru ya kuvutia wawekezaji kwenye mambo mbalimbali kama vile viwanda, Kilimo, biashara na michezo.
Uwekezaji wa Serikali katika miundombinu na uchukuzi kama vile Barabara, reli na Usafiri wa anga mambo ambayo yanaweza kuchochea maendeleo ya watu na mkoa kwa ujumla.
Prince Mwaihojo ambaye ni msomi na mdau wa maendeleo mkoani Mbeya anasema ndani ya mwaka mmoja kwenye madaraka kama mbunge wa kuchaguliwa Tulia amewekeza kwenye vitu laini ambavyo havina manufaa makubwa kwa maendeleo ya Mbeya kwa miaka ijayo bali kwa manufaa ya kisiasa tu.
Mwaihojo anavitaja vitu hivyo kuwa "Vitu laini" Kama vile ujenzi wa vituo vya mabasi na machinga pamoja na kuendesha matamasha ya utamaduni.
Msomi huyu wa chuo kikuu Cha Oxford Uingereza anasema Wakati wa utawala wa Rais kikwete aliesema kuwa baada ya kuhamisha uwanja wa ndege kutoka mbeya mjini kwenda Songwe basi uwanja huo ungetumika kama chuo Cha kimataifa Cha masuala ya anga.
Anasema ujenzi wa chuo hicho ungevutia uwekezaji mkubwa wa Wageni ambao wangekuja kusoma na ingekua fursa kubwa kwa mkoa kujitangaza kimataifa.
Pia kikwete 2012 alipokuwa akihutubia mkutano wa Wafanyakazi siku ya Mei mosi katika Viwanja vya Sokoine jijini Mbeya alinukuliwa akisema uwanja mpya wa Songwe utakuwa ni uwanja wa kimataifa na usaidie wakulima watoke na matunda Mbeya wakauze uholanzi.
Lakini uongozi wa Tulia hujaweka mkazo kwenye suala hilo na kupelekea eneo uwanja wa zamani kugawiwa kwa wamachinga na ule mpya kubaki kwa matumizi ya ndege za ndani ya nchi na sio kimataifa zaidi kama ulivyo tarajiwa na kikwete.
Pia suala la barabara kuu ya kimataifa ya Tanzania-Zambia ambayo inapita katikati ya mji inaonekana kutokidhi matumizi kwa kusababisha msongamano katikati ya mji na kuwa kero ya mda mrefu kwa watumiaji.
Jambo hili lilifikishwa mbele ya ofisi ya bunge kwa muda mrefu lakini bado hakuna jitihada zilizochukuliwa katika kujenga barabara mpya yenye upana wa kukidhi matumizi.
Mwaka mmoja wa Tulia madarakani bado una deni la kulipa matarajio ya wananchi wengi ambao waliamini kuwa utakuwa suluhisho la mengi.
Licha ya jitihada alizozifanya katika kuwezesha akina mama, Vijana, wazee na walemavu kwa kuwapa mikopo na bajaji mambo haya yanatakiwa kuendelea huku sera mpya za maendeleo ya Mbeya zikisukwa.
Wana Mbeya wanataka kuona Viwanda vinafufuliwa Kama Kiwanda Cha zana za kilimo mbeya, Kiwanda cha Kahawa, Viwanda vya bidhaa mbalimbali vinaanzishwa mkoani Mbeya kupitia Msaada wa SIDO.
Kwa nyakati tofauti Tulia mwenyewe amewahi kulalamikia kutengwa kwa mkoa wa Mbeya katika ajenda za miundombinu kitaifa huku mikoa mingine ikitengewa bajeti kubwa kila mwaka jambo ambalo linavunja hamasa kwa wananchi ambao nao wanalipa kodi.
Muda alio nao ungali bado mrefu zaidi ana nafasi ya kufanya makubwa zaidi iwapo tu ataamka na kutambua ushawishi alio nao kwenye uongozi wa taifa hili katika kuwaletea manufaa Wananchi wa Mbeya mjini pamoja na mkoa kwa ujumla Kama walivyo tarajia.
Peter Mwaihola kitaaluma ni mwandishi wa habari na mchambuzi wa masuala ya siasa na jamii.
Ndoto ya kuusaka ubunge ikatimia katika uchaguzi mkuu wa Mwezi Oktoba 2020 kwa kushinda ubunge wa Mbeya mjini pamoja na baraza la madiwani zaidi ya viti 30 vikienda chama cha mapinduzi.
Baada ya ushindi matarajio yakaanza kujaa miongoni mwa watu wa Mbeya kutokana na cheo alichonacho kitaifa kama Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Imani hiyo ilikuwa zaidi na kuchochea mtazamo mpya kwa wakazi wa Mbeya kwa kuamini kuwa Tulia atafungua milango mipya ya maendeleo ndani ya mji wa Mbeya na mkoa kwa ujumla kwakuwa anashikilia cheo chenye ushawishi kitaifa.
Kwa muda mrefu yaelekea muongo mmoja sasa, mkoa wa Mbeya umetengwa kwenye ajenda za maendeleo kitaifa ingawaje sababu hazijulikani.
Aliyekuwa Rais wa Tanzania hayati John Magufuli aliwahi kunukuliwa akisema Uwepo wa mbunge wa upinzani jijini Mbeya kwa wakati ule ulikwamisha maendeleo.
Kauli hii ya hayati Magufuli iliwapa watu imani ya mabadiliko wakiamini kuwa baada ya kumchagua Tulia ambae ni wa chama Tawala basi mambo yangebadilika waanze kushuhudia ajenda za maendeleo zikimiminika mkoani Mbeya.
Kwanini Tumzungumzie Tulia kwenye hili?
Kama ilivyoelezwa kwenye utangulizi ni kwamba Tulia alipewa Imani akiwa mbunge wa kuteuliwa na Sasa ni mbunge wa kuchaguliwa hivyo anategemewa kufanya makubwa zaidi.
Jiji la Mbeya ndilo funguo ya mkoa na Ukanda wa nyanda za juu kusini, hivyo maendeleo yake yanainua sehemu nyingine za mkoa Kama Tukuyu, Chunya, Kyela, Mbarali Na nyingine nyingi.
Uwepo wa Tulia uliaminiwa kuwa nuru ya kuvutia wawekezaji kwenye mambo mbalimbali kama vile viwanda, Kilimo, biashara na michezo.
Uwekezaji wa Serikali katika miundombinu na uchukuzi kama vile Barabara, reli na Usafiri wa anga mambo ambayo yanaweza kuchochea maendeleo ya watu na mkoa kwa ujumla.
Prince Mwaihojo ambaye ni msomi na mdau wa maendeleo mkoani Mbeya anasema ndani ya mwaka mmoja kwenye madaraka kama mbunge wa kuchaguliwa Tulia amewekeza kwenye vitu laini ambavyo havina manufaa makubwa kwa maendeleo ya Mbeya kwa miaka ijayo bali kwa manufaa ya kisiasa tu.
Mwaihojo anavitaja vitu hivyo kuwa "Vitu laini" Kama vile ujenzi wa vituo vya mabasi na machinga pamoja na kuendesha matamasha ya utamaduni.
Msomi huyu wa chuo kikuu Cha Oxford Uingereza anasema Wakati wa utawala wa Rais kikwete aliesema kuwa baada ya kuhamisha uwanja wa ndege kutoka mbeya mjini kwenda Songwe basi uwanja huo ungetumika kama chuo Cha kimataifa Cha masuala ya anga.
Anasema ujenzi wa chuo hicho ungevutia uwekezaji mkubwa wa Wageni ambao wangekuja kusoma na ingekua fursa kubwa kwa mkoa kujitangaza kimataifa.
Pia kikwete 2012 alipokuwa akihutubia mkutano wa Wafanyakazi siku ya Mei mosi katika Viwanja vya Sokoine jijini Mbeya alinukuliwa akisema uwanja mpya wa Songwe utakuwa ni uwanja wa kimataifa na usaidie wakulima watoke na matunda Mbeya wakauze uholanzi.
Lakini uongozi wa Tulia hujaweka mkazo kwenye suala hilo na kupelekea eneo uwanja wa zamani kugawiwa kwa wamachinga na ule mpya kubaki kwa matumizi ya ndege za ndani ya nchi na sio kimataifa zaidi kama ulivyo tarajiwa na kikwete.
Pia suala la barabara kuu ya kimataifa ya Tanzania-Zambia ambayo inapita katikati ya mji inaonekana kutokidhi matumizi kwa kusababisha msongamano katikati ya mji na kuwa kero ya mda mrefu kwa watumiaji.
Jambo hili lilifikishwa mbele ya ofisi ya bunge kwa muda mrefu lakini bado hakuna jitihada zilizochukuliwa katika kujenga barabara mpya yenye upana wa kukidhi matumizi.
Mwaka mmoja wa Tulia madarakani bado una deni la kulipa matarajio ya wananchi wengi ambao waliamini kuwa utakuwa suluhisho la mengi.
Licha ya jitihada alizozifanya katika kuwezesha akina mama, Vijana, wazee na walemavu kwa kuwapa mikopo na bajaji mambo haya yanatakiwa kuendelea huku sera mpya za maendeleo ya Mbeya zikisukwa.
Wana Mbeya wanataka kuona Viwanda vinafufuliwa Kama Kiwanda Cha zana za kilimo mbeya, Kiwanda cha Kahawa, Viwanda vya bidhaa mbalimbali vinaanzishwa mkoani Mbeya kupitia Msaada wa SIDO.
Kwa nyakati tofauti Tulia mwenyewe amewahi kulalamikia kutengwa kwa mkoa wa Mbeya katika ajenda za miundombinu kitaifa huku mikoa mingine ikitengewa bajeti kubwa kila mwaka jambo ambalo linavunja hamasa kwa wananchi ambao nao wanalipa kodi.
Muda alio nao ungali bado mrefu zaidi ana nafasi ya kufanya makubwa zaidi iwapo tu ataamka na kutambua ushawishi alio nao kwenye uongozi wa taifa hili katika kuwaletea manufaa Wananchi wa Mbeya mjini pamoja na mkoa kwa ujumla Kama walivyo tarajia.
Peter Mwaihola kitaaluma ni mwandishi wa habari na mchambuzi wa masuala ya siasa na jamii.