Tumeridhika (Picha)!

Napata taabu kusema kama tumeridhika au tumekata tamaa kwa sababu sina hakika kama tunajitambua na tunajua tunalolitaka.

Shida yangu ni kuwa wale ambao angalau tuko tunapiga mswaki hatujaribu kamwe kuwastua wenzetu. Tunawaongezea blanketi na shuka waendelee kuuchapa usingizi. Kama tungewanyang'anya wakaguswa na baridi kidogo hiyo picha wa wakazi wa Bonde la Mpunga ingekuwa tofauti!

DC, Hebu fafanua zaidi.

Kwa hili suala la usafi/uchafu - kujali/kutokujali nadhani tuna matatizo .Nakumbuka kuna kipindi nilijaribu kuanzisha kampeni ( kama mtu binafsi) ya kusafisha mazingira ya eneo ninaloishi mimi -hivyo vikwazo unavyokumbana navyo usiombe!Lakini tulipelekeshana tu vizuri.

Katika maeneo mengi ya makazi kuna mchanganyiko wa watu wenye fikra tofauti - wapo wenye kujali na kufanya mazingira yao yawe safi - halafu wapo wale wasiojali kabisa na hawa ni wagumu sana kushughulika nao maana wanachojali wao ni mradi kumekucha.Na usipoangalia utaishia kutukanwa mpaka ushangae.Je usafi ni class issue?

Narudi tena kwa wenzetu wapanga miji. Miji/jiji letu lilivyopangwa inashangaza kidogo- kuna mchanganyiko maalum. Utakuta mixture of high,low.medium density plots.jE, NINI mantiki ya huu mchanganyiko? haieleweki kama eneo ni slam au ni affluent surbarb na ujengaji wa nyumba nao unashangaza pia.Tazama maeneo kama Mikocheni,Msasani na hata Mbezi Beach utaona hiyo hali.Inakuwa vigumu sana kuweka madhari nzuri kwa maana huo mchanganyiko wenyewe ni kero.Sijui tufanye nini.
 
Mungu atuipushie mbali na balaa llnaloweza kutokea.
najua watanzania wenagu mmeshachoka,
Ndiyo mmechoka sana kusubiri maisha bora,
mmeendelea kukosa umeme na huduma bora


Mie huw anajiuliza maisha mambaya ya watanzania na huduma mbovu zinasababbishwa na nani?viongozi na wafanyakazi wa serikalini hawajui kuweka kipaumbele katika mabo ya msingi,wanakalia kujiandlaia semina na kujilipa posho.

Mwanakijiji umenikumbusha maneno ya Mwalimu aliyowahi kuyasema,Kipidni cha mwalimu ilikuwa haiwezekani kwa wizara kuongezewa gari jipya bila ya kusema mnataka la nini?ila kwa serikali hii tena hasa hii yenye mabadiliko ya mawaziri kila siku..kilamabadiliko yakifanyiaka waziri anapewa gari jipya.kwa mabadiliko madogo matatu yaliyotokea kuna baadhi ya mawaziri wamepata magari matatu..Yaani kubadilishiwa.Ukiangalia jumla ya magari haya yanakaribia milioni 300.Hii pesa inaweza kabisa kuweka hata huduma nzuriz za maji.

Hivi tumerogwa?
 
Na vipaumbele umeviangalia? Meya wa Ilala amezindua kampeni maalumu ya usafi wiki iliyopita...je Meya wa Kinondoni ana ajenda hii? Je nani anapaswa kuwajibika kwa hicho tunachokiona kwenye picha? ni manispaa, wakazi wa eneo husika? wapita njia au nani?

Umeya wa Bongo ni ulaji siyo kazi!!!!!!!!!!
 
Bado naendelea kufagilia siasa zetu za wa mwaka 47 za Ujamaa na Kujitegemea. Laiti kama mipango ya Ujamaa na Kujitegemea ingelivaliwa njuga na kutekelezwa ipasavyo hizo slums zilizozunguka jiji la Dar na miji mingine inayoendelea kukua zisingelikuwepo.

Marehemu Mzee Bryceson aliyekuwa mbunge wa Kinondoni wakati huo, alianzisha mpango mzuri wa makazi ya wananchi eneo la Sinza. Zilikuwepo ramani nzuri kabisa za kuonyesha mitaa iliyonyooka na jinsi nyumba zinavyotakiwa kujengwa, njia za mitaro ya maji taka na njia za mabomba ya maji safi. Lakini, iangalie Sinza leo kuna vijito visivyokauka ya maji machafu na vijana wenye mikokoteni ya madumu ya maji wakihangaika kuuza maji nyumba hadi nyumba. Bila shaka ile ramani ya Mzee Bryceson ilishaliwa na mchwa kwenye mafaili wizarani na kwenye idara husika, na hakuna alinayejali.

Siku moja nami wa 'jikoni' nilipata bahati ya kwenda Abuja. Mji ule unapendeza kweli kweli, umepangwa vizuri mno. Ni Makao Makuu mapya ya serikali ya Nigeria. Nasikia wakati sie tunaanzisha mpango wetu wa Makao Makuu Dodoma, Serikali ya Nigeria ilituma maafisa wake waje wajifunze kutoka kwetu kuhusu mpango wa kuhamisha makao makuu. Nigeria wakafanikiwa kufanya kweli, sisi hadi leo bado Serikali inapiga chenga kuhamia Dodoma!

Nikirudi kwa niliyoyaona Abuja. wakati wa pitapita tukakuta matingatinga yanabomoa ghorofa moja zuri sana. Tukaambiwa kwamba jengo lile ni jengo la Wizara fulani lakini wajenzi walikosea wakajenga kwenye eneo ambalo ilipaswa kupita barabara kwa hiyo Waziri aliyekuwa akishughulikia Mipango Miji alitoa amri jengo lile libomolewe na likabomolewa!

Yataka moyo na ujasiri wa hali ya juu kuweza kurekebisha makosa yaliyotendeka huko nyuma ili tuweze kuleta maisha bora na salama ya wananchi wa maeneo kama hayo yaliyo kwenye picha.

Nina tabia mbaya ya kurejea mifano ya kale. Wazee wenzangu wanaokumbuka Dar ilivyokuwa baada ya Uhuru watakumbuka kwamba sehemu kama za Magomeni Mapipa, Makanya, Mikumi, Mwembechai, n.k. kulikuwa na nyumba za 'full suit' yaani makuti kutoka juu hadi chini. Zilizokuwa nafuu ni zile za udongo zilizoezekwa na makuti. Waliokuwa na nyumba zilizopigwa bati walikuwa wa kuhesabu.

Serikali ya Nyerere kwa makusudi kabisa iliamua nyumba zote zibomolewe zijengwe nyumba mpya ambazo baada ya kwisha kujrngwa walikabidhiwa wale waliokuwa na nyumba zao za makuti waishi na kupangisha ili waweze kurejesha taratibu fedha za Serikali zilizotumika kuwajenga nyumba hizo. Mpango wa kuwahamisha watu na kuwalipa fidia 'wakajiju' ama wakafie maporini haukuwepo!

Maisha bora gani zaidi ya watu kuishi katika nyumba bora na kwenye mazingira safi?

Tunataka Serikali yoyote itakayotutangazia maisha bora iangalie ubora wa nyumba wanazoishi wananchi wake wa mijini na vijijini ili hata watu wakitinga na pamba zao mitaani na viselula wajulikane kwamba wametoka kwenye mazingira yanayofanana na hizo pamba na viselula.
 
Wapeni CHADEMA Manispaa kama hizi. Mabadiliko yataonekana tu. Nimeona wamefanya kazi nzuri sana TARIME.
\

Hakuna lolote uko wewe...nani kasema...washaanza kulalamika mtu waliye changua...sasa hawezi hata kupanga hoja bungeni,ana kigugumizi....

Bora diwani angekuwa ndio mbunge....ni nini kuwa na hoja harafu ukashidwa kuziwakilisha katika mpangilio...?wangine watasema...ni ugeni..mbona wengine kama zito walipo ingia walianza upiganaji day one....kweli hamna pale...pengo halijazibika.
 
Chakushangaza nikwamba ukitoka kwenye hizo nyumba huchukui hata hatua mia tano uko Shopping plaza. hatua kidogo unakwenda ile Hotel maarufu ya mhindi yenye ukumbi mzuri wa sherehe.

Ni Dar hii mnaona bonde la mpunga je wale wanaoishi mabonde ya jangwani.

MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA
 
Na ninaamini kuwa ukienda kuangalia kwenye master plan ya jiji la dar, Bonde la Mpunga halijawa indicated kama eneo la makazi

Nafikiri tukiwa na fikra kuwa maeneo mengine hayafai kwa makazi hapo tunakuwa wavivu wa kufikiri.

Kama WANADAMU dunia ni ya kwetu na tunapaswa kuifanya mahali bora pa kuishi na kimsingi with thinking, planning and designing anywhere, absolutely anywhere makazi yanafaa kuwepo. Hata hapa bonde la mpunga tena ni mahali pazuri sana kwa makazi hata pengine kuliko masaki au oysterbay.

Mfano Netherlands, Amsterdam city ni sehemu ya bahari iliyovunwa kuwa nchi kavu na jiji kujengwa, hapa ilihitajika fikra chanya na planning na hatimaye sasa ni jiji katika majiji makubwa hasa katika nyanja za usafiri wa anga duniani.

Simply anywhere panafaa kwa makazi na ndio maana tunaangalia utaratibu wa kuishsi mars and kwenye mwezi.

KIKUBWA tu ni kuwawezesha wananchi na kuwa karibu nao wanapoanzisha makazi kwa kuwapa msaada wa planning na design, creativity etc pia inahitajika, commitment, kujitolea kwa wataalamu wetu na msukumo na mtazamo kutoka kwa Rais Tawala na sio wataalamu wetu kupenda kwenda mabaa na kuongea deals za kifisadi na kuwa na fikra hasi kuwa maeneo fulani hayafai. Challenge ni kuwa ni jinsi gani eneo fulani litaweza ku-accommodate makazi na tena kwa wingi hasa kwa jiji kama Dar AMBAPO GROWTH RATE NI ALARMING.

Hayo ndiyo yangu chanya tu kwa wanaJF. Lest be positive and anticipate positive changes and development

ADIOS
 
Hali hii inatisha sana ukizingatia nchi yetu ina rasirimali za kutosha kuwasaidia wananchi wake.Ila watu achache wajulikanao kama MAFISADI wameamua kuzikwapua na kuchukua wao wenyewe . majiuliza je haya ndio maisha bora kwa kila Mtanzania? ni bora wananchi wote tungeamua kuwa kama wale jamaa wa akina Chacha wangwe labda kitaeleweka.
 
Sasa hapa tunaweza vipi kubadili hali hii moja kwa wale wanaoishi katika mazingira hayo wana nafasi gani na pili viongozi wa mitaa na serikali wako wapi
 
Hapana bana! hiyo picha siyo Tanzania na wala sio Afrika! Hatuko wala hatuishi hivyo sisi....
 
mtoto.jpg


Mkazi wa Msasani Bonde la Mpunga akipita katika matofali kukwepa maji machafu yatiririka kutoka katika makazi ya watu.(Picha kwa hisani ya Mroki)

My Take:
Picha hii ukiangalia kwa haraka ni kama picha ya kawaida tu ya hali halisi ya maisha ya watu wetu. Lakini ukianza kuiangalia kwa vipande na kuweka focus ya kitu au theme moja moja utaona kuwa inabeba ujumbe mzito kweli.

a. Nyumba
b. Maji machafu
c. Mtu
d. Makazi
e. Umeme
f. Takataka

Kitu kimoja hata hivyo nilicho na mang'amuzi nayo ni kuwa usione mazingira hayo kwa nje, hizo nyumba kwa ndani zina umeme, TV n.k na wakazi wake wanatembea na viselula huku wakitinga pamba za nguvu kila siku wakienda kujobu au kuchakarika. Wakazi wake usishangae kuwaona kwenye matamasha mbalimbali wakiwa wanaburudika na moja moto moja baridi.

Hii picha ina ujumbe mzito sana.

Watanzania tumelogwa kama si kupumbazwa kwa majini. Hayo ni maisha ya kawaida kabisa kwa watanzania na hasa ambao hawapata bahati ya kutoka nje ya Tanzania. Tuna kazi kubwa sana bado inatusubiri mbeleni.
 
Hapana bana! hiyo picha siyo Tanzania na wala sio Afrika! Hatuko wala hatuishi hivyo sisi....

Is one of the best places you can find at Msasani, hali ni mbaya zaidi manzese, temeke, magomeni......., mbaya zaidi ni DSM, sio rahisi sana kupata maeneo kama haya mikoani!!!!

Nyani hapa ni TZ, ni usikute nyumba hiyo ya upande wa kulia kuna mwana JF hapo, ohooo!!

waberoya
 
\

Hakuna lolote uko wewe...nani kasema...washaanza kulalamika mtu waliye changua...sasa hawezi hata kupanga hoja bungeni,ana kigugumizi....

Bora diwani angekuwa ndio mbunge....ni nini kuwa na hoja harafu ukashidwa kuziwakilisha katika mpangilio...?wangine watasema...ni ugeni..mbona wengine kama zito walipo ingia walianza upiganaji day one....kweli hamna pale...pengo halijazibika.


ha ha ha ha haaaaa, he he heeeee, duh hata mwezi haujaisha!!! kwani jamaa si ndiye aliyewashawishi kwenye kampeni wampigie kura; na wakashawishika wakampigia kura, iweje leo waseme hajui kupanga hoja!!! watu bwana..
 
Cha ajabu na cha kushangaza ni kwamba mkazi huyu huyu anayeishi katika maisha haya ya taabu anaichagua CCM kila uchaguzi. Mtu haoni maendeleo yoyote ya maana kwa miaka yote aliyoishi katika mazingira hayo, lakini anashindwa kufanya uamuzi wa busara wa kutumia kura yake kuleta mabadiliko. Hii mpaka lini? CCM imeshindwa kukuletea mabadiliko tangu uhuru. Kwanini usifikirie alternatives nyingine?

Kuna swali huwa najiuliza kila siku. Nani huwa anaichagua CCM? Matajiri waliofaidika na mfumo mbovu wa madaraka ulioko? Wasomi waliosomeshwa bure na serikali? Au walalahoi wasio na uhakika wa mlo wa kesho, matibabu, maji salama, barabara nzuri, nk?
 
Nasikia hapo zilianza nyumba.

Wenye pesa zao wamejenga majumba kwenye mkondo wa mfereji wa maji machafu, hivyo hayo maji yakmekosa uelekeo, ndio ikawa hivyo. Kilio cha wakazi wa bonde la mpunga ni cha muda na hakuna anayesikiliza kwa vile waliosababisha hilo tatizo ni wenye pesa. Si unajua tena Tz ukiwa na pesa basi unakuwa juu ya sheria.
 
DC, Hebu fafanua zaidi.

Kwa hili suala la usafi/uchafu - kujali/kutokujali nadhani tuna matatizo .Nakumbuka kuna kipindi nilijaribu kuanzisha kampeni ( kama mtu binafsi) ya kusafisha mazingira ya eneo ninaloishi mimi -hivyo vikwazo unavyokumbana navyo usiombe!Lakini tulipelekeshana tu vizuri.

Katika maeneo mengi ya makazi kuna mchanganyiko wa watu wenye fikra tofauti - wapo wenye kujali na kufanya mazingira yao yawe safi - halafu wapo wale wasiojali kabisa na hawa ni wagumu sana kushughulika nao maana wanachojali wao ni mradi kumekucha.Na usipoangalia utaishia kutukanwa mpaka ushangae.Je usafi ni class issue?

Narudi tena kwa wenzetu wapanga miji. Miji/jiji letu lilivyopangwa inashangaza kidogo- kuna mchanganyiko maalum. Utakuta mixture of high,low.medium density plots.jE, NINI mantiki ya huu mchanganyiko? haieleweki kama eneo ni slam au ni affluent surbarb na ujengaji wa nyumba nao unashangaza pia.Tazama maeneo kama Mikocheni,Msasani na hata Mbezi Beach utaona hiyo hali.Inakuwa vigumu sana kuweka madhari nzuri kwa maana huo mchanganyiko wenyewe ni kero.Sijui tufanye nini.

Kupiga mswaki sikumaanisha usafi au uchafu! Nililenga wewe na baadhi ya wa WaTZ ambao tayari wameamka ila hawataki kuwasaidia wale ambao hawajaamka ili waamke. Badala yake wanawasaidia wendelee kulala. Huo ndio usaliti wa vijana wetu tuliowapa nafasi ya kuona mwanga!

Suala la usafi ni rahisi sana. Ni kuwa na mipango mizuri tu ya afya ya jamii (public health) na wala hatuhitaji pesa nyingi. Bali tunahitaji watu wanaowajibika na wenye kuelewa kile kinachotakiwa na kukitekeleza. Sasa hivi kila mtu na tumbo lake. Neno jamii lilishakufa au halijazaliwa.
 
Back
Top Bottom