Tumeridhika (Picha)!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
mtoto.jpg


Mkazi wa Msasani Bonde la Mpunga akipita katika matofali kukwepa maji machafu yatiririka kutoka katika makazi ya watu.(Picha kwa hisani ya Mroki)

My Take:
Picha hii ukiangalia kwa haraka ni kama picha ya kawaida tu ya hali halisi ya maisha ya watu wetu. Lakini ukianza kuiangalia kwa vipande na kuweka focus ya kitu au theme moja moja utaona kuwa inabeba ujumbe mzito kweli.

a. Nyumba
b. Maji machafu
c. Mtu
d. Makazi
e. Umeme
f. Takataka

Kitu kimoja hata hivyo nilicho na mang'amuzi nayo ni kuwa usione mazingira hayo kwa nje, hizo nyumba kwa ndani zina umeme, TV n.k na wakazi wake wanatembea na viselula huku wakitinga pamba za nguvu kila siku wakienda kujobu au kuchakarika. Wakazi wake usishangae kuwaona kwenye matamasha mbalimbali wakiwa wanaburudika na moja moto moja baridi.

Hii picha ina ujumbe mzito sana.
 
Na humo wanazaliwa "MAFISADI" watarajiwa wengi tu. Vinginevyo hakuna namna kuondokana na hali hii.
 
Na humo wanazaliwa "MAFISADI" watarajiwa wengi tu.
Na wewe unapenda MAFISADI. Na wengi wametokea huku. Wengine walitokea kwenye nyumba walizochangia na ng'ombe lakini sasa hawawezi tena kuishi humu.
Nani anatakiwa aishi humu zaidi ya mtoto wa mlala hoi
 
Najaribu kufikiria kama kweli wakazi au wamiliki wa nyumba hizi kweli wameridhika au wamekata tamaa. Yawezekana kabisa mtu anayeamka asubuhi kutokea katika moja ya nyumba hizo akawa ni mtu mwenye mawazo mabaya interms of kwanini wao na sio sisi???

Kwa hiyo hata mafisadi wanaozaliwa katika nyumba hizo wanapopata nafasi ya kukamata kamfereji ka ufisadi huwa wananyonya mpaka wanakausha kwani wanaamini ndio njia ya kulipiza na kujifariji.....Nadhani mvua za masika zinapofika hiyo sehemu sijui inakuwa katika hali gani jamani.....Lazima tujiangalie tena kuna tatizo mahali fulani katika utendaji kama sio akili za viranja wetu!!!
 
hulka ya uchafu imetawala fikra za wengi ikiwa ni pamoja na wale wenye dhamana ya kusimamia taratibu na kanuni za usafi wa mazingira. Labda iundwe Tume kuchunguza HALAFU ITOE MAPENDEKEZO NINI KIFANYIKE!..Lol!
 
Najaribu kufikiria kama kweli wakazi au wamiliki wa nyumba hizi kweli wameridhika au wamekata tamaa. Yawezekana kabisa mtu anayeamka asubuhi kutokea katika moja ya nyumba hizo akawa ni mtu mwenye mawazo mabaya interms of kwanini wao na sio sisi???

Kwa hiyo hata mafisadi wanaozaliwa katika nyumba hizo wanapopata nafasi ya kukamata kamfereji ka ufisadi huwa wananyonya mpaka wanakausha kwani wanaamini ndio njia ya kulipiza na kujifariji.....Nadhani mvua za masika zinapofika hiyo sehemu sijui inakuwa katika hali gani jamani.....Lazima tujiangalie tena kuna tatizo mahali fulani katika utendaji kama sio akili za viranja wetu!!!

Eneo hili limo ndani ya Manispaa TAJIRI kabisa hapa Nchini, KINONDONI. Meya wake, Mstahiki Londa, ni mmoja wa matajiri wazawa wa Dar kwa sasa?
 
Eneo hili limo ndani ya Manispaa TAJIRI kabisa hapa Nchini, KINONDONI. Meya wake, Mstahiki Londa, ni mmoja wa matajiri wazawa wa Dar kwa sasa?


Na vipaumbele umeviangalia? Meya wa Ilala amezindua kampeni maalumu ya usafi wiki iliyopita...je Meya wa Kinondoni ana ajenda hii? Je nani anapaswa kuwajibika kwa hicho tunachokiona kwenye picha? ni manispaa, wakazi wa eneo husika? wapita njia au nani?
 
Maeneo mengine yalitakiwa yasiwe makazi ya wananchi. Bonge la Mpunga ni mfano halisi kabisa.

Je, lawama zingine zitupiwe kwa wale vijana wetu tuliowasomesha chuo cha ardhi? Mipango miji ni aje nyinyi?
 
Na vipaumbele umeviangalia? Meya wa Ilala amezindua kampeni maalumu ya usafi wiki iliyopita...je Meya wa Kinondoni ana ajenda hii? Je nani anapaswa kuwajibika kwa hicho tunachokiona kwenye picha? ni manispaa, wakazi wa eneo husika? wapita njia au nani?

Wapeni CHADEMA Manispaa kama hizi. Mabadiliko yataonekana tu. Nimeona wamefanya kazi nzuri sana TARIME.
 
Maeneo mengine yalitakiwa yasiwe makazi ya wananchi. Bonge la Mpunga ni mfano halisi kabisa.

Je, lawama zingine zitupiwe kwa wale vijana wetu tuliowasomesha chuo cha ardhi? Mipango miji ni aje nyinyi?

Na ninaamini kuwa ukienda kuangalia kwenye master plan ya jiji la dar, Bonde la Mpunga halijawa indicated kama eneo la makazi
 
Na ninaamini kuwa ukienda kuangalia kwenye master plan ya jiji la dar, Bonde la Mpunga halijawa indicated kama eneo la makazi


Hapo umegusia tatizo lingine....
vijislams vinajitokeza polepole kila mahali na viongozi wanaangalia na hawasemi kitu.Hivi wahusika wa mipango miji kama mpo humu JF hebu tupeni ufafanuzi ni kwanini hamfanyi kazi yenu kwa makini?As professionals, mnajiskiaje mnapoona jiji/miji mnayopaswa kusimamia inazidi kuharibika siku hadi siku? Na je, hamuoni historia itakuja kuwahukumu maana " landmarks" mnazoacha zitabaki kwenye kumbukumbu? Jirekebisheni jamani!Tusikalie kuwasema viongozi wa kisiasa tu humu JF tujiseme hata sisi wenye taaluma na dhamana.
 
Kuna matatizo katika ngazi zote.

Watawala ni vipofu na kama wanaona hawana shida ya kushughulikia hayo matatizo kwa sababu hayawagusi.

Ila wakazi wa pale nao wana matatizo tena makubwa kuliko watawala. Walitakiwa kuwambia watawala wao kile wanachokitaka. Kama hawawasikilizi wanawatimua kazi. Najua mawazo hayo hawana na ndio maana hutashangaa kukuta nyumba hizo zimejaa mabango ya wagombea wakati wa uchaguzi hata kama wagombea hao wanawalaghai. Pia kutakuwa na bendera nyingi tu za chama kilichoshindwa kuwathamini na pia wao nadhani bado wanazo t-shirts ana khanga. Utawasaidiaje watu hao??
 
Hapo umegusia tatizo lingine....
vijislams vinajitokeza polepole kila mahali na viongozi wanaangalia na hawasemi kitu.Hivi wahusika wa mipango miji kama mpo humu JF hebu tupeni ufafanuzi ni kwani hamfanyi kazi yenu kwa makini?As professionals, mnajiskiaje mnapoona jiji/mji mnalypaswa kuusimamia unazidi kuharibika siku hadi siku? Na je, hamuoni historia itakuja kuwahukumu maana " landmarks" mnazoacha zitabaki kwenye kumbukumbu? Jirekebisheni jamani!Tusikalie kuwasema viongozi wa kisiasa tu humu JF tujiseme hata sisi wenye taaluma na dhamana.

Kazi gani unataka wafanye? Kazi kubwa sana wameshafanya. Kwani hujasikia maboss wao wanawasifia?

Profession gani unaongelea? Kuna pesa pale? Kama hakuna pesa mtu aende kufanya nini??

Umewauliza wanataka kuacha legacy gani?? Mimi najua legacy zetu kama WaTz wa kizazi hiki ni kuacha "pesa nyingi sana" (bila kujali umezipataje), nyumba ndogo za kutosha, watoto kibao wasiojuana (walau mmoja kila mtaa) na misifa kibao (angalau uwe umerushwa walau mara moja kwenye bongo flava). Sasa hiyo historia unayoongelea siyo yetu!

Lakini mwisho wa yote, sisi waathirika tunajua kuwa tunaathiriwa na mazingira yetu ambayo ni matokeo ya matendo ya watawala? Mpaka hapo tutakapojua ndio tunaweza kuanza kuongea! Vinginevyo tuache tuendelee kuuchapa usingizi!!
 
Hii ndio 'ari mpya kasi mpya'watu tunazidi kutaabika sana tu.
Angalia kwa sasa mtu ukitoka nyumbani unakuja kazini kuanzia kodi ya meza nyumbani+usafiri+chai+msosi mchana+nauli kurudi nyumbani=si chini ya 10,000 mshahara kwa mwezi kwa mhindi haizidi 100,000/= sijui wa serikalini mnapeta vipi.
Ukiwa fisadi hapo unamfisadi mhindi akikaa vibaya unamkwapilia utakuwa unamwonea????
Hii ndio hali halisi ya maisha ya MTZ hali mbaya sana asikwambia mtu.
Hapo sijapiga kodi kwa mwezi pamoja na umeme wa kuchangia kila baada ya wiki 2 5000 yaani inauma sana.Ukirudi kijijini ndo balaa zaidi ya huku mjini.
 
Kazi gani unataka wafanye? Kazi kubwa sana wameshafanya. Kwani hujasikia maboss wao wanawasifia?

Profession gani unaongelea? Kuna pesa pale? Kama hakuna pesa mtu aende kufanya nini??

Umewauliza wanataka kuacha legacy gani?? Mimi najua legacy zetu kama WaTz wa kizazi hiki ni kuacha "pesa nyingi sana" (bila kujali umezipataje), nyumba ndogo za kutosha, watoto kibao wasiojuana (walau mmoja kila mtaa) na misifa kibao (angalau uwe umerushwa walau mara moja kwenye bongo flava). Sasa hiyo historia unayoongelea siyo yetu!
Lakini mwisho wa yote, sisi waathirika tunajua kuwa tunaathiriwa na mazingira yetu ambayo ni matokeo ya matendo ya watawala? Mpaka hapo tutakapojua ndio tunaweza kuanza kuongea! Vinginevyo tuache tuendelee kuuchapa usingizi!!

I like this!
mambo ya mshiko siyo? Mshiko jamani unatufikisha pabaya!Hakuna tena kujali maslahi ya taifa wala kujali historia itakuja kuhukumu vipi! Ina maana ndiyo tumeridhika au tumekata tamaa?
 
I like this!
mambo ya mshiko siyo? Mshiko jamani unatufikisha pabaya!Hakuna tena kujali maslahi ya taifa wala kujali historia itakuja kuhukumu vipi! Ina maana ndiyo tumeridhika au tumekata tamaa?

Napata taabu kusema kama tumeridhika au tumekata tamaa kwa sababu sina hakika kama tunajitambua na tunajua tunalolitaka. Mpaka hapo tutakapoweza kujua sisi tu akina nani, tunataka nini, tunataka kwenda wapi na kwa nini ndiyo tunaweza kufikia hizo hitimisho ulozitaja hapo juu. Nadhani bado tunauchapa usingizi.

Shida yangu ni kuwa wale ambao angalau tuko tunapiga mswaki hatujaribu kamwe kuwastua wenzetu. Tunawaongezea blanketi na shuka waendelee kuuchapa usingizi. Kama tungewanyang'anya wakaguswa na baridi kidogo hiyo picha wa wakazi wa Bonde la Mpunga ingekuwa tofauti!
 
Maeneo mengine yalitakiwa yasiwe makazi ya wananchi. Bonge la Mpunga ni mfano halisi kabisa.

Je, lawama zingine zitupiwe kwa wale vijana wetu tuliowasomesha chuo cha ardhi? Mipango miji ni aje nyinyi?
Kamanda naona unawatukana watu hapa...
 
Back
Top Bottom