Tuliowahi kunywa sumu tukutane hapa

S V Surovikin

JF-Expert Member
Aug 8, 2015
13,620
32,732
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, ni kwamba katika maisha tunakutana na changamoto ambazo wakati mwingine huwa kubwa kwelikweli, au huwa kubwa kulingana na mhusika atakavyoitafsiri changamoto yenyewe ndani ya ubongo wake kitu ambacho hupelekea mhusika kukata tamaa kwa asilimia zote hadi kuona bora kufa kuliko kuendelea kuishi.

Wengine huwa ni changamoto za kutatulika lakini hushindwa kuchukua hatua stahiki kutokana na ujinga au kutokana na kuathirika kisaikolojia kutokana na muda wa changamoto husika.

Sasa basi naomba nisimulie kisa changu kilichonipelekea kutaka kuutoa uhai wangu ndani ya Dar es Salaam na kingine ndani ya Kilimanjaro, japo katika visa vyote sikufanikiwa na ndio maana nipo hai hadi muda huu.

Ieleweke thread kama hizi ni kuwasaidia wengine wenye wanaopita matatizo kama ya waliotangulia, ili wasikate tamaa bali wajue ni hatua gani za kuchukua ili watoke kwenye matatizo waliyonayo na mwisho wabaki wakiusifu na kufurahia uzuri wa kazi za Mungu aliye chanzo chao.

Twende kwenye kisa cha kwanza ambacho almanusra kiondeke na uhai wangu!
Nilipomaliza elimu ya msingi moja kwa moja nikatakiwa kwenda kwa shemeji kufanya kazi ya kuuza kitimoto Arusha huku nikiendelea kusubiri matokeo, lakini safari yangu nilikuwa na wasiwasi maana nilikuwa na tabia ya kukojoa kitandani, sasa nikawa nawaza huko mjini nitakaaje na hii tabia yangu?

Nikajipa moyo tu potelea mbali liwalo na liwe. Sasa nilipofika Arusha, kwa bahati nzuri sikupangiwa kulala na yeyote ila nilipangiwa nitakuwa nalala kwenye makochi ofisini.

Kwa kifupi pale niliishi kijanjajanja na tabia yangu hiyo japo mbeleni waliijua tabia yangu ila wakawa wananisitiri tu 👏👏👏

Mdogomdogo mara nikafaulu kwenda kidato cha kwanza lakini sikukubali kuendelea na shule japo nilibembelezwa sana lakini nikawa sitaki kabisa. Hivyohivyo mpaka ilipotimu mwezi wa 7 mwaka 2010 kaka yangu akapiga simu kwa dada Arusha sasa katika kumsalimia akataka niende Dar nikakae dukani. Ile kaka kutaka niende Dar kulinichanganya kabisa mpaka nikaanza ujeuri kazini maana nilitaka niache kazi shemeji na dada wakakataa sababu nilikuwa nimeshakuwa mtu wa muhimu na mzoefu pale ofisini.

Kweli nilizidisha ujeuri hadi wakayasikia madai yangu wakanilipa changu nikasepa.
Nakumbuka nilipita kwanza nyumbani Rombo nikiwa na kiasi kama laki tatu na chenchi ila mpaka naondoka nilikuwa nimebakiwa na 125,000 wakati nilikaa siku tatu tu nyumbani.

Baada ya siku tatu mimi huyoo Dar es Salaam. Nilitoka asubuhi saa kumi na mbili lakini tulienda kufika saa mbili usiku kwa sababu kuna gari lilipata ajali mbele yetu kulekuke Rombo kabla hata hatujafika mashati. Nilipofika Ubungo nikapokewa na jamaa wa tax aliyetumwa na kaka ndio akanipeleka hadi dukani. Nilipofika nakumbuka tulisalimiana tu akaniingiza dukani usiku uleule. Kuna laki moja ilibaki mfukoni baada ya kutoa nauli nikampa aniwekee mimi nikaendelea na kazi yeye akaketi hapo mlangoni akinielekeza bei ya vitu na namna ya kufanya kazi maana ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuuza dukani.

Sasa bahati yangu nikawa nalala kwenye chumba changu mwenyewe tena, hivyo ikawa chansi ya kuficha aibu yangu ya kukojoa kitandani maana nilikuwa nikitandika nailoni usiku na asubuhi nalificha.

Kipindi hicho tulikuwa tandika ila baada ya miezi michache akahamia kwake Tabata, hivyo ikawa nikifunga duka tunalala sehemu moja!😬

Kimbembe kikaanza. Kipindi hicho nilikuwa najitahidi hata sinywi soda hovyohovyo na maji hasa ile mida ya jioni kuelekea usiku lakini wapi! Nilikuwa nikijitahidi sana naweza kukosa siku 2 ndani ya wiki. Mambo yakawa magumu kwangu.

Lile jambo liliniathiri kisaikolojia kwa wakati huo kuliko wakati mwingine wowote tangu kuzaliwa. Nimajiona sifa na nikaanza kulaumu kwanini hata nilizaliwa?

Yani nalala na mtu msafi, asiyependa uchafu, nyumba safi, kitanda kisafi, mashuka masafi, nina akili timamu lakini nakojoa kitandani? Nikawa sina amani na mawazo ya kutaka kujiua yakaanza kumea kwenye akili yangu maana nilijiona nikifa nitakuwa na amani na hakuna chochote kitakachoendelea.

Kaka alikuwa hapendi kabisa hiyo tabia yangu na tangu utotoni alikuwa hapendi
Kadri siku zilivyokuwa zinaenda mimi nikawa naanza kufikiri mbinu nzuri ya kuniondoa chapu, ilipofika mwezi wa pili mwaka wa 2011, nakumbuka siku hiyo nilifata bia na baiskeli nikakutana na jamaa anatembeza sumu za panya, mende, kunguni nk; nikamsimamisha nikamuuliza sumu ya bei ghali kabisa ni sh ngapi? Akajibu kuwa ni buku.

Nikamwuliza sifa zake akasema hiyo sumu huua panya fasta na akishakufa hanuki. Sikuongea sana nikamwambia anifungie.

Niliporudi dukani nikaendelea na mambo yangu kama kawaida huku lengo langu likiwa ni kwenda kujiulia mbali na eneo la nyumbani. Kesho yake asubuhi nikadamka nikaenda kwenye kimsitu fulani kiko pale Tabata kisukuru kwa pembeni sijui eti ni wa jeshi, maana mission yangu ilipofeli kule, muda wa kutokea barabarani kuna mbaba aliniambia we mtoto unafanya nini kwenye huo msitu wa jeshi?

Sasa baada ya kuingia kwenye hicho kimsitu nikapanda juu ya mikorosho huku nikifikiria namna nitakavyoingia makazi mapya ambayo ni ya kufikirika zaidi. Baada ya muda nikaibugia ile sumu yote ambayo ilikuwa kama vile vitambi vya kwenye packet ndogondogo.

Baada ya kuibugia nikashuka zangu juu ya ule mkorosho ili nisije kuanguka saa ya kufa. Nikakaa pale chini ya mti muda mrefu bila kuhisi chochote ndio nikaamua kutafuta njia ya kutoka ndani ya ule msitu baada ya njaa kuwa kali kwenye mida ya saa nane mchana, nikatokeza barabarani ndio huyo dingi akakutana na mimi akaniuliza, wee mtoto umetoka kufanya nini ndani ya huo msitu wa jeshi? Nikamwambia nimetoka kujisaidia.

Tukaachana mimi nikaelekea na njia ya kupandia Tabata migombani ili nikavizie chakula dukani kwa rafiki wa kakaangu ambaye pia ni rafikiangu ili nikampange endapo akiulizwa na kaka nilikuwa wapi aseme nilikuwa kwake. Kweli mpango wangu ukaenda fresh ila misheni yangu ya kuwahi kwa father God ikafeli.

Niliporudi kwa kaka nikamkuta anapambana na kazi huku anafua mashuka niliyokojolea usiku huo kitendo ambacho kiliniumiza mara dufu. Katika kuniuliza nilikoamkia asubuhi nikamdanganyadanganya ikabidi anivungie tu sababu akishaanza kuona kama dishi lango haliko poa.

Tukaendelea vizuri tu shetani wangu akawa ndio kanikomalia vizuri yani hata asubuhi najikuta nakojoa kitandani kama mtoto mdogo wakati mimi ni mkaka wa miaka 20 kabisa. Hazikuisha hata wiki mbili nikanunua sumu nyingine ya panya nikainywea bafuni muda ambao nilikuwa mwenyewe usiku lakini yenyewe niliitapika tu wala sikuhisi chochote kibaya wala nini.

Nikaona huu sasa ni uduanzi, kesho yake mchana nikashuka ile sumu ya kuulia mbu nikaipulizia kwenye kikombe alafu nikaenda kununua sindano zile za mahospitalini nikainyonya kwa ile sindano kisha nikajidunda mguuni alafu nikaionja kidogo lakini matokeo yake pale nilipojidunda pwlivimba alafu pakawa panauma sana lakini sikupatwa na tatizo lingine.

Nilitokewa na kidonda lakini kilipona chenyewe bila hata mtu kujua Mwezi wa tatu mwaka huohuo nikaenda kununua sumu nyingine ya panya ambayo ni kapakt kadogo sana kalikofungwa na karatasi mbili, nikakaweka kwenye juice fulani zilizokuwa zinaitwa juice za glass au pride juice nikanywa usiku wa saa tano ambapo muda huo kaka alikuwa anakunywa bia na marafiki zake kibarazani nje ya duka.

Ile nimeinywa tu nikahisi kuzunguzngu na dalili ya kutapika, nikajikaza nikatoka kama naenda kuoga na nilipofika nyuma ya nyumba tu nikatapika chakula chote cha mchana alafu nikaishiwa nguvu kiasi. Nikadaka ukuta nikadondokea kwa jamaa mmoja ambaye muda mwingi anakuwa hayupo nyumbani huja usiku kwa usiku na usiku huo alikuwa ameshalala ila mimi nikadondokea pembeni kidogo ya gari lake nikawa natapika maji na kujiharishia mfululizo mpaka nikaishiwa nguvu kiasi kwamba nilikuwa nikitazama balbu iliyokuwa juu yangu naiona kama imesambaa.

Muda mfupi baadae nasikia kaka akiita hadi kwa baadhi ya majirani akiniulizia maana niliacha ndoo ya kuogea kule na sabuni kule bafuni alafu hajui nilipo na ni usiku sana.

Akawa anahangaika bahati nzuri baadaye sijui alifikiria nini akapanda juu ya ule ukuta akaniona, akaja fasta akamwamsha na yule jirani huku mimi nawasikia tu ila siwezi kufanya chochote hata kutoa sauti au kukunja hata kidole cha mkono siwezi.
Wakaja mbiombio wakaenda kuleta mabarafu wakaniwekea ila nikawa hata sitingishiki ila masikio yangu yakawa yanasikia kuliko kawaida. Mara nasikia wakisema, ameshakufa, hahemi huyu, kafanyaje? Nini kimemkumba?.

Basi nilishangaa kaka akisema amekunywa sumu huyu. Kauli ile ilinishtua japo nilikuwa marehemu 90% Wakashauriana mara wakanibeba wakanitupa kwenye gali wakaniwahisha hospitali ya amana, lakini katika kunibeba kule kote nilikuwa naelewa nimebebwa lakini sihisi/yani mwili wangu ulikuwa hauhisi chochote tena hata walinifinya nikajua nimefinywa lakini sikuhisi maumivu.

Kufika amana nikapokelewa fasta nikawekewa maji tu kumbukumbu zikakomea pale hadi asubuhi nilipozinduka nimezungukwa na marafiki wa kaka wengi na mirija ya maji.

Kila mtu akawa anataka kujua nilipatwa na nini lakini nikasema sielewi ilikuwaje.
Kikubwa pale nilipona bila bata kutumia dawa tofauti na maji niliyowekewa.
Kingine nilipotoka hospitali nilipoteza uwezo wa kuonja kwa muda wa karibu mwezi mzima na kuna namna nilikuwa nikiisikia ile harufu ya sumu kwa muda huohuo ikaja kupotea Kifupi kaka alihonga pale nisipelekwe polisi kwa kosa la kujiua ndio tukaondoka. Sasa mpaka leo najiuliza madaktari na kaka walijuaje nimekunywa sumu?

Sijawahi kupata jibu ila mwaka 2016 ndio nilimwambia kaka ukweli.
Tatizo la kukojoa kitandani lilikuja kuisha baada ya kuacha mchezo wa kujichua, na hii niligundua baada ya kukaa muda wa mwezi sijajichua likaisha lenyewe ndio nikajua kumbe ndio dawa ya tatizo.

Na nashukuru baada ya kujua nilikuwa nakojoa kitandani kwa sababu ya kujichua kulikopitiliza, ilibidi niache huo mchezo mara moja!

Kisa cha pili nitakileta maana vidole vimechoka kutyp

KISA CHA PILI KIPO COMMENT YA 43
 
Daaah we jamaa yani ishu ndogo kama hiyo ukafikiria kuvhukua maamuzi heavy kiasi hicho?
Ndio maana nikasema kuna watu wana matatizo madogomadogo, lakini kutokana na namna walivyoyakuza ndani ya fahamu zao wakachukua maamuzi ambayo ni kituko mbele za jamii.

Mwanajeshi wa Tz akikoswa na bomu akirudi kambini anapongezwa tu yanaisha ilimradi hajaumia
Mwanajeshi wa Marekani akikoswa na bomu akirudi kambini anapelekwa hospitali kuchekiwa afya ya akili.

Tofauti hapo ni kubwa sana japo unaona mambo madogo
 
Mzee kwani so ungepanga chumba chako ukaishi mwenyewe tu, ukamwambia bro nataka uhuru wa kukaa mwenyewe nimekuwa mtu mzima, tatizo lingekuwa solved kwa muda, kisha ukaanza kutafuta tiba mwenyewe, maana matatizo Kama hayo yapo common sana usingekosa tiba

Mi nilishafikiria kujiua nikiwa mdogo sana kabla sijaanza hata shule, Sababu nilikuwa napigwa sana na hakuna mtu aliyenijali, nikalamba mfuko uliokuwa umewekewa mahindi ya kupanda yenye sumu ya kuuwa wadudi, sikupatwa hata na jambo lolote nipo hai Hadi leo

Kuna kipindi nakaribia kumaliza chuo nikitafakari sitapata kazi, sijuani hata na watu, pa kuishi Sina zaidi ya kijijini kwa wazazi ambako sikupendi, nikashikwa na depression Ila sikunywa sumu, nilikuwa natamani tu nipate ajali nife, Ila nikaja kupata kazi kimiujiza tu..dah



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wauza sumu ya panya wengine ni matapeli, eti hata akifa panya hanuki.
Kuhusu suala la kukojoa linatesa ( mimi nilishawahi kuwa nalo nilivyokuwa primary. Nikienda kulala kwa ndugu huwa najifikiria. Unaota kabisa mkojo umekubana unaenda chooni kukojoa, unapokojoa unaishia kukojoa kitandani, baadae liliisha tu lenyewe.
Ila sababu hiyo ilikufanya ujiue kuna matatizo makubwa kuliko hayo na watu wanakomaa nayo
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, ni kwamba katika maisha tunakutana na changamoto ambazo wakati mwingine huwa kubwa kwelikweli, au huwa kubwa kulingana na mhusika atakavyoitafsiri changamoto yenyewe ndani ya ubongo wake kitu ambacho hupelekea mhusika kukata tamaa kwa asilimia zote hadi kuona bora kufa kuliko kuendelea kuishi.

Wengine huwa ni changamoto za kutatulika lakini hushindwa kuchukua hatua stahiki kutokana na ujinga au kutokana na kuathirika kisaikolojia kutokana na muda wa changamoto husika.

Sasa basi naomba nisimulie kisa changu kilichonipelekea kutaka kuutoa uhai wangu ndani ya Dar es Salaam na kingine ndani ya Kilimanjaro, japo katika visa vyote sikufanikiwa na ndio maana nipo hai hadi muda huu.

Ieleweke thread kama hizi ni kuwasaidia wengine wenye wanaopita matatizo kama ya waliotangulia, ili wasikate tamaa bali wajue ni hatua gani za kuchukua ili watoke kwenye matatizo waliyonayo na mwisho wabaki wakiusifu na kufurahia uzuri wa kazi za Mungu aliye chanzo chao.

Twende kwenye kisa cha kwanza ambacho almanusra kiondeke na uhai wangu!
Nilipomaliza elimu ya msingi moja kwa moja nikatakiwa kwenda kwa shemeji kufanya kazi ya kuuza kitimoto Arusha huku nikiendelea kusubiri matokeo, lakini safari yangu nilikuwa na wasiwasi maana nilikuwa na tabia ya kukojoa kitandani, sasa nikawa nawaza huko mjini nitakaaje na hii tabia yangu?

Nikajipa moyo tu potelea mbali liwalo na liwe. Sasa nilipofika Arusha, kwa bahati nzuri sikupangiwa kulala na yeyote ila nilipangiwa nitakuwa nalala kwenye makochi ofisini.

Kwa kifupi pale niliishi kijanjajanja na tabia yangu hiyo japo mbeleni waliijua tabia yangu ila wakawa wananisitiri tu

Mdogomdogo mara nikafaulu kwenda kidato cha kwanza lakini sikukubali kuendelea na shule japo nilibembelezwa sana lakini nikawa sitaki kabisa. Hivyohivyo mpaka ilipotimu mwezi wa 7 mwaka 2010 kaka yangu akapiga simu kwa dada Arusha sasa katika kumsalimia akataka niende Dar nikakae dukani. Ile kaka kutaka niende Dar kulinichanganya kabisa mpaka nikaanza ujeuri kazini maana nilitaka niache kazi shemeji na dada wakakataa sababu nilikuwa nimeshakuwa mtu wa muhimu na mzoefu pale ofisini.

Kweli nilizidisha ujeuri hadi wakayasikia madai yangu wakanilipa changu nikasepa.
Nakumbuka nilipita kwanza nyumbani Rombo nikiwa na kiasi kama laki tatu na chenchi ila mpaka naondoka nilikuwa nimebakiwa na 125,000 wakati nilikaa siku tatu tu nyumbani.

Baada ya siku tatu mimi huyoo Dar es Salaam. Nilitoka asubuhi saa kumi na mbili lakini tulienda kufika saa mbili usiku kwa sababu kuna gari lilipata ajali mbele yetu kulekuke Rombo kabla hata hatujafika mashati. Nilipofika Ubungo nikapokewa na jamaa wa tax aliyetumwa na kaka ndio akanipeleka hadi dukani. Nilipofika nakumbuka tulisalimiana tu akaniingiza dukani usiku uleule. Kuna laki moja ilibaki mfukoni baada ya kutoa nauli nikampa aniwekee mimi nikaendelea na kazi yeye akaketi hapo mlangoni akinielekeza bei ya vitu na namna ya kufanya kazi maana ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kuuza dukani.

Sasa bahati yangu nikawa nalala kwenye chumba changu mwenyewe tena, hivyo ikawa chansi ya kuficha aibu yangu ya kukojoa kitandani maana nilikuwa nikitandika nailoni usiku na asubuhi nalificha.

Kipindi hicho tulikuwa tandika ila baada ya miezi michache akahamia kwake Tabata, hivyo ikawa nikifunga duka tunalala sehemu moja!

Kimbembe kikaanza. Kipindi hicho nilikuwa najitahidi hata sinywi soda hovyohovyo na maji hasa ile mida ya jioni kuelekea usiku lakini wapi! Nilikuwa nikijitahidi sana naweza kukosa siku 2 ndani ya wiki. Mambo yakawa magumu kwangu.

Lile jambo liliniathiri kisaikolojia kwa wakati huo kuliko wakati mwingine wowote tangu kuzaliwa. Nimajiona sifa na nikaanza kulaumu kwanini hata nilizaliwa?

Yani nalala na mtu msafi, asiyependa uchafu, nyumba safi, kitanda kisafi, mashuka masafi, nina akili timamu lakini nakojoa kitandani? Nikawa sina amani na mawazo ya kutaka kujiua yakaanza kumea kwenye akili yangu maana nilijiona nikifa nitakuwa na amani na hakuna chochote kitakachoendelea.

Kaka alikuwa hapendi kabisa hiyo tabia yangu na tangu utotoni alikuwa hapendi
Kadri siku zilivyokuwa zinaenda mimi nikawa naanza kufikiri mbinu nzuri ya kuniondoa chapu, ilipofika mwezi wa pili mwaka wa 2011, nakumbuka siku hiyo nilifata bia na baiskeli nikakutana na jamaa anatembeza sumu za panya, mende, kunguni nk; nikamsimamisha nikamuuliza sumu ya bei ghali kabisa ni sh ngapi? Akajibu kuwa ni buku.

Nikamwuliza sifa zake akasema hiyo sumu huua panya fasta na akishakufa hanuki. Sikuongea sana nikamwambia anifungie.

Niliporudi dukani nikaendelea na mambo yangu kama kawaida huku lengo langu likiwa ni kwenda kujiulia mbali na eneo la nyumbani. Kesho yake asubuhi nikadamka nikaenda kwenye kimsitu fulani kiko pale Tabata kisukuru kwa pembeni sijui eti ni wa jeshi, maana mission yangu ilipofeli kule, muda wa kutokea barabarani kuna mbaba aliniambia we mtoto unafanya nini kwenye huo msitu wa jeshi?

Sasa baada ya kuingia kwenye hicho kimsitu nikapanda juu ya mikorosho huku nikifikiria namna nitakavyoingia makazi mapya ambayo ni ya kufikirika zaidi. Baada ya muda nikaibugia ile sumu yote ambayo ilikuwa kama vile vitambi vya kwenye packet ndogondogo.

Baada ya kuibugia nikashuka zangu juu ya ule mkorosho ili nisije kuanguka saa ya kufa. Nikakaa pale chini ya mti muda mrefu bila kuhisi chochote ndio nikaamua kutafuta njia ya kutoka ndani ya ule msitu baada ya njaa kuwa kali kwenye mida ya saa nane mchana, nikatokeza barabarani ndio huyo dingi akakutana na mimi akaniuliza, wee mtoto umetoka kufanya nini ndani ya huo msitu wa jeshi? Nikamwambia nimetoka kujisaidia.

Tukaachana mimi nikaelekea na njia ya kupandia Tabata migombani ili nikavizie chakula dukani kwa rafiki wa kakaangu ambaye pia ni rafikiangu ili nikampange endapo akiulizwa na kaka nilikuwa wapi aseme nilikuwa kwake. Kweli mpango wangu ukaenda fresh ila misheni yangu ya kuwahi kwa father God ikafeli.

Niliporudi kwa kaka nikamkuta anapambana na kazi huku anafua mashuka niliyokojolea usiku huo kitendo ambacho kiliniumiza mara dufu. Katika kuniuliza nilikoamkia asubuhi nikamdanganyadanganya ikabidi anivungie tu sababu akishaanza kuona kama dishi lango haliko poa.

Tukaendelea vizuri tu shetani wangu akawa ndio kanikomalia vizuri yani hata asubuhi najikuta nakojoa kitandani kama mtoto mdogo wakati mimi ni mkaka wa miaka 20 kabisa. Hazikuisha hata wiki mbili nikanunua sumu nyingine ya panya nikainywea bafuni muda ambao nilikuwa mwenyewe usiku lakini yenyewe niliitapika tu wala sikuhisi chochote kibaya wala nini.

Nikaona huu sasa ni uduanzi, kesho yake mchana nikashuka ile sumu ya kuulia mbu nikaipulizia kwenye kikombe alafu nikaenda kununua sindano zile za mahospitalini nikainyonya kwa ile sindano kisha nikajidunda mguuni alafu nikaionja kidogo lakini matokeo yake pale nilipojidunda pwlivimba alafu pakawa panauma sana lakini sikupatwa na tatizo lingine.

Nilitokewa na kidonda lakini kilipona chenyewe bila hata mtu kujua Mwezi wa tatu mwaka huohuo nikaenda kununua sumu nyingine ya panya ambayo ni kapakt kadogo sana kalikofungwa na karatasi mbili, nikakaweka kwenye juice fulani zilizokuwa zinaitwa juice za glass au pride juice nikanywa usiku wa saa tano ambapo muda huo kaka alikuwa anakunywa bia na marafiki zake kibarazani nje ya duka.

Ile nimeinywa tu nikahisi kuzunguzngu na dalili ya kutapika, nikajikaza nikatoka kama naenda kuoga na nilipofika nyuma ya nyumba tu nikatapika chakula chote cha mchana alafu nikaishiwa nguvu kiasi. Nikadaka ukuta nikadondokea kwa jamaa mmoja ambaye muda mwingi anakuwa hayupo nyumbani huja usiku kwa usiku na usiku huo alikuwa ameshalala ila mimi nikadondokea pembeni kidogo ya gari lake nikawa natapika maji na kujiharishia mfululizo mpaka nikaishiwa nguvu kiasi kwamba nilikuwa nikitazama balbu iliyokuwa juu yangu naiona kama imesambaa.

Muda mfupi baadae nasikia kaka akiita hadi kwa baadhi ya majirani akiniulizia maana niliacha ndoo ya kuogea kule na sabuni kule bafuni alafu hajui nilipo na ni usiku sana.

Akawa anahangaika bahati nzuri baadaye sijui alifikiria nini akapanda juu ya ule ukuta akaniona, akaja fasta akamwamsha na yule jirani huku mimi nawasikia tu ila siwezi kufanya chochote hata kutoa sauti au kukunja hata kidole cha mkono siwezi.
Wakaja mbiombio wakaenda kuleta mabarafu wakaniwekea ila nikawa hata sitingishiki ila masikio yangu yakawa yanasikia kuliko kawaida. Mara nasikia wakisema, ameshakufa, hahemi huyu, kafanyaje? Nini kimemkumba?.

Basi nilishangaa kaka akisema amekunywa sumu huyu. Kauli ile ilinishtua japo nilikuwa marehemu 90% Wakashauriana mara wakanibeba wakanitupa kwenye gali wakaniwahisha hospitali ya amana, lakini katika kunibeba kule kote nilikuwa naelewa nimebebwa lakini sihisi/yani mwili wangu ulikuwa hauhisi chochote tena hata walinifinya nikajua nimefinywa lakini sikuhisi maumivu.

Kufika amana nikapokelewa fasta nikawekewa maji tu kumbukumbu zikakomea pale hadi asubuhi nilipozinduka nimezungukwa na marafiki wa kaka wengi na mirija ya maji.

Kila mtu akawa anataka kujua nilipatwa na nini lakini nikasema sielewi ilikuwaje.
Kikubwa pale nilipona bila bata kutumia dawa tofauti na maji niliyowekewa.
Kingine nilipotoka hospitali nilipoteza uwezo wa kuonja kwa muda wa karibu mwezi mzima na kuna namna nilikuwa nikiisikia ile harufu ya sumu kwa muda huohuo ikaja kupotea Kifupi kaka alihonga pale nisipelekwe polisi kwa kosa la kujiua ndio tukaondoka. Sasa mpaka leo najiuliza madaktari na kaka walijuaje nimekunywa sumu?

Sijawahi kupata jibu ila mwaka 2016 ndio nilimwambia kaka ukweli.
Tatizo la kukojoa kitandani lilikuja kuisha baada ya kuacha mchezo wa kujichua, na hii niligundua baada ya kukaa muda wa mwezi sijajichua likaisha lenyewe ndio nikajua kumbe ndio dawa ya tatizo.

Na nashukuru baada ya kujua nilikuwa nakojoa kitandani kwa sababu ya kujichua kulikopitiliza, ilibidi niache huo mchezo mara moja!

Kisa cha pili nitakileta maana vidole vimechoka kutyp
''Ukaamua kushuka kwenye mti ili ukifa usidondoke'' Mwisho wa kunukuu.... Ha haa pole sana na hongera kwa zawadi ya uhai mpaka leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu uzi unaweza ukaonekana hauna maana lakini haya mambo yapo. Mimi kuna muda nilipitia hali ngumu sana kwenye maisha, kuliko niliyonayo sasa. Nilikuwa nawaza kujiua ili nipotee maana hata ndugu wanakuona kituko. Wazo moja tu lilikuwa linafanya nikomae, familia. Nikawaza mimi ndio baba na mume katika familia, kama mimi nimekoswa kazi na hela ilhali nakomaa Je! Itakuwaje kwa mke wangu ambaye ananitegemea 100% katika kutimiza mahitaji ya familia? Vp watoto watakapoona nafukiwa shimoni na wasinione tena? Kwann nisisubiri siku yangu ifike ili angalau nisiihuzunishe familia mara mbili. Wakose chakula najua hapa wanawake hufanya lolote ili waishi na watoto wengine mpaka hufanya mambo haramu, nabado wakose ile faraja yangu ya ngoja nikatafute angalau ya uji. Nilikuwa nikiwaza hayo yote halafu unaenda ndugu anatumbua bia unamuomba hata buku anakunyima anakwambia hana pesa😭😭. Umasikini usikieni tu kwa watu. Kiukweli kama isingelikuwa familia huenda ningeshajifia kitaaambo. Mshana Jr aliwahi kuelezea humu kuhusu tiba za kiroho. Nilikuwa nikisoma mada zake nahisi 90% nina shida. Katika kosa sifanyi sasahv nikuwambia mtu mipango yangu ya sasa na baadaye. Nikiulizwa unafanya nn, nawaambia niko nyumbani nasubiri ajira. Maisha ni mtihani mkubwa sana kwa binadamu, ukiona dogo kwa mwenzio ni mateso.
 
Huu uzi unaweza ukaonekana hauna maana lakini haya mambo yapo. Mimi kuna muda nilipitia hali ngumu sana kwenye maisha, kuliko niliyonayo sasa. Nilikuwa nawaza kujiua ili nipotee maana hata ndugu wanakuona kituko. Wazo moja tu lilikuwa linafanya nikomae, familia. Nikawaza mimi ndio baba na mume katika familia, kama mimi nimekoswa kazi na hela ilhali nakomaa Je! Itakuwaje kwa mke wangu ambaye ananitegemea 100% katika kutimiza mahitaji ya familia? Vp watoto watakapoona nafukiwa shimoni na wasinione tena? Kwann nisisubiri siku yangu ifike ili angalau nisiihuzunishe familia mara mbili. Wakose chakula najua hapa wanawake hufanya lolote ili waishi na watoto wengine mpaka hufanya mambo haramu, nabado wakose ile faraja yangu ya ngoja nikatafute angalau ya uji. Nilikuwa nikiwaza hayo yote halafu unaenda ndugu anatumbua bia unamuomba hata buku anakunyima anakwambia hana pesa😭😭. Umasikini usikieni tu kwa watu. Kiukweli kama isingelikuwa familia huenda ningeshajifia kitaaambo. Mshana Jr aliwahi kuelezea humu kuhusu tiba za kiroho. Nilikuwa nikisoma mada zake nahisi 90% nina shida. Katika kosa sifanyi sasahv nikuwambia mtu mipango yangu ya sasa na baadaye. Nikiulizwa unafanya nn, nawaambia niko nyumbani nasubiri ajira. Maisha ni mtihani mkubwa sana kwa binadamu, ukiona dogo kwa mwenzio ni mateso.


Pole sana mkuu! Yote huwa yana mwisho!hakuna moment mbaya kama uwe huna hela na had marafiki wanakukimbia!inachoma sana!
 
Twin angu alijiua kwa sumu..ikanisumbua balaa hiyo hali..! Ilinisumbua kwasababu toka tunazaliwa hatujawahi achana naye hata kwa lisaa...pia dada yangu nayemfata zilikua haziivi..nilikua nampiga balaa...bas akaambiwa asicheze na mimi..kwahyo na mimi kwa hasira nikama nikamblock...sikumjali kabs ni dada au ndugu..mdogo wangu wa mwisho nimeachana aye miaka mingi sana naye nikawa namuona mtoto..so mtu niliyeamua kuwa naye benet ni twin wangu sikua mtu wa marafikia

Alipojiua wenyeji wakaanza kusema akifa pacha mmoja mwingine hachukui round! Ile hali ikawa inaniboa sana.alafu hom wakawa kama wamenitenga fulani( walikua wananiogopa maana niligeuka kama kichaa kbs..nilikua natembea na panga naona kila mwanafamilia ndo chanzo cha twin kujiua!) Two months later nikaamua kunywa piriton 20! Nilienda tu dispensary nikasema mama kanituma umpe piriton ..nikanywa zote...lol.niliamka niko hosp! Na drip za kutosha..nakumbuka nililala tu sema tumboni kulikua kunavuruga! Sikufa...! Nikapewa mshauri akaniweka sawa kias chake .since then sijapata mawazo hayo .!Mungu alinipa utashi tena!rip B!
 
Pole sana mkuu! Yote huwa yana mwisho!hakuna moment mbaya kama uwe huna hela na had marafiki wanakukimbia!inachoma sana!
Mimi sasahivi nilishawaambia hata ndugu. Rafiki yangu kwenye shida hata kama sio ndugu yangu, namuheshimu kuliko hata ndugu wa tumbo moja. Kuna jamaa hatukuwa na urafiki hata ule wa kusalimiana na kwao zipo kidogo, alikuwa rafiki yangu ghafla mpaka kuna muda alikuwa anawatuita mimi wife na watoto tukapige stori kwake maana tulikuwa majiranu (baadaye nimekuja kugundua alikuwa anatuita tukale kiaina maana alikuwa anatuita wakati mkewe akiwa jikoni. Yaani ilikuwa inaanza hv, mkewe akanakuja anamuita wife ampe kampan jikoni ana stori ampe, mara kidogo watoto wanaitana wanaenda kucheza, halafu baadaye unasikia fulani mwite baba aje tukae huku aikae mwenyewe) huyu hata akikosea namsamehe haraka bila hata kuomba msamaha.
 
Back
Top Bottom