Tulikosea Wapi? Tufanyeje Kujirekebisha?

Mwl Kichuguu,
BTW.......unakumbuka tuliwahi kuwa na mijadala ya namna hii......na kuna sehemu tulifika kwenye ule mjadala tukaona tunachokosa ni Katiba inayokidhi yale tuyatakayo kama nchi..............tukaanza mchakato wa kukusanya maoni na mapendekezo yetu.....yaliyotokana na ule mjadala katiba ikiwemo......mpaka ikawekwa electronic copy ya katiba........tena nakumbuka wewe ulijitolea kuhariri maoni......hivi ile kazi iliishia wapi......au ndio matatizo yenyewe tuliyonayo?
Ogah Inawezekana kweli ndilo tatizo letu; ni ada yetu watanzania kutofanya mambo siriasi!! Teh!! teh!! teh!!!

Nadhani wakati tunashughulika na swala la kuhariri maoni yale ya katiba kuna jambo lililojitokeza, ambalo sasa silikumbuki tena lakini lilikuwa lina effect fulani katika ukusanyaji wa maoni. Ni takribani miaka mitano imepita sasa; inawezekana ni wakati tulipovurugwa vurugwa kutoka Jambo Forums hadi Jamiiforums au kulikuwa na jambo la kikazi lililoniingilia, au mjadala ule ulifutwa kwa namna fulani.

Swali langu la leo zaidi ni kuhusu tabia zetu kama watanzania kubadilika vile ingawa tulikuwa chini ya katiba hiyo hiyo. Ingawa sote tunayoosha kidole kwa uongozi na utawala kwa jumla, nadhani tukubalinae kuwa tabia zetu binafsi nazo ndizo zinazosababisha tuwe na uongozi mbuvu, siyo kweli kuwa uongozi mbovu ndio unaotuletea tabia mbaya. Hali ya uchumi ni sababu moja kama ambavyo wengi tunaamini ila kama DAR si LAMU alivyoainisha tena, na nimekubaliana naye ni kuwa tuna tabia ya unafiki sana wa kufanya mambo kiuongouongo na kibabaishaji ndiyo imezalisha hayo mengine mengi. Hata kama tutakuwa na katiba nzuri lakini tukajiendesha kwa mtindo huu huu wa kutokuwa na ethics, na unafiki basi katiba itabaki ni kijitabu tu. Ni kama ambavyo hivi sasa tuna sheria dhidi ya rushwa na tuna vyombo vya kupiga rushwa lakini hakuna linaloendelea. Inabidi kwanza tuangalie namna ya kutibu tabia zetu sisi wenyewe kabla ya kuangalia sheria zikoje; jambo ambalo kama Mkandara alivyoweka bayana ni kuwa tabia hizi zimejengwa kutokana na elimu duni na umaskini.
 
Last edited by a moderator:
Mwl Kichuguu,
BTW.......unakumbuka tuliwahi kuwa na mijadala ya namna hii......na kuna sehemu tulifika kwenye ule mjadala tukaona tunachokosa ni Katiba inayokidhi yale tuyatakayo kama nchi..............tukaanza mchakato wa kukusanya maoni na mapendekezo yetu.....yaliyotokana na ule mjadala katiba ikiwemo......mpaka ikawekwa electronic copy ya katiba........tena nakumbuka wewe ulijitolea kuhariri maoni......hivi ile kazi iliishia wapi......au ndio matatizo yenyewe tuliyonayo?
Dah umenikumbusha mbali sana mkuu wangu.. Nakumbuka vizuri kile kazi tulikorogana sisi wenyewe baada ya kushindwa kupata mjenzi wa blog au tovuti, kuna mtu Marekani nimemsahau jina lake aliingia mitini basi tukabakia kushabikia mgogoro wa Jambo na Jamii.. Unajua tena wasahili wakiona ngumi huacha hata kazi zao kuja tazama masumbwi..Taasisi ndiye alikuwa mhariri wa kazi ile naye sijui kaishia wapi..Ebu fikirieni ilivyokuwa rahisi leo halafu just five or six yrs ago tulikuwa tunapata shida..
 
Nzi,

Mfumo unaojulicana kama "mixed economy" yaani mchanganyiko wa ujamaa na ubepari ndio mfumo uliozikomboa nchi nyingi sana duniani hasa huko Asia. Serikali inasimamia maswala ya elimu, huduma za afya, na kumilik biashara nyeti kwa taifa kama mali asili, nishati, na njia kuu za usafirishaji kama treni, usafiri wa anga huku ikiwahimiza raia wake (siyo raia wa nje) kuwekekaza katika biashara hizo. Wakati huo huo ikiwaachia watu binafsi wajifanyie biashara zao nyinginezo.

Ma-giants wote wa uchumi huko Asia: Singapore, Taiwan, China, Korea, na Japan walifanya hivyo. Sehemu nyingi za skandinavia zinaendesha uchumi wa namna hiyo hadi leo, na Hata Australia nayo inafuata uchumi wa aina hiyo hiyo.

Je Tanzania tuchukue hatua gani ili kurudi kwenye uchumi huo iwapo viongozi wetu walishasaini mikataba ya miaka 99 na makampuni ya nje?
Chifu Kichuguu, kwa mujibu wa sheria za ardhi namba 4 na 5 za mwaka 1999, ardhi yote ya Tanzania ipo chini ya mamlaka ya rais. Hivyo suala la mikataba ya ardhi ya aina hiyo lipo ndani ya uwezo wa rais. Kwanini? Kwa sababu sheria hizo zinampa uwezo rais kuchukua ardhi yoyote kwa manufaa ya umma na taifa; rais Ana mamlaka ya kuvunja mikataba hiyo kwa manufaa ya taifa. Lakini kwa rais huyu sioni Kama hili jambo linaweza kutekelezwa. Angalia yanayoendelea Bonde la Kiru, Babati na kule Grumeti; maslahi ya wawekezaji tena wa nje ndiyo yanapewa kipaumbele dhidi ya maslahi ya taifa. Ndiyo maana naamini kama tukiweza kuchanga na kucheza karata zetu vizuri, mwanya wa kuandika katiba mpya unaweza kutumika katika kuweka misingi imara ya kuliwezesha taifa kutekeleza 'mixed economy'.
 
Last edited by a moderator:
Chifu Kichuguu, kwa mujibu wa sheria za ardhi namba 4 na 5 za mwaka 1999, ardhi yote ya Tanzania ipo chini ya mamlaka ya rais. Hivyo suala la mikataba ya ardhi ya aina hiyo lipo ndani ya uwezo wa rais. Kwanini? Kwa sababu sheria hizo zinampa uwezo rais kuchukua ardhi yoyote kwa manufaa ya umma na taifa; rais Ana mamlaka ya kuvunja mikataba hiyo kwa manufaa ya taifa. Lakini kwa rais huyu sioni Kama hili jambo linaweza kutekelezwa. Angalia yanayoendelea Bonde la Kiru, Babati na kule Grumeti; maslahi ya wawekezaji tena wa nje ndiyo yanapewa kipaumbele dhidi ya maslahi ya taifa. Ndiyo maana naamini kama tukiweza kuchanga na kucheza karata zetu vizuri, mwanya wa kuandika katiba mpya unaweza kutumika katika kuweka misingi imara ya kuliwezesha taifa kutekeleza 'mixed economy'.
Lakini mkuu wangu mikataba yenyewe imewekwa na rais iweje yeye tena ndiye aivnje kwa sheria hiyo?..Si lazima kuwepo na ushahidi tosha kwamba alokabidhiwa ardhi hiyo amekiuka?.. Haya tumeingia mikataba ya madini kwa ruzuku halafu hadi madini yaishe kwa kuwaamini Barricks ndio wafanye mahesabu yao na kuyawakilisha.

sababu ya nchi zote kudai ubia na asilimia ktk share sio tu kumiliki hiyo mali bali pia kufahamu mahesabu na thamani ya mauzo na matumizi maana mko share. Leo hii maadam hatuko share na Barricks hesabu zozote wanazotuletea inabidi tuzikubali.

Toka 2003 hadi leo miaka 10 hawajalipa corporate tax kwa sababu wanadai hawajarudisha fedha yao..Na walivyo wajanja wakijenga shule, wakitoa misaada yote hizi zote zinaingia ktk gharama zao maana wanatakiwa kuwa answerable kwa investors na sio serikali ya Tanzania..Sasa mkuu wangu mkataba wenyewe hadi madini yaishe, utapindua vipi wakati majority chares wenyewe ni Bush, Kashogi na Moroney!.. Sii ndio tutakuwa Iran au Afghanstan nyingine....
 
Lakini mkuu wangu mikataba yenyewe imewekwa na rais iweje yeye tena ndiye aivunje kwa sheria hiyo?..Si lazima kuwepo na ushahidi tosha kwamba alokabidhiwa ardhi hiyo amekiuka?.. Haya tumeingia mikataba ya madini kwa ruzuku halafu hadi madini yaishe kwa kuwaamini Barricks ndio wafanye mahesabu yao na kuyawakilisha.

Chifu, hapo ndipo niliposema kwamba, kwa sasa hatuna rais anayeweza kufanya hivyo. Rais ana mamlaka ya kufanya hivyo, lakini kutokana na kuzingatia maslahi na matakwa ya hao wawekezaji,anakuwa hawezi kuvunja mikataba hiyo ya kinyonyaji.

sababu ya nchi zote kudai ubia na asilimia ktk share sio tu kumiliki hiyo mali bali pia kufahamu mahesabu na thamani ya mauzo na matumizi maana mko share. Leo hii maadam hatuko share na Barricks hesabu zozote wanazotuletea inabidi tuzikubali.

Hapa naamini kabisa kama tukiweza kuweka suala la umiliki wa maliasili zetu katika uandaaji wa katiba mpya, tatizo hilo laweza isha. Lakini ni lazima tuweke misingi ya namna ya kuvuna maliasili zetu, hususani pale kunapokuwa na uwekezaji wa nje.

Toka 2003 hadi leo miaka 10 hawajalipa corporate tax kwa sababu wanadai hawajarudisha fedha yao..Na walivyo wajanja wakijenga shule, wakitoa misaada yote hizi zote zinaingia ktk gharama zao maana wanatakiwa kuwa answerable kwa investors na sio serikali ya Tanzania..Sasa mkuu wangu mkataba wenyewe hadi madini yaishe, utapindua vipi wakati majority shares wenyewe ni Bush, Kashogi na Moroney!.. Sii ndio tutakuwa Iran au Afghanstan nyingine....

Chifu, nilikuwa nikizungumza kwa mtazamo wa matumizi na umiliki wa ardhi; katika kuingia mikataba ya ardhi, utaratibu wa kukodishwa ardhi ndiyo utumika. Sasa kwa miaka yoyote ile ambayo mtumiaji amekodishwa ardhi na serikali, rais anayo mamlaka ya kuvunja mkataba huo kwa manufaa ya umma na taifa kwa ujumla. Hiyo haijalishi kama serikali na shareholder ama sio; hilo lipo ndani ya mamlaka ya rais. Ila kama nilivyosema hapo awali, kwamba kwa rais huyu wa sasa (na hata waliopita haswa Mkapa na Mwinyi), suala la kuvunja mikataba hiyo ni ndoto. Kwani yeye haoni umuhimu wa kutekeleza maslahi mazima ya taifa.

Nipo tayari kurekebishwa kama suala hilo litahitaji matumizi ya sheria za kimataifa - ambazo zina ujuzi nazo.
 
Kwa maoni yangu binafsi. Matatizo ya Tanzania ni matatizo ya kijamii. Swali,kama rais au serikali ingeingia mikataba mizuri na wawekezaji katika sekta ya madini, je kungekuwa na ufanisi wowote?

Kama serikal ingekuwa na sera nzuri ya nishati na kufanya nchi kutokuwa na matatizo ya umeme, je watanzania wangekuwa na tabia nzuri za ufanyaji kazi?

Majibu katika maswali hayo juu ni hapana. Matatizo ya umeme, matatizo ya mikataba mibovu, matatizo ya kutokuwa na uwajibikaji makazini ni matokeo ya matatizo ya kijamii na sio kiini cha matatizo hayo.

Matatizo yanayotokea Tanzani sasa hivi ni mavuno ya tulichopanga miaka mingi iliyopita. Na kuondoa matatizo hayo turudi kwenye basics.

Kitu cha kwanza, sera za serikali ziandaliwe kwa kutumia resources zinazopatikana katika jamii (live within your own means). Mtu anayetegemea misaada ya wahisani kusomesha watoto wake shule au kujenga barabara, hawezi kuwajibika.

Pili, all politics is local. Umefika wakati watanzania wapewe madaraka ya kuchagua na kuongoza shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
 
Zakumi,

Hata mimi ni muumini mkubwa sana wa all politics is local; lakini nimewahi kuishi katika vijiji ambavyo vina local politics nikakuta kuwa bado viongozi hawajibiki tena. Yaani wananchi wanakuwa wanamhusudu yule kiongozi waliyemchagua anapokuwa anajineemesha kwa raslimali zao. Kumpinga inakuwa kama vile ni kumuonea wivu!

Ule ujasisri wa kumwajibisha mtu hatuna kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Hata mimi ni muumini mkubwa sana wa all politics is local; lakini nimewahi kuishi katika vijiji ambavyo vina local politics nikakuta kuwa bado viongozi hawajibiki tena. Yaani wananchi wanakuwa wanamhusudu yule kiongozi waliyemchagua anapokuwa anajineemesha kwa raslimali zao. Kumpinga inakuwa kama vile ni kumuonea wivu! Ule ujasisri wa kumwajibisha mtu hatuna kabisa.
...Kichuguu,

...Elimu ni kitu muhimu sana katika maendeleo ya mwanadamu. Nadhani kiwango cha elimu cha wananchi hao kitakuwa si cha kuridhisha, na pia elimu waliyoipata -hata hiyo ndogo- haikuwa ya kuwakomboa katika maana ya kuwafanya waweze kujitegemea kimawazo na kivitendo.

...Ujasiri wa kumwajibisha mtu unakuwepo tu pale ambapo mtu huyo hana mlinzi mwenye nguvu juu yake, kwa maana ya godfather and the like. Au, hategemewi kwa chakula cha kila siku. Pengine, mtu huyo huonekana ndiye "mjanja" kuliko wote na hamna mwingine kama yeye.

...All in all, elimu na uchumi vina play a bigger role kwenye hali kama hii.
 
Swali langu la leo zaidi ni kuhusu tabia zetu kama watanzania kubadilika vile ingawa tulikuwa chini ya katiba hiyo hiyo. Ingawa sote tunayoosha kidole kwa uongozi na utawala kwa jumla, nadhani tukubalinae kuwa tabia zetu binafsi nazo ndizo zinazosababisha tuwe na uongozi mbuvu, siyo kweli kuwa uongozi mbovu ndio unaotuletea tabia mbaya. Hali ya uchumi ni sababu moja kama ambavyo wengi tunaamini ila kama DAR si LAMU alivyoainisha tena, na nimekubaliana naye ni kuwa tuna tabia ya unafiki sana wa kufanya mambo kiuongouongo na kibabaishaji ndiyo imezalisha hayo mengine mengi. Hata kama tutakuwa na katiba nzuri lakini tukajiendesha kwa mtindo huu huu wa kutokuwa na ethics, na unafiki basi katiba itabaki ni kijitabu tu. Ni kama ambavyo hivi sasa tuna sheria dhidi ya rushwa na tuna vyombo vya kupiga rushwa lakini hakuna linaloendelea. Inabidi kwanza tuangalie namna ya kutibu tabia zetu sisi wenyewe kabla ya kuangalia sheria zikoje; jambo ambalo kama Mkandara alivyoweka bayana ni kuwa tabia hizi zimejengwa kutokana na elimu duni na umaskini.
...Nadhani, inabidi tukubali kuwa, kwa maendeleo tuliyonayo leo -ambayo, how ironic faida zake hazijaweza sambaa kwa wengi- ya kuweza kupata habari, kusoma, na kutumia teknolojia za kisasa kabisa, tumeweza kuona, kuchambua, na kufahamu matatizo yetu na hata kubainisha hatua sahihi za kuchukua. Hata hivyo, hatutafanikiwa kama taifa kwa kuwa wengi ni wajinga na ndio kwanza wanajifunza. Europe walitumia miaka mingi kufikia industrial revolution, na hata hapo bado walikuwa na kazi kubwa ya kufanya.

...My point is, lazima wananchi wajifunze -mara nyingi, kutokana na makosa- halafu wajitambue, waainishe mahitaji yao na hatimae wachukue hatua. This is going to take sometime, i'm afraid. But, when you've a great leader, the time taken may be short. Lakini kama unapata viongozi wa kawaida kawaida, it'll take years.
 
Last edited by a moderator:
Kwa maoni yangu binafsi. Matatizo ya Tanzania ni matatizo ya kijamii. Swali,kama rais au serikali ingeingia mikataba mizuri na wawekezaji katika sekta ya madini, je kungekuwa na ufanisi wowote?

Kama serikal ingekuwa na sera nzuri ya nishati na kufanya nchi kutokuwa na matatizo ya umeme, je watanzania wangekuwa na tabia nzuri za ufanyaji kazi?

Majibu katika maswali hayo juu ni hapana. Matatizo ya umeme, matatizo ya mikataba mibovu, matatizo ya kutokuwa na uwajibikaji makazini ni matokeo ya matatizo ya kijamii na sio kiini cha matatizo hayo.

Matatizo yanayotokea Tanzani sasa hivi ni mavuno ya tulichopanga miaka mingi iliyopita. Na kuondoa matatizo hayo turudi kwenye basics.

Kitu cha kwanza, sera za serikali ziandaliwe kwa kutumia resources zinazopatikana katika jamii (live within your own means). Mtu anayetegemea misaada ya wahisani kusomesha watoto wake shule au kujenga barabara, hawezi kuwajibika.

Pili, all politics is local. Umefika wakati watanzania wapewe madaraka ya kuchagua na kuongoza shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
Ni mawazo mazuri sana lakini sio kwa Maskini na Mjinga.. Umuhimu wa kuweka Umaskini na UJINGA kua vipaumbele ndio njia pekee ya kumkomboa Mtanzania. Pasipo elimu tutaendelea kuvaa mitumba, madawa feki, na households ktk fikra za kimtoni (kama Ulaya) badala ya kukabili mahitaji yetu ktk standard ya juu kulingana na mazingira..Tunaagiza juice ya machungwa, tende na hata nazi kutoka Dubai ni kwa sababu ya UJINGA na huwezi kumweleza kitu Mdanganyika aliyezoea juice ya embe kutoka Dubai.
 
Nakubaliana na wote wanaooana kuwa ujinga (ignorance) wa kutokujua wajibu wetu kama raia ndio uliochangia tubadilike tabia kuwa kama tulivyo. Lakini hapo mswali mawili yananisumbua tena

(1) Je ni kweli kuwa watu wote wanofanya mambo hayo ya kutowajibika hawana elimu ya kujua mabaya na mazuri kwa taifa? Mbona watu wtote walliowahi kushukliwa kuliingiza taifa hili kwenye hasara kubwa sana za kimataifa ni wasomi tena wa hali ya juu? Hilo linoanonyesha kuwa ignorance siyo tatizo central. Wala rushwa wote na wanoongoza kwa kutowajibika ni wasomi walio kwenye nafasi za juu sana serikalini.

(2) Je hiyo ignorance ilianguka ghafla ikajaza matope ndani ya jamii yote au ilianguka kidogo kidogo hadi taifa zima likafunikwa na hayo matope kama ilivyo leo? Iwapo ilianguka ghafla, je ilitokea lini, na ni sababu zipi zilizofanya ianguke? Iwapo ilianguka kidogo kidogo, je ilianza kuangukia wapi, na ni kwa nini ilianzia hapo? Swali hili lenye vipande viwili ndiyo jambo kubwa sana ambalo litatusaidia kuangalia wapi wa kusahihisha iwapo tatizo ndilo hilo.
 
(a) Hatujali kabisa ethics za kazi; nadhani hili linaeleweka sana.
(b) Hatujitumi kazini katika majukumu ambayo hayana rushwa; hatuogopi utendaji mbovu.
(c) Tunapowewa madaraka, tunaamini kuwa tuko entitled kuwa na madaraka hayo, na tunaweza kujipatia chochote kutokana na madaraka hayo.
(d) Tunathamini sana mali kuliko heshima; tuko tayari kulamba kiatu cha mwekezaji ili atupatie kitu kidogo.
(f) Tunapenda sana njia za mkato kwa kila kitu. Tukiwa na matatizo tunapenda kumtafuta mtu mwingine atutatulie
(g) Hatutaki kuwajibika wala kuwawajibisha tuliowapa majukumu. Kila wakati tunaamini kuwa tuko right, yanapotokea makosa katika mazingira yetu basi tunakuwa wa kwanza kutafuta mtu au kitu cha kulaumu; tukikosa kitu cha kulaumu basi tunamlaumu Mungu.

Mambo haya yameungana kiasi kuwa ni huwezi kuondoa moja ukaacha mengine. Kwa bahati mbaya mambo hayo ndiyo yanasoababisha tunashindwa kuendelea.
Nina maswali mawili ya kujiuliza:
(a) Ni wapi tulipokosea hadi tukajenga element mbovu hizo katika maisha yetu?
Nina imani hali ngumu ya uchumi iliyosababisha mapato halali ya wananchi kupungua vilisaidia kusababisha watu waanza kuachana na ethics za kazi kwa kutafuta rushwa, na kuanza kutumia nafasi za kazi zao kufanya biashara kinyume na masharti ya kazi. Lakini je kweli hiyo ndiyo iliyokuwa sababu pekee? Wizi wa mabilioni ya fedha za umma kweli ni kwa sababu ya hali ngumu ya uchumi? (b) Je tufanye nini sasa ili kurekebisha makosa hayo?
Mkuu Kichuguu na wanajamvi, ni kweli kuwa kuna mwingiliano mkubwa sana wa hayo aliyoorodhesha kichuguu.
Ninakataa kabisa kuwa kuvunja maadili, rushwa,kutowajikani hulka ya Mtanzania. Maana ya hulka ni kitu kilichopo kati 'genes' za Watanzania au basi kama si genes ni utamaduni.

Ninayo mifano ya hapa nchini ambapo mfanyakazi wa serikali anaacha kazi na kuajiriwa na shirika au taasisi nyingine.
Mtu huyo kwa siku moja anabadilika kabisa katika utendaji, maadili na uzalishaji (delivery).
Wafanyakazi wengi waliokuwa katika benki za taifa walihamia katika mabenki binafsi, huko ndiko wanafanyakazi na mabenki hayo yanapata faida kila siku. Hawajabadilika chochote isipokuwa mazingira tu ni kwanini?

Kinachosababisha hali hiyo ni mnyororo wa uzembe kuanzia juu hadi chini. Hivi ni nani ataamka saa 11 ili awahi kazini saa 2 wakati mkuu wake wa kazi afike saa 5 na kuanza kunywa chai halafu saa 7 anaelekea kwenye kongamano!
Ni nani anaweza kufika kazini saa 3 ikiwa kiongozi wake yupo ofisini saa 1 asubuhi.

Mfanyakazi gani atakuwa na morali ya kazi kuwahudumia wateja wake kwa bidii wakati boss wake anawatu wake wanaokuja kwa wakati wao na kuondoka shida zao zikiwa zimamalizwa ndani ya dakika 10.
Ni nani ana munkari wa kazi kuhudumia jamii kwa kuamka saa 10 usiku awahi dala dala wakati anapoingia getini anakutana na VX zikitoka kwenda kuchukua watoto na wake za maboss kuwapeleka sokoni, mashuleni na kwenye birth day!

Rushwa: Ni mfanyakazi gani anayepokea laki 2 kwa mwezi anaweza kuacha sh 10,000 akisikia kuwa maisha kwa mkuu wake wa kazi ni magumu sana kiasi kwamba amechukua 10% ya mradi wa bilioni 10.
Kwamba mkuu wake wa kazi licha ya mambo yote anayoyapata bado anachukua 10% sasa yeye afanye nini na laki 2 kwa mwezi.

Ni mfanyakazi gani wa sh laki 2 anayejisikia raha akisikia kuwa boss wake wanayefanya naye kazi kila siku ana account ya dollar laki 7. Hivi tumesahau kuwa hawa wafanyakazi ni wanadamu kama walivyo wengine.

Tufikirie, hivi katibu mkuu anapotoa rushwa na kuachiwa astaafu ili atumie rushwa yake vizuri hilo linaingiaje akilini mwa wafanyakazi wenzake.

Hadi hapo nihitimishe kwa kusema, kila tatizo ni zao la tatizo. Watanzania wapo duniani kote na wanafanya kazi kwa ari, maadili na misingi yake. Tunachokiona Tanzania ni tatizo la mfumo wetu wa uongozi. Hatuna uongozi wa kufuata kanuni na maadili. Tuna uongozi uliojikita katika kufikiria matumbo yao na familia zao.

Kuharibika kwa maadili na kuenea kwa rushwa,kutowajibika chimbuko lake ni uongozi mbovu wa nchi. Haiwezekani nchi iongozwe kwa tume kila siku hata pale uzembe ni wa dhahiri. Haiwezekani nchi iendeshwe kishikaji kwa kuangalia marafiki halafu tutegemee matokeo tofauti. Fikiria ni jambo gani lililoleta malalamiko miongoni mwa jamii limefanyiwa kazi kama si usanii wa tume na shtaka lipo mahakani.

Wezi wote na wala rushwa wote wanaishi katika pepo ya Tanzania, ni nani mwenye moyo wa chuma wa kuijali Tanzania zaidi ya wale wenye pepo yao. Ni kwanini nidhani karani anahujumu taifa na si genge la TANESCO linaloua taifa.
Ni kwanini waziri awajibishwe na kelele za bunge badala ya serikali kulitaarifu bunge juu ya kumwajibisha waziri.

Kinachotokea ni kukata tamaa kwasababu katika nchi ya Tanzania karani peke hawezi kuleta mabadiliko kama viongozi wake ni wala rushwa kama wabunge, ni watu wa 10% kama mawaziri na ni wahongaji kama katibu mkuu.

Tufanye nini?
Tumekosa fursa muhimu sana ya kuandaa utaratibu utakaotuongoza kama nchi.
Nafasi ya kuandika sheria na taratibu za nchi yetu tumewakabidhi wale wale wanaongoza kwa tume, rushwa, kutowajibika n.k. Fursa ya kuandika katiba ndiyo ingetupa japo pa kuanzia, kwasasa haipo.

Tumewaamini wajifungie Serena Hotel na kuandika taratibu zitakazowalinda wao kazini na baada ya kustaafu. Kuandika utaratibu wa kulindana katika uhalifu. Wenyewe wanatuaminisha ni tume ya katiba! Hapa ndipo tulipobofoa na naomba muweke maneno haya katika kumbu kumbu ili siku moja munihukumu au munipongeze.
 
Mkuu Nguruvi3; kwanza mwanzoni mwa miaka ya themanini nilisoma na jamaa mmoja pale UDSM akiitwa Nguruvi- sikumbuki jina lake la kwanza kwa vile, kutokana na utamaduni wetu wa kibongo, pale UDSM tulikuwa tukifahamiana kwa jina la pili tu. Sijui kama ana uhusano na wewe.

Kama nimekusoma vizuri, ina maana wewe unadhani kuwa matatizo yetu yanatokana na sababu mbili kubwa: (a) uongozi na (b) msukumo wa uchumi wa mtu binafsi. Kama nimekuelewa vizuri, utashangaa kuwa maswali nitakayokuuliza yatakurudisha kule kule kwenye swali langu la awali.

(a) Viongozi wote makazini ni watanzania wenzetu. Ilikuwaje wao wakaanza kujisikia ni miunguwatu kiasi kuwa wanaweza kuingia ofisini saa tano na kuondoka saa saba bila kuulizwa? Baada ya hapo, inakuwaje subordinates wao wasiwaweke to task? Hapo kwa wafuasi kushindwa kuwawajibisha wakuu wao nadhani pia kuna walakini fulani ndani ya jamii yetu. Je tufanyeje ili kila mtu ajisikie ana mamlaka ya kuwamjibisha mwenzake, hata kama bosi wake, anayekiuka maadili ya kazi?


(b) Swali la kuwa unapata laki mbili na mwenzio anapata milioni moja nalo ni jambo linalohitaji mjadala wa kuhusiana na thamani ya pesa. Uchumi wa mtu binafsi ni relative; iwapo watu wote wananapata kiasi kile kile, basi gharama za maisha miongoni mwao hazitapanda, ila iwapo kuna watu wanapata kiasi kikubwa kuliko wenzao, basi gharama zote zitokanazo na huduma zitolewazo na watu wa mapato makubwa huwa ni za juu kuliko zile za watu wasiokuwa na kipato kikubwa. Hata marekani na nchi nyingine tajiri, utashangaa kuwa gharama za kupiga simu ni kubwa sana kuliko gharama za kupiga simu kutoka Tanzania kwa vile CEO wa kampuni ya simu marekani analipwa kiasi kikubwa sana kuliko mwenzake wa Bongo. Sasa swali la msingi ni je ilikuwaje tukatifautiana mapato ghafala kiasi hicho na tufanyeje kupunguza tofauti hiyo?
 
Mkuu Kichuguu,
Kwa hakika jina Nguruvi limetokana tu na uchaguzi wangu likiwa na maana, kinachotokea ni kama mtu ajiite Mapunda pengine kwa upendo wa punda. Lakini kuna wanaoitwa mapunda kama jina na ndivyo ilivyo kwa bw.Nguruvi wa UDSM uliyekuwa naye. Cha kuchekesha neno hilo lina maana nyingi wengine wanasema ni Mungu kwa lugha yao na wengine ni Jogoo. Kwangu mimi nimependelea Jogoo ha ha ha ha ha ha ha ha!

Tukirudi kwenye mada hakika maswali yako ni mazito, labda tuyaangalie kwa kadri tulivyojaliwa.
1. Chimbuko la viongozi kujisikia ni miungu watu ni sheria zinazowaweka madarakani.
Mtu aliyechaguliwa na Rais hawezi kuwajibika hata kwa bodi ya taasisi yake.
Tunakumbuka matukio ya hivi karibuni ambapo Rais alikataa kumwajibisha mwanasheria Mkuu kumuacha astaafu.
Hakukuwa na kosa yeye kufanya hivyo kwasababu sheria zinamruhusu ingawa ni makosa kufanya hivyo kwa mtazamo wa uongozi.

Tunakumbuka kuwa katibu mkuu amehusishwa na rushwa tena kwa Wabunge. Hata pale wabunge waliposhauri awajibishwe Rais hakumwajibisha. Mtoa rushwa ameuruhusiwa kustaafu ili ale rushwa vema.

'Subordinate' hawana nguvu ya kisheria au kikazi kumwajibisha mhalifu hasa kiongozi.
Vinginevyo rungu litatua kichwani mwao. Wapo waliojaribu matokeo yake ni kuhamishwa kazi kama adhabu.
Nimewahi kushudia mkuu wa kitengo akihamishwa kwasababu tu alizuia ulaji.

Nimewahi kushudia mtu akistaafishwa kwa lazima kwasababu tu anafuata taratibu na nimewahi kushudia mtu akiundiwa kesi ya wizi ili tu asisumbue wazee wakiwa wanaingia saa 5 na kufanya madili yao.
Tumeona migomo ya wafanyakazi inavyosambaratishwa kwa kigezo cha kuvuruga amani na wahusika ima wamepoteza kazi zao au wamebaki na vilema.

Kibaya zaidi utamaduni wa kuuana sasa umekamata kasi, tunafahamu hata misitu inayohusika.
Kwa ufupi tu ni kuwa 'subordinates' hawana nguvu ya aina yoyote kupambana na mfumo huu uliojengwa kwa sheria halali.

Labda nikuulize tu sisi Watanzania milioni 40 , sote tuwe 'subordinate' wa Rais, tumewezaje kumwajibisha Rais aliyeingia mikataba ya Radar, Reli, Richmond, Migodi n.k.? Kwanini milioni 40 tushindwe na tudhani watu 50 wizara ya nishati wanaweza. Angalia sheria zinazomlinda Rais n.k.

Tunakumbuka Polisi aliye'jinyonga' Morogoro, jiulize ni kiongozi gani wa taifa aliyefuatilia kubaini madai yake na ukweli wa kifo chake? Huyu ndiye subordinate na sasa amesahaulika.

'Kovaaa' na sinema inayoendelea ni mfano tu kuwa subordinate ni victims of circumstance. 'Kovaa' anajua kuwa madai anayotoa si kweli, lakini afanyeje? Angeweza kuwa na ushujaa wa kuacha kazi kama dalili za kuwajibika, nakuhakikishia mfumo utamstaafisha kwa neno R.I.P

Kwa swali hili nadhani wenzetu wa nchi nyingine wametuzidi. Mfano tu, Marekani inapomchagua waziri (secretary) ni lazima athibitishwe na Senate na anawajibika kwa bodi ya taasisi yake na si Rais tena.
Uingereza kuna sheria za kuwalinda mavuvuzela (whistleblower) pale wanapotoa habari za uhalifu makazini, sisi zipo?

Kuhusu swali la pili;
Nakubaliana nawe 100% kuwa tofauti ya vipato imekuwa ya kutisha. Ukweli wa kuwa hatuwezi kuwa na vipato sawa hauna ubishi lakini tulipofikia panatisha. Tunaambiwa mshahara wa Mbunge lazima uwe wa commonwealth standard, si wa daktari au Mwalimu.
Hili limejenga madaraja ya kuhasimiana kimapato 'class warfare' na ndilo chimbuko la migomo.
Lakini karani au mesenja ana chama gani cha kumtetea?
Kwakwe eneo la kazi si kupata mapato ni sehemu ya dili na hapo ndipo elfu kumi haipiti pembeni kabla ya faili kushughulikiwa.

Tufanye nini?
Mahali popote duniani nidhamu inawekwa na sheria. Sheria zetu hazikulenga kuweka nidhamu bali kutetea kundi fulani.
Narudia tulitakiwa tutengeneze sheria za kumbana kila mmoja wetu kuanzia juu hadi chini.

Nikupe mfano, kuna nchi mmoja niliwahi kuetembelea. Niliona mfanyakazi anaingia kazini akiwa amechelewa. Siku hiyo CEO alikutana naye. CEO hakuongea naye alimbana Director, Director akamshukia Manager, Manager akammaliza jamaa kwa kumshukia supervisor. Mfanyakazi hakuwajibishwa na CEO aliwajibishwa na supervisor kwa nguvu ya CEO kimtirirko.

Tanzania haiwekani kwasababu ile chain of command haipo. Rais amesikia madudu ya Waziri basi anachokifanya ni kuunda tume na mazingaombwe mengine siku zinasonga. Endapo Rais angemshukia Waziri na waziri akamshukia katibu mkuu na katibu mkuu kumshukia mkuu wa kitengo, karani gani angekuwa na ushujaa au jeuri ya uzembe au Rushwa?

Haiwezekani kwasababu ya mfumo kulindana.Tunasikia madudu ya TANESCO, si Rais, waziri mkuu au waziri awaye anayeweza kuingilia kati. Sababu ni kuwa TANESCO haikutengenezwa kwa mfumo wa uongozi imetengenezwa kama genge kwasababu maalumu. Watauzaje mafuta na nani anajua mgao wa faida za mafuta anachukua nani.

Tulitakiwa tuwe na mfumo ambao Rais, Waziri, katibu mkuu, Mbunge wahisi kuwa nafasi zao ni adha si pepo, ya kwamba jioni ikifika ashukuru kuwa anayo kazi. Hapo mtiririko ungekwenda hadi kwa mfagiaji.

Wenzetu China wamefanikiwa, mfano aliyehusika na kuharibu maziwa kwa kuweka 'melanin' kuanzia mkuu wa mamlaka ya chakula, wakuu wa vitengo na wale waliojua mpango mzima wote wamelamba shaba(Risasi).

Japan ukisikika tu na tuhuma za ruswa basi mtu anajinyonga kabla, kwasababu hakuna Lawyer atakayemtetea na huyo atachezea kitanzi awe mtoto au shemeji wa mfalme au waziri mkuu.

Alieymweka Bush jnr madarakani Scooter Libby na mshauri wa Rais wa Marekani alipopatikana na hatia ya CIA leaks hakukuwa na jinsi wala kodrai, yupo 'Segerea ya Marekani' anacheza na prison warden.
Martha Stuwart tajiri mkubwa alipopatikana na hatia ya kukwepa kodi alikwenda 'Keko'

Tanzania: Nani amewajibika kwa Kagoda, Meremeta, TRC, ATC, Richmond na madudu mengine? Hakuna
Kwanini tuone hakimu wa mahakama ya mwazo, mwalim, Nurse na karani wanapaswa kuwa na uwajibikaji na uzalendo zaidi!
 
Mkuu Nguruvi, uliyosema ni kweli kabisa. Ila lile swala la rais anayeteua watu hao naye kutojali wakati yeye ni mtanzania mweneztu aliyepewa dhamana ya kulea taifa hili ndilo jambo la kujiuliza tena kuwa Wataznaia tulikosea wapi basi hadi tukawa na viongozi wa aina hiyo?
 
Mkuu Nguruvi, uliyosema ni kweli kabisa. Ila lile swala la rais anayeteua watu hao naye kutojali wakati yeye ni mtanzania mweneztu aliyepewa dhamana ya kulea taifa hili ndilo jambo la kujiuliza tena kuwa Wataznaia tulikosea wapi basi hadi tukawa na viongozi wa aina hiyo?
Kichuguu, wenye lugha zao wanasema 'The buck stops with president'
 
(1) Je ni kweli kuwa watu wote wanofanya mambo hayo ya kutowajibika hawana elimu ya kujua mabaya na mazuri kwa taifa? Mbona watu wtote walliowahi kushukliwa kuliingiza taifa hili kwenye hasara kubwa sana za kimataifa ni wasomi tena wa hali ya juu? Hilo linoanonyesha kuwa ignorance siyo tatizo central. Wala rushwa wote na wanoongoza kwa kutowajibika ni wasomi walio kwenye nafasi za juu sana serikalini.
...Ni kweli, tatizo hapo si elimu, kwao wao. Tatizo ni mwajiri wao -kwa maana ya aliyewapigia kura- amechukua hatua gani ya kuwarejesha kwenye mstari?. Na ndipo tunarudi kule kule!.
(2) Je hiyo ignorance ilianguka ghafla ikajaza matope ndani ya jamii yote au ilianguka kidogo kidogo hadi taifa zima likafunikwa na hayo matope kama ilivyo leo? Iwapo ilianguka ghafla, je ilitokea lini, na ni sababu zipi zilizofanya ianguke? Iwapo ilianguka kidogo kidogo, je ilianza kuangukia wapi, na ni kwa nini ilianzia hapo? Swali hili lenye vipande viwili ndiyo jambo kubwa sana ambalo litatusaidia kuangalia wapi wa kusahihisha iwapo tatizo ndilo hilo.
...Jamii hii haijawahi kuwa huru -kimawazo na tena hadharani- toka tupate uhuru. Na kama hauko huru, ni gharama sana kufuta ujinga katika jamii hii changa. Bahati ya jamii nyingine -wachina wanaweza kuwa mfano- zilielimika miaka mingi nyuma, na kuwa huru katika vipindi fulani fulani. Hii imewafanya wajue wanahitaji kitu gani na namna gani wakipate, bila longo longo nyingi kuwa na nafasi.
 
Ila lile swala la rais anayeteua watu hao naye kutojali wakati yeye ni mtanzania mweneztu aliyepewa dhamana ya kulea taifa hili ndilo jambo la kujiuliza tena kuwa Wataznaia tulikosea wapi basi hadi tukawa na viongozi wa aina hiyo?
...Ujinga ndio kosa letu. Lazima tukubali tu wajinga, ili, tuwe tayari kujifunza na kuelewa.
 
Zakumi,

Hata mimi ni muumini mkubwa sana wa all politics is local; lakini nimewahi kuishi katika vijiji ambavyo vina local politics nikakuta kuwa bado viongozi hawajibiki tena. Yaani wananchi wanakuwa wanamhusudu yule kiongozi waliyemchagua anapokuwa anajineemesha kwa raslimali zao. Kumpinga inakuwa kama vile ni kumuonea wivu!


Ni mawazo mazuri sana lakini sio kwa Maskini na Mjinga.. Umuhimu wa kuweka Umaskini na UJINGA kua vipaumbele ndio njia pekee ya kumkomboa Mtanzania. Pasipo elimu tutaendelea kuvaa mitumba, madawa feki, na households ktk fikra za kimtoni (kama Ulaya) badala ya kukabili mahitaji yetu ktk standard ya juu kulingana na mazingira..Tunaagiza juice ya machungwa, tende na hata nazi kutoka Dubai ni kwa sababu ya UJINGA na huwezi kumweleza kitu Mdanganyika aliyezoea juice ya embe kutoka Dubai.

Samahani kwa kupotea. Majukumu mengi.

Point yangu ya mwanzo ni kuwa tuna matatizo makubwa. Na taaluma ya kutatua matatizo mengine ni sawa na kuuliza Kuku na yai nani wa kwanza.

Tukisema watanzania tatizo letu ni elimu, ni lazima ujiulize je unaweza kupata waalimu wazuri bila ya kuwa na uchumi wa kulipa mishahara mizuri kwa walimu?

Ukisema all politics is local, ni lazima vilevile ukubali kuwa wananchi wachague viongozi wao na watoe kodi za kugharimia shughuli zao za maendeleo. Mtu akitoa mchango wake, haogopi kiongozi.

Wanachama wa Simba na Yanga wako passionate na clubs zao na wako tayari kuchapana bakora kwa sababu wanatoa michango ya kuendesha clubs hizo.

Similarly, watanzania wakichangia huduma zao watakuwa tayari kupigania ubora wake.
 
Samahani kwa kupotea. Majukumu mengi.

Point yangu ya mwanzo ni kuwa tuna matatizo makubwa. Na taaluma ya kutatua matatizo mengine ni sawa na kuuliza Kuku na yai nani wa kwanza.

Tukisema watanzania tatizo letu ni elimu, ni lazima ujiulize je unaweza kupata waalimu wazuri bila ya kuwa na uchumi wa kulipa mishahara mizuri kwa walimu?

Ukisema all politics is local, ni lazima vilevile ukubali kuwa wananchi wachague viongozi wao na watoe kodi za kugharimia shughuli zao za maendeleo. Mtu akitoa mchango wake, haogopi kiongozi.

Wanachama wa Simba na Yanga wako passionate na clubs zao na wako tayari kuchapana bakora kwa sababu wanatoa michango ya kuendesha clubs hizo.

Similarly, watanzania wakichangia huduma zao watakuwa tayari kupigania ubora wake.
Zakumi mkuu wangu karibu usipotee hivyo.. Kitu kimoja nakubaliana na wewe kuwa tatizo la Tanznaia ni sisi Watanzania wenyewe lakini sidhani kuwa ni swala la fedha na malipo sawa na thamani ya kitu. Nijuavyo interaction ya supply and demand ndio kutupa bei ama thamani ya kitu. Huwezi kumchukua maskini ombaomba kumuuzia elimu ambayo kwake sio priority ya siku wlaa maisha maana hana hata hela ya kuweka mkate mezani unafikiri kweli ataithamini elimu?. Hivyo as long as price is derived by demand and supply, the resultant market price ya mwalimu (supplier) haiwezi kuwepo ikiwa maskini hana demand na elimu hiyo.

Hivyo swala la malipo bora ya walimu haiwezi kubeba uzito mkubwa sana wa mapungufu yetu, isipokuwa kuijenga demand ya elimu kwanza. Elimu lazima iwe compasory na sii ya kulipia maana maskini hana uwezo wala sio priority yake given the choice. Wakati wa Nyerere tulipata elimu bure na bora sana japokuwa kidogo na watu waliridhika.. Nitakukumbusha ya kwamba wakati wa Nyerere na Ujmaaa wake kati ya wanafunzi 10 waliokwenda kusoma nchi za nje 9 walirudi nyumbani, leo hii baada ya kuingia Ubepari kati ya 10 wanafunzi 6 hadi 8 hubakia nje kutokana na kuanza kuthaminisha elimu zao kulingana na masoko ya nje. Before wakati wa Nyerere wasomi walithaminisha demand ya huduma zao kuwa ni muhimu kw amaendeleo ya Mtanzania hivyo walitanguliza UZALENDO mbele ya fedha ama malipo mazuri.

Sasa hivi miaka hii ya JK tumeshuhudia kundi la vijana waliosoma nje wakirudi nchini lakini wengi wao wakiwa wamebeba vyeti feki kwa sababu ndio market price inayotokana na demand iliyopo sasa hivi. Kifupi tunachokihitaji Tz leo ni vitu cheap lakini icvnafanana na vile vya Ulaya -Feki.. Mtu akiwa anazungumza kiingereza ana nafasi kubwa ya kuajiliwa kuliko msomi wa UDSM asiyejua lugha ya kiingereza infact tunamcheka sana kuona graduate wa UDSM hajui lugha ya kiingereza. Elimu kwetu ni lugha sio msingi wa kutuongoza ktk maamuzi mengi ya kimaendeleo..Huu ni wakati wa Utapeli na kufungiana kanyaboya zaidi ya malipo bora ya kazi wanayoifanya. Hii ndio reality mkuu wangu lazima tuipime, kuitafakari na kuipatia suluhishio.

Swala la mchango wa wananchi kuhusu elimu na Ubora wake sii lazima iwe hivyo isipokuwa ni standard zinazowekwa na mhusika. Mali mbovu huenda kwa yule mwenye kuacha kuthamini ubora. Kama weee hujali kuvaa vizuri basi hata ukiwa na billioni hutavaa vizuri kutokana na uthaminisho wa mavazi. Leo hii tunavaa mitumba sii kwa sababu hatuna fedha ama mchango wetu bali hatuthamini nguo mpya zaidi ya mitumba. Tunaletewa vitu feki ni kwa sababu hatuna standard vivyo hivyo elimu mbovu kwa sababu hatuna standard. Yote haya yanatokana na jinsi gani unajithamini wewe mwenyewe na bahati mbaya sisi tanzania tumeshusha thamani yetu kiasi kwamba elimu sii kitu lazima kwa maskini.

Yule maskini ombaomba mtaani siku zote hutazama vitu necessary kwake ndani ya umaskini wa ombaomba na sii kujikwamua ktk umaskini ule, yaani living within his means..(end justifies the means) hivyo anaamka asubuhi na bakuli mkononi akizunguka ktk routine yake ya kila siku kulijaza bakuli lake hawezi kufikiria nje ya ujazo wa hilo bakuli.

Zakumi, nakuhakikishia moja, hakuna maskini ombaomba yeyote anaamini ELIMU inaweza kumwondoa kusimama mtaani kuomba riziki ya siku na ndio maana husisitiza ni muhimu kuingia ktk kichwa cha mwendawazimu (Insane) kufahamu kwa nini hufanya uendawazimu. Kwake yeye muda ule wa kwenda shule jifunza kazi ama ujuzi ni kupoteza nguvu na riziki ya siku kwa sababu kipimo cha mafanikio yake ni ujazo wa bakuli ama kuweka mkate mezani mwisho wa siku. Huu ndio Ujinga unaotakiwa kuondolewa kifikra, tunatakiwa kuwahamasisha Watanzania kutambua umuhimu wa elimu na ujuzi ya kwamba kutembea na bakuli mkononi sii suluhisho. kuondoa fikra za utumwa kuamini kuwa ni kilema, hiyo sio destiny alopangiwa na Mola ama umaskini wetu ni curse, hivyo hakuna means nyinginezo isipokuwa kutembeza bakuli, tushindane kwanza na dhana hii potovu..

Inasikitisha zaidi napowaona viongozi wetu wameondokana na imani hii badala yake wakitumia akili ile ile ya maskini ombaomba kutafuta mafuta na gas kama yule maskini ombaomba ambaye hutembea mitaa ya Uhindini akizama ktk mapipa ya taka kwa mategemeo ya kuibuka na kitu cha thamani. Imani ambayo inakataa kabisa kuamini kuwa tatizo ni (yeye ama sisi) sio wapi ataipata riziki ya siku ama utajiri wa kumtoa ktk kuombaomba. Bado tuna fijkra za kimaskini ombaomba hatujaondokjana na utumwa wa fikra. Huruwezi kufikiria sawa na Mzungu aliyeondoka mtaani kuombaomba pasipo kufuata njia alozitumia kufikia hapo alipo.

Tatizo la Tanzania ni kubwa ziadi ya Ubepari maana Walimu na Madaktari wanataka kujithaminisha wao pasipo mnunuzi kuelewa thamani ya huduma zao. Wakati wa Mwinyi alijaribu kutaka kuwalipa walimu mishahara mizuri, kwa kutoza karo shule za msingi. mwaka uliofuata wanafunzi waliojiandikisha kujiunga na shule hizo iliporomoka kufikia chini ya asilimia 50...ikabidi awamu ya pili ya Mkapa arudishe elimu bure kwa shule hizo. Elimu na Afya sio swala la biashara hata siku moja kwa mtu maskini. Ni necessity - mandatory! tukisha kuwa na uwezo, then inaweza kuwa biashara..
 
Back
Top Bottom