Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 11,206
- 18,994
Hili ni jambo ambalo wenye hekima wanalielewa siku nyingi, na labda wengine wengi sasa wameanza kulielewa, kwamba kutokuwepo kwa usimamizi wa kiserikali wa upande wa bara kunatokeza nafasi kwa raisi akitoka Zanzibar kuwa na uwezekano wa kufanya mambo kwa namna ambayo inatoa maslahi makubwa upande wa Zanzibar kuliko upande wa bara au wa muungano kwa ujumla.
Lakini sio rahisi kwa raisi wa Tanzania atokaye bara kufanya kazi kwa maslahi ya bara zaidi kuliko visiwani, kwa kuwa Zanzibar ina serikali yake tayari ambayo inasimamia maslahi ya visiwani, na inajumuishwa katika serikali ya muungano.
Kuna mambo kadhaa yamekuwa yakijadiliwa ambayo nitayaainisha hapa chini. Haya ni maoni toka wadau mbalimbali na nayaweka hapa ili kutoa wigo wa kuyajadili, sio kama shutuma.
Maoni mojawapo ni kwamba udhaifu wa kutoa maslahi upande wa visiwani raisi akitoka visiwani unajitokeza hasa ukizingatia kwamba katiba ya Tanzania inampa raisi mamlaka makubwa ya kuamua mambo bila hata kujadiliana na viongozi wengine au kuwa na kikao rasmi kitakachowakilisha maoni ya upande wa bara. Rais kutoka visiwani ana uwezo wa kupanga baraza la mawaziri kimkakati ili kuinufaisha Zanzibar, na hakuna namna ya kuweza kumzuia. Labda mfano mzuri katika suala hili ni suala la DP World na bandari, ambapo Zanzibar waliikataa DP World kwa sababu wana uwakilishi wao wa kiserikali, tofauti na bara. Sasa inakuwa kama raisi wa kutoka visiwani aliiamulia Tanzania bara kuwa na DP World. Je kungekuwa na serikali ya Tanzania bara, hili lingekubalika?
Na pia kuna maoni kwamba kila inapotokea raisi akitokea Zanzibar, ule msukumo wa kutoka Zanzibar kutaka muungano urekebishwe au uvunjwe unakwisha. Swali ni kwa nini? Je, ni kwa sababu katika hivyo vipindi upande wa visiwani unaona kuwa unafaidika zaidi na uwepo wa raisi kutoka visiwani? Wengine wamedokeza kwamba wakati wa raisi Magufuli uchumi wa Tanzania ulionyesha kukua zaidi ya uchumi wa Zanzibar, lakini kwa sasa uchumi wa Zanzibar unakuwa kwa kasi zaidi ya ule wa Tanzania, kuonyesha kwamba upande wa bara kuna kushuka kwa kasi ya kukua kwa uchumi. Na wengi wanaona hili linaweza kuwa linachochewa na maslahi mengi ya kitaifa kuelekezwa upande wa visiwani kwa kuwa kuna raisi toka visiwani.
Labda lililo kubwa zaidi ni maoni kwamba ikiwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar uko katika hatari ya kuvunjika, au kwamba watu wa upande wa visiwani hawautaki japo hawasemi hivyo hadharani, hatuoni kwamba tunaweza kumpata raisi kutoka visiwani ambae hana imani na muungano, japo anadai kuutetea, na akafanya mambo kwa namna ambayo kama muungano ukivunjika basi awe amewanufaisha upande wa visiwani kwa namna ya kutosha, yaani akatumia fursa ya uraisi wake kuimarisha upande wa visiwani akijua muungano unaweza kuvunjika wakati wowote?
Mfano umetolewa kwamba wakati Jumuiya ya Afrika Mashariki ikikaribia kuvunjia miaka ya 1977, Wakenya wakijua hili kwamba walitaka kuivunja jumuia, walifanya mkakati wa mali za jumuiya ya mashariki kuhodhiwa upande wa Kenya. Siku jumuiya ya mashariki ilipovunjika Tanzania na Uganda walikuja kugundua kwamba Kenya walikuwa na mkakati huu siku nyingi na walitenda mambo wakijua hilo linakuja! Je philosophy hii inawezekana pia katika suala la muungano, kwa kuwa upande wa bara hakuna serikali itakayokuwa macho kusimamia maslahi ya bara?
Sasa haya ni mambo yanajadilika na ni muhimuhimu kuyatafakari katika suala la muungano. Ndio maana basi, tukiri kwamba katika mfumo wa muungano uliopo, inawezekana kabisa raisi kutoka Zanzibar akafanya kazi ya uraisi kwa maslahi ya Zanzibar zaidi ya bara au ya muungano. Kujifanya kama hilo haliwezekani ni kujidanganya, na haya mambo yasipojadiliwa, yanaweza kuleta madhara na chuki zisizostahili. Na lazima pia tukiri ni mambo kama haya ambayo yamekuwa yakichochea madai ya kuwapo na serikali ya kusimamia maslahi ya upande wa bara, kama ilivyo kwa upande wa visiwani.
Nini maoni yako?
Lakini sio rahisi kwa raisi wa Tanzania atokaye bara kufanya kazi kwa maslahi ya bara zaidi kuliko visiwani, kwa kuwa Zanzibar ina serikali yake tayari ambayo inasimamia maslahi ya visiwani, na inajumuishwa katika serikali ya muungano.
Kuna mambo kadhaa yamekuwa yakijadiliwa ambayo nitayaainisha hapa chini. Haya ni maoni toka wadau mbalimbali na nayaweka hapa ili kutoa wigo wa kuyajadili, sio kama shutuma.
Maoni mojawapo ni kwamba udhaifu wa kutoa maslahi upande wa visiwani raisi akitoka visiwani unajitokeza hasa ukizingatia kwamba katiba ya Tanzania inampa raisi mamlaka makubwa ya kuamua mambo bila hata kujadiliana na viongozi wengine au kuwa na kikao rasmi kitakachowakilisha maoni ya upande wa bara. Rais kutoka visiwani ana uwezo wa kupanga baraza la mawaziri kimkakati ili kuinufaisha Zanzibar, na hakuna namna ya kuweza kumzuia. Labda mfano mzuri katika suala hili ni suala la DP World na bandari, ambapo Zanzibar waliikataa DP World kwa sababu wana uwakilishi wao wa kiserikali, tofauti na bara. Sasa inakuwa kama raisi wa kutoka visiwani aliiamulia Tanzania bara kuwa na DP World. Je kungekuwa na serikali ya Tanzania bara, hili lingekubalika?
Na pia kuna maoni kwamba kila inapotokea raisi akitokea Zanzibar, ule msukumo wa kutoka Zanzibar kutaka muungano urekebishwe au uvunjwe unakwisha. Swali ni kwa nini? Je, ni kwa sababu katika hivyo vipindi upande wa visiwani unaona kuwa unafaidika zaidi na uwepo wa raisi kutoka visiwani? Wengine wamedokeza kwamba wakati wa raisi Magufuli uchumi wa Tanzania ulionyesha kukua zaidi ya uchumi wa Zanzibar, lakini kwa sasa uchumi wa Zanzibar unakuwa kwa kasi zaidi ya ule wa Tanzania, kuonyesha kwamba upande wa bara kuna kushuka kwa kasi ya kukua kwa uchumi. Na wengi wanaona hili linaweza kuwa linachochewa na maslahi mengi ya kitaifa kuelekezwa upande wa visiwani kwa kuwa kuna raisi toka visiwani.
Labda lililo kubwa zaidi ni maoni kwamba ikiwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar uko katika hatari ya kuvunjika, au kwamba watu wa upande wa visiwani hawautaki japo hawasemi hivyo hadharani, hatuoni kwamba tunaweza kumpata raisi kutoka visiwani ambae hana imani na muungano, japo anadai kuutetea, na akafanya mambo kwa namna ambayo kama muungano ukivunjika basi awe amewanufaisha upande wa visiwani kwa namna ya kutosha, yaani akatumia fursa ya uraisi wake kuimarisha upande wa visiwani akijua muungano unaweza kuvunjika wakati wowote?
Mfano umetolewa kwamba wakati Jumuiya ya Afrika Mashariki ikikaribia kuvunjia miaka ya 1977, Wakenya wakijua hili kwamba walitaka kuivunja jumuia, walifanya mkakati wa mali za jumuiya ya mashariki kuhodhiwa upande wa Kenya. Siku jumuiya ya mashariki ilipovunjika Tanzania na Uganda walikuja kugundua kwamba Kenya walikuwa na mkakati huu siku nyingi na walitenda mambo wakijua hilo linakuja! Je philosophy hii inawezekana pia katika suala la muungano, kwa kuwa upande wa bara hakuna serikali itakayokuwa macho kusimamia maslahi ya bara?
Sasa haya ni mambo yanajadilika na ni muhimuhimu kuyatafakari katika suala la muungano. Ndio maana basi, tukiri kwamba katika mfumo wa muungano uliopo, inawezekana kabisa raisi kutoka Zanzibar akafanya kazi ya uraisi kwa maslahi ya Zanzibar zaidi ya bara au ya muungano. Kujifanya kama hilo haliwezekani ni kujidanganya, na haya mambo yasipojadiliwa, yanaweza kuleta madhara na chuki zisizostahili. Na lazima pia tukiri ni mambo kama haya ambayo yamekuwa yakichochea madai ya kuwapo na serikali ya kusimamia maslahi ya upande wa bara, kama ilivyo kwa upande wa visiwani.
Nini maoni yako?