Tujikumbushe wana Azania

Gamba la Nyoka

JF-Expert Member
May 1, 2007
7,022
9,285
Wazee wa Aza boy mpoo?

Hebu leteni stori wajameni tukumbuke tulipotoka!. ngoja mi nianze na stori za yule ticha anaitwa "mchwa". siku moja mchwa alimkuta jamaa anavuta bangi, kuona vile Mchwa akamtoa mkuku yule jamaa, jamaa kuzidiwa ikabidi apande ngazi hadi madarasa ya juu, Mchwa hamwachii bado anaye tu, kuona vile jamaa ikabidi ajirushe chini ili asikamatwe.

Basi Mchwa akaenda kuripoti kwa HeadMaster, "kaka kakka kaka kwa (sauti ya kukwama kwama), nimerikuta jamaa rinakunywa bange nikarifukuza rikaruka kutoka chini mapaka juu (wakati huo mchwa akisema chini macho yanaangalia juu na kidole kinapointi juu, akisema juu macho yanaangali chini na kidole kinapoiti chini)
 
He he he he kwi kwi kwi kwi tafadhali gamba la nyoka usituvunje mbavu,..............sina mbavu sasa hivi
 
Gamba, mimi namkumbuka Kicheche na Mzee, Meja. Wewe ulikuwepo enzi hizo?
 
Da afadhali gamba la nyoka umikumbuka azania yetu.mi namkumnbuka mzee kwayu headmaster,mzee safi sana huyu,then mkongo,mama maleko,kuna mwalimu wangu alinifundisha english anaitwa mrs kirundu,kuna walimu walikuwa rafu sana kina primus na wenzake.

Nawakumbuka jamaa zangu dedo, jarufu, imani, jesse, onesphory, leodgard, mrema, ndamba, edwini, suya, mwasandube.n.k lidumu chama letu, naskia siku hizi kuna ubabaishaji sana.
 
1. Mwalimu Ibara (Hatibu) - ticha huyu alikuwa anatumia ibara/vifungu hewa vya Katiba kutoa adhabu za kiutani ila wanafunzi tulikuwa tunazitekeleza kweli mfano aliwakuta wanafunzi wanagombana akawapa adhabu ya kufagia darasa mpaka ligi kuu ya Tanzania na mwaka huo simba na yanga zilikacha kucheza mchezo wa ligi hivyo ligi haikuisha...

2. Mwalimu Miti Mingi - huyu na Mchwa Mpaka walikuwa damu damu katika harakati za kuvunja miiko ya HakiElimu na Kuleana ya 'Chapa Kazi Sio Mtoto', da Miti alikuwa na kasauti kaupole hako ila akikucharaza bakora ilikuwa balaa...

3. Mwalimu Mbaga - mzungu wetu huyu alikuwa mpole sana utadhani hua ila utundu ukizidi darasani alikuwa anaita walimu wakali watuchape ila ikifika fimbo ya pili utasikia mama wa watu anasema 'basi chapa tosha tosha'...

4. Mama Semhando - huyu mama alikuwa anatoa somo la Kiswahili la aina yake, ukiwa njuka lazima akutoe mbele ya darasa na akupe neno ulielezee mbele ya darasa...

5. Mwalimu Matley - da mwalimu wa namba huyu alituchapa sana huyu kidato cha kwanza ila akawa besti sana kidato cha pili, nakumbuka sana maswali yake ya vidoti...

6.Mwalimu Mashanga - kinara wa migomo ya walimu, aliitetemesha sana sirikali...

7. Mama Idi - huyu alikuwa my fevoriti maelezo zaidi baadae...
 
Ahaa Kweli hiyo stori ya Mchwa-Mpaka ilikuwepo tehe tehe tehe

Huyu alikuwa discipiline master matata sana kipindi chake ,alikuwa na kigugumizi pia bigwa wa reverse stori zake ukihadithiwa unaweza kudhani ni za kubuni ila ni amini na kweli maana alinifundisha Geoghaphy.Ilikuwa akimwita head master wa Azania enzi hizo Mr.Kwayu kaka!.

Habari yake nyingine nayokumbuka ni baada mechi ya mpira kuisha jioni kunako Pugu na giza ukingia alimkimbizwa na kuchapa bakora sana ila cha ajabu hakuhadithia kesho yake alibaki kumsifia kipa wetu kuwa "alikuwa anapiga mpira kisha anadoka huku akionyesha kudaka ndio kupiga na kupiga ndio kudaka" alikuwa bigwa wa reverse hakika.

Namkumbuka Mwl.Mkongo alikuwa safi sana,kulikuwepo na walimu walevi kama Mushi wa Physcics,.........kulikuweko na Huyu aliyekuwa anaitwa primus ,na Tokyo kwa kupenda kuvaa suruali za chata la tokyo ahaaaaaaaaa.Kulikuwepo na Hatibu nadhani huyu alikuwa anapenda sana michezo.Tulikuwa na mama huyu wa kihindi (Dhasi)alikuwa mzuri sana kwenye chemistry bila kusahau mama Shija mzuri mno kwenye chemistry alikuwa akifundisha A'level.Kulikuwa na mama kiarabu pia akifundisha Math.

Kuna yeyote anakumbuka maneno haya msuli kitanda ,msuli tamaa, sodoma ,gomora, masaki, mirembe
Nakumbuka kipindi chetu tulikuwa na umoja sana pale we have a lot of funy things also kuna watu nimewakumbuka sijuhi wako hapi kuna haja kutafutana.
 
1. Mwalimu Ibara (Hatibu) - ticha huyu alikuwa anatumia ibara/vifungu hewa vya Katiba kutoa adhabu za kiutani ila wanafunzi tulikuwa tunazitekeleza kweli mfano aliwakuta wanafunzi wanagombana akawapa adhabu ya kufagia darasa mpaka ligi kuu ya Tanzania na mwaka huo simba na yanga zilikacha kucheza mchezo wa ligi hivyo ligi haikuisha...

2. Mwalimu Miti Mingi - huyu na Mchwa Mpaka walikuwa damu damu katika harakati za kuvunja miiko ya HakiElimu na Kuleana ya 'Chapa Kazi Sio Mtoto', da Miti alikuwa na kasauti kaupole hako ila akikucharaza bakora ilikuwa balaa...

3. Mwalimu Mbaga - mzungu wetu huyu alikuwa mpole sana utadhani hua ila utundu ukizidi darasani alikuwa anaita walimu wakali watuchape ila ikifika fimbo ya pili utasikia mama wa watu anasema 'basi chapa tosha tosha'...

4. Mama Semhando - huyu mama alikuwa anatoa somo la Kiswahili la aina yake, ukiwa njuka lazima akutoe mbele ya darasa na akupe neno ulielezee mbele ya darasa...

5. Mwalimu Matley - da mwalimu wa namba huyu alituchapa sana huyu kidato cha kwanza ila akawa besti sana kidato cha pili, nakumbuka sana maswali yake ya vidoti...

6.Mwalimu Mashanga - kinara wa migomo ya walimu, aliitetemesha sana sirikali...

7. Mama Idi - huyu alikuwa my fevoriti maelezo zaidi baadae...

Duh umenikumbusha neno njuka ahaaaa
Mitimingi tehe tehe......

Hivi Mashanga aliendelea kufundisha kweli pale azania .
 
Duh, mimi nilimwacha Mchwampaka akiwa mgeni kumbe alikuja ukwaa U-discipline master? Hatibu alinifunidha Historia F 3, kuna siku nilimkwangulia 86% kwenye mtihani wanafunzi wengine hawakuamini! Alikuwepo pia Mwl Temba wa Gegraphy nasikia alikuja kuhamia Jitegemee maana Wanafunzi walimpachika jina kuwa ni Mwl. Bomu! Mitimingi sikumuacha lakini nakumbuak Mwl. wa Siasa aliyeitwa Mbazigwa ambaye baadaye alikjiunga na RTD sasa TBC kama Mwandishi wa habari.

Yaani Mzee kwayu mimi aliniboa sana alipokuja kuchukua nafasi ya Mwl Kisamo kama Mkuu wa shule. Enzi ya Kisamo sheria za shule zilikuwa haziruhusu kuchomekea (upo hapo?) kwa kuwa mimi nilikuwa ant-kuchomekea nilichagua Azania maana niliiona joining instruction ya jamaa yangu aliyechaguliwa mwaka mmoja kabla yangu. Alipokuja Mzee Kwayu akaiondoa hiyo sherai na akalizmaisha tuwe tunachomekea mashati. Enzi hizo tulikuwa tunavaa kaputula za khaki!

Nakumbuka UMISETA pia, Tambazawalikuja kucheza na Azania na mwisho wa mechi wakaanzisha vagi, tuliwatimua vibaya mono na hawakuamini maana walikuwa wanatuona Azania ni wangyonge wao, nakumbuka nilipigwa na na papai mbavuni katika vurugu hizo ndipo nami nikapagawa ingawa nilikuwa sipendi vurugu. Mechi tuliwafunga na kuwapiga juu baada ya mechi. Pia namkumbuka Mwalimu Faustin wa Kiingereza alikuwa akiandika 't' utadhani kaandika 'L'.

Companero, kulikwa na Waalimu wazungu wawili Mbaga na Malocho (nadhani ulimsahau au alikuwa keshaondoka).
 
Eeeeee bwanaeee,Mchwampaka alikuwa noma kichizi;ila kuna mwalimu wangu alikuwa anatufundisha physics Mwl.Mosha alikuwa peace sana;tatizo lake ni kwamba alikuwa napenda sana kuvuta fegi mara anakohoa mara samahani kidogo kumbe anaenda kuongeza nguvu kwa madai yake huku hajui kama anajiua mwenyewe taratibu.

Kiboko ya wote kuna Mwl.Matey alikuwa anatufundisha ugonjwa wa Taifa,acha kabisa ukichemsha katika hilo somo mwenyewe unakosa amani kabla hata hujaonana nae alikuwa anachapa bakora vibaya,utasikia shika meza nyooka ukijitia hujui anakuondoa stand;watu wengi walikuwa wanamnyaa huyu mchizi ile mbayaaaaa.

Chama letu lidumu zaidi na zaidi maana yake tumetokea mbali Azania Boys hadi hivi sasa sijui ni nini vile maana wamechanganyika na mademu duh!
 
Mod I think is getting too much sasa kila mtu akitaka kukumbukia secondary tulizopitia JF itajaa, maana tuna shule nyingi na almost kila moja kuna waliopitia kule....nami nianzishe ya kwangu Tukumbukane wana Kigonsera? Tukumbukane wana Kazamwendo Secondary?

Boring
 
Mod I think is getting too much sasa kila mtu akitaka kukumbukia secondary tulizopitia JF itajaa, maana tuna shule nyingi na almost kila moja kuna waliopitia kule....nami nianzishe ya kwangu Tukumbukane wana Kigonsera? Tukumbukane wana Kazamwendo Secondary?

Boring

Ni kweli Mkuu ni bora hizi thread ziondolewe kwa sababu hata Wanafunzi wenyewe tulisoma miaka tofuti sana na tunakuwa hatuna common sharing katika hizi therad za mashule.

Mod, naunga mkono, ziondolewe.
 
Ni kweli Mkuu ni bora hizi thread ziondolewe kwa sababu hata Wanafunzi wenyewe tulisoma miaka tofuti sana na tunakuwa hatuna common sharing katika hizi therad za mashule.

Mod, naunga mkono, ziondolewe.

kweli hii thread haina mpango,mimi nimesoma AZANIA wakati inaitwa ALL INDIA,sasa whatever i say nani katika hii forum atanielewa
 
Tukubali ukweli, kuna shule zilitikisa in one time or another: Kwa mtizamo wangu kanda ya kaskazini ilikuwa moto, baadhi yao ikiwa ni shule za Ilboru (smart boys), Umbwe, Old Moshi, wakulima wa Lyamungo bila kuwasahau wazee wa Maua for boys. Weruweru, Kibosho, Machame, Ashira ni baadhi ya shule za wasichana kanda ya kaskazini.

Jangwani, Azania, Tambaza (hawa walikuwa kiboko time fulani) Kilakala, Mzumbe, Msalato, Mazengo na Bihawana kanda ya mashariki na kati.

Wacha watu watalk their times. Cha muhimu ni kutatafuta mode ya kuziweka, may be after a time zote ziunganishwe na kuwa thread moja.
 
kweli hii thread haina mpango,mimi nimesoma AZANIA wakati inaitwa ALL INDIA,sasa whatever i say nani katika hii forum atanielewa

Kwa kweli tumesoma vipindi tofauti katika mazingira tofauti hata kama ni shule moja, Mod ziunganishe hizi, baadaye zitakuja tuliokuwa operation jongoo kambi ya Mgambo JKT Tanga unamkumbuka Afande Suluari? na yule Bitozi MP commander? tena colleges na Universities, story za unamkumbuka Prof Kofia pale Makerere kwenye lile darasa la Medicine mwaka 1963? hahahah wachangiaji wengine itakuwa ni kuangalia sinema ya kichina.....

Ushi
 
MAMA,MAMA,MAMA yaani umetaja shule zote umeliacha baba lao KIBAHA source no 1 ya ma intellectuals wa tanzania,hii omission constitutes a crime against the people of tanzania
 
Si ndo utamu wenyewe wa JF, kwani lazima kila wakati ukomae tu na macurrent issues? By the way the best thing ukiona thread inakuchefua, iskip. JF ni diverse community with diverse of interests.
 
Si ndo utamu wenyewe wa JF, kwani lazima kila wakati ukomae tu na macurrent issues? By the way the best thing ukiona thread inakuchefua, iskip. JF ni diverse community with diverse of interests.



Wewe umenena,katika thread zote hizi kwa nini wanaingia kwenye ile ambayo hawaipendi,just skip the damn thread and let other people have fun.
Ati tumesoma kipindi tofauti sana ,hawa hawakawii kusema wameishi kipindi Dar es salaam initwa Mzizima .
 
Poa mwana ! enzi hizo Mchwampaka ! aliwakamata madogo wamewasha moto kiwanjani saa sita mchana wanaota! kumbe walikuwa wanakamua jani kiulaini walipomuona wakatupa vipisi kwenye moto!
 
jus had to go through dis thread as nilipitia azaboy for few weeks!yaani nilisoma pale for few weeks nt even a month

hiyo ya majamaa kuwa wanachoma jani mchana kweupe wakakamatwa na ticha wakadai walikua wanaota moto imeniua kinyama,with joto la bongo lichomalo ka pasi eti bado madogo walikua wanaota moto lohhhh!!!

n hao wanaodai sijui hizi thread za shulez zifungwe wajimini huko ndo kukosa freedom of speech kwenyewe huko...yani u want to limit everyone over here to read n b interested on things u jus wanna b interested on??arent u guys fed up on those things u declare them as current issue??sijui hot ones?au kwa kulonga longa tu wat do they help kwa sana?

if urnt interested in kusoma mambo ya shulez why shud b bothered abt the whole thread n kuanza kuzisoma???

ndo nyie nyie wakataa kwenu,as mwaanza taratibu kukataa history na mkataa kwao,pabaya panamwitaaa

even if shule yako ni madongo kuinama international expensive school ya kule kisaluvachole sijui wapi hukooo if u get wenzio wa kukumbushiana history ya skonga lenu sio vibayaaa atiii it cud b one of de ways ya kupunguza stress n kupata tabasamu na vicheko on ur face ujiongezee siku zako za kuishi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom