Nilishangazwa sana na kitendo cha Nakaaya kuamua kukabidhi kadi ya CHADEMA kwa Mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni mgombea urais kupitia chama hicho. Nakaaya kwenye Magwanda ya CHADEMA nilikuwa namwona kama nuru ya vijana wenye mioyo ya kimapinduzi na wenye kutakia mema Tanzania yetu. Baada ya kutafakari sana nilimegundua nilikuwa nakosea, Nakaaya ametumia haki yake na maamuzi yake lazima yaheshimiwe. CHADEMA ni taasisi na si mtu ama watu, wengi watajiunga na wengi wataondoka ila chama kitakuwepo na kitaendelea kuimarika kwa wale wote wenye moyo na itikadi za CHADEMA.
Mapinduzi ya kweli yanahitaji askari wenye moyo na wale wenye uwezo wa kujitoa muhanga. Sasa kama unapewa ice cream na unaweza kutoa siri wapi alipojificha jemadari mkuu wako ni hatari sana! Heri ukaachana na mapambano kabla hujasaliti. Nimeonana na Nakaaya mwanzoni wa mwaka huu nikampongeza kwa wimbo wake wa Mr Politician tukaongea mengi, mipango yake ya music na siasa. Anajiamini sana hana haiba za wadada wengi wa Kitanzania, anapenda ishi maisha yake. Siku ile alikuja na ML class Mercedes Benz nyeusi, Mchungaji nikaweka heshima. Sijui kama ni la kwake ama alikuja safisha nyota!
Kama kweli Mil 30 alizoahidiwa mwisho wa Kampeni kama wale wasanii wenzake, walio kwenye kampeni za CCM, ndicho hasa kilichomtoa CHADEMA basi siasa hatoziweza maana akipewa dhamana yuko tayari kuuza hata uhuru wetu.
Kuwa Upinzani kunahitaji uwe na moyo wa Simba, si kila mtu anaweza. Mchungaji nimejitoa muhanga niko tayari hata kujilipua uongozi wa imla na kikoo wa CCM ufikie mwisho. Nimalize kwa kumpongeza sana sana kwa uamuzi wake wa kwenda kwenye kundi la ndege analofanana nalo rangi! Sababu anajua udhaifu wa kiutendaji wa Mwenyekiti wake mpya basi kura yake bado tunaihitaji CHADEMA.
Vote for Slaa
Wenu Mchungaji
Rev Masa
Peace to you all
Mapinduzi ya kweli yanahitaji askari wenye moyo na wale wenye uwezo wa kujitoa muhanga. Sasa kama unapewa ice cream na unaweza kutoa siri wapi alipojificha jemadari mkuu wako ni hatari sana! Heri ukaachana na mapambano kabla hujasaliti. Nimeonana na Nakaaya mwanzoni wa mwaka huu nikampongeza kwa wimbo wake wa Mr Politician tukaongea mengi, mipango yake ya music na siasa. Anajiamini sana hana haiba za wadada wengi wa Kitanzania, anapenda ishi maisha yake. Siku ile alikuja na ML class Mercedes Benz nyeusi, Mchungaji nikaweka heshima. Sijui kama ni la kwake ama alikuja safisha nyota!
Kama kweli Mil 30 alizoahidiwa mwisho wa Kampeni kama wale wasanii wenzake, walio kwenye kampeni za CCM, ndicho hasa kilichomtoa CHADEMA basi siasa hatoziweza maana akipewa dhamana yuko tayari kuuza hata uhuru wetu.
Kuwa Upinzani kunahitaji uwe na moyo wa Simba, si kila mtu anaweza. Mchungaji nimejitoa muhanga niko tayari hata kujilipua uongozi wa imla na kikoo wa CCM ufikie mwisho. Nimalize kwa kumpongeza sana sana kwa uamuzi wake wa kwenda kwenye kundi la ndege analofanana nalo rangi! Sababu anajua udhaifu wa kiutendaji wa Mwenyekiti wake mpya basi kura yake bado tunaihitaji CHADEMA.
Vote for Slaa
Wenu Mchungaji
Rev Masa
Peace to you all