Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,494
- 113,590
Salaam,
Habari toka nchini Afrika Kusini, zinasema,
Katibu Mkuu wa Ikulu Mstaafu, Mzee Timothy Apiyo, amelazwa kwenye hospitali ya Milpark nchini Afrika Kusini.
Mzee wetu huyu ambaye ni mjamaa wa kweli kama Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, alikuwa ni Katibu Mkuu wa Ikulu kwa Kipindi kirefu mpaka alipostaafu na kuhamia Kinyerezi hapa jijini Dar es Salaam ambapo ameendelea kuishi maisha ya kawaida ya kijamaa kwa kufuata falsafa ya Baba wa Taifa Mwl. Nyerere.
Mzee Apiyo ambaye kiumri ni mtu mzima, alifiwa na mke na mtoto siku za nyuma, na hivi karibuni, alifiwa tena na mtoto wakati tayari akiwa nchini Afrika Kusini.
Tunaomba Mungu aifariji familia ya Mzee Apiyo, awape nguvu, baraka na uwezo ili wayaweze yote katika Yeye awatiaye nguvu na kuwapa baraka za uponyaji wa haraka...Amen.
Habari toka nchini Afrika Kusini, zinasema,
Katibu Mkuu wa Ikulu Mstaafu, Mzee Timothy Apiyo, amelazwa kwenye hospitali ya Milpark nchini Afrika Kusini.
Mzee wetu huyu ambaye ni mjamaa wa kweli kama Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, alikuwa ni Katibu Mkuu wa Ikulu kwa Kipindi kirefu mpaka alipostaafu na kuhamia Kinyerezi hapa jijini Dar es Salaam ambapo ameendelea kuishi maisha ya kawaida ya kijamaa kwa kufuata falsafa ya Baba wa Taifa Mwl. Nyerere.
Mzee Apiyo ambaye kiumri ni mtu mzima, alifiwa na mke na mtoto siku za nyuma, na hivi karibuni, alifiwa tena na mtoto wakati tayari akiwa nchini Afrika Kusini.
Tunaomba Mungu aifariji familia ya Mzee Apiyo, awape nguvu, baraka na uwezo ili wayaweze yote katika Yeye awatiaye nguvu na kuwapa baraka za uponyaji wa haraka...Amen.