The Infamous
JF-Expert Member
- May 11, 2009
- 731
- 121
R.I.P, viongozi wenzako wa kifrika wamekusaliti wamejaa nyoyo za uoga kama mbwa koko...
Mkuu nimefatilia sana vyombo vya habari vya nje,vimekuwa vikisema walibya wanafurahia kuuwawa kwa Gaddafi,cha kushangaza naona ni vikundi vya watu wachache wachache......siyo kwamba namtetea Gaddafi lakini nchi hz za kiafrika ili ziweze kupata maendeleo lazma kiongoz atumie njia zote ikiwemo na dictatorship...alichotakiwa kujifunza Gaddafi ni kuwa si mtu mmoja anayeweza kuongoza nchi milele....all in all nahic Libya haitakuwa na amani ya kudumu kama ilivyo kwa Iraq,Afhganstan
Hapo amezingirwa na wapiganaji wa vikundi mbali mbali vya waasi wa nchi hiyo pamoja na vijana wadogo wa kijijini kwao.
Ajabu kubwa ni kwamba hawa vijana wanaonekana kuwa ni wenye furaha kubwa kwenye nyuso zao huku wakiendelea kujichukulia kumbukumbu za mwisho wa kiongozi huyo kwa kutumia simu za kiganjani
mzee acha uongo!
mkuu nimefatilia sana vyombo vya habari vya nje,vimekuwa vikisema walibya wanafurahia kuuwawa kwa gaddafi,cha kushangaza naona ni vikundi vya watu wachache wachache......siyo kwamba namtetea gaddafi lakini nchi hz za kiafrika ili ziweze kupata maendeleo lazma kiongoz atumie njia zote ikiwemo na dictatorship...alichotakiwa kujifunza gaddafi ni kuwa si mtu mmoja anayeweza kuongoza nchi milele....all in all nahic libya haitakuwa na amani ya kudumu kama ilivyo kwa iraq,afhganstan
Unajua usichokijua kitakusumbua! Hivi kwa mawazo yako unafikiria kuwa waasi pamoja na watu walioandamana libya ni kwa maslahi ya watu wa libya? Chunguza kwa sasa Obama anaidai mapesa mangapi hiyo libya unayojivunia kwa mapinduzi ya kishetani, vituo vya mafuta nani ameviteka mpaka fidia ya mapesa yanayodaiwa mpaka yarudi yote.
Aliiishi kama Mwanadamu lakini AKUMUHESHIMU MUNGU NDIO MAANA KAFA KIFO CHA AIBU MIKONONI MWA RAIA ZAKE MWENYEWE.Mungu daima yupo katika sura zetu wenyewe.UTU UTU UTU UTU UTU UTU HASA WA MWANADAMU [DIGNITY] ,vaaa mavazi ya UTU utaishi siku nyingi duniani na kuwa UKIWA KIONGOZI UKAVAA KIATU CHA UTU unabaki kuwa ALAMA AU KIOO CHA WALIOBAKI KWENENDA NA MATENDO YAKO.
Mungu awezi kushuka kuja kuonyesha njia ila kwa kupitia wanadamu Mungu anakuwa nasi kutonyesha UPENDO WAKE KWETU,HAKIKA INAPENDEZA SANA KIONGOZI WA TAIFA ANAPOMJUA MUNGU KWA MATENDO YA UTU NA SIO MBWEMBWE ZA KIBINADAMU,MATENDO YA KUWAJALI WATU WOTE BILA KUCHAGUA,KUWALINDA NA KUWATETEA WASIO NA SAUTI,WASIO NA MSEMAJI,WENYE UITAJI.
Hakika kinachouma ni kuwa raia wenzie wenye kuswali nae ibada ya aina moja ndio waliomtendea hayo ambayo kwa imani yao wao ni ishara kuwa MUNGU waliemuomba awaonyeshe adui yao leo hii kawaonyesha.Ndio maana waliomkamata baada ya kumuona na kumkamata SAUTI KUBWA ZILISIKIKA ZIKISEMA ALLAHU AKBAR -[GOD IS GREAT] KIBONGO -MUNGU MKUBWA.
Nyerere atabaki kuwa Mtu wa ajabu dunia aijapata kuona kwa kuwa yale yale aliyoyasimamia miaka nenda ludi ya kuunda TaIFA lenye kujali utu wa Mtu ndio yanayosumbua dunia kuwa watu wanataka UTU wao USAMINIWE NA WAHESHIMIKE.
Hapo amezingirwa na wapiganaji wa vikundi mbali mbali vya waasi wa nchi hiyo pamoja na vijana wadogo wa kijijini kwao.
Ajabu kubwa ni kwamba hawa vijana wanaonekana kuwa ni wenye furaha kubwa kwenye nyuso zao huku wakiendelea kujichukulia kumbukumbu za mwisho wa kiongozi huyo kwa kutumia simu za kiganjani[/QUOTE
picha hii inaonyesha jinsi ambavyo waafrika na hasa waarabu katika tukio hli la kumdhalilisha Gadaff tusivyo na akili. picha inaonyesha waarabu hawa wakikiuka kanuni na alama muhimu za uislamu za kutoonyesha maiti na kuungana na watu wa magharibi kufanya unyama huu.... haikubariki na ni mbaya kwa kumbukumbu ya kizazi kijacho.
Jamani sioalikuwa muumini Allah Subhana u Wataalah na anajenga miskiti? Mbona skuelewi hapa?
Aha kumbe unamaanisha hakumjua Mungu wa kweli aliyejifunua kupitia Yesu Kristo, sasa nimekupata ndugu yangu maana huyo ndiye njia kweli na uzima mtu haingii mbinguni isipokuwa kupitia katika Yeye huyo tu, soma Injili ya Yohana 14:6. Tena huyu jamaa si ndiye alisema Biblia sio kitabu cha Mungu eheee halafu tena kajiita Mfalme wa Wafalme huyu alimkufu Mungu Mkuu na muumba mbingu na dunia ndiyo maana kafanywa hivi. Kwa hiyo kwa ufupi tu kifo chake kina mkono wa Mungu aliye hai, soma Daniel 1:40-43; Ufunuo 19:15-16.
Ni maswali mengi sana watz huwa wakijiuliza pindi vitu vya msingi huwa vikitokea duniani ila cha ajabu zaidi vyombo vyetu vya habari vinakuwa vinatanguliza sana burudani kuliko habari za msingi,,
Hivi juzi yametokea mapigano na hatimaye aliyekuwa rais wa Libya kupigwa risasi na kuuawa, na baada ya kufa vyombo vya habari vya nchi za magharibi na Ulaya kama VOA, BBC,CNN,SKY NEWS na ALJAZEERA vimekuwa mstari wa mbele kuwapa habari wananchi wao na ulimwengu kiujumla kuhusu kifo cha Gadafi ila cha kushangaza ni kuwa kila nilipokuwa nafungua vyombo vyetu vya habari vilikuwa vianapiga mziki, vikionyesha maigizo ya kitz, kinigeria, kihindi, kiphilipino badala ya kuwapa watz habari juu ya habari tete iliyotokea duniani,,
Tunafahamu kuwa hivyo vyombo vya habari vya Ulaya na Magharibi ni vya kimataifa na kila mtu ana uwezo wa kuona ,,lakini siyo kila mtz ana uwezo wa kuelewa kiingereza na kama ingekuwa ndoo hivyo kuvitegemea vyombo vya magharibi kutupa habari pekee basi kusingekuwa na umhimu wa kuwa na vyombo vya habari hapa TZ,,
Na sijaelewa hivi vyombo vyetu vya habari vinafanya kazi kwa matakwa yapi na kwa faida ya nani maana hata habari wanayoitoa wanakuwa wamecopy na kupaste kwa maana hakuna hata chombo kimoja cha habari cha TZ ambacho kinapeleka mwandishi wa habari huko nje kwa ajili ya kukusanya habari zaidi ya kuangalia nao CNN, BBC, VOA na ALJAZEERA na kututangazia bila kujua kuwa wana umhimu wa kwenda huko na kukusanya habari,,,
Je tutafika kama tv zetu na radio zimeweka mbele zaidi burudani za miziki na maigizo kuliko vitu vya msingi?????