Tendwa, Mkuchika watofautiana kuhusu waliotimuliwa udiwani AR

<br />
<br />
Mtanyosha tu maelezo mwisho wa siku, sheria ni msumeno mama! Soma katiba vizuri, uanachama ndo tiketi ya wao kubaki kuwa madiwani otherwise hawana namna zaidi ya kukubali yaishe. Hawnauwezo wa kukilazimisha chama kiendelee kuwadhamini kama wameshindwa kutimiza masharti ya uanachama. Na kwenda mahakamani huku wakiacha kukata rufaa kwenye ngazi za chama ndiyo wamekoroga kila kitu kabisa!
Sheria inasemaje kuhusu kutohudhuria vikao na kususia uhalali wa halmashauri?
Kama wewe ni diwani,je unawakilisha wanachama wenzako tu? Kama hapana,wanakata wasio wanachama wa chama cha diwani mhusika wanashirikishwaje kwenye maamuzi au shughuli mbalimbali za halmashauri ya jiji? Huoni kuwa kususia vikao na kutowakilisha wananchi
ni kuwanyima haki zao?
Je, ni bora kuwa mwanachama ili uwe diwani hewa,au usiwe mwanachama ili uwe diwani wa kweli anayeshughulikia au wakilisha wanakata wenzake regerdless of party affiliation?
Kama uchaguzi wa rais ulikiukwa,mbona wabunge bado wanaingia mjengoni? Why are they submitting themselves to an illegitimate government?
Ukinivua uanachama,nikienda mahakamani halafu nikashinda,mtanirudishia dhamana niliyopewa na wananchi kuwaongoza? Je kama mwingine akiwa keshachaguliwa atafanywaje?
Jibu hayo kwanza.....bado ninayo mengine mengi tu.
 
Mkuchika fani yake ni mwanajeshi, kwa hiyo maamuzi yake siku zote ni kukurupuka tu hatumii akili. Alifanya hivyo ili kumfurahisha Chatanda kwa kuwa wote wanatoka Tanga, sasa ngoja tuone.

sidhani kama mkuchika anatokea tanga ila ninachojua ni kwamba anatokea mtwara, jaribu kutafiti!
 
Hata sijui kama unajua kilichotokea Arusha. Na kama unajua basi huelewi au una akili za Kukwanguliwa

wandima Jibu Hoja usiluke vihunzi hapo,
Wataka kutuambia wanao jibu hoja huu ni lazima wawe wakazi wa Arusha huko mkuu???
 
Kutofautiana katika misimamo ni jambo la kawaida tu hasa unapoendesha au unapowajibika kwa maamuzi makubwa.

wewe ni bonge la NDUNYA! kuna uzito mkubwa wa kutofautiana kwa misimamo NA kutoa maamuzi kinyume na katiba, usitumie 'masaburi' yako katika kutoa hoja, just try to use ur stuff upstairs, of course if there any traces of wisdom in it!
 


wandima Jibu Hoja usiluke vihunzi hapo,
Wataka kutuambia wanao jibu hoja huu ni lazima wawe wakazi wa Arusha huko mkuu???

Hujanielewa Mkuu Jethro, Madiwani wa CDM Arusha wanamuwakilisha nani baada ya kuvuliwa uanachama? Je, Mahakama inaweza kulazimisha mtu kuwa mwanachama? Hawa ni Madiwani kwa Katiba ipi? Kwenye vikao wanawakilisha chama gani? Kesi yao ya Msingi ni IPI (Kurudishiwa uanachama [hivyo tangu sasa sio wanachama] au kutoongelewa kwenye mikutano ya CDM inshu yao?
 
mkuchika kachemsha, waziri gani asiyejua katiba, ingekuwa nchi za wenye kujua maana ya kuwajibika angekuwa keshaachia ngazi au kupigwa chini lakini sio hii bongo isiyojua utawala wa sheria, mawaziri wa jk wa kuokotaokota!LOL
 
Mimi si mweledi wa sheria lakini ninadhani Mkurugenzi, Mahakama na Mkuchika wana wajibu tofauti katika jambo hili. Mkurugenzi anafahamu kuwa diwani anawekewa dhamana na chama cha siasa, na dhamana hiyo ikiondolewa na chama kwa sababu ya chama chenyewe au diwani mwenyewe - ukomo wa udiwani unakuwa umefika. Ifahamike kuwa mahakama imeombwa na walioondolewa dhamani kuwarejeshea dhamana hiyo ili waendelee kuwa madiwani. Kwa mtazamo huo, Mkuchika alipaswa kuona kuwa ni mahakama ndio tu inaweza kuwarejeshea uanachama wa CHADEMA na hivo kuendelea kuwa madiwani. Alichofanya Mkuchika ni kuwarejesha kwenye udiwani akijua kuwa hawana dhamana kutoka CHADEMA. Sheria zimevunjwa na Serikali, si madiwani wala mahakama. Ndio maana Mkuchika yuko matatani.

Ndio hawa hawa wanasema utawala wa sheria. My foot!!!
 
Naipenda Tanzania kila kiongozi nasarakasi zake
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Umeona eeh? Huyu akibinukia kulia mwingine anabinukia kushoto! Mmoja akibembea kihivi mwingine akijining'iniza kivile! Ili mradi tafrani!
 
Hivi wanaccm wengi sheria na katiba ya nchi wanasoma na kuvielewa kweli?ama kwa maksudi tu wanaamua kuzivunja! We ziada na mwita2 ni nani aliyewaroga mpaka muwe na uwezo mdogo wa kupambanua mambo ? Hivi mnaelewa maana ya dhamana?jamani tumechoka
na upupu wenu mnakiharibu kizazi hiki
Cha dotcomç
 
Ukitaka kujua kwamba hao wanaojiita wapambanaji dhidi ya ufisadi ni watu wanafiki tu angalia hii issue. Jamaa wapo kimya. Tunataka tuwasikie katika hili msimamo wenu ni upi? Ama nyie adui yenu ni Lowasa,Chenge na Rostam? Ipo wazi,taratibu zimekiukwa,na kinachoendelea ni uhuni wa viongozi wa serikali. Lakini badala ya mtu kama Waziri mkuu kutatua tatizo ambalo linaweza kutuingiza ktk umwagaji damu,ama bunge kuunda tume ya kuisukuma serikali ili tupate umeme wa kuaminika,jamaa wako busy na mambo ambayo madogo madogo.
 
Hujanielewa Mkuu Jethro, Madiwani wa CDM Arusha wanamuwakilisha nani baada ya kuvuliwa uanachama? Je, Mahakama inaweza kulazimisha mtu kuwa mwanachama? Hawa ni Madiwani kwa Katiba ipi? Kwenye vikao wanawakilisha chama gani? Kesi yao ya Msingi ni IPI (Kurudishiwa uanachama [hivyo tangu sasa sio wanachama] au kutoongelewa kwenye mikutano ya CDM inshu yao?

Ndio wa ndima nimekupatavyema nadhani hata kwa mtu yeyote atakuwa amekupata vyema bila shaka

asubuhi njema mkuu
 
ccm inapumulia kwenye ubabe lakini huu ubabe hadi lini?............................naona mwisho wa hiki chama cha mafisadi kinaelekea ukingoni hasa unapoona hata katiba ya nchi kinaibeza...................kwa msala upitao tu..................
 
Hii ndio tatizo katiba kuelekeza kutea watendaji wakuu serakalini mfano mawaziri kutoka wabunge baadala ya proffesionals. Matokeo yake ni kuwa na watendaji ambao hata basic literacy yao ni ya mashaka sembuse ufahamu sheria na kananu za uendeshaji wa wizara.
 
Hii ndio tatizo katiba kuelekeza kutea watendaji wakuu serakalini mfano mawaziri kutoka wabunge baadala ya proffesionals. Matokeo yake ni kuwa na watendaji ambao hata basic literacy yao ni ya mashaka sembuse ufahamu sheria na kananu za uendeshaji wa wizara.

hawa mafisadi wa ccm hata kama katiba mypa ikiwepo utawakuta wanatoa tafsiri za kuwasaidi wao katika mradi wa kauka nikuvae...........
 
serikali lege lege kila kitu lege lege. Wakiambiwa wanakuja juu kama moto wa kifuu. Maamuzi yao wanachukua gizani, umeme ukirudi wanarealize kuwa wamechemka. Hii issue itawacost tisubiri tu.

tuangalia uchaguzi wa Igunga ili kufahamu kama mbinu za ccm zimebadilika kama siyo kuiba kura, kuzuia wagombea mahari wa upinzani kushiriki uchaguzi kwa kuitumia vibaya NEC na mengineyo yanayofanana na hayo basi kweli watakiona cha moto siku za usoni.........vinginevyo sisi ndiyo tutaona cha moto.............
 
Back
Top Bottom