kichenchele
JF-Expert Member
- Jun 28, 2010
- 539
- 176
moja ya vituo vya television ninavyopenda kuangalia taarifa ya habari ni TBC1, lakini juzi nikiwa naangalia taarifa ya habari ya saa 2:00 usiku nikiwa ninafuatilia habari kwa umakini mkubwa, ghafla kikaingizwa kipengele kinachosemekana ni kipya kipengele hiki kinajulikana kwa jina la ENZI HIZO, tena kimechomekwa katikati ya habari, hali hii iliniondolea hamu ya kuendelea kuangalia taarifa ya habari kabisa. mimi ningewashauri TBC1 waandae kipindi maalumu cha kuweza kuonyesha kipindi hiki lakini taarifa ya habari iachwe ijitegemee kuliko kuchanganya mambo.kweli mnataka kupoteza mvuto wa habari, naomba kuwasilisha hoja.