Tatizo la mgawo/kukatika toka hivyo kwa umeme ni aibu sana kwa Serikali ya Tanzania chini ya Chama Cha Mapinduzi!

The Palm Beach

JF-Expert Member
Dec 30, 2015
808
1,647
Kama kuna eneo ambalo serikali ya JMT inayoongozwa na TANU/ASP kisha CCM tangu uhuru 1961 imefeli spectacularly kisera na kimipango ni la upatikanaji wa huduma bora na ya kuaminika ya nishati ya umeme.

Ni aibu sana kuwa na umeme usioeleweka na unaokatikakatika hata mara 50 kwa siku. Sababu ambazo hutolewa na serikali za marais wote Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Samia ni zilezile. (lakini JPM alikuja akabidili mambo, akazikataa sababu hizo na mambo yakawa nafuu saaana).

Inashangaza sana kiasi cha mtu kujiuliza hivi hawa viongozi tuliowapa dhamana ya kimaamuzi na ki - raslimali fedha na watu wana akili nzuri za kufikiri kweli au kuna shida fulani vichwani mwao.

Haiwezekani TANESCO watangaze mgawo au kukosekana kwa huduma ya umeme kwa mikoa kadhaa kwa siku nzima kwa madai ya matengenezo ya miundombinu halafu wakirejesha huduma hiyo still tatizo linabaki kuwa palepale.!

Unajiuliza hawa watu walikuwa wanatengeneza nini iwapo tatizo la kukatika na kuwaka la umeme liko palepale.?

Na tatizo hili limekuwepo na kudumu tangu miaka ya u - Rais wa Mkapa, likaja likawa baya zaidi wakati u - Rais wa Jakaya Kikwete na sababu ambazo hutolewa ni zilezile miaka yote.

Lakini, mimi nikiri wazi kabisa kuwa, wakati wa u - Rais wa John P. Magufuli tatizo hili lilikuwepo lakini lilikuwa nafuu sana kwa kiwango cha kuvumilia na kueleweka kwa zaidi ya 90%.

Cha kushangaza ni kuwa tatizo hili limekuwa baya zaidi mara tu baada ya Rais Magufuli kufa na kuingia huyu mama. Watu tunajiuliza kulikoni? Je, ni serikali inafanyia hujuma wananchi wake.?

Na hata hawa wawekezaji hususani wa kutoka mataifa ya kigeni tunapowaalika kuja kuwekeza hapa nchini kwetu wanatuelewa vipi wanapokumbana na shida hizi?

Hivi CCM humuoni aibu ingalau kwenye ishu hii tu? Mimi nadhani sasa ni wakati mwafaka mkubali kuwa kwenye eneo hili sera na mipango yenu imeshindwa then GIVE UP na kama taifa tukae pamoja, tujadili na kutafuta namna kuifanya nchi isonge mbele...

Rais Samia hii hali haivumiliki. Hawa wananchi mnaodhani mnaweza kuwatendea vyovyote mtakavyo eti tu kwa sbb nyie ni "watawala" au "serikali", wana kikomo cha uvumilivu...

Itafika wakati tutasema, ENOUGH is ENOUGH na matokeo ya kauli hii yanaweza kuja kusababisha nyie viongozi mkakiimbia nchi hii bure.!

Shauri lenu. Jirekebisheni. Toeni huduma sahihi kwa wananchi ili mdai TOZO na KODI zingine kwa uhalali na siyo kwa namna hii...!
 
Moderators: Tafadhali kuna kosa la kiundishi kwenye heading. Naomba iksomeke "......Tatizo la mgawo/kukatika-katika hovyo.........." badala ya hivyo inavyosomeka...
 
Nchi hii mambo yatanyooka iwapo wananchi wataamka usingizini.Vinginevyo tutaendelea kupiga mbizi kwenye ulofa
Mkuuu wewe ndo umeongea.viongozi hawana shida yoyote.Wananchii ndo tatizo kubwa.kwanza tumegawanyika hivo tukubali kuliwa.Hakuna anayehoji wote tunalalama mitandaoni na walishatujua hivyo wanafanya wanavyotaka.Huu mgao ni sababu tosha ya kuangusha serikali kwa wananchiii wanaojielewa.
 
wapeni watu wengine wenye akili kama CHADEMA waendeshe nchi.!
Bwashee, kiini cha mada yako ni issue nzuri na ya msingi sana inayohitaji mjadala wenye weledi.
Ila hapo kwenye hiyo 👆 nukuu ndipo umechemsha. Hiyo chadema ya kupewa kuongoza nchi ndiyo ipi, hii hii tunayoijua ambayo imeshindwa hata kujenga ofisi ya makao makuu ndiyo ipewe kuongoza nchi? Chama kimeshindwa kujiletea maendeleo, halafu tuwakabidhi nchi tukitegemea kuwa watatuletea maendeleo?
 
CHADEMA ipi ya kuongoza Nchi?! Hii CHADEMA ya Mdude Nyagali na Hilda Newton! Acheni kuleta mizaha kwenye Uongozi wa Nchi!
CHADEMA zaidi ya miaka 30 wameshindwa hata kujenga Choo achilia Ofisi yao ya Makao Makuu!! Hadi leo wamepanga pale Kinondoni Makaburini mtaa wa Ufipa!!!
CHADEMA ni sawa na mlevi yeyote yule!!
 
CHADEMA ipi ya kuongoza Nchi?! Hii CHADEMA ya Mdude Nyagali na Hilda Newton!??! Acheni kuleta mizaha kwenye Uongozi wa Nchi!
CHADEMA zaidi ya miaka 30 wameshindwa hata kujenga Choo achilia Ofisi yao ya Makao Makuu!! Hadi leo wamepanga pale Kinondoni Makaburini mtaa wa Ufipa!!!
CHADEMA ni sawa na mlevi yeyote yule!!
 
Umeandika jambo zuri bahati mbaya ukaja kuharibu baada ya kuingiza vyama, kwani hapo wavivu wa kufikiri watakomea kwenye kujadili vyama badala ya kulizungumzia tatizo husika ulilolitaja, hasa chanzo na nini kifanyike ili kulimaliza.

Mimi kwa upande wangu nitulie hapo ulipozungumzia tatizo wakati wa JPM halikuwa kubwa kama lilivyo wakati huu wa Samia, naamini hapa ndipo penye chimbuko la tatizo, na kutokana na hilo chimbuko, basi tunaweza kuijua solution.

Kwa upande wangu kinachotuumiza ni mindset tofauti za viongozi waliopo madarakani, na wale wanaopewa hiyo wizara kuiendesha, kuna wale wanaopewa na kujiona wamepewa keki hivyo wanajiamulia waanze kuitafuna upande upi[ bahati mbaya hawa ndio wengi zaidi].

Hawa watatengeneza vikwazo vya kila aina ilimradi kuufanya umeme usipatikane wa uhakika, ili waitumie nafasi hiyo kufanya biashara zao za majenereta, ni watu waliotawaliwa na ubinafsi wa hali ya juu, wasiokula wakashiba, ajabu huyo waziri kila siku anakuja na maneno ya uongo kuhusu chanzo cha kukatika umeme.

Mfano, alishatudanganya wanafanya maintanance, kwamba wakati ule wa JPM palikuwa hapafanyiki maintanance ndio maana umeme ukawa haukatiki hovyo, sasa ajabu ni kwamba, wakati huu ambapo maintanance imekuwa inafanyika, hali ndio imekuwa mbaya zaidi, kumbe sababu ya maintanance ni uongo.

Akaja na sababu nyingine, mabwawa ya umeme yanakauka maji kutokana na upungufu wa mvua, hii kauli yake ikaja kupingana na meneja anayeendesha moja ya bwawa la kuzalisha umeme [simtaji jina yasijekumkuta] akadai maji yaliyokuwepo yalikuwa yanaweza kuzalisha umeme kwa muda mrefu ujao, huu nao ukawa uongo wa waziri.

Kwa hiyo mifano michache hapo juu, inaonesha vile wizara ya nishati amepewa mtu asiye na weledi wa kuiongoza, lakini hata sababu anazotoa kuhusu kukatika umeme, nazo zinamfanya apoteze uaminifu kwa jamii.

Lakini bahati mbaya aliyemuweka hana habari, anamuona kijana wake ni mchapakazi, anaonesha vile asivyomfuatiliaji wa wasaidizi wake, au anawafuatilia wale asio na urafiki nao, kwangu wizara ya nishati inamuhitaji mtu mwingine aje kuiongoza, asiyekuwa na makandokando ili kurudisha imani kwa watanzania, sio huyu mfanyabiashara aliyepo sasa.
 
Ukweli ni kwamba Toka huyu mama aingie/ashike kiti na kumuweka kaupara nishati ya umeme ikawa shida
Halafu unamsikia anasema Mimi na jpm ni sawa hell no
 
Kama kuna eneo ambalo serikali ya JMT inayoongozwa na TANU/ASP kisha CCM tangu uhuru 1961 imefeli spectacularly kisera na kimipango ni la upatikanaji wa huduma bora na ya kuaminika ya nishati ya umeme.

Ni aibu sana kuwa na umeme usioeleweka na unaokatikakatika hata mara 50 kwa siku. Sababu ambazo hutolewa na serikali za marais wote Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Samia ni zilezile. (lakini JPM alikuja akabidili mambo, akazikataa sababu hizo na mambo yakawa nafuu saaana).

Inashangaza sana kiasi cha mtu kujiuliza hivi hawa viongozi tuliowapa dhamana ya kimaamuzi na ki - raslimali fedha na watu wana akili nzuri za kufikiri kweli au kuna shida fulani vichwani mwao.

Haiwezekani TANESCO watangaze mgawo au kukosekana kwa huduma ya umeme kwa mikoa kadhaa kwa siku nzima kwa madai ya matengenezo ya miundombinu halafu wakirejesha huduma hiyo still tatizo linabaki kuwa palepale.!

Unajiuliza hawa watu walikuwa wanatengeneza nini iwapo tatizo la kukatika na kuwaka la umeme liko palepale.?

Na tatizo hili limekuwepo na kudumu tangu miaka ya u - Rais wa Mkapa, likaja likawa baya zaidi wakati u - Rais wa Jakaya Kikwete na sababu ambazo hutolewa ni zilezile miaka yote.

Lakini, mimi nikiri wazi kabisa kuwa, wakati wa u - Rais wa John P. Magufuli tatizo hili lilikuwepo lakini lilikuwa nafuu sana kwa kiwango cha kuvumilia na kueleweka kwa zaidi ya 90%.

Cha kushangaza ni kuwa tatizo hili limekuwa baya zaidi mara tu baada ya Rais Magufuli kufa na kuingia huyu mama. Watu tunajiuliza kulikoni? Je, ni serikali inafanyia hujuma wananchi wake.?

Na hata hawa wawekezaji hususani wa kutoka mataifa ya kigeni tunapowaalika kuja kuwekeza hapa nchini kwetu wanatuelewa vipi wanapokumbana na shida hizi?

Hivi CCM humuoni aibu ingalau kwenye ishu hii tu? Mimi nadhani sasa ni wakati mwafaka mkubali kuwa kwenye eneo hili sera na mipango yenu imeshindwa then GIVE UP wapeni watu wengine wenye akili kama CHADEMA waendeshe nchi.!

Rais Samia hii hali haivumiliki. Hawa wananchi mnaodhani mnaweza kuwatendea vyovyote mtakavyo eti tu kwa sbb nyie ni "watawala" au "serikali", wana kikomo cha uvumilivu. Itafika wakati tutasema sasa ENOUGH is ENOUGH na matokeo ya kauli hii yanaweza kuja kusababisha mkatoroka nchi bure.!

Shauri lenu. Jirekebisheni. Toeni huduma sahihi kwa wananchi ili mdai TOZO na KODI zingine kwa uhalali.!
Wewe si mwanaccm kindani ndaki? Nunua Jenereta
 
A
Ukweli ni kwamba Toka huyu mama aingie/ashike kiti na kumuweka kaupara nishati ya umeme ikawa shida
Halafu unamsikia anasema Mimi na jpm ni sawa hell no
Cheni wivu twende hivi hivi.....bila katiba Mpya tutaendelea kupata viongozi wabovu tu
 
Back
Top Bottom