Edwin Mtei
Senior Member
- Dec 13, 2008
- 181
- 342
Vituko vingi vya hivi karibuni vinadhihirisha kwamba Tanzania tunahitaji kujiuliza kama tunadhamiria kwa dhati kuwa na demokrasia ya kweli.
Katiba yetu ya sasa, Ibara 18(a) inatoa haki na uhuru wa raia kutoa maoni na fikra zake (free speach), lakini uongozi, hususan polisi, wanaonekana hawajui au hawatambui hilo.
Katiba yetu ya sasa inaruhusu vyama vingi vya siasa (na hata hii mpya tunayoandaa sasa haiondoi hilo). Lakini ukimsikiliza mmoja wa viongozi, hususan MwanaSheria Mkuu, utadhani hajui au hatambui uhuru wa mawazo nje ya chama kimoja cha kisiasa. Ukifuatilia misimamo na mawazo ya viongozi wengi wa serikali na chama tawala utadhani hawatambui wapinzani wanatoa mchango katika kutoa changamoto na kuimarisha utekelezaji wa sera.
Hata ukifuatilia mienendo au vituko vinavyowakabili viongozi halali wa vyama vya upinzani, hata wale waliochaguliwa rasmi na wananchi kuwawakilisha katika Bunge au Halmashauri za wilaya utadhani Serikali yetu na Chama tawala vinawaona ni maadui au waasi waliwateuwa.
Sasa tujiulize, tunataka na tunatambua uwepo wa vyama vya upinzani katika siasa zetu? Inaonekana kuna umuhimu wa kuwa na mafunzo ya uraiya mwema miongoni mwa vijana wetu na umma kwa jumla ili muundo wa siasa na utawala tuliojiwekea kwa maksudi ueleweke na utengemae.
Katiba yetu ya sasa, Ibara 18(a) inatoa haki na uhuru wa raia kutoa maoni na fikra zake (free speach), lakini uongozi, hususan polisi, wanaonekana hawajui au hawatambui hilo.
Katiba yetu ya sasa inaruhusu vyama vingi vya siasa (na hata hii mpya tunayoandaa sasa haiondoi hilo). Lakini ukimsikiliza mmoja wa viongozi, hususan MwanaSheria Mkuu, utadhani hajui au hatambui uhuru wa mawazo nje ya chama kimoja cha kisiasa. Ukifuatilia misimamo na mawazo ya viongozi wengi wa serikali na chama tawala utadhani hawatambui wapinzani wanatoa mchango katika kutoa changamoto na kuimarisha utekelezaji wa sera.
Hata ukifuatilia mienendo au vituko vinavyowakabili viongozi halali wa vyama vya upinzani, hata wale waliochaguliwa rasmi na wananchi kuwawakilisha katika Bunge au Halmashauri za wilaya utadhani Serikali yetu na Chama tawala vinawaona ni maadui au waasi waliwateuwa.
Sasa tujiulize, tunataka na tunatambua uwepo wa vyama vya upinzani katika siasa zetu? Inaonekana kuna umuhimu wa kuwa na mafunzo ya uraiya mwema miongoni mwa vijana wetu na umma kwa jumla ili muundo wa siasa na utawala tuliojiwekea kwa maksudi ueleweke na utengemae.