Tanzania ina Bahati Mbaya sana kwa kukosa viongozi

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,075
Taifa au jamii yoyote ili kuyapata maendeleo ya kweli lazima kuwepo na viongozi. Nchi au jamii ikikosa viongozi, haiwezi kuwa na maendeleo ya kweli wala amani ya kweli.

Ili uwe na jamii yenye viongozi na wanaoongozwa ni lazima uwepo mfumo uliotengenezwa, unaoheshimika na uliokubalika na wale wanaoongozwa, ambao kimsingi ndio walio wengi. Hili Tanzania tumelikosa.

Uhalali wa mtu kuwa kiongozi, kwanza kabisa ni kuchaguliwa kiuhalali na kwa uwazi kwa mfumo uliotengenezwa na kukubalika na wale wanaoongozwa, na siyo vinginevyo.

Tanzania imekosa viongozi, ila ina watawala. Watawala wamewawekea utaratibu wananchi jinsi wao watawala watakavyokuwa wakipatikana na jinsi watakavyowatawala. Na kila wazo jema linalotaka nchi iwe na viongozi, watu wanaopatikana kwa utaratibu wa haki na wa wazi, watawala hawataki.

Watawala kukataa matakwa ya wanaotawaliwa jinsi wanavyotaka viongozi wapatikane kwa njia ya wazi na ya haki, ni uthibitisho tosha kuwa watawala wanataka wabakie kuwa watawala na siyo viongozi wa wananchi.

Ndiyo maana wameweka utaratibu wao ambao wananchi wapende wasipende, lazima waitii.

1) Watendaji wakuu wa Tume ya uchaguzi watateuliwa na watawala.

2) Kura zitahesabiwa na Tume ya Uchaguzi ya watawala.

3) Tume ya watawala ndiyo itamtangaza waliyeamua awe mshindi.

4) Tume ya watawala itahesabia kura gizani, na wananchi hawatakiwi kushuhudia wala kuthibitisha uhesabuji wa kura kama ni halisia au bandia.

Halafu wajinga wachache, naamini ni wale machawa, wanataka kuwadanganya watu kuwa Samia ni mpenda demokrasia na haki.

NB: Laana ya Tanzania imebebwa na CCM, chama ambacho hakijawahi kufikiria hata siku moja kuwapa Watanzania haki yao ya msingi ya kuwachagua viongozi wanaowataka. Wakati wote wamebakia kufikiria na kubuni mbinu za kuendelea kuwatawala Watanzania kwa mbinu zote, chafu na njema, alimradi wanaendelea kutawala, japo ni dhahiri hakuna mwanga wowote kupitia wao.


Naomba mod, rekebisha heading. Isomeke Tanzania badala ya Tamzania.
 
Tamzania ndo nchi gani hiyo? Iko bara gani?

Nime-google lakin siipati

Unaelewa maana ya typical error. Ni rahisi kwa anayetambua kwamba huwa kuna typical error, kwa kuzingatia kuwa kwenye keyboard, m na n zimekaribiana.
 
Nimeipenda na kukubali sana hoja yako hii. Mungu akubariki sana. Nina Imani ipo siku Mungu atatupa watanzania haja za mioyo yetu na babeli itaanguka.
 
Yaani bora tungenyimwa raslimali, halafu tukapewa watu wenye uwezo wa kulifikisha Taifa kwenye maendeleo makubwa ya kiteknolojia, kiuchumi, kisiasa, na pia kijamii.

Hii hali ya sasa inakatisha tamaa.
 
*Singapore has chosen its PM. After four years of strict, tedious filtering and performance index review applied on four outstanding candidates. Finally, Mr. Lawrence Wong was chosen to take the responsibility as the 4th PM of Singapore. Mr.Wong, a Double Degree and PhD. holder from Harvard University in Economics, was selected after he received the highest score in Character, Perfomance, Integrity, Quality and job KPI. Mr. Lawrence Wong scored ZERO in the following: 1. Public Complaints. 2. Police Traffic Summons. 3. Public Summon. 4. Racial hatred statements. 5. Corruption and Bribery. 6. Legal Court cases. 7. Tax fraud, 8. Abuse of Power. 9. FBI, CIA, Interpol checks. How about that for determining leadership competency, rather than flogging the old horse
emoji237.png
of democracy?
 
Kwa kwa hiyo bahati mbaya hawezi kupatikana mzuri bora tuongozwe na hao hao wasio viongozi!
 
Ni CCM Pekee iwezayo kuiongoza Tanzania na ikawa na amani na utulivu na kupata maendeleo ya haraka na kwa kasi kama tunavyoshuhudia kwa sasa.

Watanzania wana amana ,utulivu na furaha mioyoni mwao kwa sasa kuliko wakati mwingine wowote ule kwa kuwa wanasikilizwa na kupewa wanachohitaji.

Matatizo na kero huwa haziishii bali huwa zinajitokeza kwa namna tofauti tofauti na katika sura tofauti.lakini watanzania wameona kwa macho yao na kushuhudia juhudi kubwa za serikali yao chini ya uongozi shupavu, imara na madhubuti wa mama yao na Rais wao mpendwa na Jemedari wao kipenzi namna anavyo pambana katika kukabiliana na Changamoto mbalimbali zinazojitokeza mbele yetu kama Taifa.
 
Back
Top Bottom