Bila shaka tuna viongozi wenye fikra duni sana

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,058
Kuna mambo huwa yanafanywa na baadhi ya viongozi wetu, mpaka unajiuliza tunaongozwa na watu wa namna gani! Maana ni kama hata kwenye kile kiwango cha akili ya kawaida, hawamo.

Nchi zetu hizi hazipati maendeleo kutokana na kukosa viongozi katika maana ya viongozi. Kuwa kiongozi maana yake ni wewe kuwaonesha njia unaowaongoza. Kama kiongozi unakuwa mwongo maana yake utatengeneza watu wengi waongo. Kiongozi ukiwa mwizi, utatengeneza wevi wengi sana. Lakini pia kiongozi ukiwa mwadilifu utatengeneza waadilifu wengi. Kiongozi ukiwa mkweli, utatengeneza watu wakweli wengi.

Jamii yetu kujawa na watu wengi wa ajabu ajabu, kuwa na watendaji wengi Serikalini wevi, wafujaji, waongo, kunaashiria ndivyo walivyo wakuu wao.

Ninachojiuliza, hivi hawa watawala wetu kwa kuyapata madaraka huwa wanaamini wameuaga ubinadamu, wao sasa siyo wanadamu? Na kwa vile wao ni juu ya wanadamu, hawawezi kuugua wala kufa? Nadhani kwa kuamini kuwa wao ni zaidi ya wanadamu, ndiyo maana wengine huwa wanaiba mpaka wanakufuru. Mtu anaiba kiasi hata akiishi miaka 2,000 hawezi kumaliza utajiri wa wizi alioutengeneza.

Mimi naamini, kwa mwanadamu kuumwa au hata kufa, ni mambo ambayo humpata mwanadamu yeyote, na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia. Kuumwa au kifo siyo aibu na wala siyo kosa la mgonjwa au marehemu. Kama haya ninayoyasema ndiyo ukweli, kwa nini watawala wa Tanzania, kiongozi akiugua huwa wanapenda kusema uwongo?

Hayati Magufuli wakati anaugua, katikati ya minong'ono kuwa Magufuli ni mgonjwa, watawala waliamua kusema uwongo kuwa Magufuli yu mzima. Akiwa tayari ameaga Dunia, baadhi ya viongozi waliendelea kusisitiza kuwa yumzima.

Angalao Kikwete yeye aliamua kuweka wazi alipokuwa anaumwa, tena akaenda ndani zaidi hadi kuelezea alikuwa anaumwa nini.

Kule South Afrika, Mandela alipougua mafua makali, nchi ilitangaziwa. Baadaye alipougua tena na kulazwa, wananchi walipewa taarifa, na baadaye kupewa taarifa ya maendeleo yake karibia kila siku. Mseveni alipougua, wananchi walitangaziwa. Malkia Elizabeth alipovunjika mfupa, wananchi walijulishwa.

Hawa wa kwetu kusema uwongo kiongozi akiugua wanataka kutuambia kiongozi siyo mwanadamu, na hivyo haguswi na maradhi, ajali wala kifo?

Kuna minong'ono kuwa Makamu wa Rais ni mgonjwa, na kwamba yupo nje kwa matibabu, lakini watawala wanawadanganya wananchi kuwa yupo nje kikazi.

Kama ni kweli kuwa Makamu wa Rais anaumwa na yupo nje kwa matibabu, hawa wanaosema yupo nje kwa ziara ya kikazi, kweli wana akili timamu? Na kama hawana akili timamu, nchi inayoongozwa na watu wasio timilifu, mwisho wake ni nini?
 
Kila kitu wanaingiza siasa ,eti wakisema watawapa wapinzani maneno ya kusema ...Nalo ni tatizo yaani siasa ni uongo uongo ili mradi tu wao mambo yaende sawa.
 
Hii tabia ya kuficha ugonjwa kweli nashindwa kuielewa, lakini pia siielewi tabia nyingine inayoambata nayo ya kufurahia ugonjwa wa wengine.

Sijui tumekuwa taifa la aina gani, naona itikadi za kisiasa zimeanza kutufanya tukose hata ubinadamu, tumegeuka maadui tusiotakiana heri kwenye jambo lolote lile.

Huu ujinga unatakiwa uishe, kiongozi akiumwa serikali itoe taarifa, itutake wananchi tumuombee, na sisi tutakaopewa hizo taarifa tuache drama.

Tuzipokee kwa namna ambayo itawapendeza wale waliozitoa ili waache tabia za kuficha ugonjwa wa viongozi siku nyingine, kwasababu watajua watanzania wanajielewa bila kujali itikadi zao.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Vipi kama wanaosema makamu anaumwa ndiyo waongo na serikali ndiyo iko sahihi kuwa makamu yuko nje kwa ziara za kikazi?

Nadhani uzi wako umewahi sana. Ulipaswa kuja baada ya upande mmoja kati ya pande hizi 2 zinazokinzana kuaibika hadharani.

Ni kweli huko nyuma serikali ishadanganya. Lkn hatuwezi kumchukulia hicho ndiyo kigezo cha kuzikataa kauli za Sasa za serikali.

Muda ni mwamuzi asiyekuwa na upendeleo. Itajulikana tu!
 
Hii tabia ya kuficha ugonjwa kweli nashindwa kuielewa, lakini pia siielewi tabia nyingine inayoambata nayo ya kufurahia ugonjwa wa wengine.

Sijui tumekuwa taifa la aina gani, naona itikadi za kisiasa zimeanza kutufanya tukose hata ubinadamu, tumegeuka maadui tusiotakiana heri kwenye jambo lolote lile.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mnyika naye amesafiri kikazi?
 
Kuna mambo huwa yanafanywa na baadhi ya viongozi wetu, mpaka unajiuliza tunaongozwa na watu wa namna gani! Maana ni kama hata kwenye kile kiwango cha akili ya kawaida, hawamo.
yoongozwa na watu wasio timilifu, mwisho wake ni nini?
"The problem of Africans, those with ideas have no power, and those with power have no ideas."
 
Mkuu kwenye hii nchi Ukiwa na Akili timamu na ukaendelea kuyafikiria yanayofanywa na Viongozi utaishia kila siku kutenda dhambi ya kutukana tu!.


Ni vema ukajifanya punguani ili uishi kwa amani!
 
Kuna mambo huwa yanafanywa na baadhi ya viongozi wetu, mpaka unajiuliza tunaongozwa na watu wa namna gani! Maana ni kama hata kwenye kile kiwango cha akili ya kawaida, hawamo.

Nchi zetu hizi hazipati maendeleo kutokana na kukosa viongozi katika maana ya viongozi. Kuwa kiongozi maana yake ni e kwa matibabu, hawa wanaosema yupo nje kwa ziara ya kikazi, kweli wana akili timamu? Na kama hawana akili timamu, nchi inayoongozwa na watu wasio timilifu, mwisho wake ni nini?
Non sense
 
Vipi kama wanaosema makamu anaumwa ndiyo waongo na serikali ndiyo iko sahihi kuwa makamu yuko nje kwa ziara za kikazi?

Nadhani uzi wako umewahi sana. Ulipaswa kuja baada ya upande mmoja kati ya pande hizi 2 zinazokinzana kuaibika hadharani.

Ni kweli huko nyuma serikali ishadanganya. Lkn hatuwezi kumchukulia hicho ndiyo kigezo cha kuzikataa kauli za Sasa za serikali.

Muda ni mwamuzi asiyekuwa na upendeleo. Itajulikana tu!
Non sense
 
Mkuu kwenye hii nchi Ukiwa na Akili timamu na ukaendelea kuyafikiria yanayofanywa na Viongozi utaishia kila siku kutenda dhambi ya kutukana tu!.


Ni vema ukajifanya punguani ili uishi kwa amani!
Absolutely?
Siyo kuishia kutukana tu, bali unaweza hata ukapata kichaa kutokana na msongo wa mawazo.

"Ukiwa na akili timamu kabisa, kuishi Afrika ni kazi kubwa na ni mateso makubwa sana."
 
Vipi kama wanaosema makamu anaumwa ndiyo waongo na serikali ndiyo iko sahihi kuwa makamu yuko nje kwa ziara za kikazi?

Nadhani uzi wako umewahi sana. Ulipaswa kuja baada ya upande mmoja kati ya pande hizi 2 zinazokinzana kuaibika hadharani.

Ni kweli huko nyuma serikali ishadanganya. Lkn hatuwezi kumchukulia hicho ndiyo kigezo cha kuzikataa kauli za Sasa za serikali.

Muda ni mwamuzi asiyekuwa na upendeleo. Itajulikana tu!
Kiongozi akiwa nje kikazi kuna kitengo cha habari kwa kiongozi husika kuonyesha anafanya nini huko aliko,.

Mfano Rais Samia alipo mkutano wa mazingira na tabia nchi wa kimataifa kuna picha tunaziona na anachozungumza tunakisikia na kukisoma,kulikoni kwa Makamu wa Rais Dr Mpango?


Zinduka, mleta uzi yuko sahihi, serikali inaficha jambo,

Swali linabaki kwako, kuna faida kuficha?,maana serikali watumishi wake huapa kutunza siri za serikali,pengine na la ugonjwa pia ni sirikali
 
Embu acha porojo zako hapa zisizo na mshiko .kwanza andiko lako umelikoroga sana na kulichanganya na kujichanganya sana ambapo sijuwi hata kama wewe mwenyewe unafahamu ulichoandika .

Unaposema kuwa watoa taarifa ni waongo halafu ukashindwa kuweka ukweli wenye ushahidi unataka tukuelewe vipi? Unataka tuelewe nini? Wewe mwenye kuujuwa ukweli kwanini usiuweke hapa kuthibitisha huo uongo unaousema? Hoja hupingwa kwa hoja. weka hoja yako ya ukweli ndio watu wajuwe kuwa taarifa walizopewa ni za uongo.

Lakini kama huna huo ukweli unaousema ambao ni tofauti na taarifa iliyotolewa basi nakutaka ufunge mdomo wako na kutulia tu kuliko kuendelea kuropoka ropoka hapa.
 
Vipi kama wanaosema makamu anaumwa ndiyo waongo na serikali ndiyo iko sahihi kuwa makamu yuko nje kwa ziara za kikazi?

Nadhani uzi wako umewahi sana. Ulipaswa kuja baada ya upande mmoja kati ya pande hizi 2 zinazokinzana kuaibika hadharani.

Ni kweli huko nyuma serikali ishadanganya. Lkn hatuwezi kumchukulia hicho ndiyo kigezo cha kuzikataa kauli za Sasa za serikali.

Muda ni mwamuzi asiyekuwa na upendeleo. Itajulikana tu!
Ule uzi mwingine kwangu unagoma kufunguka, unanitaka nifungue kupitia browser unadai server error occured, jambo naloona kama usumbufu maana inahitajika mpaka password, but zile hoja zako hazijitoshelezi ukifunguka nitakuonesha udhaifu wake, though it may take time.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom