Tamko la kamati kuu ya CHADEMA kuhusu mchakato wa katiba

Hivi msomi haswa, anaandika hivi:

"kimepokea na kujadili kwa kina taarifa ya majadiliano"

Hivi magwanda mlikuwa mna "taarifa ya majadiliano"? ndiyo ipi hiyo?

Na hapo ndio sijaenda hata kwenye taarifa. Daaahhh, nawaonea huruma sana, hebu someni vizuri kabla hamjaanza "upiganaji" wenu na mimi. Maana kupigana mimi hamniwezi. Bora tubaki kubishana kwa hoja. Haya niambieni ni ipi hiyo taarifa ya majadiliano?
 
Tunakuja tunakuja tunakuja

Chadema endeleeni kuto a Elimu na hasa huko vijijini kuhusu mchakato huu wa Katiba

Hawa Magamba waacheni, walioangalia Star Tv Jana mjadala wa Katiba kati ya CCM B na CDM waliona, Hapo ndipo ujagundua wAtZ wamepevuka na wanajua Haki zao

CUF Wamekiri wao ni CCM B............ Kushneiiiiiiiii hawa CUF, Yaaani RIP (rEST IN pEACE)

Big up Chadema
 
Well, mswada uliopitishwa bado haujawa sheria kama tamko linvyouita, atakapousaini rais uwe sheria mie nawashauri Chadema, kama njia nyingine halali wafungue kesi mahakamani kuipinga sheria hiyo, kama mmoja ya sheria mbaya inayokiuka katiba Tanzania. Chadema tutumieni mahakama pia , ingawaje ninatambua mwanasheria mkuu na mahakama siku za hivi za karibuni wamekuwa kama jumuia za CCM kama ilivyo UVCCM au UWT-CCM, nk. Lakini ili ku-exhaust njia zote, nashauri mahakama itumike pia!
 
hoja hizi zingetolewa bungeni pengine zingesaidia kuleta muafaka kama chadema wasingesusia bunge

nani angewasikiliza kama wabunge walio wengi wamelala na wakiamka wanagonga meza kuunga hoja bado tunaendelea kuona mambo tz..
 
Ikiwa hilo ndiyo tamko la magwanda, ama kweli mna "wasomi" na si wasomi. Hivi kama chama cha upinzani mmekaa haswa mkachemsha vichwa vyenu mkaja na tamko kama hilo? nashindwa kuamini nnayoyasoma kuwa yanatoka kwenye "wasomi". Khaaaa!

Nna uhakika hayo kayaandika Mbowe.

Zitto uko wapi? tazama hawa wenzako wanavyokitia aibu chama ulichokipagania mpaka kwa afya yako. Pole sana Zitto najuwa una kazi kubwa sana, Mwenyeezi Mungu atakulinda na kukusaidia. Sikuwepo kwenye hicho kikao wala sijasikia zaidi ya hayo niliyoyasoma hapo juu, lakini nna uhakika hukutia hata lako moja. Hii si "calibre" yako.
Ulipopigwa ban JF ndio ukaacha kusoma magazeti, Zitto katoa msimamo mapema kabisa sama hili habari ya hili gazeti....
MUSWADA WA KATIBA MPYA-ZITTO KABWE AIONYA SERIKALI

ASEMA BILA MUAFAKA CHAMA CHAKE KITATAFUTA NJIA MBADALA

Waandishi Wetu, Dodoma, Dar

WAKATI mjadala wa Muswada wa Sheria ya Kuunda Katiba Mpya ukizidi kuitikisa Serikali, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe ameonya kwamba kama suala hilo litachezewa, chama chake kitatafuta njia mbadala kwa wananchi ya kupata Katiba. Mjadala kuhusu muswada huo unakabiliwa na upinzani mkali kutoka ndani na nje ya Bunge na jana wabunge wengi wa CCM waliochangia, waliwashambulia wenzao wa Chadema.
 
Sasa subirini tamko la Police. Waziri wa mambo ya ndani naye atatoa tahadhari ya Al-Shaabab.
 
Ikiwa hilo ndiyo tamko la magwanda, ama kweli mna "wasomi" na si wasomi. Hivi kama chama cha upinzani mmekaa haswa mkachemsha vichwa vyenu mkaja na tamko kama hilo? nashindwa kuamini nnayoyasoma kuwa yanatoka kwenye "wasomi". Khaaaa!

Nna uhakika hayo kayaandika Mbowe.

Zitto uko wapi? tazama hawa wenzako wanavyokitia aibu chama ulichokipagania mpaka kwa afya yako. Pole sana Zitto najuwa una kazi kubwa sana, Mwenyeezi Mungu atakulinda na kukusaidia. Sikuwepo kwenye hicho kikao wala sijasikia zaidi ya hayo niliyoyasoma hapo juu, lakini nna uhakika hukutia hata lako moja. Hii si "calibre" yako.

Nikisha ona avator yako hata sijisumbui kusoma ulichokiandika
 
Ulipopigwa ban JF ndio ukaacha kusoma magazeti, Zitto katoa msimamo mapema kabisa sama hili habari ya hili gazeti....

Hayo yote uliyoyabandika ni maneno ya muandishi hakuna hata sehemu moja aliyom "quote" Zitto. Muandishi ana uhuru wa kutoa maoni yake,

Mimi nna kuhakikishia Zitto hana lake hata moja katika hilo lililobandikwa hapo juu. Hakuna nnakataa, hilo juu hapo lipo "too shallow", Zitto kina chake ni kirefu zaidi ya hivyo.
 
Hivi msomi haswa, anaandika hivi:

"kimepokea na kujadili kwa kina taarifa ya majadiliano"

Hivi magwanda mlikuwa mna "taarifa ya majadiliano"? ndiyo ipi hiyo?

Na hapo ndio sijaenda hata kwenye taarifa. Daaahhh, nawaonea huruma sana, hebu someni vizuri kabla hamjaanza "upiganaji" wenu na mimi. Maana kupigana mimi hamniwezi. Bora tubaki kubishana kwa hoja. Haya niambieni ni ipi hiyo taarifa ya majadiliano?

Nimeuliza hayo hapo juu kwenye post yangu #86 naona magwanda kimyaaaa, hamjui mjibu nini.
 
Hayo yote uliyoyabandika ni maneno ya muandishi hakuna hata sehemu moja aliyom "quote" Zitto. Muandishi ana uhuru wa kutoa maoni yake,

Mimi nnkuhakikishia Zitto hana lake hata moja katika hilo lilibandikwa hapo juu. Hakuna nnakataa lipo "too shallow", Zitto kina chake ni kirefu zaidi ya hivyo.

Nakumbuka Zitto alishawahi kukuita wewe "Kizabizabina" sasa leo Ndio Nimeamini

B.T.W Gamba Kuu Rostam linaendeleaje?
 
Hiyo ni "abuse" nna i report, moderators wa JF wachukuwe sheria zinazostahiki.

Tafadhali kama huwezi kujibu hoja zangu nakuomba usinitukane, hunijui sikujui.
Pole sana lakini ninakuhurumia sana kwa sababu huwa unalazimisha kuongea hata ambayo hayatumii kichwa ukiambiwa ukweli unalalamika CCM chama cha majambazi na wehu tu
 
Hayo yote uliyoyabandika ni maneno ya muandishi hakuna hata sehemu moja aliyom "quote" Zitto. Muandishi ana uhuru wa kutoa maoni yake,

Mimi nna kuhakikishia Zitto hana lake hata moja katika hilo lililobandikwa hapo juu. Hakuna nnakataa, hilo juu hapo lipo "too shallow", Zitto kina chake ni kirefu zaidi ya hivyo.

We jasiri kweli ! Haya niambia unalipwa shilingi ngapi huko kuja kuchafua hewa JF ?
 
Kwa bunge la makinda hata kama wangetoa tamko linalowaka moto wale wasingekuwa tayari.cha msingi ni sisi wananchi kufahamishana bila ushabiki kwa kuzingatia ukweli na hali halisi ilivyo kwenye katiba iliyopita huku tukiangalia mambo ambayo yaliwekwa kwenye katiba ya zamani ambayo ni kuwalinda viongozi wasihojiwe wala kushitakiwa kama watakuwa watenda makosa ya jinai wakiwa madarakani.lakini kingine ni kuangalia mambo muhimu kama ardhi na rasilimali zingine ambazo ni za watanzania wote.Watanzania tuangalie pia kinacholeta ugumu wa kukubali kuweka mambo ambayo yanatulinda sote sio tu wale walioko madarakani.hiki ni kiini cha kugoma kutumia mawazo mbadala ya kutoka Chadema na kwa wanaharakati,wanazuoni na wananchi wengine,Ni hofu ya kutokuendelea kutawala kwa kuweka sheria zinazo mlinda alieko madarakani na asieko madarakani,wanaogopa kufilisiwa kwa mali ambazo kwayo zimepatikana kwa njia isiyo halali,wanaogopa kutoa kinga kwa viongozi wa juu kushitakiwa,Hizo ndo hofu kuu,bila kusahau kwamba huenda kukawa na hoja ya kuvunja muungano au kuuboresha kwa kuleta tija pande zote za muungano kwa kuweka mambo yote sawa,na hii inatokana na kuwa muungano unasiri nyingi ambazo wengi wetu hatuzijui,ziko kwa manufaa ya wakubwa hata wananchi wa kawaida kule ZNZ naamini hawajui faida hasa za muungano.Naomba sana tutafakari kinachowafanya viongozi wetu wasiwe na muafaka.lazima ni kitu ambacho upande mmoja unataka kufaidika nacho kwa siku za usoni,maana ingelikuwa ni jambo la kufaidika pande zote zinazolumbana wala kusingekuwa na mvutano huu.hapa ndipo tuangalie nani anaelekea kujivutia kwa faida yake na kundi lake?Nani anavutia kwa faida ya wengi hata kama yeye atapata dola kupitia kufaidika wengi au wote waTZ.Binafsi siungi mkono anaevutia upande wake na kundi lake tu,badala ya kuvutia kwake na wananchi wote.Je ni kweli kwamba tukiwa na tume huru ya uchaguzi kuna upande utaumia kwa wananchi?Je ni kweli kwamba kama mswaada ungesomwa kwa mara ya kwanza hii juzi na kisha ukaletwa kwetu kina yahe tukajadili na kutoa mapendekezo yetu kuna baadhi ya wananchi wangekuwa wamenyimwa haki yao kwa kufanya hivyo?Je ni kweli kwamba tukiondoa KINGA kwa raisi ajaye kuweza kumhoji na kumfungulia mashitaka kama atabainika kufanya kosa akiwa madarakani kuna haki yoyote wananchi tutakuwa tumenyimwa? au kuna madhara gani ambayo kama taifa litakuwa limepata?Je si kweli kwamba kwa baadhi ya sheria hizo zinampa raisi alieko madarakani akajimbikizia mali kwa njia ya ufisadi taifa linakuwa limeingia matatizoni?Je tunapoona serikali haichukui hatua juu ya ubadhilifu mkubwa wa fedha za umma kwa kila sekta sio mapungufu ya katiba iliyoasisiwa na chama kimoja?Anyway mimi sio mtaalamu wa chochote ila najaribu kujiuuliza sana kwa nini kumetokea mvutano sana juu ya kuunda katiba ya watanzania wote.Au labda katiba ni ya viongozi ila sisi wengine hatujui?Wakuu mnifamishe kama ni hivyo ila pia natoa wito tujadili suala hili bila ushabiki wa kichama.
 
Back
Top Bottom