Tamaduni Music hawajawahi kufanikiwa kwenye chochote kile wanachokianzisha

Mengi kama sio yote uliyoeleza ni ya kweli kabisa, jamaa ni wasanii wakali sana lakini wasio na mafanikio makubwa kimuziki. Wana mauzo duni, hawana endorsement na deals nyingine, hawana tuzo za muziki nk

Sababu ya wao kutofanikiwa ni ipi sasa?
Kwenye Kilinge umeeleza kuwa project ilikufa kutokana na wao kutokuwa na nidhamu. Hujaeleza kwa kina ni vipi walikosa nidhamu na ni vipi kukosa kwao nidhamu kukapelekea kufa kwa project.

Rap city battle
Hii nayo hujaeleza kwa undani kwa nini ilishindwa kuendelea. Nafikiri Wakazi tutamtag twitter aitolee ufafanuzi. Vivyo hivyo kwa kikosi kazi kazini na nyingine pia.

Maoni yangu
1. Hujuma na Fitna
Hawa wana Tamaduni Muzik wanafanyiwa hujuma kubwa ya kimuziki na magodfather wa kiwanda cha muziki, hiyo ndiyo sababu kuu ya wao tamaduni kushindwa kutoboa. Watu kama kina Tale na Fella, hawa ndio wanaolalamikiwa sana kuwa waamuzi wa nani atoke na nani asitoke. Hapa ilikuwa ni pamoja na marehemu Ruge kupitia Clouds fm, na yeye alikua mmoja wa wauaji wa Hiphop muziki kabla ya Tamadun na hata baada ya Tamaduni. Hujuma na Fitna zinafanywa sababu ya hao magodfather kutaka wasanii walio chini yao waende zaidi, au kutaka wagawane mapato na hawa tamaduni muzik katika uwiano ambao unaoonekana wa kinyonyaji kwa tamaduni, hali inayosababisha wanatamaduni kukataa na hivyo kudispliniwa kwa kubaniwa, Rejea wimbo wa Babu Talent wa Nikki Mbishi.


Hapa kwenye fitna unakuta makampuni makubwa hayawapi endorsement hawa wana bila sababu ya msingi. Mfano labda CRDB au AIRTEL wanataka tangazo la huduma yao lifanywe kwa Rap, wapo tayari kufanya na msanii asiyejulikana kabisa kuliko kufanya na hao tamaduni. Au wanaweza mpa AY ambaye uwezo wake kirap hauwezi kuzidi hawa wa tamaduni, na hata relevancy yake kwa sasa angeweza kuitwa msanii mkongwe.

Kibiashara, new school artist ndio huhitajika matangazoni maana wateja wengi targeted ni wa kizazi cha new school. Kuna tangazo moja la airtel money, jamaa amerap sijui ni nani, tangazo ni kali ila msanii aliyelifanya sidhani kama ni maarufu. Sasa fitna inapelekea wakose pesa na kukosa pesa inafanya wasitoke.

Fikiria Harmonize anapata endorsement ya milioni 300 hapo CRDB kufanya matangazo ya audio na picha mnato, hiyo deal angepewa Nikki Mbishi hata kwa nusu bei, si angetoboa kabisa mwana na impact ya tangazo ingekuwa sawa tu na anavyofanya harmonize.

Mwaka 2010 au 2011, tamaduni muzik walikuwa wanaitwa wasanii wa internet, yaani wasanii wanaojulikana mitandaoni tu. Hili neno lilikuwa linatumiwa na weusi pamoja na watangazaji wa radio kubwa kama clouds. Tuzo za Kili mwaka huo zikafanyika kwa kupiga kura mtandaoni, lilikuwa ni jambo jipya. Tungetegemea waliojitanabaisha kuwa wasanii wa internet washinde hizo tuzo, ila nako walipigwa fitna hata nominations tu walikosa. Uzingatie wasanii wengine hawakuwa wamezingatia soko la mitandaoni kwa wakati huo.

2. Fedha na uwekezaji
Jambo kubwa linalowaangusha hawa tamaduni ni uwekezaji. Fedha inahitajika ili kufanya ngoma kali za kiwango bora (quality) lakini kwa kujiself sponsor inasabanisha wana washindwe kufanya track za mixing kali na pia kufanya video kali na directors wakubwa.

Mfano huo wimbo wa Babu Talent licha ya kuwa na mashairi supa, video yake ni ya kiwango cha kawaida kabisa - yaani kuchezwa na tv hata za ndani inakuwa ni kwa kudra tu za Mungu.

Mfano, kwa sasa studio kama za WCB au kina Mocco genious, zina kiwango kikubwa sana cha utayarishaji wa muziki, hawa tamaduni wangeweza kufanya mixing na mastering zao huko lakini ama hawana fedha kulipa hizo studio ama hawahitajiki kwa hizo studio ama ego tu inawafanya wenyewe tamaduni waone ni uwack kwenda kwenye hizo studio.

3. Mentality
Kufanya commercial muziki tamaduni wanaona ni uwack. Hapa wanapishana pakubwa sana na biashara. Duniani kote muziki sasa hivi ni biashara. Inabidi wakubali mabadiliko kuendana na nyakati na pia soko.

Wao watakwambia, mfano sasa hivi ushoga ndio umetrend duniani, kwa hiyo na sisi tuwe mashoga ili kuendana na nyakati?? Hapo labda umewaambia wafanye muziki kwa beat zilizo kisasa (trap, drill nk). Mo Famous aka Mo Tecnic aka Jay Moe alifanya ile pesa ya madafu kwa beat ya trap na akarap kiufundi, haikumuondolea uana hiphop wake na ilimrejesha kwenye game japo hakuendeleza sana uwepo wake.

Sasa tamaduni inabidi wabadilike mtazamo, wakubali kujiendesha kibiashara. Wakubali kula na kuliwa kibiashara, heri nusu shari kuliko shari kamili. Kuna kipindi Stereo alifanya kazi na WCB na alisogea sogea sana, hata sasa nafikiri ndio msanii anayeingiza kipato kikubwa kupitia muziki kwa hao tamaduni.
Mkuu umefafanua vizuri sana .
Kwa upande wangu naona Mentality yao ndo imewanyima fursa nyingi bado wana uzamani akilini mwao.

Mtu kama Nikki mbishi ndo kabisa Ni Maskini jeuri
 
Sio nyota ni vile hataki kujiongeza, yan kwa kifupi hana maarifa
tatizo vinega, hippop culture imewaingia kwenye damu, kila kitu wanawaza harakati

Hip pop culture hata KRC ONE imemshinda usa , mziki ni dynamic unabadilika kila muda, hata hip pop ilipoanza ilikuja kufanya mabadiliko ya dominance ya rock, funk , break dance nk hivyo wajitahidi kubadilika

mwangalie mtu kama kofi olomide ndombolo yake ya kipindi anaanza kuwika na kofi wa sasa wakikutana lazima wagombane

wanamuziki wengi wa kizazi hiki wengi hawajui kuimba, huwezi kufananisha na uwezo walikuwa nao tamaduni , ila wanaangalia nini jamii wanataka kusikia na nini wamechoka kusikia, binadamu hawana shukrani akipata kitu muda si mrefu anakiona hakina maana ,anataka kipya hata kama kibaya roho yake ndio hulizika

hata ivyo ndugu yangu mansu le hana shida ndogondogo fremu nyingi nyumbani kwao pale sinza mugabe zanampa pesa nyingi. fremu moja milion anazo karibu sita , nadhani karidhika
 
Mengi kama sio yote uliyoeleza ni ya kweli kabisa, jamaa ni wasanii wakali sana lakini wasio na mafanikio makubwa kimuziki. Wana mauzo duni, hawana endorsement na deals nyingine, hawana tuzo za muziki nk

Sababu ya wao kutofanikiwa ni ipi sasa?
Kwenye Kilinge umeeleza kuwa project ilikufa kutokana na wao kutokuwa na nidhamu. Hujaeleza kwa kina ni vipi walikosa nidhamu na ni vipi kukosa kwao nidhamu kukapelekea kufa kwa project.

Rap city battle
Hii nayo hujaeleza kwa undani kwa nini ilishindwa kuendelea. Nafikiri Wakazi tutamtag twitter aitolee ufafanuzi. Vivyo hivyo kwa kikosi kazi kazini na nyingine pia.

Maoni yangu
1. Hujuma na Fitna
Hawa wana Tamaduni Muzik wanafanyiwa hujuma kubwa ya kimuziki na magodfather wa kiwanda cha muziki, hiyo ndiyo sababu kuu ya wao tamaduni kushindwa kutoboa. Watu kama kina Tale na Fella, hawa ndio wanaolalamikiwa sana kuwa waamuzi wa nani atoke na nani asitoke. Hapa ilikuwa ni pamoja na marehemu Ruge kupitia Clouds fm, na yeye alikua mmoja wa wauaji wa Hiphop muziki kabla ya Tamadun na hata baada ya Tamaduni. Hujuma na Fitna zinafanywa sababu ya hao magodfather kutaka wasanii walio chini yao waende zaidi, au kutaka wagawane mapato na hawa tamaduni muzik katika uwiano ambao unaoonekana wa kinyonyaji kwa tamaduni, hali inayosababisha wanatamaduni kukataa na hivyo kudispliniwa kwa kubaniwa, Rejea wimbo wa Babu Talent wa Nikki Mbishi.


Hapa kwenye fitna unakuta makampuni makubwa hayawapi endorsement hawa wana bila sababu ya msingi. Mfano labda CRDB au AIRTEL wanataka tangazo la huduma yao lifanywe kwa Rap, wapo tayari kufanya na msanii asiyejulikana kabisa kuliko kufanya na hao tamaduni. Au wanaweza mpa AY ambaye uwezo wake kirap hauwezi kuzidi hawa wa tamaduni, na hata relevancy yake kwa sasa angeweza kuitwa msanii mkongwe.

Kibiashara, new school artist ndio huhitajika matangazoni maana wateja wengi targeted ni wa kizazi cha new school. Kuna tangazo moja la airtel money, jamaa amerap sijui ni nani, tangazo ni kali ila msanii aliyelifanya sidhani kama ni maarufu. Sasa fitna inapelekea wakose pesa na kukosa pesa inafanya wasitoke.

Fikiria Harmonize anapata endorsement ya milioni 300 hapo CRDB kufanya matangazo ya audio na picha mnato, hiyo deal angepewa Nikki Mbishi hata kwa nusu bei, si angetoboa kabisa mwana na impact ya tangazo ingekuwa sawa tu na anavyofanya harmonize.

Mwaka 2010 au 2011, tamaduni muzik walikuwa wanaitwa wasanii wa internet, yaani wasanii wanaojulikana mitandaoni tu. Hili neno lilikuwa linatumiwa na weusi pamoja na watangazaji wa radio kubwa kama clouds. Tuzo za Kili mwaka huo zikafanyika kwa kupiga kura mtandaoni, lilikuwa ni jambo jipya. Tungetegemea waliojitanabaisha kuwa wasanii wa internet washinde hizo tuzo, ila nako walipigwa fitna hata nominations tu walikosa. Uzingatie wasanii wengine hawakuwa wamezingatia soko la mitandaoni kwa wakati huo.

2. Fedha na uwekezaji
Jambo kubwa linalowaangusha hawa tamaduni ni uwekezaji. Fedha inahitajika ili kufanya ngoma kali za kiwango bora (quality) lakini kwa kujiself sponsor inasabanisha wana washindwe kufanya track za mixing kali na pia kufanya video kali na directors wakubwa.

Mfano huo wimbo wa Babu Talent licha ya kuwa na mashairi supa, video yake ni ya kiwango cha kawaida kabisa - yaani kuchezwa na tv hata za ndani inakuwa ni kwa kudra tu za Mungu.

Mfano, kwa sasa studio kama za WCB au kina Mocco genious, zina kiwango kikubwa sana cha utayarishaji wa muziki, hawa tamaduni wangeweza kufanya mixing na mastering zao huko lakini ama hawana fedha kulipa hizo studio ama hawahitajiki kwa hizo studio ama ego tu inawafanya wenyewe tamaduni waone ni uwack kwenda kwenye hizo studio.

3. Mentality
Kufanya commercial muziki tamaduni wanaona ni uwack. Hapa wanapishana pakubwa sana na biashara. Duniani kote muziki sasa hivi ni biashara. Inabidi wakubali mabadiliko kuendana na nyakati na pia soko.

Wao watakwambia, mfano sasa hivi ushoga ndio umetrend duniani, kwa hiyo na sisi tuwe mashoga ili kuendana na nyakati?? Hapo labda umewaambia wafanye muziki kwa beat zilizo kisasa (trap, drill nk). Mo Famous aka Mo Tecnic aka Jay Moe alifanya ile pesa ya madafu kwa beat ya trap na akarap kiufundi, haikumuondolea uana hiphop wake na ilimrejesha kwenye game japo hakuendeleza sana uwepo wake.

Sasa tamaduni inabidi wabadilike mtazamo, wakubali kujiendesha kibiashara. Wakubali kula na kuliwa kibiashara, heri nusu shari kuliko shari kamili. Kuna kipindi Stereo alifanya kazi na WCB na alisogea sogea sana, hata sasa nafikiri ndio msanii anayeingiza kipato kikubwa kupitia muziki kwa hao tamaduni.
Nimekupata kinoma noma...
 
Hili andiko umeandika kisomi sana sajo ., kuna mtu ana master namjua aliwai kuimba daz , anaandika kama wewe , vipi bado upo mbeya? Bode kinyozi wako anakupa hapa sinza

Only strong survive , fitina kwenye mziki ni janbo la kawaida , nikuuliza hakuna mwanamuziki yoyote bado yupo kwenye Game ambaye alikuwa na bifu na luge , fela nk?

je kwa sasa mziki upo monopolize kama zamani?
kuna platform kibao ambazo unaweza kuweka kazi bila bugza yoyote, hata tv ,radio hazibani kama zamani, je tamaduni wametumia hizi fursa?

yote kwa yote nakupa ongela kwa uchambuzi wako, yote ni kweli ..ila kisiwe kigezo sana , kumbuka msemo huu GEMU NI GUMU
 
Tamaduni wabadilike kifikra. Kuendelea kung'ang'ania muziki ambao hauhitajiki sokoni ndo anguko lao. Hata wanamuziki wa Congo baada ya kuona wanapotea wameamua kubadilika.. zamani walikuwa wanatoa nyimbo ndefu za hadi dakika 10 ila siku hizi na wao wanatoa nyimbo za dakika 3 hadi 4. Na yale masebene wamepunguza. Kina Pepe Kale wakifufuka watashangaa sana kuona Werrason katoa wimbo wenye verse ya Hiphop. Wacongo pia walikuwa ni wabishi mno kupiga bila vyombo lakini siku hizi nao kuna matamasha wanapiga bila vyombo ili mradi mkono uende kinywani. Kimsingi muziki una mabadiliko dunia nzima. Tamaduni wao wakubali kubadilika na kuacha UJEURI. Kujifanya unasimamia misingi ya Hiphop huku unazidi kutumbukia kwenye umaskini ni upuuzi mtupu.
 
Only strong survive , fitina kwenye mziki ni janbo la kawaida , nikuuliza hakuna mwanamuziki yoyote bado yupo kwenye Game ambaye alikuwa na bifu na luge , fela nk?
Ni kweli, only the strong survive. Kina Ngwair et al walishindwa kuhimili depression wakawa mateja na mauti yakawakuta. Chanzo ni mambo hayahaya kuwa unafanya kazi sana, kipaji kipo na hutoki.

Wapo waliohimili mabifu na kina Fela mpaka leo wapo wakifanya muziki, na wapo waliokubali terms za magodfather na mpaka sasa wanaendelea. Hata hawa Tamaduni muzik bado wapo kwenye game licha ya mabifu na hao magodfather ila ndio hivyo sasa hakuna kutoboa. Unakuwa underground deile

Nyimbo ya Babu Talent ina miaka 6 youtube ila ina viewers laki 2..unaona kabisa uwiano haupo. Kuna mtu anaitwa Kalighraph Jones namba zake zinasomeka balaa, anajitapa mpaka kwa wanaijeria.. ni kwamba anabadilika badilika na anaendana na wakati. Sometimes ubishi unakwamisha mambo.


GEMU NI GUMU
Nabadilikia humu humu - Lord Eyez
 
Ni kweli, only the strong survive. Kina Ngwair et al walishindwa kuhimili depression wakawa mateja na mauti yakawakuta. Chanzo ni mambo hayahaya kuwa unafanya kazi sana, kipaji kipo na hutoki.

Wapo waliohimili mabifu na kina Fela mpaka leo wapo wakifanya muziki, na wapo waliokubali terms za magodfather na mpaka sasa wanaendelea. Hata hawa Tamaduni muzik bado wapo kwenye game licha ya mabifu na hao magodfather ila ndio hivyo sasa hakuna kutoboa. Unakuwa underground deile

Nyimbo ya Babu Talent ina miaka 6 youtube ila ina viewers laki 2..unaona kabisa uwiano haupo. Kuna mtu anaitwa Kalighraph Jones namba zake zinasomeka balaa, anajitapa mpaka kwa wanaijeria.. ni kwamba anabadilika badilika na anaendana na wakati. Sometimes ubishi unakwamisha mambo.



Nabadilikia humu humu - Lord Eyez
Magodfather hawakwepeki na wapo karibu kwenye kila biashara. Kuna mfanyabiashara alikuwa yupo vizuri sasa siku moja ma-godfather wakampa mchongo na kumwambia chao kitakuwa kiasi gani. Hela ilipolipwa akataka kuwapunja. Wazee wakamwambia bora chukua tu zote endapo utataka kwenda tofauti. Yule jamaa kweli akala zote mwenyewe. Wale mafaza wakawa wametulia kama hakuna kinachoendelea. After 2 years jamaa kajikuta jela kwa kesi ya uhujumu uchumi huku bank accounts zote zikiwa freezed na biashara kufungwa. Ni kwamba lazima ukubali watu wale na wewe ule.
 
Magodfather hawakwepeki na wapo karibu kwenye kila biashara. Kuna mfanyabiashara alikuwa yupo vizuri sasa siku moja ma-godfather wakampa mchongo na kumwambia chao kitakuwa kiasi gani. Hela ilipolipwa akataka kuwapunja. Wazee wakamwambia bora chukua tu zote endapo utataka kwenda tofauti. Yule jamaa kweli akala zote mwenyewe. Wale mafaza wakawa wametulia kama hakuna kinachoendelea. After 2 years jamaa kajikuta jela kwa kesi ya uhujumu uchumi huku bank accounts zote zikiwa freezed na biashara kufungwa. Ni kwamba lazima ukubali watu wale na wewe ule.
Dah noma sana mkuu.

Hapa ndio niliposema kuwa inabidi wana wabadili mentality, wafanye muziki kibiashara. Ukifanya biashara wewe unachoangalia ni faida, hutajali tena style au nini..kama vile wanavyofanya weusi, utaimba ili uuze. Tupac anasema, "Everybody Rap, we dont rap, we rap to make money"
Msikilize hapa dakika 1:08


Kwa hiyo wana wanatakiwa wabadilike waache kukaza, wakae na magodfather wafanye biashara. Ni kama ishu za maridhiano za CCM na Chadema,now wanapongezana na picha kwenye mabango, mambo yanaenda😃😃
 
Dah noma sana mkuu.

Hapa ndio niliposema kuwa inabidi wana wabadili mentality, wafanye muziki kibiashara. Ukifanya biashara wewe unachoangalia ni faida, hutajali tena style au nini..kama vile wanavyofanya weusi, utaimba ili uuze. Tupac anasema, "Everybody Rap, we dont rap, we rap to make money"
Msikilize hapa dakika 1:08


Kwa hiyo wana wanatakiwa wabadilike waache kukaza, wakae na magodfather wafanye biashara. Ni kama ishu za maridhiano za CCM na Chadema,now wanapongezana na picha kwenye mabango, mambo yanaenda😃😃

Imagine leo 2pac akifufuka akasikiliza rapper Snoop Dog anaimba Sensual seduction? 😀😀
 
Wafanye MARIDHIANO NA MA GOD FATHER WA HUU MZIKI ukitaka kula lazma uliwe na pia waimbe Mambo ya mapenz wajiingize kwenye SHOWBIZ,,mfano Nikki mbishi akae chini na msanii binti bongo movie mmoja ampe hela kiasi waact wapenz then penz linanoga humohumo anatoa ngoma ,,hivi hawamuonagi mdgo wao mondi harmonize
 
Back
Top Bottom