Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 8,161
- 11,563
Wapendwa ndugu zangu, majirani, marafiki na familia ya wakulima wa mazao mbalimbali maeneo tofauti nchini,.
Habari za kazi, majukumu na maandalizi ya msimu wetu pendwa wa kilimo?
Nimewiwa kuwasabahi na kuwatakia Neema na Baraka za Mwenyezi Mungu katika maandalizi kabambe ya kuingia rasmi tena shambani, kwani mvua tayari zimeshaanza kunyesha maeneo mengi nchini na dalili za mvua hiyo kunyesha wakati wowote katika baadhi ya maeneo ambayo bado hazijaanza.
Pamoja na kuwatakia maandalizi mema ndugu zangu, nachelea kuomba ushauri, ujuzi, ufahamu na uzoefu wenu kwamba, mie ni miongoni mwa wakulima wenye shamba katika wilaya ya chemba mkoani dodoma.
Na mwaka huu nakusudi kulima Mahindi na alizeti pekee. Na pengine kwa uchache Maharage.
Hebu tafadhali nishauri kutembea na mbegu aina gani yenye matokeo mujarabu na ya uhakika kwa kuzingatia hali ya hewa katika eneo hilo?
Sitaki kusema kuzidi hapo.
Nakushukuru sana kwa ushauri wako na nakutakieni nyote heri na fanaka katika maandalizi ya sikukuu za Christmas 🎄 na mwaka mpya 2024.
Habari za kazi, majukumu na maandalizi ya msimu wetu pendwa wa kilimo?
Nimewiwa kuwasabahi na kuwatakia Neema na Baraka za Mwenyezi Mungu katika maandalizi kabambe ya kuingia rasmi tena shambani, kwani mvua tayari zimeshaanza kunyesha maeneo mengi nchini na dalili za mvua hiyo kunyesha wakati wowote katika baadhi ya maeneo ambayo bado hazijaanza.
Pamoja na kuwatakia maandalizi mema ndugu zangu, nachelea kuomba ushauri, ujuzi, ufahamu na uzoefu wenu kwamba, mie ni miongoni mwa wakulima wenye shamba katika wilaya ya chemba mkoani dodoma.
Na mwaka huu nakusudi kulima Mahindi na alizeti pekee. Na pengine kwa uchache Maharage.
Hebu tafadhali nishauri kutembea na mbegu aina gani yenye matokeo mujarabu na ya uhakika kwa kuzingatia hali ya hewa katika eneo hilo?
Sitaki kusema kuzidi hapo.
Nakushukuru sana kwa ushauri wako na nakutakieni nyote heri na fanaka katika maandalizi ya sikukuu za Christmas 🎄 na mwaka mpya 2024.