Tabia za wanaume zisizowapendeza wanawake!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Ngoja nizidadavue hapa chini kama ifuatavyo...............

1. Aina ya kwanza ni ile ya mwanaume ambaye anatatabirika. Wanawake hawapendi wanaume wanaotabirika kwa sababu wanaelewa ni jinsi gani watalipokea jambo lolote linalotokea. Mwanamke anaweza kujua kabisa kwamba, leo atatolewa outing au hapana, ataletewa zawadi au la. Yaani hakuna kitu tunachokiita surprise. Wanawake wanataka kiasi fulani cha kutotabirika toka kwa wanaume. Ndio maana utakuta anaishi au kuolewa na mwanaume jeuri au mwenye roho mbaya . siyo kwamba anampenda kwa jeuri yake, bali kwa kutotabirika kwake.

2.
Aina ya pili ni ile ya mwanaume anayejisikia (mwenye maringo). Huyu kwa kawaida ni mbinafsi sana. Ni jeuri siyo kwa mpenzi wake tu, bali hata kwa mtu yeyote ambaye anamuona yuko chini yake. Kuwaringia watu wengine ni sawa na kumringia mpenzi wako moja kwa moja.

3. Aina ya tatu ni ile ya wanaume jeuri. Mtu jeuri hana aibu! Wakati mwingine anaonesha waziwazi kwamba anamtamani mwanamke mwingine mbele ya mpenzi wake! Anafikia hatua ya kumsimulia mpenzi wake kuhusu marafiki zake wa kike wa zamani na hata u.p.u.u.z.i waliokuwa wakifanya! Kwa ujumla anawadharau wanawake.

4. Aina ya nne ni ile ya mwanaume bahili. Hamnunulii mpenzi wake zawadi hata siku moja! Kila wakati watokapo outing yeye na mpenzi wake huagiza vyakula vya bei rahisi sana pamoja na kwamba, anazo hela. Anataka kumfanya huyo mpenzi wake atishike naye aagize vya bei rahisi. Na wakati wa kulipa anahesabia fedha mfukoni, anatoa fedha utadhani bajeti inabana sana au utadhani yeye na mpenzi wake wamekubaliana "kukaza mikanda." Mwanaume anaonesha ana mkono wa birika namna hiyo katika siku za kwanza tu za mapenzi! Je huko baadaye itakuwaje? Si atahesabu hata vipande vya nyama jikoni!

5. Aina ya tano ni ile ya mwanaume mbishi. Hata majadiliano ya kawaida tu, yeye anataka kubishana! Anapomtoa outing mwanamke, anakuwa kama amempeleka kwenye mashindano ya mdahalo! Mwanamke hajisikii kuwa huru kutoa maoni au kusema hisia zake, maana atabishiwa.

6.
Aina ya sita ni ya mwanaume asiyekosea. Huyu bwana anapenda sana kuhumu wenzie. Inawezekana hanywi wala havuti sigara, anataka hata wenzie wamuige yeye, wasinywe wala wasivute sigara. Toka siku ya kwanza anayotoka na mwanamke anaanza kumhubiria anayoyataka yeye, siyo asiyoyataka mwanamke. Huyu hataki kabisa mwanamke akawa huru kama yeye, bali angependa yeye amuamulie awe nani na afanye kipi au asifanye kitu gani, ebo! Sasa hapo ni mtu na mpenzi wake au mtu na mtumwa wake!

7. Aina ya saba ni ile ya mwanaume kuwachukia wanawake. Hafichi chuki yake kwa wanawake. Huyu huonesha dhihaka nyingi kwa mpenzi wake na kuwaponda wanawake kwa ujumla wao. Mazungumzo yake yote yatakuwa ni kuwadharau, kuwadhalilisha na kuwanyanyapaa wanawake. Hivi ni mwanamke wa namna gani ambaye atamkubalia mwanaume mpondaji namna hii? Labda mwanamke mwenye mkabala wa kufujwa peke yake au yule mwenye kutaka tu kuchuna buzi na kusepa zake.

Nitaendelea kuwamwagia Tabia za wanaume zisizowapendeza wanawake siku zijazo....
 
Mkuu ahsante kwa ni pweint,ngoja niongezee.
player: mwanamke hapendi lianaume shingo feni.
Pafomensi: mwanamke hapendi michezo ya kitoto,anapenda shughuli
Mpira:kila weekend unaangalia manchesta,tena bar,kwako kuna miiba?
Wazazi: dume linajali ndugu zake tu,ndo nini?
............tuendelee wakuu....
 
h, yani nadhani ntascore 5 au sita hivi, kumbe ndio maana sipendwiiiiii:A S 13:
 
Wanaume wenye vibamia: Wanawake wengi hawapendi wanaume wenye vibamia
Wanaume wenye mitarimbo: Wanawake wengi wanaogopa mitarimbo mikubwa
Wanaume wenye wowowo: Wowowo ni sunnah kwa wanawake
Wanaume wenye sauti nyembaba: Khaa!
Wanaume wasio na ndevu: heheheh dah!
Wanaume wafupi: Duh!
Wanaume wenye matege: Aisee:cool2:
Wanaume wanaokoroma usiku: Phewww
Wanaume wambea: Ni nomer

Source: Mke wa ODM a.k.a bibi yenu.
 
Wanaume wenye vibamia: Wanawake wengi hawapendi wanaume wenye vibamia
Wanaume wenye mitarimbo: Wanawake wengi wanaogopa mitarimbo mikubwa
Wanaume wenye wowowo: Wowowo ni sunnah kwa wanawake
Wanaume wenye sauti nyembaba: Khaa!
Wanaume wasio na ndevu: heheheh dah!
Wanaume wafupi: Duh!
Wanaume wenye matege: Aisee:cool2:
Wanaume wanaokoroma usiku: Phewww
Wanaume wambea: Ni nomer

Source: Mke wa ODM a.k.a bibi yenu.


babu....naomba ridhaa yako niongezee tafadhali.......
 
babu....naomba ridhaa yako niongezee tafadhali.......
Ruksa.... ila ngoja nikuwahi.

Wanaume wenye vitambi, isipokuwa ODM: Wanawake wengi wanapenda athletic figures (six pax lol)

Source: Preta, JF Arachuga.
 
Ngoja nizidadavue hapa chini kama ifuatavyo...............

1. Aina ya kwanza ni ile ya mwanaume ambaye anatatabirika. Wanawake hawapendi wanaume wanaotabirika kwa sababu wanaelewa ni jinsi gani watalipokea jambo lolote linalotokea. Mwanamke anaweza kujua kabisa kwamba, leo atatolewa outing au hapana, ataletewa zawadi au la. Yaani hakuna kitu tunachokiita surprise. Wanawake wanataka kiasi fulani cha kutotabirika toka kwa wanaume. Ndio maana utakuta anaishi au kuolewa na mwanaume jeuri au mwenye roho mbaya . siyo kwamba anampenda kwa jeuri yake, bali kwa kutotabirika kwake.

mwanaume wa aina hii hana madhara makubwa, na rahisi kumhandle loh!!!

2. Aina ya pili ni ile ya mwanaume anayejisikia (mwenye maringo). Huyu kwa kawaida ni mbinafsi sana. Ni jeuri siyo kwa mpenzi wake tu, bali hata kwa mtu yeyote ambaye anamuona yuko chini yake. Kuwaringia watu wengine ni sawa na kumringia mpenzi wako moja kwa moja.


mwanaume wa aina hii hafai yupo radhi nyumbani mke na watoto wale ugali kwa chumvi, yeye mradi kashiba waaalaaa.... na usiombe mke upate shida uhitaji assistance yake...utajutaaaa

3. Aina ya tatu ni ile ya wanaume jeuri. Mtu jeuri hana aibu! Wakati mwingine anaonesha waziwazi kwamba anamtamani mwanamke mwingine mbele ya mpenzi wake! Anafikia hatua ya kumsimulia mpenzi wake kuhusu marafiki zake wa kike wa zamani na hata u.p.u.u.z.i waliokuwa wakifanya! Kwa ujumla anawadharau wanawake.



na usiombe awe jeuri na mkono mwepesi wa kupiga.....wallah ndoa utaiona chungu....mbaya zaidi wanaume wa aina hii hawashauriki hawa...


4. Aina ya nne ni ile ya mwanaume bahili. Hamnunulii mpenzi wake zawadi hata siku moja! Kila wakati watokapo outing yeye na mpenzi wake huagiza vyakula vya bei rahisi sana pamoja na kwamba, anazo hela. Anataka kumfanya huyo mpenzi wake atishike naye aagize vya bei rahisi. Na wakati wa kulipa anahesabia fedha mfukoni, anatoa fedha utadhani bajeti inabana sana au utadhani yeye na mpenzi wake wamekubaliana "kukaza mikanda." Mwanaume anaonesha ana mkono wa birika namna hiyo katika siku za kwanza tu za mapenzi! Je huko baadaye itakuwaje? Si atahesabu hata vipande vya nyama jikoni!

ukishamjua mwanaume wa aina hii wala hakusumbui mkitoka out unaagiza vyakula vya bei, mwache yeye ale vyakula vyake vya bei rahisi...(tahadhari uwe na extra cash mfukoni hawachelewi kukuadhiri hawa..) na uwe mchakarikaji usitegemee kupata tatizo akakusaidia, ingawa yeye akihitaji pesa toka kwako atakughasi mpaka umpe....

5. Aina ya tano ni ile ya mwanaume mbishi. Hata majadiliano ya kawaida tu, yeye anataka kubishana! Anapomtoa outing mwanamke, anakuwa kama amempeleka kwenye mashindano ya mdahalo! Mwanamke hajisikii kuwa huru kutoa maoni au kusema hisia zake, maana atabishiwa.



hahahaaaa kweli wanawake wana kazi....

6. Aina ya sita ni ya mwanaume asiyekosea. Huyu bwana anapenda sana kuhumu wenzie. Inawezekana hanywi wala havuti sigara, anataka hata wenzie wamuige yeye, wasinywe wala wasivute sigara. Toka siku ya kwanza anayotoka na mwanamke anaanza kumhubiria anayoyataka yeye, siyo asiyoyataka mwanamke. Huyu hataki kabisa mwanamke akawa huru kama yeye, bali angependa yeye amuamulie awe nani na afanye kipi au asifanye kitu gani, ebo! Sasa hapo ni mtu na mpenzi wake au mtu na mtumwa wake!
Mr perfect........
wana kuwa na kipaji cha ziada, wanajua kucriticise hadi ujione huna maana


7. Aina ya saba ni ile ya mwanaume kuwachukia wanawake. Hafichi chuki yake kwa wanawake. Huyu huonesha dhihaka nyingi kwa mpenzi wake na kuwaponda wanawake kwa ujumla wao. Mazungumzo yake yote yatakuwa ni kuwadharau, kuwadhalilisha na kuwanyanyapaa wanawake. Hivi ni mwanamke wa namna gani ambaye atamkubalia mwanaume mpondaji namna hii? Labda mwanamke mwenye mkabala wa kufujwa peke yake au yule mwenye kutaka tu kuchuna buzi na kusepa zake.

Mtambuzi, inawezekana wanaume wa aina hii childhood yao ilikuwa na matatizo fulani, au malezi yao kuna vitu fulani wamekosa/wamepotoshwa au wamekuwa na baba mwenye tabia hizo...



Nitaendelea kuwamwagia Tabia za wanaume zisizowapendeza wanawake siku zijazo....

asante kwa darasa...
si tu nilikuwa najifunza lakini nimeenjoy sana maana...............(nitakwambia siku nyingine)
ila umesahau wanawake hawapendi wanaume mala*a..... yaani unakuta hata housegirl huweki, wala ndugu wa kike hawaji....kisa unahofia mumeo asipojaribu kuwabaka atawatongoza...

na wanawake hawapendi wanaume wenye ghubu....Mtambuzi ushawahi kukutana nao? yaani hawana dogo dogo kwao kubwa kubwa kwo kubwa, hawa hata kosa la miaka kumi iliyopita watalikumbushia....
 

mwanaume wa aina hii hafai yupo radhi nyumbani mke na watoto wale ugali kwa chumvi, yeye mradi kashiba waaalaaa.... na usiombe mke upate shida uhitaji assistance yake...utajutaaaa


Mimi sikubaliani na point yako kabisa, vipi mwanaume mwenye maringo asimsaidie mke wake?

Hebu nipe point wapi uliona mwanaume mwenye maringo mke wake akafa njaa.

Vipi mtu awe ana maringo wakati kwake watu wanakufa njaa, labda wanaume wa bongo hao :cool2:
 
Mtambuzi wewe hapo upo kundi lipi?.

Hii mimi imenibamba aisee..............
4. Aina ya nne ni ile ya mwanaume bahili. Hamnunulii mpenzi wake zawadi hata siku moja! Kila wakati watokapo outing yeye na mpenzi wake huagiza vyakula vya bei rahisi sana pamoja na kwamba, anazo hela. Anataka kumfanya huyo mpenzi wake atishike naye aagize vya bei rahisi. Na wakati wa kulipa anahesabia fedha mfukoni, anatoa fedha utadhani bajeti inabana sana au utadhani yeye na mpenzi wake wamekubaliana "kukaza mikanda." Mwanaume anaonesha ana mkono wa birika namna hiyo katika siku za kwanza tu za mapenzi! Je huko baadaye itakuwaje? Si atahesabu hata vipande vya nyama jikoni!

 
Ruksa.... ila ngoja nikuwahi.

Wanaume wenye vitambi, isipokuwa ODM: Wanawake wengi wanapenda athletic figures (six pax lol)

Source: Preta, JF Arachuga.

hapo kwenye bluu naomba nigandamizie wino......kabla sijaendelea kwa ridhaa yako.....
 
Hii mimi imenibamba aisee..............
4. Aina ya nne ni ile ya mwanaume bahili. Hamnunulii mpenzi wake zawadi hata siku moja! Kila wakati watokapo outing yeye na mpenzi wake huagiza vyakula vya bei rahisi sana pamoja na kwamba, anazo hela. Anataka kumfanya huyo mpenzi wake atishike naye aagize vya bei rahisi. Na wakati wa kulipa anahesabia fedha mfukoni, anatoa fedha utadhani bajeti inabana sana au utadhani yeye na mpenzi wake wamekubaliana "kukaza mikanda." Mwanaume anaonesha ana mkono wa birika namna hiyo katika siku za kwanza tu za mapenzi! Je huko baadaye itakuwaje? Si atahesabu hata vipande vya nyama jikoni!


hapo sasa.....badilika Mtambuzi........

 
Back
Top Bottom