Hivi ingekuwaje kama wanawake ndio wangekuwa wanatongoza wanaume?

THE FIRST BORN

JF-Expert Member
Apr 24, 2019
1,727
3,286
Jamii yetu inaamini kuwa Mwanaume ndiye mtongozaji na Mwanamke ndie kiumbe anastahili kutongozwa, si vinginevyo, na hii ni universal accepted, hayo ya mwanamke kuanza kusema ni ya sasa hivi kizazi cha AI.

Ila hata Biblia utaona mtu wa kwanza kuumbwa alikua mwanaume so it means alieanza kuhisi upekwe ni Mwanaume akahitaji mwenzake so ina apply hivyohivyo hadi kwenye kuanzisha relationship.

Najua utakubaliana na mimi ndugu msomaji, ni kuwa wanawake wanatongozwa sana haijalishi;
  • Kaolewa
  • Ana mchumba
  • Ni Mchungaji
  • Ni mlemavu
  • Single mother
  • Hana kazi
  • Haijalishi ana hela au hana

Wanaume huwa hawaangalii hwua wanarusha tu.

Mada yangu italenga sana hao walioolewa na wenye wapenzi au wachumba. Hawa wanawake kwenye hii hali huwa wanatongozwa sana ila sasa sio wote hua wanasaliti kuna baadhi wanashikilia bomba, wanakuwa watiifu, kuna baadhi wanakengeuka.

Nikajiuliza, hivi ingekua mwanamke ndiye mtongozaji na mwanaume ndiye anatongozwa wanaume wangapi wangekua hawacheat?

Yaani imagine mwanaume yupo kwa ndoa yake au ana mchumba wake anatoke mwanamke anasema mimi nimekuelewa we kaka au we mwanaume, nitakupa kila kitu! Wanaume wangapi tungetoboa hapa ukizingatia sisi hisia zetu huwa ni gusa unase?😂
 
Back
Top Bottom