Swali Rahisi: Nyerere aliwashughulikiaje Waganda "Illegals" wakati wa "chokochoko" Za Idi Amin?

Umeshindwa kuelezea suala hili chronologically? ... au unataka kuupindisha ukweli na kuhusisha ugomvi wa Kagame na JK kama ndiyo chanzo.

Malalamiko yalianza muda mrefu kutoka kwa wenyeji. Kumyanyasa na kumwibia mali binadamu yeyote ni kosa, tunajua hilo.

Ndugu Kobelo,

Ni kweli malalamiko ya wenyeji yalianza siku nyingi. Lakini kwa nini hatua hizo ziwe sasa? Kwani hiyo siku nyingi Rais na serikali yake walikuwa wapi? Kwani wakati wahamiaji hao wanahamia kienyeji, iwe ni kwa kutoroka makambi ya wakimbizi au kuvuka mpaka kienyeji serikali ilikuwa wapi?

Lina kuja hili la haki za hawa wahamiaji kikatiba. Katiba yetu imetamka wazi binadamu wote, watu wote kuzaliwa HURU na KUWA NA HAKI SAWA MBELE YA SHERIA. Ni kweli Wanapaswa kurejeshwa kwao kama wamekuwa humu kinyume na sheria zetu. Lakini siyo kwa kufukuzwa kienyeji. What is the meaning of diplomacy then? Ni mara ngapi hata wafungwa wanaporejeshwa makwao kunafanyika mawasiliano baina ya nchi husika, utaratibu wa kuwakabidhi na kuwapokea unafanyika kwa murua kabisa? Ni kweli kwamba Wafungwa wana hadhi kuliko hawa wageni?

Halafu kifuate hiki kipengele cha nasaba kati ya nchi jirani na wananchi waishio mipakani. Kwa waliowahi kuishi mipakani watakuwa mashahidi kuwa ni vigumu kuzingatia mpaka wa nchi. Ukienda maeneo hayo ni kawaida kuona mtoto anatoka asubuhi kwenda shule "Kenya" kwa sababu ni karibu na nyumbani kuliko ya "Tanzania" hata kama ni kwa kilomita 1. Kule ni kawaida mtu kukwambia naenda kwa mjomba ikawa anaenda "Kenya" au kukuta mtu anaaga naenda kisimani na ikawa anaenda kuchota maji Burundi. Mwisho wa siku, pamoja na malalamiko yote, siyo halali sana kuwafukuza tu kienyeji kwa sababu wengine ni Wajomba zao na Wahaya flani au ni mama mdogo wa rafiki yako wa pale mpakani na huenda mama mzazi wa Mtanzania flani! Na Kama wamekuwa "Wahamiaji Haramu" ghafla, nataka kukubaliana, kwa mantiki hiyo ya nasaba na kulinda utu, na mwana JF mmoja aliyewatambua hawa wageni kwa mtazamo wa "Wajomba zetu Haramu", "mama zetu haramu" au "Mkeo haramu" (Which is Mbaya)...Na kama wote ni wahalifu basi nasikitika kwani kuna wake za wenzetu siyo "Wananchi kabisa" na wengine wetu ni mapolisi wakuu (Law upholders)! What do you think. In the end hawa ni binadamu wa kawaida! Kuvunjika kwa sheria za uhamiaji hakuwatoi ubinadamu wao!. Jamani hata muhalifu pia ana haki zake.

Vyovyote inavyokuwa kitendo kile kilifanyika kwa jazba za kiongozi na kwa hasira ya matusi ya Rais wa jirani na si kwa kujali sana vilio vya wananchi. Na sitaki kuamini kuwa kwa vilio vya muda huo mrefu ndiyo Rais anavisikia juzi!

Mwisho nahitimisha kwa kusema ni vema tukawa mfano kwa wenzetu kwa vile tunavyotaka watufanyie sisi. Kama wote tungefanya hivyo sidhani kama kungekuwa na mahusiano mazuri na yeyote duniani. Imagine the world where ukipata wageni waliovunja sheria unawakusanya tu unakwenda nao mpakani kwao unawabwaga hapo na kuondoka! Kwamba na China ikusanye wale wauza unga "wetu" wote iwasafirishe mpaka bandarini iwaache kienyeji. Au Afrika ya Kusini ijibebee kina "Masogange wetu" wote ije iwamwage mpakani na kuondoka kimyakimya! Jamani kutakuwa kumebaki thamani ya ubinadamu duniani?......Ile ilikuwa hasira na haikuwa sawa. Siyo kitendo cha mfano wala hakifai kuigwa na si cha kupongezwa kwa namna yoyote hasa kufanywa na kiongozi tena mwenye washauri kibao.

Binafsi naona Mwanakijiji is right. And I do apologize, sincerely, if my understanding is contradictory to yours.
 
Mkuu pengine wewe ulikuwa bado kinda mwaka 1972 hadi 1978 ilipoanza vita rasmi na Idi Amin.
Nyerere alifanya kosa la kimsingi kutochukua hatua ya ku- contain the fith column.
Hata hivyo by mwaka 1978/79 somo lilikuwa limeshaeleweka baada ya Amin kuingia Kagera kama nyumbani kwake.
Mwalimu aliwakusanya kina Oyite Ojok na hata kina Museveni, waganda, wakapigane kwa ajili y ao wenyewe na kwa ajili ya Tanzania.

JK kafanya kweli, ni lazima adui ajulikane toka mwanzo kwa vile ameshajitanabahisha toka mapema, pa kupiga paeleweke mapema.
Kama mtu anafikiri kutukanwa na kutishiwa maisha kwa mkuu wa nchi na bado mtu ukachekelea kama huna akili nxuri, basi hata a
yekutukana atajua kuwa wewe ni zuzu.
Ahaa, hivi kumbe Wanyarwanda ni adui zetu? Now I get it.
 
We nawe kumbe hauna tofauti na Mwanakijiji, sasa chama kinaingiaje hapo?
pitia pitia matamko ya 'chama' kuhusu maswala na matukio mbalimbali ya nchi yetu utajua chama kinaingiaje.
Umesahau kama 'chama' huwa kinaagiza serikali juu ya jambo flani?
Kwani chama kinapofanyia vikao ikulu huwa kinaingiaje?Usijadai leo kipofu kesho unaona keshokutwa kipofu.
JIBU HOJA YA MMM!
 
umeandika kishabiki sana hata ukweli umekushinda kuweka bayana nadhani kunakitu unakitafuta au unachezea akili za watu.

No Simiyu Yetu. You are missing the big picture here. Do you think it was right to just throw them without liaising with the concerned neighbours? Do you actually think for Rwandans living in the country illegally..does that make them less human? what do you make of the constitution then? Unafikiri wao kuvunja sheria kunakupa excuse ya kukiuka haki zao kama binadamu?

Hivi nani mshabiki kwa mtindo huo?
 
mzee nlikua nakuheshimu ila kwanzia leo nakudharau,hawajafukuzwa waRWANDA tu,bali wahamiaji haramu wote wapo WACONGO(ambao mnasema kikwete ni rafiki yao),wapo WARWANDA na BURUNDI,.

alichofanya kagame na waziri wake wa mambo ya nje ni kuitangazia dunia kuwa ni WARWANDA tu wanaofukuzwa na kuna baadhi ya wajing.a kama wewe mmekubali uongo huo.!

hivi mnafurahi jinsi watanzania wa kule mipakani wanavoteseka..

KABLA MLIKUA MNAPIGA KELELE KUWA KIKWETE WASHUGHULIKIE WANYARWANDA WOTE WALIOPO NCHINI,SAHIVI MNAMPINGA,KWANZIA LEO NAKUDHARAU SANA WEWE MZEE...
 
Naona MCHUMI DARAJA LA KWANZA anashindana ukinga na Ze Marcopolo
 
Katika hili Mwanakijiji umepotoka...linapokuja suala la usalama wa nchi...sote tunatakiwa kuwa kitu kimoja...chuki uliyonayo kwa kiongozi wetu JK ime-cloud you ability to make sound judgement...

Soon watu wataanza kupuuza thread zako....take my writings...this is too low for Mwanakijiji...tumia vizuri talanta aliyokupa MUNGU....
 
Kwahiyo utamaduni wa mtanzania ni kukubali mgeni akukataze kufanya movements zako?

Hi ZeMarcoplo,
Utamaduni sahihi has been kulinda mipaka yetu Wageni wasiingie ovyoovyo. Na siyo kuacha wajiingilie kiholela nchini huku kukiwa na jeshi la Uhamiaji na Usalama wa Taifa wanaolipwa mishahara kwa kodi zetu ,halafu tungojee tukigombana na Rais wa jirani tuwafukuze kama nini sijui! Of all the days ndiyo wameonekana kwanza juzi? Wakati wanahamia Serikali ilikuwa likizo?.... Hii ni aibu.
 
Mwanakijiji is very right,
These people are very innocent and have lived here for many decades without any harm to us until JK and PK differed due to the former unwise advice.
Personally nimefanya kazi miaka mingi Kagera na all time hawa jamaa wafugao ng'ombe hawana shida kabisa as far as security is concerned tatizo lao kubwa ni environmental degredation i agree.

Hawa majambazi ni collaboration kati ya wakimbizi wa Burundi waliojichanganya na wenyeji wa Kagera na Kigoma i am sure hata authorities zetu zinajua ila wanapenda ku appease their masters.

Let us act as civilised Tanzanians tuache kushabikia upumbavu.
 
mzee nlikua nakuheshimu ila kwanzia leo nakudharau,hawajafukuzwa waRWANDA tu,bali wahamiaji haramu wote wapo WACONGO(ambao mnasema kikwete ni rafiki yao),wapo WARWANDA na BURUNDI,.

alichofanya kagame na waziri wake wa mambo ya nje ni kuitangazia dunia kuwa ni WARWANDA tu wanaofukuzwa na kuna baadhi ya wajing.a kama wewe mmekubali uongo huo.!

hivi mnafurahi jinsi watanzania wa kule mipakani wanavoteseka..

KABLA MLIKUA MNAPIGA KELELE KUWA KIKWETE WASHUGHULIKIE WANYARWANDA WOTE WALIOPO NCHINI,SAHIVI MNAMPINGA,KWANZIA LEO NAKUDHARAU SANA WEWE MZEE...

Brother huyo siyo mzee...ni kijana sana...!!...swali alilouliza peke yake...linaeleza mambo mengi...

.punguza munkari mkulu...kula iddi yako kwa amani..
..
 
MMM umewahi kutekwa na hao jamaa?je unajua mapori ya biharamulo ngara na karagwe si salama na wahamiaji haramu ndio wamejaa huko?Rais aliwaamuru kutokana na uhalifu wanaofanya na si eti alipize kisasi kwa Kagame!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
mzee nlikua nakuheshimu ila kwanzia leo nakudharau,hawajafukuzwa waRWANDA tu,bali wahamiaji haramu wote wapo WACONGO(ambao mnasema kikwete ni rafiki yao),wapo WARWANDA na BURUNDI,.

alichofanya kagame na waziri wake wa mambo ya nje ni kuitangazia dunia kuwa ni WARWANDA tu wanaofukuzwa na kuna baadhi ya wajing.a kama wewe mmekubali uongo huo.!

hivi mnafurahi jinsi watanzania wa kule mipakani wanavoteseka..

KABLA MLIKUA MNAPIGA KELELE KUWA KIKWETE WASHUGHULIKIE WANYARWANDA WOTE WALIOPO NCHINI,SAHIVI MNAMPINGA,KWANZIA LEO NAKUDHARAU SANA WEWE MZEE...

Mbona wahamiaji wako wengi tu humu? Siyo Wakongo na Warundi wala Wanyarwanda. Kuna wengi sana. Na wengine hata siyo majirani! Na siyo kweli wako Kagera tu, mbona wako kibao nchi nzima? Kwa nini ni Kagera tuuuu na kwa nini sasa? Kwa nini inakuja hiyo wakati unajibu hoja za Kagame?

What Mwanakijiji is saying ni kuwa.....Waliohamia nchini bila kufuata taratibu washughulikiwe ila siyo kwa kukiuka haki za "ubinadamu wao" Kwamba "tuzingatie matakwa ya katiba yetu wenyewe wakati wa kushughulikia tatizo hili na tuwe fair kwa wote!"

Nashauri uendelee tu kumheshimu.
 
Respect Mkuu! Nimejifunza mengi sana kwa siku hii ya leo kutoka kwako. You are really a man from Tanganyika and not a Tanzanian. Kwani nikikuhesabu wewe ni mtanzania nitakuvunjia heshima yako. Watanzania tumekuwa wanafki sana. Tumekuwa watu wa kujipendekeza pendekeza. Hatutaki kutumia ubongo wetu kujiuliza kwa nini mambo yanakuwa hivi? Sisi ni bendera fuata upepo. Hatuna nguvu za kuwapinga wahujumu. Roho zetu zimekufa hatuna means za kuweza kufight in a democratic way kwani tunajua hatuna future na ndiyo maana tunawaacha majambazi waendelee kutunyanyasa na kuwaonea watu ambao ni innocent.

Wewe ni mzalendo hasa! Gombea madaraka! Kura yangu ni yako. Watu kama nyinyi ndiyo tunao wahitaji katika taifa letu. Kwani mmejaa busara ambazo zinaweza zikaleta amani katika nchi hata kama wananchi wana matatizo.

Mkulu

Invisible na timu yake hawaruhusu matumizi ya lugha ngumu kwenye hii forum tukufu...lakini naomba ujue kwamba nimekutukana tusi kubwa sana...
 
Kwa nini watu walazimishwe na baadhi ya wapambe nuksi tukubali kila kitu anachoongea mkuu ni sawa?
Ina maana kama kuna njia tofauti ya kutumia tukaweza kuepuka migongano juu ya kuwarudisha hawa wahamiaji haramu watu wasitoe mawazo yao maana yatakuwa tofauti nakuonekana kama si wazalendo wa nchi hii.
Wako washauri wazuri na tena hawana nyadhifa za juu za uongozi.
Kama mtu kakosea hata kama anacheo gani ni kakosea tu hivyo wale wanaotoa mawazo tofauti wapewe nafasi washauri ni njia gani nzuri ya kuenda nayo. Tujifunze kukosoana na si kutishana.

Enzi ya Zidumu Fikra za Mwenyekiti Imepita Sasa ni Enzi ya Mawazo Mchanyato.
 
Mwanakijiji is very right,
These people are very innocent and have lived here for many decades without any harm to us until JK and PK differed due to the former unwise advice.
Personally nimefanya kazi miaka mingi Kagera na all time hawa jamaa wafugao ng'ombe hawana shida kabisa as far as security is concerned tatizo lao kubwa ni environmental degredation i agree.

Hawa majambazi ni collaboration kati ya wakimbizi wa Burundi waliojichanganya na wenyeji wa Kagera na Kigoma i am sure hata authorities zetu zinajua ila wanapenda ku appease their masters.

Let us act as civilised Tanzanians tuache kushabikia upumbavu.

Rwamarungu tazama hilo andiko lako hapo kwenye red....bado mnaendeleza kashfa??!!...

...tumia uhuru ulionao kwa sasa kwa hekima kubwa....

 
mbona wahamiaji wako wengi tu humu? Siyo wakongo na warundi wala wanyarwanda. Kuna wengi sana. Na wengine hata siyo majirani! Na siyo kweli wako kagera tu, mbona wako kibao nchi nzima? Kwa nini ni kagera tuuuu na kwa nini sasa? Kwa nini inakuja hiyo wakati unajibu hoja za kagame?

What mwanakijiji is saying ni kuwa.....waliohamia nchini bila kufuata taratibu washughulikiwe ila siyo kwa kukiuka haki za "ubinadamu wao" kwamba "tuzingatie matakwa ya katiba yetu wenyewe wakati wa kushughulikia tatizo hili na tuwe fair kwa wote!"

nashauri uendelee tu kumheshimu.

na mbona kikwete hakusema kagera tu.?

Hii operation ni hadi kigoma sema hata waandishi wa habari wanaona story inayouza ni ya rwanda na ndio maana wanakazania rwanda..

Na kuhusu wahamiaji kuwepo nchi nzma labda yeye kaamua kuanza na huko kagera na kigoma,unataka kulazimisha aanzie arusha au.?

Alafu mbona hii operation imewahi kufanyika hata kipindi cha mkapa.?

Tunajua kikwete si kiongozi mzuri lakini sio kila kitu mpinge jamani.!wao wenyewe wanaohamishwa wanasema hawaumizwi wala kufanywa chochote sasa hizo haki za ubinadamu zimevunjwa wapi.!

Hivi unajua huo upendo uliondikwa kwenye katiba ndio unaotucost sahivi.?kagame hakutakiwa kumtukana kikwete na kumtisha kumdhuru kwa ushauri mdogo tu kama ule,wakati anajua maamuzi yake yakutoweka ulinzi mipakani ndo inafanya rwanda ipumue kwa kuwa na raia wanaotosha..
 
hii operesheni iliwahusu wanyarwanda specifically hiyo kusema wahamiaji haramu kutoka mataifa yote ni unafki,
ni mkenya gani aliyerudishwa kwao? mganda, wazambia? wamalawi? wamozambique, wacongo, warundi walioingia bila vibali wamejaa nchini ila unfortunattely rais kawaona wanyarwanda pekee..
au ndo' wanataka kutuambia huo uharifu unafanywa na wanyarwanda pekee? kifupi kikwete kachemka katika hili!

Umefanya utafiti katika hilo...kwamba walengwa ni wanyarwanda tu..SIYO KWELI...hata kama ndivyo...hao wengine WANAADABU...

...Tuliwapenda sana na ndiyo maana tukawapokea wakati wa shida zao ..

.sasa kwao kupo shwari ...na nasikia wanamiji misafi ...ndiyo kitovu cha mawasiliano ya mitandao ya kompyuta...growth ya Per capita GDP is very promising....

..nafikiri ni wakati muafaka WARUDI KWAO...

Kama ilivyo kwa binadamu wengi ukipata mafanikio unaanza kujiinua...hata aliyekusaidia unaanza kumtoa kasoro...

MFADHILI MBUZI...UTAMNYWA SUPU.....
 
No Simiyu Yetu. You are missing the big picture here. Do you think it was right to just throw them without liaising with the concerned neighbours? Do you actually think for Rwandans living in the country illegally..does that make them less human? what do you make of the constitution then? Unafikiri wao kuvunja sheria kunakupa excuse ya kukiuka haki zao kama binadamu?

Hivi nani mshabiki kwa mtindo huo?

Nimelipenda hilo jicho...asalaam aleikum
 
Back
Top Bottom