Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
16 Novemba 2022 niliandika katika mtandao wa Twitter au X kama unavyoitwa kwa sasa kwamba vigogo wengi ndani ya CCM wanatumia bendera za CCM hasa wakati wa chaguzi kusafirisha wahamiaji haramu. Miezi 16 baadaye yani March 24, 2024 linakamatwa gari lenye bendera ya CCM likisafirisha wahamiaji haramu.
Watu wengi wako CCM sio kwa ajili ya maslahi ya nchi isipokuwa wengi wako huko kwa ajili ya maslahi binafsi. Bendera ya CCM inatumika kama kichaka cha kuficha wezi na kuliumiza taifa.
Mtandao huu wa kusafirisha wahamiaji haramu ni mkubwa sana unahitaji vyombo vya kimataifa kuudhibiti. Nikiwa gerezani nilifanya uchunguzi kiasi kuhusu biashara hii ya human trafficking kilichonisikitisha ni kwamba wengi wanaofanya biashara hii ni vigogo wa ccm na polisi. Mmoja wa vigogo wa polisi nilimuonya wakati wa kikao cha wiki ya sheria kilichowashirikisha wafungwa, mahabusu na wadau wa sheria wakiwepo polisi pale gerezani. Nilimuambia ajichunge kuna mafaili yake mabaya. Mwaka mmoja baadaye 2022 vigogo wawili wa polisi akiwemo yule mmoja niliyemuonya walikamatwa Mbeya wakisafirisha wahamiaji haramu wakawekwa lock up kisha baadaye wakahamishwa vituo vya kazi kama adhabu bila kufikishwa mahakamani wala kufukuzwa kazi. Hii inadhihilisha kwamba biashara hii ina mtandao mkubwa.
Huko Iringa kada, mfadhili na kiongozi wa CCM magari yake yalikamatwa yakisafirisha wahamiaji haramu. Kilichotokea ni kwamba magari hayo yaliachiwa na baadaye madereva wake waliachiwa huku afisa uhamiaji aliyeonyesha uzalendo wa kuhakikisha kesi hiyo inafika mahakamani alijikuta kwenye matatizo. Kumbuka sheria ya kusafirisha wahamiaji haramu ni kifungo cha miaka isiyopungua 20 jela na kutaifisha gari zilizokamatwa katika biashara hiyo.
Kwa kumalizia ni kwamba wanaCCM wa kweli ni mzee Warioba na Mzee Butiku hawa wengine ni vibaka tu wanaotumia CCM kwa maslahi yao bianafsi.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Pia soma > Asafirisha wahamiaji 20 kwa V8 yenye bendera ya CCM
Watu wengi wako CCM sio kwa ajili ya maslahi ya nchi isipokuwa wengi wako huko kwa ajili ya maslahi binafsi. Bendera ya CCM inatumika kama kichaka cha kuficha wezi na kuliumiza taifa.
Mtandao huu wa kusafirisha wahamiaji haramu ni mkubwa sana unahitaji vyombo vya kimataifa kuudhibiti. Nikiwa gerezani nilifanya uchunguzi kiasi kuhusu biashara hii ya human trafficking kilichonisikitisha ni kwamba wengi wanaofanya biashara hii ni vigogo wa ccm na polisi. Mmoja wa vigogo wa polisi nilimuonya wakati wa kikao cha wiki ya sheria kilichowashirikisha wafungwa, mahabusu na wadau wa sheria wakiwepo polisi pale gerezani. Nilimuambia ajichunge kuna mafaili yake mabaya. Mwaka mmoja baadaye 2022 vigogo wawili wa polisi akiwemo yule mmoja niliyemuonya walikamatwa Mbeya wakisafirisha wahamiaji haramu wakawekwa lock up kisha baadaye wakahamishwa vituo vya kazi kama adhabu bila kufikishwa mahakamani wala kufukuzwa kazi. Hii inadhihilisha kwamba biashara hii ina mtandao mkubwa.
Huko Iringa kada, mfadhili na kiongozi wa CCM magari yake yalikamatwa yakisafirisha wahamiaji haramu. Kilichotokea ni kwamba magari hayo yaliachiwa na baadaye madereva wake waliachiwa huku afisa uhamiaji aliyeonyesha uzalendo wa kuhakikisha kesi hiyo inafika mahakamani alijikuta kwenye matatizo. Kumbuka sheria ya kusafirisha wahamiaji haramu ni kifungo cha miaka isiyopungua 20 jela na kutaifisha gari zilizokamatwa katika biashara hiyo.
Kwa kumalizia ni kwamba wanaCCM wa kweli ni mzee Warioba na Mzee Butiku hawa wengine ni vibaka tu wanaotumia CCM kwa maslahi yao bianafsi.
Mdude Mpaluka Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Pia soma > Asafirisha wahamiaji 20 kwa V8 yenye bendera ya CCM