Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,105
Niwapongeze viongozi wa halmashauri Kasulu kwa msimamo wao. Nimpongeze kipekee yule Afisaa Uhamiaji kwa kusimama imara na kuhakikisha hatoi tamko mbele ya Makonda kuhusu Uhalali wa Uraia wa Tanzania
Kwa mijibu wa sheria ya Uraia ya Tanzania ukisoma inaeleza kwamba mwenye mamlaka ya kiutawala kumtangaza mtuhumiwa wa uraia kwamba ni RAIA ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.
Nadhani Makonda hajui sheria zilizopitishwa na Bunge zinasemaje; angekuwa anafahamu kwamba afisa Uhamiaji hana final say ya uraia wala asingeangaika na afisa Uhamiaji. Japo pia tunabudi kumshukuru afisa yule wa kike kwa kujitambua na kutotetereka wakati akishinikizwa aseme diwani wa CCM ni RAIA wa Tanzania.
Lakini pia niwapongeze wote walioonyesha msimamo kwamba Katibu Mwenezi hana mamlaka yakumtamka mtu ni RAIA. Najiuliza endapo Makonda angekuwa ni waziri wa mambo ya ndani angewapa wageni wangapi uraia kwa matamko? Ipo wakati huyu bwana atakutana na mtumishi asiyejitambua na litatoka tamko gumu sana kwa wananchi. Tusipoviheshimu vyombo vya dola tukaanza kumdharau RPC mara Uhamiaji tutaondoa imani ya wananchi kwa vyombo hivi na uhalifu itashamiri.
Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama amkeni usingizini, katazeni wasaidizi wenu kwenda kwenye majukwaa ya kisiasa wanapohitajika.......mwenye hoja aiwasilishe kwenu kwa maandishi .
Sisi RAIA mkitupa madaraka na kuturuhusu kuingia nyumbani kwenu tutaweka Kila kitu wazi coz hatuna siri wala staha ya kulinda nchi. Tunaamini amani tuliyonayo imekuja kwa majahazi kumbe kuna vyombo vinatusaidia kudhibiti
Kwa mijibu wa sheria ya Uraia ya Tanzania ukisoma inaeleza kwamba mwenye mamlaka ya kiutawala kumtangaza mtuhumiwa wa uraia kwamba ni RAIA ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.
Nadhani Makonda hajui sheria zilizopitishwa na Bunge zinasemaje; angekuwa anafahamu kwamba afisa Uhamiaji hana final say ya uraia wala asingeangaika na afisa Uhamiaji. Japo pia tunabudi kumshukuru afisa yule wa kike kwa kujitambua na kutotetereka wakati akishinikizwa aseme diwani wa CCM ni RAIA wa Tanzania.
Lakini pia niwapongeze wote walioonyesha msimamo kwamba Katibu Mwenezi hana mamlaka yakumtamka mtu ni RAIA. Najiuliza endapo Makonda angekuwa ni waziri wa mambo ya ndani angewapa wageni wangapi uraia kwa matamko? Ipo wakati huyu bwana atakutana na mtumishi asiyejitambua na litatoka tamko gumu sana kwa wananchi. Tusipoviheshimu vyombo vya dola tukaanza kumdharau RPC mara Uhamiaji tutaondoa imani ya wananchi kwa vyombo hivi na uhalifu itashamiri.
Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama amkeni usingizini, katazeni wasaidizi wenu kwenda kwenye majukwaa ya kisiasa wanapohitajika.......mwenye hoja aiwasilishe kwenu kwa maandishi .
Sisi RAIA mkitupa madaraka na kuturuhusu kuingia nyumbani kwenu tutaweka Kila kitu wazi coz hatuna siri wala staha ya kulinda nchi. Tunaamini amani tuliyonayo imekuja kwa majahazi kumbe kuna vyombo vinatusaidia kudhibiti