Swali: CCM ni Chama Cha 'Mapinduzi' Yepi?

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,573
19,456
Tarehe 5 mwezi februari mwaka 1977 nikiwa mwanafunzi wa Form 3, nilikuwa mmojawapo wa waliochukuliwa kutoka shuleni kwetu kuunda gadi moja ya kucheza halaiki tukishirikiana na wanafunzi wa shule za msingi.

Katika hotuba yake Mwalimu Nyerere aliyoitoa kutokea uwanja wa Aman kule Zanzibar alituahidi kuwa waliamua kuunganisha vyama vya TANU na ASP ili kuunda chama kiomoja chenye nguvu kitakacholeta mapinduzi ya haraka kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa watanzania wote. Wakati huo TANU ilikuwa imefikisha umri wa miaka 23 wakati ASP ilikuwa na umri wa miaka 20 tu. Katika kipindi cha uhai wa vyama hivyo vya TANU na ASP vilikuwa vimeshaleta mafanikio makubwa sana nchini. Vyote viliondoa ukoloni nchini na vilikuwa vimeshaanza kuboresha maisha ya mtanzania. Vilijenga mazingira ambamo wanachi walikuwa wanajivunia nchi yao na viongozi walikuwa wanajua kuwa wao ni watumishi wa wananchi; malalamiko ya wananchi yalikuwa yakichukuliwa kwa uzito sana na ule msingi wa CHEO NI DHAMANA ulikuwa na uzito sana.

Leo hii ni miaka 31 tangu CCM izaliwe; huo ni umri mkubwa sana zaidi ya ule wa vyama vilivyoizaa. Mazingira yaliyojengwa na chama hiki ni yale ambamo wananchi hawana imani na utawala, na vile vile watawala wamekuwa hawaogopi malalamiko ya wananchi. Yote hayo kwa pamoja yameondoa uzalendo kabisa miongoni mwa watu wetu ambapo, viongozi wetu bila woga wanaweza kusaini mkataba wa kukodisha yetu kwa mtu mwingine milele!! !!. na mtu akiuliza kulikoni, basi anapewa vitisho vikali.

Mfano mzuiri ni hili tishio lililotolewa na Katibu Mkuu wa CCM dhidi ya kijana Nape Nnauye kufuatia tamko lake kuhusu ufisadi ndani ya UVCCM. Tihio hilo linaonyesha jinsi gani chama hicho kinavyoheshimu mafisadi na kuwapuuza wananchi tofauti na ilivyokuwa wakati wa TANU na ASP. Kwa nini Makamba amtishie kijana yule badala ya kumtaka alete ushahidi ili yeye (Makamba) aweze kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya watuhumiwa hao badala ya kutoa onyo kabla ya kuangalia ushahidi unasemaje. Huko siyo kujenga mazingira ya mapinduzi.

Ndiyo maana najiuliza, je kweli chama hiki bado ni chama cha Mapinduzi yale tuliyoahidiwa mwaka 1977?
 
  • Thanks
Reactions: PNC
ccm si chama cha mapinduzi, mapinduzi makubwa alifanya nyerere, mapinduzi amabayo sasa yako kwenye vitabu vichache sana vya historia, kwa uhakika yatatotolewa.

sasa chama hiki hakina jipya, hakina mkakati wa kusaidia nchi unaotekelezeka, basi tu tupo kwa mazoea.
 
CCM kama Chama si kibaya, walio wabaya ni watendaji na viongozi wake. Ni viongozi na Watendaji ambao wamekidhalilisha Chama cha Mapinduzi na kukifikisha mahali kilipo.

Kama tunavyoongelea Chadema na Ukabila, Chadema kama chama si cha Kikabila, ila ni uongozi ambao umefanya kionekane kuwa ni cha Kikabila, same with CCM na Ufisadi.

Viongozi na watendaji wengi wa CCM, hawafuati kwa undani imani ya Chama chao, ndio maana kinaonekana kupoteza mwelekeo.

Kinachoipa CCM nguvu ni wanachama wakweli, Wakulima na Wafanyakazi ambao wamekuwa katika chama na kushuhudia uimara wake, na bado wanasubiri siku ya nuru ambapo kitarudia hadhi na heshima yake.
 
CCM si chama cha mapinduzi,hili ni jina tu lililotafutwa na wajumbe na baada ya kina Thabit kombo kulipenda kutokana na mapendekezo basi cham kikaitwa hivyo.

Mapinduzi gani?Ya kuleta hali nzuri kwa wananchi? Au mapinduzi ya zanzibar? Inategemea kilichokuwa ndani ya vichwa vya wajumbe.HEUNDA WALIKUWA WAMESHIBA PILAU NA STAREHE ZA TAARABU MMOJA AKAKURUPUKA NA NENO MAPINDUZI...
 
Tulitegemea mapinduzi yalete positive results na kwa kuwa negative na positive yote ni majibu,basi CCM inabaki kuwa chama cha mapinduzi.Sasa mapinduzi kutoka wapi kuelekea wapi ni suala lingine.
 
CCM kama Chama si kibaya, walio wabaya ni watendaji na viongozi wake. Ni viongozi na Watendaji ambao wamekidhalilisha Chama cha Mapinduzi na kukifikisha mahali kilipo.

Kama tunavyoongelea Chadema na Ukabila, Chadema kama chama si cha Kikabila, ila ni uongozi ambao umefanya kionekane kuwa ni cha Kikabila, same with CCM na Ufisadi.

Viongozi na watendaji wengi wa CCM, hawafuati kwa undani imani ya Chama chao, ndio maana kinaonekana kupoteza mwelekeo.

Kinachoipa CCM nguvu ni wanachama wakweli, Wakulima na Wafanyakazi ambao wamekuwa katika chama na kushuhudia uimara wake, na bado wanasubiri siku ya nuru ambapo kitarudia hadhi na heshima yake.

Mchungaji, hshima kwako.
Ninavyoelewa mimi, tafsiri ya chama ni; Kikundi cha WATU wenye itikadi...
sasa nashangazwa sana na mchango wako ambao unataka kukitenga CHAMA na WATU. Ninavyofahamu, chama hakiwezi kuwa chama bilawatu. Set of rules and regulations in themselves cam hardly be CHAMA, Ni lazima wana wa adamuw awepo ndipo chama kinapotimia.
 
Mpita Njia said:
Ninavyofahamu, chama hakiwezi kuwa chama bilawatu. Set of rules and regulations in themselves cam hardly be CHAMA

..an excellent observation indeed.

..wengi wetu tumechukuliwa msukule na hii dhana kwamba CCM iko kivyake, na viongozi wako kivyake.
 
cember 26, 2008
CCM: Ni chama cha Mapinduzi?

Sielewi kwa nini watu wanaamini kuwa CCM ni chama cha mapinduzi. Sijawahi kuelewa na bado sielewi kwa nini. Dhana ya mapinduzi ilielezwa vizuri na TANU, katika "Azimio la Arusha," "Mwongozo," na maandishi, hotuba na mahojiano mbali mbali ya Mwalimu Nyerere. Matokeo ya yote hayo ni kuwa Watanzania tulifahamu vizuri na kukubali dhana na maana ya mapinduzi katika nchi yetu. Yeyote ambaye hajasoma maandishi hayo, au kusikiliza hotuba hizo, ningemshauri afanye hivyo, ili aweze kufahamu msingi wa ujumbe wangu.

CCM ilipoanza, ilijinadi kuwa ni chama cha mapinduzi. Lakini baada ya muda si mrefu, mwelekeo wake ulijionyesha kuwa si wa mapinduzi. Badala ya kuendeleza fikra na mwelekeo wa "Azimio la Arusha," "Mwongozo" na mengine yote niliyoyataja hapo juu, CCM ilitoa "Azimio la Zanzibar." Ingawa CCM haikutoa fursa iliyostahili kwa wananchi kuliangalia na kulijadili "Azimio la Zanzibar," habari zilizojitokeza ni kuwa Azimio hili lilikiuka yale yaliyokuwemo katika "Azimio la Arusha." Mwalimu Nyerere alilishutumu "Azimilo la Zanzibar" kwa msingi huo.

Kitu kimoja kilichokuja kufahamika wazi ni kuwa "Azimio la Zanzibar" lilibadilisha masharti ya uongozi yaliyokuwemo katika "Azimio la Arusha" na "Mwongozo." Kwa mfano, "Azimio la Zanzibar" liliondoa miiko ya uongozi iliyokuwepo.

Baada ya CCM kuvunja misingi ya mapinduzi, kilichofuatia ni kuimarika kwa ubepari, matabaka, na ufisadi. Chini ya himaya ya CCM, "Azimio la Arusha" halisikiki, "Mwongozo" hausikiki, wala maandishi na hotuba zingine zilizofafanua maana ya mapinduzi hazisikiki. Inaonekana kuwa CCM ilikusudia tangu mwanzo kuwafanya watu wasahau hayo yote, ili iendelee na sera za kujenga ukoloni mamboleo nchini mwetu.

Inakuwaje basi CCM ijiite chama cha mapinduzi wakati inahujumu mapinduzi? Inakuwaje Watanzania hawahoji jambo hilo? Elimu ni ufunguo wa maisha; bila elimu kuna hatari ya kurubuniwa na kuburuzwa kama vipofu.

Posted by Mbele
 
Lyunyungu,
Hiki kingefaa kiitwe Reactionary Party. Chama kilichokiuka mapinduzi.
 
Kwa mtazamo wangu, CCM ni chama cha mapinduzi. Jambo la kujiuliza, ni mapinduzi ya namna gani na kwa faida ya nani? Tumeona watu/vyama vingi vikitumia rhetoric za kisiasa ambazo kiutekelezaji zinakwenda kinyume cha dhana ya hizo rhetoric k.m. democracy etc. etc.
 
inatemea una maana gani unaposema "mapinduzi." Kunamapinduzi ya kuvuruga nchi ikose mwekeleo. mapinduzi ya kubadili mwelekea wa nchi kurudi kwenye genesis, na mapinduzi ya kugeuze mweleleo wa nchi kwenda kwenye mafanikio.
 
What's in a name? Who remembers what NCCR stood for? What mageuzi is there in NCCR –Mageuzi? Chama Cha Demokrasia Makini would probably lead carefully and democratically, but the only problem is that they cannot find anybody to lead!

Does a party of socialism have to be socialist? Absolutely not! CCM is a perfect example of that. Who said a party had to be what it's called?

Was it Remi Ongala or Chongo that sang : Karibu kwetu CCM ee, Uimarishe hali ya wanyonge, Wafanyakazi viwandani, Na wale walioko mashmbani, Uweke uchumi wetu mikononi mwao" ? It would be a perfect scandal if it was Ongala, for ten years later the same artist sang: "Mrema Oo Mrema…." when Mrema tried to consign CCM to the dustbin of history.
 
Najjaribu kufikiria na kung'amua mantiki waliyokuwa nayo waasisi wa CCM....1977 TANU na ASP walipoungana kikazaliwa CHAMA CHA MAPINDUZI! Najiuliza, kwa nini kiwe cha Mapinduzi? Kwani nani alipinduliwa hapo 1977? Lakini kufuatana na mambo yalifuata, ni dhahiri MWANANCHI ndiye aliyepinduliwa. Slogans kama "Chama kushika Hatamu" na " CCM ina wenyewe" ni dhahiri kwamba mwananchi wa kawaida alikuwa hana lwake nchi hii. Akubali asikubali mambo yataamuliwa tu.
Kwa nini huyu aliyepinduliwa naye ajilkalie tu?! Baada ya kupinduliwa mwananchi alikandamizwa mpaka leo. Wahenga walishasema, kila refu lina mwisho. Mwannanchi, huu ndio mwisho wa CCM na ukandamizaji wake.

CHAGUA CHADEMA, USHINDE MAPINDUZI YA 1977.
 
Naona kuna haja ya mapinduzi kama chama chao kinavyosema,ila mapinduzi ya kifkra na mtazamo juu ya CCM ili uchaguzi ujao nao wakae chonjo uku wakiwa wanapiga Jalamba for 2015.
Unajua huwezi jua thamani ya kitu mpaka ukiwa haunacho,CCM hawaoni umuhimu wa kututumikia wananchi kwa kuwa hawajawai kutokuwa rulling party waone joto ya jiwe kama wenzao Malawi.One day yes
 
Maana halisi ya mapinduzi kwa mujibu wa waanzilishi wa chama cha mapinduzi ni harakati za kuleta mabadiliko ya haraka katika kuondoa ujinga, maradhi na umasikini miongoni mwa jamii ya watanzania. Kumbuka pia kauli; Tomeonewa kiasi cha kutosha. tumepuuzwa .... kwa hivo lengo lilikuwa jema kabisa yaani kuleta maendeleo ya haraka.Yaliyotokea baadaye ni tamaa za viongozi wachache wenye uchu na viongozi wabovu ambao wamesababisha nchi kudorora kwa kuendeleza ufisadi wa kila aina. Matokeo yake wananchi wameendelea kuteseka na mapinduzi kugeuka kuwa tabu kwa wengi na raha kwa wachache. kwa hivo sasa tunataka mapinduzi ya kweli yatakayowanufaisha walio wengi au wote. swala ni kina nani wako tayari na wamejibainisha wazi kuleta mapinduzi ya kweli.
 
walishinikizwa na wahafidhina wa asp wakina kambi ya karume waliotaka identity ya mapinduzi isipotee ktk historia ili chuki izidi kupandikizwa kizazi kwa kizazi! kina bilal ndio waliokua wamebakia naona wanamaliziwa, nyerere kwa vile alisoma akaona kua haman haja ya kuwapinga, akawapa walichotaka!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom