Swala la Mafisadi: CCM imemkabidhi nani Dola?

Arafat

JF-Expert Member
Nov 17, 2009
2,581
758
CCM imeibuka na Msemo mpya 'Kijivua Gamba!'

Kila mwanchama wa CCM anaimba huo wimbo hadi Rais ambaye ndie M/kiti wa CCM pia anaimba huo wimbo, chorus inasema 'tumewapa siku 90 Mafisadi wajiondoe katika Chama la sivyo tutawatimuwa' Mwimbishaji ni Nape, sauti ya nne anaimba Mkama, 'CCM imezaliwa Upyaaaa!'

Kweli sikio la kufa halisikii dawa, nani aliyewaambia CCM kuwa sisi bado ni Wadanganyika! Hivi CCM haijui kusoma alama za nyakati na kujua kuwa Watanzania wa leo sio wa jana! Eti kwa kuwa Mwinyi alikuwa Rais kwa kugombea na giza hivyo CCM bado inaota ndoto za aina hiyo!

Chama kilichoshika Dola kina lalama, nani atawakamata Mafisadi na wauza madawa ya kulevya kama CCM na Kikwete wote wanawaomba Mafisadi kujitoa ndani ya CCM, 'Wanawaomba!' maajabu kama siyo kiini macho.

Wezi wa EPA pia waliombwa kurudisha fedha na kuwa waliorudisha hakufikishwa mahakamani! Majina ya Wauza madawa ya kulevya Kikwete ameyalali! Chadema iliposema kuna list ya Mafisadi kumi na moja Kikwete na CCM walipinga kwa sauti moja leo Kikwete na CCM wote kwa sauti moja wanapita na kuwaomba Mafisadi waondoke ndani ya CCM, kumbe ukiwa Fisadi huwezi kukamatwa? Mahakama na Jela hutoshi humo!

Hivi kwanini Polisi wanawaonea Raia wasio na hatia na kuwabambikiza kesi za uongo wakati kuna watu wanajulikana hadi na Rais kuwa ni wahujumu uchumi wa Taifa hili lakini hawachukuliwi hatua yoyote? Kama Kikwete na CCM haiwezi kuwafikisha Mahakamani Mafisadi nani ataweza? Dola anayo nani amsaidie kikwete kushugulikia Mafisadi! Hii inatofauti gani na ile ya kuwa Mafisadi hawakamatiki!

Kwanini Kikwete hasijiuzuru kama kuna watu anawaogopa na hawezi kuwashugulikia hata kama wakifanya kosa lolote lile! Hivi swala la kushughulikia Mafisadi ni Swala la Chama au serikali? Sawa, Nape anapiga kelele kuwaomba waondoke CCM, vipi Serikali ya kikwete mbona haichukui hatua yoyote? Polisi, PCCB na UWT hawana la kuwafanya hawa Mafisadi! Hivi hamna Sheria yeyote ya Tanzania waliovunja? Taarifa za weakleaks za kikwete Kumzua Hoseah kuwashughulikia Mafisadi itayeyuka vipi? Mtoto wa Mkulima anamuenzi vipi Sokoine katika eneo hili?

Je CCM wanadhani uchafu walionao ni huo wa Mafisadi 11 peke yake, ingawa wao wanasema watatu (3) tu!? Mbona Nape na kikwete hawatwambii hawa watatu wamefanya Ufisadi upi? Sasa tunahitaji Kila watakapo pita wataje majina ya hao Mafisadi wanaotakiwa kuondoka ndani ya CCM na pia wataje Ufisadi walioufanya kila mmoja na Ufisadi wake, la sivyo Tutaendelea kuwaona CCM kama mnafanya kiini macho.

Huu ni muda wa vitendo siyo maneno matupu.
 
Umenena vema mkuu.Kitendo cha kuwaomba hao wanaitwa mafisadi wajiondoe kwenye chama chao bila kuweka wazi ni namna gani wamehusika kwenye vitendo vya ufisadi ni kutudanganya!NAPE na timu yenu ebu tuelezeni hao watu ni ufisadi gani walioufanya,ni hasara kiasi gani waliolisababishia taifa na nini kitafuata baada ya kuwaondoa!Ama sivyo ni usanii mtupu...
 
Wanawaomba kw sababu wanajua wakijifanya kuwa push waondoka wakiwa annoyed ni siku ambayo " a bag of worm" itakuwa limefunguliwa CCM na tutajua every single detail ya CCM involvement katika deal hizo, so wanafikiri the only polite way of awaking a sleeping devil ni kuwaomba waondoke! Amini! amini nawaambieni CCM hii haina uwezo wa kuwafukuza watuhumia! haina maana sioni ni nani awezaye fanya hivyo!
 
Umeiweka vizuri sana. Hii inabidi mtu akuhonge ili usione kiinimacho wanacho tufanyia hawa CCM.
Ndio maana walichakachua matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita kwani walijua kuwa, CHADEMA ndio chama pekee kinachojua uhalifu wa CCM na ndio chama pekee chenye UWEZO wa kuwakamata na kuwashughulikia MAFISADI wote bila kuwaangalia usoni.
Swali: Kwani Serikali ndio nani?
Jibu: Serikali ni wanainchi wa Twanzania.
Solution: Tuige mifano ya Egypt, Libya pamoja na kutumia "The Facebook/JF-revolution" kuikomboa Inchi yetu.

Dola haiwezi kufanya kazi kwani imevalishwa joho la kijani (Chama Cha Magamba).

Nia tunayo, sababu tunayo, ushahidi tunao, na nguvu ya Umma ndio ngao yetu.
 
Vita ya panzi sherehe kwa kunguru wa Zanzibar. CCM inaendelea na matamko yasokuwa na mashiko ktk mazingira wa wenye njaa ambao wanajua ni nani kapora msosi wao.
Laiti wangeliomba akawepo PM mwenye nguvu ambaye angelisukuma hili gurudumu kwa upande wa serikali angalau watu waendelee kuwa na matumaini, like chairman like PM, wote wanaomba wakati wamerundikiwa madaraka na mamlaka ya kutosha kuwashughulikia hao mibaka uchumi. Lakini kwa kuwa kuna-conflict of interest yaani kachama kalishinda kutokana na hao mission boys hamna jinsi ya kujinwesha sumu hadharani.
Chakupendeza watz wamegundua mchawi wao
 
Umenena vema mkuu.Kitendo cha kuwaomba hao wanaitwa mafisadi wajiondoe kwenye chama chao bila kuweka wazi ni namna gani wamehusika kwenye vitendo vya ufisadi ni kutudanganya!NAPE na timu yenu ebu tuelezeni hao watu ni ufisadi gani walioufanya,ni hasara kiasi gani waliolisababishia taifa na nini kitafuata baada ya kuwaondoa!Ama sivyo ni usanii mtupu...

Ndio tunahitaji wawataje pia waseme wameshiriki ufisadi upi ikibidi waende mbali zaidi na kusema wakati wanafanya huo Ufisadi Serikali ilikuwa Likizo wapi! Nakama bado Serikali ipo likizo pia watwambie
 
Wanawaomba kw sababu wanajua wakijifanya kuwa push waondoka wakiwa annoyed ni siku ambayo " a bag of worm" itakuwa limefunguliwa CCM na tutajua every single detail ya CCM involvement katika deal hizo, so wanafikiri the only polite way of awaking a sleeping devil ni kuwaomba waondoke! Amini! amini nawaambieni CCM hii haina uwezo wa kuwafukuza watuhumia! haina maana sioni ni nani awezaye fanya hivyo!

Je ikiwa hawata ondoka kama wanavyowaomba nini hatima yake! Vipi Serikali Mbona hatuoni kama yenye inajua hili jambo la Ufisadi ambalo CCM wanazunguka kuliimba! (Ashakum si Matusi) au CCM ina nawa uso na maji waliyochambia wapinzani?
 
Back
Top Bottom