CCM imebobea, siyo rahisi kubadilika ghafla

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,077
CCM, kiasili ni chama cha waovu, hata kwa mtu binafsi ni vigumu sana, kuiacha asili yake. Hivyo tusitegemee ni rahisi CCM kuuacha uovu.

Ukisikia mafisadi, wapo CCM: Uthibitisho: marehemu Magufuli aliwahi kutamka kwa uwazi kuwa majizi na magisadi yapo CCM.

Ukisikia waabudu ushirikina, wapo CCM:

Uthibitisho: kuna mchawi/mganga wa kienyeji mmoja kule Kigoma alikuwa anatamba, tena mpaka kutaja majina ya viongozi wa CCM ambao huwa wanaenda kwake wakati wa uchaguzi ili waweze kupata madaraka.

Ukisikia wevi waliobobea katika wizi wa kura wapo CCM:
Uthibitisho: Nape aliwahi kutamba kwamba wakishindwa kupata kura, watafunga kwa goli la mkono, na Samia aliwahi kunena kuwa hata wananchi wakiwapigia wagombea wa upinzani, kura zao zitahesabiwa CCM. Bashiru naye alinena kwa uwazi kuwa CCM itatumia dola kubakia madarakani. Mara kadhaa mabox ya kura fake yamekamatwa wakati wa uchaguzi yakiwa na kura fake za wagombea wa CCM.

Ukiwatafuta wauaji kwaajili ya kutetea madaraka yao, wapo CCM:
Uthibitisho: Rais mstaafu Kikwete aliwahi kunena kuwa CCM hawaachiani hata glass ya maji mezani kwa kuogopa kuuana. Mtuhumiwa mkubwa wa shambulio la kukusudia kumwua Lisu, ni kiongozi wa CCM. Aliyepigwa marufuku kukanyaga ardhi ya Marekani kwa sababu ni muuaji, ni kiongozi wa CCM.

Hivi chama kilichojijenga kwenye uovu wa kiasi hiki, tunatarajia kitabadilika mara moja na kuanza kuuchukia uovu na kupenda matendo mema?

Siku za karibuni, baadhi ya viongozi wakuu wa CCM, Mwenyekiti wa CCM na Makamu Mwenyekiti, wametoa kauli ambazo zinaonekana siyo halisia, ukiangalia na uhalisia katika matendo. Rais, ambaye ni mwenyekiti wa CCM, amekuwa akisistiza haki. Makamu wa Mwenyekiti wa CCM, amesikika akisema kuwa uchaguzi wa mwaka huu na wa mwakani, utakuwa huru na wa haki. Cha ajabu, kwenye uchaguzi mdogo kule Zanzibar, CCM waliiba kura za mgombea wa ACT. Na ilipodhihirika, katika kujikosha, sijui kama ni kwa maamuzi binafsi ya mgombea au kwa kulazimishwa, ikabidi mgombea wa CCM aliyepewa ushindi kupitia wizi, ajiuzulu. Leo tena tunapata taarifa toka Mtwara kuwa msimamizi wa uchaguzi mdogo amekutwa na kura fake za mgombea wa CCM, na wananchi walipochachamaa, polisi wameamua kumlinda msimamizi huyo, na kiongozi wa ACT alipojaribu kuwahoji polisi sababu za kumlinda mhalifu, ameishia kukamatwa na polisi.

Je, matendo haya, yanatoa picha gani kwa uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu na uchaguzi mkuu wa mwakani? Hivi kweli tunaweza kujipumbaza na kuamini kutakuwa na uchaguzi, katika maana halisi ya uchaguzi?

Fikiria chama ambacho wazazi walikuwa wevi wa kura. Wakawaingiza watoto wao kupitia chipukizi na UVCCM, na huko kote ama wameshiriki au wamekuwa wakifundishwa namna ya kuiba kura, sahizi ndiyo viongozi, na kila waliposhinda uchaguzi walitegemea kura za wizi, unadhani ni rahisi leo hii watu hao katika kutaka kuupata uongozi, watakubali wategemee kura halali za wananchi?
 
CCM, kiasili ni chama cha waovu, hata kwa mtu binafsi ni vigumu sana, kuiacha asili yake. Hivyo tusitegemee ni rahisi CCM kuuacha uovu...
Then upande wa pili wanafua na kuwapatia wafuasi wao kama bidhaa mpya Lowassa & Sumaye na Nyalandu!
 
Wapinzani {Chadema} wameamua kushiriki chaguzi za 2024 & 2025 kwa maana ya heri kuibiwa kidogo, kuliko kuibiwa kikubwa kama ilivyokuwa 2020.

Nitashangaa sana kama wakiibiwa hicho kidogo watalalamika, kwasababu naamini hili ni jambo linalotarajiwa kabisa hata na wao wenyewe.
 
CHADEMA wauze sera na sio kulia lia tu kila kukicha.

Wananchi wakijua mna dhamira na mka waaminisha mna viongozi(sio susa susa fc) labda 2025 mkapata viti viwili vitatu.

Chagua kwa Umakini 2025
 
CHADEMA wauze sera na sio kulia lia tu kila kukicha.

Wananchi wakijua mna dhamira na mka waaminisha mna viongozi(sio susa susa fc) labda 2025 mkapata viti viwili vitatu.

Chagua kwa Umakini 2025

Uchaguzi Tanzania huwa ni kuigiza.

Rais Samia aliwahi kusutwa na dhamira yake, akaamua kusrma ukweli kuwa hata ukimpigia kura mgombea wa chama cha upinzani, kura hiyo inaenda kuhesabika CCM. Maana yake ni kwamba uichague CCM usiichague, wao ndio wanaoamua waibe kura ngapi za kumtangaza mshindi wa CCM.
 
Wapinzani {Chadema} wameamua kushiriki chaguzi za 2024 & 2025 kwa maana ya heri kuibiwa kidogo, kuliko kuibiwa kikubwa kama ilivyokuwa 2020.

Nitashangaa sana kama wakiibiwa hicho kidogo watalalamika, kwasababu naamini hili ni jambo linalotarajiwa kabisa hata na wao wenyewe.
yALIYOTOKEA uJIJI kIGOMA YANAWASUBIRI
 
CDM msihadaike,ongezeni nguvu na kasi ya Maandamano ya kudai KATIBA MPYA ILIYO BORA + Tume huru ya Uchaguzi...WATAACHIA tu
 
Tunawaita waheshimiwa, kwenye shughuli za kijamii na imani tunawatambua kwa upekee. Na hawasiti kukufunga kwa kuwachafua unapowasema vibaya.

Channel ya vichekesho huko mbinguni.
 
Katika nchi za afrika zilizobaki kuingia vita na Tanzania hipo sababu tu CCM wamejisahau sana.na hiyo siku tunakuja kukuta patupu.
Nilishawai kuleta Uzi huu ulifutwa fasta
 
Uchaguzi Tanzania huwa ni kuigiza.
...na kwa msingi huo CHADEMA nao wanafanya maigizo.
Rais Samia aliwahi kusutwa na dhamira yake, akaamua kusrma ukweli kuwa hata ukimpigia kura mgombea wa chama cha upinzani, kura hiyo inaenda kuhesabika CCM.
Hizo ni kauli za kisiasa tu na hazi zingatii uhalisia.
Maana yake ni kwamba uichague CCM usiichague, wao ndio wanaoamua waibe kura ngapi za kumtangaza mshindi wa CCM.
20yrs chini ya Uongozi wa Mbowe, kweli, bado tu ana ishiwa na mbinu? anashindwa na mbinu za CCM Really? au Ndio yale mnatuambia ya Mabere Marando?

...najua unafikiria kuniambia, 'wanatumia vyombo vya Usalama' kana kwamba hakuna watu waliomo humo wakiwa ni wana CHADEMA!
 
CDM msihadaike,ongezeni nguvu na kasi ya Maandamano ya kudai KATIBA MPYA ILIYO BORA + Tume huru ya Uchaguzi...WATAACHIA tu

Nguvu kubwa ingeelekezwa kwenye kampeni za kuzuia uchaguzi usifanyike bilayakatiba mpya na sheria za haki za kusimamia uchaguzi.
 
...na kwa msingi huo CHADEMA nao wanafanya maigizo.

Hizo ni kauli za kisiasa tu na hazi zingatii uhalisia.

20yrs chini ya Uongozi wa Mbowe, kweli, bado tu ana ishiwa na mbinu? anashindwa na mbinu za CCM Really? au Ndio yale mnatuambia ya Mabere Marando?

...najua unafikiria kuniambia, 'wanatumia vyombo vya Usalama' kana kwamba hakuna watu waliomo humo wakiwa ni wana CHADEMA!
CHADEMA hawafanyi maagizo kwenye uchaguzi bali wanashiriki uchaguzi ambao ni wa maigizo kutokana na lengo la waliouandaa.

Mbowe ni mtu mmoja, na hata wangekuwa ishirini, wao pekee yao hawawezi kukabiliana na waovu wenye nguvu za kidola.
 
CCM ni genge la kigaidi linalotumia mabavu ya vyombo vya dola kuendelea kutawala. Kuna mstari mdogo sana unaoitenganisha CCM na Bokoharam.
 
Back
Top Bottom