AmaniKatoshi
Senior Member
- Mar 31, 2009
- 158
- 14
Sitta amshukia Zitto na kukwepa kosa la mwaka juzi
Na Beatrice Bandawe
14th July 2009
Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Na Beatrice Bandawe
14th July 2009
Spika wa Bunge, Samuel Sitta.
Spika wa Bunge, Samuel Sitta, jana ametoa ufafanuzi kuhusu madai ya kutumia lugha ya kuudhi bungeni na kusema kwamba Bunge ni uwanja wa siasa za ushindani ambapo katika kutetea maslahi ya kiuwakilishi, migongano na mitazamo na hata ya lugha haiwezi kuepukwa.
"Mwanasiasa hasa kiongozi anatakiwa awe na ngozi ngumu inayohimili mikwaruzo ya maneno makali ya siasa bila kuchubuka kwa urahisi," alisema.
Spika alitoa ufafanuzi huo baada ya mara kadhaa katika mkutano huu na iliyopita ya Bunge, wabunge kusimama na kuomba mwongozo wa Spika kwa kumtaka Mbunge anayechangia afute kauli yake kwa kuhisi kuwa ni ya kuudhi na haistahili kuwa lugha ya kibunge.
Alisema ni jambo la kawaida katika mazingira ya pekee pale ambapo mjadala unapamba moto mzungumzaji anaweza akajikuta akitumia maneno makali.
"Waheshimiwa wabunge pamoja na waheshimiwa mawaziri ni binadamu na wanaweza kuwa na hisia kali katika mambo wanayojadili. Kwa hiyo, kutafsiri kanuni hii inayozuia "maneno ya kuudhi" kwa wigo mfinyu kuna hatari ya kuminya ule uhuru wa majadiliano uliopo katika ibara ya 100 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania."
Alisema katika mabunge mengi duniani kanuni za mijadala zinazuia matumizi ya lugha za kuudhi au kwa maneno mengine, lugha isiyo ya kibunge.
"Katika kanuni za Bunge letu, Kanuni ya 64 inaanisha mambo yasiyoruhusiwa bungeni katika mijadala. Miongoni mwa mambo yaisyoruhusiwa ni kutumia lugha ya kukudhi au inayodhalilisha watu wengine – kanuni ya 64(1) (g)," alisema.
Sitta alisema ukiwataka wabunge wazungumze bungeni mithilli ya mashahidi mahakamani, "utakuwa umeiondoa ladha yote ya mijadala bungeni."
Alisema katika mifano kadhaa katika mabunge mbalimbali duniani ambapo katika mazingira hayo, wabunge wamenukuliwa wakitoa maneno makali ambayo kwa tasfiri finyu mtu anaweza kuyaita ni ya kuudhi au hata ya matusi.
Alitoa mfano wa Bunge la New Zealand ambapo baadhi ya wabunge wa huko katika nyakati mbalimbali wamenukuliwa katika Hansard mwaka 1949 baadhi ya mawaziri walitajiwa kuwa ni sungura walioduwazwa na wasio na maamuzi ya kujitegemea na mwaka 1963 waziri alimwita Mbunge mwingine kuwa ni mwanamke katili na mwaka huo huo Mbunge mmoja alimwelezea Mbunge mwingine kuwa ni kama konokono aliyechoka akirejea kutoka kwenye mazishi.
Aidha, alitoa mfano katika "House of Commons" ya Waingereza ambapo mijadala inapopamba moto maneno makali hutumika, na kutoa mfano wa Mei 15, 1846, Benjamin Disraeli alimshambulia Waziri Mkuu Sir Robert Peel kwa kumwambia "Najua kwamba kwa miaka kati ya 30 na 40 mheshimiiwa ameishi kwa kutumia mawazo na akili za wenzake.
Maisha yake yote yamekuwa ni ya ubinafsishaji wa maoni ya wenzie. Ni mporaji wa akili za wenzake…Hakuna mwanasiasa ambaye amekuwa hodari zaidi kuliko huyu katika uhalifu wa wizi mkubwa wa ajenda za kisiasa."
Hata hivyo, Sitta alisema kwa mifano hiyo si nia yake kuwashawishi wabunge watumie aina hiyo au maneno mengine makali na yanayoweza kuumiza wengine.
Alisema Wenyeviti wa Bunge ni wasaidizi wa Spika na Naibu Spika katika shughuli za Bunge. Wanapokalia Kiti cha Spika na kuendesha vikao vya bunge wanafanya hivyo kwa niaba ya Spika na kwa wakati huo wanakuwa wanatekeleza mamlaka ya Spika na wanastahili heshima ile ile wanayopewa Spika na Naibu Spika.
Kwa mujibu wa Kanuni ya 67(2) Spika anaposimama wakati Mbunge anachangia, Mbunge anatakiwa kuketi mahali pake na Bunge litabaki kimya ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa anayokusudia kuitoa.
"Spika anawajibika kutilia nguvu kanuni za Bunge na anawezakumtaka Mbunge yeyote anayekiuka utaratibu ajirekebishe," alisema.
Alisema kanuni zimeweka wazi kuwa Mbunge yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika anaweza kuwasilisha sababu za kutoridhika kwake kwa Katibu wa Bunge ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika anaweza kuwasilisha sababu za kutoridhika kwake kwa Katibu wa Bunge ambaye atawasilisha malalamiko kwa Kamati ya Kanuni kupitia kwa Spika.
"Kwa kuzingatia misingi hiyo niliyoieleza, tarehe 24, Juni, 2009 Mheshimiwa Zitto hakuathiri kanuni yoyote kwa kutamka kwamba mheshimiiwa Fulani alijibu "ovyo ovyo".
Tatizo hapa ni kwamba Mheshimiwa Zitto aliendelea kuyakaidi mamlaka ya kiti kwa kauli. '"Kwa hilo, ninamwagiza amwombe radhi Mheshimiwa Mwenyekiti, Zubeir Ali Maulid humu bungeni," alisema.
Hata hivyo, wakati Spika akitoa ufafanuzi huo,Yahya Kassim Issa, alitaka mwongozo wa Spika na kusema Tanzania ina ustaarabu wake na kwamba Tanzania inaangaliwa na nchi nyingine "sasa kauli aliyoitoa Spika hatuoni tunavuka nje ya maadili yetu."
Spika alimjibu Mbunge huyo kuwa ameshatoa mwongozo na hafahamu mbunge huyo anataka mwongozo gani mwingine.
CHANZO: NIPASHE
Last edited: