Sitaki kutukanwa, nataka nishauriwe

umechemka mkuu kuongeza mke nisehemu ya tatiyo unalojijiongezea ushauri wangu kuliko uogenye nibora umuache kwanza huyo japo pia sikushauri umuache tafuta chanzo isije kua wewe nichanzo huyo

Ahsante kwa ushauri wako lakini mimisi wewe pengine tuna fikira tofauti. Kwangu kwenda mbele ni maendeleo na maendeleo lazima yawe na changamoto. Mimi si wa kukimbia changamoto nikishakujipima.
 
huyo wa pili umeshampata?ushamuonja?kama ushampata umeshaikurubia zinaa na kama ushamuonja basi umeshazini!na wazinifu unapajua mahali pao bila shaka!achana na mawazo hayo ndugu!si vibaya mkajifunza kwetu tunaooa mke mmoja!

Mbona hukuniuliza huyu wa mwanzo kama nilizini nae kwanza au vipi? Nimeamuwa ndowa kwa misingi ya dini yangu na nitaowa kwa misingi ya dini yangu!
 
usipotoshe watu mkuu!huwa mnaambiwa unaweza kuoa zaidi kama unauwezo wa kuwatunza!na je kuwatunza ni nini ktk dunia ya leo kama si pesa au uwezo zaidi kipesa?

Dunia hii unahitaji uwe na kiasi gani cha fedha ili useme kuwa una fedha na usiwe na matatizo yoyote?
 
Nataka kuongeza Mke wa Pili!

Mzeyaaaaaaaaa!!! Mbona umeanza na kujihami, kama dini inaruhusu na unakipato cha kuwatosheleza wote, ongeza ongeza tu mkuu, hamna mtu anayeweza kukushauri kuhusu hili, kama umeshaamua hata ukiambiwa si vizuri hautakubali hata kama dini hairuhusu ndo ungejidai kuiita nyumba ndogo. Au ungebadili kichwa cha habari kisomeke hivi: NAOMBENI MCHANG WA MAWAZO, NATAKA KUONGEZA MKE WA PILI. Hapo ungepata mawazo bomba kibao!!
 
Mzeyaaaaaaaaa!!! Mbona umeanza na kujihami, kama dini inaruhusu na unakipato cha kuwatosheleza wote, ongeza ongeza tu mkuu, hamna mtu anayeweza kukushauri kuhusu hili, kama umeshaamua hata ukiambiwa si vizuri hautakubali hata kama dini hairuhusu ndo ungejidai kuiita nyumba ndogo. Au ungebadili kichwa cha habari kisomeke hivi: NAOMBENI MCHANG WA MAWAZO, NATAKA KUONGEZA MKE WA PILI. Hapo ungepata mawazo bomba kibao!!
Nataka kuongeza lakini bado sijafanya hivyo! Ushauri mara nyingi si lazima uwe kunikatalia lakini unaweza pia kunipa hadhari iwapo ushajihisi kuwa huna ushauri utakaoweza kunifanya nibadili uamuzi wangu! Au unaweza kunishauri mchumba iwapo unae unaefikiri anaweza kunifaa!

Bado nataka ushauri, sijaowa bado na wala sijaanika ninaetaka kumuowa!
 
Back
Top Bottom