Fukua
JF-Expert Member
- Jun 1, 2022
- 546
- 479
Salaam wanajukwaa.
Sio Siri miongoni mwa Mambo muhimu kabisa niliyokuwa nawaombea viongozi wetu wa Chama na serikali kuyatafakari na kuchukua hatua NI Kama yafuatayo.
Moja, maridhiano ya kitaifa.
Mbili, kuufufua mchakato wa katiba mpya.
Tatu,tume huru ya uchaguzi japo itapatikana ndani ya katiba mpya.
Watanzania wote NI mashahidi Mambo mengi mabaya Kama mateso, mauaji,vipigo na vifungo vya kisiasa kwa wapinzani wa CCM kama lissu,azori,been saa8, n.k. hata wale waliokuwa ndani ya ccm lakini wakawa wapinzani wa JPM Kama wakina Nape, Membe, makamba's, kinana n.k shida, fedheha na tanuru la Moto walilopitishwa na mwendazake hayo yote yalitosha kuwa na maridhiano ya kitaifa kwani NI kweli watu wengi Sana waliumizwa.
Tusingeweza kusonga mbele Kama taifa wakati wananchi wengi wanalia kwa maumivu makali.
Maridhiano yataliponya taifa, yatarejesha matumaini ya wananchi kwa serikali na Chama,yataleta umoja wa kitaifa na hatimaye maendeleo ya haraka kwani waleta maendeleo NI wananchi ambao ni lazima wawe na upendo,kuthaminiana umoja,kuaminiana,kushirikiana, kuheshimiana na kupendana.
Katiba mpya NI mwarobaini wa matatizo mengi Sana ya wananchi, utatuepusha na kujirudia kwa hatari kubwa ya ubabe Kama wa mwendazake.
Itasaidia kuwa na utaratibu unaoendana na Aina ya siasa tuliyonayo tanzania na dunia kwa kipindi na wakati huu wa utandawazi.
Itasaidia kuwa na umoja wa kweli na itasaidia kuleta uwajibikaji wa viongozi.
Tume huru NI muhimu Sana hasa kwa kipindi hichi ambapo tunaelekea kwenye uchaguzi 2025.kama katiba mpya itakuwa bado kwani ninaamini chakato utachukua mda kidogo.
Ninashukuru Mungu na viongozi wa Chama cha mapinduzi na serikali kwa kuyatafakari na kuyasimamia Mambo haya ambayo NI muhimu Sana kwa taifa letu kwa wakati huu.
Pia ninavishukuru vyama vya upinzani hasa chadema chini ya kiongozi wao Mh. MBOWE kwa kuishauri serikali na CCM pia kusisitiza umuhimu wa agenda hizi kwa jasho na damu Tena kwa kutumia njia za kistaarabu kabisa.
Tunajenga taifa moja tusiparuane, na tusiumizane vyama vyetu vinaweza kupita au kufa lakini TANZANIA haitopita milele.
Nimeandika mafaKama mtanzania huru niliye acha ukada wangu pembeni kabisa.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki watanzania, Mungu mbariki raisi wetu Mama Samia, Mungu ibariki CCM na Mungu vibariki vyama vya upinzani.
Ameeeen!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Sio Siri miongoni mwa Mambo muhimu kabisa niliyokuwa nawaombea viongozi wetu wa Chama na serikali kuyatafakari na kuchukua hatua NI Kama yafuatayo.
Moja, maridhiano ya kitaifa.
Mbili, kuufufua mchakato wa katiba mpya.
Tatu,tume huru ya uchaguzi japo itapatikana ndani ya katiba mpya.
Watanzania wote NI mashahidi Mambo mengi mabaya Kama mateso, mauaji,vipigo na vifungo vya kisiasa kwa wapinzani wa CCM kama lissu,azori,been saa8, n.k. hata wale waliokuwa ndani ya ccm lakini wakawa wapinzani wa JPM Kama wakina Nape, Membe, makamba's, kinana n.k shida, fedheha na tanuru la Moto walilopitishwa na mwendazake hayo yote yalitosha kuwa na maridhiano ya kitaifa kwani NI kweli watu wengi Sana waliumizwa.
Tusingeweza kusonga mbele Kama taifa wakati wananchi wengi wanalia kwa maumivu makali.
Maridhiano yataliponya taifa, yatarejesha matumaini ya wananchi kwa serikali na Chama,yataleta umoja wa kitaifa na hatimaye maendeleo ya haraka kwani waleta maendeleo NI wananchi ambao ni lazima wawe na upendo,kuthaminiana umoja,kuaminiana,kushirikiana, kuheshimiana na kupendana.
Katiba mpya NI mwarobaini wa matatizo mengi Sana ya wananchi, utatuepusha na kujirudia kwa hatari kubwa ya ubabe Kama wa mwendazake.
Itasaidia kuwa na utaratibu unaoendana na Aina ya siasa tuliyonayo tanzania na dunia kwa kipindi na wakati huu wa utandawazi.
Itasaidia kuwa na umoja wa kweli na itasaidia kuleta uwajibikaji wa viongozi.
Tume huru NI muhimu Sana hasa kwa kipindi hichi ambapo tunaelekea kwenye uchaguzi 2025.kama katiba mpya itakuwa bado kwani ninaamini chakato utachukua mda kidogo.
Ninashukuru Mungu na viongozi wa Chama cha mapinduzi na serikali kwa kuyatafakari na kuyasimamia Mambo haya ambayo NI muhimu Sana kwa taifa letu kwa wakati huu.
Pia ninavishukuru vyama vya upinzani hasa chadema chini ya kiongozi wao Mh. MBOWE kwa kuishauri serikali na CCM pia kusisitiza umuhimu wa agenda hizi kwa jasho na damu Tena kwa kutumia njia za kistaarabu kabisa.
Tunajenga taifa moja tusiparuane, na tusiumizane vyama vyetu vinaweza kupita au kufa lakini TANZANIA haitopita milele.
Nimeandika mafaKama mtanzania huru niliye acha ukada wangu pembeni kabisa.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu wabariki watanzania, Mungu mbariki raisi wetu Mama Samia, Mungu ibariki CCM na Mungu vibariki vyama vya upinzani.
Ameeeen!!
Sent using Jamii Forums mobile app