Tuko nao kitambo tunaruka nao tu.😆watu man moyo nimeona huu uzi untrend miaka yote nkasema niuchungulie nakuta sehemu ya 700.. watu mnajua kufatilia
HatariiiiNILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MRUNZI: SINGANOJR
Mono no aware
SEHEMU YA 694.
Ilikuwa ni kama Roma alivyokuwa ametegemea , kwani ile anafika katika makazi ya Mzee Sharif yaliopo Bagamoyo aliweza kukuta vurugu zilizokuwa zikiendelea.
“Ndio mmeanza vurugu?”Aliongea Roma mara baada ya kutua kwenye bustani ndani ya jumba hilo ambalo lilitumiwa kama makazi ya muda ya Mzee Sharif mara baada ya yale ya Kilimanjaro kuharibiwa.
Dakika hio watu waliokuwa hapo ndani waliweza kusikia sauti wanayoifahamu na mara baada ya kugeuka waliweza kumuona Jini Imrah na Maimuna na palepale wote kwa hofu walipiga magoti chini kusujudu.
Walikuwa wakijua Maimuna na jini Imrah walishakufa na wengine wote kutokana na miili yao kutoweza kupatikana , lakini ajabu sasa muda huo wamerudi wakiwa hai hivyo kila mmoja alishikwa na woga na yale mawazo ya kutaka kupata madaraka yalikufa palepale.
Lazima kuwa na hofu kwani walikuwa ni binadamu tu huku wao wakiwa ni majini wenye nguvu.
Roma aliishia kujichekea ndani kwa ndani na kujiambia kumbe kujifanyisha mtu mwingine kuna raha yake , kama sio kuwa na mipango mingine alijiambia angekaa hapo hapo kwa muda kwanza kujionea.
Dakika ileile aliwaambia kwamba yeye kama jini Imrah amemuokoa Maimuna kutoka kwenye mikono ya Roma Ramoni na kwanzia siku hio angekuwa kiongozi wa ukoo pamoja na kuongoza imani yote ya kikafara.
Maimuna ambaye ni Tannya aliweka msimamo wake juu ya mpango wa kupangua familia hio ki uongozi kutoka ngazi ya chini mpaka ya juu.
Tannya alihitajika kufanya hivyo ili kuhakikisha anaingiza watu wake ambao wangeweza kurithi nafasi za wafuasi watiifu na kuweza kupata taarifa zote juu ya familia hio kama misheni aliopewa na mfalme Pluto.
Roma mara baada ya kumalizana na swala hilo palepale aliondoka na kurudi kwenye muonekanno wake wa kawaida na moja kwa moja akafanya safari ya kwenda Los Angeles-Marekani.
Hakuwa ameonana na Christen kwa muda mrefu kidogo na kwasababu alikuwa anataka kumuuliza kuhusu kilichotokea usiku hivyo aliona amtembelee.
Wakati anaingia Los Angeles ilikuwa ni giza bado na kwa kutumia uwezo wake aliweza kugungua Christen alikuwa ndani ya jumba lake.
Kufumba na kufumbua Roma alikuja kutua kwenye balkoni katika floor ya pili ndani ya nyumba ya Christen , alikumbuka mara ya mwisho alivyofika kwenye nyumba hio aliweza kupata huduma kutoka kwa kijakazi wa Christen na alijiuliza kama bado yupo.
Upande wa Christen na yeye alikuwa ashahisia ujio wake na alifungua mlango na kutoka nje akiwa katika mavazi ya kulalia na kumfanya kuzidi kuonekana mrembo.s
“Hades nilijua utanipigia simu mchana , naona umesubiri mpaka giza lilipoingia na kuja kunifanyia surprise”Aliongea
“Nimechelewa , nilikuwa bize na mambo mengine..”Aliongea Roma na palepale alisogeza kiti karibu na kuketi.
“Kama ulitegemea ningekutafuta basi itakuwa sio mimi tu ninaepatwa na hizi hisia, hebu niambie ni nini kinaendelea , kwanini nguvu ya uungu ndani yangu ni kama imeongezeka , ninaweza kuhisia hata saivi bado inaongezeka taratibu sana”
“Such spoilsport , I’ m wearing this in front of you and yet you are talking about things like this…”Aliongea na paleplale alimsogelea Roma na kumkalia huku akimshikilia shingo kimadaha.
Roma alichoweza kuhisi ni marashi kutoka kwa mwanamke huyo , huku kidevu cha mrembo huyo kikiwa kimegusana na kifua chake.
Uzuri wa Christen pamoja na u’superstar’ ni sifa ambazo mbele ya mwanaume rijali hawezi kuepuka mtego wake lakini kwa bahati mbaya au nzuri Roma alikuwa na uwezo wa kujizuia.
“Kwa staili hii sidhani kama upo tayari kujibu maswali yangu, Christen unanifanya nione kuna kitu muhimu sana mnanificha”Aliongea Roma lakini Christen alikuwa akijisugua sugua mapajani ili kuamsha mhogo wa Roma.
Mara baada ya kuhisi ugumu ukiongezeka ndani ya suruali yake alimwinnamia na kumnong’oneza.
“Babe unaonaje tukifanya hivi , kama utakidhi haja zangu nitakuambia ukweli wote, nadhani unajua vizuri sijawahi kufanywa nikiwa na huu mwili na itabana vizuri tu”
Maneno ya Christen yalimfanya mapigo yake ya moyo kwenda kasi na kumlaani kwa kuongea maneno hayo ya kiuchokozi bila aibu na kuamsha ukichaa wake.
Kama ni mwanaume mwingine ambaye upo katika nafasi ya Roma angeishikilia fursa hio kwa mikono yote, kulikuwana wanaume wengi sana ambao wanajaribu kutoka kimapenzi na mwanamke huyo lakini wote wanaambulia kupigwa vibuti.
“Najua kuna wanaume kibao ambao wanakutaka na wanaweza kukidhi matamanio yako”
“Nilishakuwa na wanaume tofauti tofauti kila nilipobadilisha mwili lakini tokea nibadili huu mwili wewe ndio mwanaume ambaye umekidhi vigezo vangu”
“Asante kwa kunisifia lakini naomba niwe mkorofi kukukataa, unaonaje ukiniambia ukweli na kisha nikakidhi matamanio yako zaidi ya mara mbili”
Roma alishajua kama angetaka kuanzisha mahusiano na Christen jambo hilo lingetokea miaka mingi iliopita , isitoshe sio watu ambao walikuwa wakifungwa na sheria za kiimani.
Wote wana roho ya uungu ndani yao hivyo miili wanayotumia ni kama nyumba tu ya kutumia kwa muda tu.
Kilichomfanya Roma kutotaka kujihusisha kimahusiano na Chriten ni kutokana na mrembo huyo kuwa na hisitoria na Hades wa Zamani licha ya kwamba hakuwa akijua maelezo yote juu ya mahusiano yao.
Uwezo wao wa kuhamisha ‘ Consciousnes’ zao kutoka kwenye mwili mmoja kwenda mwingine ilitegemeana na nguvu ya ki uuungu ndani yao, Hades wa Zamani alikuwa ameshapoteza nusu yake mara baada ya kumrithisha Roma hivyo asilimia za kujivika mwili mwingine aliamini ingekuwa ngumu.
“Hades unachukiza mno , yaani najilengesha kwako lakini bato tu unanikataa , hivi nakosa nini ambacho mkeo na wapenzi wako wanacho mimi sina?”Aliongea huku akijifanyisha amekasirika.
“Aphrodite acha mambo yako bwana , sisi ni mrafiki na nakujua vizuri hivyo acha kuficha ukweli na niambie nini kinaendelea”Aliongea Roma huku muonekano wake ukiwa na hali ya usiriasi ndani yake.
Christen alitoa pumzi nyingi na kuzishusha na kisha alisimama na kumzodoa kwenye paji la uso kama vile hajaridhishwa na maneno yake na palepale alisimama kwenye uzio wa balkoni na kuangalia mataa ya jiji la Biverly hills.
“Ni moyo wa Gaia , Athena ameshaufufua”Aliongea bila ya kugeuka.
Roma alikuwa ashaotea muda mrefu, hivyo hakushangaa sana lakini bado hakuwa akijua moyo huo unahusu nini na athari zake ni zipi.
“Kufufuka kwa huo moyo inamaanisha kwamba mtaweza kurudiwa na nguvu zenu si ndio? , nakumbuka kule Korea Kusini Stern , Alice na Athena walivyokuwa wakiongea walitaja kuhusu huu moyo wa Gaia na kusema utaleta matokeo makubwa kwa dunia yote , nakumbuka pia ni kama walikuwa wakibishana na kusema ni kitu ambacho kitaharibu ulimwengu lakini wakati ule hawakutaka kunipa maelezo kabisa nnilipowauliza , kwanini wewe usiniambie kila kitu”
“Sidhani kama kuna maelezo yaliobakia ambayo ninaweza kukupatia , hata wewe mweneyewe umeweza kuhisia kufufuka kwa moyo wa Gaia, hivyo ni kweli nguvu zetu zitarudi taratibu taratibu na Athena mpango wake ni kufufua ndugu zetu walioptea na tayari ashafanikisha hatua ya kwanza”
“Ana mpango gani au anataka kuua binadamu kama alivyofanya miaka elfu ishirini iliopita mara baada ya kufeli kwa mpango wenu wa kutawala dunia?”
“Kusema ukweli sijui chochote , Athena hatabiriki na isitoshe hata kama tunajua anachopanga kufanya hatuna huo uwezo wa kumzuia”Aliongea na kumfanya Roma kutulia kimya.
Ukweli ni kwamba Athena uwezo wake ulikuwa wa juu kabisa na Roma alijua hata kama nguvu zake za kijini zimerudi inawezekana bado asifanikishe kushindana nae , isitoshe kufufuka kwa Moyo wa Gaia inamaanisha kwamba na nguvu zake pia zinaongezeka
Dakika ileile Roma alitaka kuuliza swali lingine simu yake iliita na alipotoa na kuangalia anaepiga ni babu yake Afande Kweka na alipokea palepale.
“Wewe mtukutu hebu rudi Tanzania haraka na tukutane Dodoma”Sauti ya kibabe ilisikika.
“Nini kimetokea Mzee?”Aliuliza Roma kwa msahngao.
“Haha… unafikiri kwa ulichokifanya utaachwa kirahisi , umemuweka baba yako katika wakati mgumu na Master namba Moja anataka kukutana na wewe kupitia yeye’Aliongea na kumfanya Roma kushangaa.
“Unamaanisha nini Master Namba moja anataka kukutana na mimi kupitia yeye?”
“Rudi kwanza na tukutane Dodoma ndio tutaongea vizuri”Aliongea na palepale simu ilikatwa.
“Christen natakiwa kurudi?”
“Inaonekana upo matatizoni?,GoodLuck Hades”
“I guess we’ll have to go with the flow for Gaia’s Heart , I know you didn’t tell me everything but I hope no matter what happened in the future we‘ll still be friends”Aliongea Roma akimwamia Christen kwamba anajua hajamweleza kila kitu lakini haijalishi ni nini kitatokea baadae bali wataendelea kuwa marafiki.
Christen alitaka kuongea neno lakini aliingiwa na uzito kwenye midomo yake na kuishia kutoa tabasamu la kuashiria maana na palepale Roma alipotea mbele yake.
Aliishia kuangalia upande ambao Roma amepotelea na kuishia kuvuta pumzi nyingi.
“Roma wewe ni msahaulifu sana nishakuonya mwanzo usije kumruhusu Athena kuupata moyo wa Gaia, eti marafiki wewe ni mjinga sitaku kuwa rafiki yako mimi , nataka urudiwe na ufahamu wako wote halisi ya ki’uungu na tukutane kwa mara nyingine , nikwambie maneno nilioshindwa kukuambia siku zote, Nakusubiri Hades”Aliwaza Chriten.
******
Wakati Marekani ikiwa ni usiku Tanzania ilikuwa ni alfajiri na Rufi bado alikuwa kwenye usingizi mzito sana.
Dakika hio Bi Wema alikuwa tayari amekwisha amka na kuingia katika chumba cha binti yake na kuishia kutingisha kichwa kwa kusikitika mara baada ya kuona vifaa vya tarakishi ambavyo vimezagaa ndani ya chumba chake bila mpangilio , tarakishi bado ilikuwa inawaka na namba namba ambazo hakuwa akizielewa zilionekana.
“Sijui kwanini anapenda mambo kama haya kama vile sio mwanamke , lakini nadhani ni vizuri kuwa na hobi inayomfanya kuwa bize kwani hana uwezo wa kuvuna nishati za mbingu na ardhi kama wenzake”Alijiwazia Bi Wema kwenye kichwa chake na kisha alisogea na kwenda kukaa kitandani na kuanza kumtingisha Rufi.
“Rufi amka kumekucha , tunapaswa kujiandaa mapema tuanze safari”Aliongea Bi Wema.
“Mama nataka nilale kidogo, nimechoka”Aliongea Rufi kivivu na kumfanya Bi Wema kumwangalia binti yake na kutoa tabasamu ,kuna muda alijiambia ni kama miujiza kumwamsha binti yake kama hivyo.
“Rufi mwanangu tutachelewa kufika jamani”Aliongea Bi Wema.
Siku hio Bi Wema alipaswa kwenda kumtembelea mdogo wake huko Pangani mkoani Tanga.
Mwanzoni Bi Wema alijua hakuwa na ndugu kabisa lakini miezi michache aliweza kutafutwa na mwanaume aliejitambulisha kama mdogo wake , yaani mtoto wa baba yake kwa mama mwingine.
Bi Wema mara baada ya kupata taarifa hio alifurahi sana kwani ilimfanya sasa kujua alikuwa na ndugu.
Sasa mara baada ya kurudi kwa Rufi alitaka kwenda kumtembelea mdogo wake kwa mara ya kwanza na siku ambao walipanga kwenda huko ni siku hio asubuhi asubuhi ili kuwahi kufika ndio maana alikuwa akimwamsha alfajiri kwa ajili ya kujiandaa na kuanza safari.
Dakika hio wakati Bi Wema akimuamsha Rufi upande wa balkoni alikuwa amesimama mwanaume mtanashati mno alievalia joho la rangi nyeupe akiangalia ndani ya chumba cha Rufi na macho yaliojaa kejeli.
Licha ya kwamba dirisha kutokea Balkonni lilikuwa na pazia lakini alikuwa na uwezo wa kuona kila kitu kinachoendelea ndani.
Na wakati hio ndio ambao Bi Wema alikuwa akimuamsha Rufi kwa ajili ya kujiandaa kuanza safari.
SEHEMU YA 695.
Bi Wema mwili wake ulihisi kumsisimka ajabu na ilikua ni kama amehisi hatari na kwa haraka alimuacha Rufi aliekuwa akijifikicha macho na kukimbilia upande wa dirisha na kusukuma pazia na hapo ndipo alipojikuta ni kama vile yupo ndotoni mara baada ya kukutana na sura ambayo ilikuwa ikimwangalia kwa tabasabu , manusura apige yowe lakini kwa hali ambayo hakuelewa sauti ilishindwa kumtoka kabisa.
Rufi ambaye alikuwa bado na hali ya usingizi alijikuta akigeuza macho kumwangalia mama yake na hapo ndipo alipoingiwa na ubaridi mara baada ya kuona sura anayoifahamu.
Alikuwa ni jini Lahani kaka yake na XiaoXiao ,alikuwa na muonekano ambao haukuashiria amani na ulimfanya Rufi kuingia na woga wa hatari mno
Wakati Rufi akiwa katika hali ya mshangao upande wa Lahani alisogea upande wa mlango wa Aluminium wa na kuslide mlango kwenda kulia na kufanya upepo kuingia ndani pamoja marashi makali.
Dakika ileile ni kama sasa Rufi akili ilimkaa vizuri na aliruka kutoka kitandani na kumsogelea mama yake kwa hofu.
“Mama , ondoka , ondoka haraka, kimbia kwenda nje”Aliongea Rufi akijaribu kumsukuma mama yake kutoka ndani ya chumba chake.
Bi Wema dakika hio hio alijua wapo katika hatari na aliishia kumkumbatia Rufi huku akimwangalia yule mwanaume mwenye uso wa kuvutia akingia ndani bila wasiwasi.
“Rufi unamaanisha nini , huyu mwanaume ni nani.. Rufi acha kunisukuma jamani”Aliongea Bi Wema akijaribu kushindana na Rufi
“Haha..Kwahio huyu ndio mama yako mzazi , mbona hamfanani hata kidogo”Aliongea Lahani huku akiwa amesimama akimwangalia Rufi kwa kejeli anavyohangaika kumsukumia nje mama yake.
Dakika hio hio vivuli vilitua nje ya Balkoni na Rufi mara baada ya kugeuza macho aliweza kuwajua wote , wa kwanza alikuwa ni Xiao Xiao na wa pili ni mwanaume aliekuwa akimjua vizuri alikuwa ni Mlinzi wa Lahani yaani Mzee Lao.
Wote hao walikuwa ni majini , Lahani alikuwa jini na huyo mzee alikuwa jini vilevile kasoro XiaoXiao ambaye alikuwa ni nusu jini kama ilivyokuwa yeye.
Sasa kitendo cha Rufi kumuona XiaoXiao alijua kabisa yeye ndio amemuuza na alimpiga jicho la hasira.
“Kumbe ni wewe ulieniuza , nilikuaini na hata nikamuomba mpenzi wangu kukuacha hai lakini haya ndio malipo yake>”Aliongea Rufi kwa hasira.
Ukweli XiaoXiao hakuhusika kabisa na alikuwa ameletwa hapo nje ya ridhaa yake na alionyesha kuwa na wasiwasi mno lakini kutokana na kauli ya Rufi alishindwa hata kujua namna ya kujitetea wakati huo , aliishia kutingisha kichwa chake akiwa na machozi kumuashiria Rufi kwamba hahusiki.
Upande wa jini Lahani palepale sura yake ilianza kubadilika na macho yake kubadili rangi na kusababisha upepo kuongezeka na kupeperusha vitu ambavyo vililkuwa vyepesi ndani ya chumba hicho.
“Wewe mal**ya umepata wapi ujasiri wa kunisaliti , sio tu kwamba ulitoroka ulimwengu wa majini lakini pia unamwita binadamu mpenzi mbele yangu , nadhani utakuwa umesahau jinsi ulivokuwa wa hadhi ya chini licha ya familia yako kukuuza kwetu”
Rufi aliishia kutetemeka , mpaka hapo alijua hakuna namna anaweza kuokoka , Roma hakuwa maeneo ya karibu na haelewi kinachoendelea na hata kama kulikuwa na binadamu mwenye uwezo wa kijini karibu asingeweza kushindana na huyo mzee alieambatana na Lahani.
Tena alishukuru Rose na Magdalena hawakuwepo katika maeneo hayo , pengine wangeuliwa..
Lahani ndio mrithi mtarajiwa wa ukoo baada ya baba yake na kutokana na cheo chake alikuwa akilindwa na jini mwenye nguvu sana na ndio huyo mzee ambaye alikuwa ameambatana nae.
“Siwezi kukataa kama umekuja kunichukua na kunirudisha , lakini naomba tafadhali umuache mama yangu”Aliongea Rufi na maneno yale yalimuumiza mno Bi Wema.
“Hapana .. hakuna wa kumchukua binti yangu, imenichukua miaka mingi sana kukutana nae siwezi kuruhusu mumchukue tena , labda muanze kuniua mmi”Aliongea Bi Wema huku akimkingia Rufi kwa mbele.
Bi Wema hakuwa mjinga kutokana na historia ya maisha ya Rufi alikuwa akijua waliokuwa mbele yake ni majini na ndio hao ambao walikuwa wakimsulubu binti yake kabla ya kutoroka.
“Haha.. hahaha…., kama nilivyotarajia , binadamu ni viumbe wajinga sana , wewe ni nani wa kunizuia mimi , sio mbaya hata hivyo nitaanza na wewe , nadhani itakuwa njia rahisi zaidi ya kuanza kisasi changu hapahapa”Alingea Lahan kwa hasira na Rufi alijiaribu kumshikilia kwa nguvu Bi Wema lakini chumba kilikuwa kishaanza kukumbwa na dhoruba ya upepo huku kelele kama vile ni sauti ya watu waliokufa ikisikika.
“Tafadhari kaka usmuue ni ..”XiaoXiao alitaka kumtetea Bi Wema ili kuzuia asimuue.
“Kaa kimya wewe , huna mamlaka ya kuongea mbele yangu , utapatiwa adhabu yako tukisharudi kwa kuficha ukweli kwa baba na mimi”Aliongea kwa hasira na kumfanya Xiao kuufyata.
“Master , mkuu wa ukoo ametuambia tumkamate Rufi tu na kurudi nae kimya kimya na hatupaswi kukiuka sheria kwa kuua binadamu, tafafhari fikiria mara mbilimbili unachotaka kufanya”Aliongea Mzee Lao na maneno yake yalionekana kuwa ya mantiki na palepale aliacha kile alichokuwa akipanga kufanya.
“Okey Mzee Lao nitakusikiliza na kumsamehe huyu bibi kizee”Aliongea na palepale alimsogelea Bi Wema na kumtenganisha na Rufi kwa nguvu na licha ya kutumia nguvu kidogo kwa Bi Wema alikuwa mwepesi sana kwani alikwenda kujipigiza kwenye ukuta na kupoteza fahamu palepale.
“Mamaa…!!!”
Rufi alijitahidi kufurukuta kujitoa kwenye mikono ya Lahani lakini ilikuwa ngumu na aliishia kutoa kilio , Lahani palepale alimwingizia Rufi nguvu ya kijini na kumchunguza na aliweza kugundua hakuwa bikra tena na kufanya uso wake kuzidi kujikunja kwa hasira.
“Kwahio tayari umelala nae , kwanini sumu tuliokutegeshea haijamuathiri ? hakuna mtu ambaye anaruhusiwa kugusa mwanamke ambae nilimkataa , kwasababu wewe sio bikra tena hakuna haja ya kugiza ndoa yetu kama makubaliano na ukoo wenu , kwanzia leo hii utakuwa kifaa cha majaribio ndani ya ukoo wetu kwa maisha yako yote”Aliongea kwa hasira mno.
Rufi aliishia kutoa machozi tu bila ya kuongea neno na uso wake ulimwangalia mama yake mzazi ambaye muda huo alikuwa hana fahamu,alitamani hata utokee muujiza akaangalie hali yake , hakujali anapelekwa ujinini alichokuwa akijali muda huo ni hali ya mama yake.
“Master ni muda wa kuondok, nimepotea ishara kutoka kwa Mkuu wa ukoo turudi mapema kabla uwepo wetu haujajulikana”Aliongea jini Lao na Lahani alitingisha kichwa na palepale alimshikilia vizuri Rufi na kisha alipotea nae na kumfanya Mzee Lao kuvuta pumzi za ahueni na palepale alimwangalia Bi Weka kwa sekunde na kisha alimshikilia XiaoXiao vizuri na kupotea palepale.
Alibakia Bi Wema ambaye alikuwa akitokwa na damu puani na mdomoni akiwa hana fahamu.
******
Upande mwingine ndani ya mgahawa mmoja maarufu unaopatikana ndani ya jijji la Dodoma alionekana Mzee Kweka pamoja na Roma wakiwa wameketi wakipata kifungua kinywa.
Upande wa Roma alionekana kabisa akili yake haikuwa imetulia kabisa, na kila saa alikuwa akiangalia karatasi iliokuwa kwenye mikono yake.
Nusu saa iliopita alikuwa ameenda kukutana na Master Namba moja kwa mara ya kwanza tokea asikie jina lake, kilichomshangaza Roma ni kwamba licha ya kwamba alikuwa na shauku ya kutaka kumuona Master namba moja lakini alishindwa kumuona kwa sura yake halisi.
Roma mara baada ya kukutana na Afande Kweka katika hoteli ya Highland iliokuwa ndani ya jiji hilo moja kwa moja waliepelekwa mpaka kwenye chumba maalumu ambacho kwa matarajio yao ndio sehemu ambayo wangekutana na Master Namba moja , lakini katika hali ya kushangaza ni kwamba Roma na Afande Kweka hawakuweza kukutana mtu ndani ya chumba hicho zaidi ya kusogelewa na wahudumu na kuambiwa wasubiri.
Walikaa ndani ya chumba hicho kwa zaidi ya nusu saa nzima bila ya Master namba moja kijitokeza , na ilimbidi Roma kupatwa na hasira na kuona pengine mtu huyo alikuwa akiwachelewesha kwa makusudi.
Wakati Roma aliopokuwa akipoteza uvumilivu ndio muda ambao alifika Raisi Senga ndani ya chumba hicho huku mkononi akiwa ameshika bahasha.
Raisi Senga aliishia kumwangalia Roma kwa macho ambayo hayakueleweka yalikuwa ya furaha au ya huzuni , ilikuwa ni kama vile kuna kitu ambacho kimetokea.
Roma na Afande Kweka wote walishangaa kumuona Raisi Senga nndio ambaye alifika ndani ya chumba hicho tofauti na Master Namba mmoja mwenyewe.
“Mzee msishangae , nipepewa jukumu la kuwakilisha masharti kwako kwa kosa ambalo umelifanya”Aliongea Raisi Senga huku akiwa na muonekano ambao ulikuwa na wasiwasi.
“Mashart, Senga unamaanisha nini , kwanini wewe ndio upo hapa?”
“Baba haya yote ni makosa ya Roma , familia ya Mzee Sharif sio familia ya kawaida na kilichonikuta sitaki kuweka wazi na nipo hapa kama mwakilishi tu”Aliongea na kisha palepale alimpatia Roma ile bahasha na Roma alitoa nyaraka ambazo zilikuwa ndani yake na kadri alivyokuwa akiisoma uso ulikuwa ukijikunja.
“Haiwezekani?””Aliongea Roma.
“Roma hiki ni kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wako ,mtu ambaye unashindana nae sio wa kawaida na kama unataka kuendelea kuishi kwa amani pamoja na familia yako basi unapaswa kutimiza hayo masharti”aliongea Raisi Senga kwa kwa macho yake vile ilikuwa ni kama vile hana undugu na Roma na Afande Kweka , alikuwa yupo siriasi mno.
“Naataa kutii haya masharti , kama huyo Master Namba moja amekataa kujionyesha kwangu yeye mwenyewe basi siwezi kukubali huu ujinga , haya masharti yatanigharimu zaidi ya bilioni nne hela za kimarekani mnadhani hela zinaokotwa , hili swala lilitokea kwasababu familia ya Mzee Sharif ndio ilinianza”
Roma alizidi kuongea na kumfanya Raisi Senga kuzidi kuwa na hali ya wasiwasi.
“Roma nisikilize haya ndo masharti na mimi nipo hapa kama mwakilishi tu , hivyo ni wewe kutii ama kutotii lakini kama utaamua kukaidi lazima ujiulize je na uhakika unaweza kushindana na nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif”
“Ndio ninao uwezo wa kushindana nayo ,ameamua kujificha kwasababu ni muoga”
“Wala hajajificha kwa taarifa yako yupo hapa hapa tokea mlivyofika ila kwasababu ya uwezo wako mdogo hujamuona”
Aliongea na dakika ileile ni kama vile maneno yake yalibadili hali ya hewa kwani alianza kuhisi msisimko wa ajabu wa hewa ukianza kuongezeka ndani ya kile chumba na dakika chache mbeleni ni kama vile mtu ambaye ameshikwa na jinamizi kwani alianza kukosa hewa.
Mabadiliko yale yalimfanya hata Afande Kweka aliekuwa yupo kimya pembeni kushangaa mabadiliko ya Roma.
Haikuishia kukabwa tu shingo Roma alijihisi maumivu makali mno , alijaribu kuita Cauldron kudhibiti ile hali lakini mtitiroko wa nguvu zake ni kama vile umefungwa.
Roma alijikuta akipagawa na kujiuliza ni nguvu gani hioo ya kijini, alijitahidi kupambana na nguvu hio na ya kwake lakini ilionekana nguvu hio kuwa kubwa zaidi ya vile ambavyo amefikiria kwani iliweza kumshinda kirahisi sana.
“Nipo tayari kutii masharti”Roma alijikuta akiripoka mara baada ya kuona anazidi kuwa mnyonge na jasho jingi kumtoka na dakika ambayo aliongea kauli hio palepale nguvu ile ilimuachia na kumfanya kuwa huru na kupumua tena.
“Nini kimekutokea?”Aliuliza Afande Kweka ambaye ni kama sasa alikuwa amtoka kwenye mshangao.
Upande wa Raisi Senga alikuwa kwenye hali ya tabasamu tu , ilikuwa ni kama vile alifurahia Roma kuwa katika hali aliokuwa nayo.
Sasa kilichomchanganya Roma zaidi ni kwamba mara baada ya kutoka nje ya chumba hicho cha hoteli alishangaa kukuta eneo la nje hakuna ulinzi wa aina yoyote , yaani walivyofika na walivyotoka hali ilikuwa ileile , hata Afande Kweka mwenyewe alishangazwa na hali hio.
Roma palepale akili ilimcheza alijua mtu ambae alikutana nae sio Raisi Senga halisi , dakika ileile alirudi nyuma kwenda kuangalia ndani ya kile chumba ambacho walikuwemo lakini walikuta kilikuwa tupu na kuangaliana.
“Wewe mtukutu hebu nipatie hio karatasi”aliongea Afande Kweka na Roma palepale alimpatia Afande Kweka ile katarasi , isitoshe hata yeye alikuwa kwenye mshangao.
“Hii sio sahihi ya baba yako”Aliongea Afande Kweka.
“Mzee unamaanisha….”Aliongea Roma huku akimwangalia babu yake usoni na palepale Roma aliweza kuelewa nini ambacho amekutana nacho,mtu aliekuwa ndani ya kile chumba sio Senga pengine ndio Master namba moja mwenyewe ambaye amekuja kwa muonekano wa sura ya Raisi Senga.
Roma alianza kujiuliza kama ni kweli ni nguvu ya aina gani ambayo anatumia kiasi cha kumfanya ashindwe kumgundua ni feki , ijapokuwa alikuwa na walakini tokea mwanzo wa mazungumzo lakini hakukuwa na dalili za wazi za kuonyesha sio yeye.
Afande Kweka alionekana kama vile alijua muda mrefu na hakuonyesha hali ya mshangao na palepale alipiga hatua na kuondoka ndani ya hilo eneo.
Roma mara baada ya kutoka ndani ya hoteli hio walikuja kuingia ndani ya mgahawa mmoja kando ya barabara inayoelekea Singida na muda wote ambao walikuwa kwenye gari walikuwa kimya tu kila mtu akiwaza lake.
“Vipi bado hujapatana na Edna?” Alivunja ukimya Afande Kweka mara baada ya wote kuingia ndani ya mgahawa na kuagiza supu.
“Mzee unaniuliza kitu ambacho unajua tayari”Aliongea Roma na kumfanya Afande Kweka kunywa supu kidogo na kumwagalia Roma.
“Nimeamua kukaa pembeni na kukuangalia usidhani sijali ,nataka unipatie tarehe leo hii ni lini unemrudisha Edna nyumbani?”
“Nilimuahidi Edna sitomlazimisha kubaki na mimi , nitakachofanya ni kumjali pekee nadhani ndio kitu ninachoweza kufanya kwa sasa , kuhusu mambo meingine sitaki sana kufikiria”
“Hibi wewe ni mwanaume kweli?”Aliongea Afande Kweka kwa kufoka huku akionyesha hasira waziwazi kwenye macho yake.
“Mzee unajua kabisa mahusiano yangu na Edna yalivyokuwa na mkanganyiko haina haja ya kunifokea”
“Man up!!! , hilo sio tatizo , tatizo ambalo lipo ni kwamba wewe sio mwaminifu na una mtoto na mwanamke mwingine, naona ni tatizo dogo tu tofauti na ulichopitia dakika kadhaa zilizopita”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na kauli yake lakini alihisi ni kama yupo sahihi maana ile nguvu haikuwa mchezo.
“Nakujua upo vizuri sana kwenye kudanganya wanawake lakini kwanini swala dogo hili linakushinda , kwahio unataka kuniambia wanawake wote walikupenda baada ya kuwaambia kila kitu kuhusu wewe , kama jibu ni hapana basi kuna sababu nyingine ambayo imewafanya kukupenda ,hebu tumia ubongo wako huo, hata ni kwa kumdanganya hakikisha Edna anaendelea kuwa mkeo”Aliongea
“Mzee tatizo ni kwamba…”
“Usinipe visingizio vya kipuuzi maana havina umuhimu wowote kuliko mahusiano yako , sikutaka kuingilia maswala yenu ya ndoa kwasababu nilikuamini utayamaliza ndani ya muda mfupi lakini mpaka sasa hivi unayumba tu , mama yako anaweza kukuambia kuoa mwanamke mwingine lakini usije kumsikiliza , sitaki kuja kusikia eti tayari ushasaini makaratasi ya talaka”
“Inaonekana kama unanidhihaki vile maana ushaniona tayari nina uwezo mdogo , unafikiri nitayaingilia vipi maisha ya Edna?”
“Hebu acha kunikasirisha bwana , kama ungetumia asilimia kumi tu ya akili yako kama unavyoitumia kujifunza mafunzo ya kijini yote ya akili yako haya yote yasingetokea , kwanini unafanya maamuzi kama vile unamjua sana Edna , wewe sio Edna na anaonekana anakuigizia yule, unapaswa kuelewa wanawake wanaongea vitu ambavyo hawamaanishi na mimi najua zaidi yako, hebu fikiria tokea mtengane , vipi furaha yake imeongezeka au imepungua , vipi anaonekana kuwa na furaha kuliko mwanzo?”Aliuliza akiwa siriasi na kumfanya Roma kuona kweli maneno ya babu yake ni sahihi.
Tokea atengane na Edna hakuonekana kama mwanamke mwenye furaha kwa maelezo ya Bi Wema.
“Roma fanya chochote unachoweza kumuomba msahama , hata kama ni kumlilia, fanya chochote unachoweza akusamehe na umrudishe”
“Mzee sasa mbona unaongea mambo ya kutia aibu hivyo , yaani mimi na uanaume wangu nilie mbele yake anisamehe?”
“Mambo gani ya aibu , kwangu sijali kama uanaume wako utaathirika , ninachotaka ni kumuona umemrudisha na kuendelea kuwa mkeo , kama wewe ni mwanaume wa kweli unatakiwa kufanya chochote kile kumfurahisha mke wako , kama kweli mtafikia hatua ya kuachana hakikisha wewe ndio humpendi na sio kukuacha kwa sababu ambazo hazieleweki, unafikiri Edna nilimpatia ile bangiri bahati mbaya , nilimpatia kwasababu ilimchagua na sio vinginevyo , hivyo sitaki kusikilia sijui likipanda na likishuka nataka kuona anakuja kunisalimia nyumbani”Aliongea Mzee na kisha akasimama akionekana muda wowote anaondoka.
“Weka utaratibu wowote Lanlan aje kunisalimia nyumbani hata kama akiacha kwenda shule kwa siku kadhaa haina shida ana akili yule hata asisome, najua una mambo mengi kwasasa mimi nitaondoka , unajua mwenyewe namna ya kurudi”
“Mzee hebu subiri kwanza , unapaswa kulipia sina hata hela hapa”Aliongea Roma huku akimalizia supu iliokuwa kwenye bakuri lake na kisha kusimama.
Roma ni kweli hakuwa na hela alikuwa na kadi ya benki tu na Tanzania sio kama Ulaya kwamba unaweza kupitisha kadi na kulipia.
Afande Kweka hakuwa na hiyana alifanya malipo na ndani ya muda uleule alimpa ishara dereva wake na kusogeza gari na kuingia ndani na kumuacha Roma akiwa amesimama.
Upande wa Roma aliishia kusimama kwa muda huku akiwaza , siku hio ilikuwa ni ya ajabu kwake.
Mwanzoni Roma alijua kutokana na kurudiwa na nguvu zote na kupitia mapigo ya radi tisini na tisa basi ana uwezo mkubwa lakini siku hio ni kama amekutana na mtu ambaye alikuwa na nguvu kubwa kuliko yeye na kuona bado ana safari ndefu.
Hakutaka kuwaza masharti ambayo alikuewa amepewa kuyakamilisha ili kusamehewa kile ambacho amefanya.
Ukweli ni kwamba masharti ambayo amepewa yalikuwa yakimgharibu zaidi ya dolla bilioni nne za kitanzania lakini hakuona ni pesa nyingi , kitu pekee kilichomfurahisha ni kwamba huyo mtu anaejiita Master namba moja alionekana kutokuwa na uelewa juu ya Maimuna kuwa feki.
Hivyo Roma alijiambia atachukua utajiri aliopata kutoka kwa Masterr Wadudu na kisha ataunganisha na utajiri ambao ataupata kutoka kwa familia ya Mzee Sharif na kukamilisha masharti, alijiambia ngoja awe mjinga kwa muda huo asiongeze maadui na atakuja kupambana nae tu.
Baada ya kuwaza kwa dakika kadhaa aliona hatua inayofuata ni kumrudisha Edna kwenye himaya yake kwa namna yoyote ile , hakujua kwanini Mzee Kweka ameenda mbali na kuonyesha usiriasi wa Edna kuendelea kuwa mke wake lakini aliona ni sahihi kwani hata yeye hakuwa na nia ya kumpoteza.
SEHEMU YA 697.
Ilikuwa ni mchana na jua ndani ya jiji la Dar lilikuwa likiunguza kwa wastani.
Ilikuwa tayari ni jumamosi na mitaa mingi ya kibiashara ndani ya jiji hilo ilikuwa imejaa sauti za watu na makelele ya miziki na baina ya nyimbo ambazo zilikuwa zikisikika ni za Sophia.
Kurudi kwa Sophia kwenye kiwanda cha muziki ilimfanya umaarufu wake kuongezeka zaidi na zaidi, ilionekana skendo ambayo aliipata mara ya mwisho ndio iliomfanya kuzidi kuwa maarufu.
Ndani ya makao makuu ya kampuni ya Vexto licha ya kwamba ilikuwa jumamosi lakini wafanyakazi walikuwa wako bize kufanya kazi.
Tokea kampuni hio kuwa ‘International Corporation’ wafanyakazi wengi waliajiriwa ili kupunguza wingi wa kazi na kuongeza ufanisi.
Ukiachana na ule upendeleo wa kampuni hio kuajiri zaidi wanawake awamu hio warfanyakazi wengi ambao wameajiriwa ni wanaume pia , hata hivyo wahitimu wengi wenye ujuzi mbalimbali walikuwa wakipenda sana kufanya kazi chini ya kampuni ya Vexto, sio kwasababu tu ilikuwa ikilipa vizuri lakini ilionekana kama kampuni ambayo miaka kadhaa ijayo inakwenda kuwa kampuni kubwa ndani ya bara la Afrika , pengine na dunia kwa ujumla.
Upande wa wanaume ambao wameajiriwa kufanya kazi ndani ya makao makuu ya kampni hio walikuwa na furaha kweli kwani waliweza kupata fursa ya kuweza kuongea na warembo ambao wanafanya kazi ndani ya kampun hio.
Edna hakuwa bado amehamishia makazi yake katika jengo jipya ambalo lilikuwa katika hatua za mwisho kabisa kukamilika hivyo bado ofisi yake ilikuwa ikipatikana juu kabisa ndani ya jengo hilo ambalo lilikuwa likipatikana ndani ya eneo la Posta.
Kama ilivyokuwa kwa wafanyakazi wengine kuwa bize upande wa Edna alikuwa amesimama mbele ye kioo akiangalia upande wa nje ambao watu wake walionekana kuwa na pilikapilika.
Siku hio alikuwa amevalia suti ya rangi nyeupe na viatu vya skuna na kumfanya kuzidi kuwa mrembo licha ya kwamba alionekana kuwa mbali kimawazo.
Nyuma yake alikuwa amesimama Recho aliekuwa amevaa suti iliochora mwili wake vizuri na ilionekana alikuwa akitoa ripoti kuhusiana na kazi aliokuwa amepewa.
“Boss , maongezi ya kibiashara kati ya kampuni ya Kijerumani ya Collins Group yamefikia awamu ya tatu, bado wanalazimisha malipo ya Euro milioni mia tatu kwa mwaka, tunapaswa kuendelea vipi..”
“Ongea na wawakilishi wao Euro milionni hamsini ndio ofa yetu ya mwisho kama bado wanakataa hakuna haja ya kuingia nao mkataba mpya na haina haja ya kuwasubiria watoe majibu , wasilimiana na kampuni ya Hofferman na wapatie ofa hio hio”
“Sawa bosi , pia mkurugenzi msaidizi wa kampuni ya Lorrent, Mr Thompson amekueletea kadi ya mwaliko wa kuhudhuria tafrija fupi usiku wa leo katika hoteli ya Serena ambayo itaambatana na mazungumzo ya uwekezaji kuhusiana na mradi wa ujenzi wa makazi unaondelea Bagamoyo , anasema kama hautojitokeza wewe mwenyewe basi atachukulia kama huna nia ya kufanya nae biashara na atarudi Marekani siku inayofuata”
“Muache afanye anavyotaka , ongea na Chriss na mwambie awasiliane na mwenyeketi wa bodi , na awambie Thompson ana tabia ya hovyo na kama wanataka ubia uendelee wambadilishe haraka sana”Aliongea Edna na kumfanya Recho kuitikia kwa kichwa na kisha akafunika faili lake akionekana ashamaliza kutoa ripoti.
“Bosi nishamaliza kutoa ripoti , kuna kitu kingine ambacho unataka nikusaidie siku ya leo?”
“Hali ya hewa leo ni nzuri mno Recho”Aliongea Edna mara baada ya kimya kifupi na kumfanya Recho kuwa na mshangao kidogo lakini alishindwa kongea neno.
“Recho ushapata Lunch?”
“Hapana , ndio kwanza imefika mchana boss”Alibu Recho kwa wasiwasi kwani ni Swali ambalo hakutegemea kulisikia kutoka kwa Edna.
“Unaonaje tukienda kupata chakula pamoja,… nitalipia mimi”Aliongea Edna huku akiweka sawa nywele zake ambazo zilikuwa zimemfunika sikio kutokana na kuchanguka.
Recho ilikuwa mara yake ya kwanza kuambiwa na Edna kwenda kupata wote chakula cha mchana , alijua Edna muda mwingi alipenda kufanya kazi na ni mara chache alikuwa akitoka nje ya jengo hilo kwa ajili ya chakula cha mchana.
“Nipo tayari Madam , unataka tupate chakula sehemu gani , nitaendesha mimi gari?”Aliongea Recho.
“Hakuna haja ya kuendesha gari leo , nataka kupanda yale magari ya mwendokasi”Aliongea Edna huku akinyooshea kidole gari la mwendokasi ambalo linashusha watu kituoni.
Kauli yake ilimuacha Recho kinywa wazi akiwa kama hajasikia vizuri na paepale alipotezea mshangao wake.
“Bossi kwani haujisikii vizuri au ni kutokana na kuwa na mawazo?”Aliuliza Recho.
Ukweli ni kwamba hakutaka kuamini kama Edna anaweza kupanda mwendokasi , alikuwa na uhakika tokea mwendokasi uje ndani ya jiji la Dar kama usafiri wa uma , Edna hajawahi kupanda lakini sio hivyo ni ngumu kwa mwanamke tajiri kama Edna mwenye zaidi ya Dola bilioni ishirini kupanda magari ya uma.
“Recho unafikiria nini ,tunaenda au hatuendi?””
“Ah ,,, tunaenda bosi , nisubiri kidogo naenda kuweka hivi vitu nakuchukua mkoba wangu”Aliongea Recho na palepale alitoka kwa kukimbia kwenda nje kuweka vitu vyake
Dakika chache mbele Edna akiwa anakodolewa macho na wafanyakazi aliweza kutoka nje ya jengo hilo akiwa ameambatana na Recho.
Wafanyakazi ambao walikuwa nje walijikuta wakishangazwa mara baada ya Recho na Edna kuelekea kituo cha mwendo kasi na kukata tiketi.
Edna hakujali wanaomwangalia na mara aada ya kuchukua tiketi mbili alimpatia Recho na wote kwa pamoja waliingia ndani ya eneo la kusubiria gari na bahati nzuri gari haikuchelewa na haikujaza sana na wote walipanda gari hio inayoelelekea Morocco.
Recho alikuwa akifuatisha tu maana hakujua ni wapi wanaelekea na bosi wake na mara baada ya kufikishwa Morocco Edna aliita taksi na wote wakaingia na Edna alitoa maelekezo ya kuepelekwa upepo Beach.
Na hapo ndio sasa Recho alijua ni wapi wanaelekea , lakini alifurahi na yeye pia mara baada ya kuona wanaelekea Upepo Beach , ni moja ya eneo ambalo anapenda sana kutembelea ikiwa wikiend.
Haikuwachukua dakika nyingi mpaka kufika na wote walishuka nje huku Edna akiangalia mazingira.
“Unapaonaje hapa Recho , tutakula hapa na kupunga upepo kidogo”Aliongea mara baada ya kumlipa dereva.
“Ni pazuri mno na pametulia”Aliongea Recho akitoa tabasamu , hakuwa akielewa kwanini Edna kaamua kuja mbali hivyo kwa ajili tu ya chakula cha mchana kwani kampuni ilikuwa mbali sana lakini hata hivyo alifuata nyuma nyuma kuingia ndani ya eneo hilo huku akiwa na hamu ya kupata Seafood.
Ilikuwa ni wikiend na eneo lilikuwa na watu wengi licha ya kwamba ilikuwa mchana bado.
Edna alikuwa ni kama amekariri eneo hilo kwani mara baada ya kuona sehemu ambayo alikaa na Roma mara ya mwisho alitoa pumzi ya ahueni na kunyoosha kidole akimwashiria Recho ndio wanapoenda kukaa.
Wahudumu wa eneo hilo walishangazwa na uwepo wa Edna lakini haraka haraka waliomba kuwahudumia.
Edna aliagiza aina ya chakula kilekile ambacho Roma alimwagizia mara ya mwisho na Recho na yeye alichagua hichohicho.
“Leo sio kitamu kama mara ya mwisho nilivyojaribu kula nikiwa na Roma…”Aliongea Edna huku akionyesha hali ya kukosa hamu ya kuendelea kula.
“Boss naomba niwe muwazi kwako , najua kabisa unampenda mume wako lakini kwanini unamkwepa tofauti na kukaa chini mkayamaliza, mimi na wafanyakazi wengine ndani ya kampuni tunakuchukulia kama Role model wetu , kwasababu wewe ni mwanamke mwenye maamuzi na ngangari na ndio maana umetufikisha leo tulipo lakini kwanini unakimbia changamoto za maisha yako binafsi, umenileta mbali hivi najua yote ni kutokana na kushindwa kumsahau Roma”
“Recho sio rahisi hivyo , maisha ni tofauti na biashara , kwenye biashara kama nitafeli na kampuni kufirisika naweza kuanza upya maadamu nitakuwa hai na ndio maana siogopi changamoto za biashara lakini kwenye maisha ni tofauti , kuna baadhi ya vitu kwenye maisha huwezi kubahatisha kwasababu ukipoteza ndio umepoteza na siwezi kurudisha muda nyma ndio maana nakuwa muoga”
Aliongea Edna na kumfanya Recho kushindwa kuongea neno lololote , mwanzoni alikuwa akimuonea wivu sana kwa kujaliwa uzuri , busara na mapemzi lakini kwasasa licha ya kwamba bado alikuwa akimuheshimu kutokana na uzuri wake na busara zake lakini aliona mapenzi ni kitu ambacho ni kama hakimpi furaha.
Wakati wakiendelea kuwa bize na chakula muda huo huo alionekana mtu mwingine akisogea upande wao kukaa nyuma yao.
“Wewe utakuwa ni mjinga sasa , na siku zote nakuambia hivyo, maisha ni sehemu ya mchezo wa kubahatisha , ndio unaweza kusema hutaki kubahatisha lakini usipofanya hivyo ni sawa na kujihukumu kwani hutokuwa na furaha hata kidogo”
Sauti ilisikika pembeni yao na kumfanya Edna kushikwa na mshangao kwani ni sauti ambayo alikuwa akiijua na mara baada ya kugeuza uso wake aliweza kumuona Roma akiwa na tabasamu kama kawaida yake.
“Wewe.. kwanini upo hapa??”
Hata Recho alikuwa kwenye mshangao na Roma hakujali mshagao wao na alienda kukaa kwenye meza yao.
“Niliwaona mkitoka nje ya kampuni na kupanda basi , sikujua mnaenda wapi hivyo niliwafuatia nyuma nyuma mpaka hapa , babe sijui ni jambo gani unannificha lakini siamini kama hunipendi na hujanimisi”
Edna alijikuta akiona aibu, maana alikuwa amekamatika na hakujua namna nyingine ya kuficha hisia zake.
Roma alikuwa mwepesi alichukua samaki palepale na kumtoa miba na kisha kumpa ishara Edna kuachama ili amlishe
Muda huo Edna mara baada ya kugeuka kuangalia pembeni aligundua watu wengi walikuwa wakiwaangalia kwa macho ya uchokozi hata Recho aliokuwa nao meza moja alikuwa akimwangalia kwa macho ya kichokozi.
“Unafanya nini wewe…, huoni watu wanatuangalia”Aliongea Edna kwa tahadhari.
“Wakiangalia ndio ndio , wewe ni mke wangu na naruhusiwa kukulisha , kama kuna ambaye hapendi nikimlisha mke wangu nitamfukuza hapa”Aliongea Roma kwa sauti kama vile anataka kila mtu asikie .
“Mimi , sitaki tupo kwenye mchakato wa talaka”Edna alijifanyisha kauzu lakini mashavu yake yalimaanisha kitu kingine na kumfanya kuzidi kupendeza kiasi cha kumfanya Roma kutoa kicheko.
“Wife hujui hata kuigiza hasira?”
“Mimi…”Edna hata hakujua namna ya kujitoa kwenye hio hali , hakutaka juhudi zake za kumuigizia Roma zipotee kirahisi hivyo kwa kipande cha samaki.
Upande wa Roma alipanga siku hio kuhakikisha anayamaliza na Edna kwa namna yoyote ile kama alivyoambiwa na babu yake, ilikuwa bahati kwamba Edna alitoka mwenyewe kwa ajili ya chakula cha mchana lakini mpango wake ni kufanya tukio ndani ya kampuni.
“Hey binti hebu kula basi , mumeo anajitahidi kukubembeleza vyote hivyo”Sauti ya mzee aliekuwa na mke wake pembeni walishindwa kuvumilia.
“Hehe ugomvi wa kimapenzi huo na ndio raha yake, hebu kula na wewe usimkasirikie tena , nyie ni wenza hii ndio sehemu ya kuyamaliza”Mke wa yule mzee alimuunga mkono mume wake na kumfanya Edna kuwa mwekundu kutokana na uchokozi wao.
“Ndio mpenzi wangu, sijali unasababu ya aina gani inayokufanya kunikasirikia lakini huna haya ya kuniambia na sitokulazimisha , sitaki kuigiza na kuonekana mtu mzuri mbele yako , najua mimi ni mbinafsi linapokuja swala lako , sitaki kusikia visingizio vingine na sitaki kujidanganya pia kwani najua hisia zako juu yangu na mimi najua zangu juu yako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumpiga kibao mkono ulioshikilia samaki .
“Unajua hisia zangu kivipi wewe , nimesema sikutaki tena na usinisogelee tena”Aliongea huku akitoa machozi na palepale alisimama na kukimbilia ufukweni na kumfanya Roma kushikwa na bumbuwazi.
“Hey stop sitting there ! Go after her” Mwanaumke mmoja wa kizungu aliekuwa amekaa mita kadhaa ni kama alikuwa akijua kinachoendelea na kupendezwa na drama hizo za kimapenzi.
Roma na yeye ni kama akili yake imeshituliwa na alisimama na kumkimbilia Edna na mara baada ya kumfikia alimkumbatia kwa nyuma akipitisha mikono yake kifuani.
“Niachie mimi bwana….”
Aliongea Edna huku akitaka kumng’ata Roma mkononi lakini hakuweza kuufikia na kuishia kufurukuta huku mikono yake ikisuguana na manyonyo yake .
“Siwezi kukuachia tena kwanzia leo hii”
“Wewe … Roma niachie bwana .. nishakuambia hatuwezi kuendelea kuwa pamoja”
“Edna siwezi kukuachia , nataka kuendelea kuwa mumeo na wewe kuwa mke wangu , hakuna kitu ambacho kinaniogopesha kwenye ulimwengu huu kama kukupoteza”
“Roma nakuambia utaumia na unaweza kufa ukiendelea kuwa na mimi, huogopi?”Aliongea Edna na kauli yake ilimfanya Roma kucheka kama kichaa.
“Edna nadhani hunijui vizuri , mimi siogopi kifo , hata kama nikifa leo angalau najua sijapoteza maisha yangu bila sababu , Kwangu kitu pekee ninachoogopa kwenye huu ulimwengu ni kukupoteza wewe kipenzi changu , kwasababu najua hata kama nitakuwa naendelea kuishi bila wewe lakini moyo wangu utakuwa umekufa”
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MRUNZI: SINGANOJR
Mono no aware
SEHEMU YA 694.
Ilikuwa ni kama Roma alivyokuwa ametegemea , kwani ile anafika katika makazi ya Mzee Sharif yaliopo Bagamoyo aliweza kukuta vurugu zilizokuwa zikiendelea.
“Ndio mmeanza vurugu?”Aliongea Roma mara baada ya kutua kwenye bustani ndani ya jumba hilo ambalo lilitumiwa kama makazi ya muda ya Mzee Sharif mara baada ya yale ya Kilimanjaro kuharibiwa.
Dakika hio watu waliokuwa hapo ndani waliweza kusikia sauti wanayoifahamu na mara baada ya kugeuka waliweza kumuona Jini Imrah na Maimuna na palepale wote kwa hofu walipiga magoti chini kusujudu.
Walikuwa wakijua Maimuna na jini Imrah walishakufa na wengine wote kutokana na miili yao kutoweza kupatikana , lakini ajabu sasa muda huo wamerudi wakiwa hai hivyo kila mmoja alishikwa na woga na yale mawazo ya kutaka kupata madaraka yalikufa palepale.
Lazima kuwa na hofu kwani walikuwa ni binadamu tu huku wao wakiwa ni majini wenye nguvu.
Roma aliishia kujichekea ndani kwa ndani na kujiambia kumbe kujifanyisha mtu mwingine kuna raha yake , kama sio kuwa na mipango mingine alijiambia angekaa hapo hapo kwa muda kwanza kujionea.
Dakika ileile aliwaambia kwamba yeye kama jini Imrah amemuokoa Maimuna kutoka kwenye mikono ya Roma Ramoni na kwanzia siku hio angekuwa kiongozi wa ukoo pamoja na kuongoza imani yote ya kikafara.
Maimuna ambaye ni Tannya aliweka msimamo wake juu ya mpango wa kupangua familia hio ki uongozi kutoka ngazi ya chini mpaka ya juu.
Tannya alihitajika kufanya hivyo ili kuhakikisha anaingiza watu wake ambao wangeweza kurithi nafasi za wafuasi watiifu na kuweza kupata taarifa zote juu ya familia hio kama misheni aliopewa na mfalme Pluto.
Roma mara baada ya kumalizana na swala hilo palepale aliondoka na kurudi kwenye muonekanno wake wa kawaida na moja kwa moja akafanya safari ya kwenda Los Angeles-Marekani.
Hakuwa ameonana na Christen kwa muda mrefu kidogo na kwasababu alikuwa anataka kumuuliza kuhusu kilichotokea usiku hivyo aliona amtembelee.
Wakati anaingia Los Angeles ilikuwa ni giza bado na kwa kutumia uwezo wake aliweza kugungua Christen alikuwa ndani ya jumba lake.
Kufumba na kufumbua Roma alikuja kutua kwenye balkoni katika floor ya pili ndani ya nyumba ya Christen , alikumbuka mara ya mwisho alivyofika kwenye nyumba hio aliweza kupata huduma kutoka kwa kijakazi wa Christen na alijiuliza kama bado yupo.
Upande wa Christen na yeye alikuwa ashahisia ujio wake na alifungua mlango na kutoka nje akiwa katika mavazi ya kulalia na kumfanya kuzidi kuonekana mrembo.s
“Hades nilijua utanipigia simu mchana , naona umesubiri mpaka giza lilipoingia na kuja kunifanyia surprise”Aliongea
“Nimechelewa , nilikuwa bize na mambo mengine..”Aliongea Roma na palepale alisogeza kiti karibu na kuketi.
“Kama ulitegemea ningekutafuta basi itakuwa sio mimi tu ninaepatwa na hizi hisia, hebu niambie ni nini kinaendelea , kwanini nguvu ya uungu ndani yangu ni kama imeongezeka , ninaweza kuhisia hata saivi bado inaongezeka taratibu sana”
“Such spoilsport , I’ m wearing this in front of you and yet you are talking about things like this…”Aliongea na paleplale alimsogelea Roma na kumkalia huku akimshikilia shingo kimadaha.
Roma alichoweza kuhisi ni marashi kutoka kwa mwanamke huyo , huku kidevu cha mrembo huyo kikiwa kimegusana na kifua chake.
Uzuri wa Christen pamoja na u’superstar’ ni sifa ambazo mbele ya mwanaume rijali hawezi kuepuka mtego wake lakini kwa bahati mbaya au nzuri Roma alikuwa na uwezo wa kujizuia.
“Kwa staili hii sidhani kama upo tayari kujibu maswali yangu, Christen unanifanya nione kuna kitu muhimu sana mnanificha”Aliongea Roma lakini Christen alikuwa akijisugua sugua mapajani ili kuamsha mhogo wa Roma.
Mara baada ya kuhisi ugumu ukiongezeka ndani ya suruali yake alimwinnamia na kumnong’oneza.
“Babe unaonaje tukifanya hivi , kama utakidhi haja zangu nitakuambia ukweli wote, nadhani unajua vizuri sijawahi kufanywa nikiwa na huu mwili na itabana vizuri tu”
Maneno ya Christen yalimfanya mapigo yake ya moyo kwenda kasi na kumlaani kwa kuongea maneno hayo ya kiuchokozi bila aibu na kuamsha ukichaa wake.
Kama ni mwanaume mwingine ambaye upo katika nafasi ya Roma angeishikilia fursa hio kwa mikono yote, kulikuwana wanaume wengi sana ambao wanajaribu kutoka kimapenzi na mwanamke huyo lakini wote wanaambulia kupigwa vibuti.
“Najua kuna wanaume kibao ambao wanakutaka na wanaweza kukidhi matamanio yako”
“Nilishakuwa na wanaume tofauti tofauti kila nilipobadilisha mwili lakini tokea nibadili huu mwili wewe ndio mwanaume ambaye umekidhi vigezo vangu”
“Asante kwa kunisifia lakini naomba niwe mkorofi kukukataa, unaonaje ukiniambia ukweli na kisha nikakidhi matamanio yako zaidi ya mara mbili”
Roma alishajua kama angetaka kuanzisha mahusiano na Christen jambo hilo lingetokea miaka mingi iliopita , isitoshe sio watu ambao walikuwa wakifungwa na sheria za kiimani.
Wote wana roho ya uungu ndani yao hivyo miili wanayotumia ni kama nyumba tu ya kutumia kwa muda tu.
Kilichomfanya Roma kutotaka kujihusisha kimahusiano na Chriten ni kutokana na mrembo huyo kuwa na hisitoria na Hades wa Zamani licha ya kwamba hakuwa akijua maelezo yote juu ya mahusiano yao.
Uwezo wao wa kuhamisha ‘ Consciousnes’ zao kutoka kwenye mwili mmoja kwenda mwingine ilitegemeana na nguvu ya ki uuungu ndani yao, Hades wa Zamani alikuwa ameshapoteza nusu yake mara baada ya kumrithisha Roma hivyo asilimia za kujivika mwili mwingine aliamini ingekuwa ngumu.
“Hades unachukiza mno , yaani najilengesha kwako lakini bato tu unanikataa , hivi nakosa nini ambacho mkeo na wapenzi wako wanacho mimi sina?”Aliongea huku akijifanyisha amekasirika.
“Aphrodite acha mambo yako bwana , sisi ni mrafiki na nakujua vizuri hivyo acha kuficha ukweli na niambie nini kinaendelea”Aliongea Roma huku muonekano wake ukiwa na hali ya usiriasi ndani yake.
Christen alitoa pumzi nyingi na kuzishusha na kisha alisimama na kumzodoa kwenye paji la uso kama vile hajaridhishwa na maneno yake na palepale alisimama kwenye uzio wa balkoni na kuangalia mataa ya jiji la Biverly hills.
“Ni moyo wa Gaia , Athena ameshaufufua”Aliongea bila ya kugeuka.
Roma alikuwa ashaotea muda mrefu, hivyo hakushangaa sana lakini bado hakuwa akijua moyo huo unahusu nini na athari zake ni zipi.
“Kufufuka kwa huo moyo inamaanisha kwamba mtaweza kurudiwa na nguvu zenu si ndio? , nakumbuka kule Korea Kusini Stern , Alice na Athena walivyokuwa wakiongea walitaja kuhusu huu moyo wa Gaia na kusema utaleta matokeo makubwa kwa dunia yote , nakumbuka pia ni kama walikuwa wakibishana na kusema ni kitu ambacho kitaharibu ulimwengu lakini wakati ule hawakutaka kunipa maelezo kabisa nnilipowauliza , kwanini wewe usiniambie kila kitu”
“Sidhani kama kuna maelezo yaliobakia ambayo ninaweza kukupatia , hata wewe mweneyewe umeweza kuhisia kufufuka kwa moyo wa Gaia, hivyo ni kweli nguvu zetu zitarudi taratibu taratibu na Athena mpango wake ni kufufua ndugu zetu walioptea na tayari ashafanikisha hatua ya kwanza”
“Ana mpango gani au anataka kuua binadamu kama alivyofanya miaka elfu ishirini iliopita mara baada ya kufeli kwa mpango wenu wa kutawala dunia?”
“Kusema ukweli sijui chochote , Athena hatabiriki na isitoshe hata kama tunajua anachopanga kufanya hatuna huo uwezo wa kumzuia”Aliongea na kumfanya Roma kutulia kimya.
Ukweli ni kwamba Athena uwezo wake ulikuwa wa juu kabisa na Roma alijua hata kama nguvu zake za kijini zimerudi inawezekana bado asifanikishe kushindana nae , isitoshe kufufuka kwa Moyo wa Gaia inamaanisha kwamba na nguvu zake pia zinaongezeka
Dakika ileile Roma alitaka kuuliza swali lingine simu yake iliita na alipotoa na kuangalia anaepiga ni babu yake Afande Kweka na alipokea palepale.
“Wewe mtukutu hebu rudi Tanzania haraka na tukutane Dodoma”Sauti ya kibabe ilisikika.
“Nini kimetokea Mzee?”Aliuliza Roma kwa msahngao.
“Haha… unafikiri kwa ulichokifanya utaachwa kirahisi , umemuweka baba yako katika wakati mgumu na Master namba Moja anataka kukutana na wewe kupitia yeye’Aliongea na kumfanya Roma kushangaa.
“Unamaanisha nini Master Namba moja anataka kukutana na mimi kupitia yeye?”
“Rudi kwanza na tukutane Dodoma ndio tutaongea vizuri”Aliongea na palepale simu ilikatwa.
“Christen natakiwa kurudi?”
“Inaonekana upo matatizoni?,GoodLuck Hades”
“I guess we’ll have to go with the flow for Gaia’s Heart , I know you didn’t tell me everything but I hope no matter what happened in the future we‘ll still be friends”Aliongea Roma akimwamia Christen kwamba anajua hajamweleza kila kitu lakini haijalishi ni nini kitatokea baadae bali wataendelea kuwa marafiki.
Christen alitaka kuongea neno lakini aliingiwa na uzito kwenye midomo yake na kuishia kutoa tabasamu la kuashiria maana na palepale Roma alipotea mbele yake.
Aliishia kuangalia upande ambao Roma amepotelea na kuishia kuvuta pumzi nyingi.
“Roma wewe ni msahaulifu sana nishakuonya mwanzo usije kumruhusu Athena kuupata moyo wa Gaia, eti marafiki wewe ni mjinga sitaku kuwa rafiki yako mimi , nataka urudiwe na ufahamu wako wote halisi ya ki’uungu na tukutane kwa mara nyingine , nikwambie maneno nilioshindwa kukuambia siku zote, Nakusubiri Hades”Aliwaza Chriten.
******
Wakati Marekani ikiwa ni usiku Tanzania ilikuwa ni alfajiri na Rufi bado alikuwa kwenye usingizi mzito sana.
Dakika hio Bi Wema alikuwa tayari amekwisha amka na kuingia katika chumba cha binti yake na kuishia kutingisha kichwa kwa kusikitika mara baada ya kuona vifaa vya tarakishi ambavyo vimezagaa ndani ya chumba chake bila mpangilio , tarakishi bado ilikuwa inawaka na namba namba ambazo hakuwa akizielewa zilionekana.
“Sijui kwanini anapenda mambo kama haya kama vile sio mwanamke , lakini nadhani ni vizuri kuwa na hobi inayomfanya kuwa bize kwani hana uwezo wa kuvuna nishati za mbingu na ardhi kama wenzake”Alijiwazia Bi Wema kwenye kichwa chake na kisha alisogea na kwenda kukaa kitandani na kuanza kumtingisha Rufi.
“Rufi amka kumekucha , tunapaswa kujiandaa mapema tuanze safari”Aliongea Bi Wema.
“Mama nataka nilale kidogo, nimechoka”Aliongea Rufi kivivu na kumfanya Bi Wema kumwangalia binti yake na kutoa tabasamu ,kuna muda alijiambia ni kama miujiza kumwamsha binti yake kama hivyo.
“Rufi mwanangu tutachelewa kufika jamani”Aliongea Bi Wema.
Siku hio Bi Wema alipaswa kwenda kumtembelea mdogo wake huko Pangani mkoani Tanga.
Mwanzoni Bi Wema alijua hakuwa na ndugu kabisa lakini miezi michache aliweza kutafutwa na mwanaume aliejitambulisha kama mdogo wake , yaani mtoto wa baba yake kwa mama mwingine.
Bi Wema mara baada ya kupata taarifa hio alifurahi sana kwani ilimfanya sasa kujua alikuwa na ndugu.
Sasa mara baada ya kurudi kwa Rufi alitaka kwenda kumtembelea mdogo wake kwa mara ya kwanza na siku ambao walipanga kwenda huko ni siku hio asubuhi asubuhi ili kuwahi kufika ndio maana alikuwa akimwamsha alfajiri kwa ajili ya kujiandaa na kuanza safari.
Dakika hio wakati Bi Wema akimuamsha Rufi upande wa balkoni alikuwa amesimama mwanaume mtanashati mno alievalia joho la rangi nyeupe akiangalia ndani ya chumba cha Rufi na macho yaliojaa kejeli.
Licha ya kwamba dirisha kutokea Balkonni lilikuwa na pazia lakini alikuwa na uwezo wa kuona kila kitu kinachoendelea ndani.
Na wakati hio ndio ambao Bi Wema alikuwa akimuamsha Rufi kwa ajili ya kujiandaa kuanza safari.
SEHEMU YA 695.
Bi Wema mwili wake ulihisi kumsisimka ajabu na ilikua ni kama amehisi hatari na kwa haraka alimuacha Rufi aliekuwa akijifikicha macho na kukimbilia upande wa dirisha na kusukuma pazia na hapo ndipo alipojikuta ni kama vile yupo ndotoni mara baada ya kukutana na sura ambayo ilikuwa ikimwangalia kwa tabasabu , manusura apige yowe lakini kwa hali ambayo hakuelewa sauti ilishindwa kumtoka kabisa.
Rufi ambaye alikuwa bado na hali ya usingizi alijikuta akigeuza macho kumwangalia mama yake na hapo ndipo alipoingiwa na ubaridi mara baada ya kuona sura anayoifahamu.
Alikuwa ni jini Lahani kaka yake na XiaoXiao ,alikuwa na muonekano ambao haukuashiria amani na ulimfanya Rufi kuingia na woga wa hatari mno
Wakati Rufi akiwa katika hali ya mshangao upande wa Lahani alisogea upande wa mlango wa Aluminium wa na kuslide mlango kwenda kulia na kufanya upepo kuingia ndani pamoja marashi makali.
Dakika ileile ni kama sasa Rufi akili ilimkaa vizuri na aliruka kutoka kitandani na kumsogelea mama yake kwa hofu.
“Mama , ondoka , ondoka haraka, kimbia kwenda nje”Aliongea Rufi akijaribu kumsukuma mama yake kutoka ndani ya chumba chake.
Bi Wema dakika hio hio alijua wapo katika hatari na aliishia kumkumbatia Rufi huku akimwangalia yule mwanaume mwenye uso wa kuvutia akingia ndani bila wasiwasi.
“Rufi unamaanisha nini , huyu mwanaume ni nani.. Rufi acha kunisukuma jamani”Aliongea Bi Wema akijaribu kushindana na Rufi
“Haha..Kwahio huyu ndio mama yako mzazi , mbona hamfanani hata kidogo”Aliongea Lahani huku akiwa amesimama akimwangalia Rufi kwa kejeli anavyohangaika kumsukumia nje mama yake.
Dakika hio hio vivuli vilitua nje ya Balkoni na Rufi mara baada ya kugeuza macho aliweza kuwajua wote , wa kwanza alikuwa ni Xiao Xiao na wa pili ni mwanaume aliekuwa akimjua vizuri alikuwa ni Mlinzi wa Lahani yaani Mzee Lao.
Wote hao walikuwa ni majini , Lahani alikuwa jini na huyo mzee alikuwa jini vilevile kasoro XiaoXiao ambaye alikuwa ni nusu jini kama ilivyokuwa yeye.
Sasa kitendo cha Rufi kumuona XiaoXiao alijua kabisa yeye ndio amemuuza na alimpiga jicho la hasira.
“Kumbe ni wewe ulieniuza , nilikuaini na hata nikamuomba mpenzi wangu kukuacha hai lakini haya ndio malipo yake>”Aliongea Rufi kwa hasira.
Ukweli XiaoXiao hakuhusika kabisa na alikuwa ameletwa hapo nje ya ridhaa yake na alionyesha kuwa na wasiwasi mno lakini kutokana na kauli ya Rufi alishindwa hata kujua namna ya kujitetea wakati huo , aliishia kutingisha kichwa chake akiwa na machozi kumuashiria Rufi kwamba hahusiki.
Upande wa jini Lahani palepale sura yake ilianza kubadilika na macho yake kubadili rangi na kusababisha upepo kuongezeka na kupeperusha vitu ambavyo vililkuwa vyepesi ndani ya chumba hicho.
“Wewe mal**ya umepata wapi ujasiri wa kunisaliti , sio tu kwamba ulitoroka ulimwengu wa majini lakini pia unamwita binadamu mpenzi mbele yangu , nadhani utakuwa umesahau jinsi ulivokuwa wa hadhi ya chini licha ya familia yako kukuuza kwetu”
Rufi aliishia kutetemeka , mpaka hapo alijua hakuna namna anaweza kuokoka , Roma hakuwa maeneo ya karibu na haelewi kinachoendelea na hata kama kulikuwa na binadamu mwenye uwezo wa kijini karibu asingeweza kushindana na huyo mzee alieambatana na Lahani.
Tena alishukuru Rose na Magdalena hawakuwepo katika maeneo hayo , pengine wangeuliwa..
Lahani ndio mrithi mtarajiwa wa ukoo baada ya baba yake na kutokana na cheo chake alikuwa akilindwa na jini mwenye nguvu sana na ndio huyo mzee ambaye alikuwa ameambatana nae.
“Siwezi kukataa kama umekuja kunichukua na kunirudisha , lakini naomba tafadhali umuache mama yangu”Aliongea Rufi na maneno yale yalimuumiza mno Bi Wema.
“Hapana .. hakuna wa kumchukua binti yangu, imenichukua miaka mingi sana kukutana nae siwezi kuruhusu mumchukue tena , labda muanze kuniua mmi”Aliongea Bi Wema huku akimkingia Rufi kwa mbele.
Bi Wema hakuwa mjinga kutokana na historia ya maisha ya Rufi alikuwa akijua waliokuwa mbele yake ni majini na ndio hao ambao walikuwa wakimsulubu binti yake kabla ya kutoroka.
“Haha.. hahaha…., kama nilivyotarajia , binadamu ni viumbe wajinga sana , wewe ni nani wa kunizuia mimi , sio mbaya hata hivyo nitaanza na wewe , nadhani itakuwa njia rahisi zaidi ya kuanza kisasi changu hapahapa”Alingea Lahan kwa hasira na Rufi alijiaribu kumshikilia kwa nguvu Bi Wema lakini chumba kilikuwa kishaanza kukumbwa na dhoruba ya upepo huku kelele kama vile ni sauti ya watu waliokufa ikisikika.
“Tafadhari kaka usmuue ni ..”XiaoXiao alitaka kumtetea Bi Wema ili kuzuia asimuue.
“Kaa kimya wewe , huna mamlaka ya kuongea mbele yangu , utapatiwa adhabu yako tukisharudi kwa kuficha ukweli kwa baba na mimi”Aliongea kwa hasira na kumfanya Xiao kuufyata.
“Master , mkuu wa ukoo ametuambia tumkamate Rufi tu na kurudi nae kimya kimya na hatupaswi kukiuka sheria kwa kuua binadamu, tafafhari fikiria mara mbilimbili unachotaka kufanya”Aliongea Mzee Lao na maneno yake yalionekana kuwa ya mantiki na palepale aliacha kile alichokuwa akipanga kufanya.
“Okey Mzee Lao nitakusikiliza na kumsamehe huyu bibi kizee”Aliongea na palepale alimsogelea Bi Wema na kumtenganisha na Rufi kwa nguvu na licha ya kutumia nguvu kidogo kwa Bi Wema alikuwa mwepesi sana kwani alikwenda kujipigiza kwenye ukuta na kupoteza fahamu palepale.
“Mamaa…!!!”
Rufi alijitahidi kufurukuta kujitoa kwenye mikono ya Lahani lakini ilikuwa ngumu na aliishia kutoa kilio , Lahani palepale alimwingizia Rufi nguvu ya kijini na kumchunguza na aliweza kugundua hakuwa bikra tena na kufanya uso wake kuzidi kujikunja kwa hasira.
“Kwahio tayari umelala nae , kwanini sumu tuliokutegeshea haijamuathiri ? hakuna mtu ambaye anaruhusiwa kugusa mwanamke ambae nilimkataa , kwasababu wewe sio bikra tena hakuna haja ya kugiza ndoa yetu kama makubaliano na ukoo wenu , kwanzia leo hii utakuwa kifaa cha majaribio ndani ya ukoo wetu kwa maisha yako yote”Aliongea kwa hasira mno.
Rufi aliishia kutoa machozi tu bila ya kuongea neno na uso wake ulimwangalia mama yake mzazi ambaye muda huo alikuwa hana fahamu,alitamani hata utokee muujiza akaangalie hali yake , hakujali anapelekwa ujinini alichokuwa akijali muda huo ni hali ya mama yake.
“Master ni muda wa kuondok, nimepotea ishara kutoka kwa Mkuu wa ukoo turudi mapema kabla uwepo wetu haujajulikana”Aliongea jini Lao na Lahani alitingisha kichwa na palepale alimshikilia vizuri Rufi na kisha alipotea nae na kumfanya Mzee Lao kuvuta pumzi za ahueni na palepale alimwangalia Bi Weka kwa sekunde na kisha alimshikilia XiaoXiao vizuri na kupotea palepale.
Alibakia Bi Wema ambaye alikuwa akitokwa na damu puani na mdomoni akiwa hana fahamu.
******
Upande mwingine ndani ya mgahawa mmoja maarufu unaopatikana ndani ya jijji la Dodoma alionekana Mzee Kweka pamoja na Roma wakiwa wameketi wakipata kifungua kinywa.
Upande wa Roma alionekana kabisa akili yake haikuwa imetulia kabisa, na kila saa alikuwa akiangalia karatasi iliokuwa kwenye mikono yake.
Nusu saa iliopita alikuwa ameenda kukutana na Master Namba moja kwa mara ya kwanza tokea asikie jina lake, kilichomshangaza Roma ni kwamba licha ya kwamba alikuwa na shauku ya kutaka kumuona Master namba moja lakini alishindwa kumuona kwa sura yake halisi.
Roma mara baada ya kukutana na Afande Kweka katika hoteli ya Highland iliokuwa ndani ya jiji hilo moja kwa moja waliepelekwa mpaka kwenye chumba maalumu ambacho kwa matarajio yao ndio sehemu ambayo wangekutana na Master Namba moja , lakini katika hali ya kushangaza ni kwamba Roma na Afande Kweka hawakuweza kukutana mtu ndani ya chumba hicho zaidi ya kusogelewa na wahudumu na kuambiwa wasubiri.
Walikaa ndani ya chumba hicho kwa zaidi ya nusu saa nzima bila ya Master namba moja kijitokeza , na ilimbidi Roma kupatwa na hasira na kuona pengine mtu huyo alikuwa akiwachelewesha kwa makusudi.
Wakati Roma aliopokuwa akipoteza uvumilivu ndio muda ambao alifika Raisi Senga ndani ya chumba hicho huku mkononi akiwa ameshika bahasha.
Raisi Senga aliishia kumwangalia Roma kwa macho ambayo hayakueleweka yalikuwa ya furaha au ya huzuni , ilikuwa ni kama vile kuna kitu ambacho kimetokea.
Roma na Afande Kweka wote walishangaa kumuona Raisi Senga nndio ambaye alifika ndani ya chumba hicho tofauti na Master Namba mmoja mwenyewe.
“Mzee msishangae , nipepewa jukumu la kuwakilisha masharti kwako kwa kosa ambalo umelifanya”Aliongea Raisi Senga huku akiwa na muonekano ambao ulikuwa na wasiwasi.
“Mashart, Senga unamaanisha nini , kwanini wewe ndio upo hapa?”
“Baba haya yote ni makosa ya Roma , familia ya Mzee Sharif sio familia ya kawaida na kilichonikuta sitaki kuweka wazi na nipo hapa kama mwakilishi tu”Aliongea na kisha palepale alimpatia Roma ile bahasha na Roma alitoa nyaraka ambazo zilikuwa ndani yake na kadri alivyokuwa akiisoma uso ulikuwa ukijikunja.
“Haiwezekani?””Aliongea Roma.
“Roma hiki ni kitu ambacho kipo ndani ya uwezo wako ,mtu ambaye unashindana nae sio wa kawaida na kama unataka kuendelea kuishi kwa amani pamoja na familia yako basi unapaswa kutimiza hayo masharti”aliongea Raisi Senga kwa kwa macho yake vile ilikuwa ni kama vile hana undugu na Roma na Afande Kweka , alikuwa yupo siriasi mno.
“Naataa kutii haya masharti , kama huyo Master Namba moja amekataa kujionyesha kwangu yeye mwenyewe basi siwezi kukubali huu ujinga , haya masharti yatanigharimu zaidi ya bilioni nne hela za kimarekani mnadhani hela zinaokotwa , hili swala lilitokea kwasababu familia ya Mzee Sharif ndio ilinianza”
Roma alizidi kuongea na kumfanya Raisi Senga kuzidi kuwa na hali ya wasiwasi.
“Roma nisikilize haya ndo masharti na mimi nipo hapa kama mwakilishi tu , hivyo ni wewe kutii ama kutotii lakini kama utaamua kukaidi lazima ujiulize je na uhakika unaweza kushindana na nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif”
“Ndio ninao uwezo wa kushindana nayo ,ameamua kujificha kwasababu ni muoga”
“Wala hajajificha kwa taarifa yako yupo hapa hapa tokea mlivyofika ila kwasababu ya uwezo wako mdogo hujamuona”
Aliongea na dakika ileile ni kama vile maneno yake yalibadili hali ya hewa kwani alianza kuhisi msisimko wa ajabu wa hewa ukianza kuongezeka ndani ya kile chumba na dakika chache mbeleni ni kama vile mtu ambaye ameshikwa na jinamizi kwani alianza kukosa hewa.
Mabadiliko yale yalimfanya hata Afande Kweka aliekuwa yupo kimya pembeni kushangaa mabadiliko ya Roma.
Haikuishia kukabwa tu shingo Roma alijihisi maumivu makali mno , alijaribu kuita Cauldron kudhibiti ile hali lakini mtitiroko wa nguvu zake ni kama vile umefungwa.
Roma alijikuta akipagawa na kujiuliza ni nguvu gani hioo ya kijini, alijitahidi kupambana na nguvu hio na ya kwake lakini ilionekana nguvu hio kuwa kubwa zaidi ya vile ambavyo amefikiria kwani iliweza kumshinda kirahisi sana.
“Nipo tayari kutii masharti”Roma alijikuta akiripoka mara baada ya kuona anazidi kuwa mnyonge na jasho jingi kumtoka na dakika ambayo aliongea kauli hio palepale nguvu ile ilimuachia na kumfanya kuwa huru na kupumua tena.
“Nini kimekutokea?”Aliuliza Afande Kweka ambaye ni kama sasa alikuwa amtoka kwenye mshangao.
Upande wa Raisi Senga alikuwa kwenye hali ya tabasamu tu , ilikuwa ni kama vile alifurahia Roma kuwa katika hali aliokuwa nayo.
Sasa kilichomchanganya Roma zaidi ni kwamba mara baada ya kutoka nje ya chumba hicho cha hoteli alishangaa kukuta eneo la nje hakuna ulinzi wa aina yoyote , yaani walivyofika na walivyotoka hali ilikuwa ileile , hata Afande Kweka mwenyewe alishangazwa na hali hio.
Roma palepale akili ilimcheza alijua mtu ambae alikutana nae sio Raisi Senga halisi , dakika ileile alirudi nyuma kwenda kuangalia ndani ya kile chumba ambacho walikuwemo lakini walikuta kilikuwa tupu na kuangaliana.
“Wewe mtukutu hebu nipatie hio karatasi”aliongea Afande Kweka na Roma palepale alimpatia Afande Kweka ile katarasi , isitoshe hata yeye alikuwa kwenye mshangao.
“Hii sio sahihi ya baba yako”Aliongea Afande Kweka.
“Mzee unamaanisha….”Aliongea Roma huku akimwangalia babu yake usoni na palepale Roma aliweza kuelewa nini ambacho amekutana nacho,mtu aliekuwa ndani ya kile chumba sio Senga pengine ndio Master namba moja mwenyewe ambaye amekuja kwa muonekano wa sura ya Raisi Senga.
Roma alianza kujiuliza kama ni kweli ni nguvu ya aina gani ambayo anatumia kiasi cha kumfanya ashindwe kumgundua ni feki , ijapokuwa alikuwa na walakini tokea mwanzo wa mazungumzo lakini hakukuwa na dalili za wazi za kuonyesha sio yeye.
Afande Kweka alionekana kama vile alijua muda mrefu na hakuonyesha hali ya mshangao na palepale alipiga hatua na kuondoka ndani ya hilo eneo.
Roma mara baada ya kutoka ndani ya hoteli hio walikuja kuingia ndani ya mgahawa mmoja kando ya barabara inayoelekea Singida na muda wote ambao walikuwa kwenye gari walikuwa kimya tu kila mtu akiwaza lake.
“Vipi bado hujapatana na Edna?” Alivunja ukimya Afande Kweka mara baada ya wote kuingia ndani ya mgahawa na kuagiza supu.
“Mzee unaniuliza kitu ambacho unajua tayari”Aliongea Roma na kumfanya Afande Kweka kunywa supu kidogo na kumwagalia Roma.
“Nimeamua kukaa pembeni na kukuangalia usidhani sijali ,nataka unipatie tarehe leo hii ni lini unemrudisha Edna nyumbani?”
“Nilimuahidi Edna sitomlazimisha kubaki na mimi , nitakachofanya ni kumjali pekee nadhani ndio kitu ninachoweza kufanya kwa sasa , kuhusu mambo meingine sitaki sana kufikiria”
“Hibi wewe ni mwanaume kweli?”Aliongea Afande Kweka kwa kufoka huku akionyesha hasira waziwazi kwenye macho yake.
“Mzee unajua kabisa mahusiano yangu na Edna yalivyokuwa na mkanganyiko haina haja ya kunifokea”
“Man up!!! , hilo sio tatizo , tatizo ambalo lipo ni kwamba wewe sio mwaminifu na una mtoto na mwanamke mwingine, naona ni tatizo dogo tu tofauti na ulichopitia dakika kadhaa zilizopita”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na kauli yake lakini alihisi ni kama yupo sahihi maana ile nguvu haikuwa mchezo.
“Nakujua upo vizuri sana kwenye kudanganya wanawake lakini kwanini swala dogo hili linakushinda , kwahio unataka kuniambia wanawake wote walikupenda baada ya kuwaambia kila kitu kuhusu wewe , kama jibu ni hapana basi kuna sababu nyingine ambayo imewafanya kukupenda ,hebu tumia ubongo wako huo, hata ni kwa kumdanganya hakikisha Edna anaendelea kuwa mkeo”Aliongea
“Mzee tatizo ni kwamba…”
“Usinipe visingizio vya kipuuzi maana havina umuhimu wowote kuliko mahusiano yako , sikutaka kuingilia maswala yenu ya ndoa kwasababu nilikuamini utayamaliza ndani ya muda mfupi lakini mpaka sasa hivi unayumba tu , mama yako anaweza kukuambia kuoa mwanamke mwingine lakini usije kumsikiliza , sitaki kuja kusikia eti tayari ushasaini makaratasi ya talaka”
“Inaonekana kama unanidhihaki vile maana ushaniona tayari nina uwezo mdogo , unafikiri nitayaingilia vipi maisha ya Edna?”
“Hebu acha kunikasirisha bwana , kama ungetumia asilimia kumi tu ya akili yako kama unavyoitumia kujifunza mafunzo ya kijini yote ya akili yako haya yote yasingetokea , kwanini unafanya maamuzi kama vile unamjua sana Edna , wewe sio Edna na anaonekana anakuigizia yule, unapaswa kuelewa wanawake wanaongea vitu ambavyo hawamaanishi na mimi najua zaidi yako, hebu fikiria tokea mtengane , vipi furaha yake imeongezeka au imepungua , vipi anaonekana kuwa na furaha kuliko mwanzo?”Aliuliza akiwa siriasi na kumfanya Roma kuona kweli maneno ya babu yake ni sahihi.
Tokea atengane na Edna hakuonekana kama mwanamke mwenye furaha kwa maelezo ya Bi Wema.
“Roma fanya chochote unachoweza kumuomba msahama , hata kama ni kumlilia, fanya chochote unachoweza akusamehe na umrudishe”
“Mzee sasa mbona unaongea mambo ya kutia aibu hivyo , yaani mimi na uanaume wangu nilie mbele yake anisamehe?”
“Mambo gani ya aibu , kwangu sijali kama uanaume wako utaathirika , ninachotaka ni kumuona umemrudisha na kuendelea kuwa mkeo , kama wewe ni mwanaume wa kweli unatakiwa kufanya chochote kile kumfurahisha mke wako , kama kweli mtafikia hatua ya kuachana hakikisha wewe ndio humpendi na sio kukuacha kwa sababu ambazo hazieleweki, unafikiri Edna nilimpatia ile bangiri bahati mbaya , nilimpatia kwasababu ilimchagua na sio vinginevyo , hivyo sitaki kusikilia sijui likipanda na likishuka nataka kuona anakuja kunisalimia nyumbani”Aliongea Mzee na kisha akasimama akionekana muda wowote anaondoka.
“Weka utaratibu wowote Lanlan aje kunisalimia nyumbani hata kama akiacha kwenda shule kwa siku kadhaa haina shida ana akili yule hata asisome, najua una mambo mengi kwasasa mimi nitaondoka , unajua mwenyewe namna ya kurudi”
“Mzee hebu subiri kwanza , unapaswa kulipia sina hata hela hapa”Aliongea Roma huku akimalizia supu iliokuwa kwenye bakuri lake na kisha kusimama.
Roma ni kweli hakuwa na hela alikuwa na kadi ya benki tu na Tanzania sio kama Ulaya kwamba unaweza kupitisha kadi na kulipia.
Afande Kweka hakuwa na hiyana alifanya malipo na ndani ya muda uleule alimpa ishara dereva wake na kusogeza gari na kuingia ndani na kumuacha Roma akiwa amesimama.
Upande wa Roma aliishia kusimama kwa muda huku akiwaza , siku hio ilikuwa ni ya ajabu kwake.
Mwanzoni Roma alijua kutokana na kurudiwa na nguvu zote na kupitia mapigo ya radi tisini na tisa basi ana uwezo mkubwa lakini siku hio ni kama amekutana na mtu ambaye alikuwa na nguvu kubwa kuliko yeye na kuona bado ana safari ndefu.
Hakutaka kuwaza masharti ambayo alikuewa amepewa kuyakamilisha ili kusamehewa kile ambacho amefanya.
Ukweli ni kwamba masharti ambayo amepewa yalikuwa yakimgharibu zaidi ya dolla bilioni nne za kitanzania lakini hakuona ni pesa nyingi , kitu pekee kilichomfurahisha ni kwamba huyo mtu anaejiita Master namba moja alionekana kutokuwa na uelewa juu ya Maimuna kuwa feki.
Hivyo Roma alijiambia atachukua utajiri aliopata kutoka kwa Masterr Wadudu na kisha ataunganisha na utajiri ambao ataupata kutoka kwa familia ya Mzee Sharif na kukamilisha masharti, alijiambia ngoja awe mjinga kwa muda huo asiongeze maadui na atakuja kupambana nae tu.
Baada ya kuwaza kwa dakika kadhaa aliona hatua inayofuata ni kumrudisha Edna kwenye himaya yake kwa namna yoyote ile , hakujua kwanini Mzee Kweka ameenda mbali na kuonyesha usiriasi wa Edna kuendelea kuwa mke wake lakini aliona ni sahihi kwani hata yeye hakuwa na nia ya kumpoteza.
SEHEMU YA 697.
Ilikuwa ni mchana na jua ndani ya jiji la Dar lilikuwa likiunguza kwa wastani.
Ilikuwa tayari ni jumamosi na mitaa mingi ya kibiashara ndani ya jiji hilo ilikuwa imejaa sauti za watu na makelele ya miziki na baina ya nyimbo ambazo zilikuwa zikisikika ni za Sophia.
Kurudi kwa Sophia kwenye kiwanda cha muziki ilimfanya umaarufu wake kuongezeka zaidi na zaidi, ilionekana skendo ambayo aliipata mara ya mwisho ndio iliomfanya kuzidi kuwa maarufu.
Ndani ya makao makuu ya kampuni ya Vexto licha ya kwamba ilikuwa jumamosi lakini wafanyakazi walikuwa wako bize kufanya kazi.
Tokea kampuni hio kuwa ‘International Corporation’ wafanyakazi wengi waliajiriwa ili kupunguza wingi wa kazi na kuongeza ufanisi.
Ukiachana na ule upendeleo wa kampuni hio kuajiri zaidi wanawake awamu hio warfanyakazi wengi ambao wameajiriwa ni wanaume pia , hata hivyo wahitimu wengi wenye ujuzi mbalimbali walikuwa wakipenda sana kufanya kazi chini ya kampuni ya Vexto, sio kwasababu tu ilikuwa ikilipa vizuri lakini ilionekana kama kampuni ambayo miaka kadhaa ijayo inakwenda kuwa kampuni kubwa ndani ya bara la Afrika , pengine na dunia kwa ujumla.
Upande wa wanaume ambao wameajiriwa kufanya kazi ndani ya makao makuu ya kampni hio walikuwa na furaha kweli kwani waliweza kupata fursa ya kuweza kuongea na warembo ambao wanafanya kazi ndani ya kampun hio.
Edna hakuwa bado amehamishia makazi yake katika jengo jipya ambalo lilikuwa katika hatua za mwisho kabisa kukamilika hivyo bado ofisi yake ilikuwa ikipatikana juu kabisa ndani ya jengo hilo ambalo lilikuwa likipatikana ndani ya eneo la Posta.
Kama ilivyokuwa kwa wafanyakazi wengine kuwa bize upande wa Edna alikuwa amesimama mbele ye kioo akiangalia upande wa nje ambao watu wake walionekana kuwa na pilikapilika.
Siku hio alikuwa amevalia suti ya rangi nyeupe na viatu vya skuna na kumfanya kuzidi kuwa mrembo licha ya kwamba alionekana kuwa mbali kimawazo.
Nyuma yake alikuwa amesimama Recho aliekuwa amevaa suti iliochora mwili wake vizuri na ilionekana alikuwa akitoa ripoti kuhusiana na kazi aliokuwa amepewa.
“Boss , maongezi ya kibiashara kati ya kampuni ya Kijerumani ya Collins Group yamefikia awamu ya tatu, bado wanalazimisha malipo ya Euro milioni mia tatu kwa mwaka, tunapaswa kuendelea vipi..”
“Ongea na wawakilishi wao Euro milionni hamsini ndio ofa yetu ya mwisho kama bado wanakataa hakuna haja ya kuingia nao mkataba mpya na haina haja ya kuwasubiria watoe majibu , wasilimiana na kampuni ya Hofferman na wapatie ofa hio hio”
“Sawa bosi , pia mkurugenzi msaidizi wa kampuni ya Lorrent, Mr Thompson amekueletea kadi ya mwaliko wa kuhudhuria tafrija fupi usiku wa leo katika hoteli ya Serena ambayo itaambatana na mazungumzo ya uwekezaji kuhusiana na mradi wa ujenzi wa makazi unaondelea Bagamoyo , anasema kama hautojitokeza wewe mwenyewe basi atachukulia kama huna nia ya kufanya nae biashara na atarudi Marekani siku inayofuata”
“Muache afanye anavyotaka , ongea na Chriss na mwambie awasiliane na mwenyeketi wa bodi , na awambie Thompson ana tabia ya hovyo na kama wanataka ubia uendelee wambadilishe haraka sana”Aliongea Edna na kumfanya Recho kuitikia kwa kichwa na kisha akafunika faili lake akionekana ashamaliza kutoa ripoti.
“Bosi nishamaliza kutoa ripoti , kuna kitu kingine ambacho unataka nikusaidie siku ya leo?”
“Hali ya hewa leo ni nzuri mno Recho”Aliongea Edna mara baada ya kimya kifupi na kumfanya Recho kuwa na mshangao kidogo lakini alishindwa kongea neno.
“Recho ushapata Lunch?”
“Hapana , ndio kwanza imefika mchana boss”Alibu Recho kwa wasiwasi kwani ni Swali ambalo hakutegemea kulisikia kutoka kwa Edna.
“Unaonaje tukienda kupata chakula pamoja,… nitalipia mimi”Aliongea Edna huku akiweka sawa nywele zake ambazo zilikuwa zimemfunika sikio kutokana na kuchanguka.
Recho ilikuwa mara yake ya kwanza kuambiwa na Edna kwenda kupata wote chakula cha mchana , alijua Edna muda mwingi alipenda kufanya kazi na ni mara chache alikuwa akitoka nje ya jengo hilo kwa ajili ya chakula cha mchana.
“Nipo tayari Madam , unataka tupate chakula sehemu gani , nitaendesha mimi gari?”Aliongea Recho.
“Hakuna haja ya kuendesha gari leo , nataka kupanda yale magari ya mwendokasi”Aliongea Edna huku akinyooshea kidole gari la mwendokasi ambalo linashusha watu kituoni.
Kauli yake ilimuacha Recho kinywa wazi akiwa kama hajasikia vizuri na paepale alipotezea mshangao wake.
“Bossi kwani haujisikii vizuri au ni kutokana na kuwa na mawazo?”Aliuliza Recho.
Ukweli ni kwamba hakutaka kuamini kama Edna anaweza kupanda mwendokasi , alikuwa na uhakika tokea mwendokasi uje ndani ya jiji la Dar kama usafiri wa uma , Edna hajawahi kupanda lakini sio hivyo ni ngumu kwa mwanamke tajiri kama Edna mwenye zaidi ya Dola bilioni ishirini kupanda magari ya uma.
“Recho unafikiria nini ,tunaenda au hatuendi?””
“Ah ,,, tunaenda bosi , nisubiri kidogo naenda kuweka hivi vitu nakuchukua mkoba wangu”Aliongea Recho na palepale alitoka kwa kukimbia kwenda nje kuweka vitu vyake
Dakika chache mbele Edna akiwa anakodolewa macho na wafanyakazi aliweza kutoka nje ya jengo hilo akiwa ameambatana na Recho.
Wafanyakazi ambao walikuwa nje walijikuta wakishangazwa mara baada ya Recho na Edna kuelekea kituo cha mwendo kasi na kukata tiketi.
Edna hakujali wanaomwangalia na mara aada ya kuchukua tiketi mbili alimpatia Recho na wote kwa pamoja waliingia ndani ya eneo la kusubiria gari na bahati nzuri gari haikuchelewa na haikujaza sana na wote walipanda gari hio inayoelelekea Morocco.
Recho alikuwa akifuatisha tu maana hakujua ni wapi wanaelekea na bosi wake na mara baada ya kufikishwa Morocco Edna aliita taksi na wote wakaingia na Edna alitoa maelekezo ya kuepelekwa upepo Beach.
Na hapo ndio sasa Recho alijua ni wapi wanaelekea , lakini alifurahi na yeye pia mara baada ya kuona wanaelekea Upepo Beach , ni moja ya eneo ambalo anapenda sana kutembelea ikiwa wikiend.
Haikuwachukua dakika nyingi mpaka kufika na wote walishuka nje huku Edna akiangalia mazingira.
“Unapaonaje hapa Recho , tutakula hapa na kupunga upepo kidogo”Aliongea mara baada ya kumlipa dereva.
“Ni pazuri mno na pametulia”Aliongea Recho akitoa tabasamu , hakuwa akielewa kwanini Edna kaamua kuja mbali hivyo kwa ajili tu ya chakula cha mchana kwani kampuni ilikuwa mbali sana lakini hata hivyo alifuata nyuma nyuma kuingia ndani ya eneo hilo huku akiwa na hamu ya kupata Seafood.
Ilikuwa ni wikiend na eneo lilikuwa na watu wengi licha ya kwamba ilikuwa mchana bado.
Edna alikuwa ni kama amekariri eneo hilo kwani mara baada ya kuona sehemu ambayo alikaa na Roma mara ya mwisho alitoa pumzi ya ahueni na kunyoosha kidole akimwashiria Recho ndio wanapoenda kukaa.
Wahudumu wa eneo hilo walishangazwa na uwepo wa Edna lakini haraka haraka waliomba kuwahudumia.
Edna aliagiza aina ya chakula kilekile ambacho Roma alimwagizia mara ya mwisho na Recho na yeye alichagua hichohicho.
“Leo sio kitamu kama mara ya mwisho nilivyojaribu kula nikiwa na Roma…”Aliongea Edna huku akionyesha hali ya kukosa hamu ya kuendelea kula.
“Boss naomba niwe muwazi kwako , najua kabisa unampenda mume wako lakini kwanini unamkwepa tofauti na kukaa chini mkayamaliza, mimi na wafanyakazi wengine ndani ya kampuni tunakuchukulia kama Role model wetu , kwasababu wewe ni mwanamke mwenye maamuzi na ngangari na ndio maana umetufikisha leo tulipo lakini kwanini unakimbia changamoto za maisha yako binafsi, umenileta mbali hivi najua yote ni kutokana na kushindwa kumsahau Roma”
“Recho sio rahisi hivyo , maisha ni tofauti na biashara , kwenye biashara kama nitafeli na kampuni kufirisika naweza kuanza upya maadamu nitakuwa hai na ndio maana siogopi changamoto za biashara lakini kwenye maisha ni tofauti , kuna baadhi ya vitu kwenye maisha huwezi kubahatisha kwasababu ukipoteza ndio umepoteza na siwezi kurudisha muda nyma ndio maana nakuwa muoga”
Aliongea Edna na kumfanya Recho kushindwa kuongea neno lololote , mwanzoni alikuwa akimuonea wivu sana kwa kujaliwa uzuri , busara na mapemzi lakini kwasasa licha ya kwamba bado alikuwa akimuheshimu kutokana na uzuri wake na busara zake lakini aliona mapenzi ni kitu ambacho ni kama hakimpi furaha.
Wakati wakiendelea kuwa bize na chakula muda huo huo alionekana mtu mwingine akisogea upande wao kukaa nyuma yao.
“Wewe utakuwa ni mjinga sasa , na siku zote nakuambia hivyo, maisha ni sehemu ya mchezo wa kubahatisha , ndio unaweza kusema hutaki kubahatisha lakini usipofanya hivyo ni sawa na kujihukumu kwani hutokuwa na furaha hata kidogo”
Sauti ilisikika pembeni yao na kumfanya Edna kushikwa na mshangao kwani ni sauti ambayo alikuwa akiijua na mara baada ya kugeuza uso wake aliweza kumuona Roma akiwa na tabasamu kama kawaida yake.
“Wewe.. kwanini upo hapa??”
Hata Recho alikuwa kwenye mshangao na Roma hakujali mshagao wao na alienda kukaa kwenye meza yao.
“Niliwaona mkitoka nje ya kampuni na kupanda basi , sikujua mnaenda wapi hivyo niliwafuatia nyuma nyuma mpaka hapa , babe sijui ni jambo gani unannificha lakini siamini kama hunipendi na hujanimisi”
Edna alijikuta akiona aibu, maana alikuwa amekamatika na hakujua namna nyingine ya kuficha hisia zake.
Roma alikuwa mwepesi alichukua samaki palepale na kumtoa miba na kisha kumpa ishara Edna kuachama ili amlishe
Muda huo Edna mara baada ya kugeuka kuangalia pembeni aligundua watu wengi walikuwa wakiwaangalia kwa macho ya uchokozi hata Recho aliokuwa nao meza moja alikuwa akimwangalia kwa macho ya kichokozi.
“Unafanya nini wewe…, huoni watu wanatuangalia”Aliongea Edna kwa tahadhari.
“Wakiangalia ndio ndio , wewe ni mke wangu na naruhusiwa kukulisha , kama kuna ambaye hapendi nikimlisha mke wangu nitamfukuza hapa”Aliongea Roma kwa sauti kama vile anataka kila mtu asikie .
“Mimi , sitaki tupo kwenye mchakato wa talaka”Edna alijifanyisha kauzu lakini mashavu yake yalimaanisha kitu kingine na kumfanya kuzidi kupendeza kiasi cha kumfanya Roma kutoa kicheko.
“Wife hujui hata kuigiza hasira?”
“Mimi…”Edna hata hakujua namna ya kujitoa kwenye hio hali , hakutaka juhudi zake za kumuigizia Roma zipotee kirahisi hivyo kwa kipande cha samaki.
Upande wa Roma alipanga siku hio kuhakikisha anayamaliza na Edna kwa namna yoyote ile kama alivyoambiwa na babu yake, ilikuwa bahati kwamba Edna alitoka mwenyewe kwa ajili ya chakula cha mchana lakini mpango wake ni kufanya tukio ndani ya kampuni.
“Hey binti hebu kula basi , mumeo anajitahidi kukubembeleza vyote hivyo”Sauti ya mzee aliekuwa na mke wake pembeni walishindwa kuvumilia.
“Hehe ugomvi wa kimapenzi huo na ndio raha yake, hebu kula na wewe usimkasirikie tena , nyie ni wenza hii ndio sehemu ya kuyamaliza”Mke wa yule mzee alimuunga mkono mume wake na kumfanya Edna kuwa mwekundu kutokana na uchokozi wao.
“Ndio mpenzi wangu, sijali unasababu ya aina gani inayokufanya kunikasirikia lakini huna haya ya kuniambia na sitokulazimisha , sitaki kuigiza na kuonekana mtu mzuri mbele yako , najua mimi ni mbinafsi linapokuja swala lako , sitaki kusikia visingizio vingine na sitaki kujidanganya pia kwani najua hisia zako juu yangu na mimi najua zangu juu yako”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumpiga kibao mkono ulioshikilia samaki .
“Unajua hisia zangu kivipi wewe , nimesema sikutaki tena na usinisogelee tena”Aliongea huku akitoa machozi na palepale alisimama na kukimbilia ufukweni na kumfanya Roma kushikwa na bumbuwazi.
“Hey stop sitting there ! Go after her” Mwanaumke mmoja wa kizungu aliekuwa amekaa mita kadhaa ni kama alikuwa akijua kinachoendelea na kupendezwa na drama hizo za kimapenzi.
Roma na yeye ni kama akili yake imeshituliwa na alisimama na kumkimbilia Edna na mara baada ya kumfikia alimkumbatia kwa nyuma akipitisha mikono yake kifuani.
“Niachie mimi bwana….”
Aliongea Edna huku akitaka kumng’ata Roma mkononi lakini hakuweza kuufikia na kuishia kufurukuta huku mikono yake ikisuguana na manyonyo yake .
“Siwezi kukuachia tena kwanzia leo hii”
“Wewe … Roma niachie bwana .. nishakuambia hatuwezi kuendelea kuwa pamoja”
“Edna siwezi kukuachia , nataka kuendelea kuwa mumeo na wewe kuwa mke wangu , hakuna kitu ambacho kinaniogopesha kwenye ulimwengu huu kama kukupoteza”
“Roma nakuambia utaumia na unaweza kufa ukiendelea kuwa na mimi, huogopi?”Aliongea Edna na kauli yake ilimfanya Roma kucheka kama kichaa.
“Edna nadhani hunijui vizuri , mimi siogopi kifo , hata kama nikifa leo angalau najua sijapoteza maisha yangu bila sababu , Kwangu kitu pekee ninachoogopa kwenye huu ulimwengu ni kukupoteza wewe kipenzi changu , kwasababu najua hata kama nitakuwa naendelea kuishi bila wewe lakini moyo wangu utakuwa umekufa”
Kweny group la whatsup ilishaisha muda mrefu mcheki akutumie uondokane na arostoKusoma simulizi za kutunga nazo kipaji.
Na alituahidi itaisha siku ya Eid Al fitrialisema ni ijumaa ila akugusia ni ya mwezi upi.tuwe wavumilivu na wanasiasa wetu