singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,454
- 8,120
- Thread starter
- #3,401
NILIMDHANI A KAHABA KUMBE BIKRA . MTUNZI: DR SINGANOJR
Mono no aware
SEHEMU YA 637.
Roma alijisikia maumivu makali kwenye moyo wake , hakuwahi kuwaza Edna anaweza kupotezea ndoa yao kirahisi namna hio huku yeye akiwa hayupo tayari ,lilikuwa swala la kushangaza kwake.
Ilimshangaza kutokana na kwamba ilionekana kabisa Edna alikuwa akimpenda Lanlan licha ya kwamba alikuwa akijua sasa kuhusu wazazi wake, lakini Roma alijiuliza inakuwaje anataka kuacha kila kitu.
Roma alijiambia hapana ni kweli amemumiiza lakini haikuwa ikimaanisha washaachana , pale pale alimgeukia mama yake.
“Mama mchukue Lanlan”Aliongea Roma.
Upande wa Blandina awamu hio alikuwa na shauku ya kumbeba Lanlan kweli,ilikuwa ni kama mara ya kwanza kwake kumbeba, lakini yote hayo yalitokana na hisia zake kubadilika juu ya Lanlan mara baada ya kumjua sasa ni mjukuu wake kamili , hakujali nani amemzaa Lanlan na alichojali muda huo ni kwamba Lanlan ni mtoto wa Roma, kwake aliona ni kama baraka kubeba damu ya Roma mkononi mwake.
Afande Kweka aliishia kumwangalia Lanlan aliekuwa kwenye mikono ya Blandina na misuli yake ya macho ikacheza , pengine kama angekuwa na Zenzhei basi angetoa cheko kubwa kwani ndio watu wawili pekee waliokuwa wakiujua ukweli kuhusu Lanlan.
Afande Kweka hakujali sana kuhusu Edna , kwake Lanlan alikuwa muhimu zaidi kuliko Edna ambaye alikuwa ni mwanamke mgumu sana.
“Edna kwa sasa ana hasira sidhani kuongea nae katika hali yake kunaweza kuleta majibu , kwanini usimuache kwanza kwa muda , ni mtu mzima na hakuna baya litakalo mkuta, akitulia utaongea nae”Alishauri Blandina.
“Mama tulia ,siamini kama Edna ni mkatili kiasi cha kutaka kumalizana na mimi bila ya kunisikiliza”Aliongea Roma na hakutaka kupoteza muda na alitoka nje .
Roma mara baada ya kutoka alifanikiwa kumuwahi Edna nje ya geti na Roma baada ya kumfikia alimshika mkono kumzuia.
“Niachie mimi , sitaki kukuona tena”Aliongea
“Mimi siamini , kwanini unataka kuvunja uhusiano wetu uliodumu kwa zaidi ya miaka miwili kirahisi hivyo?”
“Roma nadhani kuna kitu umesahau?”
“Nini ?”
“Unakumbuka makubaliano yetu siku ambayo tuliingia dili la mimi kumlea Lanlan??”
“Unazungumzi… unamaanisha yale makubaliano ya miaka miwili ya mdomo?”Aijiuliza Roma huku akiwaza na kuona ni kama ujinga na kujiuliza hata kama ni kweli walikubaliana kwanini huyu mwanamke kila kitu kwake anajali makubaliano tu.
Ni kweli Roma alikubaliana na Edna lakini siku ile hakuzingatia maneno yale kwani waliyaongea katikati ya kutaniana.
“Nilikuambia kabisa ukinichokoza kwa kuruhusu matatizo ya wanawake wako kuniathiri ndio mwisho wetu , je umesahau?”Roma alijikuta akiwa kama haelewi , ukweli ni kwamba makubaliano hayo hayakuendana kabisa na kinachoendelea hapo.
Asichokuwa akijua Roma kwa wakati huo anachomaanisha Edna ni swala la Salihi kumpigia simu Edna na kuanza kumtishia.,
“Wewe ndio Roma unaejuliakana kama mtoto pekee wa kiume wa kuendeleza familia ya ukoo wenu , Mfalme Pluto , Hades , naamini huwezi kuvunja ahadi yako?”Aliongea.
Roma licha ya kwamba hisia zake zilimwambia tukio la leo halikuwa likiendana na makubaliano yale lakini alijua pengine kuna maongezi mengine ambayo amesahau na wakati huo kila ambacho Edna alikuwa akiongea alijiona alikuwa na makosa.
“Roma nishachoka muda mrefu , kama isingekuwa kuvumilia kwa ajili ya mpendwa wangu Lanlan nisingefikiria hata kufika hapa , lakini sio mbaya sasa hivi Lanlan ashajulikana ni mtoto wako wa kumzaa hivyo simuhitaji tena , ninataka kurudi katika maisha yangu ya mwanzo kuliko kuendelea kuzungukwa na mtu ambaye moyo wako unaugawa kila mahali”
“Unaongea upuuzi , wewe sio mwanamke wa kawaida na huwezi kurudi kwenye maisha yako ya mwanzo”
“Najua pengine unaona nitakuachaje licha ya kwamba tumelala pamoja na kufanya mapenzi mara nyingi , si ndio?, usiwe mjinga mimi pia ni mwanamke wa kawaida ambaye nahitaji mwanaume wa kunituliza , siwezi kukataa ukweli kwamba wewe upo vizuri kitandani lakini hilo pekee sio la kunibakisha kwako , It’s just the toxic hormones doing its job”Hakusita kuongea hayo maneno tena akimalizia na neno la Kingereza.
Roma aliguswa mno na maneno hayo na alitamani hata kuziba masikio ake , ilikuwa ni kama vile kumbukumbu zote walizotengeneza na mwanamke huyo zimegeuka kuwa kitu kisichokuwa cha maana.
“Hakuna zaidi ya vitu viwili ambavyo mwanamke anavitaka kutoka kwa mwanaume , cha kwanza ni mapenzi ya kweli na cha pili ni matunzo , mimi Edna Adebayo hela za kujitunza ninazo , lakini mapenzi yako ya kimanyanyaso hayakidhi mahitajio yangu ya kihisia , hivyo ni rahisi kwa wewe sasa kuelewa kwamba ninakuacha na pengine ulipaswa kujiandaa kwa hii siku”.
Baada ya kumaliza Edna aligeuka na kutaka kuingia kwenye gari lakini Roma palepale alilipiga teke na hasira zake pamoja na mdudu wake aliekuwa ndani yake ni kama alishituliwa na nguvu iliotumika ililifanya gari lile kupinduka.
“Roma unafanya nini?” Edna aligeuka kwa hasira akimwangalia Roma.
“Hmmp..”Aliguna na palepale alibadilika na kutoa tabasamu la kifedhuli na kumwangalia Edna kwa ujeuri.
“Edna , ukiburi wako , kujitegemea kwako na kujiamini kwako vinatokana na hali yako ulionayo sasa hivi kitu ambacho ni tofauti na nyuma , Sasa hivi huna haja ya kudili na washindani wako wa kibiashara na huwezi kumuona tena baba yako wa kambo ambaye alikuwa akifanya hali yako kuwa ngumu, huna haja ya kuogopa wale majambazi wanaotaka mwili wako kwasababu una hela, nguvu na Koneksheni na sasa pia umekuwa mtu mwenye uwezo hata wa kupigana … sasa nakuambia hivi kama bado unataka kuchezeana akili na wanafiki ambao hata mwanzoni huku wajua na wakakuingizia kwenye hatari basi nakuruhusu fanya kama mwanzo uone, fanya michezo yako ileile ya kibiashara na hila zingine tuone kama unaweza kunikataa mimi mume wako kwa kiburi namna hio, Kwahio unasema kwamba hali yetu ya kindoa inabadilika kulingana na hali yako uliokuwa nayo pamoja na hadhi yako?,
Hicho ndio unachojaribu kuniambia sasa hivi?”Aliongea Roma na palepale alijipiga kifuani mara mbili ishara ya majivuno.
“Ndio , Mimi Roma Ramoni nina uwezo wa kupata kila ninachohitaji katikadunia hii, Mimi ni tajiri na pia nina nguvu na ninao uwezo wa kufilisi matajiri wakubwa zaidi ya mia tano kirahisi sana tena ndani ya siku moja na sio hivyo tu ninao uwezo wa kuvamia nchi na kuiweka chini yangu ndani ya siku moja , ninao uwezo wa kufanya mambo ambayo ni nje ya fikra za binadamu ili mradi nataka kufanya hivyo , Kiwango cha utajiri wangu , nguvu zangu na uwezo wangu unaweza kuvutia idadi ya watu wasiohesabika , nina ujuzi ambao unawafanya watu kuwa na wivu lakini kwa wakati mmoja wakashindwa kuiga wala kujifunza , lakini hayo yote nimeyapata hatua kwa hatua bila kupotezea fursa , ni vitu ambavyo nimevipata kupitia jasho langu , kupitia maisha yangu.
Hebu jiulize kama ningekuwa Roma mwanaume masikini ambaye naishi kwa kipato cha siku , au ningekuwa mwanaume wa nyumbani tu nisie na uwezo wowote ungeendelea kuwa na mimi , naamini usingeweza hata kuniangalia usoni mara baada ya mkataba ule wa miezi sira kuisha , usingefikiria mara mbili mbili hata kunisogelea na kulala na mimi kitanda kimoja , umeweza kufika hapa leo na mimi na kunivumilia miaka yote hiyo kwasababu ya kitu nilichokuwa nacho , ulijua kuendelea kuwa na mimi ingekusaidia katika vitu vingi , there is no love for no reaseon and no hate for no reason.
Ninakuambia hivyo kwamba mimi sio aina ya mwanaume ambae ninaweza kukusindikiza kwenda kazini kwanzia asubuhi mpaka jioni , wala kukuita CEO Edna ili kukupa heshima yako , mimi ni mwanaume ambaye siwezi kukusubiria kurudi nyumbani nianze kukunyenyekea na kuanza kukufanyia masaji na udambidamwi mwingineili tu kukufurahisha kama vile wewe ndio mwanamke mmoja tu ndani ya dunia hii , mimi ndio mimi na najulikana tokea nikiwa mdogo kwa msimamo wangu , Mtu dhaifu atakuwa mawindo ya mwenye nguvu , mwenye nguvu siku zote ni mtawala , hivyo unapaswa kujua mimi nina nguvu kuliko wanaume wengine na hiki ndio nilichokuwa nacho , ndio sifa yangu kubwa , nina wanawake wengi wa kuwajali na sina mpango wa kumuacha hata mmoja , hivyo ndio ilivyo na siwezi kugeuka nyuma , kama kweli unanipenda basi nikubali na uendelee kuishi na mimi.”
“Hivi unajua mtazamo wako wa uwazi na ujasiri wako utamfanya mtu asieogopa chochote mbele yako aonekane ni mnyonge?”Aliongea Roma kwa sauti huku akimwangalia machoni bila kupepesa.
“Sawa na mtazamo wako wa kifalme, lakini kwangu mimi sitaki kuendelea kuishi katika hali ya unyenyekevu na unyonge”Aliongea Edna.
“Kwani vipi , unapaswa kujua hakuna usawa kwenye ulimwengu huu , mimi nina nguvu ndio maana nina kundi la wanawake wanaonizunguka kwa hiari zao wenyewe , ulikuwa ni wewe mwenyewe ambaye ulisema hutojali na sasa unasema mimi nachukiza , ndio, najua kwamba nina deni kubwa kwako lakini je huna hata punje ya hatia ya uwajibikaji?, Unataka nifanye mangapi kwako ili nionekane ni wa thamani?”
“Haina maana kuongea hivyo kwa sasa , kama hao wanawake wako wanataka kuendelea kukaa na wewe basi ni juu yao , ndoa yetu ambayo ilianzia kama mkataba inaishia hapa , nilijituma pia na kujitoa kwako kama unaona haitoshi basi nakuruhusu nilazimishe kwasababu una nguvu nibakie kwako , lakini nimemaliza na siwezi tena kwa hiari yangu kuwa mkwe wa familia ya ukoo wa kweka kwani siwezi kuendelea kuwa mkeo , kama kweli wewe ni mwanaume mwenye nguvu na jasiri basi hutoshindwa kuniacha mwanamke mnyonge kama mimi nikichukua njia zangu , hatukuweza kuendana vizuri ndani ya ndoa yetu hivyo tunapaswa kuachana kwa amani..”
Aliongea Edna akiwa hana chembe ya hasira na kumfanya Roma kumwangalia kwa muda na kisha akavuta pumzi yake na kuishusha na akaingiza mkono kwenye mfuko wake na kuibuka na ufunguo wa gari wa BMW na kumuwekea mkononi.
“Unaweza kwenda , lakini sipendi kuona mwanamke ambaye nishawahi kuwa nae akimilikiwa na kufurahiwa na mwanaume mwingine … unaweza kusema mimi ni mnyama au shetani na sitojali lakini nakushauri tu usije kuthubutu kuwa na mwanaume mwingine kwani nakuhakikishia nitamuua na akijitokeza mwingine itaendelea hivyo hivyo..”
Baada ya kusema hivyo Roma aligeuka na kuingia ndani ya geti pasipo kugeuka nyuma na kivuli chake kilipotelea ndani akiwa katika hali ya upweke.
Edna alijikuta akiwa amesimama bila kusogea , maneno yake ya mwisho ambayo yalikuwa kama onyo yalimshangaza , alijikuta akivuta pumzi na kushikilia ufunguo wa gari uliokuwa kwenye mikono yake kwa muda na kisha aligeukia gari ambayo imeegeshwa kando ya geti.
Haikuwa ikieleweka anaenda wapi , lakini moja kwa moja ilieleweka hakuwa tena na sababu ya kukaa tena Iringa.
Baada ya kuingia barabara kuu aliendesha kuelekea mjini , ilikuwa ni usiku sana na giza limetawala na alikanyaga pedeli kwa nguvu na kusonga mbele na kuifanya gari hio kutoa mngurumo kama wa mnyama alieona kitoweo.
Spidi ya mwendo wa gari hio ni kama ilikuwa njia pekee ya kutuliza wasiwasi wake na maumivu na kilichoonekana ni michirizi ya machozi ambayo ilishakauka kuanza tena kupitisha maji.
Ghafla tu palepale alijikuta akihisi maumivu makali kwenye moyo wake na maumivu yale yalishitua kichwa chake na alijikuta akihisi maumivu makali ya kichwa yalioambatana na kengele kwenye masikio huku macho yakianza kuingiwa na ukungu wa kutokuona mbele.
“Pipiiii … Papaaaa…..!!!”
Ilikuwa ni gari iliobeba mbao iliokuwa mbele yake ikipiga honi kwa nguvu ikimwashiria Edna kupunguza mwendo na kutoka katikati ya barabara.
SEHEMU YA 638.
Ilikuwa ni bahati kwake kwani akili yake iliweza kurudi haraka na alifanikiwa kuzungusha usukani kwa nguvu na kukwepa gari ile.
Baada ya kujiimarisha katika usukani alijikuta akishindwa kujizuia tena na palepale jasho lilianza kumtoka kwenye paji la uso wake na alijikuta akianza kulia kwa kwikwi kiasi cha machozi ya chumvi kuingia kwenye midmo yake.
“Honey .. I’ m sorry … this is last thing ,, that I can do for you..”Alionekana kuongea akimaanisha kwamba ni kitu pekee ambacho anamfanyia Honey wake.
Lakini licha ya sauti yake hio , kutokana na upepo pamoja na ngurumo ya gari sauti yake haikuweza kusikika, isitoshe hakuna ambaye alikuwa akimsikiliza kwa wakati huo.
*****
Roma mara baada ya kuingia eneo la sebuleni alionekana kama mtua mbaye hakuna chochote ambacho kilikuwa kimemtokea , aliweza kutoa tabasamu lake hafifu na kisha akaenda kukaa mezani kwa ajili ya chakula.
Alipoulizwa kilichotokea alisema tu bila ya kuonyesha wasiwasi kwamba Edna amemua kutalakiana nae.
Tabasamu lake na utulivu ilifanya kila mtu aliekuwa akimwangalia kumuonea huruma mno , walijua ni kwa kiasi gani Roma anampenda Edna hivyo kuonyesha tabasamu ni shara ya kuficha maumivu.
Ukweli ni kwamba maumivu ambayo alikuwa akiyasikia hayakuwa yakivumilika , lakini licha ya hivo Roma hakuwa mtu dhaifu , hakuwa mtu ambaye ni wa kutaka kufarijiwa katika matatizo yake kwa kuonewa huruma.
Wanafamilia hao na wenyewe walionekana kujua mpango wake kwani hawakuongea chochote zaidi ya kuongea topiki tofauti.
Hakuna ambaye alitaka kuhoji kosa ni la nani au kumuuliza kama angejaribu kuokoa ndoa yake , hakuna ambaye alikuwa mjinga mpaka kufikia hatua hio.
Baada ya Show ya Sophia kuanza kila mmoja alikaa kwenye masofa na kuangalia kama vile ni familia ya kawaida ambayo maisha yao ni ya furaha.
Upande wa Lanlan wakati Roma anaingia aliangaza macho yake kila saa mlangoni kuona kama mama yake ataingia lakini hakuweza kuona kitu na aliishia kuwa na huzuni na hali ya kujikatia tamaa.
Lanlan hakuwa akielewa kwa undani hali halisi lakini aliweza kuhisi baba yake alikuwa na huzuni mno hivyo hakunyanyua mdomo wake na kuuliza mama yake yupo wapi.
Baada ya kumuona Shangazi yake Sophia kwenye runinga akiimba macho yake yalichanua na kusahau huzuni yake kwa muda.
Ilikuwa ni kama Sophia alivyosema ,ilikuwa ni kama hakuna ambacho kimetokea , aliweza kuonekana katika steji akivutia mno na vazi lake la kimtindo , huku kuimba kwake na namna ambavyo anacheza , ukijulimsha urembo wake ulipagawisha watu na kilichosikikika ni sauti za watu kushangilia.
Kwa jinsi watu walivyoweza kujaa pamoja na ‘engagement’ ya tukio hilo ilidhihirisha kitengo cha ‘Public relation’ kilivyokuwa imara .
Kuanzia namna ambavyo ujio mpya wa Sophia kwenye tasnia ilivyokuwa ukisambaa kwenye mitandao ilikuwa ni jambo la ya kushangaaza mno, ilikuwa ni kama vile wale ‘influencers’ wakubwa kwenye mitandao walikuwa wamelipwa kufanya hivyo, kuongea topiki inayohusiana na Sophia pekee.
Lanlan aliekaa alijikuta na yeye akionyesha furaha yake na kusimama na kupiga makofi huku akianza kumwigizia Sophia anavyoimba mpaka mwisho.
Baada ya Show kuisha wanafamilia hao walianza kumuuliza Roma kuhusu maisha ya Seventeen , mama mzazi wa Lanlan na Blandina alijikuta akisikitishwa mno na jambo hilo na kumuonea na Lanlan maisha yake yalivyokuwa mpaka kuja kumpata baba yake na Blandina alijiambia atachukua nafasi hio kumjali mjukuu wake ili tu kumsaidia mtoto wake kupunguza hatia aliokuwa nayo moyoni.
Upande wa Afande Kweka licha ya kwamba kila kitu kilianzia kwake , lakini kusikia stori fupi ya
Seventeen hatia na yenyewe haikumuacha salama, lakini kwa kujua kwamba Edna na Seventeen ni ndugu hakutaka kutia neno lolote.
Ijapokuwa Edna alisema anaachana nae kwa maneno lakini upande wa Roma hakutaka kuendelea kubakia mkoani Iringa na aliaga kabisa siku inayofuata angeondoka na Lanlan, lakini kabla ya hapo alipaswa kwanza kwenda Kigombola Medical Research institute kumtafuta Clark ili kujua matokeo ya uchunguzi wake wa kiafya.
Asubuhi yake wakati Roma na Lanlan wanataka kuondoka , waliweza kupokea ugeni wa Neema Luwazo aliekuwa ameambatana na binti yake Donyi.
Wazazi wa Neema Luwazo walikuwa na ukaribu na Afande Kweka hapo mwanzo na alifika hapo kwa nia ya kumsalimia kwani ni miaka mingi hajawahi kukutana nae, lakini ukiachana na hilo alionekana kama mwanamke ambaye ni kama alikuwa akijaribu kutafuta nafasi yake kama mojawapo ya wanawake wa Roma katika familia hio.
Afande Kweka alifurahi pia kuwaona na alipendezwa na namna Donyi alivyokuwa mkubwa , ijapokuwa ni mtoto wa marehemu Kigombola ambaye alikuwa ni hasamu wake kwenye baadhi ya mambo lakini hakuwa akimchukia Kigombola , wazungu wanasema hakuchukulia utofauti wa mitazamo yao kuwa ‘personal’ .
Roma alimuuliza Neema Iringa anafanya nini na Roma alishangaa mara baada ya kujua Neema alikuwa ni mbunge wa viti maalumu mkoa wa Njombe.
Roma hakuwa na uwelewa na maswala ya kisiasa sana hivyo siku zote alikuwa akijua Neema Luwazo alikuwa ni naibu waziri na mbunge kwa wakati mmoja.
“Neema nimesikia kuna kaka yako ambaye anasimamia biashara zako Urusi ni kweli?”Aliuliza Afande Kweka.
“Ndio , anaitwa Msechu amerudi juzi nchini kwasasa yupo Dar es salaam kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa mwaka na atarajea kazini Janauri”
“Oh..nadhani ni vyema vijana wakaenda kuishi nje ya nji uli kujua ulimwengu vizuri … nimesikia habari za jeshi letu kuwa katika mazungumzo ya kusafirisha silaha kutoka Urusi kuja Tanzania mwaka ujao katika muda wa nusu mwaka , biashara yako inafanya vyema nchini Urusi kuliko kampuni yoyote hapa nchini , nadhani hili ni swala zuri kwa taifa..”Aliongea na kumfanya Neema macho yake kuchanua , alikuwa ashaelewa ni taarifa gani Mzee Kweka anajaribu kumfikishia.
Ukweli ni kwamba mataifa mengi ya Afrika yalikuwa yakitumia fursa ya Vita inayoendelea kati ya Urusi na Ukraine kununua siraha kwa wingi kuingia nchini, ilikuwa ni fursa kwani vita ilikuwa ni kama mpango wa Urusi kupumbaza mahasimu wake wa kibiashara ili kuweza kuuza zaidi na zaidi siraha katika mataifa yaliohitaji bila ya kushitukiwa na Marekani kwa kivuli cha kusaidia mataifa hayo Nafaka.
Ilikuwa ni ngumu Kwa Neema kujua mchakato wa serikali katika kuagiza siraha kutoka nje ya nchi na watu ambao walikuwa na koneksheni za aina hio ni kama Afande Kweka ambaye mzizi yake ndani ya jeshi ilikuwa mirefu sana hivyo alikuwa akijua kila mipango iliokuwa ikiendelea.
Ukiwa na njaa ya pesa ni rahisi pua zako kunusa harufu ya chakula , hivyo Afande Kweka alichokifanya ni kuachia harufu ya chakula kwa Neema mwenye njaa.
Baada ya Neema kuelezea muundo wa biashara yake ndani ya taifa la Urusi alionekana kuridhika na kisha alitoa simu yake na kupiga sehemu na kisha akatoa maagizo flani ambayo yalimfanya Neema moyo kudunda, alijua hata kama alikuwa akienda kuisaidia serikali kuingiza siraha nchini lakinni faida yake ingekuwa mara mbili na biashara yake ya mahoteli.
Baada ya kuongea na Neema kwa muda Afande
Kweka aliitwa na kuambiwa kuna wageni wamefika kwa ajili ya kikao na aliwaacha Roma kuendelea kuongea.
“Lanlan naona unachukulia faida ya uwepo wa mimi shangazi yako hapa , haya niambie mama yako yupo wapi?”Aliuliza Neema.
Alishangazwa na kutokumuona Edna lakini tofauti na kumuuliza Roma aliona atumie akili kumuuliza Lanlan.
“Mommy was angry and she left..”Alijibu Lanlan akimaanisha mama yake alikuwa na hasira na akaondoka.
Neema alishangazwa na maneno ya Lanlan na alijikuta akimwangalia Roma kwa namna ya kutaka maelezo.
Upande wa Roma aliishia kutoa tabasamu la uchungu na alijikuta akielezea kwa ufupi kile kilichotokea usiku wa jana yake
“Kama ni hivyo basi naamini atakuwa amerudi moja kwa moja Dar es salaam kwa sasa?”
“Kwanini unaongea kwa uhakika hivyo?”
“Kwanini nisiongee hivyo, kwanza kabisa hapa Iringa kwasasa ni eneo ambalo hana mtu wa kuongea nae na lenye huzuni na pili kampuni ya Vexto ipo katika mabadiliko makubwa ambayo yanapangwa kufanyika kwanzia mwezi wa kwanza mpaka wa sita na Edna anapaswa kuyasimamia mwenyewe.. “Aliongea Neema na kumuona Roma kuwa kwenye mshangao na alijua fika pengine hakuwa akijua kuhusu hilo.
“Usiniambie hujui kitu ambacho Edna alikuwa akifanya kwenye siku hizi za hivi karibuni?”
“Huwa hatuongei sana kuhusu maswala yake ya kikazi , lakini si alikuwa akimsaidia Sophia kurudi katika tasnia ya sanaa?”
“Ah..! ni kwasababu ndio kwanza umerudi hivyo huwezi kujua kilichokuwa kikiendelea kwa mwezi mzima , kurudi kwa Sophia ni ili kuipa nguvu kampuni ya Vexto kama sehemu tu ya mipango yake , Kujiuzulu kwa Edna ilikuwa ni mwanzo wa kitu kingine kabisa , wakati alipojiuzulu alipunguza hisa zake zote kutoka asilimia tisini mpaka asilimia hamsini na moja,kwa ajili ya kuongeza ‘Shareholder’s’ wengi kwenye kampuni yake ili aweze kukidhi vigezo vya kimataifa kuibadilisha kampuni kutoka katika uhalisia wa jina la Vexto International kwenda Vexto Group”
“Vexto Grup , lakini si ilikuwa ni Vexto Group hapo kabla?”Aliuliza Roma na kumfanya Neema kutoa kicheko.
“Inaonekana kufanya kwako kazi ndani ya Vexto kulikuwa ni bure kabisa, ni kweli ilikuwa hivyo lakini haikuwa imekidhi vigezo vyote , unapaswa kuelewa kwamba ili kampuni kuweza kuitwa Group of Companies na kushiriki katika masoko ya hisa kimataifa inapaswa kuwa na Bodi ya wakurugezi ambayo ina nguvu ya kumuondoa na kumuweka Mkurugenzi mkuu kwa kumchagua ili kulinda maslahi yao ndani ya kampuni, hio ni sifa ambayo Vexto haikuwa nayo,yaani Edna alikuwa ndio mwamuzi wa mwisho kutokana na kuimiliki kampuni yote , lakini mara baada ya kuuza hisa za umiliki wa kampuni kwa nusu nzima inamaanisha kwamba kampuni sio ya kwake peke yake bali yeye
ni mmiliki mkubwa hivyo maamuzi makubwa ya kikampuni lazima yapite kwenye bodi kabla hayajafanyiwa kazi, Mpango wa Edna ni kuifanya Vexto kuwa kundi la makampuni huku yeye akiwa ni mtendaji mkuu na atakuwa amejiongezea nguvu mara mbili na ile ya mwanzo , kwanza kampuni itapanuka sana , lakini pia atakuwa na uwezo wa kujiingiza katika biashara ambazo hana hata uwelewa nazo , kwa mfano anaweza kuunda kampuni ya maswala ya kiteknolojia na ikafanya vizuri kwa kuajili watu wenye uwezo huo au anaweza kufunga zilizopo na kununua nyingine”
Neema alimpa shule Roma na kumfanya kukosa neno la kusema , alijiambia ndio maana Edna alikuwa mwepesi kumpisha Ernest kushika wadhifa wake kumbe kulikuwa na mpango mwingine anawaza kichwani.
Haikuwa hivyo tu Roma alikuwa akijua Edna alijiuzulu kwa ajili ya kujiweka bize na familia kama alivyoongea kumbe yote ni uongo alikuwa akitafuta kujipa thamani zaidi na zaidi.
Ilionekana Ernest siku zote ataendelea kuwa chini ya Edna na kupokea maagizo kutoka kwake.
Kwa maelezo ya Neema ni kwamba kampuni ya Vexto ambayo anaongoza kwa sasa Ernest Komwe ingekatwa kati na kubakia kuwa Kampuni inayohusiana na mavazi na fasheni pamoja na usimamizi wa usambazaji wa malighafi mpya , huku ikiundwa kampuni nyingine Tanzu ambayo ingehusika na maswala ya mafuta ya petroli na mambo mengine.
“Umeliona lile jengo refu zuri ambalo linajengwa pale Mwenge?”Aliuliza Neema.
“Unamaanisha lile lenye urefu kwenda hewani ambalo ndio lipo hatua ya mwisho?”
“Ndio hilo?, lile ndio jengo ambalo litakuwa makao makuu mapya rasmi ya kampuni ya Vexto Group”
“Nilijua lile jengo linajengwa na Vexto Constructor na mmiliki wake ni kampuni ya Nebula inc, maelezo hayo niliyapata kwa Daudi nilipokuwa mkurugenzi?” “Upo sahihi linajengwa kwa ajili ya kuwa makao makuu ya Nebula Inc lakini mmiliki wa kampuni ya Nebula Inc kwasasa ni Edna , sijui kilichotokea lakini ninachojua ni kwamba safari yake ya mwisho ya kikazi kwenda Hongkong iliwezesha hilo”Aliongea Neema na Roma kuhisi kuchanganyikiwa na kujiuliza Edna sio mwanamke wa kawaida.
Roma alikumbuka siku ambayo Edna ameenda
HongKong kikazi alimuunganisha na Edward wa Rothchild kumrahisia shida yake, pengine aliamini kuna mengi zaidi ambayo yaliendelea na Edward hata hakumwambia.
“Kwanini unayajua hayo yote?”
“Kama mpango wa Edna utafanikiwa basi sio kwamba tu atakuwa mshindani wangu wa kibiashara bali makampuni mengi ndani ya Tanzania yanaweza kumezwa, hivyo lazima na mimi nijiandae namna ya kuifanya kampuni yangu iendelee kuishi, ndio maana napanga kujiuzuru nafasi yangu ya uwaziri nibakie katika uendeshaji wa biashara”Aliongea na Roma hakutia neno.
Roma aliishia kujikuna kichwa chake , alijiambia mbona anazidi kuwa butu wa kifikra au ni kwasababu hakuwa na uwezo wa kutumia uwezo wake , maana IQ yake ilikuwa imeshuka mno”
“Halafu ukichana na hayo , nahishi kilichotokea jana yake sio kawaida”Aliongea Neema akimwangalia Roma anaejikuna kichwa.
“Unamaanisha nini?”
“Sidhani kama Edna ni mtu wa kushindwa kujizuia na kutaka kumuua Sophia kwasababu tu ya wivu , kama ni hivyo si anapaswa kuniua na mimi?”Aliongea.
“Unaongea utani mpaka sasa hivi tu?”Aliongea Roma akitoa tabasamu la kulazimisha.
“Najaribu kukufurahisha , wewe mwanaharamu usie na shukrani”
“Unapaswa kutania vitu vingine , sitaki kuona yeyote kati yenu akiumia la sivyo itanifanya kuonekana nimefeli”Aliongea na kumfanya Neema kujisikia vizuri.
“Nilichokuwa nikitaka kumaanisha ni kwamba , Edna anaonekana na tatizo ambalo linamsumbua hata kabla hujarudi nilishawahi kumuuliza lakini hakuongea chochote”
“Kwahio unamaanisha hujui chochote kwasababu hajakuambia chochote?”Aliongea Roma akijikatia tamaa.
“Mimi naongea tu , nitajuaje anachoficha kwenye moyo wake ,isitoshe si vizuri tu kwani nimepunguza mshindani mwingine , unajuaje siku moja nikabakia peke yangu”Aliongea na kumfanya Roma kumchapa kibao cha mapajani.
“Ukiendelea hviyo nitaondoka sasa hivi na Lanlan nimtafute nimuulize mwenyewe”
“Haha.. ukweli ni kwamba najua swala la Lanlan lilikuwa kubwa kwake lakini kwa ninavyoona kwa kutoshindana kwake na wewe katika maswala ya nani amlee Lanlan ,naamini wewe anakuchulia ni wa muhimu zaidi kwake”
Roma aliona maneno ya Neema yapo sahihi , ijapokuwa Edna mara baada ya kujua kuhusu Lanlan hakuonyesha kutatizwa na hilo na alichokuwa akiongea ni tofauti kabisa kama sababu ya kumuacha.
Roma mara baada ya kuachana na Neema moja kwa moja alichukuana na Lanlan na kuelekea nae chuoni maaabara kwa ajili ya kumtafuta Clark ili ampatie majibu yake.
Baada ya kufika na kuongea kidogo na Clark kwa kumtambulisha Lanlan kama mtoto wake wa damu aliemzaa na Seventeen waliingia kwenye maswala ya matibabu lakini licha ya hivyo Clark alionekana kushangaa kwani hakutegemea kama Seventeen aliacha mtoto.
Lakini licha ya hivyo alifurahi na kumbeba Lanlan na alijiambia ndio maana alikuwa anafanana sana na Edna kumbe alikuwa ni mtoto wa Seventeen ambaye alikuwa akifanana na Edna.
“Huu ndio uchambuzi wa taarifa za uchunguzi niliokufanyia , unaweza kujionea mwenyewe”Aliongea Clark akimpatia Roma makaratasi.
“Mimi sijui chochote hapa , nadhani ni vyema kama utanielezea mwenyewe”
“Kwa haraka haraka naweza kusema kwamba kuna taarifa nzuri na mbaya , ipi ndio unataka ianze”
“Tuanze na hio taarifa nzuri kwanza”
“Taarifa nzuri ni kwamba mwili wako umekuwa na nguvu zaidi ya mara tatu kuliko mwanzo tokea mara ya mwisho nilipokufanyia vipimo , hii ni tofauti kwasababu nilitegemea uvimbe wako kuongezeka kwake ndio kupungua kwa uwezo wako , lakini vipimo vinaonyesha ni tofauti , kwasasa naweza kusema mchakato wako wa ukuaji wa kimwili ni kama ‘Metarmophosis’.. lakini umeruka hatua mbili mbele za kiukuaji”Aliongea na Roma alielewa kwa haraka.
“Vipi kuhusu taarifa mbaya”
“Taarifa mbaya ni kwamba ni nusu ya taarifa nzuri , sikujua mwanzo lakini mara baada ya kuvuna nishati za mbingu mwenyewe nimeweza kujua baadhi ya vitu ambavyo havina maelezo ya kisayansi … utendaji wako wa kazi katika ubongo umekuwa wa tofauti sana na nilikosa taarifa za kisayansi kugundua sababu ya mabadiliko hayo , lakini kwa haraka haraka naweza kusema kuna nguvu iliopo ndani yako inayoshindana na mfumo wako wa mawasiliano wa kawaida wa mwili , ni nguvu ambayo naweza kusema haipaswi kutokea kwa wakati mmoja(Mutual exclusive)… na kwasasa nguvu hizo zipo katika hali ya uwiano sawia… kwa maneno marahisi ni kwamba licha ya nguvu zote kuwa kubwa kwa kulingana itakuwa ngumu kwako kuishinda na kuvunja huo uwiano ,,, kwahio ni kama umefungwa”
SEHEMU YA 639.
Roma alishika kichwa chake akionyesha hali ya kushikwa na mawazo na palepale alivuta hewa nyingi na kuitoa nje akionyesha hali ya huzuni kidogo.
“Ulivyoelezea ni kama ambavyo nimefikiria na umethibitisha tatizo langu, lakini tatizo lingine ni kwamba ni kipi napaswa kufanya”
“Kwa ninavyoona kutumia njia za kawaida za kisayansi haziwezi kuwa na ufanisi , lakini … umesahau kwamba wewe sio mtu pekee ambaye unamiliki nguvu za kijini?”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha ni swala la kinadharia … ninajiuliza je haitowezekana kutumia nguvu kubwa ya nje kukuongezea uwezo wa kuweza kutawala nguvu inayoshindana na ya kwako , kitu pekee ambacho kwasasa unaweza kufanya ni kuendelea kushikilia uwiano lakini vipi kama kuna nguvu nyingine ya nje ambayo inaweza kukusaidia kwa kukuongezea nguvu , Rose na Magdalena wote washaingia katika levo ya Nafsi , licha ya kwamba wanaweza kuwa na nguvu ambazo ni za chini na ya kwako watakuwa na nguvu ya kijini ya kuweza kukusaidia na kuvunja uwiano na wewe kushinda”
Roma macho yalichanua mara baada ya kusikiliza pendekezo hilo zuri lakini alitingisha kichwa kukataa .
“Hapana , itakuwa ni hatari sana kwao, roho ya mnyama ni ya hatari sana na ina nguvu ya giza , kama mambo yakienda vibaya Rose na Magdalena wanaweza kupatwa na tatizo”
“Basi usiwe na wasiwasi naamini kutakuwa na mbinu nyingine zaidi , isitoshe nitaelekea Dar na nitakutana na Rufi na atanipa baadhi ya taarifa ambazo zinaweza kunisaidia kutengeneza njia mbadala ya kukusaidia”
Roma aliishia kukubali, ijapokuwa swala lake hakutaka lifahamike kwa wanawake wake lakini kwa upande wa Rufi aliona tu ngoja ajue ,lakini alijihakikishia kwamba asingetumia pendekezo la Clark la kuwatumia Magdalena na Rose kumsaidia mpaka awe na uhakika wa usalama wao.
******
Upande wa Dar hali ya hewa ilikuwa ya mawingu na vipindi vya jua ikiashiria muda wowote mvua inaweza kunyesha , ilikuwa ni kama ilivyotabiriwa katika kipindi cha hali ya hewa jana yake kuonya mvua kubwa ingeweza kunyesha.
Najma alikuwa na ugeni ndani ya sehemu anayoishi , alikuwa ni Shangazi yake na wifi yake ambao walilala hapo na asubuhi hio walikuwa wakijiandaa kwenda kutembea.
Shangazi yake Najma hakupata utulivu , tokea mara ya kwanza kuonja utamu wa kupanda gari ya pesa nyingi kila saa alitaka kulipanda na siku hio ambayo Najma alikuwa Off alilazimisha kwa kumtaka Najma kwenda kutalii talii kupoteza muda ndio warudi nyumbani kwao.
Najma hakuwa na tatizo kwani alikuwa off lakini ukweli ni kwamba alitamani siku hio kuitumia katika mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi na jioni kwenda kumtembelea rafiki yake Nasra lakini ujio wa shangazi yake na wifi yake ni kama ulivuruga ratiba zake.
“Katika maisha yangu sijawahi kuwaza kama kuna mwanafamilia katika ukoo wetu ambaye anaweza kumiliki gari kama hii”Aliongea Shangazi yake Najma huku akitoa kicheko .
“Shangazi unasemaje hivyo , lilikuwa swala la muda tu kwa Najma , uzuri wake sio wa kawaida hata hivyo”
“Haha.. umeongea kweli mwanangu, Najma amezaliwa kwa ajili ya vitu kama hivi.. Najma kama asingekuwa ubishi wake kipindi kile angekuwa sasa hivi ashazalishwa na yule Ahmed kina kifupi na gari angekuwa anaiota ndotoni tu”Aliongea huku wakicheka na kugongesheana mikono na mke wake Juma.
Najma alishindwa kuchangia neno na maneno ya shangazi yake yalimkumbusha mwaka uliopita namna ambavyo Shangazi yake na kaka yake walivyokuwa kidedea kumtaka aolewe na Ahmedi ,lakini kwa namna ambavyo shangazi yake anaongea ni kama amesahau kabisa na hakuonekana kuwa na hatia tena saivu anamwita Ahmedi kina kifupi.
Ni mara baada ya Najma kuingiza gari barabarani ghafla tu ilitokea gari aina ya Ford SUV ya rangi nyeusi na kuwazibia njia mbele yao.
Najma aliekuwa ni dereva alijikuta akikunja sura na alijaribu kupiga honi na kuwasha taa kuashilia kwamba apishwe njia lakini dereza wa gari hio alionekana hawakuwa na nia yoyote ya kumpisha.
Baada ya dakika kama tatu kupita gari ile ilifunguliwa milango yote na waliweza kutokezea wanaume wanne wenye miili mikubwa ya mazoezi wote wakiwa weusi waliovalia mavazi ya suti nyeusi kama mabodigadi pamoja na miwani za jua huku wote kwa pamoja wakiwa wameshikilia mitalimbo ya chuma mkononi.
Najma palepale alijikuta akinusa hatari na alimwangalia Shangazi na Wifi yake ambaye alikuwa amepakata mtoto mdogo na kuwaambia watoke kwenye gari haraka.
Lakini licha ya Najma kuongea wale wanaume kwa haraka walisogelea gari na kwenda kusimama kwenye mlango wa gari huku kiongozi wao aliekuwa akivuta sigara alitoa cheko la kebehi akiwa mbele ya gari.
“Bang!!”
Yule kiongozi wao mara baada ya kusogea mbele aliinua chumba chake kigumu na kupiga kwa nguvu mbele ya boneti ya gari ya Najma na kulifanya libonyee kwa mbele palepale na taa zote kuvunjika.
Waliokuwa ndani ya gari waliishia kutoa kilio cha mshituko huku sura zao zikijawa na wasiwasi na kuanza kutetemeka kwani sio tukio la kawaida.
Ilikuwa ni kama wameagizwa vile kwani wale watatu waliokuwa wamesimama kwenye milango ya kutokea walianza na wao kulipiga na vyuma lile gari kuanzia nyuma mpaka juu ya paa.
Hawakujali mtoto aliekuwa akitoa kilio ndani ya gari na wao waliendeleza kazi , Mke wa Juma alijikuta akimziba mtoto wake masikio huyu yeye akitetemeka kwa hofu.
Ilikuwa ni bahati kwamba waliweza kufanikiwa kutoka bila kupata madhara lakini gari iliharibika sana na kubadilika muonekano na haikuwa gari tena ile mpya ambayo ilikuwa ya bei ghali.
Tena mara baada ya Najma na ndugu zake walivyotoka ndio walivyozidi kuliharibu lile gari kwa spidi kubwa na walipasua vioo vyote na kuchokonoa na eneo la injjini na moshi ulianza kufuka.
“Nyie ni wakina nani , kwanini mnatufanyia hivi?”Aliuliza Najma aliekuwa akitetemeka kwa hasira , hakuamini gari ambayo amepewa kama zawadi na mpenzi wake imepatwa na majeraha ya aina hio tena ndani ya siku mbili tu.
Yule kiongozi mara baada ya kumuona Najma amenyanyua mdomo na kuongea alimwangalia kwa dharau.
“Mrembo , ni kosa lako mwenyewe kutoka kimapenzi na mwanaume ambaye sio saizi yako na kumkasirisha yule mwanamke, hili ni onyo tu ambalo tumejaribu kukufikishia kutoka kwa mwanamke uliemchokoza , usije kuthubutu kuwa karibu na Boss wa kiume tena , siku nyingine haitoishia kwenye kuharibu gari tu bali ni …”Aliongea huku akionyesha ishara ya kuua.
Baada ya kuongea maneno hayo Najma palepale alijua nani ambaye amewatuma hao majambazi , kumbe ni mwanamke ambaye anamjua kama mama yake Naibu waziri Salihi ndio ambaye amekuja kumshambulia kwa kuagiza watu wake bila sababu za msingi kisa kumuona akiongea na Salihi.
Najma alijikuta akitokwa na machozi na kumwangalia shangazi yake ambaye amekatwa na kioo kwenye bega na alijikuta akipatwa na ahueni mara baada ya kuona mtoto hajapatwa na majeraha.
“Kama ni hivyo kwanini mnaingiza watu wengine ambao hawahusiki, hawa ndugu zangu wamefanya nini , kwanini msingesuburi nikiwa peke yangu ndio mnishambulie”
“Haha… wewe msichana tena nyamaza, nishaharibu magari mengi tu kama hivi lakini sijawahi kuona msichana jasiri kama wewe ambaye unaongea mara baada ya kukushambulia kama hivi , ni bahati mbaya kwamba licha ya kutufokea kwako ni bure , kazi nilioagizwa leo hii ni kuharibu gari yako basi nikirudi jua ni zamu yako”
Najma alijikuta akikosa neno la kuongea na kuishia kuwaangalia kwa hasira lakini wanaume wale hawakuonekana kuwa na hofu kabisa licha ya kufanya tukio hilo mchana kweupe na baadhi ya watu wanaangalia.
Najma palepale wazo la kupiga simu polisi lilimjia na alitoa simu yake na kutaka kupiga , lakini wale watu walikuwa wakimwangalia tu anachotaka kufanya.
“Hehe ndio unajaribu kupiga simu polisi.. haha utakuwa unachekesha , kama tungekuwa tunaogopa polisi tusingeharibu gari yako wale watu wakiwa wanaangalia tena mchana kweupee”Aliongea na kuwafanya wale wanaume wengine kucheka na kisha walipeana ishara na kuingia kwenye gari yao .
Najma licha ya kuona gari yao imeondoka hakughairisha kwenye kupiga simu polisi na mara baada ya kuelekzea kila kitu palepale alimkimbilia wifi yake.
“Wifi mtoto yupo salama?”Aliuliza na mke wake Juma alishia kutingisha kichwa huku machozi yakimtoka.
“Najma umemchokoza nani , hawa majambazi ni wakina nani?”Aliuliza Shangazi yake Najma huku akishika jeraha lake ambalo lilikuwa likivuja damu.
“Sijui chochote Aunt , ngoja tusubiri polisi wafike na tuone watapata nini kupitia uchunguzi wao”Aliongea kwa kutetemeka.
“Najma inaoneana aliefanya hivi anakisasi ,ijapokuwa sijasikia vizuri lakini inaonekana ni mwanamke aliegiza ufanyiwe hivi , Najma hebu niambie ni mke wa Roma ndio kakufanyia hivi?”Aliuliza Shangazi yake Najma kwa wasiwasi.
Ijapokuwa alikuwa akijua Edna alikuwa mtu mzuri mpaka kumsaidia Juma kupona kwa kulipia matibabu lakini swala la Najma kujihusihsa kimapenzi na Roma lilikuwa ni tofauti hivyo aliona kwa upole wa Najma ambaye ni ngumu kutengeneza maadui basi mtu pekee anaeweza kutuma kumshambulia ni Edna.
“Shangazi hapana, Sister Edna hawezi kunifanyia hivi, ni swala ambalo halihusiani na Roma kabisa , msiwe na wasiwasi hili nitalimaliza mwenyewe”Aliuongea
“Utalimaliza vipi Najma? , licha ya kwamba unafanya kazi wizarani nafasi yako ni ya kawaida na huna koneksheni yoyote , nadhani umewasikia wenyewe hawaogopoi polisi , unadhani bila ya kuwa na nguvu unaweza kuwashitaki , mpigie Roma umwelezee sasa hivi , ndio mtu pekee anaeweza kukusaidia mpigie umwambie kila kitu…nimechukia sana”Aliongea huku akionyesha kukosa uvumilivu na kuongea kwa sauti ya kufoka.
“Lakini Roma hayupo hapa Dar”
“Mpigie kama kweli anakupenda hawezi kudharau matatizo yako, fanya hivyo Najma kwa usalama wako , awamu nyingine watakuja kukua wewe mwenyewe ohoo”
“Najma kweli fanya kama Shangazi anavyosema, inaonekana mtu aliefanya hivi ana kinyongo na sio mwepesi kudili nae kupitia polisi”
Najma alijikuta aking’ata lips zake kwa aibu , alikuwa pia akitamani kumpigia Roma simu na kumwambia yaliotokea lakini aliogopa Roma angemwelewa vibaya kuhusu kuhusika kwa mama yake Waziri Salihi , isitoshe gari la mamilioni ya pesa ambalo amemnunulia juzi tu ndio hilo lishaharibiwa na hakujua namna ya kumwelezea Roma , ki ufupi aliogopa.
Najma aligeuza macho yake na kumwangalia Shangazi yake aliekuwa akimkodolea macho akiwa na hasira kwa udhalilishaji waliofanyiwa na Najma aliishia kujawa na hofu na kisha palepale aliitafuta namba ya Roma na kupiga.
Lakini alikuja kugundua namba ile haikuwa hewani kwani aliambiwa simu ilikuwa imezimwa.
“Amezima simu yake na hapatikani pengine kuna kinachoendelea”
“Basi nadhani hatuna jinsi , subiri baadae umpigie kwasasa tunapaswa kusubiri hao polisi tuone wataongea nini mara baada ya kufika,Looh zote hizi ni laana ya umasikini inayotunyanyasa…pukeee!!”Aliongea Shangazi huyo akitema mate chini huku hata yeye licha ya kushambuliwa lakini alihurumia gari mbaya ambayo haikuwa na ule muonekano wa mwanzo.
“Najma ikitokea anataka kununulia gari nyingine mwambie akunulie hata ka Spacio , nadhani mizimu ya ukoo haitaki tupande magari ya kifahari”Aliendelea kuongea.
*****
Upande wa Roma muda huo ndio alikuwa akiingia ndani ya ndege na alitii sheria na kuzima simu yake.
Roma alikuwa amekaa na binti yake katika daraja la kwanza katika ndege hio ya shirika la taifa na ilichukua dakika chache tu mara baada ya kutulia Lanlan alipitiwa na usingizi.
Mdada mrembo mhudumu mara baada ya kufika kuwahudumia abiria wa daraja la kwanza alijikuta akivutiwa na mwonekano wa Lanlan na mara baada ya kujua baba yake na yeye amefumba macho alitoa simu yae akitaka kupiga picha lakini Roma aliyafumbua na kumwangalia.
Roma hakuonyesha kufurahishwa na kitendo cha muhudumu huyo anachotaka kufanya na alinyoosha mkono kama vile anataka kitu kutoka kwa mhudumu huyo lakini yule mrembo aliishia kutabasamu huku akiona aibbu amekamatwa.
“Samahani kwa kukusumbua Sir , je naweza kukuuliza ni kipi unahitaji?”
“Pesa bila shaka , kipi kingine naweza kutaka , huwezi kumpiga picha binti yangu mrembo bila malipo , hata ukienda mbuga za wanyama kuna kiingilio cha pesa unacholipia sembuse binti yangu mzuri hapa,”Aliongea Roma akiwa siriasi.
Yule mrembo aliishia kuona aibu lakini kwa siri akivuta mdomo na kujiuliza imewezekanaje mwanaume asie na aibu kama huyo kukaa daraja la kwanza , alijiambia ashukuru Mungu kwa kumtunuku binti mrembo kama huyo maana hakuwa akiendana na mwonekano wake.
Ijapokuwa alikuwa akimdhihaki Roma ndani kwa ndani lakini kutokana na taaluma yake iliendelea kumwonyeshea tabasamu la ukarimu.
Palepale alitoa baadhi ya matunda na Sambusa wa nyama kwenye kijitoroli chake na kumpatia Roma kama rushwa ya kumtuliza.
Roma mara baada ya kushika sambusa aliisogeza karibu na pua za Lanlan na palepale alishituka kutoka usingizini na kupokea ile sambusa na kuila yote ndani ya dakika na kisha Roma akachukua na nyingine na kumpatia na aliipiga yote ikaisha na kisha aligeuza macho yake na kumwangalia mhudumu wa ndege.
Mhudumu yule aliishia kushangaa tu na ilikuwa afadhali kwani ndani ya daraja la kwanza chakula cha abiria kilikuwa cha kutosha hivyo alimpatia Lanlan nyingine na kisha akawaacha.
“Daddy , are we going to find mommy?”Aliuliza Lanlan na kumfanya Roma kukakamaa mwili na kumwangalia Lanlan akitafuta jibu la kumpa.
“Mama sasa hivi hana furaha baada ya kugombana na Daddy, .. Daddy atamshawishi mama baada ya muda ili arudi , kwasasa uwe mtiifu kumsubiri mpaka arudi”
“Kwahio Daddy unamaannisha siwezi kulala na mama tena?”
“Ndio , mama yako hatoturuhusu turudi nyumbani kwasasa”Aliongea Roma akionyesha mwonekano wa kimawazo.
“Can Lanlan Sleep with Aunt Nasra?”Aliuliza kwamba je anaweza kulala na shangazi yake Nasra.
“Wewe mtoto msaliti , unataka kumuacha mama yako kirahisi hivyo , unampenda Aunt Nasra sana?”
“Bibi amesema watoto hatupaswi kuingilia maswala ya wakubwa na kama nitaendelea kuwa mtiifu basi nitaendelea kula chakula kitamu , Aunt Nasra anapika chakula kitamu”Aliongea na kumfanya Roma kuelewa sasa kumbe ukaribu wa Lanlan na Nasra ni kwenye mapishi.
Roma kwa alivyokuwa akijua wanaojua kupika sana ni Nasra na Najma , Dorisi alikuwa fundi kwenye upishi lakini alikuwa mvivu ila Nasra alikuwa akipenda kupika sana na chakula chake ni kitamu ,hakujua Lanlan amekionja lini lakini hakutaka kuuliza sana.,
Ukweli ni kwamba Blandina alimwambia Lanlan akakae kwa Nasra mpaka mama yake atakapomtafuta.
Roma licha ya kwamba alijua Lanlan kwenda kukaa kwa Nasra kunaweza kumfanya Edna azidi kukasirika lakini hakuwa na chaguo lingine zaidi ya kumpeleka huko alikotaka.
Baada ya lisaa limoja na nusu Roma aliweza kufika Dar es salaam huku Lanlan akimwambia baba yake kama wangepaa wangekuwa washafika , lakini Roma aliishia kumjibu Lanlan atapaa nae siku nyingine ila ajitahidi aweze kupaa mwenyewe.
Roma mara baada ya kuwasha simu yake alishangaa baada ya kuona Missed call ambazo zilikwua zimeingia kwenye simu yake zikitoka kwa Najma.
Roma alisimama akiwa amemshikilia mkono Lanlan na kuanza kufanya mawasiliano kwani alihisi kuna kitu hakipo sawa na mara baada ya kupiga kwa dakika kadhaa simu haikupokewa kwani haikuwa ikipatikana hewani na jambo hilo lilimpa mashaka
na palepale aliitafuta namba ya simu ya Juma na kupiga na iliita mara moja tu na kupokelwa.
“Roma Bro mbona hukuwa ukipatikana hewani , tafuta namna ya kumsaidia Najma , amekamatwa na polisi”Aliongea Juma akiwa na wasiwasi na kumfanya Roma kushangaa.
SEHEMU YA 640.
Roma alijikuta akipatwa na wasiwasi na kujiuliza imekuwaje Najma akaishia kwenye mikono ya polisi.
“Juma hebu ongea taratibu taratibu uniambie nini kimetokea”Aliongea Roma na pale Juma alimpatia simu shangazi yake na kuanza kuelezea tukio.
Ilionekana mara baada ya polisi kufika ndani ya nusu saa walijairbu kumhoji Najma juu ya kilichotokea na mara baada ya kuelezea polisi walimchukua na kuondoka nae huku wakisema anaenda kusaidia maswala ya uchunguzi zaidi.
Lakini ajabu ni kwamba baada ya lisaa Najma simu yake haikuwa ikipatikana tena na wamejaribu kwenda kwenye kituo cha Oysterbay ambacho inasemekana alipelekwa lakini walikosa ushirikiano kutoka polisi.
“Basi naomba mpunguze wasiwasi nitadili na hili swala mwenyewe”Aliongea Roma na muda huo walikuwa tayari washaingia kwenye taksi.
Roma aliambiwa Najma alipelekwa kituo cha Oysterbay na alitamani kwenda moja kwa moja lakini alijiambia anaweza kafanya kitu kibaya hivyo aliona hatua ya kwanza ni kumpeleka kwanza Lanlan nyumbani huku yeye akitumia koneksheni zake kujua nini kinaendelea.
Baada ya kufikiria nani ambaye anaweza kumsaidia swala lake palepale jina la Omari Tozo liliibuka kwenye kichwa chake na hakutaka kupoteza muda na alimpigia.
“Hey! Bro ni mzimu gani umekupitiia mpaka ukakumbuka kunipigia simu leo , sio kawaida yako?. Nimefika Iringa jana na mpango wangu ni kukutafuta leo kwa ajili ya kwenda kupata moja moto moja baridi baada ya kupewa ruhusa na mke wangu..”
“Hebu acha ngonjera zako kwanza ,,, nina shida ya haraka nataka unisaidie, nipo Dar sasa hivi nishatoka Iringa”
“Kwanini umerudi haraka hivyo , nilijua bado upo Iringa ndio maana nimekuja huku tuonane, anyway ni jambo gani ambalo unataka nikusaidie”
“Mwanamke wangu mmoja anaefahamika kwa jina la Najma amekamatwa na watu wa polisi na kupelekwa kituo cha OysterBay na ndugu zake wameenda huko lakini hakuna ushirikiano , hebu nisaidie kutuma mtu wa kueleweka akarahisishe hilo swala na atoke polisi, najua hukosi koneksheni ndani ya jeshi la polisi maana upo kitengoni” Ukiachana na baba yake Omari kuwa mkuu wa majeshi lakini pia mjomba wake Omari yaani kaka yake mama yake ni mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa na pengine ndio maana ilikuwa rahisi kwa Oamri kujiunga na usalama wa taifa tofauti na kitengo cha jeshi.
“Hahaha.. kuna watu wanajiamini aisee , nani kapata ujasiri wa kukuchokoza kwa kumkamata mrembo wako”
“Hebu acha utani na fanya jambo la haraka upigie mtu afanye kurahisisha hili”
“Sawa bro usiwe na wasiwasi najua ni kipi nifanye”Aliongea Oamri na kisha akakata simu palepale.
Roma asingeweza kumpigia simu Mage kumsaidia katika hilo kwani Mage alishaachana na maswala ya upolisi na alikuwa akijiandaa kuelekea Visiwa vya wafu, lakini pia hakutaka kufanya hivyo kwani aliona sio vizuri kumpigia mwanamke wake kumsaidia mwanamke wake mwingine .
Upande mwingine ndani ya kitua cha polisi Masaki alionekana mwanaume mzee kidogo ambaye kwa kumwangalia tu ni makadirio ya miaka hamsini hivi akiwa ameketi ndani ya ofisi ndani ya kituo hicho akiwa na sigara ameishikilia mkono wa kushoto huku kulia akiwa ameshikilia gazeti la mwananchi.
Alikuwa ni Mkuu wa kituo mpya ambaye amepandishwa cheo hivi karibuni mara baada ya Mage kujiuzulu , alikuwa akifahamika kwa jina maarufu la Afande Mkanye.
Afande Mkanye alikuwa na miaka hamsini na saba na alikuwa mkali mno kiasi cha watu kuanza kumfananisha na jina lake na ilikuwa hata polisi wenzake walikuwa wakimuogopa.
Licha ya ukali wake huo kutokana na elimu yake kuwa ndogo hakuweza kupata cheo kikubwa kwa muda mrefu lakini mara baada ya Mage kuachia ngazi ndio sasa akaweza kupata nafasi ambayo ilikuwa ni ya ndoto yake kabla ya kustaafu.
Unaambiwa tokea apewe cheo hicho alikuwa akilala kituoni ndani ya ofisi yake kwenye masofa na alipoulizwa alisema anafidia siku ambazo serikali imemcheleweshea kumpandisha cheo.
Wakati akiendelea kuwa bize kusoma gazeti lake linalohusiana habari za kitaifa palepale mlango wa ofisi yake uligongwa na kuruhusu mgongaji kuingia.
Mlango mara baada ya kufunguliwa alionekana mwanaume kijana aliekuwa katika sare za polisi mwenye makaridio ya miaka therathini , alienyoa upara na ndevu zote , huku akiwa na Komwe pana na kumfanya kuonekana kama mtu mwenye kichwa kikubwa.
Bwana huyo ndio alikuwa mkuu msaidizi(Junior Superintendent) wa kituo hicho ambaye alihamishiwa mwaka huo kituoni hapo , kabla ya kuja jijini Dar es salaam alikuwa ni polisi wa kawaida wilayani kisarawe.
Baada ya kusalimiana na Afande Mkanye palepale alienda kwenye mada ya kitu kilichomfanya kuingia ofisini hapo kwa mkuu wake.
“Chief nipo hapa kuulizia kama kuna mwanamke anaefahamika kwa jina la Najma Waziri kushikiliwa hapa kituoni ,ni mfanyakazi wa Wizara ya elimu”Aliongea na kumfanya Afande Mkanye kukunja ndita na kuweka gazeti lake chini huku akizima sigari yake kwenye sahani ya udongo.
“Afande Jamali kwanini unaniuliza swala hilo mimi , ulipaswa kujua wewe kabla ya mimi kuju”Aliongea.
“Afande ni kwamba nimepokea simu ambayo inasema mwanamke huyo anazuiliwa hapa kituoni kwetu lakini mara baada ya kuulizia taarifa zake inaonekana hakuna jina lake kati ya wanawake waliokamatwa , nimekuja kuuliza kama swala hili ni la kimya kimya,Chief nadhani unajua mabadiliko ambayo yamefanyika ndani ya jeshi la polisi na msisitizo ni kufanya mambo kwa uwazi na kutoa ushirikiano kwa watu wote wanaongiziwa ili kuepusha lawama”
Uso wa Afande Mkanye ulijikunja , swala la Najma yeye ndio alikuwa nyuma yake lakini mtu ambaye amempa kazi ya kumkamata Najma alikuwa akibweka sana, ijapokuwa alijua Najma alikuwa ni mfanyakazi wa wizara lakini nafasi yake haikuwa tishio sana kumletea shida , isitoshe watu ambao wamempatia kazi hio walikuwa wakubwa zaidi ya wizara yenyewe.
“Jamali hio taarifa umetoa wapi au ndio umepokea simu kutoka kwa watu wasiofahamika na upo hapa kuniuliza maswali ya kijinga , nadhani unajua kwamba miaka yangu ya kuhudumu katika jeshi la polisi inaheshabika napanga hii nafasi yangu wewe kuichukua , hivyo hupaswi kuuliza maswali mengi , kama kuna mtu amekuliza wewe mpotezee”Aliongea akimwashiria kuondoka ofisini kwake lakini Afande Jamali alionekana kusita.
Afande Mkanye mara baada ya kuona Afande Jamali yupo kimya na anaonekana kukosa ujasiri wa kuongea aliona kabisa huyo mwamba atakuwa anamuogopa na alitoa tabasamu la ushindi.
Lakini alikuwa amedhania vibaya kwani upande wa Afande Jamal alikuwa akijishauri kama aweke wazi utambulisho wake mwingine tofauti na kuwa polisi au akae kimya.
Baada ya kufikiria kwa muda mfupi aliingizia mkono kwenye kombati yake na kutoa kitambulisho na kumpatia Afande Mkanye.
“Chief , lazima nipate majibu kwa maswali yangu muda huu , hivyo niambie ukweli wote”Aliongea huku akiwa anatabasamu na Afande Mkanye alitoka katika kuegamia Sofa kibosi na kisha aliinama na kuchukua kitambulisho ambacho kilikuwa kama
Passport ya kusafiria na kufungua ndani na palepale alijikuta akitoa macho na kukaa vizuri huku mikono yake kuanza kutetemeka .
“Tanzania intelligence and security Service(TISS)!!!”
Licha ya kwamba hana elimu kubwa haikumaanisha kushindwa kujua kitambulisho cha mwanausalama wa taifa.
Bwana huyo alijikuta akishangaa na kujiambia ndio maana Jamali alionekana kuwa mkimya sana nyakati nyingi lakini aliweza kupata cheo kikubwa ndani ya muda mfupi tena akipita polisi waliokuwa wakifanya kazi ndani ya kituo hicho kwa muda mrefu hata yeye mwenyewe ambaye siku zote alikuwa akisotea cheo cha Senior inspector wakati Jamali alikuja moja kwa moja na kupewa cheo cha Superintendent kumbe ni kwasababu alikuwa mwanausalama aliepandikizwa ndani ya jeshi la polisi na serikali , kengele ya kukosa mafano na kiinua mgongo iligonga kwenye masikio yake.
“Chiefu vipi vielelezo vyangu vipo sawa?”
“Ndio.. ndio , siwezi kukataa hata kama ni kipofu”Aliongea huku akijaribu kutabasamu.
“Kama ni hivyo je naweza kupata majibu juu ya Miss Najma anashikiliwa kituo gani na kwasababu zipi?”Aliuliza na kumfanya Afande Mkonyi jasho kumtoka.
Mpaka kitendo cha Jamali kuamua kujitoa kivulini kama mwanausalama na kuweka wazi uhusika wake ilimaanisha mtu aliekamatwa sio wa kawaida kama alivyofikiria.
“Jamali .. ukweli ni kwamba mwanamke huyo anaieitwa Najma amekamatwa lakini hakuletwa hapa”Aliongea kwa wasiwasi mno .
………………
Dakika chache mbele Afande Jamal aliweza kutoka huku akiwa na mwonekano wa kuchoka mno kutokana na ugumu wa swala lenyewe.
Mwanzonni alijua ni swala la kawaida tu ambalo anaweza kulifanyia maamuzi lakini mara baada ya kujua muhusika aliekuwa nyuma ya kukamatwa kwa Najma alijikuta akichoka na aliona asingeweza kukamilisha kazi yake kwa cheo chake.
Baada ya kurudi ofisini kwake na kikaa chini alimpigia Omari Tozo kwa mara nyingine kumrudishia majibu maana alipata maagizo kutoka kwake.
“Kaimu ni mimi..”
“Najua ni wewe ndio , vipi kazi imekamilik?”:
“Kazi imeshindikana kutokana na uzito wenyewe , familia ya Nguzo ya Taifa inahusika katika hili”Aliongea na kumfanya Omari upande wa pili kuguna.
*******
Roma mara baada ya kufika nyumbani kwa Nasra aliweza kuwakuta wakiwa wanamsuburi nje akiwa ameambatana na Qiang.
Roma alishatoa maagizo tokea akiwa Aiport kwa Qiang kukusanya nguo za Lanlan na kuzipeleka nyumbani kwa Nasra na ataishi huko kwa muda akendelea kumlea Lanlan.
Upande wa Nasra alikuwa ashajua kilichotokea na aliweza kusikia Edna alifika Dar jana usiku taarifa ambayo ilimshangaza na alijua tu lazima kuna ugomvi uliotokea.
Wakati akijiuliza nini kilichotokea aliweza kupigiwa simu na Blandina na kupewa maagizo ya kukaa na Lanlan kwa muda mpaka Roma kuweka sawa maswala yake na Edna na Nasra alichukua fursa hio kuuliza nini kinaendelea na hapo ndipo Blandina alipomwelezea kwa ufupi.
Nasra alishangaa kile kilichotokea na kujiuliza nini kinachoendelea , ijapokuwa hata yeye mwenyewe alihisi ni swala la muda tu kwa Roma na Sophia kuingia katika mahusiano lakini swala la Edna kuchagua maamuzi hayo kwasababu ya Sophia ilimshangaza mno, Alijiuliza ni kweli Edna anataka kuachana na Roma.
Nasra alijiuliza maswali mengine na kila kitu kinachoendelea hakiku mfanya kuwa na furaha hata kidogo na alikuwa na wasiwasi sana juu ya Edna.
Baada ya Lanaln kuingia ndani ya geti akiwa ameshikiliwa mkono na Roma alijikuta akipatwa na hisia mchanganyiko mara baada ya kumwangalia Roma usoni.
Alimwangalia Roma kuona kama ana tatizo maana alikuwa akijua alikuwa akimpenda sana Edna hivyo yaliotokea yangempa mawazo lakini hakuona utofauti mkubwa sana.
“Aunt Nasra , Lanlan ana njaa “Aliongea Lanlan mara baada ya kupakatwa na Nasra.
“Lanlan hujapata chakula cha mchana bado?”Aliuliza Nasra akimwangalia Lanlan , ukweli hata yeye alikuwa na hisia tofauti mara baada ya kugundua Lanlan alikuwa ni mtoto wa damu kwa Roma.
“Bado hujashiba tu wewe kibonge licha ya kula sambusa zote zile kwenye ndege , kama utakula tena sasa hivi utazidi kuwa bonge , haya nenda kalale kwanza ukiamka ndio utakula”Aliongea Roma na kisha akamsalimia Qiang Xi.
“Qian naomba ukae hapa kwa Nasra kwa muda na
Lanlan mpaka nitakapoweka mambo sawa ”Aliongea Roma na Qiang bado alionekana kuwa na wasiwasi.
“Mr Roma je haya yote ni kutokana na makosa yangu , nadhani kama ningesema mapema mambo yasingekuwa hivi”
“Usifikirie sana , haya ni maswala yangu na Edna wewe hayakuhusu , hakikisha tu unamlea Lanlan vizuri maana wewe ndio unamjua na utamwambia Nasra mahitaji ya Lanlan.”Aliongea Roma na kisha akamgekukia Nasra.
“Nasra huyu mwanamke mwenzio hapa kasema anataka kukaa kwako maana unajua kupika hivyo nitamuacha hapa”Aliongea Roma na kisha akatoa kadi ya benki na kumpatia Nasra.
“Kwenye akaunti ya hii kadi kuna zaidi ya bilioni za kitanzania wewe chukua kiasi kinachotosha kwa ajili ya matumzi ya Lanlan, lakini usimsikilize kila anachotaka , mahitaji yake nadhani yatakuwa ni ada ya kule shuleni kwao , chakula kitamu na vinywaji , hata kama mimi ni tajiri sitaki kumharibu mtoto wangu hivyo naomba usimdekeze sana”Aliongea.
“Najua chakufanya wala usajli , ijapokuwa mimi sio tajiri kama Edna lakini nitakuwa na uwezo wa kumlea Lanlan”Aliongea huku akimrudishia Roma ile kadi na kumfanya Roma kutabasamu.
“Sijasema kwamba huna hela , ni kwamba tu sijatimiza wajibu wangu kama baba tokea alipozaliwa , hivyo nataka nifanye vitu kwa hela yangu nadhani nitajisikia vizuri , naomba tusipingane kwa vitu vidogo kama hivi”Aliongea Roma.
Nasra aliweza kujua hisia za Roma kupitia maneno yake na kimya kimya aliichukua ile kadi, ijapokuwa ni kadi yenye hela nyingi lakini kama Roma alivyosema hela sio swala la kubwa sana na alishazoea hilo tokea aanze kuwa nae kwenye mahusiano.
“Kuna swala napaswa kulishuhuglia hivyo nitaondoka na ninaweza kurudi usiku “Aliongea Roma
Alikuwa hajapata taarifa zozote kutoka kwa Omari juu ya kazi aliompatia hivyo alikuwa na wasiwasi na jambo baya kumtokea Najma na hakutaka kumwambia Nasra juu ya hilo kwani aliogopa kumfanya kuwa mwenye wasiwasi kutokana na urafiki wao hivyo aliondoka mara baada ya kuona amemkabidhi Lanlan kwenye mikono salama
OFA YA CHRISTMASS IPO NICHEKI WATSAPP 0687151346
Sent from my 23021RAAEG using JamiiForums mobile app
Mono no aware
SEHEMU YA 637.
Roma alijisikia maumivu makali kwenye moyo wake , hakuwahi kuwaza Edna anaweza kupotezea ndoa yao kirahisi namna hio huku yeye akiwa hayupo tayari ,lilikuwa swala la kushangaza kwake.
Ilimshangaza kutokana na kwamba ilionekana kabisa Edna alikuwa akimpenda Lanlan licha ya kwamba alikuwa akijua sasa kuhusu wazazi wake, lakini Roma alijiuliza inakuwaje anataka kuacha kila kitu.
Roma alijiambia hapana ni kweli amemumiiza lakini haikuwa ikimaanisha washaachana , pale pale alimgeukia mama yake.
“Mama mchukue Lanlan”Aliongea Roma.
Upande wa Blandina awamu hio alikuwa na shauku ya kumbeba Lanlan kweli,ilikuwa ni kama mara ya kwanza kwake kumbeba, lakini yote hayo yalitokana na hisia zake kubadilika juu ya Lanlan mara baada ya kumjua sasa ni mjukuu wake kamili , hakujali nani amemzaa Lanlan na alichojali muda huo ni kwamba Lanlan ni mtoto wa Roma, kwake aliona ni kama baraka kubeba damu ya Roma mkononi mwake.
Afande Kweka aliishia kumwangalia Lanlan aliekuwa kwenye mikono ya Blandina na misuli yake ya macho ikacheza , pengine kama angekuwa na Zenzhei basi angetoa cheko kubwa kwani ndio watu wawili pekee waliokuwa wakiujua ukweli kuhusu Lanlan.
Afande Kweka hakujali sana kuhusu Edna , kwake Lanlan alikuwa muhimu zaidi kuliko Edna ambaye alikuwa ni mwanamke mgumu sana.
“Edna kwa sasa ana hasira sidhani kuongea nae katika hali yake kunaweza kuleta majibu , kwanini usimuache kwanza kwa muda , ni mtu mzima na hakuna baya litakalo mkuta, akitulia utaongea nae”Alishauri Blandina.
“Mama tulia ,siamini kama Edna ni mkatili kiasi cha kutaka kumalizana na mimi bila ya kunisikiliza”Aliongea Roma na hakutaka kupoteza muda na alitoka nje .
Roma mara baada ya kutoka alifanikiwa kumuwahi Edna nje ya geti na Roma baada ya kumfikia alimshika mkono kumzuia.
“Niachie mimi , sitaki kukuona tena”Aliongea
“Mimi siamini , kwanini unataka kuvunja uhusiano wetu uliodumu kwa zaidi ya miaka miwili kirahisi hivyo?”
“Roma nadhani kuna kitu umesahau?”
“Nini ?”
“Unakumbuka makubaliano yetu siku ambayo tuliingia dili la mimi kumlea Lanlan??”
“Unazungumzi… unamaanisha yale makubaliano ya miaka miwili ya mdomo?”Aijiuliza Roma huku akiwaza na kuona ni kama ujinga na kujiuliza hata kama ni kweli walikubaliana kwanini huyu mwanamke kila kitu kwake anajali makubaliano tu.
Ni kweli Roma alikubaliana na Edna lakini siku ile hakuzingatia maneno yale kwani waliyaongea katikati ya kutaniana.
“Nilikuambia kabisa ukinichokoza kwa kuruhusu matatizo ya wanawake wako kuniathiri ndio mwisho wetu , je umesahau?”Roma alijikuta akiwa kama haelewi , ukweli ni kwamba makubaliano hayo hayakuendana kabisa na kinachoendelea hapo.
Asichokuwa akijua Roma kwa wakati huo anachomaanisha Edna ni swala la Salihi kumpigia simu Edna na kuanza kumtishia.,
“Wewe ndio Roma unaejuliakana kama mtoto pekee wa kiume wa kuendeleza familia ya ukoo wenu , Mfalme Pluto , Hades , naamini huwezi kuvunja ahadi yako?”Aliongea.
Roma licha ya kwamba hisia zake zilimwambia tukio la leo halikuwa likiendana na makubaliano yale lakini alijua pengine kuna maongezi mengine ambayo amesahau na wakati huo kila ambacho Edna alikuwa akiongea alijiona alikuwa na makosa.
“Roma nishachoka muda mrefu , kama isingekuwa kuvumilia kwa ajili ya mpendwa wangu Lanlan nisingefikiria hata kufika hapa , lakini sio mbaya sasa hivi Lanlan ashajulikana ni mtoto wako wa kumzaa hivyo simuhitaji tena , ninataka kurudi katika maisha yangu ya mwanzo kuliko kuendelea kuzungukwa na mtu ambaye moyo wako unaugawa kila mahali”
“Unaongea upuuzi , wewe sio mwanamke wa kawaida na huwezi kurudi kwenye maisha yako ya mwanzo”
“Najua pengine unaona nitakuachaje licha ya kwamba tumelala pamoja na kufanya mapenzi mara nyingi , si ndio?, usiwe mjinga mimi pia ni mwanamke wa kawaida ambaye nahitaji mwanaume wa kunituliza , siwezi kukataa ukweli kwamba wewe upo vizuri kitandani lakini hilo pekee sio la kunibakisha kwako , It’s just the toxic hormones doing its job”Hakusita kuongea hayo maneno tena akimalizia na neno la Kingereza.
Roma aliguswa mno na maneno hayo na alitamani hata kuziba masikio ake , ilikuwa ni kama vile kumbukumbu zote walizotengeneza na mwanamke huyo zimegeuka kuwa kitu kisichokuwa cha maana.
“Hakuna zaidi ya vitu viwili ambavyo mwanamke anavitaka kutoka kwa mwanaume , cha kwanza ni mapenzi ya kweli na cha pili ni matunzo , mimi Edna Adebayo hela za kujitunza ninazo , lakini mapenzi yako ya kimanyanyaso hayakidhi mahitajio yangu ya kihisia , hivyo ni rahisi kwa wewe sasa kuelewa kwamba ninakuacha na pengine ulipaswa kujiandaa kwa hii siku”.
Baada ya kumaliza Edna aligeuka na kutaka kuingia kwenye gari lakini Roma palepale alilipiga teke na hasira zake pamoja na mdudu wake aliekuwa ndani yake ni kama alishituliwa na nguvu iliotumika ililifanya gari lile kupinduka.
“Roma unafanya nini?” Edna aligeuka kwa hasira akimwangalia Roma.
“Hmmp..”Aliguna na palepale alibadilika na kutoa tabasamu la kifedhuli na kumwangalia Edna kwa ujeuri.
“Edna , ukiburi wako , kujitegemea kwako na kujiamini kwako vinatokana na hali yako ulionayo sasa hivi kitu ambacho ni tofauti na nyuma , Sasa hivi huna haja ya kudili na washindani wako wa kibiashara na huwezi kumuona tena baba yako wa kambo ambaye alikuwa akifanya hali yako kuwa ngumu, huna haja ya kuogopa wale majambazi wanaotaka mwili wako kwasababu una hela, nguvu na Koneksheni na sasa pia umekuwa mtu mwenye uwezo hata wa kupigana … sasa nakuambia hivi kama bado unataka kuchezeana akili na wanafiki ambao hata mwanzoni huku wajua na wakakuingizia kwenye hatari basi nakuruhusu fanya kama mwanzo uone, fanya michezo yako ileile ya kibiashara na hila zingine tuone kama unaweza kunikataa mimi mume wako kwa kiburi namna hio, Kwahio unasema kwamba hali yetu ya kindoa inabadilika kulingana na hali yako uliokuwa nayo pamoja na hadhi yako?,
Hicho ndio unachojaribu kuniambia sasa hivi?”Aliongea Roma na palepale alijipiga kifuani mara mbili ishara ya majivuno.
“Ndio , Mimi Roma Ramoni nina uwezo wa kupata kila ninachohitaji katikadunia hii, Mimi ni tajiri na pia nina nguvu na ninao uwezo wa kufilisi matajiri wakubwa zaidi ya mia tano kirahisi sana tena ndani ya siku moja na sio hivyo tu ninao uwezo wa kuvamia nchi na kuiweka chini yangu ndani ya siku moja , ninao uwezo wa kufanya mambo ambayo ni nje ya fikra za binadamu ili mradi nataka kufanya hivyo , Kiwango cha utajiri wangu , nguvu zangu na uwezo wangu unaweza kuvutia idadi ya watu wasiohesabika , nina ujuzi ambao unawafanya watu kuwa na wivu lakini kwa wakati mmoja wakashindwa kuiga wala kujifunza , lakini hayo yote nimeyapata hatua kwa hatua bila kupotezea fursa , ni vitu ambavyo nimevipata kupitia jasho langu , kupitia maisha yangu.
Hebu jiulize kama ningekuwa Roma mwanaume masikini ambaye naishi kwa kipato cha siku , au ningekuwa mwanaume wa nyumbani tu nisie na uwezo wowote ungeendelea kuwa na mimi , naamini usingeweza hata kuniangalia usoni mara baada ya mkataba ule wa miezi sira kuisha , usingefikiria mara mbili mbili hata kunisogelea na kulala na mimi kitanda kimoja , umeweza kufika hapa leo na mimi na kunivumilia miaka yote hiyo kwasababu ya kitu nilichokuwa nacho , ulijua kuendelea kuwa na mimi ingekusaidia katika vitu vingi , there is no love for no reaseon and no hate for no reason.
Ninakuambia hivyo kwamba mimi sio aina ya mwanaume ambae ninaweza kukusindikiza kwenda kazini kwanzia asubuhi mpaka jioni , wala kukuita CEO Edna ili kukupa heshima yako , mimi ni mwanaume ambaye siwezi kukusubiria kurudi nyumbani nianze kukunyenyekea na kuanza kukufanyia masaji na udambidamwi mwingineili tu kukufurahisha kama vile wewe ndio mwanamke mmoja tu ndani ya dunia hii , mimi ndio mimi na najulikana tokea nikiwa mdogo kwa msimamo wangu , Mtu dhaifu atakuwa mawindo ya mwenye nguvu , mwenye nguvu siku zote ni mtawala , hivyo unapaswa kujua mimi nina nguvu kuliko wanaume wengine na hiki ndio nilichokuwa nacho , ndio sifa yangu kubwa , nina wanawake wengi wa kuwajali na sina mpango wa kumuacha hata mmoja , hivyo ndio ilivyo na siwezi kugeuka nyuma , kama kweli unanipenda basi nikubali na uendelee kuishi na mimi.”
“Hivi unajua mtazamo wako wa uwazi na ujasiri wako utamfanya mtu asieogopa chochote mbele yako aonekane ni mnyonge?”Aliongea Roma kwa sauti huku akimwangalia machoni bila kupepesa.
“Sawa na mtazamo wako wa kifalme, lakini kwangu mimi sitaki kuendelea kuishi katika hali ya unyenyekevu na unyonge”Aliongea Edna.
“Kwani vipi , unapaswa kujua hakuna usawa kwenye ulimwengu huu , mimi nina nguvu ndio maana nina kundi la wanawake wanaonizunguka kwa hiari zao wenyewe , ulikuwa ni wewe mwenyewe ambaye ulisema hutojali na sasa unasema mimi nachukiza , ndio, najua kwamba nina deni kubwa kwako lakini je huna hata punje ya hatia ya uwajibikaji?, Unataka nifanye mangapi kwako ili nionekane ni wa thamani?”
“Haina maana kuongea hivyo kwa sasa , kama hao wanawake wako wanataka kuendelea kukaa na wewe basi ni juu yao , ndoa yetu ambayo ilianzia kama mkataba inaishia hapa , nilijituma pia na kujitoa kwako kama unaona haitoshi basi nakuruhusu nilazimishe kwasababu una nguvu nibakie kwako , lakini nimemaliza na siwezi tena kwa hiari yangu kuwa mkwe wa familia ya ukoo wa kweka kwani siwezi kuendelea kuwa mkeo , kama kweli wewe ni mwanaume mwenye nguvu na jasiri basi hutoshindwa kuniacha mwanamke mnyonge kama mimi nikichukua njia zangu , hatukuweza kuendana vizuri ndani ya ndoa yetu hivyo tunapaswa kuachana kwa amani..”
Aliongea Edna akiwa hana chembe ya hasira na kumfanya Roma kumwangalia kwa muda na kisha akavuta pumzi yake na kuishusha na akaingiza mkono kwenye mfuko wake na kuibuka na ufunguo wa gari wa BMW na kumuwekea mkononi.
“Unaweza kwenda , lakini sipendi kuona mwanamke ambaye nishawahi kuwa nae akimilikiwa na kufurahiwa na mwanaume mwingine … unaweza kusema mimi ni mnyama au shetani na sitojali lakini nakushauri tu usije kuthubutu kuwa na mwanaume mwingine kwani nakuhakikishia nitamuua na akijitokeza mwingine itaendelea hivyo hivyo..”
Baada ya kusema hivyo Roma aligeuka na kuingia ndani ya geti pasipo kugeuka nyuma na kivuli chake kilipotelea ndani akiwa katika hali ya upweke.
Edna alijikuta akiwa amesimama bila kusogea , maneno yake ya mwisho ambayo yalikuwa kama onyo yalimshangaza , alijikuta akivuta pumzi na kushikilia ufunguo wa gari uliokuwa kwenye mikono yake kwa muda na kisha aligeukia gari ambayo imeegeshwa kando ya geti.
Haikuwa ikieleweka anaenda wapi , lakini moja kwa moja ilieleweka hakuwa tena na sababu ya kukaa tena Iringa.
Baada ya kuingia barabara kuu aliendesha kuelekea mjini , ilikuwa ni usiku sana na giza limetawala na alikanyaga pedeli kwa nguvu na kusonga mbele na kuifanya gari hio kutoa mngurumo kama wa mnyama alieona kitoweo.
Spidi ya mwendo wa gari hio ni kama ilikuwa njia pekee ya kutuliza wasiwasi wake na maumivu na kilichoonekana ni michirizi ya machozi ambayo ilishakauka kuanza tena kupitisha maji.
Ghafla tu palepale alijikuta akihisi maumivu makali kwenye moyo wake na maumivu yale yalishitua kichwa chake na alijikuta akihisi maumivu makali ya kichwa yalioambatana na kengele kwenye masikio huku macho yakianza kuingiwa na ukungu wa kutokuona mbele.
“Pipiiii … Papaaaa…..!!!”
Ilikuwa ni gari iliobeba mbao iliokuwa mbele yake ikipiga honi kwa nguvu ikimwashiria Edna kupunguza mwendo na kutoka katikati ya barabara.
SEHEMU YA 638.
Ilikuwa ni bahati kwake kwani akili yake iliweza kurudi haraka na alifanikiwa kuzungusha usukani kwa nguvu na kukwepa gari ile.
Baada ya kujiimarisha katika usukani alijikuta akishindwa kujizuia tena na palepale jasho lilianza kumtoka kwenye paji la uso wake na alijikuta akianza kulia kwa kwikwi kiasi cha machozi ya chumvi kuingia kwenye midmo yake.
“Honey .. I’ m sorry … this is last thing ,, that I can do for you..”Alionekana kuongea akimaanisha kwamba ni kitu pekee ambacho anamfanyia Honey wake.
Lakini licha ya sauti yake hio , kutokana na upepo pamoja na ngurumo ya gari sauti yake haikuweza kusikika, isitoshe hakuna ambaye alikuwa akimsikiliza kwa wakati huo.
*****
Roma mara baada ya kuingia eneo la sebuleni alionekana kama mtua mbaye hakuna chochote ambacho kilikuwa kimemtokea , aliweza kutoa tabasamu lake hafifu na kisha akaenda kukaa mezani kwa ajili ya chakula.
Alipoulizwa kilichotokea alisema tu bila ya kuonyesha wasiwasi kwamba Edna amemua kutalakiana nae.
Tabasamu lake na utulivu ilifanya kila mtu aliekuwa akimwangalia kumuonea huruma mno , walijua ni kwa kiasi gani Roma anampenda Edna hivyo kuonyesha tabasamu ni shara ya kuficha maumivu.
Ukweli ni kwamba maumivu ambayo alikuwa akiyasikia hayakuwa yakivumilika , lakini licha ya hivo Roma hakuwa mtu dhaifu , hakuwa mtu ambaye ni wa kutaka kufarijiwa katika matatizo yake kwa kuonewa huruma.
Wanafamilia hao na wenyewe walionekana kujua mpango wake kwani hawakuongea chochote zaidi ya kuongea topiki tofauti.
Hakuna ambaye alitaka kuhoji kosa ni la nani au kumuuliza kama angejaribu kuokoa ndoa yake , hakuna ambaye alikuwa mjinga mpaka kufikia hatua hio.
Baada ya Show ya Sophia kuanza kila mmoja alikaa kwenye masofa na kuangalia kama vile ni familia ya kawaida ambayo maisha yao ni ya furaha.
Upande wa Lanlan wakati Roma anaingia aliangaza macho yake kila saa mlangoni kuona kama mama yake ataingia lakini hakuweza kuona kitu na aliishia kuwa na huzuni na hali ya kujikatia tamaa.
Lanlan hakuwa akielewa kwa undani hali halisi lakini aliweza kuhisi baba yake alikuwa na huzuni mno hivyo hakunyanyua mdomo wake na kuuliza mama yake yupo wapi.
Baada ya kumuona Shangazi yake Sophia kwenye runinga akiimba macho yake yalichanua na kusahau huzuni yake kwa muda.
Ilikuwa ni kama Sophia alivyosema ,ilikuwa ni kama hakuna ambacho kimetokea , aliweza kuonekana katika steji akivutia mno na vazi lake la kimtindo , huku kuimba kwake na namna ambavyo anacheza , ukijulimsha urembo wake ulipagawisha watu na kilichosikikika ni sauti za watu kushangilia.
Kwa jinsi watu walivyoweza kujaa pamoja na ‘engagement’ ya tukio hilo ilidhihirisha kitengo cha ‘Public relation’ kilivyokuwa imara .
Kuanzia namna ambavyo ujio mpya wa Sophia kwenye tasnia ilivyokuwa ukisambaa kwenye mitandao ilikuwa ni jambo la ya kushangaaza mno, ilikuwa ni kama vile wale ‘influencers’ wakubwa kwenye mitandao walikuwa wamelipwa kufanya hivyo, kuongea topiki inayohusiana na Sophia pekee.
Lanlan aliekaa alijikuta na yeye akionyesha furaha yake na kusimama na kupiga makofi huku akianza kumwigizia Sophia anavyoimba mpaka mwisho.
Baada ya Show kuisha wanafamilia hao walianza kumuuliza Roma kuhusu maisha ya Seventeen , mama mzazi wa Lanlan na Blandina alijikuta akisikitishwa mno na jambo hilo na kumuonea na Lanlan maisha yake yalivyokuwa mpaka kuja kumpata baba yake na Blandina alijiambia atachukua nafasi hio kumjali mjukuu wake ili tu kumsaidia mtoto wake kupunguza hatia aliokuwa nayo moyoni.
Upande wa Afande Kweka licha ya kwamba kila kitu kilianzia kwake , lakini kusikia stori fupi ya
Seventeen hatia na yenyewe haikumuacha salama, lakini kwa kujua kwamba Edna na Seventeen ni ndugu hakutaka kutia neno lolote.
Ijapokuwa Edna alisema anaachana nae kwa maneno lakini upande wa Roma hakutaka kuendelea kubakia mkoani Iringa na aliaga kabisa siku inayofuata angeondoka na Lanlan, lakini kabla ya hapo alipaswa kwanza kwenda Kigombola Medical Research institute kumtafuta Clark ili kujua matokeo ya uchunguzi wake wa kiafya.
Asubuhi yake wakati Roma na Lanlan wanataka kuondoka , waliweza kupokea ugeni wa Neema Luwazo aliekuwa ameambatana na binti yake Donyi.
Wazazi wa Neema Luwazo walikuwa na ukaribu na Afande Kweka hapo mwanzo na alifika hapo kwa nia ya kumsalimia kwani ni miaka mingi hajawahi kukutana nae, lakini ukiachana na hilo alionekana kama mwanamke ambaye ni kama alikuwa akijaribu kutafuta nafasi yake kama mojawapo ya wanawake wa Roma katika familia hio.
Afande Kweka alifurahi pia kuwaona na alipendezwa na namna Donyi alivyokuwa mkubwa , ijapokuwa ni mtoto wa marehemu Kigombola ambaye alikuwa ni hasamu wake kwenye baadhi ya mambo lakini hakuwa akimchukia Kigombola , wazungu wanasema hakuchukulia utofauti wa mitazamo yao kuwa ‘personal’ .
Roma alimuuliza Neema Iringa anafanya nini na Roma alishangaa mara baada ya kujua Neema alikuwa ni mbunge wa viti maalumu mkoa wa Njombe.
Roma hakuwa na uwelewa na maswala ya kisiasa sana hivyo siku zote alikuwa akijua Neema Luwazo alikuwa ni naibu waziri na mbunge kwa wakati mmoja.
“Neema nimesikia kuna kaka yako ambaye anasimamia biashara zako Urusi ni kweli?”Aliuliza Afande Kweka.
“Ndio , anaitwa Msechu amerudi juzi nchini kwasasa yupo Dar es salaam kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa mwaka na atarajea kazini Janauri”
“Oh..nadhani ni vyema vijana wakaenda kuishi nje ya nji uli kujua ulimwengu vizuri … nimesikia habari za jeshi letu kuwa katika mazungumzo ya kusafirisha silaha kutoka Urusi kuja Tanzania mwaka ujao katika muda wa nusu mwaka , biashara yako inafanya vyema nchini Urusi kuliko kampuni yoyote hapa nchini , nadhani hili ni swala zuri kwa taifa..”Aliongea na kumfanya Neema macho yake kuchanua , alikuwa ashaelewa ni taarifa gani Mzee Kweka anajaribu kumfikishia.
Ukweli ni kwamba mataifa mengi ya Afrika yalikuwa yakitumia fursa ya Vita inayoendelea kati ya Urusi na Ukraine kununua siraha kwa wingi kuingia nchini, ilikuwa ni fursa kwani vita ilikuwa ni kama mpango wa Urusi kupumbaza mahasimu wake wa kibiashara ili kuweza kuuza zaidi na zaidi siraha katika mataifa yaliohitaji bila ya kushitukiwa na Marekani kwa kivuli cha kusaidia mataifa hayo Nafaka.
Ilikuwa ni ngumu Kwa Neema kujua mchakato wa serikali katika kuagiza siraha kutoka nje ya nchi na watu ambao walikuwa na koneksheni za aina hio ni kama Afande Kweka ambaye mzizi yake ndani ya jeshi ilikuwa mirefu sana hivyo alikuwa akijua kila mipango iliokuwa ikiendelea.
Ukiwa na njaa ya pesa ni rahisi pua zako kunusa harufu ya chakula , hivyo Afande Kweka alichokifanya ni kuachia harufu ya chakula kwa Neema mwenye njaa.
Baada ya Neema kuelezea muundo wa biashara yake ndani ya taifa la Urusi alionekana kuridhika na kisha alitoa simu yake na kupiga sehemu na kisha akatoa maagizo flani ambayo yalimfanya Neema moyo kudunda, alijua hata kama alikuwa akienda kuisaidia serikali kuingiza siraha nchini lakinni faida yake ingekuwa mara mbili na biashara yake ya mahoteli.
Baada ya kuongea na Neema kwa muda Afande
Kweka aliitwa na kuambiwa kuna wageni wamefika kwa ajili ya kikao na aliwaacha Roma kuendelea kuongea.
“Lanlan naona unachukulia faida ya uwepo wa mimi shangazi yako hapa , haya niambie mama yako yupo wapi?”Aliuliza Neema.
Alishangazwa na kutokumuona Edna lakini tofauti na kumuuliza Roma aliona atumie akili kumuuliza Lanlan.
“Mommy was angry and she left..”Alijibu Lanlan akimaanisha mama yake alikuwa na hasira na akaondoka.
Neema alishangazwa na maneno ya Lanlan na alijikuta akimwangalia Roma kwa namna ya kutaka maelezo.
Upande wa Roma aliishia kutoa tabasamu la uchungu na alijikuta akielezea kwa ufupi kile kilichotokea usiku wa jana yake
“Kama ni hivyo basi naamini atakuwa amerudi moja kwa moja Dar es salaam kwa sasa?”
“Kwanini unaongea kwa uhakika hivyo?”
“Kwanini nisiongee hivyo, kwanza kabisa hapa Iringa kwasasa ni eneo ambalo hana mtu wa kuongea nae na lenye huzuni na pili kampuni ya Vexto ipo katika mabadiliko makubwa ambayo yanapangwa kufanyika kwanzia mwezi wa kwanza mpaka wa sita na Edna anapaswa kuyasimamia mwenyewe.. “Aliongea Neema na kumuona Roma kuwa kwenye mshangao na alijua fika pengine hakuwa akijua kuhusu hilo.
“Usiniambie hujui kitu ambacho Edna alikuwa akifanya kwenye siku hizi za hivi karibuni?”
“Huwa hatuongei sana kuhusu maswala yake ya kikazi , lakini si alikuwa akimsaidia Sophia kurudi katika tasnia ya sanaa?”
“Ah..! ni kwasababu ndio kwanza umerudi hivyo huwezi kujua kilichokuwa kikiendelea kwa mwezi mzima , kurudi kwa Sophia ni ili kuipa nguvu kampuni ya Vexto kama sehemu tu ya mipango yake , Kujiuzulu kwa Edna ilikuwa ni mwanzo wa kitu kingine kabisa , wakati alipojiuzulu alipunguza hisa zake zote kutoka asilimia tisini mpaka asilimia hamsini na moja,kwa ajili ya kuongeza ‘Shareholder’s’ wengi kwenye kampuni yake ili aweze kukidhi vigezo vya kimataifa kuibadilisha kampuni kutoka katika uhalisia wa jina la Vexto International kwenda Vexto Group”
“Vexto Grup , lakini si ilikuwa ni Vexto Group hapo kabla?”Aliuliza Roma na kumfanya Neema kutoa kicheko.
“Inaonekana kufanya kwako kazi ndani ya Vexto kulikuwa ni bure kabisa, ni kweli ilikuwa hivyo lakini haikuwa imekidhi vigezo vyote , unapaswa kuelewa kwamba ili kampuni kuweza kuitwa Group of Companies na kushiriki katika masoko ya hisa kimataifa inapaswa kuwa na Bodi ya wakurugezi ambayo ina nguvu ya kumuondoa na kumuweka Mkurugenzi mkuu kwa kumchagua ili kulinda maslahi yao ndani ya kampuni, hio ni sifa ambayo Vexto haikuwa nayo,yaani Edna alikuwa ndio mwamuzi wa mwisho kutokana na kuimiliki kampuni yote , lakini mara baada ya kuuza hisa za umiliki wa kampuni kwa nusu nzima inamaanisha kwamba kampuni sio ya kwake peke yake bali yeye
ni mmiliki mkubwa hivyo maamuzi makubwa ya kikampuni lazima yapite kwenye bodi kabla hayajafanyiwa kazi, Mpango wa Edna ni kuifanya Vexto kuwa kundi la makampuni huku yeye akiwa ni mtendaji mkuu na atakuwa amejiongezea nguvu mara mbili na ile ya mwanzo , kwanza kampuni itapanuka sana , lakini pia atakuwa na uwezo wa kujiingiza katika biashara ambazo hana hata uwelewa nazo , kwa mfano anaweza kuunda kampuni ya maswala ya kiteknolojia na ikafanya vizuri kwa kuajili watu wenye uwezo huo au anaweza kufunga zilizopo na kununua nyingine”
Neema alimpa shule Roma na kumfanya kukosa neno la kusema , alijiambia ndio maana Edna alikuwa mwepesi kumpisha Ernest kushika wadhifa wake kumbe kulikuwa na mpango mwingine anawaza kichwani.
Haikuwa hivyo tu Roma alikuwa akijua Edna alijiuzulu kwa ajili ya kujiweka bize na familia kama alivyoongea kumbe yote ni uongo alikuwa akitafuta kujipa thamani zaidi na zaidi.
Ilionekana Ernest siku zote ataendelea kuwa chini ya Edna na kupokea maagizo kutoka kwake.
Kwa maelezo ya Neema ni kwamba kampuni ya Vexto ambayo anaongoza kwa sasa Ernest Komwe ingekatwa kati na kubakia kuwa Kampuni inayohusiana na mavazi na fasheni pamoja na usimamizi wa usambazaji wa malighafi mpya , huku ikiundwa kampuni nyingine Tanzu ambayo ingehusika na maswala ya mafuta ya petroli na mambo mengine.
“Umeliona lile jengo refu zuri ambalo linajengwa pale Mwenge?”Aliuliza Neema.
“Unamaanisha lile lenye urefu kwenda hewani ambalo ndio lipo hatua ya mwisho?”
“Ndio hilo?, lile ndio jengo ambalo litakuwa makao makuu mapya rasmi ya kampuni ya Vexto Group”
“Nilijua lile jengo linajengwa na Vexto Constructor na mmiliki wake ni kampuni ya Nebula inc, maelezo hayo niliyapata kwa Daudi nilipokuwa mkurugenzi?” “Upo sahihi linajengwa kwa ajili ya kuwa makao makuu ya Nebula Inc lakini mmiliki wa kampuni ya Nebula Inc kwasasa ni Edna , sijui kilichotokea lakini ninachojua ni kwamba safari yake ya mwisho ya kikazi kwenda Hongkong iliwezesha hilo”Aliongea Neema na Roma kuhisi kuchanganyikiwa na kujiuliza Edna sio mwanamke wa kawaida.
Roma alikumbuka siku ambayo Edna ameenda
HongKong kikazi alimuunganisha na Edward wa Rothchild kumrahisia shida yake, pengine aliamini kuna mengi zaidi ambayo yaliendelea na Edward hata hakumwambia.
“Kwanini unayajua hayo yote?”
“Kama mpango wa Edna utafanikiwa basi sio kwamba tu atakuwa mshindani wangu wa kibiashara bali makampuni mengi ndani ya Tanzania yanaweza kumezwa, hivyo lazima na mimi nijiandae namna ya kuifanya kampuni yangu iendelee kuishi, ndio maana napanga kujiuzuru nafasi yangu ya uwaziri nibakie katika uendeshaji wa biashara”Aliongea na Roma hakutia neno.
Roma aliishia kujikuna kichwa chake , alijiambia mbona anazidi kuwa butu wa kifikra au ni kwasababu hakuwa na uwezo wa kutumia uwezo wake , maana IQ yake ilikuwa imeshuka mno”
“Halafu ukichana na hayo , nahishi kilichotokea jana yake sio kawaida”Aliongea Neema akimwangalia Roma anaejikuna kichwa.
“Unamaanisha nini?”
“Sidhani kama Edna ni mtu wa kushindwa kujizuia na kutaka kumuua Sophia kwasababu tu ya wivu , kama ni hivyo si anapaswa kuniua na mimi?”Aliongea.
“Unaongea utani mpaka sasa hivi tu?”Aliongea Roma akitoa tabasamu la kulazimisha.
“Najaribu kukufurahisha , wewe mwanaharamu usie na shukrani”
“Unapaswa kutania vitu vingine , sitaki kuona yeyote kati yenu akiumia la sivyo itanifanya kuonekana nimefeli”Aliongea na kumfanya Neema kujisikia vizuri.
“Nilichokuwa nikitaka kumaanisha ni kwamba , Edna anaonekana na tatizo ambalo linamsumbua hata kabla hujarudi nilishawahi kumuuliza lakini hakuongea chochote”
“Kwahio unamaanisha hujui chochote kwasababu hajakuambia chochote?”Aliongea Roma akijikatia tamaa.
“Mimi naongea tu , nitajuaje anachoficha kwenye moyo wake ,isitoshe si vizuri tu kwani nimepunguza mshindani mwingine , unajuaje siku moja nikabakia peke yangu”Aliongea na kumfanya Roma kumchapa kibao cha mapajani.
“Ukiendelea hviyo nitaondoka sasa hivi na Lanlan nimtafute nimuulize mwenyewe”
“Haha.. ukweli ni kwamba najua swala la Lanlan lilikuwa kubwa kwake lakini kwa ninavyoona kwa kutoshindana kwake na wewe katika maswala ya nani amlee Lanlan ,naamini wewe anakuchulia ni wa muhimu zaidi kwake”
Roma aliona maneno ya Neema yapo sahihi , ijapokuwa Edna mara baada ya kujua kuhusu Lanlan hakuonyesha kutatizwa na hilo na alichokuwa akiongea ni tofauti kabisa kama sababu ya kumuacha.
Roma mara baada ya kuachana na Neema moja kwa moja alichukuana na Lanlan na kuelekea nae chuoni maaabara kwa ajili ya kumtafuta Clark ili ampatie majibu yake.
Baada ya kufika na kuongea kidogo na Clark kwa kumtambulisha Lanlan kama mtoto wake wa damu aliemzaa na Seventeen waliingia kwenye maswala ya matibabu lakini licha ya hivyo Clark alionekana kushangaa kwani hakutegemea kama Seventeen aliacha mtoto.
Lakini licha ya hivyo alifurahi na kumbeba Lanlan na alijiambia ndio maana alikuwa anafanana sana na Edna kumbe alikuwa ni mtoto wa Seventeen ambaye alikuwa akifanana na Edna.
“Huu ndio uchambuzi wa taarifa za uchunguzi niliokufanyia , unaweza kujionea mwenyewe”Aliongea Clark akimpatia Roma makaratasi.
“Mimi sijui chochote hapa , nadhani ni vyema kama utanielezea mwenyewe”
“Kwa haraka haraka naweza kusema kwamba kuna taarifa nzuri na mbaya , ipi ndio unataka ianze”
“Tuanze na hio taarifa nzuri kwanza”
“Taarifa nzuri ni kwamba mwili wako umekuwa na nguvu zaidi ya mara tatu kuliko mwanzo tokea mara ya mwisho nilipokufanyia vipimo , hii ni tofauti kwasababu nilitegemea uvimbe wako kuongezeka kwake ndio kupungua kwa uwezo wako , lakini vipimo vinaonyesha ni tofauti , kwasasa naweza kusema mchakato wako wa ukuaji wa kimwili ni kama ‘Metarmophosis’.. lakini umeruka hatua mbili mbele za kiukuaji”Aliongea na Roma alielewa kwa haraka.
“Vipi kuhusu taarifa mbaya”
“Taarifa mbaya ni kwamba ni nusu ya taarifa nzuri , sikujua mwanzo lakini mara baada ya kuvuna nishati za mbingu mwenyewe nimeweza kujua baadhi ya vitu ambavyo havina maelezo ya kisayansi … utendaji wako wa kazi katika ubongo umekuwa wa tofauti sana na nilikosa taarifa za kisayansi kugundua sababu ya mabadiliko hayo , lakini kwa haraka haraka naweza kusema kuna nguvu iliopo ndani yako inayoshindana na mfumo wako wa mawasiliano wa kawaida wa mwili , ni nguvu ambayo naweza kusema haipaswi kutokea kwa wakati mmoja(Mutual exclusive)… na kwasasa nguvu hizo zipo katika hali ya uwiano sawia… kwa maneno marahisi ni kwamba licha ya nguvu zote kuwa kubwa kwa kulingana itakuwa ngumu kwako kuishinda na kuvunja huo uwiano ,,, kwahio ni kama umefungwa”
SEHEMU YA 639.
Roma alishika kichwa chake akionyesha hali ya kushikwa na mawazo na palepale alivuta hewa nyingi na kuitoa nje akionyesha hali ya huzuni kidogo.
“Ulivyoelezea ni kama ambavyo nimefikiria na umethibitisha tatizo langu, lakini tatizo lingine ni kwamba ni kipi napaswa kufanya”
“Kwa ninavyoona kutumia njia za kawaida za kisayansi haziwezi kuwa na ufanisi , lakini … umesahau kwamba wewe sio mtu pekee ambaye unamiliki nguvu za kijini?”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha ni swala la kinadharia … ninajiuliza je haitowezekana kutumia nguvu kubwa ya nje kukuongezea uwezo wa kuweza kutawala nguvu inayoshindana na ya kwako , kitu pekee ambacho kwasasa unaweza kufanya ni kuendelea kushikilia uwiano lakini vipi kama kuna nguvu nyingine ya nje ambayo inaweza kukusaidia kwa kukuongezea nguvu , Rose na Magdalena wote washaingia katika levo ya Nafsi , licha ya kwamba wanaweza kuwa na nguvu ambazo ni za chini na ya kwako watakuwa na nguvu ya kijini ya kuweza kukusaidia na kuvunja uwiano na wewe kushinda”
Roma macho yalichanua mara baada ya kusikiliza pendekezo hilo zuri lakini alitingisha kichwa kukataa .
“Hapana , itakuwa ni hatari sana kwao, roho ya mnyama ni ya hatari sana na ina nguvu ya giza , kama mambo yakienda vibaya Rose na Magdalena wanaweza kupatwa na tatizo”
“Basi usiwe na wasiwasi naamini kutakuwa na mbinu nyingine zaidi , isitoshe nitaelekea Dar na nitakutana na Rufi na atanipa baadhi ya taarifa ambazo zinaweza kunisaidia kutengeneza njia mbadala ya kukusaidia”
Roma aliishia kukubali, ijapokuwa swala lake hakutaka lifahamike kwa wanawake wake lakini kwa upande wa Rufi aliona tu ngoja ajue ,lakini alijihakikishia kwamba asingetumia pendekezo la Clark la kuwatumia Magdalena na Rose kumsaidia mpaka awe na uhakika wa usalama wao.
******
Upande wa Dar hali ya hewa ilikuwa ya mawingu na vipindi vya jua ikiashiria muda wowote mvua inaweza kunyesha , ilikuwa ni kama ilivyotabiriwa katika kipindi cha hali ya hewa jana yake kuonya mvua kubwa ingeweza kunyesha.
Najma alikuwa na ugeni ndani ya sehemu anayoishi , alikuwa ni Shangazi yake na wifi yake ambao walilala hapo na asubuhi hio walikuwa wakijiandaa kwenda kutembea.
Shangazi yake Najma hakupata utulivu , tokea mara ya kwanza kuonja utamu wa kupanda gari ya pesa nyingi kila saa alitaka kulipanda na siku hio ambayo Najma alikuwa Off alilazimisha kwa kumtaka Najma kwenda kutalii talii kupoteza muda ndio warudi nyumbani kwao.
Najma hakuwa na tatizo kwani alikuwa off lakini ukweli ni kwamba alitamani siku hio kuitumia katika mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi na jioni kwenda kumtembelea rafiki yake Nasra lakini ujio wa shangazi yake na wifi yake ni kama ulivuruga ratiba zake.
“Katika maisha yangu sijawahi kuwaza kama kuna mwanafamilia katika ukoo wetu ambaye anaweza kumiliki gari kama hii”Aliongea Shangazi yake Najma huku akitoa kicheko .
“Shangazi unasemaje hivyo , lilikuwa swala la muda tu kwa Najma , uzuri wake sio wa kawaida hata hivyo”
“Haha.. umeongea kweli mwanangu, Najma amezaliwa kwa ajili ya vitu kama hivi.. Najma kama asingekuwa ubishi wake kipindi kile angekuwa sasa hivi ashazalishwa na yule Ahmed kina kifupi na gari angekuwa anaiota ndotoni tu”Aliongea huku wakicheka na kugongesheana mikono na mke wake Juma.
Najma alishindwa kuchangia neno na maneno ya shangazi yake yalimkumbusha mwaka uliopita namna ambavyo Shangazi yake na kaka yake walivyokuwa kidedea kumtaka aolewe na Ahmedi ,lakini kwa namna ambavyo shangazi yake anaongea ni kama amesahau kabisa na hakuonekana kuwa na hatia tena saivu anamwita Ahmedi kina kifupi.
Ni mara baada ya Najma kuingiza gari barabarani ghafla tu ilitokea gari aina ya Ford SUV ya rangi nyeusi na kuwazibia njia mbele yao.
Najma aliekuwa ni dereva alijikuta akikunja sura na alijaribu kupiga honi na kuwasha taa kuashilia kwamba apishwe njia lakini dereza wa gari hio alionekana hawakuwa na nia yoyote ya kumpisha.
Baada ya dakika kama tatu kupita gari ile ilifunguliwa milango yote na waliweza kutokezea wanaume wanne wenye miili mikubwa ya mazoezi wote wakiwa weusi waliovalia mavazi ya suti nyeusi kama mabodigadi pamoja na miwani za jua huku wote kwa pamoja wakiwa wameshikilia mitalimbo ya chuma mkononi.
Najma palepale alijikuta akinusa hatari na alimwangalia Shangazi na Wifi yake ambaye alikuwa amepakata mtoto mdogo na kuwaambia watoke kwenye gari haraka.
Lakini licha ya Najma kuongea wale wanaume kwa haraka walisogelea gari na kwenda kusimama kwenye mlango wa gari huku kiongozi wao aliekuwa akivuta sigara alitoa cheko la kebehi akiwa mbele ya gari.
“Bang!!”
Yule kiongozi wao mara baada ya kusogea mbele aliinua chumba chake kigumu na kupiga kwa nguvu mbele ya boneti ya gari ya Najma na kulifanya libonyee kwa mbele palepale na taa zote kuvunjika.
Waliokuwa ndani ya gari waliishia kutoa kilio cha mshituko huku sura zao zikijawa na wasiwasi na kuanza kutetemeka kwani sio tukio la kawaida.
Ilikuwa ni kama wameagizwa vile kwani wale watatu waliokuwa wamesimama kwenye milango ya kutokea walianza na wao kulipiga na vyuma lile gari kuanzia nyuma mpaka juu ya paa.
Hawakujali mtoto aliekuwa akitoa kilio ndani ya gari na wao waliendeleza kazi , Mke wa Juma alijikuta akimziba mtoto wake masikio huyu yeye akitetemeka kwa hofu.
Ilikuwa ni bahati kwamba waliweza kufanikiwa kutoka bila kupata madhara lakini gari iliharibika sana na kubadilika muonekano na haikuwa gari tena ile mpya ambayo ilikuwa ya bei ghali.
Tena mara baada ya Najma na ndugu zake walivyotoka ndio walivyozidi kuliharibu lile gari kwa spidi kubwa na walipasua vioo vyote na kuchokonoa na eneo la injjini na moshi ulianza kufuka.
“Nyie ni wakina nani , kwanini mnatufanyia hivi?”Aliuliza Najma aliekuwa akitetemeka kwa hasira , hakuamini gari ambayo amepewa kama zawadi na mpenzi wake imepatwa na majeraha ya aina hio tena ndani ya siku mbili tu.
Yule kiongozi mara baada ya kumuona Najma amenyanyua mdomo na kuongea alimwangalia kwa dharau.
“Mrembo , ni kosa lako mwenyewe kutoka kimapenzi na mwanaume ambaye sio saizi yako na kumkasirisha yule mwanamke, hili ni onyo tu ambalo tumejaribu kukufikishia kutoka kwa mwanamke uliemchokoza , usije kuthubutu kuwa karibu na Boss wa kiume tena , siku nyingine haitoishia kwenye kuharibu gari tu bali ni …”Aliongea huku akionyesha ishara ya kuua.
Baada ya kuongea maneno hayo Najma palepale alijua nani ambaye amewatuma hao majambazi , kumbe ni mwanamke ambaye anamjua kama mama yake Naibu waziri Salihi ndio ambaye amekuja kumshambulia kwa kuagiza watu wake bila sababu za msingi kisa kumuona akiongea na Salihi.
Najma alijikuta akitokwa na machozi na kumwangalia shangazi yake ambaye amekatwa na kioo kwenye bega na alijikuta akipatwa na ahueni mara baada ya kuona mtoto hajapatwa na majeraha.
“Kama ni hivyo kwanini mnaingiza watu wengine ambao hawahusiki, hawa ndugu zangu wamefanya nini , kwanini msingesuburi nikiwa peke yangu ndio mnishambulie”
“Haha… wewe msichana tena nyamaza, nishaharibu magari mengi tu kama hivi lakini sijawahi kuona msichana jasiri kama wewe ambaye unaongea mara baada ya kukushambulia kama hivi , ni bahati mbaya kwamba licha ya kutufokea kwako ni bure , kazi nilioagizwa leo hii ni kuharibu gari yako basi nikirudi jua ni zamu yako”
Najma alijikuta akikosa neno la kuongea na kuishia kuwaangalia kwa hasira lakini wanaume wale hawakuonekana kuwa na hofu kabisa licha ya kufanya tukio hilo mchana kweupe na baadhi ya watu wanaangalia.
Najma palepale wazo la kupiga simu polisi lilimjia na alitoa simu yake na kutaka kupiga , lakini wale watu walikuwa wakimwangalia tu anachotaka kufanya.
“Hehe ndio unajaribu kupiga simu polisi.. haha utakuwa unachekesha , kama tungekuwa tunaogopa polisi tusingeharibu gari yako wale watu wakiwa wanaangalia tena mchana kweupee”Aliongea na kuwafanya wale wanaume wengine kucheka na kisha walipeana ishara na kuingia kwenye gari yao .
Najma licha ya kuona gari yao imeondoka hakughairisha kwenye kupiga simu polisi na mara baada ya kuelekzea kila kitu palepale alimkimbilia wifi yake.
“Wifi mtoto yupo salama?”Aliuliza na mke wake Juma alishia kutingisha kichwa huku machozi yakimtoka.
“Najma umemchokoza nani , hawa majambazi ni wakina nani?”Aliuliza Shangazi yake Najma huku akishika jeraha lake ambalo lilikuwa likivuja damu.
“Sijui chochote Aunt , ngoja tusubiri polisi wafike na tuone watapata nini kupitia uchunguzi wao”Aliongea kwa kutetemeka.
“Najma inaoneana aliefanya hivi anakisasi ,ijapokuwa sijasikia vizuri lakini inaonekana ni mwanamke aliegiza ufanyiwe hivi , Najma hebu niambie ni mke wa Roma ndio kakufanyia hivi?”Aliuliza Shangazi yake Najma kwa wasiwasi.
Ijapokuwa alikuwa akijua Edna alikuwa mtu mzuri mpaka kumsaidia Juma kupona kwa kulipia matibabu lakini swala la Najma kujihusihsa kimapenzi na Roma lilikuwa ni tofauti hivyo aliona kwa upole wa Najma ambaye ni ngumu kutengeneza maadui basi mtu pekee anaeweza kutuma kumshambulia ni Edna.
“Shangazi hapana, Sister Edna hawezi kunifanyia hivi, ni swala ambalo halihusiani na Roma kabisa , msiwe na wasiwasi hili nitalimaliza mwenyewe”Aliuongea
“Utalimaliza vipi Najma? , licha ya kwamba unafanya kazi wizarani nafasi yako ni ya kawaida na huna koneksheni yoyote , nadhani umewasikia wenyewe hawaogopoi polisi , unadhani bila ya kuwa na nguvu unaweza kuwashitaki , mpigie Roma umwelezee sasa hivi , ndio mtu pekee anaeweza kukusaidia mpigie umwambie kila kitu…nimechukia sana”Aliongea huku akionyesha kukosa uvumilivu na kuongea kwa sauti ya kufoka.
“Lakini Roma hayupo hapa Dar”
“Mpigie kama kweli anakupenda hawezi kudharau matatizo yako, fanya hivyo Najma kwa usalama wako , awamu nyingine watakuja kukua wewe mwenyewe ohoo”
“Najma kweli fanya kama Shangazi anavyosema, inaonekana mtu aliefanya hivi ana kinyongo na sio mwepesi kudili nae kupitia polisi”
Najma alijikuta aking’ata lips zake kwa aibu , alikuwa pia akitamani kumpigia Roma simu na kumwambia yaliotokea lakini aliogopa Roma angemwelewa vibaya kuhusu kuhusika kwa mama yake Waziri Salihi , isitoshe gari la mamilioni ya pesa ambalo amemnunulia juzi tu ndio hilo lishaharibiwa na hakujua namna ya kumwelezea Roma , ki ufupi aliogopa.
Najma aligeuza macho yake na kumwangalia Shangazi yake aliekuwa akimkodolea macho akiwa na hasira kwa udhalilishaji waliofanyiwa na Najma aliishia kujawa na hofu na kisha palepale aliitafuta namba ya Roma na kupiga.
Lakini alikuja kugundua namba ile haikuwa hewani kwani aliambiwa simu ilikuwa imezimwa.
“Amezima simu yake na hapatikani pengine kuna kinachoendelea”
“Basi nadhani hatuna jinsi , subiri baadae umpigie kwasasa tunapaswa kusubiri hao polisi tuone wataongea nini mara baada ya kufika,Looh zote hizi ni laana ya umasikini inayotunyanyasa…pukeee!!”Aliongea Shangazi huyo akitema mate chini huku hata yeye licha ya kushambuliwa lakini alihurumia gari mbaya ambayo haikuwa na ule muonekano wa mwanzo.
“Najma ikitokea anataka kununulia gari nyingine mwambie akunulie hata ka Spacio , nadhani mizimu ya ukoo haitaki tupande magari ya kifahari”Aliendelea kuongea.
*****
Upande wa Roma muda huo ndio alikuwa akiingia ndani ya ndege na alitii sheria na kuzima simu yake.
Roma alikuwa amekaa na binti yake katika daraja la kwanza katika ndege hio ya shirika la taifa na ilichukua dakika chache tu mara baada ya kutulia Lanlan alipitiwa na usingizi.
Mdada mrembo mhudumu mara baada ya kufika kuwahudumia abiria wa daraja la kwanza alijikuta akivutiwa na mwonekano wa Lanlan na mara baada ya kujua baba yake na yeye amefumba macho alitoa simu yae akitaka kupiga picha lakini Roma aliyafumbua na kumwangalia.
Roma hakuonyesha kufurahishwa na kitendo cha muhudumu huyo anachotaka kufanya na alinyoosha mkono kama vile anataka kitu kutoka kwa mhudumu huyo lakini yule mrembo aliishia kutabasamu huku akiona aibbu amekamatwa.
“Samahani kwa kukusumbua Sir , je naweza kukuuliza ni kipi unahitaji?”
“Pesa bila shaka , kipi kingine naweza kutaka , huwezi kumpiga picha binti yangu mrembo bila malipo , hata ukienda mbuga za wanyama kuna kiingilio cha pesa unacholipia sembuse binti yangu mzuri hapa,”Aliongea Roma akiwa siriasi.
Yule mrembo aliishia kuona aibu lakini kwa siri akivuta mdomo na kujiuliza imewezekanaje mwanaume asie na aibu kama huyo kukaa daraja la kwanza , alijiambia ashukuru Mungu kwa kumtunuku binti mrembo kama huyo maana hakuwa akiendana na mwonekano wake.
Ijapokuwa alikuwa akimdhihaki Roma ndani kwa ndani lakini kutokana na taaluma yake iliendelea kumwonyeshea tabasamu la ukarimu.
Palepale alitoa baadhi ya matunda na Sambusa wa nyama kwenye kijitoroli chake na kumpatia Roma kama rushwa ya kumtuliza.
Roma mara baada ya kushika sambusa aliisogeza karibu na pua za Lanlan na palepale alishituka kutoka usingizini na kupokea ile sambusa na kuila yote ndani ya dakika na kisha Roma akachukua na nyingine na kumpatia na aliipiga yote ikaisha na kisha aligeuza macho yake na kumwangalia mhudumu wa ndege.
Mhudumu yule aliishia kushangaa tu na ilikuwa afadhali kwani ndani ya daraja la kwanza chakula cha abiria kilikuwa cha kutosha hivyo alimpatia Lanlan nyingine na kisha akawaacha.
“Daddy , are we going to find mommy?”Aliuliza Lanlan na kumfanya Roma kukakamaa mwili na kumwangalia Lanlan akitafuta jibu la kumpa.
“Mama sasa hivi hana furaha baada ya kugombana na Daddy, .. Daddy atamshawishi mama baada ya muda ili arudi , kwasasa uwe mtiifu kumsubiri mpaka arudi”
“Kwahio Daddy unamaannisha siwezi kulala na mama tena?”
“Ndio , mama yako hatoturuhusu turudi nyumbani kwasasa”Aliongea Roma akionyesha mwonekano wa kimawazo.
“Can Lanlan Sleep with Aunt Nasra?”Aliuliza kwamba je anaweza kulala na shangazi yake Nasra.
“Wewe mtoto msaliti , unataka kumuacha mama yako kirahisi hivyo , unampenda Aunt Nasra sana?”
“Bibi amesema watoto hatupaswi kuingilia maswala ya wakubwa na kama nitaendelea kuwa mtiifu basi nitaendelea kula chakula kitamu , Aunt Nasra anapika chakula kitamu”Aliongea na kumfanya Roma kuelewa sasa kumbe ukaribu wa Lanlan na Nasra ni kwenye mapishi.
Roma kwa alivyokuwa akijua wanaojua kupika sana ni Nasra na Najma , Dorisi alikuwa fundi kwenye upishi lakini alikuwa mvivu ila Nasra alikuwa akipenda kupika sana na chakula chake ni kitamu ,hakujua Lanlan amekionja lini lakini hakutaka kuuliza sana.,
Ukweli ni kwamba Blandina alimwambia Lanlan akakae kwa Nasra mpaka mama yake atakapomtafuta.
Roma licha ya kwamba alijua Lanlan kwenda kukaa kwa Nasra kunaweza kumfanya Edna azidi kukasirika lakini hakuwa na chaguo lingine zaidi ya kumpeleka huko alikotaka.
Baada ya lisaa limoja na nusu Roma aliweza kufika Dar es salaam huku Lanlan akimwambia baba yake kama wangepaa wangekuwa washafika , lakini Roma aliishia kumjibu Lanlan atapaa nae siku nyingine ila ajitahidi aweze kupaa mwenyewe.
Roma mara baada ya kuwasha simu yake alishangaa baada ya kuona Missed call ambazo zilikwua zimeingia kwenye simu yake zikitoka kwa Najma.
Roma alisimama akiwa amemshikilia mkono Lanlan na kuanza kufanya mawasiliano kwani alihisi kuna kitu hakipo sawa na mara baada ya kupiga kwa dakika kadhaa simu haikupokewa kwani haikuwa ikipatikana hewani na jambo hilo lilimpa mashaka
na palepale aliitafuta namba ya simu ya Juma na kupiga na iliita mara moja tu na kupokelwa.
“Roma Bro mbona hukuwa ukipatikana hewani , tafuta namna ya kumsaidia Najma , amekamatwa na polisi”Aliongea Juma akiwa na wasiwasi na kumfanya Roma kushangaa.
SEHEMU YA 640.
Roma alijikuta akipatwa na wasiwasi na kujiuliza imekuwaje Najma akaishia kwenye mikono ya polisi.
“Juma hebu ongea taratibu taratibu uniambie nini kimetokea”Aliongea Roma na pale Juma alimpatia simu shangazi yake na kuanza kuelezea tukio.
Ilionekana mara baada ya polisi kufika ndani ya nusu saa walijairbu kumhoji Najma juu ya kilichotokea na mara baada ya kuelezea polisi walimchukua na kuondoka nae huku wakisema anaenda kusaidia maswala ya uchunguzi zaidi.
Lakini ajabu ni kwamba baada ya lisaa Najma simu yake haikuwa ikipatikana tena na wamejaribu kwenda kwenye kituo cha Oysterbay ambacho inasemekana alipelekwa lakini walikosa ushirikiano kutoka polisi.
“Basi naomba mpunguze wasiwasi nitadili na hili swala mwenyewe”Aliongea Roma na muda huo walikuwa tayari washaingia kwenye taksi.
Roma aliambiwa Najma alipelekwa kituo cha Oysterbay na alitamani kwenda moja kwa moja lakini alijiambia anaweza kafanya kitu kibaya hivyo aliona hatua ya kwanza ni kumpeleka kwanza Lanlan nyumbani huku yeye akitumia koneksheni zake kujua nini kinaendelea.
Baada ya kufikiria nani ambaye anaweza kumsaidia swala lake palepale jina la Omari Tozo liliibuka kwenye kichwa chake na hakutaka kupoteza muda na alimpigia.
“Hey! Bro ni mzimu gani umekupitiia mpaka ukakumbuka kunipigia simu leo , sio kawaida yako?. Nimefika Iringa jana na mpango wangu ni kukutafuta leo kwa ajili ya kwenda kupata moja moto moja baridi baada ya kupewa ruhusa na mke wangu..”
“Hebu acha ngonjera zako kwanza ,,, nina shida ya haraka nataka unisaidie, nipo Dar sasa hivi nishatoka Iringa”
“Kwanini umerudi haraka hivyo , nilijua bado upo Iringa ndio maana nimekuja huku tuonane, anyway ni jambo gani ambalo unataka nikusaidie”
“Mwanamke wangu mmoja anaefahamika kwa jina la Najma amekamatwa na watu wa polisi na kupelekwa kituo cha OysterBay na ndugu zake wameenda huko lakini hakuna ushirikiano , hebu nisaidie kutuma mtu wa kueleweka akarahisishe hilo swala na atoke polisi, najua hukosi koneksheni ndani ya jeshi la polisi maana upo kitengoni” Ukiachana na baba yake Omari kuwa mkuu wa majeshi lakini pia mjomba wake Omari yaani kaka yake mama yake ni mkurugenzi mkuu wa idara ya usalama wa taifa na pengine ndio maana ilikuwa rahisi kwa Oamri kujiunga na usalama wa taifa tofauti na kitengo cha jeshi.
“Hahaha.. kuna watu wanajiamini aisee , nani kapata ujasiri wa kukuchokoza kwa kumkamata mrembo wako”
“Hebu acha utani na fanya jambo la haraka upigie mtu afanye kurahisisha hili”
“Sawa bro usiwe na wasiwasi najua ni kipi nifanye”Aliongea Oamri na kisha akakata simu palepale.
Roma asingeweza kumpigia simu Mage kumsaidia katika hilo kwani Mage alishaachana na maswala ya upolisi na alikuwa akijiandaa kuelekea Visiwa vya wafu, lakini pia hakutaka kufanya hivyo kwani aliona sio vizuri kumpigia mwanamke wake kumsaidia mwanamke wake mwingine .
Upande mwingine ndani ya kitua cha polisi Masaki alionekana mwanaume mzee kidogo ambaye kwa kumwangalia tu ni makadirio ya miaka hamsini hivi akiwa ameketi ndani ya ofisi ndani ya kituo hicho akiwa na sigara ameishikilia mkono wa kushoto huku kulia akiwa ameshikilia gazeti la mwananchi.
Alikuwa ni Mkuu wa kituo mpya ambaye amepandishwa cheo hivi karibuni mara baada ya Mage kujiuzulu , alikuwa akifahamika kwa jina maarufu la Afande Mkanye.
Afande Mkanye alikuwa na miaka hamsini na saba na alikuwa mkali mno kiasi cha watu kuanza kumfananisha na jina lake na ilikuwa hata polisi wenzake walikuwa wakimuogopa.
Licha ya ukali wake huo kutokana na elimu yake kuwa ndogo hakuweza kupata cheo kikubwa kwa muda mrefu lakini mara baada ya Mage kuachia ngazi ndio sasa akaweza kupata nafasi ambayo ilikuwa ni ya ndoto yake kabla ya kustaafu.
Unaambiwa tokea apewe cheo hicho alikuwa akilala kituoni ndani ya ofisi yake kwenye masofa na alipoulizwa alisema anafidia siku ambazo serikali imemcheleweshea kumpandisha cheo.
Wakati akiendelea kuwa bize kusoma gazeti lake linalohusiana habari za kitaifa palepale mlango wa ofisi yake uligongwa na kuruhusu mgongaji kuingia.
Mlango mara baada ya kufunguliwa alionekana mwanaume kijana aliekuwa katika sare za polisi mwenye makaridio ya miaka therathini , alienyoa upara na ndevu zote , huku akiwa na Komwe pana na kumfanya kuonekana kama mtu mwenye kichwa kikubwa.
Bwana huyo ndio alikuwa mkuu msaidizi(Junior Superintendent) wa kituo hicho ambaye alihamishiwa mwaka huo kituoni hapo , kabla ya kuja jijini Dar es salaam alikuwa ni polisi wa kawaida wilayani kisarawe.
Baada ya kusalimiana na Afande Mkanye palepale alienda kwenye mada ya kitu kilichomfanya kuingia ofisini hapo kwa mkuu wake.
“Chief nipo hapa kuulizia kama kuna mwanamke anaefahamika kwa jina la Najma Waziri kushikiliwa hapa kituoni ,ni mfanyakazi wa Wizara ya elimu”Aliongea na kumfanya Afande Mkanye kukunja ndita na kuweka gazeti lake chini huku akizima sigari yake kwenye sahani ya udongo.
“Afande Jamali kwanini unaniuliza swala hilo mimi , ulipaswa kujua wewe kabla ya mimi kuju”Aliongea.
“Afande ni kwamba nimepokea simu ambayo inasema mwanamke huyo anazuiliwa hapa kituoni kwetu lakini mara baada ya kuulizia taarifa zake inaonekana hakuna jina lake kati ya wanawake waliokamatwa , nimekuja kuuliza kama swala hili ni la kimya kimya,Chief nadhani unajua mabadiliko ambayo yamefanyika ndani ya jeshi la polisi na msisitizo ni kufanya mambo kwa uwazi na kutoa ushirikiano kwa watu wote wanaongiziwa ili kuepusha lawama”
Uso wa Afande Mkanye ulijikunja , swala la Najma yeye ndio alikuwa nyuma yake lakini mtu ambaye amempa kazi ya kumkamata Najma alikuwa akibweka sana, ijapokuwa alijua Najma alikuwa ni mfanyakazi wa wizara lakini nafasi yake haikuwa tishio sana kumletea shida , isitoshe watu ambao wamempatia kazi hio walikuwa wakubwa zaidi ya wizara yenyewe.
“Jamali hio taarifa umetoa wapi au ndio umepokea simu kutoka kwa watu wasiofahamika na upo hapa kuniuliza maswali ya kijinga , nadhani unajua kwamba miaka yangu ya kuhudumu katika jeshi la polisi inaheshabika napanga hii nafasi yangu wewe kuichukua , hivyo hupaswi kuuliza maswali mengi , kama kuna mtu amekuliza wewe mpotezee”Aliongea akimwashiria kuondoka ofisini kwake lakini Afande Jamali alionekana kusita.
Afande Mkanye mara baada ya kuona Afande Jamali yupo kimya na anaonekana kukosa ujasiri wa kuongea aliona kabisa huyo mwamba atakuwa anamuogopa na alitoa tabasamu la ushindi.
Lakini alikuwa amedhania vibaya kwani upande wa Afande Jamal alikuwa akijishauri kama aweke wazi utambulisho wake mwingine tofauti na kuwa polisi au akae kimya.
Baada ya kufikiria kwa muda mfupi aliingizia mkono kwenye kombati yake na kutoa kitambulisho na kumpatia Afande Mkanye.
“Chief , lazima nipate majibu kwa maswali yangu muda huu , hivyo niambie ukweli wote”Aliongea huku akiwa anatabasamu na Afande Mkanye alitoka katika kuegamia Sofa kibosi na kisha aliinama na kuchukua kitambulisho ambacho kilikuwa kama
Passport ya kusafiria na kufungua ndani na palepale alijikuta akitoa macho na kukaa vizuri huku mikono yake kuanza kutetemeka .
“Tanzania intelligence and security Service(TISS)!!!”
Licha ya kwamba hana elimu kubwa haikumaanisha kushindwa kujua kitambulisho cha mwanausalama wa taifa.
Bwana huyo alijikuta akishangaa na kujiambia ndio maana Jamali alionekana kuwa mkimya sana nyakati nyingi lakini aliweza kupata cheo kikubwa ndani ya muda mfupi tena akipita polisi waliokuwa wakifanya kazi ndani ya kituo hicho kwa muda mrefu hata yeye mwenyewe ambaye siku zote alikuwa akisotea cheo cha Senior inspector wakati Jamali alikuja moja kwa moja na kupewa cheo cha Superintendent kumbe ni kwasababu alikuwa mwanausalama aliepandikizwa ndani ya jeshi la polisi na serikali , kengele ya kukosa mafano na kiinua mgongo iligonga kwenye masikio yake.
“Chiefu vipi vielelezo vyangu vipo sawa?”
“Ndio.. ndio , siwezi kukataa hata kama ni kipofu”Aliongea huku akijaribu kutabasamu.
“Kama ni hivyo je naweza kupata majibu juu ya Miss Najma anashikiliwa kituo gani na kwasababu zipi?”Aliuliza na kumfanya Afande Mkonyi jasho kumtoka.
Mpaka kitendo cha Jamali kuamua kujitoa kivulini kama mwanausalama na kuweka wazi uhusika wake ilimaanisha mtu aliekamatwa sio wa kawaida kama alivyofikiria.
“Jamali .. ukweli ni kwamba mwanamke huyo anaieitwa Najma amekamatwa lakini hakuletwa hapa”Aliongea kwa wasiwasi mno .
………………
Dakika chache mbele Afande Jamal aliweza kutoka huku akiwa na mwonekano wa kuchoka mno kutokana na ugumu wa swala lenyewe.
Mwanzonni alijua ni swala la kawaida tu ambalo anaweza kulifanyia maamuzi lakini mara baada ya kujua muhusika aliekuwa nyuma ya kukamatwa kwa Najma alijikuta akichoka na aliona asingeweza kukamilisha kazi yake kwa cheo chake.
Baada ya kurudi ofisini kwake na kikaa chini alimpigia Omari Tozo kwa mara nyingine kumrudishia majibu maana alipata maagizo kutoka kwake.
“Kaimu ni mimi..”
“Najua ni wewe ndio , vipi kazi imekamilik?”:
“Kazi imeshindikana kutokana na uzito wenyewe , familia ya Nguzo ya Taifa inahusika katika hili”Aliongea na kumfanya Omari upande wa pili kuguna.
*******
Roma mara baada ya kufika nyumbani kwa Nasra aliweza kuwakuta wakiwa wanamsuburi nje akiwa ameambatana na Qiang.
Roma alishatoa maagizo tokea akiwa Aiport kwa Qiang kukusanya nguo za Lanlan na kuzipeleka nyumbani kwa Nasra na ataishi huko kwa muda akendelea kumlea Lanlan.
Upande wa Nasra alikuwa ashajua kilichotokea na aliweza kusikia Edna alifika Dar jana usiku taarifa ambayo ilimshangaza na alijua tu lazima kuna ugomvi uliotokea.
Wakati akijiuliza nini kilichotokea aliweza kupigiwa simu na Blandina na kupewa maagizo ya kukaa na Lanlan kwa muda mpaka Roma kuweka sawa maswala yake na Edna na Nasra alichukua fursa hio kuuliza nini kinaendelea na hapo ndipo Blandina alipomwelezea kwa ufupi.
Nasra alishangaa kile kilichotokea na kujiuliza nini kinachoendelea , ijapokuwa hata yeye mwenyewe alihisi ni swala la muda tu kwa Roma na Sophia kuingia katika mahusiano lakini swala la Edna kuchagua maamuzi hayo kwasababu ya Sophia ilimshangaza mno, Alijiuliza ni kweli Edna anataka kuachana na Roma.
Nasra alijiuliza maswali mengine na kila kitu kinachoendelea hakiku mfanya kuwa na furaha hata kidogo na alikuwa na wasiwasi sana juu ya Edna.
Baada ya Lanaln kuingia ndani ya geti akiwa ameshikiliwa mkono na Roma alijikuta akipatwa na hisia mchanganyiko mara baada ya kumwangalia Roma usoni.
Alimwangalia Roma kuona kama ana tatizo maana alikuwa akijua alikuwa akimpenda sana Edna hivyo yaliotokea yangempa mawazo lakini hakuona utofauti mkubwa sana.
“Aunt Nasra , Lanlan ana njaa “Aliongea Lanlan mara baada ya kupakatwa na Nasra.
“Lanlan hujapata chakula cha mchana bado?”Aliuliza Nasra akimwangalia Lanlan , ukweli hata yeye alikuwa na hisia tofauti mara baada ya kugundua Lanlan alikuwa ni mtoto wa damu kwa Roma.
“Bado hujashiba tu wewe kibonge licha ya kula sambusa zote zile kwenye ndege , kama utakula tena sasa hivi utazidi kuwa bonge , haya nenda kalale kwanza ukiamka ndio utakula”Aliongea Roma na kisha akamsalimia Qiang Xi.
“Qian naomba ukae hapa kwa Nasra kwa muda na
Lanlan mpaka nitakapoweka mambo sawa ”Aliongea Roma na Qiang bado alionekana kuwa na wasiwasi.
“Mr Roma je haya yote ni kutokana na makosa yangu , nadhani kama ningesema mapema mambo yasingekuwa hivi”
“Usifikirie sana , haya ni maswala yangu na Edna wewe hayakuhusu , hakikisha tu unamlea Lanlan vizuri maana wewe ndio unamjua na utamwambia Nasra mahitaji ya Lanlan.”Aliongea Roma na kisha akamgekukia Nasra.
“Nasra huyu mwanamke mwenzio hapa kasema anataka kukaa kwako maana unajua kupika hivyo nitamuacha hapa”Aliongea Roma na kisha akatoa kadi ya benki na kumpatia Nasra.
“Kwenye akaunti ya hii kadi kuna zaidi ya bilioni za kitanzania wewe chukua kiasi kinachotosha kwa ajili ya matumzi ya Lanlan, lakini usimsikilize kila anachotaka , mahitaji yake nadhani yatakuwa ni ada ya kule shuleni kwao , chakula kitamu na vinywaji , hata kama mimi ni tajiri sitaki kumharibu mtoto wangu hivyo naomba usimdekeze sana”Aliongea.
“Najua chakufanya wala usajli , ijapokuwa mimi sio tajiri kama Edna lakini nitakuwa na uwezo wa kumlea Lanlan”Aliongea huku akimrudishia Roma ile kadi na kumfanya Roma kutabasamu.
“Sijasema kwamba huna hela , ni kwamba tu sijatimiza wajibu wangu kama baba tokea alipozaliwa , hivyo nataka nifanye vitu kwa hela yangu nadhani nitajisikia vizuri , naomba tusipingane kwa vitu vidogo kama hivi”Aliongea Roma.
Nasra aliweza kujua hisia za Roma kupitia maneno yake na kimya kimya aliichukua ile kadi, ijapokuwa ni kadi yenye hela nyingi lakini kama Roma alivyosema hela sio swala la kubwa sana na alishazoea hilo tokea aanze kuwa nae kwenye mahusiano.
“Kuna swala napaswa kulishuhuglia hivyo nitaondoka na ninaweza kurudi usiku “Aliongea Roma
Alikuwa hajapata taarifa zozote kutoka kwa Omari juu ya kazi aliompatia hivyo alikuwa na wasiwasi na jambo baya kumtokea Najma na hakutaka kumwambia Nasra juu ya hilo kwani aliogopa kumfanya kuwa mwenye wasiwasi kutokana na urafiki wao hivyo aliondoka mara baada ya kuona amemkabidhi Lanlan kwenye mikono salama
OFA YA CHRISTMASS IPO NICHEKI WATSAPP 0687151346
Sent from my 23021RAAEG using JamiiForums mobile app