Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

SEHEMU YA 564.

Roma mara baada ya kuona namna ambavyo Sauroni anaongea aliona aongozane nae akaangalie nini kinaendelea.

“Inaonekana kuna jambo baya limetokea , kwasababu umekataa kuniambia hapa tuondoke nikajionee mwenyewe”Aliongea Roma na kisha akawageukia Rose na Magdalena.

“Nyie wawili mbaki hapa , haina haja ya kukutana nao kwa sasa’Aliongea Roma na hawakujali sana hata hivyo isitoshe ndani ya hoteli hio kulikuwepo na sehemu nyingi za kutembelea.

Baada ya kumfuata Ron nyuma nyuma , hatimae waliweza kuingia eneo la mapokezi katika floor ya vyumba vya VIP.

Karibia watu wote waliochini yake walikuwa washajikusanya ndani ya eneo hilo wakiwa wamesimama kwa kupanga mstari wakiwa katika mavazi ya kawaida ya suti kasoro tu Sauron alikuwa amevalia gwanda.

Jopo lote liliinamisha vichwa chini kwa ishara ya kutoa heshima lakini Roma hakujali sana.

Kwa muonekano wa Roma kwa nje na jopo hilo la watu wenye miili iliojengeka kimazoezi , hakika ilikuwa ikishangaza kwa namna yake , ni kama sasa amefika katika utawala wake rasmi.

Roma alizungusha kichwa chake na alipoangalia kwa umakini mbele yake alisimama kwa kuonyesha ishara ya mshangao.

“Clark!”Aliita.

Alikuwa ni mwanamke mrembo aliepiga magoti huku akiwa amefungwa na pingu kwenye mikono yake , akiwa amevalia koti la kitabibu kama daktari.

Lakini Clark huyo alikuwa akimwangalia Roma kwa macho yasio ya kawaida , akionyesha kabisa ishara ya dharau.

Roma palepale akili yake ilicheza na kuona kuna kitu ambacho sio cha kawaida na alimwangalia mwanamke yule kwa umakini mkubwa sana na akatingisha kichwa kupinga kauli yake.

“Hapana wewe sio Clark , licha ya kwamba unafanana nae, macho yako , muonekano wako vinakutofautisha kwa kiasi kikubwa na yeye”Aliongea Roma.

Wengine wote mara baada ya kusikia maneno ya Roma walijikuta wakivuta pumzi na kuzishusha lakini kumkubali mara moja Master wao kwa kumua Clark huyo ni feki kwa kuangalia tu.

“What is going on, Who is this?”Aliuliza Roma huku sauti yake ikianza kubadilika , mpaka hapo alianza kuhisi maana ya kauli ya Ron dakika chache zilizopita.

Roma alijikuta akianza kuwaangalia kwa macho makali kila mtu aliekuwa ndani ya eneo hilo na watu wote walijikuta katika hali ya kunywea na kuwa wadogo kabisa.

Sauron aliekuwa upande wake wa kulia akiwa na gwanda zake za kijeshi alisogea mbele na kisha akapiga magoti mbele ya Roma.

“Your Majesty Pluto it’s my dereliction of duty, Princess Clark was kidnapped”

“Mfalme Pluto ni kutoweza kutimiza wajibu wangu , Princess Clark alitekwa nyara”Aliongea Sauron na palepale kauli yake ilipiga kama shoti katika mwili wa Roma na dakika hio hio alikuwa tayari ashamsogelea Sauron na kumshika na mkono mmoja kwenye Collar na kumuasha huku akimkaba kwa hasira.

“Will you come again?”Aliuongea akimaanisha arudie tena.

Makedon na wengine walikuwa na wasiwasi na walitaka kumshawishi apunguze hasira lakini Ron aliwapa ishara wasiongee chochote.

“Yes… Princess Clark , she was kidnapped”Aliongea Sauron.

“Ujinga Clark kama alikuwa Uingereza imewezakanaje akatekwa , unafanya nini nimekupatia mamlaka makubwa ya kamandi , hao wanajeshi wako siku hizi wamegeuka kuwa mapambo?”Aliongea kwa sauti nzito kabisa na kufanya chumba chote kuwa na ubaridi wa aina yake wa woga na wasiwasi wa kile ambacho kinakwenda kutokea.

Hakuna ambaye alikuwa akishangaa kwa Roma kuwa na hasira za namna hio kwasababu walikuwa wakimfahamu Clark na mama yake ni watu wa kipekee katika maisha ya Roma.

Roma wakati akiwa na miaka kumi na nne tayari ashamfahamu Clark , na katika miaka yote hio tokea wafahamiane alikuwa karibu sana na msichana huyo katika makuzi yake yote , mpaka kuja kuwa mtu mkubwa, ukiachana na yote Clark alikuwa kwa ndoto moja tu ya kuwa daktari ili kumsaidia Roma na ugonjwa wake.

Clark alikuwa ni mwanamke ambaye maisha yake yote aliishi kwa kujitengeneza kuwa na thamani ya kuhitajika na Roma na ndio maana pale tu Roma aliposema anashida mwanamke huyo angetimiza bila ya kujitaji malipo ya aina yoyote.

Kama Clark alikuwa akifanya kulipa fadhila basi angekuwa ashakamilisha fadhila hizo miaka mingi iliopita kwani amefanya mengi, ni yeye pekee ambaye alimsaidia Roma kuweza kudhibiti hali yake ya ukichaa.

Sasa watu wote waliokuwa hapo , akiwemo Edward, Ron na wengine walikuwa wakifahamu nini maana ya Clark katika maisha ya Roma.

Usalama wa Catherine mpaka leo hii upo chini ya Roma na hata baada ya yeye kuamua kurudi nchini Tanzania madaraka aliotoa kwa Sauron wajibu wake pia ni kuhakikisha usalama wa Malkia Catherine na Clark unaimarishwa.

“Ni kushindwa kutimiza wajibu wangu , watu waliomteka Princess Clark walitumia akili ya kumuweka mwingine feki ili isigundulike kama ametekwa , wakati nikiwa nataka kumleta kwenye Caesar Conference niliweza kugundua utofauti wa Clark na hapo hapo nikajua aliekuwepo ni feki, kwasababu Clark licha ya kuwa bize lakini hajawahi kusahau miadi yake na wengine”

Roma alimtupa Sauroni chini , kwa hali kama hio hata kama alikuwa ni komredi mwenzake katika jeshi asingeweza kumtendea vizuri kwa kosa ambalo amefanya.

“Kwahio huyu mwanamke ni feki umesema?”

“Ndio “Aliitikia huku akinyanyuka na kusimama kikakamavu mbele ya Roma na kisha akaendelea kuongea.

“Mfalme Pluto nimekuja kwa kuchelewa kwasababu nilikuwa sijui namna ya kulifikisha hili kwako na lingine ni kutoa maagizo kwa watu wangu kufanya utafiti wa kujua mwanamke huyu ni nani haraka iwezekanavyo, na tuliweza kugundua aliwahi kuwa shushu kutoka Urusi chini ya kundi la kigaidi lifahamikalo kwa jina la Black Widow l akini aliasi , sura yake imeweza kubadilishwa kwa kutumia mjumuisho wa Nanotechnology na 3D printing technology, teknolojia ambayo bado haijawa hadharani , ni teknolojia ya viwango vya juu sana”Aliongea Sauroni akimaanisha mtu huyo alikuwa akifanana na Clark kutokana na sura yake kutengenezwa kwa kutumia teknolojia ya Nano na ya uchapishaji ya 3D(Three dimension).

“Kwahio unamaanisha bado hamjapata Clark?”Aliuliza na Sauron alitingisha kichwa kukubali .

“Mfalme Pluto , nimetuma majasusi wote wa Mossad waliochini yangu kutafuta kila kona ya dunia , kama kutakuwa na taarifa yoyote itaripotiwa kwetu kwa haraka sana”Aliongea Makedon na Roma alimpotezea na kumgeukia Edward.

“Catherine anajua kuhusu hili?”

“Shangazi yangu hajui chochote mpaka sasa , yupo bize na maandalizi ya Summer Bank holiday kwa zaidi ya wiki tatu sasa nchini Scotland na hajakutana kabisa na binamu yangu na hatujapanga kumwambia bado”Aliongea.

Katika maelezo yao ilionyesha kwamba ni zaidi ya wiki mbili tokea Clark kutekwa na haikuwezekana kugundulika kutokana na kwamba kulikuwepo na feki yake.

“Kama ni hivyo agiza vijana kuongezea ulinzi wake kwa siri ili isije ikawa analengwa na yeye pia kama ilivyomtokea kwa binti yake”Aliongea Roma na baada ya hapo alimgeukia yule mwanamke na kisha alinyoosha mkono wake bila ya kumshika na nguvu kubwa ya kijini ilitoka kwenye mikono yake na kumwinua yule mwanamke huku akiwa kama vile amekabwa shingonii bila ya kushikwa.

Huyo Clark Feki alikuwa na sura ya dharau licha ya kwamba alikuwa akiona kifo chake na hakutaka kuongea neno lolote ni kama alikuwa ashajiandaa kufa kwa muda mrefu.

“Najua kwamba wewe ni Ajenti ambaye una mafunzo ya hali ya juu na najua sana mbinu zenu za kujiua lakini pia hutoongea chochote licha ya kukutesa lakini hata hivyo sina mudi ya kupoteza muda kukutesa hivyo kama hutaki kutoa ushirikiano kwa hiari yako nitakupasua kichwa chako”Aliongea Roma na yule mwanamke alitoa tabasamu la kejeli.

“Hades wewe ni shetani , Umechokoza watu na kuamsha ghadhabu ya Mungu na muda wowote yatakufikia mabaya , kwasababu nilikuja kushiriki katika hii opereshini sijawahi kuwaza kurudi nikiwa hai , niue na nitakuwa kuzimu nikisubiria kila mmoja anaekuzunguka kuungana na mimi”Aliongea kwa kejeli kwa lugha ya kingereza.

“Naona umekiomba kifo chako mwenyewe na sina budi kukupatia”Aliongea Roma na palepale hakusita tena kwani alisukuma nguvu yote ya kijini kutoka katika mkono wake na ni sauti ya mivunjiko ya mifupa tu ilioweza kusikika na palepale kichwa chake kilipasuka kama tikiti na ubongo wote ukamwagika huku damu nyingi zikimwagika na kuchafua kapeti.

Kwa jinsi mwanamke huyo alivyopelekwa kuzimu ilikuwa ni kikatili mno kiasi kwamba watu wote hapo ndani walikunja sura na kujiambia ukatili huo ni kama vile Roma amerudi katika enzi zake akiwa kama shetani mwenye kiu ya damu.

Kipindi hicho ambacho hakujali kufanya ukatili huo mbele ya Seventeen na Clark.

Kila mmoja alikuwa na wasiwasi mno na hakuna ambaye alithubutu kuongea neno lolote la kutoa michango yao namna ya kumpata Clark.

Wakati kila mmoja akisubiria kwa hofu nini kinakwenda kutokea , palepale Roma aliirusha ile maiti ya mwanamke katika miguu ya Makedon.

“Nenda na chukua Fingerprint zake na DNA uthibitishe ni wakati gani ambao aliingia ndani ya maabara ya Clark , inaonyesha Clark alitekwa kwa muda mrefu na hamkuweza kujua kwasababu ya uwepo wa sura yake feki , pengine wanajaribu kuvuta muda wakitaka kupata tafiti zote za Clark alizogundua , nina uhakika mpaka sasa yupo hai , kwa hao watu naamini wanachokita kutoka kwa Clark ni kwa ajili ya kutengeneza siraha za maangamizi , hivyo basi kwa umakini mkubwa anzeni kutafuta katika maeneo yote ambayo yana viwanda vya kudhalisha siraha za kipekee”

Baada ya kusikia maelezo ya Roma wote waliunga mkono , ilikuwa ni kweli kama walimteka kwa ajili ya kutaka kitu chochote kutoka kwao wasingeweka mtu feki kama mbadala , lakini licha ya hivyo ilionekana walichagua muda mbaya kwani kipindi hicho ni cha Caesar Conference na Clark alikuwa ni moja wapo ya watu waliokuwa wakihudhuria kila tukio hilo linapofanyika”

Ron na wenzake waliogopa kwamba kama taarifa hio ingemfikia Roma basi asingeweza kudhibiti ukichaa wake uliokuwa ukimwendesha miaka na miaka na kuishia kuwaua , lakini ilionekana mfalme wao ameimarika tokea ajipe likizo ya kwenda Tanzania..

Makedoni aliahidi na kisha akawapa maelekezo vijana wake kusafisha na baada ya hapo aliondoka katika eneo hilo akiwa na watu wake kwa ajili ya kuanza kazi ya kumtafuta Clark , alijua kabisa kama chochote kikimtokea Clark basi halitakuwa jambo jepesi .

“We the Rothchild family are involved in the international undergound trading of all rare metals and elements , I will chek it ou and hope it helps”Aliongea Edward akitoa pendekezo kwamba familia yao ya Rothchild inahusika na biashara zote zinazohusu madini adimu na kuahidi kwamba atajaribu kuulizia huko ili kuona kama inaweza kusaidia.

“Ni bora uanzie kwa wanafunzi wa Clark wote wakubwa na kuona Projekti zao za hivi karibuni”

“Understood”

Roma mara baada ya hapo alimwangalia Sauron kwa muda huku akionekana kuwaza, Sauron uso wake ulikuwa mwekundu mno kwa wasiwasi akiwa amesimama katika eneo moja pasipo ya kusogea hata hatua moja.

“Sauron unapaswa kujiandaa , kama Clark asipoweza kurudi akiwa salama hakikisha haitokei wewe ndio wa kulaumiwa , siwezi kukuua lakini huu uwezo wako mdogo utakuandama kwa maisha yako yote mpaka unaingia kaburini”

“Mfalme Pluto wewe ndio ulifanya familia yangu mpaka sasa ipo hai , ni mwenye soni juu ya ahadi yangu kwa kufeli kumlinda Princess Clark , nipo tayari kwa hiari yangu kuwajibika , tafadhari nipe nafasi nyingine ya kurekebisha makosa yangu , nitamtafuta Profesa Clark alipo ndani ya muda mfupi sana”

“You better not Disappoint me again”Aliongea Roma akimaanisha kwamba ni kheri kama hatamwangusha tena na Sauron alipiga saluti ya kikakamavu akiahidi atafanya kila namna ya Clark kupatikana.

Baada ya pale wanajeshi wote wa kikosi cha The Eagles na viongozi wa juu wa New Zero walipiga saluti na kisha wakaondoka wakiongozwa na Sauron.

Baaada ya watu kuondoka aliekuwa amebakia ni Ron na alimsogelea Roma akionekana na maoni yake binafsi.

“Mfalme Pluto kama adui aliefanya hivyo akawa na uwezo mkubwa wa kimapigano Sauron anaweza asiweze kufanikiwa kumshinda”

‘Unafikiri sijaliona hilo?”Aliongea Roma katika hali ya urafiki.

“Hapana ,, najua mfalme Pluto hukutaka kumlaumu kila kitu Sauron ndio maana ukaamua kumuacha bila kumuadhibu”

“Najaribu tu kuwaaamsha watimize majukumu yao ipasavyo , yule mwanamke alichoongea ni sahihi nimeua watu wengi sana hivyo nimejitengenezea maadui dunia nzima wanaotaka kuinywa damu yangu ikiwa ya moto , ndugu zao , marafiki zao na hata wapenzi wao niliwaua , na sasa wanatafuta nafasi ya kutaka kulipiza kiasasi, hata kama nilishastaafu na kuacha mambo hayo kwa zaidi ya miaka mitatu , lakini hawa watu wana madoa makubwa ya damu na chuki katika mioyo yao, kuna msemo maarufu kutoka Asia usemao ‘Iwe ni kwa kuwahi au kwa kuchelewa hakuna muda sahihi wa mwanaume kulipiza kisasi’, hivyo hata kama hawatakamilisha ndani ya mwaka mmoja au miwili kwao hata ichukue miaka kumi haitakuwa tatizo mpaka siku wapate nafasi”

“Nafikiri awamu hii huyu adui anajaribu kutumia muda kwa faida kutokana na nguvu ya chuki za watu ambazo zinaelekezewa kwako ili kujificha , hatujawahi kutegemea kama ataenda moja kwa moja mpaka London na kuteka mtu nyara”

“Kuna uwezekano wa mambo ambayo hatujawahi kutegemea yakatokea hapo mbeleni.Halafu wale watu wa mavazi meupe kuna taarifa zozote mlipopata zinazowahusu?”

“Oh, Fidero tayari ashapata baadhi ya taarifa na nilikuwa nikihatiaji kukuambia”Aliongea na kisha alimpa karatasi iliokunjwa .

Roma alisoma karatasi ile kwa haraka haraka na palepale uso wake ulijikunja huku akitabasamu kifedhuli.

“Mbinu yao kujificha..”Aliongea.

Sababu ya kuongea hivyo ni kwamba , ukiachana na neno Deicide au godkiller washiriki wote wa kundi hilo hawakuandikwa kwa majina yao halisi bali ni namba tu zilizotumika kuwatambulisha kama washiriki.

Hata hivyo ulikuwa ni utaratibu wa wasimamizi wote wa Caesar conference washiriki wote kutoka makundi tofauti hawakutambulika kwa majina yao halisi.

“Wamekuja wakiwa wamejiandaa sana”Aliongea Roma huku akitoa kicheko hafifu.

“Mfalme Pluto je kuna ulazima wa kutuma mtu kuwafatilia ili kujua kila wanachokifanya? Nina wasiwasi kwamba inawezekana ndio waliohusika na kumteka Princess Clark”

“Achana na hilo , ukituma watu watakachoambulia ni majeraha tu , mimi mwenyewe nimeshindwa kugundua wanatokea wapi inamaanisha wamejiandaa kwa kila kitu , ngoja nisubiri Christen na wenzake wakiwa hapa nione ni kipi wanafahamu na maamuzi watakayo chukua”

Roma hakuona haja ya kumtafuta Clark yeye mwenyewe , na isitoshe Clark hakuwa na mafunzo yoyote ya nguvu za mbingu na ardhi huenda ingekuwa rahisi kumtafuta kwa kutumia Aura yake hivyo aliona njjia pekee ni kutulia na kusubiria taarifa kutoka kwa Makedo na Sauron.

Lakini pia hakutaka taarifa hio kumfanya kukosa raha na kuwaathiri Magdalena na Rose ambao ameambatana nao kuja hapo kufurahi.

Roma mara baada ya kurudi katika chumba alichowaacha Rose na Magdalena aliambiwa kwamba wanawake hao wametoka na kwenda Casino , taarifa hio ilimshangaza kwa kutotarajia Rose kuweza kupata sehemu ya kupoteza muda .

Kasino iliokuwepo ndani ya hoteli ya Casaano licha ya kwamba asilimia kubwa ya watu wanaocheza kamari wlaikuwa ni mabandidu wa makundi ya kimafia , lakini walitii sheria zote za kamari na hakukuwa na utapeli.

Cassino yao ilikuwa na kila aina ya michezo ya Kamari kutoka katika kila tamaduni dunia nzima na sio hivyo tu hali ya hewa ilikuwa nzuri zaidi kutokana na kwamba kulikuwa na wanawake warembo waliokuwa wakitoa huduma na kufanya wacheza kamari wasiathirike kimawazo , ni eneo ambalo lilikuwa likifanya kazi usiku na mchana bila mapumziko, wengine kucheza kamari wanachukulia kama kazi yao ya kujiingizia kipato.

Roma akiwa ameambatana na Ron waliweza kumpata Rose na Magdalena katika meza ya gemu ya karata maarufu kama Blackjack na walionekana kuweka umakini wao katika gemu..

Ni Magdalena pekee ambaye hakuwa akicheza zaidi ya kumwangalia Rose kwa wasiwasi kwani tokea aanze kucheza alikuwa amepoteza Chips(hela katika mfumo wa vipande) za kutosha mpaka zote zimeisha na bado tu hakuwa ni mwenye kukata tamaa.

Roma alijaribu kumshawihi Rose aache maana hatoshinda kwa wazungu hao wataalamu , lakini aliweka ngumu na kusema mpaka arudishe hela zake zote alizopoteza na Roma hakutaka kumlazimisha ilimradi alikuwa akichezea hela zake.

Ilibidi amchukue Magdalena aliekuwa na wasiwasi akimwambiwa wakatembee tembee nje maana Kasino haikuwa mahali pake.

Magdalena alipata ahueni mara baada ya kuambiwa waondoke hapo ndani maana alijihisi kukosa uvumilivu.

******

UNKOWN SECRET BASE.

Ni katika mojawapo ya kambi ya siri sna ambayo haijulikani ipo eneo gani katika dunia.

Ndani ya chumba kikubwa kulikuwa kumefungwa taa za mwanga mweupe ambazo ziliangaza chumba kizima na kufanya kila kitu kilichopo ndani yake kuonekana, ni chumba ambacho kilionekana kabisa kimejengwa kwa chuma kigumu , mathalani kama mahali pakufungia mateka.

Muda huo huo mlango wa chumba hicho ulifunguliwa kwa kuteleza kwenda kulia na alionekana mwanaume wa kizungu mwenye nywele za kahawia zilizojikunja kunja ambaye amevalia koti la maabara.

Ni mwanaume ambaye alikuwa na mwonekano mwembaba lakini macho yake yalikuwa ni yale yasiokuwa na utani huku akiwa ameyafinika kwa miwani ya macho.

Katika chumba hicho kulikuwa na meza pamoja na kiti pekee na katika kiti alionekana mwanamke ambaye alikuwa amevaaa koti pia la kimaabara akiwa amekalishwa huku akiwa ameinamisha kichwa chake na kufanya nywele zake ndefu zilizochanguka kumfunika na asionekane sura.

“Professor , I came to see you again”Aliongea yule mwanaume na kumfanya yule mwanamke kuamsha kichwa chake taratibu na kufanya angalau sura yake ionekane.

Alikuwa ni Profesa Clark ambaye sura yake ilionekana kupauka sana , huenda ni kutokana na hofu pamoja na kukosa kula na kiua ya maji.

“Jerry tafadhari naomba uache”Aliongea Clark huku akimwangalia yule mwanaume kwa macho ya kukata tamaa. Lakini kauli yake licha ya kwamba haikuwa ikichekesha lakini mwanaume alieitwa kwa kjina la jerry alianza kucheka mfululizo.

“Profesa ni kipi ambacho unaota mpaka sasa , yaani niache , tangu nilipokutembelea mara ya mwisho nilikuwa nikiisubiria sana hii siku halafu unaniambia vipi niache , hivi unajua kwamba sina mpango wowote wa kuacha eti”

“Jerry wewe ndio mwnafuzni wangu pekee ambaye ulionyesha uwezo mkubwa licha ya kwamba nilikuwa na hofu na uelekeo wa tafiti zako lakini bado nikakuamini na kuendelea kukufundisha mambo mengi lakini sikuwahi kuwaza unaweza kunifanyia hivi , umenihuzunisha sana”Aliongea na kumfanya kidogo Jerrey kupatwa na hatia lakini alipotezea.

“Teacher I will ask you again , what is the last sythethic element of FURY?”Aliuliza Jerry akimuuliza Clark ni element ipi ya mwisho ya utengenezai wa FURY, alionekana alikuwa na kanuni ambayo haijakamilika na ni Clark pekee ambaye alikuwa akiifahamu ndio maana alikuwa akimuuliza.















SEHEMU YA 567

Clark mara baada ya kuulizwa hilo swali alivuta pumzi nyingi na kuzishusha , mtu huyu anaefahamika kama mwanafunzi wake alikuwa ameuliza mara kibao swali la aina moja lakini hakuwa amempatia majibu anayoyataka.

“Kwanini unatamaa sana na kanuni hio, nilifikiri kama utakuja kujua nini maana ya FURY utaacha kuuliza kabisa”

“Kwanini niache , nilikufuata kwa miaka miwili yote na hatimae nimepata ninachokitaka kwanini niache”

“Jerry acha kuruhusu chuki zako kukufanya kipofu , unajua kabisa kama FURY itatengenezwa nini kitatokea , baada ya kutengeneza muundo kamili wa kimfumo miaka mitatu iliopita sikuwa na mpango wa kuendeleza zaidi , itakuwa ni dhambi kwa kizazi chote cha binadamu, ni kitu ambacho sisi wanasayansi hatupaswi kutengeneza na kama kuna mtu yoyote atajaribu kutengeneza basi ni matusi kwa binadamu wote”

“Lakini bado huu muundo kamili uliojaribu kutengeneza si bado unao , Profesa wewe ni Idol wangu , hapo zamani za kale wakati nilipokuwa chini yako nilijitahidi kusoma na kuelewa kila unachofundisha na nilichimba nikachimba haswa na kila ulichonielekeza na nikajua maana yake niliendelea kukuheshimu , kitu pekee ambacho kilikufanya kunipenda kama mwanafunzi ni kwasababu tuna tabia zinazofanana , wote sisi ni wagumu sana kupotezea gunduzi zetu licha ya uhatari wake , ijapokuwa unasema hutaki kuunda FURY lakini bado taafiti yake hujaiharibu na kuificha , hakuna uchizi kama huo sisi wote tunafanana”

“Inaonekana kila nitakachoongea hakitakufanya uache, kama ni hivyo unaweza kuondoka kwani hata kama nikifa hapa siwezi kukuambia kanuni yake”

“Profesa unadhani nitashindwa kuijua hio karuni hata kama hutoniambia , kuna mamilioni ya Elementi katika dunia hii ambazo zinaweza kukamilisha kanuni ya uwiano wa kikemikali, ninao uwezo wa kujaribu moja moja mpaka nifanikiwe, hivyo acha ubishi jaribu kutoa ushirikiano kwetu , nina uhakika kwa talanta yako wakuu wangu hawatokuacha bure, kwanini unajisumbua kufanya kazi kwa ajili ya yule shetani si kheri sisi”Aliongea na kumfanya Clark kucheka sana.

“Unacheka nini?”

“Shetani uliemtaja ni kweli kwamba ameua watu wengi na naelewa wapo watu wengi ambao wanataka kulipiza kisasi lakini nini unafanya sasa hivi , hebu fikiria je kama utafanikiwa kutengeneza FURY unadhani utaweza kumuua , hivi unajua uwezo wake ukoje kwanza?”

“Hilo sio juu yako , hata kama sitoweza kumuua nitawaua watu wake wa karibu wanaomzunguka ili nimwonyeshe nini maana ya sherehe ya kifo na uhai”

“Kwa kufanya hivyo utakuwa mkatili zaidi kuliko shetani mwenyewe, Roma yeye kaua watu wengi lakini mpango wako wewe ni kuua binadamu wote”Aliongea na kumfanya Jerry kutabasamu kwa kebehi.

“Profesa huna haja ya kuwazia usalama wa dunia , kama nitaingudua hii elementi ya mwisho kubalansi matokeo ya kikemia . utakuwa ndio mwanzo wa sisi kutengeneza New word order”

“Wewe ni mpumbavu Jerry , hivi unadhani mpaka mimi kuwa mwalimu wako naweza kulingana na wewe? , kama FURY elementi yake inaweza kupatikana kirahisi basi mimi sio Clark”Aliongea na kumfanya Jerry kushituka na kukunja sura.

“Kama usemavyo ni sahihi je hii elementi ni ya kutengeneza?”

“Upo sahihi katika dunia nzima hakuna ambaye anafahamu elementi hio zaidi yangu na haitokuja siku ukaweza kufahamu”Aliongea na kumfanya Jerry kuwa katika hali ya kujidharau , amefanya kazi kwa muda mrefu kuweza kgundua elementi hio lakini kazi yake inaonekana haikuleta mafanikio.

“Profesa kweli kuna gepu kubwa kati yako na mimi sikuwaza kwamba utakuwa na uwezo wa kufiria nje ya binadamu wa kawaida lakini haijalishi kama hutatotoa ushirikiano na kutuambia basi elewa lile kundi la watoto katika kanisa la Santa Maria hawatoliona jua la kesho”Aliongea na kumfanya Clark kumwangalia kwa macho makali.

“Wewe ni kichaa? Wale ni watoto tu wanakosa gani kwanini unataka..”

“Ninaweza kuwafanya chochote ndio , kwanza kama huwezi kuwatibia Saratani kwanini nisiwakutanishe na Mungu mapema, nakupa nafasi ya mwisho toa ushirikiano wako”Aliongea na kumfanya Ckark kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha akainua kichwa chake.

“Okey , nitaongozana na wewe ili kukuonyesha inavyofanyika ..”Aliongea na kumfanya Jerry kutoa kicheko cha juu sana kwa furaha zote .

‘”Hahaha.. profesa ijapokuwa una akili kuliko mimi lakini bado wewe ni mtoto , angalia sasa umekubali, FURY , oh FURY wangu wewe. Haha”

Kicheko cha mwanaume wa kizungu kilisikika akicheka kama vile ni chizi.

******

Wakati Roma akiwa na Magdalena katika mgahawa pamheni ya hoteli wakimalizia kula chakula cha baharini , palepale alijiambia ni zaidi ya lisaa limepita tokea aachane na Sauroni na wengine lakini mpaka muda huo hakuna majibu , hivyo aliona atoe simu yake kujaribbu kumpigia Ron ili kujua nini kinaendelea.

Kabla hata hajaanza kupiga aliweza kuona kundi la watu likiwasogelea na aliekuwa akiongoza ni Sauron na walionekana na sura zilizokuwa na mwonekano wa wasiwasi pamoja na kuwa na msisimko.

“Mfalme Pluto , tumeweza kugundua kitu”Aliongea Sauron mara baada ya kungia ndani ya magahawa huo.

Ijapokuwa walikuwa wengi na ndani ya eneo hilo kulikuwa na watu , lakii kama ilivyokuwa kwa jiji hilo watu hawakushangaa sana wala kuhofia kwani Sauron alikuwa kwenye mavazi ya kijeshi.

“Umempata Clark?”

“Hakuna uelekeo maalumu wa sehemu aliopo lakini majasusi wa Mossad hivi karibuni wameweza kukusanya baadhi ya taarifa ambazo zina viashiria , Korea Kaskazini hivi majuzi wamefanya kazi na moja wapo la kundi la kigaidi kwa siri ndani ya Ulaya ya Mashariki kupitia mkondo wa kimawasiliano wa Kusini mashariki mwa Asia , ulikuwa ni ushirikiano wa majaribio ya utafiti wa siraha ya kinyuklia ambao ulianza mwaka mmoja uliopita , kama sio uhusikaji wa ghafla wa Korea kaskazini isingekuwa rahisi kuweza kupata viashiria kwa haraka”

“Korea Kaskazini , Majaribio ya nyuklia , Ulaya ya Mashariki … unajairbu kuamini kwamba ndio waliomkamata Clark ili kumalizia utafiti huo?”

“Inawezekana kabisa , tumeweza pia kugundua North Buyeo umoja wa siri uliopo nchini Korea Kusini ndio waanzilishi(instigators) wa mpango mzima , taarifa zinaonyesha wamenunua kiasi kikubwa cha madini adimu kutoka kwa Wamarekani wanaofanya biashara kimagendo pamoja na Maabara za siri na kuyaingiza Ulaya kitu kilichopelekea ushirikiano wa ghafla , na madini hayo adimu kwa maelezo ya Ashley Senga mwanafunzi wa karibu wa Profesa Clark anasema kwamba madini hayo licha ya kugundulika uuwepo wake lakini ni wanasayansi wachache sana duniani wanaojua kazi zake na namna ya kuyatumia na Profesa Clark ni mmoja wapo ,Pointi ya msingi ni kwamba tumeweza kukadiria muda kupitia Vinasaba vya damu vya yule mwanamke shushu wakati alipongia ndani ya maabara na imeonyesha ni zaidi ya wiki tatu sasa . kati ya wanafunzi ambao wapo chini ya Clark kuna anaefahamika kwa jina la Jerry , aliomba likizo wiki tatu zilizopita na hakuonekana mpaka sasa na hajulikani alipo , hivyo tunaamini huenda mipango yao imefanikiwa kwa kupitia mtu wa ndani wa karibu na Clark ambaye ni huyu Jerry”

“Hawa Buyeo wa Kaskazini …”Roma alitaka kuongea lakini alijikuta akianza kwaza kidogo , hakutaajia kwamba watu ambao waliomsumbua ndani ya Korea kusini walikuwa na mipango mikubwa zaidi , ijapokuwa hakujua ni sababu ipi ya kuwekeza katika tafiti za maswala ya nyuklia na wapi wanalenga lakini aliamini ni mpango ambao sio mdogo kabisa.

“You have said so much , then how narrow is the scope?”Anauliza kwa kusema ameongea sana lakini je ni namna ipi ameweza kufupisha utafutaji.

“Mfalme Pluto baada ya madini hayo adimu kuingia Ulaya yalitolewa katika mfumo wa kawaida wa kiusafirishaji na kuingizwa katika mfumo wa Black Market na tumeshindwa kujua uelekeo upi ni sahihi na upi sio sahihi na naogopa kama tukiendelea kutafuta kwa staili hii hatuwezi kumuokoa Princess Clark ndani ya muda”

“Kama ni hivyo kwanini upo hapa?”Aliuliza Roma akionyesha sio mwenye furaha.

“Ijapokuwa hatuwezi kutafuta uelekeo sahihi lakini tunaweza kujaribu kutafuta katika njia zote lakini hata hivyo kulingana na uelewa wako wa ramani ya ulaya pamoja na spidi yako inaweza kurahisisha kazi”Aliongea na sasa akamfanya Roma kuelewa kile ambacho Sauron anataka kumaanisha.

Ni kweli kama ataenda yeye mwenye kufuatilia basi ingekuwa rahisi zaidi kuliko watu wake na kitu kingine yeye alikuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa mambo yasiokuwa ya kawaida kwa haraka kuliko wao.

Baada ya kufikiria Clark amefungiwa kwa muda mrefu na huenda yupo katika hali ya kukata tamaa , moyo wake ulifurukuta na palepale alisimama.

“Kama ni hivyo niambie uelekeo upi nianzie kupitia simu yangu na nitafuta kila eneo moja baada ya lingine”

“Utuwie Radhi mfalme tunaona hata aibu ya kukuomba kulifanyia kazi hili mwenyewe..”

“Haina shida , umefanya sahihi kuja kwangu”Aliongea Roma na kisha alimwangalia Magdalena.

“Magdalena nisamehe nadhani sitoweza kukutembeza katika eneo nililokuwambia , tufanye siku nyingine”

“Hakuna shida , muhimu ni kuweza kumtafuta Clark kwanza , je unataka nikusaidie chochote?”Magdalena alikuwa akijua maana aliambiwa na Roma.

“Haina haja , huwezi kuelewa kwa ukubwa wake Ramani ya Ulaya ya Mashariki , unaweza kurudi hotelini kwa sasa ,Ron ataandaa utaratibu wote namna ya kushiriki katika mashindano ya Caesar Conference”

“Okey kuwa makini lakini”Aliongea Magdalena na kumfanya Roma amwangalie kwa dakika na kisha akatabasamu na kuondoka.

Sehemu ya kwanza ambayo alipaswa kwenda kutafuta ni katika kisiwa cha Gotland kwenye bahari ya Baltic.

****

Muda huo huo wakati akiondoka katika maabara sehemu ambayo amekamatwa Clark .

Alionekana Clark ambaye alikuwa amevalia Gloves mkononi na miwani maalumu ya kulinda macho huku nywele zake ambazo zilikuwa zimechanguka dakika chache zilizopita alikuwa amezifunga kwa nyuma, akiendelea kufanya majaribio ya kisayansi.

Maabara aliokuwemo ilikuwa ni kubwa , huenda zaidi ya maabatra kubwa za kitaifa ambayo inamilikiwa na shirika binafsi ambalo halijajulikana bado , ilikuwa na kila aina ya vifaa ambavyo vina teknolijia ya halli ya juu, ulikuwa ni uwekezaji mkubwa sana uliofanyika kutokana na ubora wa maabara hio.

Clark alikuwa amesimama kwenye tarakishi kubwa ya kioo iliokuwa imewekwa kwenye meza ya kupangusa kwa mikono na alikuwa akiandika kwa spidi kubwa akijaribu kutengeneza muunganiko wa kikanuni wa kemia ambao ulikuwa mgumu kueleweka hata kwa mtu ambaye ana msingi wa kawaida sana wa somo la Kemia.

Sasa katika sehemu aliosimama upande wa mbele kulikuwa na mkono wa roboti ambao ulikuwa ukifanya kila kitu unachoelekezwa kwa kutumia kanuni zinazo andikwa katika tarakishi.

Nyuma yake kulikuwa na wanaume wenye miili iliojengeka waliokuwa wamesimama , wakiwa wamevalia makoti ya maabara wakimwangalia Clark kile anachokifanya kwa shauku kubwa na kadri alivyokuwa akichapa kwa haraka katika keybord ndio walivyozidi kutoa macho yao , kwa muda huo walionekana kama walinzi lakini kwa wakati mmoja walionekana kama wanafunzi.

Kati ya wote ambao walikuwa na macho kodo ni bwana aliefahamika kwa jina la Jerry , alikuwa akiangalia na kukariri kila aina ya taarifa iliokuwa ikionekana kwenye Skrini hio kubwa , ijapokuwa taarifa hizo zilionekana kuwa nyingi na ngumu kukariri lakini alijitahidi kwa kadri ya uwezo wake kuweza kupata msingi wake huku akipotezea baadhi ambazo hazikuwa na msingi, macho yake yalikuwa yamejaa tamaa kubwa.

“Its wonderfull.. I never thought that there would be such a way to perfom fusion reactuon .. the power fo FURY was originally constructed like this”

“Hakika inashangaza , sikuwahi kufikiria kutakuwepo na njia ya kuunganisha matokeo ya kikemia ya namna hio .. nguvu ya FURY ilitengenezwa mwanzoni kama hivi”Aliongea.

Mwonekano wa mrembo aliekuwa akiandika mlolongo wa taarifa, katika maisha yake aliwafanya wanawake wengine kumuonea wivu , hakujaliwa uzuri tu lakini pia amejaaliwa uwezo wa kuchanganua maarifa na kudhalisha maarifa mengine , ilifanya hata watu kuona wasiwasi kumsogelea na kumtongoza kwa kuona kwamba hawana hadhi ya kuwa nae.

“Profesa usingekuwa upande wa yule shetani hakika lingekuwa jambo zuri sana..”Aliongea lakini Clark alikuwa kama mtu ambaye hajamsikia kwani aliendelea na kazi yake pasipo kumzingatia na aliendelea kuchapa kwenye skrini kwa dakika kadhaa na kisha akaacha na baada ya hapo alisogea upande wa kulia mwa meza iliokuwa na baadhi ya kemikali na kuanza kuziandaa.

“Profesa unafanya nini , kwanini umeacha?”

“Itachgukua zaidi ya masaa nane mpaka kukamilisha muunganiko , kwasasa nahitaji kuthibitisha usafi wa baadhi ya elementi ambazo zinakwneda kuathiri moja kwa moja matokeo ya Elementi unayotaka”Aliongea.

Jerry alimwangalia Clark kwa macho ya shaka , ijapokuwa hata yeye amebobea katika fani ya kemia lakini alikuwa mbali sana na maarifa aliokuwa nayo Profesa wake ndio maana alikuwa katikati kwenye kuamini maneno yake au asiyaamini.

“Profesa nakushauri usije ukafanya hila ya aina yoyote , nadhani unajua nini matokeo yake”

“Haina haja ya kunikumbusha”Aliongea pasio ya kuamsha kichwa chake , wakati akiendelea na kile anachokifanya kumbukumbu za utoto wake zilimjjia akilini , alikumbuka siku ambayo alikuwa ndani ya hosteli ya kanisa katika jiji la Milan akiwa na mama yake , wakiwa kama watu wakimbizi na ghafla tu akatokea kijana mdogo alievalia nguo za kininja na kuwaokoa katika mikono ya maadui zao , mwanaume aliewaokoa siku hio ni mwanaume huyo huyo ambaye amkuwa upande wake mpaka kufikia umri huo, lakini katika hali aliokuwa nayo alikosa tumaini na kujiuliza je mwanaume huyu atakuja kumuokoa kwa wakati kama huo ambao anamhitaji sana, ili kuepusha kutoa kanuni ambayo ingekuwa na athari kubwa kwa watu wa dunia.

*******

Baada ya Roma kuondoka Ron aliweza kuja katika mgahawa na kulipia gharama za chakula Roma alichokula na Magdalena.

“Miss Magdalena , je utahitaji kuudi hotelini sasa hivi au unataka kuendelea kuzunguka zunguka , ninaweza kumuita binti yangu ili kuwa mwenyeji wako na kukutembeza tembeza”Aliongea Rona kwa lugha ya unyeyekevu.

“Asante sana Mr Ron kwa ukarimu wako , kwasasa nadhani nitarudi hotelini kuungana na mwenzangu”Aliongea Magdalena alionekana kukosa ile furaha aliokuwa nayo.

“Naelewa unajisikia vibaya mara baada ya mfalme Pluto kuondoka ghafla , ninatamani sana wewe na Miss Rose kuwa na furaha kwa Trip yenu”Aliongea.

Ni kweli Magdalena mara baada ya Roma kuondoka alihisi hisia mchanganyiko huku ile ya kukasirika ikiwa imemtawala zaidi ,katika maisha yake tokea ayafahamu mapenzi mtu wa kwanza kumpenda ni Roma, lakini mwanaume huyo licha ya kwamba anaishi nae karibu lakini kwake ni kama alikuwa umbari mrefu sana ambao anakosa kabisa namna ya kumfikia.

Siku hio alijisikia vizuri sana kutembea pembeni ya mwanaume huyo anaempenda na alijikuta akipenda kuweka hisia zake wakati wakiendelea kula chakula, ilikuwa ni mara yake ya kwanza kutembea na Roma ki upande upande , safari yao ya China ilikuwa ni kwa misheni maalumu lakini hapo ilikuwa ni kwa ajili ya matembezi na ndio maana kulikuwa na utofauti mkubwa , lakini sasa wakati akiwa ndio kwanza anaionja raha ya kukaa meza moja na mwanaume anaempenda wakifurahia chakula ghafla tu kunatokea dharula tena dharula yenyewe ni kwenda kutafutwa mwanamke mwingine kama mwanamke alijisikia uchungu.

“Ni sawa tu Mr Ron , siwezi kufa kwa kukosa mwanaume na isitoshe nimezoea maisha ya kuwa peke yangu”Aliongea na kumfanya Ron kushangaa.

“Hakika una hulka sawa kabisa na Malkia Persephone”Aliongea.

“Persephone !!.. unamanisha Edna?”

“Ndio japo imekuwa huzuni hayupo hapa”Aliongea

Magdalena aliona maneno ya Ron yamekaa kinyume, yamkini hawana uelewa kwamba mwanaume wanaemwita Pluto alikuwa akimuogopa sana mke wake na kumnyenyekea na asingekuwa hata na ubavu wa kumleta eneo kama hilo, hayo yalikuwa mawazo ya Magdalena.

Wakati wakiwa wanakaribia kuingia hotelini ghafla tu walisogelewa na mwanaume mzungu mwenye nywele nyeusi zilizojikunja , pamoja na macho ya bluu huku akiwa na tatoo kubwa eneo la shingoni , alikuwa akitembea kwa kuonyesha namna ambavyo anajiamini, hakuwa mbaya wa sura alikuwa na mwonekano mzuri.

Magdalena baada ya kumwangalia vizuri tu aliweza kumjua kwani sura yake alishawahi kuiona.

“Hades yuko wapi?”Aliuliza kwa lugha ya kingereza mara baada ya kumsogelea Magdalena.

“Ares”Aliita Magdalena , alikuwa akimfahamu Ares kwani aliweza kumshuhudia kipindi alipokuwa akipambana na Roma katika mlima wa Oldonyo ole lengai , waliweza kumfahamu mara baada ya kufanya uchuguzi wa kuijua sura yake chini ya jeshi na yeye kama mkuu wa kitengo cha wachawi aliweza kuwa na taarifa ya sura yake licha ya kwamba uchugnuzi wao ulifanywa kuwa taarifa za siri za jeshi.

Magdalena hakushangazwa na uwepo wa Ares katika maeneo hayo kwani Roma aliongea nao na kuwaambia kwamba angeita miungu mingine kuja mpaka hapo, upande wa Ron ndio kwanza anamfahamu Ares kwani alikuwa akimsikia tu na palepale aliinama kuonyesha heshima baada ya kumfahamu.

“Mfalme Ares , Mfalme Pluto ameelekea bahari ya Baltic na ataendelea kusafiri kuzunguka baadhi ya maeno ya Ulaya kumtafuta mtu kwa zaidi ya siku mbili”

“Nini!!, kwahio unamaanisha kwamba hayupo hapa visiwani , ndio maana imenishangaza namtafuta simuoni”Aliongea huku akionyesha hali ya kutokuwa na furaha.

“Nilikuwa nikipanga angalau twend raundi moja ya mapambano, nadhani siwezi kufanya lolote”Aliongea.

Upande wa Magdalena huenda kabla ya kuingia levo ya Nafsi angemhofia Ares, lakini tokea aifikie levo hio alijihisi kabisa kuwa mkubwa juu ya binadamu wengine, moja ya athari kubwa ya nguvu za kijini ni hali ya kuwa na aina flani hivi ya ukiburi na hali hio ilimvaa Magdalena kwa wakati huo.

“Inahaja gani , ulipoteza pambano kipindi kile kule Tanzania, alikuwa na nguvu kidogo lakini kwasasa amezidi kuimarika , unafikiri unaweza kuwa mshindani wake?”

“Wewe mwanamke unajua nini , sikuwa nikipambana kwa uwezo wangu wote kipindi kile na pia nilimdharau adui yangu , kama ningejua alikuwa na mbinu zilizojificha kipindi kile ningejipanga , unaniambia ameimarika kwasasa , ngoja nikuelezee sisi tushapigana na wale viumbe wasionekana na tukawashinda licha ya levo zao kuwa za juu, unafikiri naweza kumuogopa Hades”Aliongea lakini licha ya hivyo haikumuogopesha Magdalena kwani alikuwa na taarifa zote juu ya kwamba Ares ndio aliekuwa dhaifu kuliko wote.

“Haha.. inapendeza , ni muda mrefu sana tokea mara ya mwisho tulipokutana lakini bado tabia yako ya kujikweza haijaisha tu”Sauti ya kume ilisikika nyuma yao na kuwafanya wote kugeuka

Alikuwa ni mwanaume mrefu , mzungu na ‘Handsome’ alievalia shati la mikono mirefu lenye michoto , hakuwa peke yake ameongozana na mwanamke mrembo mwenye nywele zake nyeupe., alikuwa ni Stern aliembatana na Alice ambao walifahamika kwa jina la Apollo na Artemis.

Alice mara baada ya kumwangalia Magdalena alitoa tabasamu pana na kumnyooshea mkono kumsalitimia.

“Hello beutifull wewe ni mmoja wa wanawake wa Hade pia ? Hehe naona unatoa msisimko wa nguvu za mbingu na ardhi . sio mbaya..”Aliongea

“Kuna haja gani ya kuuliza , kama sio mwanamke wa Hades ningekuwa nishamuua sasa hivi , hujui kuna sheria ya kuua binadamu na majini yote yaliofikia levo ya Nafsi yanayotuingilia katika ulimwengu wa kawaida?”Aliongea Ares.

“Acha kujigamba , swali muhimu la kujiuliza je unaweza kuniua?”Aliongea Magdalena kwa kiburi

“Unasemaje wewe?”Aliuliza Ares huku akianza kupandisha hasira zake.
Hatariiii
 
singanojr anajua kuwakomesha wapenda bwereree.Hebu mlioko kwenye magroup ya whatsapp tupieni humu muendelezo!
Hapo ndipo anapokosea, wadau au wateja hawakomeshwi isipokuwa anajiharibia mwenyewe coz;
1. Anaonekana he is not a man of his words(haaminiki) kwa hiyo jihadharini na mtu wa namna hii ipo siku mtalia.
2. Hajui kupanga ratiba yake.
3. Si mtu wa kujali hisia za wengine au ana majivuno na haonekani kujutia kwa mambo madogomadogo.
4. All in all mimi ndo naacha kufuatilia story yake maana lengo ilikuwa kupata burudani na si karaha. (Tafuteni mbadala).
5. Wengine hatukushindwa kununua hii story isipokuwa tulikuwa tunajiuliza je pesa yetu inakwenda kwa mtu sahihi au ndo wale wa story zisizoisha?.(Mtu aliyeng'atwa na nyoka hata akiona ung'ong'o hushituka). Bye


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo ndipo anapokosea, wadau au wateja hawakomeshwi isipokuwa anajiharibia mwenyewe coz;
1. Anaonekana he is not a man of his words(haaminiki) kwa hiyo jihadharini na mtu wa namna hii ipo siku mtalia.
2. Hajui kupanga ratiba yake.
3. Si mtu wa kujali hisia za wengine au ana majivuno na haonekani kujutia kwa mambo madogomadogo.
4. All in all mimi ndo naacha kufuatilia story yake maana lengo ilikuwa kupata burudani na si karaha. (Tafuteni mbadala).
5. Wengine hatukushindwa kununua hii story isipokuwa tulikuwa tunajiuliza je pesa yetu inakwenda kwa mtu sahihi au ndo wale wa story zisizoisha?.(Mtu aliyeng'atwa na nyoka hata akiona ung'ong'o hushituka). Bye


Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona watu mnapenda kulalamika sana? Mtu kaleta mwenyewe kwa nafasi yake, halafu tumpangie as if ni Lazima alete story humu. Kama anaandaa hsijakamilika alete tuu? Ni mali yake acha atambe nayo. Anaweza hata kuacha kuleta humu na maisha yakaenda poa tuu. Story kuishia njiani humu ni kawaida sana. Ni story nyingi na waandishi wengi hawajamalizaga story zao wakasepa.

Kuna maisha mengine sawa na mimi na wewe hawa waandishi wanaishi. Yaani mtu aache kwenda kwenye vibarua vyake vya hapa na pale abaki kukuletea story humu wewe ufurahi?
 
Mbona watu mnapenda kulalamika sana? Mtu kaleta mwenyewe kwa nafasi yake, halafu tumpangie as if ni Lazima alete story humu. Kama anaandaa hsijakamilika alete tuu? Ni mali yake acha atambe nayo. Anaweza hata kuacha kuleta humu na maisha yakaenda poa tuu. Story kuishia njiani humu ni kawaida sana. Ni story nyingi na waandishi wengi hawajamalizaga story zao wakasepa.

Kuna maisha mengine sawa na mimi na wewe hawa waandishi wanaishi. Yaani mtu aache kwenda kwenye vibarua vyake vya hapa na pale abaki kukuletea story humu wewe ufurahi?
Mkuu ktk majukumu yako huzingatiii muda na ratiba uliyojiwekea? Au we unajiendea tu ka gari bovu.
Siku zote kwa watu makini kama shughuli zao hazizingatii muda basi huwa hawatoi muda specific ili kuepuka kuharibu ratiba za wengine.
Shida hapa si yeye kuleta mwenyewe shida ni kutoa ahadi ambazo hazitimii kwa wakati. Fikiria kwa upana wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NILIMDHANIA KAHAB KUMBE BIKRA

MTUNZI: SINGANOJR -(Mono no aware).
WATSAPP: 0687151346.


SEHEMU YA 617.
Ghalfa tu anga lote lilijaa sauti za ngurumo za Majoka ambayo yalikuwa katika kiwango cha juu cha hasira , sauti zao zilikuwa kubwa kiasi kwamba zilikuwa zikitoa hofu ya aina yake.
Majini mengine mara baada ya kusikia ngurumo hizo paleale yaliita mapepo yao ya ndani na macho yao na meno vilianza kubadilika na kuwa viumbe vya kutisha.
Ni sekunde tu ni kama vile wale majini waliokuwa katika umbo la binadamu miili yao ilitengana na roho zao kwani kulionekana vivuli vya roho wa kipepo vikiwatoka huku vikiwa na siraha na kuwasogelea kundi la majini joka kwa ajili ya kuanza mapigano.
Master Zao akiwa na filimbi yake mkononi palepale aliipuliza na kufumba na kufumbua filimbi yake ile iligeuka na kuwa panga refu lililokuwa likitoa mvuke wa moto wa rangi ya Zambarau, ukiwa ni moto ambao ulisafiri kueleka angani ukiwa na nguvu ya uharibifu.
Bwana huyo ambaye alikuwa katika daraja la tisa la nguvu za kijini cheo chake hakikuwa cha bure tu , inaweza ikaonekana levo yake kuwa juu tu lakini msisimko uliokuwa ukitoka kwenye upanga wake haukuwa wa kawaida kabisa .
Lakini licha ya hivyo Mfalme Wuja hakuonyesha kuhofia kabisa ile siraha yake , baada ya kuua majini wawili wa levo ya anga na wa kundi la Master Zao palepale alisogelea kundi la Mbweha wa Jade.
“Inatia aibu kwamba Mbweha wa Jade hamtaki kushiriki katika haya mapambano”Aliongea Mfalme Wuja na kama kichaa vile alisogelea jini moja ambalo lilikuwa daraja la saba na alitoa kucha zake na kabla jini ile halijafanikiwa kukwepa lilikuwa tayari limeshavamiwa na kucha zile kuzama katika mwili wake na kuchanguliwa changuliwa na kilichoonekana ni vipande vya nyama pekee.
Aoiline alipandishwa hasira na kitendo kile cha uchokozi wa wazi wazi kiasi cha kufanya misuli ya uso kumsimama huku uso wake ukibadilika katika ule urembo wake na kuwa wa kikauzu ambao haupendezi.
“Wuja , nilikupotezea kwa kipindi kirefu lakini naona unakitafuta kifo”Aliongea Aoiline kwa hasira mno na palepale vazi ambalo alikuwa amevaa lilibadilika na kuanza kua na kamba kamba za hariri zilizokuwa zikiepepea heweani.
Kwa jinsi ambavyo zilikuwa zikipepea ni kama vile nyoka anatoka katika shimo lake kwani zilipinda pinda bila ya kuathiriwa na upepo.
Dakika ileile Majoka mengine yaliwasogelea kwa kasi na moja wapo la rangi nyeusi, kabla hata halijamsogelea karibu Aoiline kujaribu kumshambulia liliweza kusambaritiswa kucha zake na zile kamba za nguvu ya kijini za muonekano wa hariri.
“Mnashangaa nini nyie , shambulieni muwaue hayo majoka wote”Aliongea Aoiline kwa sauti.
Dakika hio hio majini ya anga palepale yalitii amri ya mkuu wao na yalianza kusogelea majoka yaliokuwa yakiambaa ambaa kama Madragoni angani na kuanza kuyashambulia.
Ni ndani ya dakika chache tu juu angani majini pepo wa anga na majini shetani anga na Majoka walikuwa wakipambana kwa kiwango cha juu sana kwa hali ya kikatili mno.
Kwa namna hali ilivyokuwa ni kama vile ile sheria ya mashindano haikuwa ikifuatwa tena kwani Mfalme wa Majoka alibadilisha hali ya hewa mara baada tu ya kufika katika eneo hilo.
Ni nguvu isiokuwa ya kawaida ya kijini iliokuwa imesambaa katika eneo hilo na kama ni binadamu wa kawaida asingeweza kuendelea kuishi katika eneo hilo kwani nguvu yake haikuwa ya kawaida.
Majini ni viumbe ambavyo vimebarikiwa nguvu kubwa ya kiroho tofauti na binadamu na ndio maana ilikuwa ngumu kwa binadamu wa kawaida kuweza kuhimili nguvu yao.
Roma hakutaka kuwa na haraka kwa wakati huo ,kipaumbele chake ni kwanza kumlinda Sophia ambaye alikuwa karibu yake , hivyo alimchukua na kumtoa mbali na eneo hilo huku akiendelea kuangalia mapambano.
Mpasuko wa nguvu za kijini ambao alikuwa akihisi kutokea mbali ulimfanya kutapika kwani ndio tu kwanza ameingia kwenye levo ya Nafsi na kumfanya Roma kumzingira vizuri na nguvu ya kijini ili asizidi kuathirika.
Roma aliangalia mapigano hayo na alijikuta akishangaa kwani Mfame Wuja alionekana yupo mbali sana kuweza kumshinda Aoiline lakini alishindwa kuelewa ni kitu gani ambacho kinampa hali ya kujiamini mpaka kuwachokoza makundi yote mawili ya kijini yaani la Master Zao na la Aoiline.
Lakini katika mapambano hayo kilichomshangaza zaidi ni uwezo wa mtu ambaye alikuwa amevaa mask , kwani alionekana kuyadhibiti majoka kwa uwezo wa hali ya juu sana tena kwa ustadi wa ajabu, tena haikuwa ni swala la kushambulia tu muda huo huo alikuwa akimlinda Moli ambaye alionekana kutokuwa katika levo ya juu zaidi.
Roma mara baada ya kumuona yule mtu mwenye Mask kutumia maji ya kiroho kuyeyusha Roho za wale majoka alijikuta akijawa zaidi na shauku kwani mbinu yake ilikuwa iikifanana na yeye kwa kiwango kikubwa na ilikuwa ni tofauti kabisa na za majini pepo.
Roma alijiuliza je na yeye atakuwa amejifunza mbinu kama ya kwake ya Andiko la urejesho usio na kikomo, alijiuliza inawezekanaje.
Katika dunia yote ukiachana na Lanlan ambaye ndio ambaye amemfundisha mwenyewe namna ya kuvuna nishati za mbinu na ardhi kwa njia ndefu , mtu mwingine tofauti na yeye aliekuwa akijinfuza mbinu hizo alikuwa akikumbuka amekwisha kufariki kwa kuuliwa na Zeros organisation kabla ya kuisambaratisha.
“Au atakuwa ni…,” Roma alitaka kujiambia au ni Master wake lakini alipotezea mawazo yake , ijapokuwa hakuwahi kushuhudia Master wake akifa mbele yake lakini alikuwa akijua alikufa.
Pambano kati ya Aoiline na Mfalme Wuja lilikuwa limefikia katika hali ya juu kabisa.
Wuja mwili wake wote ulikuwa umefunikwa na nguvu ya kijini ambayo ilikuwa ikidhihirika kutokana na wingu kama moshi ambao ulikuwa umemzingira.
Baada ya kuendela kurushushiana mapigo na Aoiline, palepale alianza kutoa ngurumo ya hali ya juu yenye kutetemesha anga na kutengneza mwangi wa kujirudia rudia.
Dakika ile ile ya ngurumo mwili wake ulianza kubadilika na kuongezeka ukubwa na palepale ni kama imepokelewa kwani Mfalme Wuja alibadilika kabisa muonekano wake kutoka katika mwili wa kibinadamu na kuwa katika mwili wa Joka mwenye vichwa tisa.
“Wuja unadhani unaweza kunitisha kwa kuweza kuonyesha upande wako uliozaliwa nao ?”Aliuliza Aoiline huku akimwangalia kwa tabasamu la kejeli na palepale mikia yake yote tisa iliweza kutoka nyuma ya sketi yake
Mikia ile ilikuwa ikipepea kama vile ni nyoka wa umeme aliekuwa akielea angani na ni kama vile inapeerushwa na upepo na kufanya waliokuwa wakimwangalia kuwa katika hali ya mshangao.
Roma alishangazwa na pande zote , alimshangaa Mfalme Wuja kuwa Joka la Vichwa tisa na akamshangaa Aoiiline kuonyesha mikia yake yote tisa.
“Splash, Spash , Splash!!!”
Ni kitendo cha dakika tu palepale vichwa vitatu vya mfalme wa Majoka vilikatwa na mikia mitatu ya Aoiline kwa ustadi wa hali ya juu ambao ulimfanya hata Mfalme wa Majoka kutotegemea shambulizi lile.
Roma alishangazwa na nguvu ya ile mikia , ilikuwa na kasi ya ajabu kama vile ilikuwa ikiendeshwa na umeme na aliogopa namna ambavyo Aoiline alikuwa na uwezo wa kuitawala yote tisa na kufanya mashambulio ya aina tofauti tofauti.
Roma alijiambia kama Aoiline angekuwa mtu wa tamaa kubwa basi ulimwengu wote huo wa majini pepo ungekuwa chini yake.
Licha ya vichwa vya Joka mkuu kukatwa palepale vilichomoza upya kuonyesha kupona na havikuonyesha kuwa katika hali ya hofu kabisa ya kumshambulia Aoiline , isitoshe kujiamini kwao kulitokana na roho ya Mfalme Wuja.
Majjoka yale yalianza kutema moto wa kijini usiokuwa wa kawaida kama vile yanapumua kama madragoni , ulikuwa moto ambao huenda kwa jini ambalo lipo katika daraja la saba lingeshambuliwa lingeungua moja kwa moja na kupoteza maisha.
Lakini licha ya Aoiline kushambuliwa na moto hakuonyesha hofu yoyote ni kama vile alitafsirni mchezo wa kitoto kwake na palepale mkia uliokuwa umefungwa na kamba hariri uliweza kutokezea.
Kuna uhusiano mkubwa sana wa nguvu za kijini na hariri na ndio maana asilimia kubwa majini mengi yalikuwa yakivaa nguo zilizotengenezwa na hariri tupu.
Upande wa Mfalme wa Majini ya kishetani , bwana Zao alikuwa na hasira mno na alikuwa akitembeza upanga wake wa Zambarau kwa kasi ambayo haikuwa ya kawaida akifyeka majoka.
Kila anapokata ni damu za majoka hayo zilizokuwa zikiruka kila mahali lakini licha ya hivyo pigo moja halikuweza kutosha kuua Dragoni kwani yaliugulia mauvimu na kuendelza mashambulizi.
“Wewe mlevi unaweza ukakata hivi vichwa tisa lakini bado havitoacha kukua tena , kama unataka kuviua kabisa lenga moyo wake”Aliongea Aoiline mara baada ya master Zao kuja na kuanza kumshambulia Mfalme wa Majoka.
Baada ya Master Zao kuelewa maneno ya Aoiline palepale alisogelea vichwa vya Mfalme wa Majoka katika eneo la mgongo wake na kulichoma na panga lake kwa nguvu.
Baada ya Mfalme wa Majoka kuchomwa na upanga mgongoni vichwa vyake vilianza kutoa sauti kubwa ya maumivu na paleplae nguvu ya kijini ilizidi kuzalishwa katika mwili wake na mwili ulianza kuimarika zaidi ya mara kumi.
‘Bang , Bang , Bang!!!
Kila muda ambao Master Zao akishambulia na kugusana na magamba ya joka ulitokea mgongano uliopelekea mlipuko mkubwa wa nguvu za kijini.
“Roar!!!...huwezi kuufikia moyo wangu kirahisi”sauti ya Mfalme Wuja iliweza kusikika na ilikuwa ni kama inatokea kuzimuni.
“Master wako hapa sijafanya shambulizi la maana nini kunakufanya kujivunia ewe joka wa vichwa tisa?”
Aoiline alionekana kuanza kukosa uvumilivu na palepale nguvu ya kijini ambayo ilionekana kama kamba za hariri iliweza kumtoka na uwezo wa nguvu zake uliweza kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana na palepale mikia yake yote tisa iliungana na kuwa mkia mmoja.
Baada ya mikia ile kuungana ile sehemu ya mbele yae ilikuwa imechongoka kama mkuki wenye makali yasiokuwa ya kawaida na ulianza kuongezeka urefu kwa spidi kumsogelea Mfalme wa Majoka kwa kulenga eneo la kifua chake na mara baada ya kumfikia ulitokea mlipuko wa nguvu za kijini wa aina yake na kumfanya Roma aliekuwa akiangalia kwa mbali kuanza kutetemeka.
Hata Master Zao ambaye alikuwa akishambulia kwa kasi alijikuta akipigwa na wimbi la nguvu za kijini na kurudishwa nyuma
Palepale gamba la rangi nyeusi la mfalme Joka lilikuja kugusana na mshale wa muunganiko wa mikia tisa na baada ya kiwingu cha moshi kutokea palepale eneo la kifua cha mfalme Joka kilionekana kutobolewa na mkia ule.
“Owiiii..!!”
Vichwa vyote tisa viliweza kutoa kilio cha maumivu huku vikianza kujipinda pinda.
Mkia ule uliingia ndani zaidi ya kifua cha Joka lile na kutoboa nje kabisa kwenye mgongo na palepale damu nyingi zilirudkka na kumwagikia ziwani zikiungana na damu nyingi zilobadilisha rangi ya ziwa hilo za majini mengine.
“Mfalme..!!”
“Mfalme Wetu”
Majoka mengine yaliokuwa yamebakia yalipiga kelele mara baada ya kushuhudia shambulizi lile ambalo amepokea Mfalme wa Majoka, walikuwa wakisubiria mfalme wao kuweza kutoa siraha yake ya damu ya majini Joka lakini tofauti na hivyo wanaona akichomwa na mkia wa Aoiline.
Mfalme Wija alikuwa ni mchanganyiko wa uzao wa Kijoka na aina nyingne ya majini na ndio maana alitokea kuzaliwa na vichwa tisa , mwanzoni alipozaliwa ukoo wa kijini joka ulimdharau kutokana na kutofanana na wengine lakini mara baada ya kukua aliweza kumuua mfalme wa Mojoka wa enzi hizo na yeye kuchukua madaraka katika miliki yote ya Korongo la Joka.
Alikuwa tofauti kabisa na kizazi cha majini joka mengine na hata kama kichwa chake kikikatwa kinazaliwa upya tena kwa haraka lakini hio yote ni kutokana na uwezo mkubwa sana wa mwili wake lakini licha ya hivyo udhaifu wake ulikuwa ni moyo wake.
Aoiline alikuwa akijua udhaifu mkubwa wa majoka ni moyo na ndio maana alifanya shambulizi la kushitukiza kuutoboa moyo wake
Master Zao alijikuta akishangazwa na tukio lile , ijapokuwa alijua Mfalme Wa Majoka na yeye walikuwa katike levo ya tisa na uwezo wao ulikuwa ukilingana na wa Aoiline lakini hakutegemea kuona Aoiline alikuwa ni wa uwezo mwingine kabisa kwani aliweza kumfanyia shambulizi mfalme Wuja kwa spidi kubwa ambayo yeye mwenyewe hakuweza kutegemea.
Master Zao siku zote alikuwa akijikweza na kujiweka katika daraja sawa na Aoiline lakini kwa kilichotokea hapo aliona kabisa huyo mwanamke hakuwahi kuwachukulia siriasi, pengine ndio maana hawakuweza kuujua uwezo wake wote ni mkubwa kiasi gani.
Hali ya kimapambano iliweza kubadilika ndani ya muda mfupi mara baada ya Mfalme wa majoka moyo wake kutobolewa.
Na hata vile vichwa tisa vilionyesha kufurukuta na kuanza kupoteza maisha na mabawa ya Mfalme Wuja hayakuweza tena kuhimili mwili wake na palepale aliporomoka kutoka angani na kwenda kutumbukia katika maji ya ziwa.
“Boom !!”
Baada ya mwili wake kudondoka chini maji yaliokuwa na miili iliokuwa ikielea na damu yaliruka juu na kutengeneza shimo kubwa .
Baada ya kuona mfalme Wuja kashauliwa na mbweha wa mikia tisa , majoka yaliokuwa yamebakia yalishikwa na mshituko lakini kwa wakati mmoja yakianza kukumbwa na hofu ya woga.
Kutokana na hofu yao pamoja na mshangao , ile ari yao ya kimapigano ilishuka na kundi la Master Zao na la Aoiline walichukua nafasi hio kwa faida na kuanza kuyaua kwa spidi zote na ndani ya dakika chache tu miili ya majoka yote yalilelea katika ziwa.
Yalikuwa ni mauaji ambayo hayakuwa ya kawaida kuweza kutokea katika ulimwengu huo wa majini pepo kwa miaka mingi sana , kwani majoka yaliokuwa yamefika hapo ndio mhimili wa mamlaka ya kijoka.
Majini ya miliki ya Mbweha wa Jade yalikuwa katika furaha kubwa sana , hawakuweza kuamini kama Master wao alikuwa katika lavo za juu sana za kimapiingao mpaka kuweza kumuua Mfalme wa Majoka.
Kila mmoja aliweza kuona hapo baadae , ulimwengu wote wa majini pepo utakuwa chini ya Mbweha wa Jade kwasababu Master Zao uwezo wake ulikuwa ukilingana na wa Mfalme Wuja basi asingeweza kuwa tishio kwa Aoiline.
Miliki ya Korongo la Joka licha ya kuwam na wapigananji waliojificha ingekuwa ngumu kurudisha utukufu wa jina lao.
“Inaonekana baada ya leo historia ya miliki ya kijini itaandikwa upya”Aliongea Master Zao akimwangalia Aoiline kwa muonekano usiokuwa wa kawaida.
Aoiline palepale alirudisha mikia yake lakini macho yake yalikuwa bado na mashaka wakati akiendelea kuangalia mwili Mfalme wa Majoka aliekuwa akielea kwenye maji , alionekana kama kuna kitu ambacho alikuwa akiwazia na hakijamridhisha.
“Master , sasa tayari mfalme wa Majoka amekwisha kufa , kwanini nisiongoze wenzangu na kuelekea katika bonde la majoka na kuliweka jumba lote la kifalme chini ya ulinzi?”Aliuliza Iluwa.
“Bado kuna kitu nina mashaka nacho , Mfalme Wuja sio mtu wa kuharakisha mambo na asiekuwa makini , isitoshe mnara unakaribia kufunguka hivyo tumalizane na maswala ya hapa kwanza”Aliongea Aoiline akikataa ombi la Iluwa.
“Kwa sasa sidhani kama kuna haja ya mashindano tena na mnara unatakiwa kuwa chini ya miliki yetu ya Mbweha wa Jade”Aliongea Iluwa akiwaangalia majini ya upande wa Master Zao.
Walionekana kuchoka sana kwa kutoa kiasi kingi cha nguvu zao katika kupambana na majoka hivyo walijua kabisa ingekuwa ngumu kwa Master wao kuweza kumshinda Aoiline.
“Haiwezi kuwa hivyo , mashindano yanatakiwa kufanyika kama ilivyopangwa na sina haja ya kuanza kuwaza nani ana nguvu zaidi hapa , ili mradi hakuna uchokozi unaotokea upande wowote isiwe shida, tunao muda wa kutosha mpaka kufunguka kwa mnara na sasa hii minyoo mirefu(nyoka) kutoka Korongo la joka imekufa ni juu ya Roma kushindana sasa na Master Tian, ambaye atashinda atakuwa na haki ya kuingia katika mnara kama kanuni ya mashindano inavyotaka”Aliongea Aoiline na kufanya kila mmoja aliekuwa hapo kushindwa kuelewa mpango wa Aoiline ulikuwa ni nini kwani ilikuwa ni dhahiri hakukuwa na haja ya mapambano.
Upande wa Roma aliona pengine Aoiline ashaona Master Tiani alikuwa na uwezo unaofanana na wa kwake wa kutumia nguvu ya Andiko la urejesho usio na kikomo na kutarajia kuona nani ana nguvu zaidi.
Upande wa angani Master Tian hakuonyesha hofu yoyote wala kusogea na alikuwa akisikiliza maongezi hayo kwa ukaribu huku akimwangalia Roma.








SEHEMU YA 618.
Hakukuwa na haja ya kuwambiwa piganeni kwani Roma na Mastr Tian walikuwa wakiangaliana kwa matarajio ya kuanza mapigano.
Upande wa Roma aliweza kuona macho ya matarajio kutoka kwa Master Tian na palepale licha ya kuwa na mashaka nae alimsogelea kwa kasi na kuanza kumshambulia.
Wakati pande zote mbiili zikianza kuvuta hewa kwa ajili ya kuangalia mtanange huo , upande wa wapiganaji kila mmoja aliiita nguvu za kijini na msisimko wa nguvu zao ulikuwa ni wa kufanana kabisa.
“Foosh”
Donge la moto wa njano liliweza kuonekana katika mkono wa Roma na msisimko wake pamoja na joto lake lilifanya majini yaliokuwa karibu kusogea pembeni.
Master Tian hakuonyesha kushangazwa na Donge la moto ule na palepale mkono wake na wenyewe kulionekana Donge kubwa la maji ya kiroho.
Wote kwa pamoja waliangaliana huku wakiwa katika kimya cha muda mfupi ni kama walikuwa wakisomana mawazo na ghafla tu wote kwa pamoja kila mtu alimrushia mwenzake shambulizi lake.
“Bang!!”
Mlipuko mkubwa uliweza kutokea palepale mara baada ya donge la maji na Donge la moto wa njano kugusana ni kama vilikataana na kutengeneza mlipuko na dakika ileile walijikuta wakipaa zaidi kwenda angani na kuanza kushambuliana kwa kasi na kwa macho ya kawiada ilikuwa ni ngumu kuweza kuwatofautisha.
Ni mwanga wa siraha zao ndio ulioweza kuwatofautisha , Roma alikuwa akitumia moto kushambulia na Master Tian alikuwa akitumia maji katika kushambulia na mara baada ya donge la rangi nyeupe la moto kugusana na la donge la maji ya bluu palepale ulitokea mlipuko uliosambaa hewani lakini hawakuishia hapo kwani walisogeleana kwa kasi na kurushiana ngumi ambazo ziligongana hewani.
Kila mmoja alionekana kutotaka kutumia nguvu nyingi za kijini na kuzipoteza na walianza kutumia njia za kawaida katika kushambuliana huku mapigo ya kawaida ya miguu na ngumi yakichukua nafasi kubwa.
Mara nyingi inapotoktea mshindani na mshindanni kuwa na nguvu za kawaida za kijini kama hivyo , njia pekee ya kutofautisha nani ana nguvu zadi ni kutumia mbinu za kimapigano za kawaida na hapo ndio atajulikana nani mkubwa na nani mdogo.
Wale majini wa kipepo walijikuta wakiwa katika mshangao na mshituko kwa wakati mmoja , kwani hawakuweza kuelewa ni mbinu gani ya kijini waliokuwa wakitumia watu hao m kwani kilikuwa kitu kigeni kwao ambacho msisimko wake uliumiza roho zao na mapemo yaliokuwa ndani ya miili yao kufurukuta.
Ilikuwa ni kama vile nguvu zao zilikuwa zikipigana na zile ambazo Master Tian na Roma walikuwa wakitumia katika kupambana.
Hawakuelewa kwanini walikuwa na uwezo wa kuweza kudhibiti moto pamoja na maji , kwani vitu vyote hivyo vilikuwa nje ya uwezo wao.
Roma alijikuta palepale akipokea pigo la mzunguko lakini wakati huo akawa tayari amekwisha kuachia donge la moto wa njano lakini Master Tian aliweza kupangua kwa wepesi zaidi kwa kutumia ngao yake lakini moto ule wa shambulio la Roma ulioneka kutozimika na katika hali ya kawaida na yeye alichia nguvu ya kijini ilioambatana na maji na kuzingira lile pigo la Roma na kurudisha kwake.
Roma baada ya kuona kitendo kile cha kumshangaza paepale aliita nguvu zake za kijini na kujikinga na palepale ulitokea mlipuko kama wa bomu na kuwasogeza mbali mbali Zaidi.
Roma hakutaka kupumzika kwani mlipuko ulikuwa wa sekunde tu na kupotea na palepale alibadilisha pigo lake na kuja na moto wa Bluu .
“Blue True fire!!!”
Aliongea Master Tian kwa mshangao kidogo huku akikwepa shambulizi lile kwani alijua athari yake ni nini kama angegusana nao kwani roho yake ingekuwa ndio inaungua na mwili ukiwa katika hali ya uzima.
Roma palepale alitengeneza vitenesi viwili katika mikono yote vya moto wa bluu na kutaka kushambulia lakini hofu ilimwingia Master Tian kwa kuogopa anaweza kushindwa kukwepa mapigo yote lakini upande wa Roma alionyesha kusita sita kwani sauti ya Master Tian ilianza kutekenya akili yake.
“Hii sauti … ni kama ya.. , Master?”Aliongea Roma kwa nguvu lakini palepale ni kama suati ile ilikuwa ikijiurida rudia katika akili yake na moto wake wa bluu ulizima palepale.
Master Chi palepale aliachia cheko na palepale alitoa ile Mask yake na kuonyoshe sura yake kwa Roma.
Roma alijihisi ni kama vile kuna wimbi la shoti ambalo limempiga , hakuweza kuona sura hio kwa zaidi zaidi ya miaka kumi tokea kipindi ambacho alikuwa na miaka tisa tu kwenda kumi lakini hata hivyo sura yake ni kama ilikuwa ikiishi ndani ya akili zake kutokana na kuwa na shukrani isiokuwa na mwisho juu yake.
Kabla ya Roma kurudi Tanzania, kama kuna mtu yoyote ambaye anamheshimu katika dunia hii basi ni Master Chi , alikuwa ni yeye kabisa, alikuwa ni Master Tang Chi mwanaume aliekuwa akimkumbuka kwa wema aliomtendea kwa kumfundisha kwa muda mfupi mbinu za nguvu ya andiko la urejesho usio na kikomo.
“Master chi , Master Chi … hahaha.., Mjomba ni wewe kweli , siamini”Aliongea Roma huku akicheka kama mtoto ambaye amepewa zawadi.
Master Chi nywele zake ndefu za kichina zilikuwa zikipeperushwa na upepo huku akimwangalia Roma kwa macho yake yenye upendo ndani yake , upendo ambao hajawahi kuonyesha kwa mtu yoyote kwenye maisha yake , baada ya kuona kijana aliemjua miaka kadhaa iliopita amekuwa mtu mzim alihisi hisia ambazo hazikuwa za kawaida , iijapokuwa haikupaswa kwake kujiita mwalimu kwa Roma lakini kwa namna moja ama nyingine ni yeye ambaye alimfungulia kodi kuhusu mafunzo ya mbinu za anga.
“Kijana , naona ulikuwa ukiendelea vizuri”Aliongea mara baada ya Roma kumsogelea karibu , ni yeye pekee ambaye alikuwa akijua kauli yake ilikuwa ikimaanisha nini katika ulimwengu wa kujifunza mbinu za kijini.
Master Zao na Aoiline hawakuonyesha mshangao mkubwa kwani walikuwa washatarajia jambo hilo muda mrefu na hata hawakutaka kuingilia maongezi yao.
“Master nani ni mshindi?”Aliuliza Iluwa akilenga swali lake kwenda kwa Aoiline.
“Master Tian licha ya kuwa katika levo sawa na Roma amepitwa kwenye mambo mengi , siraha yake kubwa ni kutumia maji ya kiroho lakini Roma ana ujuzi wa moto mweupe , moto wa bluu na moto wa njano pamoja na maji ya kiroho , hivyo hawezi kumshinda , naweza kusema kwamba mpaka sasa tumeshinda”Aliongea Aoiline.
Dakika hio Roma alikuwa katika kiwango cha furaha na palepale alimwita Sophia aje asalimiane na Master wake.
“Sophia huyu ni Master wangu , anaitwa Master Tang chi ndio mtu wa kwanza kuniingiza katika ulimwengu wa mafunzo ya mbinu za kijini”Aliongea na kumfanya Sophia kushangazwa na jambo hilo.
“Unaonekana una msingi mzuri wa mafunzo ya Kung fu na ya kijini , nani ni mwalimu wako wa Kung Fu?”Aliuliza Master Chi mara baada ya kusalimiana na Sophia.
“Mwalimu wangu ni Master Yumiao kiongozi wa dhehebu la Shushani?”Aliongea Sophia na kumfanya Master Chi kutoa mshangao kidogo.
“Abbess Yumiao ni ndugu yangu upande wa mama , ukipata nafasi ya kutoka nje ya ulimwengu huu naomba ufikishe salamu zangu za kumuomba radhi kwa kumfelisha”Aliongea Master Chi.
“Master Chi unamaanisha nini?”Aliuliza Roma kwa mshangao mara baada ya kuona hali ya majuto.
“Shushani lingekuwa Dhehubu kubwa ndani ya china pengine dunia nzima , hususani katika mafunzo yote ya kurithisha binadamu na nguvu za kijini zaidi hata ya Dhehebu la Tang , lakini malengo hayo yalipotea kutokana na tamaa za mjomba wangu”Aliongea.
“Master bado sijakuelewa unachotaka kumaanisha”Aliongea Roma.
“Kabla ya yote napaswa kwanza kukuelezea ilikuwaje mpaka nikapotea katika maisha yako na kuja kuonekana hapa”Aliongea Master
Kwasababu mnara bado haukuwa umefunguka bado , walipata muda wa kuongea kuhusu mambo yaliopita na upande wa majini pepo walitumia muda huo kuanza kujiponyesha.
Master Chi hakuwa muongeaji sana na hata katika baadhi ya pointi ambazo zilikuwa na mashaka hakuzunguka zunguka .
Stori ya Master Chi ilianzia wakati wa Roma kuanza kusikia uzushi juu ya kuuliwa kwa Master Chi na kundi la Zeros chini ya kikosi cha kundi la Dhoruba nyekundu, lakini uzushi huo Master Chi anapingana nao na kusema hakuweza kufa licha ya kwamba ilikuwa ni kweli alichomwa sindano ya sumu na wanajeshi wa kikosi cha Dhoruba nyekundu.
Master Chi anasema hata yeye hakujua kilichotokea kwani mara baada ya kupoteza fahamu na kujihisi mfu kabisa alijishutukia akiamka katika eneo tofauti kabisa na Black Site ya Dhoruba nyekundu.
Kuamka kwake hakukumshangaza kwani aliweza kujua nini kilichotokea wakati akiwa katika hali ya kufariki , sumu ambayo aliwekewa katika mwili wake ilimuwezesha kuingia katika levo ya kifo na Uhai na hatimae kuzaliwa upya na kukamilisha levo zote za nguvu ya andiko la urejesho isiokuwa na kikomo.
Kwa lugha nyepesi ni kama kilichomtokea Roma mara baada na yeye kuwekewa sumu na kundi la Takamagahara kule Japani mara baada ya kuingia kwenye mtego wa mwanamke ambaye alikuwa na sura ya Seventeen, sasa ilionekana alichopitia Roma kinafanana na alichopitia Master Chi.
Roma alishangazwa na meneno hayo kwani hakutegemea wakati ambao Master Chi alikuwa akielekea kufariki ndipo alipoweza kupata ufunuo wa levo ya Kifo na uhai na kuingia katika levo ya kuzaliwa upya.
Kwahio kwa haraka haraka ilionekana mara baada ya Zeros organisation kujua Master Chi ameweza kufariki waliamua kumtupa msitunni kwa ajili ya kuliwa na wanyama lakini matokeo yake ni kwamba hakuwa amefariki bali alikuwa akipitia utambuzi mpya wa levo ya nane ya kifo na uhai kuingia ya tisa ya kuzaliwa upya.
Kipindi hicho haya yote wakati yakitokea Roma alikuwa na miaka kumi tu na tayari alikuwa ashakutana na Master Chi na kumrithisha kanuni za andiko la urejesho lisilokuwa na kikomo.
Yaani kwa maneno marahisi kama kile ambacho Roma alifanya kwa Lanlan ndio ambacho alifanya Master Chi kwa Roma , yaani hakukuwa na maelezo ya kutosha tofauti na Roma kuelekezwa katika jangwa la Gobi nchini Mongolia na ya kupanda levo.
Ikumbukwe tokea mwanzo Zeros organisation ndio walikuwa wakiratibu shuhugli zote za Mpango LADO chini ya maelekezo ya kiongizi kivuli , yaani The Doni.
Kama tutajaribu kuunganisha na maneno ya jini Zenzhei aliekuwa mlinzi wa Afande Kweka tunaona kwamba Hades wa Zamani ndio ambaye alimtafuta Zenzhei na kumwambia amsaidie namna ya kupata master wa mafunzo ya mbinu za kijini na ndipo Zenzhei alipomtajia Master Chi, Hades wa zanani ili kurudisha Shukrani alimwachia Zenzhei maneno ambayo yatamsaidia kupata msaada wakati ambao atataka kulipiza kisasi na hata pale alipoyaongea maneno hayo mbele ya Roma aliweza kuyatambua na kuwa tayari kumsaidia kwa kumuahidi siku moja angeenda katika miliki za kijini na kumkomboa katika kifungo cha wazee.
Kwahio ni kwamba, pengine Athena ambaye alikuwa ni mratibu mkuu wa mpango LADO hakutaka Roma kujifunza mbinu za kijini na kumtaka ajifunze namna ya kupata ufahamu wa kanuni za anga lakini upande wa Hades wa Zamani na mipango wake hakutaka Roma kujifunza mbinu za ufahamu wa kanuni za naga bali mafunzo ya kijini ndio maana akamkutanisha na Master Chi bila yeye mwenyewe kujua kama kukutana kwao hakukuwa kwa bahati mbaya.
Ikumbukwe Hades wa zamani alikuwa akitimiza mipango yake ndani ya mpango wa Athena na wakati huo na Athena alikuwa akitimiza mipango yake ndani ya mpango wa Hades wa Zamani.
Inasemekana Master Chi ndio mtu pekee ambaye alikuwa na akili nyingi sana ambazo ndio zilimuwezesha kuweza kujifunza kanuni ya kimaandiko ya urejesho isiokuwa na kikomo.
Master chi anaelezea kwamba mara baada ya kutoka katika mikono ya Zeros na kufahamika kwamba ni mfu ndipo alipoenda kujichimbia katika msitu mmoja kusini mwa bara la Asia na kuanza sasa kufatilia kuvuna nishati ya mbingu na ardhi na kuingia katika levo ya nusu mzunguko , mzunguko kamili , levo ya Nafsi na kuendelea.
Master Chi anasema kwamba licha ya kujichimbia msituni alikuwa bado akifatilia maendeleo ya Roma lakini hakutaka kujitokeza kwake , kwani aliamini ili Roma kuweza kufanikiwa lazima ajitegemee mwenyewe bila kujua uwepo wake.
Anaendelea kusema mara baada ya kuendelea kujichimbia hatmae aliweza kupata njia bora ya kuweza kuficha uwezo wake na kuonekana binadamu wa kawaida.
“Master kwahio uliweza kuniona hata nilivyoweza kuingia levo ya kuzaliwa upya , kama ulikuwa karibu na mimi nchini Tanzania kwanini hukunisogelea?”Aliuliza Roma akiwa kwenye mshangao.
“Nini kinakufanya useme hivyo , nilikuwa karibu yako muda wote lakini ukashindwa hata kunifahamu ,niliwweza pia kutumia muda mwingi kuwaza namna ya kukufikishia binti yako”Aliongea na kumfanya Roma kutoa macho palepale.,
“Binti yangu, unamaanisha nini?”Aliuliza Roma, ilikuwa ni kama vile amepigwa na bomu kichwani na alijikuta akiyumba na kutaka kudondoka chini.
Upande wa Sophia pia alikuwa ameshangazwa na maneno ya Master chi kwani hakuelewa.
Master chi mwenyewe alijikuta akishngazwa na muonekano wa Roma na kujua hana taarifa yoyote.
“Una matatizo gani wewe? , inamaana Lanlan hajaja kuishi na nyie , Bado tu hujui?”Aliuliza.
“Lan… Lanlan?!!!”
Roma alijihisi kama vile anataka kuutapika moyo wake , aina ya maelezo hayo yalifanya akili yake kuanza kupatwa na ukichaa.
“Master unaaanisha nini ? Lanlan ni binti yangu?”Aliongea Roma huku akianza kubadilika na palepale alimshika mabega yake na kuanza kumtingisha kwa nguvu.
“Ndio , Lanlan ni binti yako ambaye amezaliwa na Seventeen”Aliongea huku akitingisha kichwa kwa kujiamini.
“Seventeen!!!, unamaanisha ,, Lanlan ametokana na mimba aliokuwanayo Seventeen?”Aliongea Roma huku macho yake yakiwa sio ya kawaida , yalibadilika kutoka rangi ya kawaida na kuwa nyekundu lakini kwa Master chi ni kama ashazoea hali hio ya Roma.






SEHEMU YA 619.
Sophia pia alikuwa kwenye mshituko mkubwa , alishawahi kusikia kuhusu jina la Seventeen kutoka kwa mwanadada Christen lakini hakuwahi kujua habari zake.
Lakini hakuweza kuamini pia kwamba mtoto ambaye Edna na Roma wamemuasili amegeuka na kuwa ni mtoto wa damu kabisa wa Roma.
“Sio kawaida hili .. kabla ya kuondoka , nilimwachia Qiang Xi barua lakini na kitambulisho cha ishara(token) na nilimaptia maelekezo akupatie , inamaana Qiang Xi tusema amesahau?”Aliongea Master Chi huku mwenyewe akiwa katika mshangao.
Roma mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi mno , hakutaka kujali tena na palepale alimshika mkono Master Chi na kumbeleleza amwambie kila kitu.
“Master naomba unieleze ni nini kinaendelea , Lanlan ni kweli ni binti yangu, kama ni hivyo vipi kuhusu Seventeen?”
Roma hakuonyesha utulivu , alionekana kuhitaji majibu yote kuhusu Lanlan na mpenzi wake Seventeen.
Master Chi baada ya kuona Roma yupo katika hali ya kuchanganyikiwa aliona amwambie kila kitu.
………..
Ni miaka kadhaa iliopita katika mapigano yaliokuwa yakifanyikia baharini, Roma aliweza kumshuhudia Seventeen akilipukiwa na bomu na kutumbukia baharini akiwa mjamzito.
Lakini ukweli ni kwamba licha ya Roma kushuhudia tukio hilo ukweli ni kwamba Seventeen hakupoteza maisha bali alijeruhiwa kwa kiasi kikubwa..
Na yote hayo yaliweza kujulikana mara baada ya Master Chi kukutana na Seventeen katika msitu ambao alikuwa amejichimbia akivuna nishati za mbingu na ardhi.
Ilikuwa ni rahisi kwa Master Chi kumjua Seventeen kwani alishawahi kukutana nae wakati akiwa yupo chini ya Zeros organisation.
Master Chi anasema mara baada ya kukutana na Seventeen Lanlan alikuwa tayari amekwisha kuzaliwa na ni mkubwa tu ambaye ana akili zake timamu za kutambua jema na baya.
Master Chi anasema licha ya kwamba Seventeen alionekana kupona kwa nje lakini bado alikuwa na majeraha ya ndani ambayo hayakuwa yamepona bado na alikuwa akitema damu.
Master Chi anasema kwake ilikuwa ni kama bahati kukutana na Seventeen kwani ilikuwa ni wakati ambao alikuwa pembezoni mwa fukwe akisubiria meli ya bidhaa za magendo kutia nanga ili kuweza kutafuta kile ambacho alikuwa anahitaji na kurudi mafichoni.
Upande wa Seventeen pia aikuwa akimfahamu Master Chi na alionekana kujawa na ahueni mara baada ya kumuona .
Master Chi anasema Seventeen alikuwa amekonda mno kuliko isivyokawaida na alionekana alikuwa mgonjwa sana na muda wowote angepoteza maisha na alionekana kujikaza tu.
Na hata mara baada ya kukutana hawakuongea sana kwani walikaa pamoja kwa siku tatu tu ndio Seventeen akampa maagizo Master chi kumtafuta mahali popote Roma alipo na kumkabidhi Lanlan binti yake.
Katika maongezi hayo ya kimaagizo, Seventeen pia alimwachia kipande cha kisu ambacho kimekatwa katikati na kumwambia atakapompata amuonyeshe Roma ili kumthibitisha Lanlan kama mtoto halali wa Roma.
Master Chi anasema kwamba alijaribu kutumia kanuni ya kimaandiko kujaribbu kumponyesha Seventeen lakini majeraha yake ya ndani yalikuwa makubwa mno lakini kwa Seventeen alionekana kutokuwa na majuto tena kwani alimuacha Lanlan katika mikono salama na kisha akaondoka huku akimuaga Lanlan kwa kumdanganya kwamba anaenda sehemu ya mbali na kumwambia Master Chi ni babu yake.
Seventeen alifanya hivyo ili tu kutomfanya Lanlan kuwa na huzuni na kuanza kumlilia.
Hivyo kwa maneno marahisi ni kwamba Baada ya Lanlan kukabidhiwa kwa Master Chi Seventeen aliondoka kwenda kufia mbali, Mastr Chi anaamini Seventeen kufariki kwasababu majeraha yake yalikuwa makubwa mno ambayo hayangemchukua siku hata mbili mara baada ya kuondoka kwake.
Roma mara baada ya kusikia simulizi hio ya kusisimua ambayo alijikuta akitoa machozi ya kiume alijikuta akimuuliza Master Chi swali kinyonge.
“Master lakini haya yameweza kutokea vipi kwa muda ambao umesema ulikutana na Seventeen , Lanlan si angekuwa na mwaka mmoja tu, kwanini alikuwa na utimamu wa akili tayari?”
“Kwanini unauliza hivyo , kwasababu anaonekana kama wa miaka kumi na moja si ndio?”Aliuliza Master Chi huku akitoa tabasamu la uchungu lakini hata hivyo aliweza kuelewa.
“Nadhani ni jambo la kupangwa litokee , majeraha aliokuwa nayo Seventeen ilikuwa ngumu sana kwa mimba yake kutoharibika au kupata matatizo , lakini Lanlan aliweza kuzaliwa akiwa hana shida yoyote na mimi wakati nakutana na Lanlan alionekana kuwa kama mtoto wa miaka minne licha kwa maelezo ya Seventeen alikuwa na miezi michache, hakuwa mkubwa kwa muonekano wa nje tu lakini hata ubongo wake ulikuwa ukikua kwa haraka sana , kwani niliishi nae kwa miaka michache tu na tayari alikuwa na akili ya mtoto wa miaka saba, nadhani yote hayo ni kutokana mabadiliko ya DNA zako za mwili na hata Seventeen mwenyewe hakuwa na majibu sahihi ya kuelezea hali ya Lanlan mpaka anamuacha , lakini niseme kwamba ilimsaidia sana kuweza kuishi katika mazingira ya hatari msituni kwani uwezo wake wa akili ulimsaidia kujikinga na wanyama wakali , baada ya kukaa nae kwa muda mfupi ukuaji wake ulirudi katika hali ya kawaida na kilichokuwa kikipanuka ni ubongo wake pamoja na mwili wake kuimarika ,nadhani ni halali kusema ndio maana anaonekana sio binadamu wa kawaida”
Roma hakushangazwa zaidi na maneno ya Master Chi , kutokana na mtazamo wa kibailojia uliokuwa katika mwili wake , mara baada ya kuweza kumulikwa na Divine light Genes za mwili wake zilibadilika kabisa na akawa tofauti na binadamu wa kawaida hivyo iliwezekana Lanlan kurithi gene hizo kutoka kwake.
Na kwsababbu Lanlan alikuwa mtoto wake ilikuwa ni swala la kueleweka na kukua kwa haraka , lakini licha yahivyo ukuaji wa Lanlan bado ulikuwa na sababu ambazo hazikuwa wazi kibaiolijia.
Roma sasa alianza kuelewa kwanini Lanlan alikuwa akisema alikuwa akiendesha Tembo , ilikuwa ni kweli kabisa katika misitu mingi ya kusini mwa bara la Asia kulikuwa na Tembo.
Roma alijikuta akijiona sio mwenye bahati, kama kweli Master Chi aliweza kuishi karibu na kituo cha Son and daughter Orphanage kwa ajili ya kumkutanisha na Lanlan lakini bado tu akashindwa kumuona alianza kuhisi hatia.
Baada ya namna ambavyo amekutana na Lanlan na kuwaza mambo mengi yaliopita alijikuta akiona kila kitu kilikuwa ni ujinga wake na kumfanya kuanza kupatwa na majonzi ya kushindwa kumtambua binti yake lakini kwa bahati nzuti ndio sasa anaweza kujua ukweli lakini katika mazingira ambayo bado alikuwa na mashaka kama anaweza kumuona Lanlan tena.
Sasa Swali bado linabakia kama Master Chi anasema Seventeen alikufa je yule aliekutana na Zoe Kovac Maldives ni nani , je Seventeen aliekuwepo kwenye Cryosleep katika maabara ya Athena ni nani.
Yule alietokezea Tanzania na kumwangalia Lanlan akiwa usingizini ni nani.
Roma mara baada ya kuweza kuujua ukweli mawazo ya kummisi Lanlan yalianza kumvaa , hakuamini alikuwa akiishi na mtoto mwenye damu na nyama yake bila kumtambua , hisia kubwa zaidi zilijikuta zikitawala kichwa chake huku macho yake yakianza kubadilika kutoka rangi nyekundu na kurudi njano kijani na kurudi kuwa sawa.
Hali ya kutaka kutoka katika huo ulimwengu wa majini pepo iliaongezeka maradufu.
“Master kama uliujua ukweli kwanini..”Sophia alionekana kutaka kuuliza na palepale Roma aliekuwa katika simanzi alijikuta akirudi katika akili yake na kumwangalia tena Master Tang Chi.
“Sikutaka kurahisisha mambo , kutokea kwa ghafla kwa mtoto kungekuwa na athari kubwa kwenye ndoa changa ambayo umeanzisha ,, isitoshe licha ya kuweza kujua wapi ulipo niliona ni hatari kumleta kwako Lanlan”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa lakini akianza kuelewa pointi yake.
“Nilianza kufanya matembezi na Lanlan, tulianza kwenda China na nikakaa kule kwa zaidi ya nusu mwaka , mwanzoni nilikuwa na wasiwasi namna ya kukuelezea kwamba Seventeen amekwisha kufariki moja kwa moja, pili bado sikuwa na uhakika na hali ya kiafya ya Lanlan namna ukuaji wake wa haraka ulivyokuwa , lakini pia kwa kipindi kile uwezo wako wa kijini ulikuwa mdogo na bado niliogopa kama afya yako imeimarika , hivyo niliogopa kukuongezea mzigo mwigine wa mawazo ya kukuchanganya ilihali ulikuwa ukiendelea vizuri , lakini zaidi ya yote waawake walianza kutokea mmoja baada ya mwingine katika maisha yako na kilichonishangaza zaidi ulikuwa umemuoa mwanamke ambaye alikuwa akifanana na Seventeen , sikutaka kujua taarifa nyingi kuhusu mkeo lakini niliweza kuona kama nitamleta moja kwa moja Lanlan kwako , huenda familia uliokuwa ukianza kujenga ingebomoka , sikuzote nilidhania kuanzisha familia kwako ingekuwa ngumu lakini nilifarijika kuona maendeleo uliokuwa nayo…”
Maneno ya Master Chi yalimgusa Roma , aliona ilikuwa kweli kabisa hata yeye mwenyewe mwanzoni alijua kabisa alianzisha mahusiano na Edna kama mbadala wa Seventeen kwasababbu tu walikuwa wakifanana na hata upande wa Edna bado hisia zake zilikuwa za mashaka hivyo kama Lanlan angekuja katika maisha yake haraka na kujitambulisha kama binti yake aliezaliwa na mwanamke anaefanana nae ingekuwa ngumu sana kwa Edna kukubaliana na swala hilo.
Ukienda mbali zaidi alijua kwamba sehemu ya Seventeen na ya binti yake ingekuwa ni ngumu kuhamishika.
“Master najua ulikuwa sahihi , lakini bado Lanlani alikuwa ni binti yangu , haukuwa ukatli kunifanya nishindwe kumfahamu?”
“Hilo nilizingatia , ukweli nilijua kwamba iwe ni kwa kuchelewa au kwa kuwahi lazima wewe na mtoto wako mtafahamiana ndio maana mwanzoni nilisita lakini nikaishia kumchukua Lanlan na kufika nae Tanzania na kuishi nje kidogo ya jiji la Dar es salaam , lakini katika kipindi hicho niliweza kukutana na matatizo yangu binafsi jambo ambalo lilianza kunifanya nione Lanlan anaweza kuwa hatarini zaidi”
“Matatizo gani?”
“Napaswa kuanza kukuelezea namna ambavyo nimefika huku kwenye ulimwengu wa majini pepo?”
………..
Kwa maelezo ya Master Chi ni kwamba mara baada ya kuingia katika levo ya kupita Dhiki ni kama aliibua majini yaliokuwa katika ulimwengu usionekana.
Kama ilivyokuwa kwa Roma kupigwa na mapigo ya Radi ndio kilichotokea hata kwa Master Chi.
Ikumbukwe mara nyingi licha ya dunia kuona mapigo ya radi kuwa kitu cha kawaida kama janga ambalo linatokea wakati wa mvua kali na mawiungu lakini zile radi za mfululizo huwa zinamaana kubwa katika ulimwengu wa viumbe wasioonekana yaani Majini.
Majini hata kama yapo katika maeneo yao ya kujificha lakini pale ambapo binadamu yoyote anaejifuza mbinu za nishati ya mbingu na ardhi anapitia mapigo ya radi hugundilika kirahisi sana.
Sasa Master Chi anasema katika kipindi hicho chote aliweza kukutana na mshindani wake ambaye alikuwa akitaka mbinu ya andiko la urejesho isiokuwa na kikomo.
Anasema mara nyingi wakati alipokuwa akikumbana na huyo mtu alikuwa na Lanlan na hata kushindwa kupambana nae kisawa sawa na wakati huo huo alikuwa akificha siri ya Roma pia kujifunza mbinu yake.
Master Chi anasema kwamba adui ambaye alikuwa akimhangaisha licha ya kuwa na uwezo mkubwa lakini alikuwa akimjjia kwa sura tofauti tofauti ili tu kumchanganya , anasema kwamba mara ya mwisho kabisa adui yake aliweza kutokea katika sura ya Seventeen na jambo hilo lilizidi kumtia wasiwasi mno kwa kuhofia usalama wa Lanlan.
Anasema mara baada ya kuona hawezi kumlinda Lanlan tena ndipo alipofanya maamuzi ya kumrudisha Lanlan kwa baba yake na hapo ndipo alipoamua kuandika barua na kumkabidhi Qiang Xi pamoja na kipande cha kisu na kumwambia kwamba kama hatoweza kuonekana kwa siku ishirini na tisa basi ampeleke Lanlan kwa mwanamke ambaye Lanlan humuita mama na barua na kisu kumkabidhi mume wake.
Na anasema ndio hapo alipofanya uamuzi wa kukutana na Mama Issa mkuu wa kituo cha Son and Daughtet Orphanage na kumuacha pale Qiang Xi na Lanlan kwa muda kutokana na kwamba alhofia kuwaacha wakiishi wenyewe ndani ya Tanzania bila kujuana na mtu.
“Roma ninachokuambia huyo adui niliekutana nae ni mwanamke na uwezo wake ni wa juu zaidi , huenda zaidi ya kuipita dhiki na alikuwa akitumia maji ya kiroho ya nguvu za juu kabisa , ijapokuwa uwezo wangu ulikuwa ni wa juu katika kuipita dhiki lakini yeye alikuwa ameenda mbali sana katika mafunzo ya kijini na alionekana sio wa kawaida na ameishi miaka mingi sana kwani alionyesha kuwa na uzoefu, nadhani unaelewa kwamba licha ya nguvu za kimajini kuwa na njia tofauti fupi na ndefu lakini wote malengo yetu ni ya aina moja , inawezekana njia ndefu ni rahisi kuweza kuipita dhiki lakini kuna namna ambavyo majini hutumia Dhana na kuweza kuhimili mapigo tisa ya radi.
Mwanamke huyo hakuwahi kujjionyesha kwangu kwa sura yake halisi kwani nilikutana nae mara nyingi akiwa na sura tofauti tofauti lakini ninachoweza kujua ni kwamba msisimko wake unatoa aina flani ya mafunzo ya kijini yanayofamika kwa jina la Genji , nguvu hizo ni hatari mno na za kikatili
Baada ya kuhakikisha kwamba hata kama nikifa Lanlan anaweza kukufikia ndipo nilipojidhihirisha kwa mara nyingine kwa huyo mwanamke na tukaanza kupigana lakini niliamua kukaa mbali na ukaribu wako hivyo nilianza kumfanya anifukuze kwa kumpeleka katika maeneo mbalimbali ya eneo la China ili tu nisiweze kuamsha miungu watu na kutushambulia , siku moja usiku wakati tukiwa tunafukuzana tuliweza kupita katika kilele cha mlima wa Emei na kwa bahati mbaya niliuamsha mnara wa Demon Lock .. nadhani utakuwa unajua sasa unaitwa Tosha au Tongtian, basi ndio huo na baada ya kuuamsha nilivutwa na nguvu ya ajabu mno na haikuwa upande wangu tu hata kwa yule mwanamke na yeye alianza kuvutwa pia lakini jambo ambalo nilikuja kugundua kabla sijamezwa ni kwamba huyo mwanamke anaonekana sio binadamu pekee , kwani kabla hajamezwa palepale aliachia kifaa kama ngao isiokuwa ya kawaida ambayo ilitengeneza mlipuko wa aina yake na yeye kuachiliwa na sijui kilichotokea lakini wakati nikishindana na nguvu ya mnara niliweza kumuona akiweza kutoweka baada kuishinda nguvu ya mnara na mimi ndio nilipovutwa na kutokezea kwenye huu ulimwengu, ijapokuwa niliweza kuingia kwenye huu ulimwengu nilijitahidi kutafuta njia ya kutokea , lakini kwa bahati nzuri nikaweza kukutana na Braza Zao nje ya msitu wa mianzi zambarau na ndio hivi unavyoniona sasa”
Roma alijikuta akishgnazwa na jambo hilo , hakuamini kwani hata yeye haikuwa mara ya kwanza kukutana na adui ambaye alikuwa akitaka mbinu yake , wa kwanza ni yule wa kule China kwenye ngome ya Tang ambaye alikuwa kama kivuli na kutawala akii za wale wazee wa kichina na wa pili ni yule Abeo mwafrika ambaye alimteka Edna na kumlazimisha kutoa mbinu yake na kumuua, sasa alijiuliza huyo mwanamke ambaye hakuwa binadamu wa kawaida na mwenye kutumia ngao ni nani?.
“Nadhani sasa unaelewa kwamba sikutaka kumuona Lanlan akiteseka kwenye mikono yangu wala katika mikono yako , nadhani utakuwa na kumbukumbu niliweza kukutana na mkeo Edna na kumwambia kama atakuwa tayari kuachana na wewe ningempatia Lanlan amlee lakini alikataa , ijapokuwa mpango wangu ulikuwa wa kijinga lakini niliamini kama atatokea mwanamke ambaye angempenda Lanlan kama mtoto wake itakuwa ni kheri kwani atakuwa mbali na mimi na wewe pia , na ingempatia mazingira salama ya kuweza kukua na kuwa imara”
Roma alijikuta akianza kuona ni yeye mwenyewe ambaye alianza kupotezea mambo , kwani hata mara baada ya Edna kutaka kumlea Lanlan hakuonekana kupatwa na wazo hilo kwa upande wake , lakini Edna alilazimisha na mwisho wa siku inageuka Lanlan ni mtoto wa pacha wake , aliona ni sahihi huenda damu ya Seventeen na ya Edna ziikuwa ndani ya Lanlan ndio maana mvutano wao ulikuwa mkubwa sana kuliko yeye mwenyewe, au huenda ni kutokana na Lanlan kwa kipindi hicho kuweza kuishi na Seventeen tu bila ya kumjua yeye ndio maana aliweza kutengeneza muunganiko wa uzazi na Edna kwa haraka sana.
“Nadhani kwasa imekuwa vizuri unaelewa haya mambo , lakini bado inashangaza kwanini Qiang Xi hakufuata maagizo yangu baada ya mwezi kupita, Qiang Xi ni mwanamke wa hali ya chini ambaye niliweza kukutana nae nchini China nikiwa katika matembezi yangu na Lanlan na kutokaa na hali yake ya maisha ya chini niliamua kumfanya awe mlezi wa Lanlan , lakini inashangaza alikiuka maagizo”Aliongea huku akikunja sura na kuonyesha wasiwasi wake.
Roma alijikuta akishangaa pia kuhusu hilo na alihofia huenda QianXi ni pandikizo(Spy au shushu) na amewekwa ndani ya familia yake kwa madhumuni maalumu , alijiambia kama tu alishindwa kuweza kujua jambo hilo licha ya kuishi nae kwa muda mrefu basi atakuwa mtu wa hatari maana kama ni wa kawaida kwannini ashindwe hata kuona hata dalili tu.
Baada ya kufikirai hivyo Roma alijikuta hamu ya kutaka kutoka katika ulimwengu huo ikizidi kungezeka maradufu .
“Master kwaini mnara ukifunguka tusiondoke pamoja , vinginevyo utasubiri tena miaka sitini na kufikia kipindi hicho utakuwa umechelewa?”
Bila ya Master Chi kuweza kuongea palepale Master Zao aliweza kusikia maneno yao na kuwaingilia.
“Roma sidhani kama ni wazo zuri wewe na Braza Chi kutaka kujaribu , mapigo tisini na tisa ya radi ya rangi ya zambarau sio mchzo , sikumbuki hata ni idadi kubwa kiasi gani kwa majini yalioweza kufariki mara baada ya kujaribu , hivyo hamna tofauti yoyote na kwenu pia”
“Bila kujaribu huwezi kuelewa ,ni kheri nife kwa kupigwa na hizo radi kuliko kushindwa kujaribu “Aliongea Roma kwa kujiamini.
“Kaka muache afanye kama anachotaka na isitoshe kutokana na sheria Braza Roma ameweza kushinda na watu wa miliki ya Mbweha wa Jade ndio wanaopaswa kuingia , nadhani tumuache ajaribu kwani ndo anachotaka”Aliongea Moli
“Siwezi kumzuia Roma kama ndio anachotaka lakini kwa kaka yangu Chi siwezi kukubali kumuona akiingia na kutafuta kifo chake , nimekaa ndani ya ulimwengu huu kwa milenia moja lakini bado tu sijawahi kupata kujiamni kufanya hivyo , kwanini niruhusu kumuona afe kifo kisichokuwa na thamani?”
“Braza Zao , hata kama huwezi kunizuia siwezi kuondoka na kuingia ndani ya mnara”Aliongea
Sophia na Roma waliweza kushangazwa na maneno yake huku wakimwangalia Master Chi kwa macho yasiokuwa ya kawaida , inaonekana amemua kuishi maisha yake ndani ya ulimwengu huu
“Msishangae , hebu jaribu kufikiri ninaweza kweli kutoka hapa na kwenda huko nje lakini siwezi kuishi kwa amani kwani nnitawindwa na mwisho wa siku naweza kufa na mimi sina mahusiano yoyote , ni kheri kubakia kwenye ulimwengu huu na rafiki yangu Braza Zao na kuishi maisha ya raha mustarehe bila bughuza”Roma aliona kabisa Master Chi hakuwa akitania na maamuzi yake yake yalikuwa ya wazi.
“Master humkumbuki Lanlan na kutaka kumuona tena?”
“Lanlan ni binti yako na kama utapata bahati ya kutoka basi inatosha , maswala ya namna hio nimekuwa muwazi kwa muda mrefu”Aliongea huku akitabasamu.
Wakati ambao Roma anafikiria kumshawishi Master Chi ili wajaribu kutoka pamoja ghafla tu Roma alihisi ubaridi uliomsababishia msisimko nyuma yake.
Aoiline ambaye alikuwa kimya muda wote alianza kuonyesha mabadiliko na kujawa na nia ya kimauaji na hio ni mara baada ya kuona kitu ambacho hakikuwa sawa katika maiti zilizokuwa zikielea.







SEHEMU YA 620.
“Roma unaficha kwa siri hizi maiti za majoka si ndio?”Aliuliza Aoiline na kumfanya Roma kuwa katika hali ya mshangao.
“Haiwezekani , kuna mifupa mingi ya Majoka kwenye hifadhi yangu na imekwisha kujaa “
“Kama ni hivyo basi hizi maiti za hawa minyoo kuna kinachoendelea ndani ya hili ziwa “Aliongea huku akikunja sura na palepale nguvu ya kijini ambayo ilitoka kama kamba ya hariri iliweza kurefuka na kupepea kuingia katika maji ya Ziwa .
Lakini Ghafla kabla hariri ile haijafika katika maji ya ziwa ilikuwa ishaanza kusababisha msuguano wa nguvu wa kijini katika maji na kusababisha mawimbi.
Boom!!
Ni kama kimbunga cha maji kilichotokea mara baada ya nguvu yake ya kijini kupitia hariri ilipogusana na maji na kusababisha mzunguko mkubwa wa maji pamoja na miili ya majini yale.
Majini yote yaliokuwa hapo hakuna yalichoelewa kinachoendelea baada ya kuona Aoiline kile anachokifanya .
Wakati kila mtu akiwa katika mshangao na kutokuelewa anachojaribu kufanya Aoiline gafla tu ilipiga boriti ya shoti ya rangi ya silver kutoka chini ya ziwa .
“Puff, Puff ,Puff …”
Mishale ya shoti za rangi ya shaba ziliweza kupiga kwa kusambaa na yale majini ambayo yalikuwa yamekaa kizembe zembe yalijikuta yakipoteza maisha palepale kwani hayakuweza kukwepa ndani ya muda.
Upande wa maiti ambazo zilikuwa juu ya ziwa zikielea na zenyewe zilianza kupigwa na shoti ya aina yake na ilikuwa ni kama vile inayeyuka kwa spidi kubwa na kuanza kupotelea chini ya maji .
Wakati huo huo majini hayo yaliokuwa katika muonekano wa kutisha na yale yaliokuwa katika maumbo ya kibinadamu yalikuwa katika mshituko na ilikuwa ni ndani ya sekunde chache tu maiti ya mfalme Wuja haikuonekana tena
Aoiline alijikuta akikunja ndita na haraka sana ile kamba yake ya hariri aliikata na kuacha itokomee ziwani huku akiangalia ni adui gani ambaye anajiandaa kutoka, lakini dakika hio hio Roma na Aoiline walijikuta wakishangaa.
“Ant – matter energy ni Joseph Bikindi?”Aliongea Roma kwa mshangao.
Roma kwa haraka aliweza kugundua nani ambaye anasababisha yote hayo na alijikuta akitoa hewa ya kupumua kwa uchungu , licha ya kwamba lilikuwa swala la muda tu lakini ilionekana alikuwa ameingia kwenye mtego wa Lekcha kwa mara nyingine.
“Palace Master , kuwa makini na huyo mtu anatumia nishati ambayo sio ya kawaida na ana uwezo wa hali ya juu , ni nguvu ambayo inaweza kuyeyusha na kumeza mwili wa mtu na uwezo wake na ni ngumu sana kuiharibu”aliongea Roma akijaribu kumuonya Aoiline.
“Nilijua tu Mfalme Wuja sio mjinga , haishangazi alikuwa sio yeye Wuja ninaemfahamu mimi”Aliongea Aoiline huku akiwaza ina maana muda wote alikuwa akidanganywa.
Maneno yake yaliibua kicheko kikubwa cha Lekcha kutoka majini , ni kile kicheko cha ushindi na majigambo.
“Heheee..Mmeshachelewa kunifahamu , nguvu ya damu ya majini joka na majini anga nimeifyonza yote nyie wajinga , mnadhani mnaweza kunishinda”Baada ya sauti yake kusikika na palepale ni kama ujiuji wa madini ya silver unachemka kama Volkano kutoka Ziwani na palepale Lekcha aliweza kuonekana akiwa katika muonekano wake halisi.
Mara baada ya kumuona mtaalamu Lekcha ameweza kuchoropka chini ya maji , majini yote yalijikuta yakiwa katika hali ya presha kubwa ya hofu.
“Msuguano wa nguvu zake na msisimko umezidi ule wa Mfalme Wuja lakini sio nguvu za kijini za kawaida , ni nini kinaendelea haoa , sijawahi kuhisi msisimko wa ajabu wa namnaa hii”aliongea Master Zao kwa mshituko.
Lekcha alianza kuchunguza kila mtu aliekuwa hapo na kisha akageuzia uso wake kwa Roma huku akimwangalia kwa tabasamu la kejeli.
“Roma unaonaje awamu hii , ulianza kunikejeli kwamba ooh siwezi kuonyesha sura yangu kwasababu sijiamini na ni muoga , haya sasa awamu hii nimesimama mbele yako nikiwa katika sura halisi , lakini hebu jiangalie ulivyo dhaifu na kutia huruma, yaani umekuwa mdogo na sikuoni kama mshindani wangu tena, au bado huoni utofauti mkubwa uliopo baina yetu?”Aliongea kwa Kejeli na Roma palepale alimrudisha Sophia nyuma yake.
“Nadhani unajali sana ninavyokuona mimi kuliko unavyojiona mwenyewe , hili linaniambia kwamba bado tu hujiamini na mawazo yako ni kitumwa, nadhani ule msemo wa watu hawabadiliki ni kweli”
“Ongea vvyovyote unavyoweza , sijui hata kujiamini kwako kunatokea wapi , sio mbaya ngoja nikuache ujigambe kwa madakika kadhaa kabla sijawaua wote mliopo hapa , nitameza kila kitu na baada ya hapo na uharibu huu mnara na tuone nani anaweza kunichukulia poa kwenye huu ulimwengu “Aliongea na palepale Lekcha mwili wake ulibadilika tena na kuwa kama chuma au roboti na ndani ya sekunde chache tu alikuwa ni nishati halisi ya mchanganyiko wa nguvu ya ant matter pamoja na ile ya kijini na mwili wake ulikuwa mkubwa mno na haikuchukua muda tu alibadilika na kurudi kuwa Joka la vichwa tisa.
Kwasababu alikuwa ameweza kuvuna kila nishati iliokuwa kwenye maiti zilizokuwa ziwani alikuwa anatoa msisimko mkubwa mno kuliko Mfalme Wuja wa mwanzo.
Aoiline na Master Zao walikuwa kwenye hasira isiokuwa ya kawaida , kwanza wanaanzaje kutokuwa kwenye hasira mara baada ya kutishiwa kwamba watamezwa na mtu huyo alietokea kusikojulikana.
“Unakitafuta kifo chako mwenyewe”Aliongea Aoiline huku uso wake ukiwa wa kikauzu mno na ule urembo wake kupotea huku macho yake yakiwa sio ya kawaida na mikia yake tisa iliweza kuchipukia na kubadilika kama siraha na kuanza kumsogelea Lekcha kwa kumlenga eneo la moyo.
Master Zao mwenyewe hakutaka kusita sita na palepale alirusha kisu chake kwa spidi ambacho kilienda moja kwa moja kufyeka kichwa cha Joka lile .
Lekcha hakukwepa pigo hata la aina moja na alikubali kuyapokea mapigo kwa raha zote na mara baada ya mkia wa Aoiline kutoboa moyo wake palepale ulipona na vichwa vyake mara baada ya kukatwa katwa na vyenyewe vilirudi katika ubora wake kama vile havikuguswa.
Lakini haikuwa hivyo tu shoti zilianza kumtoka huku zikimshambulia Aoiline pamoja na Master Zao.
Lakini ilikuwa bahati nzuri kwamba walikuwa katika daraja la juu kabisa la nguvu za majini na walitumia nguvu zao kuweza kujikinga na nguvu ya ant-matter.
Lakini hali ya kutokufa ya Lekcha iliwafanya kuwa katika mshangao na kushindwa kujua namna ya kuweza kumdhibiti
“Unadhani mwili wa Mfalme wa Majoka ni sawa na wa kwangu kwamba unaweza kuutoboa utakavyo na kuuharibu , thubutuu tena ukome na hata usifikirie kama unaweza kuniua kwa staili hio , mimi ndio napaswa kuwatesa nitakavyo”Aliongea huku akicheka kama kichaa na palepale vile vichwa tisa vilivyokuwa vikiongea vilianza kupumua shoti ya Anti matter na kuanza kuwashambulia wale majini kwa spidi kali.
“Boom , Boom , Boom …!!!”
Ilikuwa ni shoti ambazo ziliruka hewani na kudonoka kama vile ni kimondo kinajiandaa kuigonga dunia na kufanya majini kuwa katika duara ambalo ni kama sehemu ya machinjio kwa kukosa pakukimbilia
Hayakuwa majini yote ambayo yaliweza kukwepa na yale ambayo yaliweza kugusana na shoti za nguvu ya ant-matter yaliweza kupatwa na uharibifu wa aina yake na kushindwa kusogea kwenda popote
Kutokana na kuanza kuyeyuka kwa ngozi zao na roho kilichosikika ni vilio na kusaga meno.
Roma palepale alimchukua Sophia na kuondoka nae karibu na eneo la hatari , huku Master Chi na yeye akifanya hivyo hivyo , ilikuwa ni bahati kwake alikuwa na vidonge ambavyo alimeza kwa haraka ili kurudisha uwezo wake katika viwango.
Master Zao na Aoiline walijikuta wakiwa katika sintofahamu ya kukosa cha kufanya kwani watu wao wengi walikuwa wameshikiliwa na nguvu ya nishati ya ant- matter ambayo ilikuwa ikiwayeyusha na kuna wale ambao walijaribu kuiondoa kwa kutumia nguvu zao lakini ilionekana walikuwa wakikosa nguvu na kuanza kuoza.
Lekcha alikuwa kama yupo kwenye sherehe kwani aliweza kufyoza nguvu zao kwa kasi ya ajabu na kuziba pale palipopungua .
“Wewe mkorofi ni mdudu gani umetuletea kwenye ulimwengu wetu?”Aliongea Aoiline akimwangalia Roma huku akiwa na wasiwasi na alikuwa ashasahau yale malingo yake sasa maana kilichokuwa mbele ni zaidi ya hatari.
Roma kwa siri alimlaani Lekcha kwani aliona anazidi kuwa kichaa .
“Unaogopa nini , fanya kumuua basi”Aliongea Roma na baada ya hapo alimchukua Sophia aliekuwa amemshikilia na kumpatia Master chi amshikilie na kumlinda na yeye alisogelea Joka la vichwa tisa kwa ajili ya kupambana nalo.
Roma palepale alianza kuongea na nafsi yake kwa kusema neno ‘Chaos Cauldron’ na kufumba na kufumbua lijitanuru linalofanana na chungu kilichopinda mdomo liliweza kuonekana hewani.
Katika hali kama hio Roma hakutaka kujiuliza mara mbili mbili athari ambazo anaweza kuzipata , mawazo yake yalikuwa ni kupambana na Lekcha na chungu hicho ndio njia pekee ambayo aliona inaweza kufanikisha hilo.
Master Zao na Master Chi wote kwa pamoja waliangalia lijichungu hilo kwa macho ya mshangao na walishangazwa na nguvu yake ya mvutano
Chungu hicho kiliweza kumeza mpaka upepo na ndani ya dakika chache tu eneo lote liligeuka na kuwa kama kimbunga na wakati huo huo kivuli cha mnyama kiliweza kuonekana kikitoa shingo yake katika chungu hicho huku kikiwa na macho ya rangi nyekundu . roho hio ya mnyama ilionekana kushindana na mwili wake kama vile inataka kutoka katika hicho chungu huku kikipanua mdomo wake na kumeza kila kilichokuwa karibu yake.
Roma aliweza kutoa nguvu zote za kijini zilizokuwa katika mwili wake na kukiendesha kile chungu kumsogelea Lekcha kichaa.
Ilikuwa ni kufumba na kufumbbua tu eneo lote la anga lilibadilika na kufunikwa na wingu kubwa na mvua ilionekana kama ivle inajiandaa kunyesha na ngurumo nzito zilianza kusikika.
Huenda ni kutokana na msisimko mkubwa wa nishati ulimsha mnara , kwani juu kabisa ya mnara kuelekea kileleni wingu lilianza kuzunguka kwa spidi ambayo haikuwa ya kawaida katika mfuno wa kimaajabu na kufanya maji yaliokuwa chini yake ne yenyewe kuvingirika , ilikua ni kama ‘singularity’ inayotokea kwani ile nishati ya pazia iliokuwa imeuzingira ule mnara kwa chini ilianza kupanda taratibu.
“Oh , jamani mnara ndio huo unataka kufunguka?”Aliongea Master Zao wa saui ya mshituko bara baada ya kuona ile ukuta wa nishati uliokuwa ukinzingira mnara unaanza kujikusanya juu ya mnara huku upande chini ukianza kuachia taratibu.
Kufunguka kwa mnara huo kulikuwa ni kwa muda mfupi tu kabla haujarudi katika hali yake ya mwanzo na kuwa kimya kwa miaka sitini tena.
Roma alianza kukosa uvumilivu mara baada ya kuona tukio hilo kwani mnara ulianza kuonekana sasa vizuri kwa macho yake kwani mwanzoni ulionekana kama umezingirwa na pazia la wingu.
Cauldron ilitaka kumeza nguvu za Ant -matter lakini ilionekana nguvu aliokuwa nayo Lekcha awamu hio haikuwa ya kawaida kwani ni kama mvutano wao ulianza kushindana
Lekcha mara baada ya kufanikiwa kushinda kani mvutano ya Cauldron palepale zilianza kumtoka shoti za mishale na kuanza kukishambulia kile chungu kwa spidi ya kasi kutataka kukibomoa.
Roma alijikuta akishagnazwa na jambo lile na palepale ilibidi akiondoe kwa haraka kwa hofu ya chungu chake kuharibika , na aliishia kuangalia Joka hilo lenye vichwa tisa kwa kutetemeka kwenye moyo wake.
“Haina maana , nishakuambia hiko chungu kingekuwa hatari kama una nguvu kubwa ya kijini lakini kwa hali yako huwezi kushindana nae”Aliongea Aoiline na sasa kwa mara ya kwanza alipandisha uwezo wake katika daraja la mwisho kabisa na kuachia nguvu yake ya kijini
Mikia yake ilianza kurefuka kwa urefu wa futi nyingi huku ikielea elea kama vile ni nyoka za angani na kuanza kushambuliana na Joka la vichwa tisa.
“Licha ya yote siwezi kukaa hapa na kusubiria kifo changu , mimi ndio nilioruhusu hili lizimwi kuendelea kuishi na kama nisipomuua leo sitoweza kutoka nikiwa na amani”Aliongea Roma.
Muda huo Lekcha alikuwa ashaaza tena mashambulizi yake huku akijaribu kumeza nguvu za majini waliokuwa katika eneo hilo na milipuko mikubwa ya nguvu za anti matter zilianza kushindana na nishati ya anga na kushuka chini kama vile ni mvua ya matone ya moto mweupe.
Na kila maiti iliokuwepo karibu iliweza kuyeyushwa na kuanza kumfanya Lekcha kuanza kufanana na anga taratiu taratibu aliaonza kutokuonekana.
Master Chi alijiaribu kumzingira Sophia na nguvu zake zote lakini alijikuta akishangaa amefikia kikomo katika kutumia uwezo wake wote na aliishia kukunja ndita.
Ijapokuwa Roma na Master Chi wote walikuwa katika levo sawa lakini miili yao ilikuwa tofauti , mwili wa Roma haukuwa kawaida hivyo alikuwa na faida kubwa lakini kwa wakati mmoja anayo dhana ya Cauldron.
Ilikuwa ni rahisi ya kusema kwamba mwanafunzi amemzidi mwalimu , kwani Roma alikuwa ni wa levo ya juu na uzoefu wake wa kimapambano ulionekana kuwa mkubwa ziadi kuliko wa kwake.
Master Zao na Aoiline walikuwa wakijitahidi kulinda majini wao lakini pia kwa wakati mmoja Aoiline alikuwa akilinda mikia yake isigusane na nishati ya ant- matter.
Lakini kwa hali ilivyokuwa ni kama Aoiline anaweza kufikia mwisho kabisa wa uwezo wake muda wowote , lakini upande wa Lekcha uwezo wake ulikuwa wa juu kabisa na alionekana kutumia kiasi kidogo tu cha nguvu zake kushambulia , hivyo ni kama alikuwa na karata za mashambulizi hajacheza bado wakati mpizani wake ndio kwanza anamaliza.
Roma palepale alitoa kidonge na kukimeza na hatakukata kusubiria nguvu zake kumrejea zote na alipanga kutumia nafasi hio ya mapambano kutafuta njjia ya kummaliza Lecha na kisha kuzama mnarani ambao tayari pazia lake lilikuwa lishaachia kwa zaidi ya floor nane kwenda juu.
“Kuwa makini”Alikemea Aoiline akimuonya Roma kama vile ashajua ni mpango gani anataka kufanya.
Roma alijikuta akimwangalia huyo mwanamke kwani licha ya kukabiliana na msikuko suko inayotolewa na Lekcha lakini alionekana kuwa na utulivu bado wa kuweza kumjali yeye.
“Usisahau kwamba mnara tayari umetoa kizuizi chake na kufungka , kuendelea kupigana na huyu mtu ni kupoteza muda na unaweza kupoteza fursa ya kuingia mnarani na kusubiri miaka sitini mingine , huyu mwanaharamu naona nia yake ni sisi kupoteza nguvu zetu ili atumeze na kupata uwezo mkubwa zaidi, huenda yeye hana tatizo la kusubiria miaka sitini mingine ya mnara kufunguka”aliongea Aoiline.
Roma aliona kabisa maneno ya Aoiline ni sahihi , hapaswi kushindana na Lekcha na umakini wake wote uwe ni kutoka ndani ya ulimwengu huo.
“Mwanzoni nilitaka baada ya kushinda mapambano tuingie mnarani pamoja huku nikikuelezea zaidi baadhi ya mambo kuhusu mimi lakini sasa hivi hali imekuwa nje ya matarajio , hivyo mchukue Sophia na uingie nae ndani ya mnara na uone kama unaweza kutoka katika huu ulimwengu”aliendelea kuongea Aoiline.
Roma alijikuta akiguswa na maneno yake , hakuamini kumbe mpango wa Aoiline ni kumsaidia yeye na Sophia kuweza kutoka katika ulimwengu huo , Roma mara baada ya kukumbuka namna ambavyo mrembo huyo alivyowasaidia hakutaka kuwa na mashaka na nia yake, isitoshe ni rahisi kufa kwa mikono yake.
Kumbuka hapa Aoliine hakuwa akiongea na Roma kwa sauti bali alikuwa akiongea nae kwa njia ya kimawazo na Roma alikuwa ni kama anasikia sauti masikioni lakini wingine hawakuwa wakisikia.
Lekcha ambaye alikuwa akipambana alijua kuna kitu kinaendelea na alitoa sauti nzito.
“Roma kwanini unakuwa kama Kobe na kuficha kichwa chako , njoo na wewe acha kujificha nyuma ya huyo mbweha”Aliongea na Roma alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira na alipaa na kumsogela Master chi
“Master najua unataka kuendelea kuishi hapa , lakini siwezi kubakia na wewe , naomba nimchukue Sophia niondoke nae”Aliongea Roma na Master Chi alionekana kutegemea hilo na alitoa tabasamu hafifu na pale pale alitoa mkufu wa rozali kama ile ya kibuza .
“Huu mkufu umetengenezwa kwa tamaduni ya nguvu ya kihindi na nilitumia kumuombea Lanlan usalama na uhai wake kwa kipindi chote na anaujua , hivyo licha ya kwamba unaharibika haraka lakini kama utaweza kutoka naomba umpatie Lanlan na ataukumbuka na naamini hataweza kunisahau mimi babu yake hata pale ambapo atakuwa mtu mzima”Aliongea kwa huzuni ya kumkumbuka mjukuu wake Lanlan na kisha akampatiia Roma baada ya kuuvua shingonni.
Mapenzi yake kwa Lanlan yalikuwa makubwa kwani alikuwa amemlea kwa muda mrefu sana hivyo ilikuwa ni ngumu sana kumsahau.
Roma palepale alichukua Rozali ile na kisha akaitupia katika hifadhi ya pete yake ya kijini na kisha alimtingishia Master Chi kichwa kwa namna ya kumuaga akiwa na muonekano usiokuwa wa kawaida na kisha akamchukua Sophia na kuondoka nae.
“Trying to escape , not so fast”Aliongea Lekcha akisema unajaribu kunikimbia sio kirahisi hivyo na palepale aligeuka kuwa binadamu na kumfukuza Roma kwa nyuma na wote kwa pamoja wakatumbikia ndani ya floor ya kwanza ya mnara huo.
Aoiline na yeye hakusita na palepale alifukuzia kwa nyuma na kuiingia ndani lakini huku akiwapa ishara Master Chi pamoja na Master Zao kutowafuata.
Unadhani Roma atafanikiwa kuchoropoka katika huo mnara, vipi Roma ataweza vipi kumlinda Sophia na mapigo tisinni na tisa ya radi.
NB:Mwanamke ambaye anamsemea Master Chi kwamba ndio alisababisha kuja kwenye ulimwengu huyo ni mwanamke ambaye aliongekana akiongea na Hermes katika kilele cha mlima nchini Tanzania
Nimewafungulia hio Code ili kuweza kuunganisha matukio yanayokuja.
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI : SINGANOJR.

Mono no aware
Ilipoishia
Tuliishia Lekcha akimfukuzia Roma na Sophia mara baada ya kuingia kwenye mnara na baada ya hapo na Aoiline akafuatia huku akiwapa ishara Master Chi na Master Zao kutokuwafuata.

SEHEMU YA 621.
Master Chi na Master Zao walijikuta wakiangaliana kwa mshangao na palepale wakajiuliza swali la aina moja , je ulikuwa ndio mpango wa Roma na Aoiiline kumfanya Lekcha kuingia kwenye mnara.
Wote kwa pamoja walikuwa wakielewa kwamba uwezo wa Aoiline ulikuwa mkubwa sana hata kwa kuunganisha uwezo wao wote wawili hivyo waliishia kutii maagizo yake na kutowafuata.
Upande wa Roma alikuwa akijihisi ni kama yupo kwenye hatari kubwa huku akiwa amemshikilia Sophia , marashi yaliokuwa yakitoka katika mwili wa mlimbwende huyo hayakuacha kuzitesa pua zake lakini hakuwa katika wakati wa kufurahia.
Lekcha spidi yake ilikuwa ni ya juu mno lakini licha ya kwamba alionekana kuwa na spidi na nguvu kubwa haikumaanisha kwamba hawezi kupata madhara.
Katika floor ya kwanza ya mnara huo hakukuwa na kitu cha kushangaza zaidi ya wingu kubwa lililotanda na ubaridi wa aina yake, walichokuwa na uwezo wa kuona ni kuta za mnara huo ambazo zilikuwa zimejengwa na malighafi za ajabu ambazo zilikuwa na weusi wa aina yake huku kukiwa na maandishi ambayo yalikuwa katika lugha ambayo ilikuwa ngumu kwa Roma kuielewa.
Ni kama Aoiline alivyoweza kusema kwani pia katikati ya eneo hilo kulikuwa na mimea ambayo ilikuwa imeota yenye kutoa maua na baadhi ya matunda , ijapokuwa Roma hakuweza kuifahamu lakini kwa haraka haraka alijua tu ilikuwa na nguvu kubwa kama itatumika katika kutengenezea vidonge , ilikuwa ni mingi sana , hivyo Roma aliamini hata kama wanaongia hapo ndani wanataka kuchukua kila kinachopatikana basi ni ngumu kufanya hivyo kwani muda wa kukaa ndani ya mnara huo ulikuwa ni wa muda mfupi sana kabla ya pazia la mnara huo halijajifunga, na kwa inavyosemekana kama likijifunga radi ya zambarau ilikuwa ikipiga mpaka katika floor ya kwanza.
Ukweli ni kwamba Roma hakuwa kabisa na muda wa kuangalia hio mimea kwasababu ya Lekcha aliekuwa akimfukuzia kwa nyuma na ilikuwa ni bahati tu kwamba spidi ya Aoiline ilikuwa ni kubwa na mikia yake tisa iliweza kumzingira Lekcha kwa mbele ili asiendelee kumsogelea Roma.
Lekcha mara baada ya kuzingirwa na mikia ya Aoiline alitoa tabasamu la kejeli na palepale kwenye mikono yake lilionekana panga kubwa kama mkuki na kabla hata Aoiline hajashitukia tayari mkia wake ulikuwa ushakatwa vipande vipande na kufanya damu nyingi kumtoka na kumwagika chini.
Aoiline alisikia maumivu makali mno huku macho yake yakiangalia kwa mshangao siraha aliokuwa ameshikilia Lekcha.
Ilikuwa ni ile siraha ambayo ilimaarishwa uwezo wake kwa kumwagiwa damu ya maelfu ya majini na kisha kukaushwa kwenye moto wa Lava.
Msisimko wa panga hilo ulimfanya kuweza kujua nini kipo ndani yake na alijikuta akishangaa kwani hakuamini kama Mfalme Wuja katika maisha yake alikuwa akitengeneza siraha ya namna hio na sio tu kwa kutumia majini wa koo zingine lakini mpaka majoka ambao walikuwa ni watu wake.
“Akajiona mjanja sana huku akidhani kwamba sijui ataniua , nilifanya makusudi kumpatia maelezo ya kumfanya anishuku ili kunifuata mwenyewe kwa ajili ya kuniadhibu ili niweze kumteka akili yake bila wengine kujua , sasa hivi siraha hii ya damu ni ya kwangu na ninakwenda kukuchinja nayo leo hii na baada ya hapo nitatengeneza tundu kubwa kwenye huu mnara na kuondoka”Aliongea.
Ilionekana Lekcha ndio aliekuwa ni Joka Mjumbe wa Barafu na kwa maneno yake ilikuwa ni mpango wake kumwambia maneno ambayo yatamfanya mfalme Wuja kumshuku , na mwisho wa siku Mfalme Wuja aliingia katika mpango wa Lekcha na kuishia kumezwa nafsi yake pamoja na sura yake.
Upande wa Aoiline alikuwa akitetemeka kwa hasira kubwa mno , mwanamke huyo alikuwa akiulinda muonekano wa mwili wake kuliko hata anavyolinda maisha yake.
Ijapokuwa alikuwa amebadilika na kuwa katika mwili wa kibindamu lakini bado urembo wake wa Mbweha wa mikia Tisa ulikuwa kwenye mifupa yake , mikia yake tisa ya manyonya ya rangi nyeupe ilikuwa ndio hadhi yake na utu wake , kitendo cha Lekcha kutumia mbinu zake za hila na kukata moja wapo ya mkia wake ilimfanya kupatwa na uchizi.
“Wewe mnyama umennichokoza mwenyewe , nninakwenda kukumaliza leo hii”Aliongea Aoiline kwa hasira kubwa mno.
Na palepale alirudisha mikia yake ndani na kumsogelea Lekcha kwa ukaribu na kuanza kupigana nae ana kwa ana.
Vidonge ambavyo alipewa na Roma viliweza kumsaidia sana katika mapambano hayo kwani mwili wake ulikuwa na nguvu ya kuweza kushindana na upanga wa kichawi uliokuwa umeshikiliwa na Lekcha ambao ulikuwa ukitoa nguvu ya kijini ambayo haikuwa ya kawaida kabisa.
Licha ya kurudishiana mapigo mazito mazito kama vile ni mabomu lakini ajabu ni kwamba hakukutokea hata mtikisiko wa aina yoyote kutoka kwa mnara huo.
Lekcha mwenyewe alijikuta akishangazwa na ugumu wa mnara huo , aliona kama ni kitu ambacho hakitowezekanakutumia kisu chake hicho kuharibu mnara huo kama ilivyokuwa mpango wa Mfalme Wuja.
Ukweli ni kwamba hakuwa na haraka kabisa ya kutoka kwenda katika ulimwengu wa kawaida , aliamini kama ataendelea kubakia katika ulimwengu huo wa majini pepo basi anao uwezo wa kuweza kunyonya kila aina ya nguvu na kufikia katika levo ya juu kabisa ya kuweza hata kuuharibu na kutoka.
“Roma unafanya nini?, mnaweza kuondoka niachieni huyu mnyama nitamuua leo hii”Aliongea Aoiline mara baada ya kumuona Roma anamwangalia akipigana na Lekcha.
Roma hakuona maneno ya Aoiline kuwa ya kimakosa , ijapokuwa aliona huruma kumuacha kupambana mwenyewe lakini alijua fika kama ataendelea kubakia hapo na Aoiline kuendelea kupungukiwa na nguvu zake basi inaweza kumpa shida kutoka ndani ya muda katika mnara huo, isitoshe Lekcha kwa wakati huo alikuwa katika mwili ambao ulikuwa ni ngumu kufa.
Roma hakupenda kuishi akiwa na deni hivyo kwa kuondoka hapo aliamini atakuwa na deni kubwa kwa Aoiline ambalo kamwe hawezi kulilipa.
Roma alijiuliza kwanini Aoiline akatumia nguvu kubwa sana ya kuwafikiria kuhusu usalama wao na hata wakati huo kupambana na Lekcha ili mradi tu waweze kufanikiwa kutoka , Roma aliwaza lakini alikosa majibu.
Upande wa Lekcha alionekana kutokuwa na wasiwasi wakati akipambana na Aoiline na aliishia alimwangalia Roma kwa tabasamu la kejeli.
“Roma unajaribu kutaka kuvuka kwenye huu mnara , huwezi hata kushindana na mimi lakini unafikiria huo upuuzi , unakitafuta kifo chako mwenyewe?”Aliongea .
Roma alijikuta akikunja ngumi yake kwa hasira kama vile alikuwa ameghairisha safari na kutaka kupigana nae lakini palepale aliita chungu chake na kisha akachukua kidonge kimoja na kukimeza kubusti uwezo wake na kisha akausogeezea mdomo wa Cauldron upande wa Lekcha.
“Unajuaje , pengine imepagwa wewe kupigwa na radi ili mimi niweze kutoka kwenye hu mnara”Aliongea Roma na palepale alitoa vidonge viwili na kisha akamwekea Sophia mdomoni ili kurudisha nguvu zake lakini kwa wakati mmoja kumfanya awe na mwili imara.
Na kabla hata ya Sophia hajajua nini mpango wa Roma tayari alishamshikilia kwa nguvu na kuruka nae.
Haikuwa kuruka kuelekea juu bali Roma na Sophia wote kwa pamoja walitumbukia katika Cauldron kana kwamba wao ndio wamenezwa.
Ukubwa wa chungu hicho ulikuwa chini ya udhibiti wa Roma mwenyewe ndio maana waliweza kukaa watu wawili ndani yake bila shida
Lekcha alijikuta akishangazwa na jambo hilo na wakati huo akiwa ameshangaa Aoiline alichukua nafasi hio na kupasua kichwa chake lakini hata hivyo ilikuwa bure kwani sekunde ile ile mwili wake ulirudi upya tena huku akishindwa kuelewa kwanini Roma na Sophia wameingia wao ndani ya chungu cha kijini lakini dakika hio hio aliweza kujua mpango wao.
Chungu kile kilianza kuelea hewani kama vile ni ungo wa kichawi na kuanza kuzunguka kwa spidi huku kikielea angani kuelekea juu zaidi ya mnara.
Roma na Sophia walikuwa wamekaa ndani ya chungu hicho katika hali ya utulivu huku wakikitumia kama ngao ya kujikinga na chochote ambacho kinaweza kuwakuta ndani ya mnara huo.
Roma licha ya kufanya maamuzi hayo lakini bado alikosa ule ujasiri wa kukaa ndani yake kwa muda mrefu.
Upande wa Aoiline yeye hakuwa katika hali ya mshangao , ukweli ni kwamba hata yeye huo ulikuwa ni mpango wake , alitaka kumwambia Roma tokea mwanzo kwamba anaweza kutoka nje ya ulimwengu huo kwa kukitumia chungu hicho kama ngao , lakini hakutaka kusema mapema kwani kama ingejulikana basi kila mtu angetaka kumshambulia na kutaka kupata nafasi ya kupata chungu hicho.
Isitoshe majini pepo hao licha ya kukukaa katika ulimwengu huo ambao ulikuwa na kila kitu , lakini ukweli ni kwamba ni kama walikuwa gerezani na hawakuwa na furaha na kila mmoja ndoto yake ni siku moja kuweza kutoka kwenda katika ulimwengu wa kawaida.
Kulingana na wazo ambalo alikuwa nalo Aoiline lakini piua maarifa yake ya kuishi miaka mingi alikuwa akielewa kwamba Cauldron ni dhana ambayo ni immortal(isiokufa) na ndio maana majini wa enzi hizo waliitumia kuwa mtego wa mnyama wa maafa ambaye alishawahi kuwepo na kuwa tishio kwa usalama wao.
Hivyo kwa mantiki hio kama chungu hicho kilikuwa na sifa ya ui ‘immortal’ ndani yake basi kisingepata tatizo kupitia mapigo tisini na tisa ya radi ya rangi ya zambarau kama Roma angekitumia katika usahihi.
Kwa wakati huo Dhana hio ilikuwa chini ya maelekezo ya Roma kwasababu ilimchagua kama Master hivyo roho iliokuwa ndani yake ndio ingekuwa ni kama ngao yake ya kumlinda na kuweza kuhimili mapigo yote tisini na tisa na hatimae kuweza kutoka katika mnara huo akiwa salama.
Zaidi ya yote ni kwamba roho ya mnyama iliokuwa ndani ya chungu hicho isingependa kuishi kwa kukamatwa na mnara huo maisha yake yote hivyo kwa namna yoyote ile lazima ingeweza kutafuta njia ya kutoka , isitoshe ni roho ambayo ilikuwa na ufahamu wake.
Tokea kuumbwa kwa mnara huo watu wote waliokuwa wamevutwa kuingia katika ulimwengu wa majini pepo ni wale ambao walikuwa ni hatari kwa dunia au mnara uliwaona kama ni hatari hivyo ni rahisi kusema ulimwengu wa majini pepo ulitumika kama gereza kwa viumbe vyote hatarishi kwa binadamu ndio maana haikuwahi kutokea anaevutwa akatoka nje na pengine Roma ni mtu wa kwanza kama angefanikiwa.
Lekcha mara baada ya kuona Caulrdon ikiambaa ambaaa kuelekea Floor ya pili ya mnara huo alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira.
“Roma wewe ni muoga , acha kunikimbia”
Lekcha alijiarib kuruka kuelekea upande wa Cauldron lakini Aoiline alikuwa nyuma yake na aliishika shingo yake kwa nguvu na kuanza kuizungusha kwa nguvu.
Lakini dakika hio hio nguvu ya ant-matter iliweza kuuruidsha mwili wake kuwa kama kawaida lakini hakuwa na muda wa kuwafukuzia Roma na Sophia tena zaidi ya kupambana.
“Unapaswa kuendelea kubakia hapa na kupigana na mimi, nitahakikisha leo hii nakuua”Aliongea Aoiline.
“Malaya mkubwa wewe”Aliongea Lekcha huku akichukia na kutoa panga lake la kichawi na kuanza kupambana nalo.
Yalikuwa ni mapigano makali sana kati ya Lekcha na Aoiline tena ndani ya mnara huo wa hatari katika floor ya kwanza
Upande mwingie katika mwanga hafifu ndani ya Caulrdon , Roma alikuwa amemkumbatia Sophia kwa nguvu huku mwii wake akiuelekezea juu huku akjitahidi kumwambia Sophia maneno ya kumuondoa woga.
“Usiwaze Sophia , nipo hapa na nitakulinda”Aliongea Roma.
Sophia kwa wakati huo alishajua mpango wa Roma ulikuwa ni nini na aliishia kutingisha kichwa chake huku akijikumbatisha kwa Roma.
“Siwezi kuogopa , nitakuwa na wewe Roma hata kama nitakufa”Aliongea na kumfanya Roma kutamani kumfinya lakini moyo wake ulikuwa mzito kutokana na kumuacha Aoiline akipambana na Lekcha peke yake.
Roma kabla hata hajafikiria nini cha kufanya aliweza kusikia ngurumo kubwa kwenye masikio yake na ghafla tu:
“BOOM!!!
Ilikuwa ni kama vile amepigwa na kitu kizito kichwani na kuhisi mwili wake unataka kumlipuka , roho yake ilikuwa ikitaka kumtoka huku nguvu zake za kijini zikianza kufurukuta kwa kiasi kikubwa.
Sophia hakuweza pia kuhimili pigo hilo la radi na aliishia kutema damu nyingi ambayo ilimchafua Roma kifuani.
Upande wa nje wa chungu hicho ni kwamba kilikuwa ndio kinapita katika floo ya kwanza kuelekea ya tatu , sasa kumbe kila floor ilikuwa ikilindwa na tabaka la radi ya rangi ya zambarau ambazo zilikuwa zimekishikilia chumba kana kwamba kuna vifaa maalumu ambavyo vilikuwa vikiwezesha jambo hilo.
Ulikuwa ndio mwanzo tu wa pigo la kwanza lakini bado hawakuwa wamepitia mapigo yote tisini na tisa lakini walikuwa kwenye hali kama hio.
Kulingana na maelezo ambayo Roma aliweza kuyapata, mnara huo ulikuwa na Floor mia moja kwenda juu na katika kila floor ilikuwa ikilindwa na tabaka moja la radi na ili tu kuweza kutoka katika ulimwengu huo inamlazimu kupanda mpaka floor ya juu kabisa swala ambalo litaweza kufanikiwa kama tu ataweza kuhimili kila pigo.
Ilikuwa afadhali alimpatia Sophia vidonge vya kijini la sivyo angekuwa katika hali ya madhara makubwa mara baada ya pigo hilo.
Kwa upande wa Roma hakuwa na jinsi licha ya hatari iliokuwepo hakuwa na namna ya kumuacha Sophia katika uliwmengu huo na kuondoka peke yake.
Sasa walikuwa ndio wanakaribia katika tabaka la pili kuelekea floor ya tatu ya mnara huo na Roma mara baada ya kusikia ngurumo ya radi hakuwa na jinsi tena na alikipa maelekezo chungu kupanua mdomo wake na kuwa mkubwa zaidi ili kuweza kumeza kila radi inayopiga na kweli palepale chungu kile kilikuwa ni kama kimefurahishwa na maagizo hayo kwani roho ya mnyama iliokuwa ndani yake ilinguruma na mara baada ya radi ile kupiga ilimezwa.
Roma alishangazwa na jambo lile, hakuamini kama Cauldron ilikuwa na uwezo wa kumeza radi , lakini hata hivyo hakikuweza kumeza yote kwa asilimia mia moja kwani kuna baadhi ya mapigo yalimfikia yeye na Sophia.
Roma furaha yake haikudumu kwa muda mrefu , aliweza kupata tumaini la kuweza kuhimili lakini kitu cha ajabu ni kwamba mara baada ya Chungu hicho kumeza radi nguvu yake iliongezeka maradufu zaidi na mpaka hapo aliona hio ni hatari kabisa.
Ilionekana dhahiri roho ya mnyama iliokuwa ndani ya chungu hicho ilikuwa ikichukulia jambo hilo kwa faida yake , ilikuwa ikitumia changamoto ya Roma kuweza kujijengea nguvu nyingi ya nishati.
Lakini licha ya hivyo sio kwamba asilimia yote ya nguvu za radi zilizokuwa zikimezwa na chungu hicho zilikuwa zikienda kwa roho ya mnyama , kuna asilimia kadhaa na zenyewe zlikuwa zikimrudia Roma lakini licha ya hivyo ilikuwa ni hatari kwani aliamini mbeleni huko angeshindwa kuwa na uhakika kama akili yake itaweza kutekwa na roho hio basi roho yake itazimwa moja kwa moja.
Katika hali kama hio Roma hakuwa na chaguo asingekuwa na uwezo wa kupambana na radi bila Cauldron kwani madhara yangemfikia Sophia.
Roma mara baada ya kungalia macho ya maumivu yaliokuwa yakitoka kwa Sophia alijikuta roho yake ikifurukuta na kujiambia katika moyo wake ataweza kukidhibiti na kukitawala chungu hicho hata mara baada ya kutoka katika mnara huo.
******
Upande wa dunia ya kawaida katika dhehebu la Shushani kulikuwepo na kambi ya muda mfupi ya wanajeshi wa vikosi vya Tanzania vya kichawi pamoja na kikosi cha kupambana na uchawi kutoka jeshi la China maarufu kama Yellow flame iron Brigade.
Maamuzi hayo yalifanyika ili kuweza kupata ishara yoyote ambayo inaweza kuonekana katika mnara huo na kuifanyia kazi.
Master Abbess Yumiao na yeye alikuwa ni moja wapo ya watu walioweka umakini katika kuangalia mnara huo.
Ilifikia hatua baadhi ya wataalamu kutoka China kutaka kuchimba kuelekea chini ardhini ili kupata kujua namna ambavyo mnara huo ulivyotengenezwa kwa miaka mingi lakini Master Abbes alikataa kabisa na kusema dhehebu lake limepewa jukumu la kulinda mnara huo hivyo haruhusu mtu yoyote kuweza kuugusa.
Ukweli ni kwamba hata yeye alikuwa na wazo hilo lakini imani yake ilikuwa ikimwambia wanaweza kweli kuuharibu mnara huo lakini mwisho wa siku wakakosa majibu ya kile wanachokitafuta hivyo wakaishia kukaa kimya na kusubiria mwisho wa matokeo.
Ilikuwa ni wakati wa asubuhi katika dhehebu hilo, Master Abbes kama kawaida alikuwa ni wa kwanza kuamka na kuendelea kujifunza mbinu mbalimbali za kimapigano kwa ajili ya kujiimarisha zaidi lakini kuvumbua zingine ambazo angeendelea kuwafundisha wanafunzi wake.
Abbess alikuwa ni mwanamke mrembo t licha ya kuitwa Master, alikuwa na muonekano wa ujana na ilisemekena Master Tang Chi na Abbess walikuwa wapenzi.
Abbess alikuwa na muonekano wa kutozeeka kutokana na kwamba alikuwa tayari katika levo ya Nafsi katika mafunzo ya kijini hivyo urembo wake ni sawa na kusema sio wa kawaida , ni kwamba tu hakuwa akijali sana kuhusu muonekano maana hata kichwa chake hakikuwa na nywele.
Alichukua mazoezi alfajiri hio ya saa kumi wakati wengine wote wakiwa katika usingizi kwa muda mrefu na mara baada ya kukaa chini kupumzika alijikuta macho yake yote yakikodolea mnara huo ambayo katika miaka yake mingi ya kuishi hakuwahi kudhania itatokea siku ya kuangalia mara kwa mara kwani ni mnara ambao wake alikuwa ameuzea na kuona hauna kitu chochote cha maajabu.
“BOOM!!”
Ghafla tu wakati akiwa anawaza kwamba haiwezekani Roma na Sophia kuonekana tena kwani muda mrefu umepita iligonga radi ya Zambarau na palepale aliweza kuona watu wakifyatuka kutoka juu ya ule mnara na kwenda kutua chini kama vifurushi.
“Sophia , Mr Roma”Ndio sauti pekee ya juu ya mshituko alioweza kuongea katika hali hio.







SEHEMU YA 622.
Master Abbess alijiona ni kama amechanganikiwa na ugonjwa wa ukichaa wa kuona picha za watu kwenye akili yake ambazo hazina uhalisia, lakini mara baada ya kushangaa kwa dakika kadhaa aliona sio kama alikuwa kwenye ndoto au alikuwa akiona watu katika akili yake.
Dakika hio akiwa katika vazi lake la Robes alikimbia kueleka upande wa Sophia ambaye alikuwa amepoteza fahamu huku bila ya kusahau kuita wengine waliokuwa usingizini.
Baada ya kumfanyia uchunguzi Sophia alijikuta akipigwa na mshituko wa aina yake baaada ya kugundua nguvu aliokuwa nayo Sophia ilikuwa kubwa mno pengine kubwa kuzidi hata ya kwake.
Alishangaa kuona Sophia alikuwa kwenye levo ya Nafsi kwa siku hizo chache ambazo alipotea , jambo hilo lilimshangaza na kumuogopesha kwa wakati mmoja na kujiuliza nini kilichomtokea mwanafunzi wake na kuwa na mafanikio ya aina hio ya haraka sana.
Alijiuliza wamewezaje kutoka katika huo mnara baada ya kupotea kwa siku nyingi na kuweza kupata mafanikio ya aina hio.
Aliijiuliza au ni Hades aliemfanyia hivyo Sophia mpaka kuweza kuwa na uwezo wa aina hio.
Master Abbess ni moja wapo ya watu waliokuwa wakimfahamu Roma , katika mafunzo yake asingeshindwa kufahamu jina lake kwani alikuwa ni mwanafunzi wa mwanaume ambaye alikuwa ni mpenzi wake yaani Master Chi.
Master Abbess mara baada ya kuona Sophia hakuwa katika hatari yoyote ya kiafya alijikuta akivuta pumzi ya ahueni na sasa alimkumbuka Roma ambaye amedondokea upande mwingine akiwa hana fahamu na mara baada ya kumsogelea alijikuta akishikwa na bumbuwazi.
Roma hakuwa amepoteza fahamu bali kwa nguvu zake na uzoefu wake Roma alionekana kuna kitu ambacho alikuwa akipambana nacho katika akili yake , kwani kuna muda hata kichwa chake kilikuwa kikitingishika kama mtu aliekuwa ndotoni.
Haikuwa hivyo tu mwili wa Roma ulionekana kutoa nguvu ya kiroho ya giza na kuuzingira mwili wake kwa kiasi kikubwa cha kumuogopesha.
Roma alidumu vile kwa dakika chache na palepale aliweza kuyafumbua macho yake , lakini ajabu ni kwamba hayakuwa macho ya kibinadamu bali macho ya mnyama ndio aliokumbana nayo Master Abbess na kujikuta akirudi nyuma.
Wakati akishindwa kujua cha kufanya akiendelea kumwangalia Roma , palepale Roma alitoa ngurumo kama ya mnyama na kisha macho yake yakajifunga kwa mara nyingine na alionekana kupoteza fahamu.
Dakika hio hio kundi la wanajeshi wa kichina na wa kiafrika waliweza kumsogela Master Abbes huku wakiwa wanapiga kelele ya mshangao na mara baada ya kuona mwanaume na mwanamke wakiwa wamelala kwenye ardhi kila mmoja alitoa macho ya mshituko huku wakigeuza macho kwenye ule mnara uliokuwa mbele yao.
“Msaidieni Mr Roma na Sophia na kuwapeleka katika vyumba vya mapumziko na kisha toeni taarifa nchini Tanzania na kuwaeleza wamerudi”aliongea Master Abbes akipotezea mshangao wao.
Wanajeshi wale hawakuwa na muda wa kushangaa na palepale waliitt maagizo na kisha waliwabeba Sophia na Roma na kuwaingiza ndani kwenye Matemple hayo ya Dhehebu la Shushani.
******
Hakuna ambaye alikuwa akijua kama Roma alikuwa kwenye mapambano ya nafsi yake pamoja na nafsi ya mnyama iliokuwa inaishi katika dhana ya kijini ya Cauldron.
Katika ulimwengu wa mawazo, roho ya mnyama kama kawaida ilikuwa imeiba sura ya Roma na awamu hio roho ilioekana kuwa na nguvu kubwa kuliko mara ya mwisho nafsi ya Roma ilivyomshuhudia.
Ilikuwa ni sahihi kusema Nafsi hio imepanda levo katika kuvuna nishati za mbingu na ardhi mara baada ya kupitia mapigo tisini na tisa ya radi ya zambarau katika mnara wa Demonic Lock..
Roma aliweza kuona mwili wake ulikuwa umetawaliwa kwa kiasi kikubwa na roho hio ya mnyama kwani nafsi yake ilionekana dhaifu kidogo huku ya mnayama ikionekana kuwa na nguvu kubwa.
“Wewe mtoto , nadhani hili hujatarajia kuliona likitokea , ijapokuwa mapigo tisini na tisa ya radi ya zambarau na bluu ni ya tofauti na radi za kawada lakini nguvu yake inaweza kugeuzwa na kuwa nishati ya mbingu na ardhi ile safi , sasa nusu ya nguvu yote ipo ndani yangu , tuone sasa kama awamu hii unaweza kunishinda”Nafsi ya mnyama iliokuwa katika sura ya Roma iliongea huku ikiangalia nafsi ya Roma kwa tabasamu la kejeli.
Upande wa Roma hakuwa na nguvu lakini alichoweza kutegemea kushinda nafsi hio ni kutegemea imani yake tu na ule utayari wa kushinda , ni kama vile ambavyo mchawi anavyopambana na mtu mwenye imani.
Wakati wakikaribia kutoka katika mnara huo wakiwa juu kabisa ya kilele Roma alikuwa amekosa nguvu kabisa ya kuweza kuhimili pigo la mwisho la radi ya awamu ya tisini na tisa hivyo katika hali ya kutaka kuyaokoa maisha yake ilibidi aruhusu chungu kuweza kumeza asilimia zaidi ya sabini ya nguvu yake.
Ukweli ni kwamba katika mazingira yale ya Radi roho ya mnyama haikuchukulia swala lile kama changamoto kwani radi kwake ni kama kirutubisho cha kurudisha nguvu yake.
Sasa katika wakati huo nafsi ya mnyama ilikuwa katika nguvu za juu sana kwa kuweza kupata faisa ya kupitia mapigo tisini na tisa ya radi.
Roma alijua kwamba kama atakipa nafasi moja tu chungu hicho basi ingekuwa ndio mwisho wake na nafsi yake ingemezwa na roho hio na kutawaliwa moja kwa moja.
“Nini kijana … bado tu unataka kujidhibiti .. nipe mwili wako huu wa kibinadamu uweze kuonja utukufu wa milele”Nafsi ya Cauldron iliongea huku ikitoa tabasamu la kishetani.
“Pumbavu zako wewe utabakia kuwa myama uliefungiwa ambaye unajaribu kutaka kumzidi Master wako badala ya kuendelea kuwa mtumwa wangu milele, Ni kichekesho cha aina yake kutaka kujikweza zidi yangu”Nafsi ya Roma iliongea huku ikitoa tabasamu la kejeli lakini maneno yake yalionekana kuamsha hasira ya nafsi ya myama na ikaanza kucheka kwa hasira.
“Sawa.. sasa hivi unajiona mjanja kijana baada ya kurudi katika huu ulimwengu si ndio , ngoja tuone utaendelea kudumu kwa muda gani , nikuambie tu kama utajaribu kutumia nguvu zako za kijini kwa namna yoyote ile nitakufanya uwe kichaa na huo ndio wakati ambao nitautumia mwili wako , kama huamini jaribu kufanya hivyo tuone nini kitakachokutokea . Hehe … najua kuna watu ambao wanakuwinda na kutaka kuinywa damu yako , kama una akili ni kheri uniachie ni utawale mwili wako kwa adabu kabisa na nitahakikisha hamna ambaye anaweza kukugusa”
Roma alijua kabisa anaongea ukweli,roho hio ya mnyama ilikuwa imepata jeraha na tokea aanze kuitawala ilikuwa ikitumia nafasi hio kuponya jeraha lake na muda wowote ambao atatumia nguvu zake za kijini basi roho hio itaweza kutawala uwezo wake na anaweza kugeuka kichaa.
Roma aliekuwa katika nafsi alianza kujutia kukitumia chungu hicho tokea mwanzo kule katika fukwe za Australia vinginevyo asingekuwa katika hali kama hio.
Lakini tena bila chungu hicho pengine muda huo angekuwa mfu tayari kwani kilimsaidia katika mambo mengi.
Mnyama huyo alionekana kuridhika kabisa na nguvu zake na alikuwa akisubiria Roma kwa hiari yake kumpatia mwili ili aweze kuutawala, hivyo hakutaka kushindana nae ilihali tayari kuna mtego amemuwekea Roma kwenye nguvu zake za kijini na palepale iliamua kumwachia Roma utambuzi wake wa kifikra na Roma na yeye akarudisha uwezo wake wa kimawazo na fahamu na pale kwa namna ya taratibu aliweza kufumbua macho yake na kuvuta hewa safi na sura ya kwanza kuweza kuiona ilikuwa ni ya Sophia ambayo ilionekana ilikuwa ikisubiria kuamka kwake kwa hamu zote.
“Sophia…”Roma alijikuta akishindwa kujiuzuia na kutoa kicheko cha furaha mara baada ya kuona Sophia hakuwa katika hali yoyte ya hatari.
Aliamka taratibu na kukaa kitako huku akianza kuangaza mazingira ya chumba hicho lakini si palepale akajaribu kutumia uwezo wa kijinni kujaribu kukagua mazingira ya eneo alipo lakini ilikuwa ni kitendo ambacho kilimfanya akili yake kuanza kufyonzwa na nguvu ya ajabu na kama sio uwezo wake wa nguvu ya andiko la urejesho basi angepoteza tena fahamu kwa mara nyingine na pengine angeamka akiwa mwingine.
Roma mara baada ya kushinda jaribio hilo kijasho cha ubaridi kilimtoka katika paji la uso wake .
“Roma upo sawa? , unaonekana haupo sawa ghafla tu”Sophia aliongea huku akihoji.
Roma hakuthubutu kumwambia Sophia kile ambacho kilikuwa kikiendelea , kwani ni dakika hio hio ambayo nafsi ya mnyama ilitaka kuimeza akili yake.
Sasa hapa ndio ujue kutofautisha utofauti wa majini wazuri na wale wabaya , majini wabaya ni kama hicho ambacho Roma anapitia, kama Roma angefaka kuwa mtu mbaya basi angeruhusu roho ya kipepo ambayo ndio hio nafsi ya mnyama kuutawala mwili wake ili kuweza kuwa na nguvu lakini kwasababu hakuwa akitaka hilo litokee ndio maana alikuwa akishindana nayo.
Sasa majini wazuri wanajifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi ili kuishinda ile laana ya kipepo iliopo ndani yao na wale wabaya wanaipa nguvu ile laana iliokuwa ndani yao ili waweze kuwa na nguvu kubwa zaidi na kutokana na hilo wakaamua kufungiwa katika ulimwengu wa majini pepo.
Upande wa Roma katika hali kama hio aliamini kitu pekee ambacho anaweza kutumia katika kupambana ni kujaribu kujifunza kanuni za anga na kuzielewa , ijapokuwa alikuwa na uelewa mdogo lakini aliamini kama atatumia muda mwingi kuzielewa basi ingeweza kumsaidia kupambana na maadui zake ambao wangejitokeza katika kipindi hicho ambacho asingeweza kutumia nguvu za kijini.
Katika kipindi kama hicho kutumia nguvu za kijini ilikuwa ni zaidi ya hatari kwani kuna mtego wa nafsi ya mnyama iliokuwa ndani yake.
Katika maisha yake Roma aliweza kupitia changamoto nyingi na hata hio ambayo alikuwa akipitia muda huo alijiambia kwamba angeweza kupata njia ya kuishinda na kuweza kurudi katika hali yake ya kawaida , alikuwa na imani kwama kila tatizo lina njia yake.
Roma mara baada ya kutoka katika dimbwi la mawazo hatimae aliweza kumuuliza Sophia nini kilichotokea na hapo wapo wapi.
Kwa maelezo ya Sophia ni kwamba Roma alikaa katika hali ya kupoteza fahamu kwa siku mbili tokea watoke katika ulimwengu wa kijini pepo.
Ijapokuwa wataalamu wa kijeshi walishauri Roma kupewa matibabu ya nje lakini Master Abbess alikataa na kuwaonya kwamba hakuna namna ambayo wanaweza kumsaidia Roma bali yeye mwenyewe ndio anaehitajika kupambana mpaka kurudi katika hali yake.
Alishaona nguvu ya giza iliokuwa ikitawala mwili wa Roma , nguvu ambayo ilikuwa kubwa zaidi kwa mtu yoyote kuweza kuishinda ndio maana akazuia aendelee kubakia hapo mpaka atakaporejewa na fahamu.
“Roma huu ni mwezi wa kumi tarehe kumi na nne , inaonekana muda wa ulimwengu ule na huu unalandana”Aliongea Sophia na Roma hakushangaa sana.
“Umemuambia Master wako kilichotokea katika ulimwengu wa majini pepo?”
“Ndio ameniuliza na sikuwa na namna ya kumficha, si haina tatizo si ndio?”
Roma alijua maarifa ya Sophia hayakuwa makubwa kuliko ya kwake hivyo aliishia kumpa ishara ya kupunguza hofu na wasiwasi.
Upande wa vikosi vya kichawi kutoka Tanzania na China waliishia kurekodi maelezo ya Sophia na kuyafanya kuwa ya siri kwani maelezo yake yalikuwa ni ya kufikirika sana ambayo hata wao wenyewe walishindwa kuyaamini.
Baada ya Roma kuamka na kuonana na Master Abbess na kufanya maongezi kwa ufupi hatimae Roma alitolewa katika milima ya Shushani kwa kutumia helicopter kuelekea mji mkuu wa taifa hilo wa Beijing akiwa na Sophia kwa ajili ya kuanza safari ya kurudi nchini Tanzania.
Sophia hakuwa na haja tena ya kukaa katika Dhehebu la Shushani kwani alichokifuata alishakipata katika ulimwengu mwingine na sasa alikuwa na furaha kwani alikuwa katika levo ya juu ya mafunzo ya kijini tena akiwa na mbinu tofauti kuliko wengine wote kwa kuweza kurithi uwezo wa Mbweha wa mikia tisa lakini pia alikuwa ni mpenzi wa Roma.
Roma kwa upande wake moyo wake haukuacha kumuwazia Aoiline katika ulimwengu wa majini pepo , licha ya kuwa na wasiwasi alijiambia Aoiline lazima alikuwa na mpango wake kichwani wakati anamruhusu kuondoka hivyo ana uhakika Lekcha atakuwa amedhibitiwa , licha ya kutokuwa na uhakika aliamua kufikiria upande chanya na kuachana upande hasi, lakini kwa wakati mmoja akimshukuru kwa yote ambayo amemfanyia.
Angalau sasa inaonekana Lekcha ambaye alikuwa ni hatari hakuweza kutoka na yeye kurudi katika ulimwengu wa kawaida , hii ilikuwa ni taarifa nzuri kwani hakutakuwa na usumbufu tena.
Taarifa zilikuwa zimekwisha kutolewa nchini Tanzania tokea kurudi kwa Roma na Sophia hivyo mara baada ya kufika Airport ya Beijing aliweza kukutana na Kassimu mpenzi wake Donyi aliefika kwa ajili ya kumrudisha Tanzania kwa ndege binafsi iliotolewa na raisi Senga.
Roma na Sohia sasa waliweza kubadili mavazi mara baada ya kuingia hotelini na kujisafisha , kwani mavazi waliokuwa nayo ni yale waliopewa na Aoiline katika ulimwengu wa majini pepo kiasi cha kufanya watu wa dunia kuwashangaa kwa mtindo wao wa kizamani.
Wakati Roma akipanda ndege upande wa Sophia yeye alipokelewa na wazazi wake na kutaka kurejea nae kwenda Japani kwa muda kabla hajaanza safari ya kwenda Tanzania , hivyo Roma aliondoka peke yake.
******
Upande wa Tanzania taarifa za kurudi kwa Roma zilipokelewa kwa shangwe zote na hazikumfikia Afande Kweka tu bali ndugu wote wa karibu waliweza kupatiwa taarifa hizo na kusafiri mpaka Iringa kumpokea pamoja na kujjionea wenyewe kama kweli karudi.
Raisi Senga ambaye ashapoteza mtoto tayari wa kiume alietarajia kuwa mrithi wake alijikuta hata yeye akijawa na shauku ya kurudi kwa Roma kwani ndio mtoto pekee wa kiume aliebakia ambaye ni kama tumaini la ukoo wake na kila kitu ambacho angeacha hapa duniani kukiendeleza.
Raisi Senga akiongozana na rafiki yake Raisi Jeremy waliweza kufika Iringa kwa ajili ya kumpokea Roma.
Raisi Jeremy kutokana na kukosa nafasi ya kushiriki katika maombolezo ya kifo cha Denisi alitumia nafasi hio kama kisingizio cha kuja Tanzania mkoani Iringa , lakini ukweli ni kwamba yeye pamoja na Master 4 walikuwa na shauku ya kumuona Roma kwani za ndani kabisa zinasema alikuwa kwenye hali ya kupoteza fahamu kwa siku mbili mfululizo.
Hivyo hawakutaka kuambiwa alipotokea bali walitaka kushuhudia wao wenyewe.
Roma akiwa kwenye ndege aliweza kupewa kila kilichokuwa kinaendelea Iringa na Kassimu aliefika China kumsindikiza.
Wakati huo akiwa kwenye ndege kama kawaida alionyesha utulivu wake , ni kama vile amerudi katika ufalme wake maana huko alikotoka mtawala alikuwa ni Aoiline hivyo maisha ya kule na huku yalikuwa ya tofauti sana.
Ijapokuwa katika ulimwengu huu kuna mbabe wake Athena lakini bado hakumhofia na kuamini siku moja tu atampiga mwanamke huyo kipigo cha juu mpaka aombe msamaha na baada ya hapo hakutokuwa na mwingine duniani ambaye ataweza kumzidi kimapambano..
Alikuwa amevalia suti ya rangi nyeusi kama mwana usalama huku akiwa na miwnai ya jua na mkononi akiwa ameshikilia pakiti ya sigara alioweza kupewa kama zawadi na bwana Cai Yuncheng , Kamanda mkuu wa kikosi cha wachawi kutoka China.
Wakati Raisi Senga akiwa na hisia mchanganyiko za kusubiria ujio wa Roma , upande wa Afande Kweka yeye alikuwa sasa ameacha ile hali yake ya wasiwasi na kwa mara ya kwanza kutoa tabasamu la kizee.
Na siku hio katika familia hio ni kama kulikuwa na sherehe ya kumkaribisha mwana mpotevu kwani ng’ombe dume mkubwa alichinjwa na vyakula mbalimbali viliandaliwa.
Upande wa Edna na yeye alikuja kupewa taarifa siku ya pili baada ya Roma kuanza safari ya kurejea nchini, walifanya hivyo ili kutomfanya kuwa na mawazo.
Sasa Edna wakati akipatiwa taarifa ya kurejea kwa Roma alikuwa akimuogesha Lanlan na kidogo tu atumbukie kwenye Bathtub kwa mshituko.
Edna akawa ndio mtu ambaye alikuwa na shauku kubwa sana ya kumsubiria Roma kurudi na kumuona tena , alikuwa amemkumbuka mume wake , ijapokuwa hakuwa mkamilifu katika mambo mengi lakini alifurahi alikuwa kwenye maisha yake na kumpokea alivyo , hivyo kurudi kwake ni taarifa ambazo zilirudisha furaha yake kwa mara nyingine.
Taarifa haikutolewa kwa Edna tu bali kwa Neema Luwazo na Nasra walipewa taarifa hio ili kuwaondolea wasiwasi.





SEHEMU YA 623,
Safari nzima Kassimu alijitahidi kumuuliza Roma juu ya kile kilichotokea na alikuwa wapi lakini Roma hakumueleza kwa kuona kwamba kijana huyo mdogo asingeweza kumuelewa.
Roma mara baada ya kushuka katika uwanja wa ndege wa Songwe moja kwa moja walisafiri kwa chopa mpaka Iringa mjini na kisha wakachukua gari iliowapeleka mpaka nyumbani na mara baada ya kufika nje ya geti aliweza kushuhudia magari ya aina nyingi ya kifahaari ambayo yalikuwa yameegeshwa ikiashiria ugeni uliokuwa huko ndani ulikuwa mkubwa.
“Bro naona watu wengi wanasubiria kwa hamu ujio wako”Aliongea Kassimu na Roma alitingicha kichwa na kisha akajiangalia kwenye kioo kwenye gari la pembeni kama muonekano wake upo vizuri na kisha akatoa sigara moja kwenye pakti aliokuwa nayo na kisha akaiwahsa na kuvuta moshi.
Kwa mwonekano wake ni kama vile ni Gangstar flani hivi ambaye ndio sasa anarudi nyumbani.
Upande wa ndani, Afande Kweka alikuwa ameketi kwenye sofa katika sebule kubwa ndani ya jumba hilo huku akiwa ameshikilia kikombe cha chai.
Edna alikuwa amekaa pembeni ya Blandina upande wa kushoto akiwa ameshikilia Lanlan huku baadhi ya wageni na wana ukoo wakiwa wameketi kila mmoja kwenye siti yake.
Raisi Jeremy kutoka Rwanda pia alikuwepo akiwa chini ya ulinzi wa Master 4 ambaye muonekano wake ulikuwa umebadilika kwa asilimia kubwa , hakuwa tena ni yule wa kuvalia mavazi yasiokuwa ya kawaida , hapo ndani alikuwa amepiga suti huku akiwa na muonekano wa kisomali uliompatia utanashati wa hali ya juu.
Roma licha ya kuoga na kubadilisha mavazi hakuwa amebadilika sana na hata mara baada ya kuingia eneo la sebuleni nywele zake zilikuwa zimejikunja kunja na hakuwa amezichana kabisa.
“Haha.. naona mpo watu wengi mliokuwa mkinisubiri kwa hamu.. nakuona waziri Wambe pale .. Afande Tozo pia upo”Aliongea Roma huku akiweka tabasamu la bashasha akiongea bila aibu na kuvua miwani yake na kuanza kumpa mkono kila aliekuwa karibu yake.
Watu waliokuwa hapo ndani walikuwa hata wakiogopa kupeana nae mkono kwani walimuogopa lakini licha ya hivyo kila aliepewa mkono aliupokea kwa kutetemeka wakikosa ujasiri wa kwenda kinyume na Roma maana walikuwa wakimjua vizuri na nguvu yake pamoja na wepesi wa kutoa adhabu.
Roma mara baada ya kumfikia Raisi Jeremy macho yake kwanza aliyahamisha kwa Master 4 ambaye alikuwa nyuma yake kama bodigadi , ijapokuwa Roma alimuona bwana huyo kuwa na uwezo wa juu wa kimapigano lakini alijiambbia kama ataingia nae katika ugomvi basi itakuwa ngumu kupambana nae maana yeye asingeweza kutumia nguvu za kijini.
Lakini upande wa Roma licha ya kuwa na kitu kinachoendelea lakini alijitahidi kadri awezavyo kuonekana hana wasiwasi wa aina yoyote na ni yule yule wa jana na leo.
Upande wa Master 4 alikuwa hapo kwa ajili tu ya kumuona Roma alivyo na wapi ametokea na je uwezo wake ulikuwa umeongezeka zaidi na zaidi maana alikuwa ni mtu maarufu sana katika ulimwengu wao wa majini.
Ni dakika hio hio Master 4 alijikuta akipatwa na hisia tofauti kutoka ka Roma ,ilionekana nguvu zake zilikuwa zimebadilika kuliko alivyokuwa mwanzo.
Hakuwa na uwezo wa kuona Roma alikuwa kwenye levo ya ngapi, wala hakuweza kuhisi kama Roma alikuwa na mtego kwenye nguvu zake, bali alichoweza kuhisi ni kama kuna kiwingu cheusi ambacho kimezishikilia nguvu zake.
Alishindwa kzuia shauku yake na kisha akatumia ujini wake kujaribu kumchunguza Roma lakini dakika hio ambayo alitaka kujua uwwezo wa Roma alijihisi ukichaa ukitaka kuitawala akili yake , ilikuwa ni kama kuna nguvu ya ajabu ilimwingia na kutaka kumfanyia uharibifu kwenye roho yake na kumezwa.
Shukrani kwa mbinu zake na uzoefu aliweza kujitoa haraka haraka na kujirudisha katika halli ya kawaida huku jasho jembaba likianza kumtoka na alionyesha hofu ya aina yake.
Alijitahidi kuficha hofu yake na kumwangalia Roma kwa tabasamu bandia. Huku akijiuliza kwanini huyu mtoto alikuwa akitisha na kuwa na madhara makubwa kwake?
Ilikuwa wazi kwamba uwezo wake ulikuwa umeongezeka kwa kiasi kikubwa lakini cha ajabu ni kwamba umejificha ndani kabisa kiasi cha kufanya wengine kuwapa shauku ya kutaka kuutafuta lakini mwisho wa siku wale wanaojaribu walijikuta wakipambana na kitu kisichokuwa cha kawaida.
Alijiuliza ni matukio gani ya kushangaza alikutana nayo huko alikoenda , ni ufunuo gani ambao amepata na ni kwa namna gani uwezo wake umeongezeka nguvu kwa namna hio kwa siku chache alizopotea.
Alijiambia kama ataendelea kuwa na nguvu kwa namna hio basi anaweza kuamini wale ‘Super Masters’ kutoka katika ulimwengu wao ambao ni maarufu kwa zaidi ya karne na karne basi wanaweza wakapata shida ya kupambana na Roma.
Alimwangalia Roma huku akiogopa na kujiambia anapaswa kukaa nae mbali maana alikuwa akiogopesha na yeye alikuwa akiyataka maisha yake.
Roma hakutumia nguvu zake kwa wakati huo lakini haikumaanisha kwamba uwezo wake hana , alikuwa na uwezo wa kuutumia lakini alihofia akifanya hivyo nafsi ya mnyama ingeweza kumtawala moja kwa moja na kugeuka kuwa kichaa.
Kuhusu uwezo wake , ukweli ni kwamba ulikuwa umeongezeka kwa kiasi kikubwa sana tofauti na alivyoondoka , hata yeye mwenyewe hakuelewa kama kupita kwenye ule mnara kumempeleka mbali sana zaidi ya mara mia moja katika kuwa na nguvu za kijini jambo ambalo hakuna jini ambalo linaweza kupata bahati ya namna hio.
Ni sawa na kusema uwezo wa Roma sasa ulikuwa umebakisha mapigo ya radi ya aina moja tu na kufikia levo ambayo Aoiline alikuwa akimwambia kwamba inaweza kumkutanisha na yule mtu.
“President Jeremy , I am so flattered with your presence here”Aliongea Roma kwa kingereza mara baada ya kupeana mkono na Raisi Jeremy.
“Hehe.. Bila shaka , wewe ni mume wa binti yangu Edna hivyo nilipaswa kuwepo”Aliongea huku akigeuzia macho yake kwa Edna huku ikishindwa kujulikana alifanya makusudi kuongea hivyo au ni kutokana na ukweli kwamba alikuwa baba kwa Edna.
Roma alimlaani bwana huyo kimoyo moyo kwa hila zake za maneno mbele ya Edna, lakini hata hivyo aliachana nae na kisha kumalizia kusalimiana na Afande Kweka na baba yake.
“Mzee nilikuwa nimekamatika kwenye matatizo , je kila kitu kinaenda sawa hapa nyumbani?”
“Kila kitu kipo sawa na angalau hujachelewa kurudi, unapaswa kutoa shukrani pia kwa kila mtu aliefika hapa kwani uwepo wao ni kuonyesha ni kwa namna gani wanakujali”Aliongea na kumfanya Roma awaze na kujiambia haikuwa na haja kwa wao kuja kumpokea kwani hana mpango wa kuwajali hata kama wao walionyesha kumjali.
Baada ya kuambiwa hivyo ilibidi kwanza ageuke na kuwakaribisha kwa kuwaambia wabakie kwa ajili ya chakula cha mchana kwa anaetaka.
Ukweli ni kwamba watu hao sio kama walikuwa wakimjali wala nini , ila walifika hapo ili kuangalia kama huyo mwanaharamu ameumia popote mpaka kumpelekea kupoteza fahamu siku mbili lakini matokeo yake ni kwamba yaliwasikitisha sana baada ya kuona alikuwa salama tena yule yule mwenye majigambo na waliishia kusonya kimoyo moyo maana ukweli ni kwamba hawakuwa wakipenda kutokana na hulka zake.
Hilo lilidhihirika kwani kila mmoja alianza kuweka sababu yake binafsi na kusema kwamba ana dharula na hawezi kujumuika chakula cha mchana na kisha wakaaga na kuondoka mmoja mmoja mpaka wakaisha.
Roma mara baada ya kuona watu hao kila mmoja ameondoka ilibidi sasa amsogelee Afande Kweka ambaye na yeye alikuwa nje akiagana na wageni.
“Mzee naomba unisamehe kwa kuchelewa , nilikuwa mahali ambapo nimeshindwa kujisaidia”
“Haina shida , Afande Tobwe alishaniambia kilichotokea na naelewa , unaweza kurudi ndani kwanza hujasalimiana na binti yako Lanlan”Aliongea.
Roma sasa mara baada ya kusikia jina la Lanlan maneno ya Master chi yalijirudia rudia na alijikuta akiingia ndani kwa haraka na alijikuta sasa akimwangalia Lanlan vizuri kwanzia chini mpaka juu.
Ilikuwa ni kama vile Lanlan alikuwa mpya kwake na hisia za ajabu zilianza kuvaa moyo wake.
Baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzitoa alitembea mpaka alipo mke wake na kisha alimuonyesha ishara ya kumpatia Lanlan.
“Mlete nimkumbatie”Aliongea Roma kwa sauti ya kitetemeshi.
Kwa hali isiokuwa ya kawaida Edna alijikuta akihisi hisia za ajabu kama vile ni za wivu , ni hisia ambazo hakuwa akizielewa .
Alijiambia yaani mtu ndio kwanza anarudi lakini mtu anemuwazia muda wote alikuwa ni Lanlan , alitamani kabla ya Lanlan yeye ndio awe wa kwanza.
Aliona kabisa ni dhahiri kwa zaidi ya mwezi ya mwanaume huyo kuondoka mtu aliemmisi sana ni Lanlan, lakini licha ya hivyo hakuongea neno zaidi ya kutingisha kichwa kimya kimya na kumsogeza Lanlan mbele ya Roma.
Roma alijikuta akitoa tabasamu mara baada ya kumpakata Lanlan aliekuwa mzito kwenye mikono yake ,tofauti na alivyoondoka aliona Lanlan ameongezeka mwili kidogo pengine ni kutoakna na nyama zilizokuwa zikipikwa mara kwa mara ndani ya familia hio.
Alishindwa hata kujielewa ni wakati gani imetokea lakini macho yake yalikuwa yashabadilika rangi na kuwa mekundu kama mtu ambaye anataka kulia.
Roma alishikwa na hatia ya aina yake na kujiambia kwanini alishindwa kumjua Lanlan ni binti yake , muonekano wa Lanlan ulikuwa ukifanana na kila kitu na wa Seventeen alivyokuwa mdogo lakini bado tu alishindwa kuliona hilo.
“Daddy are you crying . do you miss Lanlan?”Lanlan aliuliza mara baada ya kumuona Roma akitoa machozi ya kiume.
“Well , yeah , daddy missed Lanlan so much..”Aliongea Roma huku akijibaraguza na kufuta machozi yake.
“I missed daddy too , but I am hungry”Aliongea Lanlan na kumfanya Roma kutoa cheko.
Ilikuwa ikileta maana, ilikua ni mchana tayari wa saa saba kwenda nae wakati Roma anaingia ndani ya familia hio na Lanlan bado hajakula chochote.
Sasa wakati huo kila mtu alikuwa akishangazwa na mabadiliko ya Roma kwa Lanlan lakini kwa wakati mmoja ikimfanya Edna kuchanganyikiwa na kuwa na wasiwasi.
Baada ya kufika kwenye ukumbi wa chakula ndio sasa muda ambao Blandina alijikuta akivuta pumzi na kuchukua nafasi hio kumwangalia mtoto wake kwa ukaribu maana muda wote alikuwa akijaribu kuhudumia wageni kwa kadri awezavyo.
Wanafamilia hao baada ya nusu saa mbeleni waliweza kukaa wote mezani , kutokana na kilichomtokea Roma kufanywa siri Afande Kweka hakuuliza chochote huku upande wa Raisi Senga na yeye hakuongea chochote zaidi kuwa na mwonekano ambao hisia zake hazikueleweka.
Roma aliekuwa ameketi kwenye kiti pembenni ya Edna alijikuta sasa akimgeukia na kumwangalia mke wake na kwa haraka haraka aliweza kuona Edna amekasirika.
Roma alikuwa amejisahau kutokana na ile shauku ya kutaka kumona Lanlan mtoto wake alieachiwa na Seventeen hivyo akasahau kumpa ‘attention’ Edna.
Edna alikuwa ni kweli amekasirika , siku hio alikwua amevalia kikawaida sana , pengine ni kutotaka kufanya watu kumwangalia sana , alikua na mwonekano wa kimama zaidi tofauti na wa kisichana lakini alionekana mrembo kwenye mavazi hayo mepesi.
Vazi hilo alilovaa alilichagua kwa muda mrefu na alilivaa maalumu kwa ajili ya kumpokea mume wake lakini ajabu na alivyotegemea mume wake mara baada ya kuja hakumwangalia hata mara moja na macho yake yote yalikuwa kwa Lanlan na kumsahau yeye.
“Babe Edna naona unazidi kupendeza na kuwa mrembo siku hadi hadi siku , kidogo tu nishindwe kukutambai , je ulinimisi katika siku zote ambazo hatujaonana?”Aliongea Roma kama kawaida yake akiwa amepamba uso wake na tabasamu.







SEHEMU YA 624.
Roma licha ya kujishobokesha kwa Edna hakupewa jibu alilotarajia kwani Edna alijiweka bize na kumsogezea Lanlan Mboga za majani.
“Lanlan acha kula tu nyama muda wote , kula na mboga za majani”Aliongea na kumfanya Lanlan aliekuwa na mafuta mafuta mdomoni kumwangalia mama yake na uso usiokuwa na furaha maana hakuwa akipenda mboga za majani lakini aliishia kuchukua mboga zile zote na kuzipeleka mdomoni na kuzila zote kwa awamu moja na kisha alirejea kwenye utukufu wake wa kula nyama.
Edna aliishia kumshika shavu na kumwambia apunguze spidi ya kula na baada ya hapo aligeukia sahani yake na kuwa bize na chakula akimpotezea Roma.
Roma mara baada ya kuona mwanamke huyo hakuonyesha dalili ya kutaka kuongea nae na alikuwa amenuna alijikuta akila kivivu chakula chake huku akiwaza namna ya kuweza kumrudisha katika hali ya kawaida maana alishajua ni kosa gani alifanya.
Ukweli ni kwamba mzigo wa kisaikolojia aliokuwa nao Roma kwa wakati huo ulikuwa mkubwa mno kwani swala la Lanlan asingeendelea kulibakisha siri kwa muda mrefu.
Isitoshe Seventeen hakuwa mwanamke wa kawaida kwa Roma na Edna hakupenda hata kusikia jina lake kwani alijua fika ni mwanamke wa kwanza kupendwa na Roma na hata mwanzo waliweza kuingia katika migogoro mara baada ya Edna kuona ni kama anafanywa mbadala.
Sasa kama Edna atakuja kujua kama Lanlan mtoto aliekuwa akimpenda kwa moyo wake wote na kuamua kumuasili alikuwa ni binti wa Ex wake hakujua Edna angelichukulia vipi swala hilo.
Kuwaza jambo hilo ilimfanya Roma kuwa na moyo mzito na kutaka kadri awezavyo kumfanya Edna awe ni mwenye furaha , isitoshe ni yeye ambaye alihusika katika kumleta Lanlan katika maisha yake na mwisho wa siku anajua ni binti yake.
Baada ya chakula cha mchana , Blandina alimwambia Edna kumsindikiza Roma kwenda chumbani ili aweze kuoga na kupumzika, ijapkuwa Roma alikuwa vilevile lakini kwa Blandina alisema eti Roma amekonda na anapaswa kutendewa vizuri ili kurudisha afya yake jambo ambalo liliwashangaza watu lakini hakuna aliehoji hata hivyo ni mapenzi ya mama kwenda kwa mtoto.
Lanlan alijikuta akisinzia mara tu baada ya kula chakula cha kutosha na Blandina alimchukua na kwenda kupumzika nae.
Ukweli ni kwamba watu wote waijua Edna kakasirika kutokana na matendo ya Roma kujifanya kutokumuona mara baada ya kufika ndio maana walitaka kuwapa muda wa kuyasuruhisha mambo yao wakiwa chumbani.
Edna ndio aliekuwa ametangulia na mara baada ya Roma kuingia katika chumba chake alifunga mlango kwa funguo kabisa na kisha akamkumbatia Edna kwa nyuma huku akishika kiuno chake , Edna hakuleta ukinzani na kumfanya Roma kugeuka na kumwangalia usoni.
Walijikuta wote kwa pamoja wakiangaliana kwa dakika kiasi cha kufanya pumzi zao kuweza kusikika kwa kila mmoja
Roma alijikuta akishindwa kuvumilia na palepale alimeza mate mengi na kumsogezea Edna mdomo kwa ajili ya kutaka busu huku akishika shingo yake .
Upande wa Edna licha ya kwamba alitaka kufanya kitendo hicho kutokana na kukimisi lakini bado hakuonyesha ile hali ya kuridhika na aliishia kumwangalia tu Roma akihangaika lakini kwa wakati mmoja alionekana kushindana na hisia zake kwani alihisi msisimko.
Roma alijiambia kitu pekee cha kurudisha hali ya Edna ni kumfanyia vitendo vya kimapenzi kuliko kukaa chini na kuongea.
Alipitisha mkono wake kwenye blazier aliovaa na kisha akaanza kusugua sungua manyonyo huku mkono mmoja ukiwa umeshikilia kiuno.
Ngozi ya Edna ilikuwa laini mno kama vile ni ya mtoto mchanga na kumfanya Roma kuzidi kupatwa na hisia , isitoshe alikuwa amekaa muda mrefu bila kufanya hicho kitendo ndio maana hisia zake zlikuwa za juu.
Wakati Roma akiwa bize kufanya manjonjo yake ili mradi tu kumlegeza mke wake mara alihisi maji ya moto yakimdondokea na kumfanya ainue uso wake na kumwangala na hapo ndipo alikutana na Edna ambaye alionekana kulia jambo ambalo lilimshangaza.
“Honey .. kwanini unalia , hey niambie kama hutaki kufanyiwa hivi niache na sio kulia”Aliongea Roma huku akitoa mkono wake ulioshikilia mwili wa Edna.
Roma alitaka kumfuta machozi kwa mkono wake lakini Edna aliuondoa kihasira huku akiyafuta mwenyewe.
“Naonekana mwepesi sana kwako si ndio , unafikiri mimi ni mwepesi kuchokoza? , umekuja tu bila kuniuliza chochote na kuanza kunishika shika unadhani ndio namna ya kunilainisha eh? , unajua ni siku ngapi sikuweza kupata usingizi kwa ajili yako? , naota usiku na nikiamka nazidi kuwa na wasiwasi lakini bado tu nilijifanya nipo sawa mbele ya Lanlan , lakini kuna wewe ambaye ulituacha kwa zaidi ya mwezi bila taarifa yoyote , hivi unajua kama sisi tulitekwa?, unajua kama Lanlan alipigwa ?, yote hayo hujui lakini hata hukutaka kujisumbua kuuliza na hukusema kitu chochote hata baada ya kuniona , kwanini unakuwa mkatili hivyo?”Aliongea Edna huku akionyesha hasira zake waziwazi.
Roma wakati huo alijihisi ni kama kuna kitu kizito kimempiga kichwani , huku hasira zikianza kujikusanya.
“Nani kawafanyia hivyo..”
“Walisema ni wanajeshi waliokuwa chini ya Afande Razaq, walijua haukuwepo ndio maana walituteka kwa ajili ya kulipiza kisasi huku wakitaka pia mbinu yako ya mafunzo , baadhi yao walikuwa hata na mafunzo ya kijini levo ya nusu mzunguko , Lanlan alirushwa ukutani mpaka kwenye sakafu na kupigwa mateke mengi lakini akaamua kukaa kimya..”
“Nini kilitokea baaada ya hapo..”Roma alijihisi moyo wake ukijikunja kunja huku akiuliza kwanini hakuna ambaye amemwambia mara baada ya kurudi tu.
Edna alifuta macho yake na kisha alianza kumwambia Roma kila kitu kilichotokea .
“Afande Tobwe alisema niliwaua watu wote lakini mimi sikumbuki chochote nilichofanya kwani nilipoteza fahamu baada ya hapo na Afande Tozo na wengine hawajui kwanini niliweza kufanya vile..”
Roma mara baada ya kusikiliza alijikuta aking’ata meno yake kwa hasira , hakuamini kuondoka kwake kidogo tu kuna watu wamekosa adabu mpaka kuja kumchokoza , alijiambia hayo yote ni makosa yake ya kukata nyasi pasipo kuondoa mizizi yake.
Roma mara baada ya kumuona Edna akiwa katika hali ya majonzi alijikuta akimuonea sana huruma , ijapokuwa alishangazwa a namna ambavyo Edna amesema amewaua lakini hakujali kuuliza maswali zaidi, alijikuta akipatwa na ahueni kwa Lanlan kutoongea chochote na alijiambia hakika kweli Lanlan alikuwa ni damu yake , alikuwa amerithi kila kitu kutoka kwake , kwani kama ni mtoto mwingine wa kawaida pengine angeishi kwa hofu baada ya tukio hilo lakini Lanlan alionekana kuwa kawaida.
Roma ilibidi amkalishe Edna kwenye kitanda na kisha akaishika mikono yake na kumfuta machozi kwa upole.
“Najua walikukosea sana kwa kukuchokoza na hakuna mtu ambaye ameniambia kuhusu hili licha ya mambo mengi kutokea , lakini pia kwa upande wangu nilikuwa nikihatarisha maisha yangu , nilikuwa katika hofu ya kuogopa siwezi kukuona tena wewe na Lanlan”
Baada ya kusema hivyo Edna alikuwa ashanyamaza , ijapokuwa alikuwa na hasira lakini alikuwa akijali usalama wa Roma na aliishia kumwangalia kwa macho ya kutaka kusikiliza zaidi.
“Sikutaka kuongea sana kwa watu wa nje juu ya kilichonitokea lakini wewe ni mke wangu na lazima nikuambie kila kitu kilichotokea..”Aliongea Roma na kumfanya Edna kuonyesha tabasamu la furaha, isitoshe hata Blandina na wengine hawakuweza kujua alikotokea Roma na hakuwaeleza hivyo Edna alitafsiri Roma alitaka kumwambia yeye ya kwanza kama mke wake juu ya kila kitu kilichtokea.
Inamaanikika kwamba haijalishi mwanamke ana akili kiasi gani lakini siku zote atapenda kufanywa wa pekee katika akili ya mpenzi wake , maneno ya Roma alijua kabisa ni ya kumpamba lakini mwisho wa siku aliyakubali na kumfanya awe na furaha,hakuweza kujiuzuia kwani huyo ndio mwanaume ambaye anampenda kwa moyo wake wote.
Roma alijitahidi kuanza kumweleza kwanzia namna walivyovutwa kwenye ulimwengu wa majini pepo kadri awezavyo lakini kuhusu Sophia kuwa na mahusiano nae ya kimapenzi hakuongea kwani hakutaka kumkasirisha tena Edna.
Roma hakuelezea pia kama hakuwa na uwezo wa kutumia nguvu zake za kijini tena ili tu kutoleta wasiwasi kwa Edna.
Edna mara baada ya kuelezewa yaliojiri katika ulimwengu huo alijikuta akishangaa mno na kuwaonea huruma kwa yale walioweza kupitia lakini hata hivyo kuna baadhi ya sehemu ziliibua mashaka katika kichwa cha Edna.
“Huyo Aoiline naamini atakuwa mzuri sana si ndio , nina uhakika atakuwa anakupenda ndio maana akaamua kukusaidia , vipi kuna ulichomfanyia mpaka kuwa na upendo wa namna hio?”
“Unaongea ujinga gani , unadhani mimi ni mwanaume ambaye ninaweza kugusa kila mwanamke ambaye yupo mbele yangu , isitoshe yule ni jini tu mwenye umbo la kibinadamu”Aliiongea Roma huku maneno ya Edna yakimfanya kuwa na aibu maana alikumbuka namna alivyopigana denga na yule Mbweha.
Edna hata yeye mwenyewe alifikiria licha ya uzuri waliokuwa nao majini mwisho wa siku watabakia kuwa majini tu ambao wamejitengenezea miili ya kibinadamu .
“Lakini vipi kuhusu Sophia ? wewe na yeye mkoje kwa sasa?”Aliuliza Edna mara baada ya kukumbuka Sophia aliwekaga hisia zake wazi kama anampenda Roma kimapenzi ndio maana jambo hilo lilimpa wasiwasi.
“Acha hizo …”Roma aliongea kwa haraka akijaribu kukataa.
“My Dear wife , kwanini huniamini mimi mumeo? Nilifanya kila kitu ili kuweza kurudi na kukuona , ukiendelea kuongea hivyo utanifanya nijisikie vibaya”Aliongea Roma huku akijifanyisha mpole.
“Kadri unavyojiweka hivyo ndio inaniambia kuna kitu hakipo sawa , Roma siamini unaweza kuwa na ukaribu wa kawaida na Sophia kwa yale yaliotokea..”
Roma alijikuta fuvu lake likipatwa na ganzi kwa muda, alikuwa akiogopa ukweli kujulikana kama ameanzisha mahusiano na Sophia, hakujua Edna angelichukuliaje hilo swala , na kutokana na kwamba hakutaka kuendelea kumuona Edna anaongea aliona atoe siraha yake haraka haraka ili tu kumtuliza.
Licha ya kwamba hakuwa akitumia nguvu za kijini lakini kufungua anga ya ya pete ya Sumeru haikuhitaji nguvu zozote hivyo aliweza kufanya hivyo na kutoa zawadi kwa ajili ya Edna.
Edna alijikuta macho yae yakichanua huku akishindwa kujizuia na kuziba midomo yake kwa mikono yote miwli.
Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuona dini kubwa la namna hio la kupendeza ambalo halijapitia kwenye mikono ya wahunzi , kwa ukubwa wa jiwe hilo la Rubi aliamini kama litawekwa kwenye mnada basi linaweza likavunja rekodi ya dunia kwa kuuzwa kwa thamani kubwa lakini kwa kuwa jiwe la kwanza kubwa la Rubi kuuzwa duniani..
Roma aliishia kutabasamu kutokana na mshangao wa Edna na alichokifanya ni kushikilia mikono yake na kuweka lile jiwe la madini ya rubi kwenye mikono yake na kumfanya Edna kulishika kama vile ni kitoto kichanga ambacho ndio kimezaliwa.
“Babe niliua jini Joka moja lenye nguvu na nikaweza kupata hio Rubi kwenye kiota chake , baada ya kulipata nilikuwa nikiwaza kutoka tu katika ulimwengu huo ili nije nikupatie kama zawadi, nadhani ni muda sahihi wa mimi kutimiza hitajio langu, hio ni zawadi yangu kwako mke wangu kipenzi”
Baada ya kusikilizia uzito wa jiwe hilo Edna alijishawishi na kujiambia hakuwa akiota , Roma alishawahi kumuahidi kwamba atampa jiwe kubwa la madini kama jicho la Tembo mara baada ya kumpa Nasra pete ya Almasi lakini licha ya ahadi hio hakuwahi kuamini kama itatokea , , lakini mara baada ya kupatiwa jiwe kubwa la madini ya Rubi aliona nafasi yake kama mke wa Roma imeweza kurudi na sasa yeye ndio anamiliki zawadi ya thamani kubwa kuliko wanawake wake wote.
“Umeipenda?”
“Ndio..”Aliongea huku akitingicha kichwa mara nyingi kama vile alihisi Roma anaweza kubadilisha mawazo na kumpokonya.

Unafikiri nini kilimtokea Aoiline na Lekcha? , Miungu ipo kumi na mbili jumla yao na hatujaiona yote mpaka sasa , je unajua ni stori gani ipo nyuma yao? .
Ndio tunaanza anza kuzikaribia nyama baada ya kumaliza hivi vijimtori vya juu juu hivyo tusipoteze hamu
ITAENDELEA.
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 625.
Roma mara baada ya kumuona Edna ameacha kuuliza maswali na kushangaa jiwe la madini aliompatia alijikuta akivuta pumzi ya ahueni maana alijua kama Edna angeendelea kuongea mwisho wa siku angeshia kumwambia ukweli wote.
“Nitamuambia Ron kutafuta mhunzi wa kuaminika , hilo jiwe ni kubwa sana na linaweza kukatwa katikati nakutegnenezwa vito vya vingi na unaweza kuchagua kinachokufaa”Aliongea Roma.
“Hapana , sioni inaweza kuwa salama kumpa mtu mwingine , isitoshe nitatafuta huyo mhunzi mimi mwenyewe , kama utalitoa wewe wanawake wengine wataliona na wanaweza wakataka uwapatie na wao”Aliongea na kumfanya Roma misuli yake ya uso kucheza.
“Babe kwahio unasema utalifiicha ndani milele bila watu kuliona?”Aliuliza na Edna alitingisha kichwa lakini hata hivyo akionekana kuwa na furaha kupatiwa jiwe hilo na hakujali kama litakaa ndani ili mradi tu awe na uwezo wa kuliangalia pale anapohitaji pasipo ya kuwafanya wanawake wa Roma kuliona.
Roma hakuongea neno lolote lakini wakati huo aliona kwamba alikuwa na majiwe kama hayo mengi tu ambayo ameyachukua kwa ajili ya hao wanawake, haraka sana hakutaka kumuonyesha Edna kwani angeweza kuyachukua yote hivyo aliona huko mbeleni angetafuta namna ya kuwakabidhi kwa siri.
“Nadhani umeniletea mimi tu , lakini nataka nikuonye , isije ikatokea nikagundua umewapa na wanawake wengine”Aliongea Edna akiwa siriasi.
“Ah.. kwanini nifanye hivyo sasa!?”Roma alijikuta akikosa ujasiri , ijapokuwa aliongea hivyo lakini kijasho cha baridi kilianza kumtoka , alijiambia huyo mwanamke ni kama anayajua mawazo yake , alikuwa akipanga kuwapatia wanawake wengine mawe hayo kwa siri lakini Edna alishaona tayari mpango wake.
Kumuona Edna akiwa ameshikilia jiwe hilo kwa mkono mmoja uzuri wake ulizidi kuongezeka na alikuwa ni kama ua huku tabasamu lake likizidi kuyafanya mapigo yake ya moyo kudunda kwa kasi zaidi , Roma mwishowe alishindwa kabisa kuvumilia njaa yake na kiu aliokuwa nayo kwa muda mrefu na palepale alimsogelea na kumrushia katikati ya kitanda huku jiwe lake likidondokea kwenye mto.
“Ah…nini wewe,, kwanini unaharaka hivyo , hebu kaoge kwanza..”Aliongea kujitetea lakini Roma hakujali maneno yake na tayari alikuwa ashajichimbbia katikati ya kifua chake.
“Siwezi kusubiri zaidi ,,, nimevumilia kwa muda mrefu..”
“Lakini ni siku nyingi zimepita kwanini ushindwe dakika chache za kuoga..”
“Basi tukaoge wote”
“Mh.. usinifanye mjijnga , najua mpango wako ni kufanyia bafuni”
“Kama ni hivyo tulia basi wewe mwanamke … halafu hii sketi ni ya namna gani , vishikizo vyake viko wapi?”
Roma alipeleka mkono kila mahali bila ya kujua kama kweli alikuwa akitafuta vishikio au ndio alikuwa akitaka kuminya makalio , dakika hio hio mkono wake ulikuwa ushatumbukia sehemu nyingine kabis akitafuta vishikizo.
Edna hakuwa hata na nguvu ya kumzuia anachotaka kufanya katikati ya mapaja yake na alijiambia kuziba na mkono ni kujisumbua tu , hivyo aliacha afanye anavyotaka isitoshe kwa wakati huo na yeye moto ulikuwa ushawaka kwenye mwili wake.
Ikiwa ni jioni Blandina alimwagiza kijakazi kwenda kuwaamsha kwani Lanlan alikuwa akiwahitaji lakini kijakazi huyo alirudi akiwa na sura iliokuwa imepata moto kutokana na kile alichokisikia na Blandina kwa uzoefu wake aliweza kujua nini kinaendelea na aliishia kutabasamu.
Alijiambia ni vizuri hivyo kwasababu wanaweza kupata mtoto mapema , hivyo alimsaidia Lanlan kukamilisha homework yake kazi ambayo ilikuwa ni ya Edna.
Katika kitanda cha sita kwa sita Edna Edna alionekana akiwa amejilaza kichomvu huku nusu ya mwili wake ukiwa juu ya Roma , katika hali kama hio kichwa chake kilikuwa kikiwaza vitu vingi.
Baadhi ya wanawake pengine hawawezi kupata uzoefu wa hali ya juu wa utamu ambao anaupata kwenye maisha yao yote lakini kwake yeye mume wake alikuwa akimfikisha kunako bila shida yoyote, hio ndio faida kubwa ambayo alikuwa akiipata kwa mwanaume huyo ambaye amekaa kihuni huni.
Upande wa Roma alikuwa amejiachia m mkono mmoja alikuwa ameupitishia begani kwa Edna akimfanya amlalie kifuani huku yeye akiwa na sigara yake kubwa aliotoka nacho China akiivuta huku akipuliza moshi wake kwa raha zote , hakujali kabisa kuhusu mwili wake uliokuwa uchi na muda huo kiungo chake kilikuwa kimesimama kama mlingoti wa bendera ya raisi.
Edna alijikalia kivivu kwa nusu saa na nguvu zake angalau ziliweza kumrudia , mafunzo ya kijini yalikuwa yamemsaidia sana kuendana na spidi ya Roma la sivyo kwa mikiki yake angepoteza fahamu, aliishia kutabasamu na kisha akampiga Roma busu la shavuni na kusimama kisha akalisogelea kabati na kutoa kipande cha khanga na kujifunga.
“Honey , nina wazo kuhusu Sophia….”Aliongea Edna na kumfanya Roma ambaye alikuwa katika hali ya utulivu kumwangalia.
“Wazo gani?”
“Wiki moja zilizopita kampuni ya Vexto upande wa habari na burudani tulipitisha zaidi ya bilioni nne za kitanzania zinazowenda kuwekezwa kwenye udhalishaji wa filamu mjongeo ya hadithi ya ‘Shetani Rudisha akili zetu” kutoka kwa mwandishi Singanojr , huu ni uwekezaji mkubwa wa kwanza kufanyika nchini Tanzania na kampuni ya Vexto Media and Entertainment ndio wasimamizi wakuu , mpango wetu ni muvi hii kufanya vizuri na sio kufeli au kwenda kinyume chake..:”
“Hebu subiri , kama ni hivyo Sophia anahusiake na hio bajeti?”Aliongea Roma huku akikunja sura.
“Sophia anakwenda kuwa Sterling wa kike kwenye hii filamu, muvi yake iliopita iliweza kufanya vizuri sana kwenye mtandao wa Netflix na kuibua hisia za watu wengi kutoka mataifa mbali mbali hususani Ulaya na Amerika , nadhani pengine ni kutokana na kuwa ‘endorsed’ na Christen ndio maana, viongozi wa Vexto wamekuja hapa na kunishawishi uhusika wa Sophia na kweli nimekuja kugundua ukiwa Star huwezi kukwepa Skendo , hivyo tofauti na kukimbia ni kuzichukulia Skendo hizo kuzidi kujipandisha ki umaarufu, hivyo wengi wameshauri kwamba Sophia ashiriki katika filamu hii kwani ni ‘Action Movie’ na ile iliotoka chini ya Director Lassay Sophia alifanya vizuri sana hususani upande wa mapigano”Aliongea huku Edna akikaa pembeni ya kitanda akijarbu kumwelezea.
“Edna usinifanye mimi mumeo ni mjinga , Sophia alishatangaza kuachana na maswala ya usanii inawezekanaje filamu ikafanya vizuri , labda unionyeshe ushahidi au unataka tu Sophia kurudi katika maswala ya usaniii?”
“Ndio nataka arudi , huu ni uwekezaji mkubwa na kama Sophia atahusika na filamu ikafanya vizuri kampuni yangu itaimarika na kuwa kubwa zaidi , sio Tanzania tu bali mpaka nje ya mipaka ya Tanzania na hayo ndio yalikuwa malengo yangu tokea mwanzo katika kuianzisha”Aliongea .
Roma alivuta moshi wa sigara mwingi na kabla Edna hajashituka moshi wote ulipulizwa usoni mwake na kuishia kukohoa kwa nguvu.
“Kwanini unannifanyia hivi..?”aliongea huku akimfinya.
“Nimefanya hivi ili kuirudisha akili yako katika mstari , Edna kwanini unapenda hela namna hio , ile kampuni ni tawi tu na hata ikifirishika huwezi kupata hasara kubwa , kwanini unataka kumrudisha Sophia ili kuikuza kampuni yako ili ujipatie pesa , halafu sio kwamba hela zenyewe huna , kwanini unataka kumsumbua kama yeye mwenyewe alitangaza hataki maswala ya usanii?”
“Nini ? Kwahio wewe ndio unajifanyisha sasa hivi ndio unamjali sana , Bibi yangu alinifunza jinsi ya kuwa mfanyabiashara tokea nikiwa mdogo , kama nisipojali hela kama mfanyabiashara kuna kipi kingine napaswa kujali , je napaswa kujali wanawake kama wewe , mimi sina njaa ya hela lakini vipi kuhusu wafanyakazi wangu , vipi kuhusu timu ya udhalishaji wa hio filamu , na wenyewe wanafamilia na ndoto za kukamilisha na walifanya kazi kubwa kumpaisha Sophia kimuziki lakini akaamua tu kuachana na usanii na kukimbia kwenda kujificha , kampuni sasa hivi haifanyi vizuri je unadhani ni sawa , sio kama nataka kumlazimisha kufanya kazi , ninachoatka ni yeye kurudi na kufanya kitu anachokipenda mbele ya kila mtu”
Roma aliona ni kweli watu wengi walifanya kazi kubwa kuhakikisha Sophia anaupata umaarufu na kupitia yeye wengine waliweza kupata ujira wao lakini akaacha na kufanya kampuni kuzorota na kuwapa watu mzigo wa kuirudisha katika uimara wake.
“Una uhakika na unachotaka kufanya , sitaki akawe topiki ya kila mmoja kama ilivyotokea , yule baba yake sio mtu mzuri sana jambo baya linapomkuta binti yake” Aliongea lakni Edna alimwangalia Roma kwa jicho la pembeni.
“Kuna kitu kinachoendelea kati yenu sio ndio na unanificha , kwanini hutaki akirudi?”
“Hamna kinachoendelea , naongea kama shemeji yake”
“Naamini hujawehuka na kumgusa na Sophia , itakufanya uonekane mnyama”
Maneno hayo yalimfanya Roma kuingiwa na majuto , alikuwa tayari ni zaidi ya mnyama , alijikatia tamaa yeye mwenyewe na tabia yake lakini hakuwa na la kufanya, Sophia alikuwa amekufa na kuoza juu yake , anaweza kuwa mpole lakini alikuwa siriasi kuhusu hisia zake.
Roma hakuwa akitaka Sophia arudi kwenye usanii kwani ingepelekea mwisho wa siku kugundulika alikuwa aki’dat’e nae , sasa alijiuliza atawezaje kuzuia swala hilo bila ya kuibua mashaka.
“Vipi simu ya Sophia inafanya kazi?”
“Nadhani itakuwa imezimwa”
“Kama ni hivyo basi nitamtafuta mama yake , nina namba yake , nitamweleza mpango wangu na nadhani lazima anikubalie”Aliongea Edna huku akisimama na kuisogelea simu yake.
“Sio lazima kuwa na haraka hivyo , isitoshe wewe sio CEO tena hio kazi anaweza kufanya mtu mwingine”
“Najua lakini Ernest hawezi kulifanyia kazi hili vizuri , hivyo napaswa kuhusika, kuna siku mbili tu ambazo zimewekwa kwa ajili ya kuchagua wahusika hivyo lazima nimshawishi Sophia ndani ya siku hizo”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kitu kingine cha kukwamisha mpango huo na palepale macho yake yalichanua.
“Ah .. Edna mke wangu hatuwezi kufanya hivyo kuna tatizo?”
“Tatizo gani tena?”
“Kumbuka nilikuambia Sophia yupo kwenye levo ya Nafsi kwa msaada wa Aoiline , lazima atapaswa kwenda ulimwengu wa kijini kama sheria inavyomtaka, atawezaje kuwa msainii?”Aliuliza na kumfanya Edna kufikiria kidogo na kisha alitoa tabasamu la kupata njia.
“Kwanini tusifanye hivi , nimesikia kikosi cha wachawi ndani ya Tanzania kimeunda ushirikiano wa maswala ya kijeshi na kikosi cha wachawi kutoka China ambacho ndio kina muunganiko mkubwa na Hongmeng , kwanini usiongee na Afande Tobwe akajaribu kufanya mawasiliano , isitoshe Sophia ni msanii mkubwa tu na kama mara ya mwisho uliweza kumhonga yule mjumbe wao na akakubali basi nadhani na la Sophia linawezekana ,isitoshe yupo hata Omari Tozo ambaye yupo levo ya nafsi na yupo uraiani”
“Unadhani njia hio itafanya kazi?”
“Naamini itafanya kazi, tunaweza kuwapa rushwa hata ya vidonge wakati watakapotaka kumchukua Sophia”Aliongea na kumfanya Roma ashindwe kuongea chochote , mpango wake aliona unaweza kufanya kazi vizuri na aliona kama ataendelea kukwamisha mpango wa Sophia kurudi basi inweza kuibua mashaka kwa mke wake.
Roma baada ya kuona hakuwa na chaguo lingine ilibidi awasiliane na Afande Tobwe na kumuelezea mpango wake kama anaweza kuwaungaisha na wajumbe wa Hongmeng wanaoishi duniani ili Sophia sheria isimguse na Afande Tobwe licha ya kutokuwa na uhakika lakini alisema atajitahidi.
Roma hakuacha kuuliza kuhusu habari za Edna kuua wanajeshi pamoja na wachina waliokuwa katika levo ya nusu mzunguko lakini upande wa Afande Tobwe mwenyewe hakuuwa na maelezo ya kutosha juu ya tukio hilo na hata uchunguzi ambao wamefanya haukuleta mwanga wa aina yoyote.
Baada ya Edna kutoka akimuacha Roma mwenyewe chumbani , Roma mawazo yake hayakuacha kumuwazia Aoiline juu ya kilichotokea baada ya yeye kuondoka.
Baada ya kuona hatoweza kuwa na majibu hata kama akiwaza aliachana na mawazo hayo na kuanza kuwazia juu ya uwezo wake wa kijini ambao hakuwa na uwezo wa kuutumia.
Alifikira namna ya kufanya na katika kuwaza kwake aliona mtu pekee ambaye anaweza kumshirikisha katika swla hilo ni Profesa Clark.
Hakutaka kupoteza muda palepale alitafuta simu yake na kisha akaitafuta namba ya Clark na kuipiga na ndani ya dakika chache tu iliweza kupoktelewa.
“My Dear Roma ramoni , is it reallly you? Are you really back ?”Aliuliza Clarka na kumfanya Roma kushangaa kwani alijua jambo la yeye kupotea lilikuwa siri kama alivyoelezewa na Afande Kweka.







SEHEMU YA 626.
“Clark ulikuwa unajua nilipotea?”Aliuliza Roma akiwa amekunja ndita kidogo akionyesha mshangao wake.
“Bila shaka , nilikuwa nikikufikiria sana lakini nipo huku mbali na sikujua ni wapi ulipo”Aliogea na kumfanya Roma kutabasamu , alijiambia siku zote ilileta raha pale unapojua kuna mtu anakujali.
“Clark vipi lakini kuhusu maendeleo ya mafunzo yako?”
“Naendelea taratibu sana , bado tu nipo kwenye levo ya mwanzo mwa nusu mzunguko, nimejiingiza katika mafunzo ya Kung Fu ili kupanda kwa haraka na kufanya viungo vyangu kufanya kazi vizuri, lakini niseme tokea nimeanza kujifunza kuna vitu nashindwa kuvielewa kisayansi”Aliongea na kumfanya Roma kucheka.
“Hebu kwanza tuachane na hayo , nina tatizo kwasasa na nahitaji unisaidie kunifanyia uchunguzi wa kiafya”
“Una tatizo!! , unapitia tena mavumivu ya kichwa?”Aliuliza Clark akiwa na sauti ya wasiwasi .
“Sio maumivu ya kichwa ni kitu kingine tofauti na hicho , kwasasa siwezi kutumia uwezo wangu wa kijini..”aliongea Roma huku akimwelezea kile ambacho kimetokea mwanzo hadi mwisho na Clark upande wa pili alionekana kusikiliza kwa umakini.
“Kama ni hivyo basi nadhani haina haja ya kusafiri mpaka huku Uingereza , nitakuja huko huko kujaribu kuangalia tatizo lako nikichukulia kama nafasi ya mapumziko , pia inaweza kupunguza macho ya wengi “Aliongea na Roma alijikuta akiguswa na maneno yake , kwa namna ambavyo alikuwa akiongea ni kama tatizo lake lilikuwa dogo lakini upande wake yeye aliliona ni kubwa lakini hata hivyo alimkubalia na kupanga wakutane Tanzania.
Upande mwigine Roma alikuwa na wasiwasi kwani yeye na Clark walikuwa ni wapenzi rasmi tokea siku ambayo alimuokoa , hivyo aliomba Edna asije akagundua hilo.
Ukweli ni kwamba Roma alikuwa na wasiwasi kwani mbele yake ana mizigo mitatu ya kumwambia Edna ambayo hakuwa na uhakika kama angeweza kuchukuliaje.
Edna alipaswa kujua kuhusu Lanlan , wakati huo huo Roma alikuwa ashafanya kosa na Magdalena mpaka kulala nae , bado yupo Sophia na Clark , wote alishaanzisha mahusiano nao na Edna hakuwa na uelewa wa maswala hayo , hivyo moja kwa moja ni kwamba uendelevu wa mambo hayo ni kama bomu ambalo linahesabu dakika kurudi nyuma na siku yoyote lingeweza kulipuka huku mwenyewe aishindwa kujua ni madhara ya aina gani ambayo yanaweza kutokea.
Wakati Roma akifikiria makosa yake ambayo yalikuwa nje ya uwezo wake kuyaeupuka palepale aliwakumbuka Rose na Magdalena ambao walikuwa katika visiwa vya bahari ya Mediterranian na ilikuwa ni muda mrefu hajawatafuta kujua maendeleo yao.
Roma palepale na wazo lingine liliibuka katika kichwa chake na kujiuliza kama Sophia anaweza kusamehewa na kuendelea kubakia uraini licha ya kuwa katika levo ya Nafsi , je na Magdalena anaweza kusamehewa, isitoshe Magdalena alikuwa katika mfumo wa kijeshi.
Roma baada ya kuwaza kwa muda mfupi kidogo aliamua kutafuta namba ya Magdalena na kumpigia na ilipokelewa kwa shangwe zote upande wa pili , kwani ilikuwa ni taarifa nzuri kwao kama Roma ameweza kurudi salama.
Roma alimpamba pamba na maneno ya hapa na pale na baada ya hapo alimwelezea swala la yeye pia kuruhusiwa kuishi kawaida licha ya kuwa katika levo ya Nafsi.
“Roma umeshashau kama Mzee Tobwe ni baba yangu? , alishaniuliza pia hilo kabla yako na kuniambia anaweza kutumia koneksheni zake niendelee kubakishwa uraiani”
“Sasa kwanini hukuniambia kuhusu hilo au ilikuwaje?”
“Sikutaka kumpa baba mzigo mkubwa , ulishasema ni sheria ambazo zimeweka kwa ajili ya kuimarisha usalama wa dunia hivyo sikutaka baba avunje sheria kwa ajili yangu , isitoshe sio kwamba ni kuhusu mimi tu kuna Rose na yeye, kwasasa nina furaha mazingira ya huku ni mazuri sana na ya amani pamoja na watu wake kuwa wakarimu , sina haja ya kuomba na mimi kuruhusiwa”
“Inaonekana hamna mpango tena wa kutaka kuishi karibu na mimi , wewe na Rose?”Aliuliza Roma.
“Sisi hatuna shida , tunaweza kuishi popote , tunaweza kurudi pia kama Edna hana shida”Aliongea Magdalena akijaribu kutania na kumfanya roma kucheka kivivu.
“Okey basi hakuna shida , nilidhani hamna furaha kuishi huko mbali na familia ila kama mko sawa basi hakuna shida , mpe simu na Rose niongee nae, nijue ana mishe gani siku hizi?”
“Rose hayupo hapa , anavua samaki anataka mchana wa leo kula chakula cha baharini tu , Mr Ron alituletea wapishi lakini Rose kawakataa na kusema atapika mwenyewe”Aliongea na maneno yake yalimfanya Roma kuona kweli warembo hao walikuwa wakifurahia maisha maana walionekana kuzoea mazingira tayari.
Upande huo mwingine wakati Roma akiongea na Magdalena , Rose alikuwa ameakaa juu ya jiwe kubwa lililotokezea majini huku akiwa amevalia miwani ya jua.
Alikuwa amevalia mavazi ya fukwe , mtindo unaofahamika kwa jina la Hawaian styled Bikini , mtindo ambao ulifanya umbo lake lote kuonekana na kuzidi kuvutia.
Dakika hio hio akiwa bize kusubiria ndoano yake kunasa samaki , alitokea Magdalena nyuma yake akiwa ameshikilia simu.
“Roma anataka kuongea na wewe”Aliongea Magdalena lakini Rose hakuonyesha mshangao zaidi ya kuweka umakini wake kwenye ndoano.
“Amerudi , amekuambia yupo salama?”
“Ndio yupo salama , vipi hutaki kuongea nae mwenyewe”
“Vizuri kama yupo salama .. subiri ,, Ah Magdalena angalia ndoano imekamata , Samaki mkubwa jamani”Aliongea huku akianza kuvuta kwa kuzungusha.
Rose hakuwa mtu ambaye alikuwa akifanya matembezi ya kusafiri , pengine ndio maana kila kitu kilichokuwa kwenye kisiwa hicho kilimshawishi kukifanya , alikuwa na ratiba zake maalumu kuna siku alikuwa akizama chini ya maji kuangalia viumbe hai , siku nyingine alizama msituni kuwinda , siku nyingine ndio kama hivyo alikuwa akivua samaki.
Alikuwa na mambo mengi ya kufanya lakini kwa bahati mbaya ni kwamba uwepo wao kisiwani hapo sio kwa ajili tu ya kustarehe .
Roma hakutaka kuwasumbua sana baada ya kuona wanafurahia maisha hivyo alikata simu na kuwaambia atakuja muda si mrefu kuwatembelea.
Siku iliofuata Roma mpango wake ni kurudi Dar es salaam akiwaacha Edna na Lanlan, alikuwa akitaka kurudi kwa ajili ya kumhoji Qiang Xi kwanini alimuweka gizani licha ya kupewa maagizo na Master Chi.
Roma mara baada ya kuaga wakati wa chakula cha usiku wengine wote hawakuwa na tatizo lakini kwa Edna alijua tu lazima atakuwa amewakumbuka wanawake wake waliopo Dar es salaam lakini hata hivyo hakuwa na muda wa kujali kile anachokwenda kufanya.
******
Wakati mengi na mengi yakiendelea katika maisha ya Roma ya kila siku , upande mwingine nchini Rwanda katika makazi ya Raisi Jeremy alionekana Master 4 akiwa ameketi kwenye Sofa huku akiwa ameshikilia kishikwambi cha kampuni ya Sumsung akipangusa kutoka kulia kwenda kushoto.
Inawezekana kabisa alikuwa ni jini kutoka miliki ya Panasi lakini haikumaanisha kwamba maisha yake yalikuwa tofauti sana na ya binadamu wa kawaida , kwa jinsi tu alivyokuwa akionekana kwa mtu wa kawaida hawezi kugundua kama sio mtu wa kawaida.
“Jeremy hizi ndio taarifa pekee ulizopata kuhusu Roma Ramoni au kuna zingine?”Aliliza .
Raisi Jeremy wakati huo alikuwa ameketi pembenii akimwangalia Master 4 aliekuwa akipekua taarifa alizompatia , ambazo zilikuwa katika mfumo wa kidigitali.
“Ndio Master 4 , ukiachana na taarifa nyingine za international underground organisation”aliongea na kumfanya Master 4 kuishia kuguna.
“Huyu Roma Ramoni ni mtu hatari sana , ndio kwanza yupo kwenye miaka yake ya ishirini kwenda therathini lakini ana mafanikio makubwa namna hii katika mataifa ya Ulaya na Amerika”
“Hakika , ni ngumu sana kushindana nae akiwa katika mataifa yaliondelea tofauti na akiwa huku Afrika ya mashariki , kila serikali kubwa duniani ina wasiwasi nae kutokana na koneksheni zake kuanzia kwenye jeshi na makampuni ya kutengeneza siraha , ni rahisi kusema kwamba kwasasa ndio mfalme wa underwold , bila kusahau pia anamiliki eneo kubwa ambalo amepatiwa hati ya umiliki na serikali ya Uingereza katika bahari ya Mediterranian , ni muunganiko wa visiwa ambavyo vinaitwa Visiwa vya wafu na ndio makao yake makuu na shughuli zake zote zinafanyikia hapo , wahalifu wakubwa walioamua kuachana na maisha yao ya nyuma hutafuta makazi ndani ya visiwa hivyo , ni kwa bahati mbaya kwamba hatuna uwezo wa kupata taarifa uelekeo wa eneo hilo kwani limetolewa katika mfumo wa ramani ya dunia na hata satilaiti zinashindwa kupokea taarifa katika hilo eneo”
“Mh.. hakika ni mtu hatari , ndio maana ni mtu wa majigambo sana , ni kwa bahati mbaya mtu kama huyu hawezi kufanya kazi na sisi ..”Aliongea huku akiendelea kukagua taarifa hizo kupitia Kishikwambi.
“Uwezo wake wa kijini ni mkubwa kiasi cha kufikirika , uongozi wa miliki umeniagiza kuipata mbinu yake ya mafunzo na kumfanya kuwa mmoja wetu lakini naona kabisa misheni hii haiwezi kuwa nyepesi , labda tuweze kupata udhaifu wake”Aliongea.
Wakati huo raisi Jeremy alionekana kuna kitu ambacho alikuwa akitaka kuongea lakini alikuwa akisita sita.
“Master 4 ile siku ya tatu yake baada ya mapambano hapa Rwanda Namba moja alinitafuta kwa ajili ya kikao”
“Namba moja alikutafuta yeye mwenyewe kwa ajili ya kikao?”Aliuliza kwa mshangao
“Ndio , ni muda mrefu sana tokea alivyofanya hivyo”
“Aliongea nini?”aliuliza Master 4 huku akikunja sura.
“Alisema tunavuka mpaka wa kisheria uliowekwa , watu wengi mnatoka katika ulimwengu wa kijini na kusumbua raia”
“Tokea kuundwa kwa umoja wa koo zote za kijini na Namba moja kuwa kiongozi wetu haijawahi kutokea akaingilia katika maswala yetu , sikutegemea awamu hii angezungumzia kuhusu hili”Aliongea Master 4 huku akionyesha wasiwas.
“Master 4 kwani anatisha sana mbona anaonekana wa kawaida?”
“Nakutahadharisha Jeremy , kama kweli Namba moja amesema tumevuka mipaka basi lazima atakuwa anatuchunguza kwa kila tunachofanya , mtu kama yule hawezi kukuita kutaka kuongea na wewe hivi hivi , jaribu kutumia akili yako kufikiria kuhusu hili , je kwanini haijawahi kutokea akabadilishwa na kuendelea kuishi maisha ya kawaida licha ya mambo mengi kutokea kwa zaidi ya miongo ?”Aliuliza na palepale alimfaya Raisi Jeremy kujikuta katika hali ya wasiwasi.
“Ila usiwe na wasiwasi , nadhani anajaribu kuwa makini tu na sheria , wewe bado ni kiongozi wa ukoo wetu katika ulimwengu wa kawaida, kama ungekuwa hufai basi ungeshaondolewa muda mrefu”Aliongea akijaribu kumtoa Jeremy wasiwasi na kisha akaendelea kupitia faili la Roma ambalo limesheheni kila mtu ambaye alikuwa na mahusiano nae.
Master 4 mara baada ya kuendelea kupitia kurasa za maisha ya Roma nchini Tanzania hususani wanawake aliokuwa nao katika mahusiano alijikuta akisimama kwenye picha ya msichana mdogo mweupe.
“Huyu msichana na yeye ni sehemu ya wanawake zake?”Aliuliza huku akimsogezea Jeremy kile kishikwambi.
“Ndio , jina lake anaitwa Rufi, kwa taarifa ambazo tunazo mama yake ni Wema Sufiani kijakazi wa muda mrefu katika familia ya Adebayo na ndio amemzaa huyu binti na mchina mmoja ambaye alikuwa ni machinga anaefahamika kwa jina la Kunlun na baada ya kuzaliwa kwa Rufi alipotea nae.
“Huyo msichana inasemekana alikutana na Roma nchini Marekani na kuanzia hapo ndio uhusiano wao ulipoanzia mpaka ilipoweza kufahamika ni mtoto wa Wema ,kwasasa anaishi na mama yake jijini Dar es ssalaam”Aliongea.
“Mozheng my friend .. hahaha… Rufi!! ni yeye namkumbika ,, hahaha.. inavutia , inavutia , Roma katoa wapi huu ujasiri kuwa na mahusiano na huyu msichana”Aliongea Master 4 alionekana kumfahamu Rufi na baba yake.
“Master 4 kuna kitu kingine kinachohusiana na huyo msichana?”
“Mh ,, hakuna kitu kikubwa zaidi kuhusu yeye lakini naweza kusema ni hazina kwa watengenezaji wa vidonge ,huwezi kuelewa kuhusu hili hata nikikuelezea , tunapaswa kutoa taarifa ya swala hili kwa wahusika wanaomtafuta ,… Roma unaweza ukawa mjanja na kujitosheleza lakini itafikia wakati utahitaji msaada wetu”Aliongea huku akitoa cheko kubwa la ushindi mara baada ya kupata taarifa muhimu ya aina hio.
******
Saa moja moja ndio muda ambao Roma aliweza kufika Dar , alikuwa amechelewa kufika kwasababu alikuwa amechelewa kutoka.
Roma alilaani kitendo chake cha kutoweza kutumia nguvu za kijini kwani pengine kwa muda aliotoka Iringa angeweza kufika Dar ndani ya dakika tu lakini kwa bahati mbaya uwezo huo hakuwa nao na kumbidi kuendesha gari umbali mrefu.
Saa moja na nusu ndio muda ambao aliweza kufika nje ya geti la nyumba ya Dorisi , mazingira yalikuwa yametulia na alitegemea iwe hivyo kwani Dorisi alikuwa akiishi peke yake tokea kuondoka kwa Rose na njia nzima alikuwa akimfikiria , ilikuwa kheri kwa Nasra ambaye Najma alikuwa ni rafiki yake hivyo hakuwa mpweke lakini Dorisi hakuwa na ndugu.
Roma mara baada ya kujifikiria aliona haina haja ya kugonga mlango zaidi ya kuruka ukuta na kwenda kutua ndani kwa ustadi wa hali ya juu.
Baada ya kukagua mazingira, taa za ndani zilikuwa zimewashwa na ilimwambia Dorisi alikuwa yupo hivyo palepale alitembea kitahadhari na kuingia ndani.
Baada ya kufungua mlango wa Sebuleni hakukuwa na ishara ya uwepo wa mtu na moja kwa moja alipandisha ngazi mpaka juu kwenye chumba chake na mara baada ya kufika nje ya mlango aliweza kusikia bomba la maji ya bafuni likitiririsha maji na kujiambia Dorisi muda huu atakuwa ndio anaoga.
Alitoa tabasamu na kisha akashika kitasa na kusukuma mlango taratibu na kuufungua na kitu cha kwanza alichoweza kuona ni nguo za ndani ambazo zilionekana kutoka kuvaliwa zikiwa zimetupwa ovyo juu ya kitanda na hapo hapo aliweza kujiambia hisia zake zipo sawa , Dorisi alikuwa akioga.
Roma macho yake yalivutiwa na nguo hizo na kutoa tabasamu la kifedhuli na kusogea kuelekea ndani ili mradi kuziangalia , lakini ile anapiga hatua ya kwanza na ya pili alijikuta akiguswa na kitu cha baridi kwenye kisogo chake, lakini haikuwa hivyo tu palepale mkono wa kulia wa mtu ambaye amemuwekea siraha kichwani alileta kisu usawa wa shingo na Roma kwa ustadi wa hali ya juu aliruka na kukwepa na kugeuka kwa wakati mmoja na kumshika adui yake mikono.
“Dorisi…!!!”
Roma alijikuta akishangaa mara baada ya kugundua aliekuwa akimshambulia ni Dorisi.
“Hubby ni wewe …!!”
Mapigo ya Dorisi yalikuwa juu juu na alijikuta akiwa na afadhali mara baada ya kugundua ni Roma.
Roma alishangaa kwani Dorisi muda huo alikuwa amevalia suti yake na ilikuwa ni dhahiri ndio kwanza anarudi tokea kazini.
“Babe Dorisi nashindwa kuamini nimeweza kuingia katika mtego ulioniwekea .. haha , umejifunzia wapi haya?”
“Kwaninni hukupiga simu na umekuja kimya kimya , nilijua ni jambazi ndio maana , hebu niachie mikono yangu unaniumiza”Aliongea Dorisi na Roma palepale alijua ni kweli alikuwa ameshikilia kwa nguvu mikono yake yenye siraha.
“Hii mbinu yako ni ya hatari , kama kweli angekuwa ni jambazi basi ungekuwa umemmaliza”
“Hehe.. sikuwa na jinsi , ukiishi mwenyewe unajikuta unatafuta namna ya kujilinda , nimeweza kujifunza hivi kupitia filamu”Aliongea huku akisogea na kwenda kukaa kitandani na kumfanya Roma kumwagalia kwa tabasamu.
Hakuwa amemuona mrembo huyo kwa muda mrefu na aliridhishwa na maendeleo yake kwani alionekana muda wowote angeweza kufika mwishoni mwa levo ya mzunguko kamili.
“Hii mbinu yako imenifurahisha sana Babe Dorisi nadhani tuendelee nayo hivi hivi , mimi nitakuwa kaka jambazi na wewe ni mwanamke unaetoka kazini na kuvamiwa na mimi kaka jambazi na sasa anataka kukubaka”Aliongea Roma na kumfanya Dorisi kuachia cheko huku akivuta mdomo na kumwangalia kwa jicho la pembeni.
“Sitaki kusikia huo ushenzi wako mimi…”
“Hehe leo tutaona , mimi jambazi ndio naanza mambo yangu hivyo”Aliongea Roma huku akimvamia Rose alieanza kujifanyisha analeta vurugu.
Ijapokuwa maneno yake hayakuendana na umri wake lakini ukweli yalimfurahisha Dorisi , inasemekana mtu akiwa mbele ya mpenzi wake anakuwa mtoto na ndio alichokiona Dorisi na alijikuta akikubali kuendelea na filamu yao huku akibakwa na kaka Jambazi.
“Eti wewe mwanamke mbona unaonekana kumpenda kaka Jambazi”
“Wewe kaka Jambazi utakuwa na kimzizi sio bure ..argghh ..Uwiiiii…”
*******
Siku iliofuata Roma alimpigia simu Nasra na kumwambia yupo kwa Dorisi na Nasra mara baada ya kusikia taarifa hio alisema anakuja kupatia kifungua kinywa huko kwani mama yake kasafiri.
Roma hakuwa na kipingamizi , isitoshe Dorosi na Nasra walikuwa ni marafiki wanaofanya kazi ndani ya kampuni moja.
Baada ya wote kukusanyika Roma alipata nao kifungua na warembo wake hao huku akijisikia raha kuwaona kwa mara nyingine na muda wa kwenda kazini ulipo wadia Dorisi na Nasra waliondoka na Roma ndipo sasa alipoanza safari ya kuelekea nyumbani kwa Bi Wema.
Qiang Xi alikuwa akiishi na Bi Wema tokea kuondoka kwa Edna kuelekea Iringa , hivyo Roma alitumia nafasi hio kwenda kumsalimia na Rufi pamoja na Bi Wema lakini pia kupata muda wa kumhoji Qiang Xi kwa kitendo chake cha kumficha juu ya Lanlan kuwa binti yake ilihali alipewa maagizo na Master Chi kumuelezea kila kitu.
Roma hakuwa na gari hivyo alitembea lakini wakati akiwa anakaribia kupita nje ya nyumba yake kuunganisha moja kwa moja kwenda kwa Bi Wema aliitwa nyuma yake upande wa kulia na sauti ya mtu aliemuita aliweza kuitambua ni ya Bi Wema.
“Mr Roma mmerudi!!?”Aliuliza Bi wema akiwa kwenye bashasha.
Bi Wema alionekana kunenepa na mwoneknao wake ulikuwa umebadilika na kurudi kwenye ujana zaidi , pengine ni kutokana kipindi hicho hakuwa akiishi kwa mawazo tena ndio maana uzee ulikuwa ukipotea.
“Nimerudi, Edna yeye bado nimemuacha Iringa na Lanlan”Aliongea Roma na Bi Wema alimuelewa na kumuuliza habari za Iringa.
Bi Wema hakuwa na taarifa za kupotea kwa Roma na kurudi kwake na alijua katika kipindi chote hicho Roma alikuwa Iringa na hakuuliza sana maswali hata alipokuwa akiongea na Edna alijua wapo wote nyumbani.
“Bi Wema ndio nilikuwa nikija kwako”
“Oh!.. ndio nakuja nyumbani , Qiang Xi amenitangulia , tulipanga kusafisha mazingira ya nje leo kwenye bustani”Aliongea na sasa Roma kuelewa na aliona hana haja ya kuendelea na safari bali aligeuza na kufungua gati na kuingia ndani akitangulizana na Bi Wema.
Nyumba ilikuwa imepooza mno , lakini licha ya hivyo ni kama kuna watu waliokuwa wakiishi , mazigira yake hayakuwa ya kipweke sana , hata hivyo hawakuwa wameondoka kwa muda mrefu , ilikuwa ni kama mwezi na siku kadhaa tokea waondoke kuelekea Iringa.
Roma mara baada ya kuona hakukuwa na mabadiliko makubwa zaidi ya nyasi ambazo hazikukaa vizuri aliiingia hadi ndani na ile anafika sebuleni aliweza kumuona Qiang Xi akielekea jikoni akiwa ameshikilia beseni.
“Mr Roma karibu nyumbani”Aliongea Qiang kwa lugha ya kiswahili ilioathiriwa na lugha ya kichina , Roma hakushngazwa na Qiang Xi kuongea lugha ya kisawahili hata hivyo alikuwa ameishi Tanzania kwa muda mrefu hivyo inaleta maana kuanza kuelewa kuongea.






SEHEMU YA 627.
Roma alijikuta akiishia kumwangalia Qiang Xi kwa macho ya kiuchnguzi , ukweli ni kwamba kutokana na upole aliokuwa nao ilikuwa ngumu kusema Qiang alikuwa mtu mbaya.
Baada ya Roma kuongea kidogo na Bi Wema alimwambia Qiang Xi amfuate kuelekea juu ana maongezi na yeye.
Bi Wema kidogo alishangazwa na jambo hilo kwani Roma alionekana kuwa siriasi lakini hakutaka kuuliza wala kujua nini kinachoendelea zaidi ya kujiweka bize kwa kile kilichomleta asubuhi ndani ya nyumba hio.
Upande wa Qiang alimkabidhi Bi Wema Beseni alilokuwa ameshikilia na kisha alipandisha juu kumfuata Roma pasipo ya kuwa na wasiwasi.
“Qiang , babu yake Lanlan kuna chochote ambacho alikuagiza baada ya kukuambia umlete Lanlan kwetu ?”Aliuliza Roma mara baada ya Qiang Xi kuingia katika chumba cha kujisomea cha Edna.
Swali la Roma lilimfanya Qiang Xi kushituka kidogo lakini alijituliza na kumwangalia Roma.
“Mr Roma sijajua ni nini unataka kumaanisha”
“Ni kweli huelewi ni nini namaanisha?”Aliuliza Roma huku sauti yake ikiwa juu kidogo.
“Sijui ndio..”
Aliongea na Roma palepale alitoa ule ushanga kama Rozari aliopewa na Master Chi akipewa maagizo kumpatia Lanlan kwani angeikumbuka na kumuonyesha Qiang Xi.
“Ushanga wa Master!!!, Mr Roma umezipatia wapi , umekutana na Master?”Aliuliza kwa mshangao huku macho yake yakichanua.
“Hio sio pointi , ninachotaka kusikia kutoka kwako ni barua ulioachiwa na Master Chi iko wapi pamoja na kithibitisho cha Lanlan kuwa binti yangu?”Aliuliza Roma na swali lake lilikuwa bomu kwaQiang Xi na palepale alijikuta mwili wake ukipauka kwa hofu na kuanza kutetemeka.
“Mr Roma , naomba unisikilize…”
“Viko wapi?”Aliongea Roma huku hasira zikianza kumpanda na palepale Qiang Xi akiwa anatetemeka na machozi yakianza kumvaa alijikuta akipiga magoti mbele ya Roma.
“Mr Roma , tafadhari naomba usikilize maelezo yangu , nilikuwa na sababu”
Roma alijikuta akimwangalia , licha ya kwamba alikuwa akitia huruma lakini bado hakuweza kupungza hasira zake mara baada ya kushikwa na hatia ya kuishi na Lanlan muda mrefu pasipo ya kufahamu ni binti yake.
Kwa wenza wa kawaida pengine kuambiana wanapendana ni jambo la kawaida lakini upande wa Roma na Seventeen ambao maisha yao yalikuwa ni ya kupambania maisha yao hawakupata muda hata wa kuelezana ni kwa namna gani wanapendana lakini licha ya yote hayo hisia zao ziliongea mpaka kufanikisha kupata mtoto , hisia zao za pamoja zilikuwa zimetengeneza mizizi ambayo ilikuwa ngumu kung’olewa.
Roma alijiambia pengine Qiang Xi ana bahati , kama jambo hilo lingetokea miaka kadhaa nyuma akiwa na ukichaa wake basi asingeweza kumpa hata nafasi ya kujielezea na muda huo angekuwa ashamuua.
Alijitahidi kuzuia hasira zake na kumwangalia Qiang Xi aliekuwa akitia hruma na kisha akavuta pumzi nyingi na kuzishusha.
“Niambie sababu zako”Aliongea Roma na palepale Qiang Xi alijikuta akishukuru na kufuta machozi yake na mkono
“Mr Roma ninaweza kusema kwamba wewe sio binadamu wa kawaida na hata sasa kwa wakati wote ambao nimeweza kuishi ndani ya hii nyumba naweza kusema wewe ni mungu mtu , kama ilivyokuwa kwa Master, na siwezi kuthubutu kufanya kinyume na maagizo yenu”
“Huwezi kuthubutu , ulinifanya niwe gizani kwa muda mrefu na pengine usingeniambia kama tu nisingekutana na Master”
“Hapana Mr Roma , najua nilifanya makosa lakini nilifanya hivi kwa ajili ya familia yako , kwa ajili yako , Madam na Lanlan”
“Usije kujaribu kunifanyia hila , unadhani mimi ni mwepesi kudanganyika”
“Siwezi kuthubutu , sina uelewa mkubwa na mimi sio msomi na niliacha masomo nikiwa primary tu, hakukuwa na faida yoyote kwa upande wangu miimi kukaa kimya”
“Kama ni hivyo kwanini hukuniambia”
“Nitakuambia kila kitu na sitothubutu kukuficha tena , niliangalia barua aliondika Master mara baada ya kuhisi hatari ya anachotaka kufanya .. nilifanya yote hayo kujua ni wapi anaenda , Master ni mtu ambaye aliniokoa nikiwa hatarini hivyo aligeuka kuwa wa thamani kwangu , hivyo yote nilifanya kuweza kupata kujua ni nini anapanga kufanya ,,, sikujua barua hio ilikuwa ikihusiana na wazazi wa Lanlan”
“Barua iko wapi pamoja na kisu ulichopewa?”Aliuliza Roma akiwa katika mwonekano ambao ni ngumu kujua anafikiria nini.
Qiang Xi mara baada ya kuulizwa swali lile aliwaza kidogo na kisha akasimama na kukimbilia nje na dakika kadhaa aliweza kurudi akiwa ameshikilia kipande cha kisu lakini mkono wa kulia alikuwa ameshikilia simu.
“Mr Roma naomba msamaha wako , barua sikuweza kuitunza lakini nilifanikiwa kui’scan’ kwa kutumia simu …”Aliongea huku akitetemeka.
Roma alimwangalia kwa hasira na kisha akapokea kile kisu na kisha akachukua simu ya Qiang Xi .
Roma alikuwa amezindiwa na hisia za huzuni wakati akiangalia kisu ambacho kipo mikononi mwake , kilikuwa ni kisu ambacho kimefungwa fungwa katika kitambaa cha rangi ya bluu cha hariri.
Hakikuwa kisu cha thamani kubwa lakini historia yake ndio ilimfanya Roma kuona kisu hicho kama cha thamani kubwa kwani mara baada tu ya kukiona mawazo yake yalisafiri miaka mingi iliopita.
Haikueleweka Qiang Xi alitoa wapi akili ya kuiscan barua alioachiwa na Master Chi na kuihifadhi kwa mfumo wa PDF , katika hali kama hio alishukuru kufanya hivyo.
Roma licha ya kukasirishwa na jambo hilo lakini aliishia kusoma barua hio mwanzo hadi mwisho na kila kitu kilikuwa sawa na alivyoelezwa na Master Chi namna ambavyo amekutana na Seventeen na kumuacha Lanlan , Master Chi mwishonni kabisa alikuwa ameandika maneno ya Codes ambayo Roma mara baada ya kuyasoma aliwweza kuyaelewa , yalikuwa ni maneno ambayo ni sawa na ‘signature’ ya barua hio kutbitisha kama yeye ndio ambae aliandika , hakuacha pia kumuusia kuhusu uwepo wa maadui wanaowinda mbinu ya kimaandiko ya urejesho.
“Mr Roma naomba unisamehe , sikuweza kukupatia barua hio na kufanya kama nilivyoagizwa kwani nilijua ukweli wote”
“Kwanini?”
“Mr Roma nimeishi kwa kumlea Lanlan kwa muda mrefu sana mpaka siku ambayo tuliweza kukutana na ninyi , tokea nimeanza kumlea Lanlan nilimchukulia kama binti yangu wa kumzaa lakini kwa upande wake hakuacha kumuulizia mama yake na baba yake , tuliweza kusafiri pamoja huku na kule tukiwa na Master , licha ya kwamba Master alikuwa akimpenda sana Lanlan na kumjali lakini bado Lanlan hakuacha kuulizia kuhusu wazazi wake kila mara alipoweza kuona watoto wakiongozana na wazazi wao , iliniumiza sana kipindi hicho kumuona Lanlan akiwa ni mwenye huzuni ya kukosa wazazi kama watoto wengine , alikuwa ni mtoto wa kipekee na watoto wa aina yake ambao wana akili na nguvu mara nyingi maisha yao huishia kuwa ya upweke , pengine angalau angezaliwa katika familia ya kawaida lakini kipindi hicho hakuwa hata na wazazi , hakuweza kupata kujua nini maana ya mapenzi ya wazazi , hakujua kama wazazi wake walikuwa wanaishi na aliishia kuwaonea watoto wengine wivu..”
“Mr Roma tokea siku ya kwanza Lanlan kumuona Miss Edna , kila siku alikuwa akienda kukaa pale nje ya geti akisubiria kumuona tena , kwa mara ya kwanza tokea nimlee niliweza kuona furaha yake , aliniambia ameweza kumpata mama yake lakini anaogopa ataondoka tena kwasababu hakuwa akimpenda , alikuwa akitia huruma sana na iliniumiza kumuona vile , bahati nzuri Miss Edna akatokea kumpenda Lanlan na kuanza kufikiria kumuasili , Lanlan alikuwa na furaha sana na kwa mara ya kwanza nilimuona akiwa katika hali ya kuridhika .. najua Miss Edna anaweza akafanana na mama yake mzazi lakini mimi kama mwanamke niliweza kuhisi Edna alikuwa akimjali sana Lanlan , alikuwa akimpenda kwa moyo wake wote kama mzazi na swala hilo lilinifanya niridhike na kutotaka kitu kingine zaidi , Lanlan hakuwa akipenda kulala kabisa nilipokuwa naishi nae lakini mara baada ya Madam kuja kwenye maisha yake alianza kulala vizuri na hashituki shituki usiku”Qiang Xi alijitahidi kujielezea , alionekana hakuwa akidanganya , alionekana alikuwa akijali furaha ya Lanlan.
Roma alijikuta akikumbuka namna Lanlan anavyolala na kujikuta moyo wake ukiwa wa moto.
“Mr Roma sijaishi kwenye familia yenu kwa muda mrefu lakini ninawashukuru sasa wewe na Miss Edna , Madam Blandina na Bi Wema na wengine wote ambao ni wazuri kwangu , mimi ni mgeni ndani ya taifa hili lakini niliamua kubakia hapa kwa ajili ya kuendelea kumuona Lanlan.. nashukuru hakuna ambaye amenibagua licha ya kwamba mimi sio wa taifa hili … Sikutaka kukuambia ukweli kwasababu niliogopa familia yako inaweza kuingia kwenye migogoro ambayo inaweza kuwa mikubwa kiasi cha kutengana na athari zikampata Lanlan , najua Miss Edna bado hayupo tayari kuwakubari wanawake wengine lakini hisia zao kwako ni za kweli na wewe ulikuwa ukijaribu kuimarisha familia yako kwa kujitahidi kumbembeleza mkeo ..
“Mimi si kitu , sijasoma lakini nilichotaka ni kumuona Lanlan akiwa na maisha mazuri , nilikuwa nikitaka kumuona akikua kwenye familia yenye furaha na upendo , nilikuwa mbinafsi ndio maana sikutaka kuondoka kwenye hii familia lakini …”Alijikuta akitoa kilio cha kwikwi.
Qiang Xi alijitahidi kujitetea na maneno yake kwa uzoefu wa Roma aliona hayakuwa na walakini , alionekana dhamira yake ilikuwa wazi , alichokuwa akitaka ni kumuona Lanlan akipata malezi stahiki.
Upande wa Roma aliona pengine ingekuwa sawa kama Lanlan angezaliwa na mwanamke mwingine , lakini Lanlan mama yake alikuwa ni Seventeen ambaye Edna anamchukulia kama mshindani wake.
Seveenteen alikuwa ameondoka moja kwa moja lakini kubaki kwa Lanlan kungemfanya kumkumbuka mara kwa mara.
Roma alijua Edna ni mtu ambae ana hasira za haraka ni ni mwepesi kubadilika na asingeweza kupotezea swala hilo kirahisi , pengine angeweza kumvumilia kwa kuwa na wanawake wengine nje lakini sio swala la Roma kuwa na mtu mwingine anaempenda zaidi yake.
Edna alikuwa akimvumilia Roma na kuendela kuishi nae kwa kujua kwamba ni yeye pekee ndio ambaye alikuwa akipendwa zaidi ya wengine wote.
Upande wa Roma aliona pengine Qiang Xi yupo sahihi , kama angejua mapema Lanlan ni binti yake kabla hata mahusiano yake na Edna kuimarika pengine maisha yake yangekuwa tofauti na sasa;.
Licha ya Roma kufikiria mengi lakini ni kwamba kwa wakati huo alikuwa akijua ukweli wote na asingeweza kwenda kinyume na hitajio la Seventeen la kumtambua Lanlan.
Roma mara baada ya kufikiria kwa muda aliishia kumwambia Qiang kwamba asimame na swala hilo alifanye siri mpaka atakapo mpa ruhusa ya kuongea na asiwe na hofu tena na aendelee kuishi nao na iang Xi alishukuru sana huku furaha yake ikionekana.
Mchina huyu alionekana kupenda mazingira ya Tanzania na katika kujitetea kwake alisema alikuwa Yatima huko kwao China na mara baada ya kukutana na Master Chi pamoja na Lanlan wakawa ni kama ndugu zake , sasa Master Chi ameondoka na Lanlan ameweza kumpata baba yake hivyo kama angerudi China ilikuwa ni kwenda kuanza moja, hivyo familia pekee alioona inamfaa ni ya Roma.
Alipenda wanafamilia hao walivyokuwa wakimjali mpaka kufikia hatua ya kumfundisha tamaduni za kitanzania na alikuwa ameridhika.
Roma akili yake ilikuwa imemjaa , alishindwa hata kujua ni kipi ambacho anapaswa kufanya kwa muda huo kwani kila kitu ni kama kipo hatarini kama ukweli utawekwa wazi alihofia familia yake kuvunjika , alihofia mapenzi yake kufikia tamati, dhamiri yake ilikuwa ikimsuta kwa wakati mmoja.
Roma mara baada ya kushuka chini aliweza kukutana na Bi Wema na kumpa maelezo kwamba yeye na Edna wangerudi januari baada ya mwaka mpya hivyo kama kuna tatizo lolote asisite kumpigia simu na Bi Wema hakuona tatizo na alikubali.
Roma siku hio hio alipanga kurudi Iringa , hakutaka kukutana na warembo wake kwani akili yake haikua sawa lakini hata hivyo alisita kuanza safari moja kwa moja kwani wakati akiwa njiani aliweka miadi ya kuonana na Najma nyumbani kwao kwani Juma alikuwa na sherehe ndogo ya kumtoa mtoto wake mara baada ya kutimiza siku arobaini.
Roma mara baada ya kukumbuka ahadi yake palepale alizama kwenye gereji yao ya magari na ksiha akatoka na Lexus na kuianza safari ya kuelekea Mbagala.
Hakuona haja ya kuwasiliana na Najma kwani walipanga kuonana huko huko yeye akishatoka kazini hivyo aliunganisha.
Ilikuwa mchana hivyo msongamano wa magari ulikuwa mdogo na aliweza kutumia dakika chache tu kufika Rangi tatu mbagala na kuchukua njia iliokuwa ikielekea Bias.
Alikuwa ameikumbuka hio mitaa , alikuwa na muda mrefu kidogo hajawahi kufika tokea mara ya mwisho kuja kujitambulisha mbele ya wanafamilia kama mchumba wa Najma na ilimshangaza kuona njia hio ilikuwa imewekwa rami yote na kupendeza tofauti na mwanzo.
Roma mara baada ya kukaribia karibu na nyumba ya Juma aliweza kuona gari zuri ya bei ghali aina ya Lamborgin ikisimama nje ya geti la nyumba ya Juma , mwanzoni wakati gari hio ilivyokuwa mbele aliishia kutoa tabasamu la uchungu kwa kujiambia magari hayo kuwepo Tanzania ni kama uharibifu wa hela kutokana na aina ya barabara kutoruhusu lakini mara baadda ya gari hio kusimama nje ya geti la nyumba ya Juma alijikuta akishikwa na shauku kubwa zaidi ya kumuona mmiliki.
Ni ndani ya dakika moja tu badala ya gari hio kusimama , ikiwa imekodolewa macho na watu wengi wa mtaa hio , hatimae aliweza kushuka mwanaume mtanashati aliekuwa amevalia suti nyeusi na kufungua mlango wa mbele kushoto na kisha alionekana mwanamke mrembo alievalia hijabu akishuka.
Roma aliishia kuguna mara baada ya kugundua mwanamke alieshuka kwenye gari hio alikuwa ni Najma.







SEHEMU YA 628.
Tokea kurudi kwa Najma ncini Tanzania na kuanza kufanya kazi wizarani alikuwa na mabadiliko makubwa , alikuwa ametoka katika usichana na kuwa mwanamke sasa ambaye alikuwa tamanio la wanaume wengi.
Najma alionekana kutotaka kumkaribisha mgeni aliemleta kwani alionyesha ishara ya kuaga ili kuingia ndani , lakini yule mwanaume alimzuia akionyesha kama vile kuna kitu anataka kuongea nae.
Hali hio ilimfanya Roma kuona pengine mwanaume huyo alikuwa katika harakati za kumpata Najma.
Alifikiria hivyo kwani hakuamini Najma ni mwanamke mwepesi ambaye anaweza kumsaliti , lakini licha ya hivyo hali ile haikumfanya kuwa katika hali ya utulivu na alizima gari yake na kisha akatoka nje na kisha akailoki na kuanza kupiga hatua kuwasogelea.
Roma mara baada ya kusogea karibu zaidi ndio sasa aliweza kumuona mwaname mwenyewe ambaye alionekana kuwa na pesa mpaka kumiliki gari kali la namna hio.
Alikuwa ni kijana mrefu wa saizi ya kati ambaye alikuwa na sura ya kihandsome kumzidi yeye na kwa haraka haraka alimkadira umri wa miaka yake inaweza kuwa ishirini na tano kuendelea..
Alikuwa akivutia kwani alionekana ni mtu wa mazoezi na kubwa zaidi alionekana kujiamini , pengine ni haki yake kuweza kumtongoza mwanamke mrembo kama Najma kwani kimuonekano ni sawa na kusema wanaendana.
Roma macho yake ya haraka haraka yaliweza kumkagua kwanzia suti yake ya Versace , viatu vya kung’aa vilivyoendana na mavazi yake pamoja na muonekano.
Upande wa Roma wakati huo alikuwa amevalia kikawaida sana, shati la mikono mirefu la drafti ya rangi ya kijani na nyeusi, jeans nyeusi pamoja na Moka na saa ya bei ghali alionunuliwa kama zawadi na Edna.
“Mheshimiwa nadhanni leo sio muda mzuri , unaonaje tukaweka miadi siku nyingine , naomba unisamehe..”Aliongea Najma huku akiwa kama mwanamke anaemkataa mtu kistaarabu.
“Najma nishakuambia uniite kwa jina langu tu inatosha , ila kwanini leo isiwe muda mzuri,isitoshe sio kama ni mara ya kwanza kukutana na kaka yako pamoja na ndugu zako , nina shauku pia ya kumuona mwanaume ambaye unatoka nae , hujawahi kuwa hivi leo umebadilika sana”
“Si..”
Najma alitaka kuongea lakini palepale alijikuta akiishia njiani mara baada ya kumuona Roma akiwasogelea na macho yake yalichanua huku furaha yake ikiupamba uso wake.
“Roma!!”
Roma alitembea na kumsogelea Najma huku akimpotezea mwanaume alieitwa mheshimiwa na kisha akamkumbatia na kumpiga Najma busu la Shavuni.
Kwa wakati huo Roma alitaka kwenda mbali zaidi na kumbusu mdomoni lakini alimheshimu Najma kutokana na watu wengi walikuwa wakiwaangalia.
Kitendo cha Najma kukumbatiwa kwa haraka hivyo mbele ya watu kidogo tu adondoshe pochi yake lakini aliishia kufurahi mara baada ya kuona Roma alikuwa na wivu na yeye.
Upande wa mwanaume alieitwa Mheshimiwa na yeye hakujali kitendo cha Roma cha ghafla bali alikuwa akimwangalia Najma na kwa uzoefu wake aliweza kuona Najma alionekana alikuwa amependa kweli na hata matumani yake kushuka zaidi na zaidi.
Jambo hilo lilimkasirisha mno kwani ni zaidi ya mwezi tokea aanze kumchombeza mrembo Najma amkubalie hata kumuahidi ndoa moja kwa moja .
Bahati tu ni kwamba alikuwa mzoefu kwani palepale alipotezea hasira zake za kupokonywa tonge mdomoni na mwanaume ambaye alikuwa na mwonekano wa kawaida kabisa.
“Babe huyu mwanaume ndio nani?”Aliuliza Roma huku akimwachia Najma na kujifanyisha ndio eti anamuona huyo mwanaume .
“Huyu ni naibu waziri wa elimu , Mr Salihi Ibuyawanga nilikuwa nikisubiria Uber ili kuanza safari ya kuja huku na aliniona na kunipa lift”Aliongea Najma kwa sauti ya chini.
Roma alishangazwa na maneno ya Najma kidogo , mwanaume aliekuwa mbele yake alikuwa ni mdogo mno kimuonekano lakini alikuwa ni Naibu waziri, alijiuliza ni kipi amefanya mpaka kuaminiwa kwa umri wake huo.
Roma pia aliona mwanaume huyo hakuwa wa kawaida maana kama kweli kazi yake pekee ni ya Unaibu waziri asingeweza kuendesha gari ya gharama kiasi hicho.
“Mr Roma , wewe ndio boyfriend wa Najma?”Aliuliza yule mwanaume , alionekana alikuwa akilijua jina la Roma pengine ni mara baada ya Najma kulitamka.
“Hapana sio sahihi kusema boyfriend , mimi ndio mwanaume wake”Alijibu.
“Oh ! kwahio unamaanisha umemuoa?”Aliuliza bwana Salihi.
Ukweli ni kwamba alishafanya uchunguzi kuhusu Najma na alishangazwa kwa kuona kwamba Najma hakuwa na skendo nyingi hata kipindi alichokuwa anasoma na jambo hilo ndio lilipa motisha ya kutaka kuwa nae karibu zaidi.
“Bado hatujafunga ndoa lakini nnitaendelea kumpenda mpaka siku ambayo yeye mwenyewe ataacha kunipenda”Alijiibu Roma kwa kujiamini.
Upande wa Najma alijikuta akiguswa na jibu la Roma lakini kwa wakati mmoja akiona aibu na alijiambia anawezaje kumuacha ilihali alimpigania kumpata kwa muda mrefu kiasi hicho.
“Hahaha.. wewe ni noma , kila mwanaume anahaki ya kutoka kimapenzi na mwanamke mrembo kama Najma, ila kwasababu hujamuoa natumaini huwezi kutuingilia sana kwani sitaki tuwe na wakati mgumu ilihali ndio mara yetu ya kwanza kukutana , kwasasa kuna maswala napaswa kuyashughulikia hivyo nitaondoka , natumaini tutaonana tena”Aliongea huku akimwangalia Roma kwa tabasamu ambalo limejaa kebehi na kisha akamgeukia Najma.
“Najma msalimie Shangazi na kaka yako Juma , nitawatembelea muda wowote m tafadhari naomba usinikatalie utaumiza nia utu wangu”
Mheshimiwa Salih hakusubiri jibu kutoka kwa Najma kwani palepale aliingia kwenye gari yake na kuigeuza kwa tambo na kuondoka.
Upande wa Roma alijikuta akiguswa na maneno ya kiuchokozi ya Salihi na alitamani kuipiga teke gari yake na kuiharibu palepale , lakini alijitahidi kujizuia.
“Najma ni kwa muda gani amekuwa akikusumbua?”Aliuliza Roma huku akijitahidi kujituliza na Najma alitoa kicheko cha utani kutokana na namna Roma alivyyobadilika.
“Sikuweza kufanya chochote , yeye ndio mkuu wangu wa kazi na nisingeweza kumkataa bila ustaarabu kwani ningefanya mazingira ya kazini kuwa magumu , naogopa pia kupoteza kazi yangu kwani mama ndio kanisaidia”
“Hilo sio tatizo , ninaweza kukuhamishia wizara nyingine kama anakuchukiza”Aliongea Roma kama vile yeye ndio raisi wa nchi.
“Hapana napenda nafasi yangu ya kazi kwa sasa kwani inaendana na nilichosomea na isitoshe unaweza kunihamishia sehemu nyingine na nikakutana na wanaume wengine ambao wananitaka , ni bora nilipo kwasasa kwani waziri Salihi kuonyesha kunitaka kumewafanya wengine wote kutothubutu kunisogelea”
Roma alijikuta akihema ndani kwa ndani na kujiambia Najma asingeacha kutongozwa kwani hakuwa amemuoa , ni swala ambalo halikuwa likiepukika labda tu aachane na maswala ya kazi.
Roma aliishia kukosa chaguo lingine na kuona ni kheri atulie tu licha ya kwamba hakupenda mwanamke wake kusumbuliwa kama hivyo.
“Babe naomba usiwe na wasiwasi , niamini mimi hakuna kitu ambacho kinaweza kutokea kati yetu , natembelea tu upepo kwa sasa , mwanaume wa aina yake ni wale ambao sio wavumilivu na muda wowote atajikatia tamaa , isitoshe kuna samaki wengi ziwani wa kuvua , pengine amevutiwa na mimi kwa muda tu na muda si mrefu anaweza kuona samaki mwingine, isitoshe tetesi ninazosikia anaweza kupandishwa cheo muda si mrefu”Aliongea Najma na kumfanya Roma kuguna.
“Familia yake ikoje , bado anaonekana mdogo na nafasi yake ni kubwa na unasema atapandishwa cheo?”
“Sijafatilia sana ila kwa ninavyosikia ni kwamba baba yake ni mfanyabiashara na kipindi ambacho raisi Senga yupo kwenye harakati za kampeni alisaidia kwa kiasi kikubwa kwenye kumfadhili , licha ya hivyo nasikia ametoka na GPA ya kwanza kutoka chuo cha Yale Marekani , hivyo ni sawa na kusema nafasi yake inalingana na elimu yake , ni mtu mwenye malengo na elimu ya Tanzania , mheshimiwa amemuweka kama naibu waziri mara baada ya kumpatia ubunge kutokana na mawazo yake ya kutaka kubadilisha mtaala wa elimu wa Tanzania ambao hauendani na kasi ya teknolojia hivyo inaaminika ili malengo yake kutimia atapandishwa cheo na kuwa waziri kamili au katibu mkuu wa Wizara , hizo ni fununu tu”Aliongea Najma kwa kirefu.
Ilikuwa ni kama Roma alivyotegemea , lakini hata hivyo alijiambia Najma hawezi kumuacha yeye na kwenda kwa ndugu naibu waziri Salihi.
Baada ya kuongea kwa dakika chache wakiwa pembeni ya geti Najma aliweza kuitwa na mwanamke ambaye Roma alimtambua ni shangazi yake na wote kwa pamoja waliona wasitishe mazungumzo na kuingia ndani.
Roma mara baada ya kuingia ndani aliweza kupokelewa na Juma ambaye alikuwa amevalia kanzu.
Mazingira ya nyumba ya Juma yalikuwa yamebadilika mno na kwa haraka haraka Roma aliamini nyumba haikuwa ikipangishwa tena kwani ilifanyiwa usafi kuanzia nje mpaka ndani na hata chumba chake cha kihistoria kilikuwa kimebadilishwa muonekano.
Sherehe ilionekana haijaanza bado na kuna wanawake wengi waliokuwa ndani ya geti wakionekana kuwa bize na mapishi , hata hivyo ilileta maana kwani muda ulikuwa ni saa nne za asubuhi kwenda saa tano.
“Bro..!!”Juma aliita huku akiweka tabasamu bashasha huku wakipeana kumbatio ambalo waswahili wa mtaani wanasema ni la kisela.
“Mazingira yamebadilika sana , naona hata room yangu imebadilika kimuonekano”
“Hahaha.. upo sahihi shem , kudra za mwenyezi Mungu zimefanya haya yote kuwezekana, karibu sana bro nyumbani , nilikuwa nikiona kila kinachoendelea hapo nje ila nilitulia kwanza muyamalize hahaha..”
“Hahaha.. kumbe ulikuwa ukituona?”
“Ndio nakuambia hivyo ndugu yangu , unapaswa kuchukua hatua mapema Najma anazidi kuwa maarufu na hadhi yake imepanda”
“Kwa maneno yako , inaonyesha sio mara ya kwanza kuletwa na gari?”Aliuiza Roma mara baada ya kukaa kwenye kiti cha plastiki chini ya turubai.
“Siwezi kusema ni mara nyingi kwani muda mwingine analala huko kwenye apartment yake , ila naweza kusema kila wakati anaokuja anaongozana na Naibu waziri , nadhani pia shida ya usafiri unachangia”Aliongea na kumfanya Roma aone tatizo lipo wapi na alitamani kujipiga kibao.
Aliweza kumsaidia Najma kupanga kwenye Apartment lakini akasahau kitu muhimu sana kumpatia,
Hakukumbuka kumnunulia gari , isitoshe Najma hadhi yake ilikuwa ya juu hivyo asingeweza kupanda daladala ,pengine pia Najma alihitaji usafiri lakini alishindwa kumwambia.
Roma palepale aliona hili haliwezi kuendelea hivi , ngoja atumie upluto wake kuhakikisha gari inasafirishwa hata kwa ndege kuja Tanzania.
Palepale alimwita Najma huku akiingia mtandaoni na kutafuta picha za magari tofauti tofauti ili kumuonyesha ni aina gani anapenda amuagizie.
ITAENDELEA KUHUSU SIKU NO PROMISE'S
 
Hapo ndipo anapokosea, wadau au wateja hawakomeshwi isipokuwa anajiharibia mwenyewe coz;
1. Anaonekana he is not a man of his words(haaminiki) kwa hiyo jihadharini na mtu wa namna hii ipo siku mtalia.
2. Hajui kupanga ratiba yake.
3. Si mtu wa kujali hisia za wengine au ana majivuno na haonekani kujutia kwa mambo madogomadogo.
4. All in all mimi ndo naacha kufuatilia story yake maana lengo ilikuwa kupata burudani na si karaha. (Tafuteni mbadala).
5. Wengine hatukushindwa kununua hii story isipokuwa tulikuwa tunajiuliza je pesa yetu inakwenda kwa mtu sahihi au ndo wale wa story zisizoisha?.(Mtu aliyeng'atwa na nyoka hata akiona ung'ong'o hushituka). Bye


Sent using Jamii Forums mobile app
Mm siachi nipo hapa hapa till the end
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom