Simulizi: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student)

RIWAYA:MWANAFUNZI MCHAWI - SEHEMU YA 39

...."Ina maana Doreen ni mchawi kiasi hiki?" Alijikuta anaropoka kwa mshangao mama Pamela. Pamela alizidi kushangaa huku akimtazama mama yake kwa mshangao kisha akimtazama chatu yule mwenye sura ya Doreen. Baba Pamela aliendelea na maombezi yake kwa imani kali. Yule chatu alijigeuza geuza kwa vitisho vikali sana huku akijaribu kupambana Na Baba Pamela kwa kujitoa kwenye lile shimo dogo.

Lakini kwa bahati njema chatu yule alipigwa na radi Kali sana iliyoharibu uso wake na kuweka mipasukopasuko iliyoacha damu ichuruzike kirahisi. Baba Pamela hakuacha kuomba na kuithibitisha imani yake thabiti. Ghafla ukatoka moshi mkali kutoka kwenye mdomo wa sura ya Doreen iliyopo kwa yule chatu.

Moshi ule ulikuwa wa ajabu sana Kwani ulikuwa katika mstari ulionyooka mpaka kifuani kwa Pamela, na hata Pamela alipojaribu kukimbia moshi ule ulimfuata kila alipoenda na kumfanya Pamela aogope zaidi. Pamela alipoona hawezi kuukwepa moshi ule akasimama wima akisubiri kuona kitakachotokea huku akihema nguvu sana.

Moshi ule ulitua taratibu kifuani kwa Pamela kisha ule mstari uliokuwa umejitengeneza ukapotelea kifuani kwa Pamela taratibu sana. Pamela alijishangaa sana Kwani alihisi mabadiliko Fulani mwilini mwake. Alitulia kimya huku akimtazama baba yake.

Baba Pamela alipohitimisha maombi yake yule chatu alipigwa radi Kali kisha akatoweka machoni kwa wanafamilia wale.

"Jina la Bwana lihimidiwe kwani ametenda tulichokitaka.. Amejidhihirisha mbele yetu.. Oh asante Bwana wa Majeshi" alisikika baba Pamela huku akiinua macho yake na mikono yake juu ili kumshukuru Mungu kwa ajili ya maombi yake.
"Pamela hebu jitazame kifuani kwako" alisema Baba Pamela huku akitabasamu na kutoa kitambaa laini mfukoni na kujifuta jasho lililokuwa limetapakaa usoni kwake kama chemchem ya maji.

Mama Pamela alimsogelea mwanae na kumsaidia kushuhudia kilichotokea kifuani kwake. Walisogea pembeni kidogo, kisha Pamela akajifunua shati lake na kujitazama kwa umakini. Wote hawakuamini kilichotokea kwani titi lake lilikuwa limerudi kama lilivyokuwa. Pamela alishtuka sana na kupiga kelele za shangwe huku akiruka kama ndama. Akamkimbilia baba yake na kumkumbatia kwa nguvu.

"Baba! Nashukuru baba! Asante!" Alisema Pamela kwa furaha kuzidi kiasi.
"No Pamela! Mshukuru Mungu sio mimi" alisema Baba Pamela huku akitabasamu.
Pamela alimuachia baba yake na kumfuata mama yake, chozi likamdondoka kwa uchungu huku akimkumbatia mama yake.
"Nisamehe sana mama! Naomba unisamehe kwa kukufanya ukose amani na kujisikia vibaya kwaajili yangu. Nakupenda sana mama.. Nisamehe mama!" Alisema Pamela huku akilia kwa uchungu.

"Pamela mwanangu! Usijali kwa yote yaliyotokea nilishakusamehe" alisema mama Pamela huku akimkumbatia kwa mahaba mazito binti yake mpenzi.
Baba Pamela alisimama pembeni yao kisha akapiga hatua za taratibu na kuwasogelea.
"Mke wangu... Familia yetu ingekuwa pabaya sana kwaajili ya yule adui! Lakini ni funzo kwako kuwa usimwamini kila mtu pia jifunze kumcha Mungu kwa moyo wote"
"Ashukuriwe Mungu sana! Tangu Leo wote tutamcha Mungu" alisema Mama Pamela.

"Kweli kabisa.. Mungu ni mkuu" alisema Pamela kisha Wote wakakumbatiana kwa furaha, ile furaha ya mwanzo ikawa maradufu. Kila mmoja alionekana kufurahi sana ule umoja uliotaka kuvurugika ukarejea tena katika familia ile ikazidi kung'ara na kuwa familia bora.
"Hakuna wa kumfananisha na Mungu!" Walisema kwa pamoja huku wakiwa na furaha ya ajabu.

*****
Leyla alipokea ugeni kutoka kanisani kwake ambapo wanamaombi watano walitia timu nyumbani kwake na kuiikuta familia ile ikiwa imepoteza furaha kabisa.
Leyla aliwakaribisha wageni wake vizuri na kuwakaribisha viti.

Mwalimu John na Judith walikuwa wapo kimya tu ingawa moyoni mwao walifurahia ujio wa watu wale.
Leyla akaamua kuwaambia kila kitu kilichotokea ndipo Walipoanza maombi yao. Walijtahidi kusali kwa imani kubwa sana. Baada ya maombi ya kama SAA zima ndipo maombi yao yalipoanza kujibiwa. Mambo ya ajabu yalianza kutokea ambApo mwalimu John alianza kuzungumza lakini cha ajabu funza walianza kutoka tena miguuni.
"Kuna mtu ni mchawi hapa" alisema Mwalimu John na kuwafanya wote wastaajabu.
"Tulia mume wangu watu wanakusaidia..." Alisema Leyla akimwambia mumewe.

"Nasema kuna Mtu anaroga hapa... Atoke.." Maneno hayo ya Mwalimu John yaliwafanya wote watazamane na kusitisha maombi kwa muda. Mwalimu John aliendelea kuongea.
"Wewe acha kuroga maombi ya wenzako... Wewe! Nikuseme?" Alisikika mwalimu John wakati huo wote walikuwa wameinamisha sura zao chini wakiogopa kutajwa. Baada ya dakika kadhaa kupita Mwalimu John alimsogelea mwanamke mmoja na kumshika bega.
"Sema ukweli la sivyo hawa funza wanahamia mwilini mwako.." Alisema mwalimu John huku akimkazia macho mwanamke yule.

"Mi..mimi..nime.. Mimi.." Alibabaika yule mwanamke.
"Ukidanganya tu funza wanakuhamia..."
"Ahm..aah.. Kweli.. Nilitaka..nilikuwa naroga msiendelee na maombi.." Alisema yule mwanamke akiwa anaona aibu kupita kiasi.
"Haya tokaa" aliamrisha mwalimu John na yule mwanamke akaondoka haraka huku kila mtu akimtazama kwa mshangao.

Hawakupoteza muda maombi yakaendelea na hawakutumia muda mrefu sana funza kwa mwalimu John wakapotea wote. Na mara ile Judith aliona ulimi wake ukiwa mwepesi sana na akaweza kuongea. Mwalimu John alikuwa kama aliyetoka usingizini alishtuka mno kuona kila kinachoendelea.
"Jamani.. Doreen ulitaka kuniua? Kwanini Doreen?" Alisema mwalimu John.

"Doreen ni nani?" Aliuliza mwanamaombi mmoja.
"Ni mwanafunzi wangu... Ni mchawi sana alitaka kuniua na alinifanyia mambo ya aibu sana" mwalimu John akasimulia kila kitu kuhusu Doreen.
Judithi pia akaeleza kila kitu kilichompata Mwalimu Jason ambaye tayari alishafariki dunia.

"Oh poleni sana watumishi Mungu ni mwema... Cha msingi mumrudie yeye!"
"Amen!"

Hatimaye mwalimu John na Judith wakarudia hali ya kawaida na furaha yao ikarejea tena. Walimshukuru sana Mungu.
Mwalimu John alimsogelea mkewe na kumbatia kwa dhati na upendo.
"Asante kwa upendo wako wa dhati uliokufanya uwe mvumilivu mno kwangu... Nakupenda!" Alisema mwalimu John na Leyla akatabasamu tu.
Wanamaombi wale walishukuru Mungu na kuwasihi familia ile pamoja na Judith kutomuacha Mungu. Kisha wakaondoka zao.

*****

Doreen alipokuwa anakimbia ndivyo kadri kipigo kilipomzidia. Kwani aliadhibiwa sana na Dorice na wakati huohuo Mungu alikmwadhibu kupitia maombi ya watumishi wake waaminifu.

Doreen alihisi mwisho wake umefika. Alilia kwa uchungu huku akipiga hatua za kichovu kuelekea nyumbani kwa kina Eddy kama Alivyoambiwa na Dorice ili akajisalimishe na kuombs msamaha.
Safari ilikuwa ndefu kwa binti yule aliyeuwa watu wengi shuleni kwao na kuwadhuru walimu wake wasiokuwa na hatia.
Hakuwahi kufika nyumbani kwa akina Eddy lakini alifika bila kupenda.
Umati wa watu uliokuwa nyumbani kwa mr Aloyce uliongezeka zaidi baada ya Doreen kufika pale.

Kulizuka hali ya tafrani katika eneo lile.
"Mimi ndo Maimuna halisi... Sio mama Eddy kama ulivyodhani.." Alisema Maimuna akiwa na sura mbaya kupita kiasi. Alikuwa ni mweusi mithili ya mkaa wa chunya, macho makubwa makali, mekundu kama pilipili, alikuwa na tumbo kubwa sana lililojaa michiriz, nywee zilikuwa chafu tena zimesokotana sana huku midomo yake mipana myeusi ikiyasitiri meno yake yaliyokaa hovyohovyo kinyani mwake.

Mr Aloyce aliishiwa nguvu, alishindwa kulia akadhindwa kuongea akabaki kimya amejiinamia.
Ujio wa Doreen na umati mwingine wa watu ukawa utata mwingine kwa Mr Aloyce.
"Nisamehe Eddy..
Alisikika Doreen akilia kwa sauti na wakati huo Eddy alikuwa anatembea taratibu kutokea ndani na kuja kymushuhudia kinachoendelea. Waandishi wa habari walikuwa wengi wakipiga picha tukio lile la ajabu.

Itaendelea....
 
Mbona mnakatisha utamu, raha ya utamu ni ufike mwisho. sa mbona mnakuwa ivo??? Malizieni basi
 
Thursday, July 14, 2016

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi (A Wizard Student) - Sehemu ya 14



...MWALIMU John alijishangaa kupita kiasi kwani miguu yake yote miwili ilikuwa imeoza vibaya. Alikuwa hahisi maumivu yoyote hapo kabla lakini pindi alipojitizama tu alianza kuhisi maumivu makali sana. Punde funza wakaanza kutoka mguuni. Akabaki anajiuliza nini kimetokea bila kujua sababu.

Mkewe na baadhi ya ndugu zake walibaki kimya, wakimtazama Mwalimu John kwa woga.



"Mke wangu bado unaniogopa? Hunionei hata huruma mumeo? Ama kweli mapenzi yapo kwenye raha tu!" Alisema Mwalimu John kwa huzuni iliyochochea huruma nyingi machoni mwa mkewe. Taratibu akaanza kumsogelea mumewe lakini kuna ndugu yake mmoja akata kakumzuia.



"Niache! Nampenda mume wangu ingawa yupo kwenye hali hiyo.." Alisema mke wa mwalimu John huku akimsogelea mumewe kisha akamkumbatia kwa mapenzi mazito, bila kujali hali aliyokuwa nayo mumewe.



"Nakupenda mume wangu.. Nashukuru umeurudia uhai ili tuendelee kuwa pamoja" alisema mwanamke yule huku machozi yakimchuruzika.



"Nakupenda sana mke wangu, nilikuwa nakuwazia sana hali ambayo ungeikabili kama ningekufa.."

"Sijui ningemweleza nini mwanao aliyeko tumboni mwangu!" Walizungumza yote hayo wakiwa bado wamekumbatiana. Maneno ya mke wa Mwalimu John yalimfariji sana John, akahisi kwamba kweli amerudi duniani.


Ndugu walibaki wametumbua macho wakiwatazama wawili wale, hawakuwa na la nyongeza zaidi ya kumkaribisha mwalimu John ambaye hakuweza hata kutembea kutokana na maumivu ya miguu. Funza walizidi kuongezeka miguuni.



"Mke wangu naumwa sana hii miguu, sijui kama itapoa!"

"Usijali itapona tu mume wangu.. Ila naomba unieleze kila kitu kilichokutokea..!" Alisema mke wa mwalimu John huku akimwinua taratibu mumewe pale chini alipokuwa ameketi.

Mwalimu John alilalama sana kutokana na maumivu Yale lakini ikabidi ajikaze mpaka walipoingia ndani.

"Mke wangu Leyla.. Kweli nimeamini unanipenda!"

Leyla akatabasamu na kumbusu mumewe kisha akasema

"Nakupenda sana mume wangu hebu nisimulie imekuwaje..!"

"Ni stori ndefu sana mke wangu..lakini ngoja nikusimulie mbele ya hawa ndugu zangu wote..!"

Wote sebuleni pale walitulia kimya kusikiliza kisa cha ajabu kilichompata Mwalimu John. Lakini cha ajabu Mwalimu John alipotaka kusimulia tu..


*******

Wazazi wa Eddy walichanganyikiwa sana wakahisi mtoto wao mpendwa tayari amefariki dunia. Wakazidi kumtikisatikisa huku mama yake akiushusha mchozi kama maji, ndipo wakagundua Eddy hajafa ila amepoteza fahamu. Kofi alilopigwa halikuwa la mchezo, lilikuwa kama radi ingawa wazazi wake hawakujua kitu.

Na hiyo ilikuwa ni kazi ya mzimu unaomsaidia Doreen.


Mr.Alloyce alitumia nguvu zake zote kumpepea Eddy mpaka alipozinduka. Alikuwa amevimba USO mzima jambo lililowashtua wazazi wake. Wakatazamana kwa nyuso zilizojaa viulizo bila kujua majibu ya uhakika.

"Eddy" Mr.Alloyce aliita.

"Naam!" Eddy aliitikia kwa sauti ya chini.

"Vipi?"

"Nimepigwa!"

"Umepigwa? Umepigwa na nani?"

"Sijui!"

Yote yaliyomtokea Eddy yalibaki kuwa viulizo kwa wazazi wake, yaliibua fumbo ambalo lilikuwa gumu sana kulitatua.

"Baba Eddy"

"Sema mke wangu..!"

"Mi naona twende kwa mganga tu!"

"Wapi?"

"Tanga kwa mganga Tembo wa Bahari.. Umewahi kumsikia?"

"Mmh! Hapana..!"

"Nasikia ni kiboko sana kwani hata Mama Zuwena aliwahi kwenda akasaidiwa!"

Mama Eddy aliamua kumshauri mumewe waende kwa mganga wa kienyeji anaepatikana Pangani Tanga. Mganga Hugo alifahamika kwa jina la Tembo wa Bahari kwani alisifika kwa kutatua matatizo yaliyoshindikana lakini Mr.Alloyce alisitasita kuhusu suala hilo.

"Waganga siwaamini mke wangu..!"

"We unafikiri tutafanyaje sasa! Kama hutaki niachie kila kitu Mimi nitahangaika na mwanangu..!" Mama Eddy alilivalia njuga suala lile hatimaye Mr.Alloyce akaingia laini na kumkubalia mkewe.

"Sawa tutaenda!"

"Twende kesho!"

"Haina shida"


Walikubaliana kuianza safari yao siku ya kesho yake.


Siku ile hawakumsumbua Eddy kwa swali lolote lile, usiku aliingia kulala akiwa bado hana raha kabisa huku akiisubiri siku ya kesho yake ili waende kwa mganga.


Eddy alipojilaza kitandani tu, usingizi mzito ukampitia. Ghafla akamuona Doreen ndotoni akija na kisu kikali sana kinachowaka moto. Eddy aliogopa sana akatamani kuamka lakini akashindwa.

"Eddy ukithubutu kusema lolote kuhusu Mimi utakiona cha moto... Kubwa zaidi ukithubutu kwenda kwa mganga hiki kisu ni halali hapo kifuani pako.. Utakufa!"

Ilisikika sauti ya Doreen ikiongea kwa msisitizo sana huku ikijirudiarudia.


"Mamaaaa!" Eddy alishtuka usingizini na kumwona mama aliyekuwa amelala chumbani kwake ili kujua maendeleo ya Eddy kila wakati.

"Vipi mwanangu?" Mama Eddy alishuka kitandani na kukisogelea kitanda cha Eddy.

"Ndoto mama.. Naogopa!"

"Pole mwanangu.. Usiogope tupo wote humu..! Alisema mama Eddy lakini Eddy bado aliogopa.


Usiku ule ulikuwa mrefu sana kwa Eddy kwani alikumbana na vitisho Vinci kutoka kwa Doreen. Kulipokucha Eddy aliona ahueni kidogo ili aachane na mauza uza ya usiku.


Majira ya SAA kumi na mbili na nusu asubuhi wazazi wa Eddy walikuwa tayari wamejiaandaa. Wakamwamsha Eddy ili anywe chai kisha waanze safari, cha ajabu Eddy aligoma kuondoka.

"Siwezi kwenda kwa mganga! Siendi!"

"Huendi?" Mama Eddy alishtuka

"Siendi mama! Hata kwa greda!"

"Kwanini?"

"Sitaki!"

Eddy aligoma kabisa kuondoka lakini mama yake alimlazimisha na kumweka kwenye gari akisaidiana na baba yake. Safari ikaanza.


********

Doreen aliamua kusubiri usiku uingie ili amfuate Nadia na kumfanyia uchawi wake ili aondoke na ziwa.


Usiku ulipoingia Doreen alikuwa akijipanga kwa kuita mizimu yake yote ili imwongezee nguvu. Alikuwa amejitenga peke yake kwenye kichaka huku akijpakapaka madawa yake ili aongeze nguvu zake za kichawi. Akainuka akiwa uchi huku akijiaminisha kuwa sasa yù kamili. Akatamka maneno yake ya kichawi akatoweka eneo lile..

Muda huo ilikuwa ni saa name usiku.


Akaenda moja kwa moja mpaka bwenini kwa Nadia na kukifikia kitanda chake, mh! Alichokutana nacho hakuamini.. Moto ilikizingira kitanda kizima na hakumuona Nadia Joseph alipo. Akaamua kukisogele kitanda kile taratibu lakini ghafla akapigwa dhoti Kali na kudondoka chini puuuh! Kama mzigo. Na kila alipojaribu kuinuka alishindwa.. Hofu ikamjia akajua tayari amekamatwa kwenye mtego....

Itaendelea....
About time
 
Back
Top Bottom