Siku nilipotoa rushwa

Mwanakijiji,

Mimi jana nimetoa rushwa BRELA, ndio, nasema kweli, hakuna haja ya kuficha wala kuona aibu.

Nimekupata.. nilidhani hapo mwanzo ulikuwa unawajibika wewe mwenyewe. Unajua kitu ambacho nadhani kinasumbua kuhusu hii rushwa ya nyumbani ni kwamba haionekani kuwa ni "adui ya haki" kwa sababu kama ukilipa kitu kidogo unapata unachotaka (kwenye mfano wako faili) na usipolipa inakuwa ni kuzungushana basi mtu anajikuta analipa na hivyo anarahisisha anachokitaka.

Ndio katika minajili hiyo najiuliza tunaweza vipi kushindana na rushwa wakati rushwa inaonekana kana kwamba iko upande wetu?
 
Nimekupata.. nilidhani hapo mwanzo ulikuwa unawajibika wewe mwenyewe. Unajua kitu ambacho nadhani kinasumbua kuhusu hii rushwa ya nyumbani ni kwamba haionekani kuwa ni "adui ya haki" kwa sababu kama ukilipa kitu kidogo unapata unachotaka (kwenye mfano wako faili) na usipolipa inakuwa ni kuzungushana basi mtu anajikuta analipa na hivyo anarahisisha anachokitaka.

Ndio katika minajili hiyo najiuliza tunaweza vipi kushindana na rushwa wakati rushwa inaonekana kana kwamba iko upande wetu?

Mwanakijiji,

Tatizo hapo ni kwamba wakati wewe unatoa pesa na kupata huduma vipi Mtanzania ambaye hana kitu?

Mimi siwalaumu watu ambao wanabanwa mpaka inabidi watoe pesa, huko ni sawa na kunyang'anywa.

Ninaowalaumu ni wale wanaotangulia kutoa rushwa mbele na pia wale malaya ambao hawatimizi wajibu wao mpaka wapewe chochote. Hawa wawili inatakiwa waadhibiwe sawa kwenye sheria.

Rushwa inaweza kukomeshwa kama wahusika wataamua kufanya kazi. Tunahitaji process ambayo inaweza kutambua mianya ya rushwa mapema sana.
 
Mwanakijiji,

Tatizo hapo ni kwamba wakati wewe unatoa pesa na kupata huduma vipi Mtanzania ambaye hana kitu?

Mimi siwalaumu watu ambao wanabanwa mpaka inabidi watoe pesa, huko ni sawa na kunyang'anywa.

Ninaowalaumu ni wale wanaotangulia kutoa rushwa mbele na pia wale malaya ambao hawatimizi wajibu wao mpaka wapewe chochote. Hawa wawili inatakiwa waadhibiwe sawa kwenye sheria.

Rushwa inaweza kukomeshwa kama wahusika wataamua kufanya kazi. Tunahitaji process ambayo inaweza kutambua mianya ya rushwa mapema sana.


Mkuu Mtanzania...hapa una maana gani..ili tuweze kuchangia vizuri hii dimension..sina uhakika kama nimekupata hapa.
 
Hivi kama ukiwa katika position ambayo unaiba/unapata chochote bila kukamatwa, japo ukikamatwa umevunja sheria na unafukuzwa kazi. Lakini uwezekano huo ni mdogo.
Je utapokea/utaomba rushwa? au utaiba?
Say hakuna mtu wa kukusakama, ni nafsi yako tu, shida za kiamaisha ndio hizi, familia extended mpaka mwisho wa mipaka ya nchi.
Hapo tunaweza kuhisi mafisadi walikuwa katika temptation gani.
 
Mwalimu Julius K. Nyerere aliwahi kusema, Rushwa ni adui wa haki...sasa ni zaidi ya miaka kumi toka ametutoka, na ni dhahiri rushwa imekuwa ni kama sehemu ya maisha wa kawaida ya watanzania. Mhudumu wa chumba cha maiti haoni aibu kuomba rushwa ndugu wa marehemi ili atoe mwili wa mpendwa wao uliohifadhiwa mortuary kinyume cha utaratibu, afisa masoko wa kampuni kubwa hana hata chembe ya aibu anapotoza asilimia kumi kwa matangazo yanayoenda kwenye vyombo vya habari, mhudumu wa zamu chumba ya kutoea damu muhimbili anaona ni sawa kuuza mifuko ya damu kwa ndugu wa wangonjwa wenye upungufu wa damu. Mwalimu wa shule ya msingi ya binafsi haoni aibu kuomba malipo ya ziada kwa wazazi ili awafundishe watoto wao tuition wakati akijua kufundisha ni kazi yake. Ofisa mkuu wa taasisi ya kuzuia rushwa haoni kasoro kuuza siri za serikali yake kwa majasusi wa nchi za magharibi ..." eti Rais wa nchi hana utashi wa kupigana vita dhidi ya rushwa.... ilimradi kila nyanja imechafuliwa na rushwa...JE NINI UZOEFU WAKO KWENYE HILI?​
 
police mbezi kwa yusuph tena ilibidi wife aendee town faster ,mambo ya magari na traffic
 
kupata leseni mpya tra mayfair plaza... Ili kupata leseni daraja E la kuruhusu kuendesha malori, nilitoa elfu 30 kama rushwa,,, kwasababu cheti nilikua sina, na muda wa kwenda driving school sikua nao, wala pesa ya kulipia hiyo driving school nilikua sina, na udereva wa malory naujua na nimeshauzoea.
 
I say ninaposafiri kwenda mikoani lazima niweke alfu tano tano kwenye gari kama Tshs 50,000/- kwa ajili ya usumbufu wa trafiki njiani. Juzi hapa nilipigwa mkono kwa kwenda 53km/hr kwenye eneo la 50km/hr, wakanishikia bango kwamba nimezidisha speed nilipe faini ya Tshs 30,000/- hadi nikatoa kitu kidogo.

Point yao ni kwamba ni afadhali niende hata 10km/hr kuliko 51km/hr, kwa sababu hata ningekuwa hiyo 51km/hr ningetozwa fine!
 
Jana tu nimempa traffic 10,000 alinikamata. Niwapo na safari ndefu huwa naweka 2,000 pembeni mwa sterling + magazeti ambayo huwa nawaachia na 'hawanipekui' hata kwa dawa.

Ukiwa pale banana kuna matraffic huwa wanakwenda ile njia ya Kitunda jirani ya Tanesco (kona), wao wakinikamata yaani huwa hakuna maelezo ni buku 2 nasepa.

Pale Misigiri napo huwa wanazuia, ukiwaachia magazeti ya siku hiyohiyo toka Dar nakwambia hawakugusi wala kukuuliza maswali.

Pale Hungumalwa napo wamejazana, mwendo ni mdundo tena wa pale unawaambia naenda kuchukua mchele nitakupitishia kiroba kimoja na jamaa hawajali.

Buhongwa center kuna traffic huwa wanakaa pale, ni full rushwa yaani wao ni buku-buku tu unasepa na wala hawajali.

Yaani rushwa kwa traffic haiwezi kuisha, na kila dereva/mwenye gari lazima mpaka sasa awe ameshahiriki kutoa rushwa na nikazi kubwa kumtokomeza adui rushwa, maana wengi wanampanda adui huyu.
 
Wakuu embu fungukeni,
umeshawahi kutoa rushwa na ilikuwa kiasi gani na unaona kuwa rushwa inasaidia au ni mbaya.

Mi nishawahi kutoa rushwa mara nyingi sana ila nachukia rushwa na ilinibidi nitoe maana sheria ingechukua mkondo wake ningeumia zaidi au ningefilisika.

Ila najiuliza ni kwasababu nchi yetu ni masikini au kwasababu nilishawahi kwenda Dubai ile nchi hakuna rushwa kabisa na rai wapo vizuri ni kwanini sisi rushwa inakuwa kubwa kiasi hiki?
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
kuna jamaa yangu ni clearence wa makontena na walikuwa tra wanamsumbua sana kuingia mjini baada ya kutoa mzigo mpakani walikuwa wakimkamata wanamwbia wakakague tena hilo contena na bidhaa zake maana alikotoa hawajaridhishwa na ushuru aliopigia kwa hivyo ili kufupishwa mambo anatoa ml 1 ,baadae wakamwambia kila akiingia mjini awapigie simu tra na atatoa laki mbili ila wakimkamata atatoa ml1
 
Mi nimewahi kupokea na kutoa zaidi ya mara20

kwa hiyo unadhani uwepo wa rushwa unarahisisha mambo yako kwenda vizuri?
kwa mfano umefika hospital umekuta foleni watu 50 alafu nesi akakuambia toa 10,000 akuhudumie utampa?
_au umekamatwa na mali ya magendo ya ml20 alafu wakakuambia toa ml 5 uende hata kama huo mzigo hauna hiyo faida na usipotoa wasizi mzigo na ukiangalia sheria inasema hivyo kweli na mali sio ya wizi ni yako....
 
Muda mwingine nashindwa hata kulifafanua hili neno kwa hapa kwetu tz, muda mwingine unakuwa huna nia ya kutoa ila mazingira yanakulazimu ufanye hivyo, binafsi nimeshatoa rushwa mara tatu na zote kwa askari, mara mbili kwa wa usalama barabarani na moja kwa wale wanaoitwa tigo wanaozurura na pikipiki.

Sisemi rushwa ni nzuri ila nataka kusema tu kuwa mara zote nilizotoa ilinisaidia kufanikiwa kilichofanya nikatoa rushwa.

Maoni yangu.......Rushwa sio nzuri hata kidogo maana kwanza ni ubinafsi na roho mbaya, nachukia ninapoitoa.......hembu fikiria unafika hospital unatoa rushwa utibiwe pengine haraka kuliko wale uliowakuta kwenye line, unajisikiaje ktk hali kama hiyo?
Hii maana yake ni mwenye nguvu kumkandamiza mnyonge, unajisikiaje wewe kama polisi unamkamata mtu na kumlazimisha kuwa bidhaa alizonazo si za uhalali, pamoja nakuonyeshwa risiti lakini unamsumbua na kumpotezea muda mpaka upewe chochote, hii si sawa lkn kwa Taifa letu lilipofikia hakuna hata anayejali na rushwa imekuwa sehemu ya maisha yetu, tunatoa na kupokea kila kukicha.......wakubwa walitaka kuihalalisha kwa kuibatiza izaliwe upya na kuitwa TAKRIMA.
 
rushwa ni mbaya sana watu tunatoa kutokana na mfumo ambao upo wa rushwa rushwa, mimi nlipata tatizo mafia wakatI fulanI ilinibidi nitoe rushwa maana bila hivyo mambo yangekua mabaya sana kwangu, ila lazima tufahamu rushwa ni adui wa haki
 
Back
Top Bottom