Siasa Zakielemea Chuo Kikuu Mlimani

Uchaguzi wa serikali ya wanafunzi chuo kikuu mlimani imeingia katika wakati mgumu baada ya vyama vya siasa na mafisadi kuingilia katika uchaguzi huo. Hadi kufikia sasa mgombea mmoja raia wa kigeni ambaye ameonekana ni tishio kwa chama tawala na mafisadi kuanza kutishiwa na kisha kusimamishwa masomo kwa muda usiojulikana yeye na kambi yake nzima ya kampeni.
Mambo yanayowezekana kuwa sababu ya yeye kusimamishwa ni pamoja na kuhoji matumizi ya hela za mradi wa MLIMANI CITY pamoja na kauli zake za kuwa wagombea wengine ni makada wa CCM, na kwamba yeye hata kuwa tayari kuendeshwa na wanasiasa


NADHANI MKANDALA ANATUMIWA SANA NA CHAMA TAWALA KUTIMIZA MALENGO YAKE, NA PENGINE ANAHONGWA HELA NYINGI SANA KATIKA HILI, NA YEYE BILA KUFIKIRI ANATII, HAJUI KUWA ANAJISHUSHIA HESHIMA YAKE, HATHAMINIKI TENA, SASA HIVI KWENYE JAMII YA CHUO NI KAMA MWEHU.
NAE ACHUNGUZWE KAMA FISADI
 
Mkamap, UDSM migomo haijaanza miaka mitatu iliyopita. Nilisoma pale kwa miaka 3 nakatika hiyo miaka 2 ilikuwa na migomo mikubwa mno. Kusema chhuo sio makini wakosea, pia taja jina la profesa unayeona anaboronga na usigeneralise. Siungi mkono yanayotokea pale na ninayapinga kabisa ila yaelekea una kakitu moyoni mwako na UDSM au staff wake sijui.

Haya niambie katika vyuo vya Tanzania ni chuo gani wanafunzi wake wamewahi kugoma ukiachia SUA, Mzumbe. Unataka kuniambia kuwa wanafunzi wa vyuo vingine hawagomi kwa vile vyuo vyo ni makini sana. Kugoma kwa kweli kunaleta hasara kubwa sana kwa chuo na Taifa kwa ujumla, lakini mgomo hutumika pale diplomasia inaposhindikana though its is not true for all the time.


Mama kwa kweli kakitu kangu moyoni Ni huo Uborongaji wanaofanya hao wakuu wa udsm ni hako tu mama hakuna kengine,mimi kwa kweli sisiti kuhoji upofesa wao

Yani:mgomo wa udsm unasababishwa na uongozi na si wanafunzi .Na migomo yao ni mfululuzo mno unalitia taifa hasara Na hoja yangu haswa iko hivi Kama hawa wasomi wamebobea wanashindwa kupatia suluhu ya kudumu taasisi ya udsm tu je tuwategemee ktk tasisi ya watanzania wote kututatulia matatizo??? Hiyo ndio hoja kuu
wakipewa muafaka wa ccm na Cuf si ndio basi kabisa.

Mimi nawasakama udsm maana ndio BABA yao kwa tz vyuo vingine vinajifunza na kuiga kutoka kwao,hivyo wakiachiwa na haya maamuzi yao UCHWARA yatasambaa kote ,kumbe lazima tuanze kudhibiti na maamuzi yao ya kinazi nazi.
 
NADHANI MKANDALA ANATUMIWA SANA NA CHAMA TAWALA KUTIMIZA MALENGO YAKE, NA PENGINE ANAHONGWA HELA NYINGI SANA KATIKA HILI, NA YEYE BILA KUFIKIRI ANATII, HAJUI KUWA ANAJISHUSHIA HESHIMA YAKE, HATHAMINIKI TENA, SASA HIVI KWENYE JAMII YA CHUO NI KAMA MWEHU.
NAE ACHUNGUZWE KAMA FISADI

mama mmoja wamekutajia na jinsi anavyoonekana ktk familia yake
 
Uchaguzi wa wanafunzi ulisimamishwa juzi usiku kwa barua ya kaimu makamu mkuu wa chuo profesa Maboko Makenya kwa kusema eti kwa kuwa mwenyekiti wa kamati ya rufaa amejiuzulu basi wanafunzi hawatatendewa haki haswa watakao kuwa na rufaa zao ila la kuustaajabisha ni kuwa aliruhusu uchaguzi wa makamu wa rais uendelee na huku akiusimamisha ukle wa nafasi ya urais pamoja na wenyeviti wa vitivo.

Jana kuna wanafunzi watano ambao mmoja wapo alikuwa ni meneja wa kampeni wa huyu ndugu kutoka Afrika ya m,ashariki UGANDA ambaye anaitwa Odory Odwang na meneja wake wa kampeni anaitwa Ole Wawa pamoja na wanafunzi wengine watano wamesimamishwa kwa muda usiojulikana sasa huu ni uhuni na wapenda demokrasia wote tusiangalie tuu kule kwa Mugabe na kulalamika hata hapa kwetu kuna wahuni wa kiutawala kama chuo kikuu cha DSM ,nawatafuta waadhirika na huenda leo jioni nikaweza kuonanan nao ili wanipe hizo barua na nyaraka then nitaweza kuwaletea hapa na kuona jinsi wahuni hawa wanataka kuendesha chuo kama tawi la CCM.

hii ni mara ya tatu kwa wanafunzi kutoka Afrika mashariki kunyiwa fursa ya kuongoza hapa chuoni, itakumbukwa habari ya yule kijana wa kenya mika ya tisini pamoja na yule msichana kutoka kenya pia miaka ya tisini.

Eeh! Mama yangu, hivi nchi yetu inaenda wapi? Najua sababu yake kubwa ni kusoma bila kuelemika na kukosa viongozi waadilifu wenye kusema uongo mwingi na kuupaka sura ya ukweli.

Yaani, kwa sasa kutofautisha ukweli na uongo siyo rahisi kwani vyote vinafanana hapa kwetu.
 
Mama kwa kweli kakitu kangu moyoni Ni huo Uborongaji wanaofanya hao wakuu wa udsm ni hako tu mama hakuna kengine,mimi kwa kweli sisiti kuhoji upofesa wao

Yani:mgomo wa udsm unasababishwa na uongozi na si wanafunzi .Na migomo yao ni mfululuzo mno unalitia taifa hasara Na hoja yangu haswa iko hivi Kama hawa wasomi wamebobea wanashindwa kupatia suluhu ya kudumu taasisi ya udsm tu je tuwategemee ktk tasisi ya watanzania wote kututatulia matatizo??? Hiyo ndio hoja kuu
wakipewa muafaka wa ccm na Cuf si ndio basi kabisa.

Mimi nawasakama udsm maana ndio BABA yao kwa tz vyuo vingine vinajifunza na kuiga kutoka kwao,hivyo wakiachiwa na haya maamuzi yao UCHWARA yatasambaa kote ,kumbe lazima tuanze kudhibiti na maamuzi yao ya kinazi nazi.



Kwa hiyo unathibitisha kuwa UDSM ni chuo makini. Hasa huyo Mkandala ambaye unaogopa sana kumtaja kwa jina (labda ni shemeji yako)amekuwa culprit wa CCM toka zamani, na asante aliyopewa ni hiyo ya uVC. Katika moja ya matokeo ya utafiti wake kabla ya uchaguzi 2005, alisema CCM itashinda na ikashinda. Akiwa REDET ameshawahi kulaumiwa na vyama vya upinzani kuwa research zake ziko biased na aliegemea sana kwa CCM. Sasa hapo chuo ni CCM kwa CCM maana wanafunzi wengi ni wanaCCM. Akili kumkichwa kwa hao wanafunzi wanaCCM, wachuje pumba na mchele kwa mfano wa jambo hili linalowakuta wahamie upinzani au wabaki neutral kama mimi.
 
Kwa hiyo unathibitisha kuwa UDSM ni chuo makini. Hasa huyo Mkandala ambaye unaogopa sana kumtaja kwa jina (labda ni shemeji yako)amekuwa culprit wa CCM toka zamani, na asante aliyopewa ni hiyo ya uVC. Katika moja ya matokeo ya utafiti wake kabla ya uchaguzi 2005, alisema CCM itashinda na ikashinda. Akiwa REDET ameshawahi kulaumiwa na vyama vya upinzani kuwa research zake ziko biased na aliegemea sana kwa CCM. Sasa hapo chuo ni CCM kwa CCM maana wanafunzi wengi ni wanaCCM. Akili kumkichwa kwa hao wanafunzi wanaCCM, wachuje pumba na mchele kwa mfano wa jambo hili linalowakuta wahamie upinzani au wabaki neutral kama mimi.

huyo ni one among
Mukandala hajawa mkuu wa chuo miaka mingi lakini strike za udsm hazipatiwi majibu na zimekua za kudumu kitu kinachoashiria wapo wengi.
fact ni kwamba ktk maamuzi hayo waliyoyatoa walikaa kamati zaidi ya the said profs 5 ama zaidi.
 
Eeh! Mama yangu, hivi nchi yetu inaenda wapi? Najua sababu yake kubwa ni kusoma bila kuelemika na kukosa viongozi waadilifu wenye kusema uongo mwingi na kuupaka sura ya ukweli.

Yaani, kwa sasa kutofautisha ukweli na uongo siyo rahisi kwani vyote vinafanana hapa kwetu.

Huo ndio ukweli wenyewe,kuheshimu makaratasi ndio kunapelekea hadi watu kuyaghushi.
Muelimika hawezi tumiwa wala kuiangamiza jamii yake kwa vitu vilivyo ndani ya upeo wake.
 
Bila Migomo Na Maandamano Katika Nchi Hii Haki Huwa Haitendwi.

Hii Ndo Njia Ya Rahisi Ya Kuwasilisha Hisia Zako Bila Ukiritimba.

Sheria Zipo Zimekanyagwa Na Baadhi Ya Makabaila
 
huyo ni one among
Mukandala hajawa mkuu wa chuo miaka mingi lakini strike za udsm hazipatiwi majibu na zimekua za kudumu kitu kinachoashiria wapo wengi.
fact ni kwamba ktk maamuzi hayo waliyoyatoa walikaa kamati zaidi ya the said profs 5 ama zaidi.

Wanafunzi UDSM hugoma kwa sababu mbalimbali achana na hii ya sasa ambayo inaonekana kabisa kuwa uongozi wa juu uko responsible. Strike za UDSM ni matunda ya ufisadi wa viongozi wetu, mambo kama ya mikopo, vifaa vya kufundishia, vyumba vya kulala na hygiene ya mabweni, allowances ni katika mambo ya muhimu ambayo wanafunzi wa UDSM wamekuwa wakigoma. I commend them kwa mambo kama haya, haki haitafutwi tuu bali pia hupiganiwa na kugoma ni njia mojawapo ya kupigania haki kwani matokeo yake mara nyingi yamekuwa kwa viongozi kujitoa muhanga maisha yao (kwani mara nyingi hufukuzwa chuo). Sababu nyingine za migomo inakuwa nje ya uwezo wa uongozi wa chuo na go ahead ya kufunga chuo wakati mwingine hutoka serikalini moja kwa moja.

Uongozi wa chuo mara nyingi unapata lawama kwa kushindwa kutete maslani ya wanafunzi na kujali maslahi ya serikali. Hapa ndipo wanapoboa
 
Nipe muda nitakuletea rants zako zote ulizozitoa dhidi ya UDSM just because Profesa mmoja wa UD amekataa kuitambua Dar Tech!

Katika hili mkuu jipe time usome tena ile thread yako usome ulichoandika!



Sidhani kama unataka kusema kuwa maprof wa UD wote wanahusika hapa na huu uchuro



Ninafanya kazi mkuu kupata pesa yangu na sina sababu ya kuiba pesa za watanzania kama vile wana ccm mnavyofanya huko bongo day in day out!

Ninarudia tena kuwa ccm wawaachie wanafunzi wa UD wachague kiongozi wao wanayemwona anafaa!

nooo. you have errored, totally a technical error. ulikuwa wapi wakati anatoa hoja zake. kwa nini hukujitokeza kupinga au kujenga hoja. leo hii wakati tunaongelea mambo ya wakati huu ndio unaibuka na ajenda za threads zilizopita? what a pit my friend? ila nadhani humepitiwa maana wewe sio mwafrika wa kike ninayemfahamu, au haukulof out, na hivyo kuna mtu kaja na kukoment.

I wander!!
 
Ni kuwa jana asubuhi waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo ndugu Mtatiro Julius amesimamishwa masomo eti alienda kwenye kipindi cha jeneral on monday na kukisema cghu vibaya juu ya uchaguzi wa wanafunzi.
 
Ni kuwa jana asubuhi waziri mkuu wa serikali ya wanafunzi chuoni hapo ndugu Mtatiro Julius amesimamishwa masomo eti alienda kwenye kipindi cha jeneral on monday na kukisema cghu vibaya juu ya uchaguzi wa wanafunzi.


Naona sasa uongozi UDSM unaelemea kwenye politics badala ya academics. C'on guys. Mnajidhalilisha na kujishushia heshima yenu kwa kuendelea kujikomba kwa serikali..mkijikomba kihivyo ndio bajeti yenu itapitishwa bila kukatwa panga!!??
 
Wakati umefika wagombea wa nafasi mbali mbali za uongozi wa serikali za wanafunzi Vyuo vikuu waombe kupitia vyama vya siasa vilivyosajiliwa yaani kama CCM, CHADEMA, CUF, TLP, NCCR-MAGEUZI n.k

Kwa hiyo ningependekeza vyama viruhusiwe kuwa na matawi vyuo vikuu na watu wakagombea kupitia vyama hivyo na wagombea binafsi waruhusiwe pia.

Kwa mtindo huo tutaweza kurekebisha kasoro nyingi za uchaguzi zinazojitokeza huku nje ya chuo.

wanachuo wagombee kupitia vyama vya siasa kama inavyofanyika katika nchi nyingi za kusini mwa Afrika kama Botswana. Chuo kikuu cha Botswana wanagombea kupitia vyama vya siasa na wanaserikali za wanafunzi ambazo zinakuwa zinendeshwa kwa ilani ya chama kilichoshinda uchaguzi, hakuna mizengwe, na mzani ungebalance maana Chama Cha Mafisadi kinapotaka ku-influence uchaguzi kitakuwa monitored na Vyama vyenye sera mbadala.
 
nooo. you have errored, totally a technical error. ulikuwa wapi wakati anatoa hoja zake. kwa nini hukujitokeza kupinga au kujenga hoja. leo hii wakati tunaongelea mambo ya wakati huu ndio unaibuka na ajenda za threads zilizopita? what a pit my friend? ila nadhani humepitiwa maana wewe sio mwafrika wa kike ninayemfahamu, au haukulof out, na hivyo kuna mtu kaja na kukoment.

I wander!!

Ishengoma,

Ukisoma hiyo thread ya MkamaP akitoa rants dhidi ya chuo kikuu, kuna watu ambao wanakijua chuo kuliko mimi walikuwa wanamjibu kwa kiasi chake. Sikuwa na nafasi au sababu ya kuchangia katika hiyo mada pia.

Kwa hili, nimeona kuwa anazidi hii generalization yake na nimeamua kumweka kwenye meza (accoutable) ili ajibu au atolee maelezo rants zake. So far nadhani unaona amefanya hivyo na kubadili tone!
 
Back
Top Bottom