Ashoboza Kabalim
Member
- Jan 20, 2012
- 21
- 1
Ikiwa ni zaidi ya mwezi sasa zitoke tetesi kwa wanachuo kuletewa fedha za kujikimu, watendaji ndani ya bodi hiyo wamekuwa wakifanya mawasiliano yasiyo rasmi na wasomi hao kuwa fedha zimekwishatumwa vyuoni hivyo 'waukomalie' uongozi wa vyuo hivyo ili kupata fedha zao! Hii imeleta imani kuwa fedha hizo huwa zinatumwa vyuoni nakuwekwa kwenye 'fixed' account ili uongozi wa vyuo hivyo upate faida ya 'fasta fasta'.
Hata hivyo, uongozi wa vyuo hivyo unakiri kuwapo kwa uchonganishi huo usio rasmi kati yake na wanachuo kutokana na ukweli kwamba fedha zilizotumwa ni kwa ajili ya ada (tuition fee) na si fedha ya kujikimu. Mkanganyiko huu unazidi kuwaweka katika hali mbaya ya kiuchumi wasomi hawa, wengi wao wakipiga 'dash' (kushinda njaa) kutokana na kucheleweshwa kwa fedha hizo.
Hata hivyo, uongozi wa vyuo hivyo unakiri kuwapo kwa uchonganishi huo usio rasmi kati yake na wanachuo kutokana na ukweli kwamba fedha zilizotumwa ni kwa ajili ya ada (tuition fee) na si fedha ya kujikimu. Mkanganyiko huu unazidi kuwaweka katika hali mbaya ya kiuchumi wasomi hawa, wengi wao wakipiga 'dash' (kushinda njaa) kutokana na kucheleweshwa kwa fedha hizo.