Shule ya NIMROD MKONO

Huyu Mh. Nimrod Mkono ni habari nyingine, hana maneno mengi. Yaani ni maneno mafupi na vitendo virefu. Akiwa M/K bodi ya mikopo, aliwahi kuikopesha bodi hiyo na kutoa mikopo ya asilimia 100 kwa wote.

Kitaaluma ni mwasheria kaajiri mabesti wa sheria mpaka wazungu.

Kiini cha utajiri ni ukaribu na serikali enzi za mwalimu. Ndiye aliyekuwa wakili wa mikataba yote ya serikali.

Alichuma sana alipokuwa wakili wa BOT, alitoza gharama kubwa sana na alizichelewesha baadhi ya kesi zisiishe nyingine mpaka leo ili aendelee kuvuta.

Shuleni UD hakuwa kichwa. Degree yake ya sheria, its just a PASS na hakufanya masters lakini he is smart!.
 
ndugu unaongea pumba, unaonekana hujaenda shule, mwenzako nimrod anatunimia guidelines za elimu sio, na kuwa na masters eti una kichwa, utakuwa na first class degree, masters na hata phd, na bado maisha yako ni taabani. mpe hongeni zake huyu mzee kwa kutumia elimu yake na fedha zake kwa manufaa ya wananchi walio maskini.
 
mmhh, kwa kweli shule ni nzuri sana. Je ni kazi ya Mkono peke yake?
 
Shuleni UD hakuwa kichwa. Degree yake ya sheria, its just a PASS na hakufanya masters

Umeongopa.

Au hujui kitu kuhusu background ya Mkono.

Basi fanya ka research ka uongo na kweli kidogo kabla ya ku posti kitu kuhusu facts za mtu. Mkono ni mbunge, ungeanzia kwenye website ya Bunge angalau kupata ka background kidogo hapa.

Na degree ya PASS ndio nini hicho? Chuo gani chako hicho wenye hicho kitu? Acha kuji expose Pasco wewe!
 
Nimrod Mkono katuhujumu sana pale BoT...ila lazima tumpongeze kwa kazi anayowafanyia wananchi wa vijijini ili kuwakomboa na ufukara...kwa hili anapaswa kuungwa mkono sana. Sehemu ndogo ninapoona katatizo ni kwenye ile Project ya Mwalimu Nyerere College. Introduction yake inasema:

"Hon. Mkono, as the heart behind this unique development project for Musoma Rural, together with the board members of the United World Colleges, are establishing a University/College in Honor of Mwalimu Nyerere, the Father and Founder of the Tanzanian Nation, under the name of "Mwalimu Nyerere UWC for Self - Reliance".

The location of the University/college in Butiama, which is the home village of Mwalimu Nyerere , is ideal to conduct agricultural and rural development studies, and would attract students from the Northern Tanzania and Southern Kenya as well as Burundi , Rwanda and Western Congo , as a safe heaven."


Nafikiri angetarget watanzania wote ambao Nyerere ni Baba wa Taifa lao.
 
humjui ww huyu mzee hawa ndo wale mafisss wa mwanzo tokea enz za awamu ya kwanza sema wanajua kula na vipofu tu, ndo huoni mistake zao na wanajua kuhesabu hatua zao
 
Mkono pamoja na kwamba ni fisadi lakini anakumbuka nyumbani. Sehemu ya Pesa anayopata anaitumia kujenga mashule na zahanati mkoani kwake. Shule ambayo anajenga sasa inakadiriwa kuwa na gharama za $1.6m na watoto wanakwenda shule bure ama kwa gharama kidogo sana.
 
MKJJ duh! shukran sana

cha ajabu katika website yake hajaweka watu ambao wanamsponsor ukibonyeza sponsors wake huoni kitu
 
Huyu jamaa kajitahidi.. sasa kwa nini Chenge akapeleka 'vile visenti' New Jersey Islands, asijenga hata shule ya sekondari kule Tabora?
 
JF XXL,
Mkono anajisponsor mwenyewe.
Sio Kweli..Mkono works very closely with the Import Support Boys..wenyewe wanajiita OLD MONEY WA TANZANIA!!
Wakina Subash Patel and Crew..

But respect has to be paid when its due kwa kujenga mashule na mambo mengi ya maendeleo inapunguza hasira za wananchi!! hahahahaha

KIDUMU CHAMA CHA KUPINGA MAPINDUZI
 
Hiyo shule sio ya Mkono. It is a proposed project to be part of the international high schools known as United World Colleges (UWC)

UWC

Yeye ni trustee tu, michango ya kujenga shule inatoka kwenye hiyo foundation.
Hizi shule zipo katika nchi mbali mbali, mfano Swaziland, Wales, Italy, Norway, Phillipines, India, Hong Kong, USA, Canada na moja Latin America.
Sasa wanataka kuanzisha moja Tanzania ili kumuenzi Mwl Nyerere na his theories of Self Reliance. Vijana kutoka pande mbali mbali ya dunia wataweza kuja hapo na kusoma masomo yanayohusiana na Agriculture na Maendeleo ili kupata cheti cha IB - Sawa sawa na Form 6 fulani hivi...

Tazama website ya shule:

http://www.mnuwc.org/
 
Hili swala la kila mwenye upenyo kuanzisha shule kwa kweli mimi naliona lina walakini. Ndio tunahitaji shule kwa wingi ili kuweza kuinua kiwango chetu cha elimu. Lakini hawa waanzishaji kweli wana msukumo wa kuongeza elimu nchini au lengo lao ni kuneemesha mifuko yao?

Na kwa nini shule tu? Vipi kuhusu maktaba na maabara? Mtu binafsi atakayekuja kujenga maktaba ambayo itashiba books, references, catalogs, na maabara kwa ajili ya utafiti wa kisayansia; then huyo mtu ndio atastahili kupigiwa makofi ya pongezi za dhati. Tunahitaji a modern library...ile ambayo itaifunika ile maktaba kuu kuu pale Kisutu.
 
Umeongopa.

Au hujui kitu kuhusu background ya Mkono.

Basi fanya ka research ka uongo na kweli kidogo kabla ya ku posti kitu kuhusu facts za mtu. Mkono ni mbunge, ungeanzia kwenye website ya Bunge angalau kupata ka background kidogo hapa.

Na degree ya PASS ndio nini hicho? Chuo gani chako hicho wenye hicho kitu? Acha kuji expose Pasco wewe!
.
Correction. Mkono ndio most succesiful lawyer in TZ in terms of money. Waliosoma naye darasani was an avarage student. Baada ya kupata LL.B hakufanya masters ya sheria.(sorry the omission)
Nilisema the man is smart. Kwa maneno mengine to get sucess in life, you dont have to be the best brain or a university degree.
Pamoja na mengine yote, 'The end justifies the means' Mkono anastahili pongezi zake.
Kwa mengine yote, samahani.
 
Back
Top Bottom