Mjomba wa taifa
JF-Expert Member
- Apr 20, 2012
- 231
- 161
Serikali imepitisha sheria rasmi kuwa hakuna mtumishi yeyote anaeweza kuchukua mafao yake katika mfuko wowote wa pensheni mpaka tu afikie umri wa kustaafu miaka 55 kwa hiari au 60 kwa lazima.
Uamuzi huu unazua maswali yafuatayo:-
1. Je, mdau wa kwanza katika hili ambaye ni mfanyakazi amehusishwa katika maamuzi haya?
2. Je, Mifuko hii ya Pensheni itaongeza riba katika michango? maana ikumbukwe kuwa thamani ya milioni moja ya leo si sawa na milioni moja baada ya miaka 10 ijayo.
3. Iwapo mtumishi hahitaji tena kuajiriwa na kuchangia katika mfuko, kwanini pesa hii asipewe afanyie kazi anazozijua mwenyewe za kimaendeleo?
4. Kwanini serikali inawakumbuka wananchi pale tu inapohitaji jasho la wananchi?
5. Kwanini serikali impangie mtu binafsi mahitaji yake?
6. Uwezo wa kutumia mafao haya kujipatia mkopo wa nyumba ni kweli au changa la macho?
Majibu mengi yanahitajika katika hili kuweza kuwasaidia wafanyakazi kujua nini faida na hasara za kusubiri hadi umri wa kustaafu ndipo mfanyakazi aweze kuchukua mafao yake.
Uamuzi huu unazua maswali yafuatayo:-
1. Je, mdau wa kwanza katika hili ambaye ni mfanyakazi amehusishwa katika maamuzi haya?
2. Je, Mifuko hii ya Pensheni itaongeza riba katika michango? maana ikumbukwe kuwa thamani ya milioni moja ya leo si sawa na milioni moja baada ya miaka 10 ijayo.
3. Iwapo mtumishi hahitaji tena kuajiriwa na kuchangia katika mfuko, kwanini pesa hii asipewe afanyie kazi anazozijua mwenyewe za kimaendeleo?
4. Kwanini serikali inawakumbuka wananchi pale tu inapohitaji jasho la wananchi?
5. Kwanini serikali impangie mtu binafsi mahitaji yake?
6. Uwezo wa kutumia mafao haya kujipatia mkopo wa nyumba ni kweli au changa la macho?
Majibu mengi yanahitajika katika hili kuweza kuwasaidia wafanyakazi kujua nini faida na hasara za kusubiri hadi umri wa kustaafu ndipo mfanyakazi aweze kuchukua mafao yake.