Sheikh Ponda ajeruhiwa vibaya baada ya kupigwa Risasi mjini Morogoro

Status
Not open for further replies.
Niko hapa natizama Habari ya saa2 usimu kwenye local chanel lakin hakuna Habari yoyote ile iliyotangazwa kutokana na tukio la Ponda sasa sijui wanasubiri mpaka dola ichakachue na kuhariri hiyo Habari ndo waitangaze? labda nijaribu kisikiliza redio Kama naweza kuisikia hiyo Habari lakini hakuna cha Tv yoyote ile iliyotangaza! Labda tusubiri magazeti kesho asubui!
 
Mda kama dakika 20 zilizopita mjini Morogoro shehe Ponda amepigwa risasi na polisi .

Dhahama hiyo imempata baada ya kushuka kwenye tax ambako kulikuwa leo akiendesha mhadhala baada ya mhadhala huo kukawa kama kuna maandamano kueleke barabarani, gafla polisi walitokea na kuanzanza kutawanya wakati huo yeye alikuwa hayupo.

Ndipo mda mdogo akawasili akashuka na ndipo akapigwa risasi.


------------------------------------

UPDATE:

Haijulikani hali yake. RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.


Watu wangu hupotea kwasababu ya kukosa maarifa...!! Itafika siku polisi wa Tanzania wataua hata Waziri wao wenyewe....recall Amran Kombe's shooting...!!?
 
Mhhhhhhh!Tunakoelekea sasa!Kama ana makosa,akamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria kama walivyokuwa wamefanya mwanzoni.Hili la kutumia risasi siafiki hata kidogo!Pole sana Ponda.
 
Nadhani wewe ndiyo --------, watu wanaleta uchochezi wa kidini Tanzania kumbe mnafurahia, Mtu anahimiza watu wafanye maandamano kama ya Misri kupitia mgongo wa dini.....tunacheka cheka tu. KAMA ANATAKA SIASA SI AKAANZISHE CHAMA IJULIKANE? Ifike mahari tuheshimu uwepo wa serikali hata kama ni ya CCM au CHADEMA.
Pumba @ work,
Pinda @ work
 
hivi kwa nini hawa polisi wanamfatilia sana Shehe Ponda kama mtu asiye huru hapa nchini?
hivi kwa nini polisi watumie silaha za moto kutawanya watu?
Kwanini polisi wanafikiri kuwa risasi ni suluhu?

mkuu n kweli unaona sheikh ponda hastahl kufuatliwa.?
 
Habari hii ni kweli au ni uzushi? Kama ni kweli I think for the first tym nitakuwa against Mwema
Kwa kauli yako hii inamaanisha matukio haya yaliyofanywa na polisi yalikufurahisha/Yanakufuruhisha
1. Kuuliwa wafuasi watano wa CDM kule Arusha
2. Kuuliwa kwa Ally Dona pale Morogoro
3. Polisi kumuua mwandishi wa habari Mwangosi kule Nyororo Iringa
4. Polisi kulipua Bomu na kupiga risasi Mkutano wa CDM kule Soweto Arusha na kuua watu wanne
5. Polisi anaowaongoza kujiingiza katika biashara ya nyara za serikali pamoja na madawa ya Kulevya
6. Polisi kusimamia kupigwa kwa wabunge wa CDM kule mwanza na Green Guard wa CCM

Hautakiwi kuwa mbaguzi kiasi hiki kwani wote waliodhuriwa na hao polisi ni Watanzania bila kujali dini au Itikadi zao za kisiasa.
 
Mda kama dakika 20 zilizopita mjini Morogoro shehe Ponda amepigwa risasi na polisi .

Dhahama hiyo imempata baada ya kushuka kwenye tax ambako kulikuwa leo akiendesha mhadhala baada ya mhadhala huo kukawa kama kuna maandamano kueleke barabarani, gafla polisi walitokea na kuanzanza kutawanya wakati huo yeye alikuwa hayupo.

Ndipo mda mdogo akawasili akashuka na ndipo akapigwa risasi.


------------------------------------

UPDATE:

Haijulikani hali yake. RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.

:smile-big:
 
Mhhhhhhh!Tunakoelekea sasa!Kama ana makosa,akamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria kama walivyokuwa wamefanya mwanzoni.Hili la kutumia risasi siafiki hata kidogo!Pole sana Ponda.
Wanafuata maagizo ya Pinda
 
Polisi na CCM watahakikisha kila nayewapinga anauwawa kabla ya 2015....Lakini sasa ndugu zetu waislam wakafumbua macho, wakayaona udhalimu wa CCM na polisi wao. Hapa wamevuka mipaka. Sheikh Ponda amekuwa akiwa akitafutwa sana. Hapa watasema ughaidi kama kawaida yao

Sitashangaa CHADEMA wakitwisha hilo gunia la mchanga !

Kwani polisi ni wa CDM???
 
Ilikuwa ni lazima zitumike risasi za moto? Je alikuwa anatafutwa na polisi? Je ni gaidi? Hakuna mwingine aliyejeruhiwa?
 
MWISHO WA TANZANIA UMEKARIBIA. MARK MY WORDS, NAIONA TANZANIA a.k.a Tanganyika ikigawanyika nchi ndogo zaiidi ya tano au kumi, kama hatua sahihi hazitachukuliwa dhidi ya dhulma kati ya jamii moja hadi nyingine.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom